Category: Uncategorized

D.R.C NDANI YA E.A.C, MFANYABIASHARA ANAFAIDIKA VIPI?

Hatimaye tar29 March Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ilipata kibali cha kuwa mwanajumuiya wa Afrika Mashariki (EAC) na mwezi July mwaka huo 2022 DRC iliingia rasmi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuwasilisha matakwa yote makao makuu ya jumuiya hio jijini Arusha. Hii ni baada ya kuendesha mchakato uliodumu kwa takriban miaka minne. Sasa DRC inapoingia ndani ya EAC mfanyabiashara anafaidika vipi?

DRC inakuwa mwanachama namba 7 wa EAC huku ikiwa ndio nchi kubwa zaidi kijiografia katika ukanda huo. Inasemekana DRC ndio nchi yenye rasilimali (madini, mafuta, misitu n.k) nyingi zaidi duniani. Pia nchi hio ina idadi ya watu takribani milioni 90 ambao ni mtaji muhimu kiuchumi.

MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU D.R.C:

Kukubalika kwa DRC kunamaanisha kwamba soko la Afrika Mashariki linatanuka na kuwafikia watu zaidi ya milioni 300 waishio ndani ya jumuiya hio tu, huku uchumi wa jumla ukiwa na thamani ya 250$ bilioni. Sasa DRC ina nini cha ziada usichokijua?

1. MIPAKA YA KIJIOGRAFIA:

Ikiwa ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa jiografia barani, DRC inapakana na nchi zingine 9. Nchi hizo ni Angola, Burundi, Jumhuri ya Afrika ya Kati, Rwanda, Jamhuri ya Congo (Brazaville), Sudani Kusini, Uganda, Zambia na Tanzania. Muingiliano wa kibiashara ni mkubwa sana hapa.

Zaidi upande wa magharibi mwa jiji la Kinshasha inapakana na bahari ya Atlantiki. Sasa Kongo kupakana na nchi 9 na kuwa na ufukwe wa bahari ya Atlantiki kunaifanya iweze kutanua fursa kwa wafanyabiashara kupitisha mali kwenda nchi nyingi zaidi barani na hata nje ya bara.

DRC na mipaka yake. Milango ya biashara za kimataifa kwa EAC.

2. KUHUSU VIVUTIO VYA UTALII:

Mbuga ya wanyama kongwe zaidi barani ipo DRC, inaitwa Virunga. Hapo utawakuta wale Sokwe wakubwa (Gorillas), simba na tembo. Lakini mbuga hii ipo kwnye tishio la kutoweka kwa sababu kuna mafuta na kampuni ya Uingereza ya Soco tayari imetia timu kuanza kuchimba mafuta hapo mbugani.

Hawa gorilla ni kivutio kizuri sana cha utalii lakini miaka ya hivi karibuni wamekuwa adimu na kutokana na shughuli za mwanadamu, wanyama hawa wapo kwnye tishio la kutoweka kabisa. Je, DRC kuingia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kutadhibiti hatari ya sokwe hawa kutoweka?

Kuhusu namna utalii unaweza kuleta manufaa katika biashara tafadhali fuatana na makala hii hapa chini:

3. KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NA MIUNDOMBINU:

Ni 1.8% tu ya barabara nchini DRC ndio ina kiwango cha lami, huku chini ya 10% ya nyumba za makazi ndio zina umeme. Hii ni hali mbaya sana katika kukuza uchumi wa Taifa. Hata hivyo Benki ya Dunia imetangaza kifurushi za 1$ bilioni kwa ajili ya miundombinu ya DRC.

Moja kati ya vitu vinavyorudisha nyuma juhudi za wajasiriamali na mashirika kuwekeza nchini DRC ni maendeleo duni ya miundombinu. Ukizingatia ukubwa wa nchi hio, imekuwa ni nafuu kusafiri kwa njia ya anga kuliko barabara. Sasa @jumuiya itachangia vipi maendeleo ya miundombinu?

4. BIASHARA ZA NJE YA NCHI (EXPORTS):

Muziki wa DRC ndio mali inayouzwa zaidi nje ya nchi (export). Kuanzia miaka ya 90 muziki wa Bolingo ndio ulikua unasikilizwa na kupendwa zaidi bara zima la Afrika. Ndio maana wasanii kama Fally Ipupa na Koffi Olomide ni matajiri sana. Madini na malighafi zingine zote chali.

5. LUGHA INAYOTUMIKA ZAIDI:

Jiji la Kinshasa ni la pili kwa matumizi ya lugha ya Kifaransa likitanguliwa na jiji la Paris. Yaani Wakongo hawa wanaongea kifaransa zaidi kuliko hata miji ya nchini Ufaransa. Hata hivyo hii inachangiwa na idadi ya watu wanaoishi kwenye jiji hilo, watu milioni 10 mchezo!

Ukiacha Kifaransa raia wa Kongo pia wanazungumza lugha zingine kama Kilingala, Kiingereza, Kiswahili na lugha za makabila asilia. Hivyo ukiwa kama mfanyabiashara na moja kati ya lugha tajwa unazifahamu vyema basi nafasi ni yako kuingia DRC na kutanua biashara zako.

6. KUHUSU UGONJWA WA EBOLA:

Kwamba kupata Ebola nchini DRC ni rahisi kama kupata mafua ukiwa sehemu nyingine? HAPANA. Baada ya ugonjwa huo kufumuka mwaka 1995 na kuua watu zaidi ya 200, milipuko mingine ya ugonjwa huo imekuwa ikidhibitiwa kwa kiwango kikubwa. Hivyo Congo ni salama.

7. KUHUSU MADINI:

Lile bomu la atomiki lililodondoshwa kwenye miji ya Hiroshima na Nagasaki katika WWII lilitengenezwa kwa madini ya Uranium kutoka mgodi wa Shinkolobwe, mkoani Katanga nchini DRC. Hata hivyo mgodi huo ulifungwa mwaka 2004 kutokana na kuishiwa madini ukiiacha DRC patupu.

Kongo imenyonywa sana katika madini yake. Hali kadhalika nchi zingine katika Jumuiya zimepitia hali hio. Hivyo itakapowekwa sera ya pamoja ya kulinda na kusimamia rasilimali zilizopo ndani ya Jumuiya, bila shaka madini na rasilimali ambazo zipo DRC zitakuwa na manufaa sana.

8. HISTORIA YA UNYONYAJI:

Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alijitangazia Kongo kuwa mali yake binafsi kuanzia mwaka 1870. Koloni hilo ndio lilikua mali binafsi kubwa zaidi kuwahi kumilikiwa na mtu mmoja kwenye historia. Umiliki huo ulisababisha vifo vya watu milioni10. Huu ndio mwanzo wa nchi kuharibika.

Mfalme Leopold II aliagiza watu kukusanya zao la mpira ambalo kwa kipindi hiko ndio lilikua zao bora zaidi la kibiashara. Wale walioshindwa kukusanya zao hilo kama kodi waliadhibiwa kwa kunyimwa chakula na kukatwa mikono yao. Ukatili huo ulikua mbaya sana dhidi ya ubinaadam.

9. HALI YA USALAMA NA VITA:

DRC imekuwa ikikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na migogoro isiyokwisha ambayo imepelekea vifo vya watu takriban milioni 6. Hali hio ya vita visivyokwisha imepewa jina la “Vita vya Dunia vya Afrika”.

Vita hivyo kwa sehemu kubwa vimekuwa vikisababishwa na vikundi fulani (kampuni, mashirika na raia wa kawaida) kugombania rasilimali katika eneo fulani. Huyu anataka kuchimba, raia wanataka kunufaika. Je, DRC kuingia kwenye @jumuiya itasaidia kumaliza janga la vita visivyokwisha?

10. KUHUSU MTO CONGO:

Ukiwa na urefu wa kilomita 4,700, mto Congo ndio mto mrefu wa pili barani Afrika ukitanguliwa na mto Nile. Pia huo ndio mto wenye kina kirefu zaidi duniani. Cha kufurahisha zaidi, Mto Congo na Mto Nile yote inapatikana katika EAC. Inakupa picha gani hii kiuchumi?

Je, EAC itaweza kuzalisha umeme wa pamoja kupitia sehemu za mto huo? Je shughuli za kiuchumi kama uvuvi, usafiri, utalii biashara ya mazao ya misitu zitaweza vipi kusimamiwa na Jumuiya kuhakikisha faida zinarudi kwa wanachi wa Kongo na wa jumuiya nzima kiujumla?

ZIADA: MSITU WA CONGO

Msitu wa pili kwa ukubwa duniani, msitu wa Congo unapatikana nchini DRC. Hata hivyo msitu huo ni mkubwa kiasi kwamba umeingia kwenye nchi zingine kama Cameroon, Jamhuri ya Afrika Ya Kati, Jamhuri ya Congo(Brazaville), Guinea ya Ikweta na Gabon. Msitu huu ni utajiri mtupu.

msitu wa mvua wa Congo
Msitu wa Congo

Katika msitu huo kuna fursa nyingi zikiwamo biashara ya magogo, madawa ya kutibu watu, mazao na wanyama, mbao, karatasi na bidhaa zote zitokanazo na misitu. Ukiwa kama mfanyabiashara ambaye sasa una uhuru wa kwenda kuwekeza DRC kirahisi, utaitumiaje fursa hii?

Sasa hayo ni baadhi ya mambo ambayo pengine ulikua huyafahamu kuhusu DRC. Mambo hayo kama yakifanyiwa kazi ipasavyo ndani ya @jumuiya basi ni wazi kutapunguza hali ya umasikini na kuimarisha amani kwa watu wa Kongo na kuimarisha uchumi wa Jumuiya nzima. Mapema mwaka 2021 jumuiya ya nchi za Afrika kwa kauli moja ilianzisha eneo huru la biashara barani (AfCFTA) ambapo nchi wanachama wanaweza kufanya biashara kwa uhuru bila ya vizuizi vya mipakani. Zaidi soma hapa chini

Jumuiya hii inatoa uhuru kwa wanachi wake kuishi na kufanya biashara popote ndani ya nchi wanachama. Jambo hili linatoa fursa kwa Wajasiriamali wa aina zote kuzurura na kutafuta masoko yao kirahisi. Ukiweza vema kutumia majukwaaa ya kimtandao kama websites, mitandao ya kijamii ujue unayo nafasi ya kuwafikia watu milioni 300 waishio ndani ya Afrika Mashariki. Sasa tuambie wewe mtu wa Teknolojia, website designer, mtaalam wa kutengeneza android app, mkulima, engineer nk, unataka ufaidike vipi hapa? Tuambie..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

M-PESA LIPA NAMBA

MY NEW AGE SPECIAL PRESENT

On the 6th of this September, I celebrated 30 years of life, health, and countless blessings. I thank GOD for this gift of life and health. As a believer, I always live with this: “The LORD is my Shepherd, I lack nothing.”- Psalms 23:1. This is my new age special present only for you. Read to the bottom of this article to get it.

I was 21 years of age when I graduated from my high school education, a very ambitious young man. Motivated by that youth energy in me, I dreamt of an exciting future in my life, and working at million dollars tech company/organization was in my mind always.

I was just awarded a certificate of recognition from the Youth of the United Nations in Tanzania (YUNA) in 2010. You can imagine how energetic I was.

Unfortunately, things were very different out of school and college life. All that energy I had when I was a student just vanished. With all the certificates I had, they couldn’t help me get that dream job of “working for the million dollars tech company/organization”.

I was devastated, but I could not allow myself to be consumed by that mocking period of “failures”. 

In 2017 that little energy that was left in me triggered some thoughts of establishing an initiative for serving small businesses with a digital infrastructure that will help them store and monitor their daily business records in an online environment. I called that project BIMOS (Business Monitory System).

online business

That project carried the whole motivation I had toward reaching my dream. Unfortunately, the project was not successful as how it was intended due to numerous challenges we faced back then.

However, in the process, I realized the significance of working in a team, serving the clients with higher customer care standards, human capital(they call it “connections” nowadays), Business analysis, and Organization management.

That project gave me lessons that I could not get in school and college. The project was significant to get me and Rednet Technologies where we are today.

With my team at Rednet Technologies, we managed to launch a number of projects and digital services for our clients from 2017 until today. We learned and improved as we worked with various individuals and organizations on serving their business requirements.

It is about meeting the client’s satisfaction that you can succeed as an entrepreneur in your business .

Joyce (my sister-in-law)

The 9 years journey from when I was 21 was never easy. You can imagine, 9 years of growing up and gathering myself, studying and facing countless challenges, heartbroken and disappointments, processing the algorithms, testing the strategies, and exploring the vast world of technology and business. 

However, the journey is worth it. Since we launched our website in 2017, we have worked on it and set it to be an extremely informative platform with news and updates on tech and business, self-serving for a client to choose what service they want and when they can set a deadline, and a center of communication between Rednet and her clients. Now, look how satisfied and informative the website has become by clicking here.

NEW AGE PRESENT

After saying all that, today allow me present to you this present that will enhance your daily business operations in your office.

  1. Now have you thought of giving yourself the privilege to get your office Stationery materials like Printer Cartridges, Rim Papers, boxes of ball pens and so many items found on our Business Profile below just by the click of a button?
  2. Also, have you thought about how may serve yourself with comfortable online digital services like Website Design, Custom Software Development, and Social Media management just through your smartphone?
  3. How about making sure your business is appearing faster when someone is searching for the service/goods that you provide? In today’s world, you need to make sure that your online business is well optimized by using Search Engine Optimization (SEO) services. Here is how you can do it;

Well as your trusted supplier and ICT expert, we want to meet your business satisfaction by serving you without interrupting other daily schedules you may have. Moreover, we will expect the payments from you within 30 days from the delivery date. Isn’t this helpful to your business?

Now Click these links to see, experience the services and press your orders:

  1. https://rednet.co.tz/services/your-order/ (For Stationeries)
  2. https://rednet.co.tz/services/jihudumie-leo-kwa-huduma-bora-za-tehama-kutoka-kwetu/ (For Web Design)

If you work for an organization, an institution, or a private individual, this Present is Special for YOU. Contact us right now to get started receiving our services.

Get more details on our Business Profile by downloading it here.

Today, by the Grace of GOD, I am looking forward to challenging, rewarding, and exciting 10 years of this Third floor until 40 years of age and more years of serving our clients and exploring the world of technology and business.

focus on your plans and make sure you win.

Cheers.

10 ZA JE WAJUA?

Kama unajua ni kheri, sasa unapata nafasi ya kujua zaidi. Na kama ulikuwa hufahamu basi leo unapata nafasi ya kujua mambo mapya zaidi. Katika jukwaa letu la @ElimikaWikiendi . Sasa leo tuzione zile 10 za je wajua katika Teknolojia na Biashara.

1. Je, wajua kuwa tovuti ya kwanza kabisa kuundwa duniani bado ipo hewani? Hii hapa kwenye link http://info.cern.ch Tovuti hio imetengenezwa kwa kutumia lugha ya HTML na inaonyesha mistari michache tu.

chanzo: https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-teknolojia-ya-intaneti-na-kompyuta-katika-biashara-yako/

2. Ile Teknolojia ya kuongeza uwezekano wa Taarifa kupatikana kwa urahisi na kiwango cha juu katika injini za mitafuto za mtandaoni (Search Engine Optimization, SEO) ilianzishwa mwaka 1991. Teknolojia hii ina umri mkubwa kuliko GOOGLE ilioanzishwa mwaka 1998.

3. Mtandao maarufu wa kutizama mubashara filamu na tamthilia wa NETFLIX ulianzishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1997 huko Carlifonia nchini Marekani. Mtandao huo una umri mkubwa kuliko YouTube ambayo ilianzishwa mwaka 2005. Tuambie, Netflix umeijua lini wewe?

4. Takriban 10% ya pato la Taifa kwa nchi za Kusini mwa Afrika huchangiwa kupitia huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi. Hii ni zaidi ya 7% ya GDP kutoka Asia na chini ya 2% ya GDP kutoka sehemu zingine dubiani.

chanzo: https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/

5. Kusafirisha gari kutoka Japan mpaka Abidjan nchini Ivory Coast (km 14,075) hugharimu $1500. Lakini kusafirisha gari hilihilo kutoka Abidjan hadi Addis Ababa(km 6626) inagharimu takriban $5000. Gharama hii ni ghali mara 3 zaidi ya ile ya kutoka Japan.

Pia kusafirisha gari ndogo kutoka Japan mpaka Dar es salaam (km 11,256) inagharimu $900 bila makato na kodi. Hata hivyo, kusafirisha gari hilo hilo kutoka bandari ya Dar es salaam mpaka jijini Lusaka (km 1937.3), Zambia inafikia $650 bila makato na kodi.

Kutokana na hali duni ya miundombinu, gharama za usafirishaji barani Afrika ni kati ya zile ghali zaidi duniani. Hii pia huletwa na viwango vikubwa vya forodha, tozo za ucheleweshaji, ajali pamoja na ukosekanaji wa fursa zingine.

chanzo: https://rednet.co.tz/usafirishaji-na-miundombinu-katika-ustawi-wa-biashara-afrika/

6. Kufikia Octoba 2018, duniani tovuti bilioni 1.9 zilikuwa zipo hewani (online). Pia kuliripotiwa kuwapo na machapisho mapya (posts) zaidi ya milioni 5 kila siku kutoka kwenye tovuti na blogu mbalimbali duniani. Fikiria leo hali iko vipi..

chanzo: https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-teknolojia-ya-intaneti-na-kompyuta-katika-biashara-yako/

7. Kila siku kunaongezeka watumiaji wapya wa huduma za Intaneti takriban milioni moja duniani kote. Kwa wastani mtumiaji wa kawaida hutumia masaa 6:42 akiwa mtandaoni kwa siku. Kama wewe ni mjasiriamali bila shaka umeshaona fursa hapa.

8. Unalikumbuka shambulizi lililoitwa NOTPETYA? June 27, 2017 malwares hizo ziliathiri kutoka biashara ndogo za software nchini Ukraine mpaka kusambaa duniani kote. Hilo liliitwa “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA DUNIANI”

chanzo: https://rednet.co.tz/yafahamu-mashbulizi-ya-kimtandao-cyber-attacks-na-athari-zake-katika-biashara-kampuni-yako/

9. June 23, 2020 Jumuiya ya SADC ilipitisha muongozo wa kurasinisha(to harmonize) shughuli za kibiashara baina ya nchi wanachama. Sasa mtu akisema watu waende Burundi kutafuta unafuu wa maisha, watu watatumia fursa hio wakaenda Zambia na kwinginepo ndani ya nchi wanachama wa SADC kufanya biashara na maisha yataendelea kama kawaida.

chanzo: https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-urasinishaji-harmonization-katika-biashara/

10. Kufikia mwaka 2022, mwakani tu hapo, 10% ya watu duniani watakuwa wakivaa nguo zilizounganishwa na Intaneti. Imagine nguo yako ina lebo ambayo inaweza kutumika kama tiketi ya kuingia kweny muvi, mpirani au club. Baunsa anascan nguo tu mzigo unajipa.

BONUS: Serikali za duniani zitaanza kutoza kodi katika jukwaa la Blockchain kwa mara ya kwanza mwaka 2023. Sasa wale Traders na Investors wa Bitcoins na Cryptos kupitia Blockchain mjiandae kisaikolojia mkimalizia Tax-holiday yenu huko kwenye Blockchain.

Hayo ndio tuliyotaka kukujuza leo katika 10 za je wajua. Jambo lipi limekushangaza zaidi? Tujuze katika comments hapo chini kisha share makala hii kwa ndugu, rafiki na jamaa zako ili nao wapate kufahamu haya tulokujuza leo.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mpesa lipa namba ya Rednet Technologies.

OFA YA MSIMU WA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN

Tunawatakia Ndugu zetu Waislamu wote Ramadhan Kareem! Rehema za Mwenyezi MUNGU zikawe pamoja nanyi katika kipindi hiki. Kwa kutambua umuhimu wa Kipindi Hiki kitakatifu, OFA YA MSIMU WA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN IMEFUNGUKA ambapo sasa utajipatia huduma hizi kwa gharama nafuu ili kuzidi kuimarisha biashara yako:

i. Website Design (500k ✔️ 1.2m❌)

ii. Business Plan + 100 Business cards (350k ✔️ 600k❌)

iii. Ushauri na Usimamizi (mentorship) BURE kabisa.

Kuendana na OFA hio kuna makala hizi hapa ambazo kwa hakika zitakusaidia sana katika kuendesha biashara yako huku mtandaoni. Fuatana nazo mpaka mwisho:

https://rednet.co.tz/yafahamu-mashbulizi-ya-kimtandao-cyber-attacks-na-athari-zake-katika-biashara-kampuni-yako/ yenye kichwa YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO (CYBER ATTACKS) NA ATHARI ZAKE KATIKA BIASHARA/KAMPUNI YAKO.

https://rednet.co.tz/kwanini-uitangaze-biashara-yako/ yenye kichwa KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?

https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-teknolojia-ya-intaneti-na-kompyuta-katika-biashara-yako/ yenye kichwa UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA KATIKA BIASHARA YAKO.

https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE/TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO.

Zaidi, Karibu DM tuwasiliane kwa undani. Muda wa kuimarisha biashara yako ndio huu. Usiache OFA hii ikupite.

Simu/Whatsapp: 0765834754
email: info@rednet.co.tz / fvitalice@gmail.com
Web: https://rednet.co.tz

MAWAZO YANGU

Bado nawaza kuhusu mambo mengi sana. Sijui itakuaje. Hizi sheria ambazo zinalenga kuhamasisha makusanyo ya kodi na mapato kwa serikali (which is not bad) zinanitafakarisha sana. Hata hivyo kodi na makusanyo haya yanapokuwa makubwa kuliko wastani wa uwezo wa walipaji hugeuka kuwa Unyonyaji kiuhalisia, hata kama zina-backup ya sheria halali. Serikali kama Baba/Mlezi na Msimamizi mkuu wa rasilimali za nchi inapaswa kuhakikisha watu inayowaongoza hawabanwi wala kubinywa haki zao za kikatiba. Nafikiri ni muhimu kuhakikisha zile sheria ambazo zilipitishwa lakini zinaonekana kunyonya na kukandamiza uhuru wa watu kutumia ubunifu wao katika kukuza uchumi kihalali, zifanyiwe marekebisho ama zifutwe kabisa. Mathalani Sheria ya vyombo vya habari, Sheria ya makosa ya Kimtandao ya mwaka 2015 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019 pamoja na sheria ya Uchaguzi. Sheria hizi zinapaswa zitazamwe upya kabisa.

Yani sijui tufanyaje, lakini natamani sheria hizo zitungwe kwa kufuata maoni ya wadau wa nyanja husika pamoja na kuwahusisha katika mchakato mzima. Isitokee kama ilivyokuwa katika tume ya Warioba (watu wakatoa maoni yao wee, mwisho wa siku rasimu ikapigwa chini). Hizi sheria ndio muongozo wa wananchi katika shughuli zao za kila siku, sasa kwanini ziwazibie fursa ya kufika pale wanapopataka kimaendeleo kwa wepesi?

Ukiwa kiongozi wa umma, maana yake ni kwamba unawajibu kwa umma kupitia katiba kuhakikisha unalinda maslahi ya umma kwanza (sio chama wala kikundi fulani cha watu). Ndio maana viongozi wote hula kiapo cha Utumishi wa Umma kabla ya kuanza kutekeleza majukumu yao kisheria. Kile kiapo kina maana kubwa sana. Nawaasa viongozi wetu tuteteeni sisi tulio UMMA wa Watanzania. “Sauti ya Umma ni Sauti ya MUNGU” wamesema wahenga. Lakini kwa kuwa kuna Serikali, basi shida/malalamiko/changamoto zetu nyinyi viongozi mnapaswa kuzipaza katika baraza letu rasmi la wananchi (BUNGENI) na kuhakikisha zinafanyiwa kazi. Wawakilishi wetu huko Bungeni, mnatakiwa mfahamu kuwa ni wajibu wenu kutetea maslahi ya Wananchi KWANZA kabla ya Chama au kikundi fulani cha watu. Kuwa kiongozi wa umma ni wito na ni mzigo mzito.

Huwa nashangaa sana kusikia baadhi ya watu wanatumia nguvu kubwa na rushwa ili kupata uongozi wa umma. Watu hao hawatufai kabisa. Kuna muda natamani hata ikiwezekana mishahara na posho za Wabunge na viongozi wanaochaguliwa na wananchi iwe ni ile ya kiwango cha serikali. Yaani kila kiongozi aliyeapa kile Kiapo cha Utumishi wa Umma, alipwe kutokana na elimu yake na uzoefu wa kitaaluma. Mfano; Kiongozi huyu ana shahada, basi alipwe mshahara unaostahili kulipwa mtu mwenye shahada, kadhalika mwenye stashahada, cheti na kadhalika. Yasiwepo yale mambo ya kwa kuwa huyu ni Mbunge basi makusanyo yake kwa mwezi yawe ni milioni 12 au vitu kama hivyo. Kwa kuwa Sisi kama wananchi tuna vyombo vyetu vya ulinzi na usalama. Tafadhali vyombo vyetu mtusaidie kuwabaini watu hao na kuwazuia wasitulaghai na kupora chombo chetu kikuu cha maamuzi (Serikali). Tunawashukuru kwa kazi kubwa mnayoifanya usiku na mchana. Lakini tunawaomba mjiepushe na wanasiasa. Nyinyi ni watu muhimu sana kwetu sisi Umma wa Watanzania. Nyinyi ndio Taa yetu gizani na viatu vyetu kwenye miiba. Tunawategemea sana.

Mwisho, Kuondokewa na Rais wetu Mh. Dr. John Pombe Magufuli ni pigo kubwa kwa Taifa zima. Tumeumia sana kwa kuwa Rais wetu bado alikua na mipango na miradi mingi ambayo alitamani kuisimamia na kuiona ikiisha kwa mafanikio. Tumeumia sana. RIP Rais wetu Magufuli.

Lakini kwa kuwa sisi Tanzania ni Taifa imara, Mungu atatupitisha salama katika kipindi hiki na kwa uimara wetu tutayaendeleza mema yote ambayo Rais wetu ametuachia. His Legacy will live among us forever. Tuchape kazi. Tuirekebishe na kuilinda mifumo yetu. Tujivunie Utanzania wetu. Sisi ni Wamoja Daima.