Tarehe 22 June, wakati natangaza maandalizi ya ujio wa OFA hii kupitia Whatsapp, alinijia rafiki yangu mmoja anaitwa Freddy. Yeye ni mfanyabiashara wa viatu pale magomeni. Akaniuliza, “Mimi huwa napost viatu vyangu kupitia whatsapp na Instagram, sasa hio website mimi itanisaidia vipi?”
Website inakupa Utambulisho halali na kudumu mtandaoni. Yani website ndio ID muhimu ya biashara yako kama ilivyo ID yako ya NIDA.
Website inawafikia watu wengi zaidi ambao wanaweza kuwa wateja wako kuliko whatsapp ama Instagram.
Kumbuka website ikiwa hewani inapatikana dunia nzima na wengi wataoifungua ni wanakuwa na interests na bidhaa/huduma yako.
Zaidi unaweza kutembelea tovuti yetu kupitia link zilizowekwa hapo juu ili kuzipata makala hizo na kuongeza maarifa.
Fast forward.. Sasa bwana Freddy nilipomueleza hayo akapata shauku sana ya kufungua tovuti yake, lakini bahati mbaya hakua na pesa ya kutosha kupata OFA hii, Hivyo nikaamua yafuatayo;
OFA hii itawafikia wafanyabiashara watano TU kutoka watatu waliopangwa kufikiwa mwanzo.
Muda wa kurequest OFA hii ni kwanzia leo Ijumaa mpaka Jumatatu asubuhi. Baada ya hapo hakutakuwa na OFA tena.
Malipo ya kupata OFA hii yatakuwa katika mtindo wa 300k advance, na 200k italipwa kazi itakapokamilika.
OFA ITAKUPATIA HAYA:
Website kamili ya biashara yako.
Maintenance BURE mwaka mzima.
Business Cards 50 BURE.
Tutakufanyia SEO Bure mwaka mzima ili tovuti yako ipatikane Google mtu yeyote atakapokutafuta..
Kama una swali kuhusu chochote, Tafadhali niulize nami nitakuhudumia kama inavyostahili.
Dunia ya leo inatawaliwa na Mapinduzi ya 4 ya Viwanda yanayoongozwa kwa Teknolojia, hivyo kuwa na website katika biashara yako ni muhimu sana. 85% ya vijana hutumia intaneti kwa matumizi yao ya kila siku. Kama ni hivyo, basi website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako? Fuatilia makala hii ya leo mpaka mwisho kufahamu zaidi..
Katika makala yetu iliyowasilishwa hapa mnamo June 25, mwaka 2020 ilieleza kwa mapana kuhusu KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO, yaani kwanini uwe na website katika biashara yako leo hii? Hata hivyo leo hii tutazitazama na kuzichambua kazi sita (6) tu muhimu zaidi za website katika biashara yako. Faida nyingine nyingi kuhusu website huwa tunaziweka kwenye status zetu za WhatsApp kwa kugusa namba yetu hii hapa 0765834754. Save hio namba kisha tuma ujumbe wenye jina lako ili uanze kufaidi tips, updates, ushauri na huduma nyingi kutoka Rednet Technologies.
Unajua website inakupa faida zipi katika biashara yako? Ungana nami leo mpaka mwisho wa makala hii tuchimbue kila kitu. Twende kazi..
Sasa, website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako leo?
Mtandao wa Google ni sehemu kubwa na muhimu ya kutoa huduma hio ikifuatiwa na injini zingine kama Bing na Yahoo. Website inakupa utambulisho rasmi na usio na shaka kwa mtu yeyote duniani.
Hivyo usipoweka biashara na mawasiliano yako mtandaoni, hakuna mtu atajua kuwa biashara yako ipo hai. Website huziambia Injini za matafuto (Search Engines) kama Google kuwa biashara inafanya kazi fulani na huonyesha pia mawasiliano yako, hii huwezeshwa na mfumo wa matafuto na ulinganifu uitwao Search Engine Optimization (SEO). Hapa pia kuna tips na updates nyingi zaidi huwa tunashare kupitia namba yetu ya WhatsApp umeiona pale juu.
Kama biashara haipatikani kwenye matafuto ya kimtandao, inamaanisha biashara hio haipo mtandaoni. kufahamu kwa mukhtasari kuhusu SEO fuatilia makala hii hapa chini;
2. ENGAGEMENT(USHIRIKA): Uwepo wa tovuti mtandaoni huongeza Ushirika kati yako mtoa huduma/bidhaa na wateja wako wote. Tovuti hutengeneza mahali mahususi kwa wateja kushiriki kwa kuelimika kuhusu bidhaa/huduma, kutoa maoni, kero, kununua na kuwasiliana na muuzaji kirahisi.
Tovuti bora hutoa fursa kwa mteja kuuliza kuhusu bidhaa/huduma, kuomba appointment, kutoa maoni au/na kujifunza zaidi kuhusu bidhaa/huduma zinazopatikana katika biashara hio. Hakika huyu ndiye mfanyakazi unayemtaka kwenye biashara yako, ambaye yupo macho 24/7 kuhudumia wateja wako.
3. KUKUSANYA WATEJA: Kama kuna mahali unaweza kutega nyavu ya kuvua wateja wengi kirahisi, basi ni kwa kumiliki website ya biashara yako. Hii hukutaarifu pale mteja atakapokutafuta kupitia mawasiliano ambayo yamewekwa kwenye website.
Pia unaweza kukusanya data kuhusu mwenendo wa idadi ya watu wanaotembelea tovuti yako na hivyo kujua biashara yako inakuwa kwa kiwango gani. Hii huwezeshwa kwa kupitia kipimo cha Google kiitwacho Search Console ambayo hutoa taarifa kuhusu mwenendo mzima wa wateja wanaotembelea tovuti ndani ya wiki, mwezi, robo na mwaka mzima. Haya yote yanawezeshwa kirahisi sana unapotumia huduma za internet na teknolojia za Google. Kufahamu zaidi kuhusu hili fuatana na makala hii hapa chini:
4. KUOKOA MUDA: Website yako inakusaidia kuokoa muda na pesa kama mfanyabiashara. Hebu fikiria maelezo ambayo inakubidi kuyatoa kila mara kwa kila mtu unayekutana naye kuhusu biashara yako. Lakini mara hii hilo halipo tena. Website yako itafanya kazi hio 24/7 bila kuchoka. Hakikisha tu unalo bando la huduma za internet ili kukurahisishia kutoa taarifa muhimu kuhusu bidhaa na huduma unazotoa kupitia kurusa za website yako. Hii ni kwa sababu Bando lako ni Mtaji tosha kabisa katika kuokoa muda na kuimarisha website yako.
5. KUWAFIKIA WATU WENGI ZAIDI: Website inakupa nafasi ya kuwafikia watu wengi sana ndani ya muda mfupi. Fikiria namna unavyoweza kutembelewa na wateja wengi kama inavyoonekana kwenye picha hapa. Je ungeweza kufanya haya mwenyewe? Hii ndio njia bora kutanuka haraka kibiashara. Hapa ukitumia vizuri Nguvu ya Mitandao ya Kijamii kwa hakika utaweza kuwafikia watu wengi sana ndani ya muda mchache.
6. FAIDA YA KIUSHINDANI: Kama unahitaji kuwa na watu wa uhakika ambao watakutafuta ili wawe wateja wako wa kudumu na kuwashinda washindani wako katika biashara, basi bila shaka unahitaji kuwa na Website. Website yako lazima iwe na taarifa zote muhimu kuhusu bidhaa/huduma zako.
Hapa ndipo unapokuja kujitofautisha na washindani wako na kuweza kuwashinda. Hakikisha website yako inasheheni taarifa muhimu zote, si zile unazozijua wewe, lakini ziwe zile ambazo mteja atazihitaji kuhusu bidhaa/huduma unazotoa. Makinika vizuri hapa.
Zaidi ya yote, Website yako ni Bango namba moja katika kuitangaza Biashara yako. Website Inakusaidia sana katika kutangaza bidhaa/huduma zote ambazo unazitoa. Ukiwa na website gharama ya kujitangaza kupitia televisheni au kuwalipa watu hushuka maradufu. Shukrani kwa website. Kuhusu namna bora ya kuitangaza biashara yako fuatana na makala hii hapa kujua kwa undani.
Leo bila shaka umepata majibu muhimu kuhusu website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako? Tips, Updates na Ushauri mwingine tunaendelea kuutoa BURE kabisa kupitia Status zetu za WhatsApp kwa kugusa namba yetu hii hapa 0765834754. Hakikisha umeisave halafu tuma ujumbe wenye jina lako uanze kujua zaidi kuhusu Faida na Umuhimu wa Website katika biashara yako.
Una maoni au lolote kuhusu website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako? Tafadhali, acha comment yako hapo chini na changia hoja yako. Karibu sana.
Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?
Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.
Hebu fikiria wewe ni mgeni mahali fulani, baada ya kushikwa na njaa unaelekezwa migahawa miwili, mmoja ukiutafuta mtandaoni unaweza kupata taarifa zake mwingine hauna taarifa yoyote mtandaoni. Uelekeo wako utakuwa upande gani? Leo sasa tutakwenda kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako. Makinika mpaka mwisho wa makala hii.
Kuishi katika ulimwengu wa kidijitali, tovuti ni zana muhimu sana katika biashara na masoko ya kidijitali. Cha kushangaza inakadiriwa 35% – 50% ya biashara ndogondogo duniani hazina tovuti zao binafsi, jambo linalozinyima fursa ya kuweka taarifa zao kirahisi mtandaoni na kupata wateja wapya kirahisi.
Kuna wanaosema kuwa matumizi ya Tovuti yanamezwa na uwepo wa mitandao ya kijamii ambayo pia watu wanaweza kuweka na kutangaza biashara zao humo. Ni kweli, aghalabu, kwa kutumia Mitandao ya kijamii hauna uhakika wa kumiliki taarifa na maudhui unayoweka humo muda wote. Watengenezaji ambao pia ni wamiliki wa Mitandao hio wanao uwezo wa kusimamisha/kufuta akaunti au maudhui yako muda wowote ikiwa biashara/maudhui yako yanakwenda kunyume na matakwa na masharti yao.
Vile vile Mitandao ya kijamii unayotumia inaweza kupungua umaarufu au kufilisika muda wowote usioutegemea mfano kuna mitandao ilikua maarufu sana zamani kama Hi5 lakini umaarufu wake kwa sasa umepungua au kupotea kabisa. Hivyo, uwezekano wa kudorora kwa biashara yako kunategemea pia umaarufu wa mtandao wa kijamii unaoutumia, jambo linalichangiwa sana na ujio wa mitandao mipya ya kijamii kama Instagram, Whatsapp na TikTok. Hii kwako unaionaje? Nitaeleza Tofauti katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Tovuti wakati Ujao.
Faida ni nyingi sana za matumizi ya website katika kuimarisha biashara yako kupitia ulimwengu wa Teknolojia. Tayari tumekuandalia makala maalum kupitia link hii hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.
Leo hii ntakwambia mambo 10 kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika biashara yako:
1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:
Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu huenda wapi kutafuta vitu kama suppliers, bidhaa na huduma mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi. Injini za matafuto mtandaoni zimekuwa kimbilio namba moja huku GOOGLE Ikiziacha mbali Injini zingine kama Yahoo, Bing na Ask. Maana yake hii ni kwamba kama huna tovuti, jua mauzo yako ni 7% tu ya soko zima ambalo hujui kuwa unalo. Upo apo? Yani unapoteza 93% ya mauzo yako kila siku bila hata wewe mwenyewe kujua.
2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)
Kama una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo. Kwa biashara zenye malengo makubwa kuwa na tovuti huwaweka kwenye nafasi za juu katika kupata tenda na wateja, na huonyesha Uweledi bora katika utendaji wa biashara kuanzia katika muonekano na utendaji wa tovuti. Inakadiriwa 80% ya watu duniani huonyesha kutokua na imani na Biashara ambazo hazina tovuti pale wanapotaka huduma/bidhaa fulani mtandaoni.
3. KUPATIKANA KWA URAHISI
Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi, tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako. Ndivyo ilivyo kwa tovuti ambayo inajieleza kwa kila kitu kama ilivyo tovuti maridhawa ya http://rednet.co.tz . Ile raha ya kupata taarifa, huduma au bidhaa kirahisi kupitia simu yako ya mkononi, hufanya wateja waongezeke maradufu na kusambaza sifa bora kwa uharaka sana katika jamii na katika mitandao ya kijamii hali kadhalika.
Hii huongezwa chumvi ya SEO (Search Engine Optimization) ambayo ni teknolojia iliyowekwa katika Injini za matafuto ya kimtandao inayowasiliana na tovuti yako na kuweka taarifa katika Injini hizo na hivyo kufanya taarifa za tovuti yako kuonekana haraka zaidi katika matafuto. Biashara imerahisishwa sana kupitia SEO kuliko kutumia Mitandao ya kijamii. Kama watu wanakwenda Google kutafuta taarifa, basi fahamu taarifa hizo hupelekwa hapo GOOGLE kwa kutumia teknolojia iitwayo S.E.O. Kufahamu zaidi kuhusu SEO gusa hapa chini
Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo huduma ya internet inapatikana. Tangazo la bure kabisa hili. Kama tovuti yako ina ubora wa kuvutia zaidi katika muonekano, maudhui na utendaji, basi bila shaka biashara yako ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri sokoni na kupata wateja wengi kila siku. Jiulize hivi, unapofunga ofisi/biashara yako wakati wa jioni kila siku, wateja wapya wanaweza vipi kupata taarifa sahihi muda watakaohitaji?turudi kwenye mada yetu, kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Hii pia inawezeshwa sana na teknolojia ya S.E.O.
5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)
Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa. Kupitia tovuti yako, unaweza kuweka testimonials kwa idadi uitakayo bila kurudia rudia na katika mpangilio maalum na watu wakaweza kuona ushahidi utakaowaridhisha kuendelea kutumia huduma/bidhaa zako. Mara nyingi Mitandao ya kijamii huzuia kuoneka kwa biashara kwa urahisi kutokana na wimbi la watumiaji wenye maudhui tofauti tofauti katika ratiba ya saa (timeline) yako unayopitia katika mitandao hio, hivyo kusababisha usumbufu (distractions) katika biashara yako.
6. UAMINIFU (TRUST)
Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza mahusiano na mteja kama UAMINIFU. Ili kupata wateja wa kudumu katika sekta nyingi, kuwa na tovuti hai ni muhimu katika kudumisha mahusianao katika ya mfanyabiashara kwa muda wowte mteja atakaohitaji.
7. POSITIVE ROI
Ikiwa ni Return On Investment (ROI) au Rejesho baada ya Uwekezaji, unapoendesha biashara ambayo ina gharama zake kama umeme, kodi, maji, mafuta n.k, ukijiuliza utaweza vipi kurudisha gharama hizo upate faida? Njia moja nzuri ni matumizi ya tovuti bora yenye uwezo kunasa wateja wapya kwa njia ya mtandao muda wote (24/7) kirahisi kabisa.
8. THAMANI INAYODUMU
Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote itakapohitajika kufanya hivyo. Hivyo thamani ya biashara yako itaendelea kuwepo muda wote tovuti yako inapokuwa hewani.
9. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA
Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei, ushauri nakadhalika. Hivyo kuimarisha mahusiano na ukaribu wako na wateja wako wakiwa popote duniani kwa urahisi kupitia miundombinu mbalimbali unayoweza kuiweka katika tovuti yako kama matumizi ya chatbots na barua pepe maalum za kibiashara (zenye jina/domain name ya tovuti yako).
10. MASIJALA (DATA CENTER) RAHISI YA MTANDAONI
Tovuti yako inaweza pia kuwa masijala rahisi kwa wafanyakazi, wateja na mtu yeyote anayehitaji kujua taarifa kuhusu huduma/bidhaa unazohusika nazo. Mfano mzuri ni tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz ambayo zaidi tu. ya kwamba inatoa taarifa kuhusu huduma tunazohusika nazo za kutengenza websites, softwares, apps n.k, lakini pia tovuti inatoa taarifa muhimu mbalimbali kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia. Taarifa hizi zimetengenzwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha Biashara za wateja wakiwa popote duniani. Pia taarifa hizo zinalenga kuhamasisha matumizi ya Teknolojia katika njanja mabimbali za kiuchumi haswa kwa wafanyabiashara waliopo kusini mwa jangwa la Sahara.
NOTE: Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa muhimu kama jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.
BONUS POINT: Tovuti yako unapoisajili, unashauriwa pia upate kirurushi cha barua pepe yenye jina/domain name sawa na tovuti yako. Mfano, tovuti yako inapatikana katika anwani ya www.mfano.com, hivyo barua pepe yako ya kiofisi unaweza kuchagua kuwa info@mfano.com au maulizo@mfano.com au jinalako@mfano.com. Kwa kutumia barua pepe zenye jina sawa na anwani ya tovuti yako, unajiweka katika nafasi nzuri ya kuimarisha biashara yako na kuongeza wateja wapya na kazi zenya manufaa haraka zaidi katika biashara/kampuni yako. Hii ni sababu muhimu sana unapojiuliza kwanini ni muhimu kuwa na website (tovuti) rasmi ya biashara yako. Website inakufanya unakuwa official kiukweli kweli.
Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna bora za kuimarisha uchumi wa biashara yako kwa kutumia Teknolojia:
Umejifunza nini kupitia makala hii ya kuhusu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Tafadhali unaweza kuwasilisha maoni yako kupitia sanduku la maoni (comments box) lililo hapo chini au kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yanayopatikana katika Footer Bar chini kabisa ya ukurasa huu. Pia usisite kuwashirikisha wenzako makala haya kwa kushare link yetu ya https://rednet.co.tz mara zote. Karibu!
Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?
Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.