Tag: vijana na mitandao

mbinu ya ufungani (commitment) katika biashara

JITAFUTE KWANZA ILI UFANIKIWE

Mwaka 2017 wakati tunaanzisha Rednet Technologies tulikua na vision kubwa sana, kama ile watoto wadogo wanavyoota kuwa Marubani na Wanasheria. Hata hivyo kuifanyia kazi vision hio haijawahi kuwa rahisi. Jasho, Damu na Machozi haviepukiki. Mwaka 2020 nikagundua kwamba unatakiwa u jitafute kwanza ili ufanikiwe.

Vision ya Rednet Technologies ilikuwa ni “Kuhakikisha Tunawafikia Wafanyabiashara wote wadogo na wale wa kati wanaofanya shughuli zao katika eneo la Afrika Mashariki na Kati, na kuimarisha Biashara zao kwa matumizi ya Teknolijia za kisasa kutoka kwetu”.

Hio Vision inahitaji Maarifa, Ujuzi, Muendelezo (Consistency), Ubunifu na zaidi, Teamwork. Kama wewe ni mfanyabiashara na una ndoto za kufanikiwa katika shughuli zako basi hili la Teamwork unapaswa kulitazama kwa macho matatu. Leo tutachambua kwa undani hapa kwenye TEAMWORK.

Ile Team yetu ya kwanza tulitamani ingeweza kufanikiwa kuifikisha Rednet pale inatakiwa kufika. Lakini haikuweza kufanya hivyo. Hivyo, mwezi March, 2018 kwa huzuni kubwa Rednet Technologies ilisitisha Operations zake kwa kipindi cha Mwaka mzima mpaka May 2019. Kilikua ni kipindi kigumu mno kwangu binafsi kwa sababu mimi ndiye nilikua Visionary Leader.

Nilitamani sana Rednet Ifanikiwe, roho yangu ilikua ikiniuma sana kuona juhudi zangu hazikuwa zikizaa matunda. Kila mbinu niliyokua naitumia haikunipa majibu ya kufurahisha. Nilikata tamaa kabisa. Hata hivyo hio 2019 tulipata kazi chache za kuwahudumia wateja wetu, lakini bado hatukuweza kutanua vizuri mtandao wa wateja wetu na kushirikiana nao kwenye shughuli zao vile inavyotakiwa.

Hali hii ilikwenda mpaka Octoba, 2020, kabla ya ule Uchaguzi Mkuu ndipo ambapo ndugu yangu wa zamani sana, JEOFFREY alinipa idea ya kimapinduzi sana.

JEOFFREY NI NANI?

Huyu Jeoffrey ni rafiki yangu wa zamani sana. Tulisoma wote shule ya msingi japo yeye alinizidi darasa moja. Na zaidi tuliishi wote mtaa mmoja kwa kipindi kirefu sana katika maisha yetu, zaidi ya miaka 18. Kipindi chote icho sikuwahi kujua kuwa mfumo wake wa biashara utanifaa.

Huyu jamaa ana biashara yake ya kusambaza vifaa vya miundombinu ya maji kama koki, elbows, mabomba n.k. Zaidi yeye amejisajili kwenye mfumo wa manunuzi ya serikali (TaNEPS). Huko anapata tenda nyingi sana kuhusu miradi ya maji ya serikali nchi nzima. Kifupi anafanya vizuri sana sokoni.

Hio siku sasa alinijia akihitaji nimtengenezee ecommerce website ili kusudi aweze kuuza bidhaa zake kwa rejareja kwa wateja wake walio nje ya mfumo wa manunuzi. Hivyo akanipatia nyaraka za wasifu wa kampuni (Company Profile) yake. Sasa wakati naifanya hio kazi yake nikawa najiuliza, hivi mimi nashindwaje kutanuka kama jamaa yangu hapa. Hapa kuna kitu muhimu sana, jitafute kwanza ili ufanikiwe.

Najua hata wewe unayesoma unajiuliza hili swali “NAWEZAJE KUTANUA BIASHARA YANGU?” Well, kupitia vikao vichache nilivyokaa na huyu jamaa yangu, nikaweza kugundua namna ambayo tunaweza kusambaza Bidhaa na Huduma zetu kwa watu wengi na kwa haraka zaidi.

Hivyo, tukaanzisha Huduma ya Kusambaza Vifaa vya Ofisini na Computer kama mafile, diaries , flash disks, antivirus na vitu vya stationery unavyovijua. Wateja wetu wakubwa tuloanza nao walikua ni makampuni na taasisi ambazo kimsingi wametupa ushirikiano mkubwa sana.

Tumekuwa tukipokea Oda kutoka sehemu mbalimbali na tumeweza kukuza mtandao wa wateja wetu haraka na kwa ufanisi mkubwa kupitia huduma hii. Jambo hili likatulazimu kwenda mbele zaidi ambapo sasa kupitia tovuti yetu ya https://rednet.co.tz unaweza ku-request oda na tukakufikia.

Urafiki wetu na Jeoffrey ukazidi kuota mizizi ambapo sasa tunashirikiana kwenye mambo mengi sana ya kikazi. #VijanaWenzangu mimi huwa nawaambia “Tutumiane vizuri katika shughuli zetu za kiuchumi. Delegate your tasks kwa kuwa baraka zipo kwenye KUTOA zaidi kuliko kwenye KUPOKEA“.

Mimi rafiki zangu nawapa michongo mingi sana, ya muda mrefu na ile ya muda mfupi. Kadhalika rafiki zangu wananipa michongo mingi sana, ya muda mrefu na ile ya muda mfupi. Wataalam wanakwambia “Your Network is Your Net worth“. Kuna maana kubwa sana kwenye huo msemo ukitafakari.

Kama connections ulizonazo hazikutumii vizuri sasa usilalamike, watumie wewe kwenye mishe zako. Yes, maana hai-make sense kuwajua watu wazuri wanaoweza kuipush biashara yako halafu huwatumii eti kwa kuwa wao hawakutumii kwenye mishe zao. How? Make sure you get upper hand on it.

KARIBU KATIKA HUDUMA MPYA:

Website yetu sasa tumeiweka ili kusudi kukupa wewe uwezo wa kuchagua huduma unayotaka kisha sisi tutapata request yako, tutakutumia Quotation ukiridhia tunakupatia huduma yako katika muda ambao utapanga wewe. Upewe nini zaidi?

Kwa vifaa vya Ofisini (stationeries) kama wino wa printa, flash disks, rim paper, peni (box) n.k gusa link hii https://rednet.co.tz/services/your-order/… Link hio itakupeleka direct kwenye ukurasa utakaokupa nafasi ya kutuambia huduma unayohitaji ukiwa popote Duniani.

Pia tumekuletea huduma mahsusi kwa ajili yako iitwayo “JIHUDUMIE” kupitia link hii https://rednet.co.tz/services/jihudumie-leo/… ambapo humo ndani utajipatia huduma kama zinavyoonekana kwenye picha hapa.

CHANGAMOTO:

1. KUWA RASMI: Najua watu wengi humu mitandaoni biashara zenu si rasmi, kwa maana ya kwamba hazijasajiliwa katika Mamlaka za Kiserikali (BRELA, TRA, HALMASHAURI, BENKI etc). Sasa mtindo huu wa Usambazaji unakutaka kusajili biashara yako kwa kuwa biashara/kampuni yako sasa inakwenda kufanya kazi na biashara/kampuni zingine (B2B). Matumizi ya Quotations, Proforma Invoice, Tax Invoices, EFD receipts na Delivery Notes kwenye mtindo huu wa Biashara ni kama Katiba katika utawala wa Nchi. Eneo hili kama Mjasiriamali unapaswa kuwalo makini sana yani.

Hivyo ifanye biashara/kampuni yako kuwa rasmi kwanza ili kujihakikishia unafanya shughuli zako bila kubughudhiwa na mtu yeyote.

2. UCHELEWESHWAJI WA MALIPO: Kuwa msambazaji/Supplier maana yake ni kwamba unafanya kazi kwa pesa yako na pesa hio utaingiziwa baada ya mwezi mmoja mpaka miezi sita. Hivyo, kukaa muda mrefu bila kuingiziwa pesa si kazi ndogo, uvumilivu lazima uchukue nafasi yake hapa.

3. MTAJI: Kama ulivyoona hizo changamoto zingine hapo juu, kufanya usambazaji lazima uwe na Mtaji wa kutosha kuweza kuhudumia Wateja wako kikamilifu kabla wao hawajakuingizia pesa siku za mbeleni. Hapa lazima uwe na pesa ya kufanya kazi mkononi ili usije ukatolewa katika game.

Hata hivyo, changamoto hizi hazitakiwi kukurudisha nyuma, katika harakati jitafute kwanza ili ufanikiwe lazima uhakikishe unapambana kwa njia zozote ili kusudi mafanikio yako yakapate kujidhihirisha. #VijanaWenzangu muda wa kupambania future zenu ndio sasa. Pambaneni haswa.

ijue nguvu ya mitandao ya kijamii katika biashara

IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA

Zama hizi kuhoji umuhimu wa mitandao ya kijamii ni sawa na kuhoji umuhimu wa mwanga wa Jua duniani. Google, Facebook, Twitter, Instagram na Whatsapp ndio injini za biashara mitandaoni. Kivipi? Sasa kwenye makala ya leo nataka ijue nguvu ya mitandao ya kijamii katika biashara hio unayoifanya. Twende pamoja mpaka mwisho.

Imefika muda sasa, mitandao ya kijamii si sehemu ya anasa tena bali ni nyenzo muhimu katika uendeshaji wa biashara. Sasa imekuwa rahisi kuwasiliana na wapendwa wetu wakiwa popote duniani, tena kwa gharama ndogo sawa na bure. Pia imekuwa rahisi sana kuwasiliana na wateja wapya.

Mpaka kufikia January 2018 duniani kulikua na watumiaji wa huduma za internet takriban 4.02 bilioni, sawa na 53% ya idadi nzima ya watu. Kati ya hao, watumiaji wa mitandao ya kijamii wanafikia 3.2 bilioni sawa na 42% ya watu wote duniani. Hii ni kwa mujibu wa jarida la Forbes. Hapa Tanzania mpaka kufikia mwezi Mei 2021 kumeripotiwa kuwa na watumiaji wa huduma za intaneti zaidi ya milioni 29. Huku watumiaji wa huduma za kifedha kwa njia ya kielekroniki wakifika milioni 32, chanzo TCRA.

#VijanaWenzangu kama wewe ni mfanyabiashara basi bila shaka namba hizi huwezi kuzipuuza. Utafiti huo kwako unapaswa kuwa ni hazina katika biashara zako ambayo utaitumia kwenye kusaka wateja wapya, kuwasiliana nao, kuwaongeza na kuhakikisha wanabaki kuwa wateja wako.

Matangazo ya televisheni na redio yanakwenda kufa kifo cha taratibu. Mitandao ya kijamii inateka jukwaa la Ushindani wa biashara hasa katika idara ya Masoko na Mauzo. Kama hutumii mitandao ya kijamii kwa kukuza na kuimarisha biashara yako basi jua uko nyuma sana kiushindani.

Kujua kwanini unapaswa kuitangaza biashara yako, fuatana na Makala hii hapa KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?. Sasa ukishajua sababu hizo, Leo tunakwenda kujua Kwanini Utumie Mitandao ya Kijamii kama nyenzo muhimu katika biashara yako. Makinika.

MANUFAA YA MITANDAO KATIKA BIASHARA:

Kama umekuwa ukijiuliza “Hivi hii akaunti yangu ya twitter/instagram/facebook naweza vipi kuitangazia biashara zangu? Hivi nitaweza kweli?” Basi leo tuzione faida muhimu za mitandao ya jamii katika kuimarisha biashara.

i. KATIKA KUKUZA BRAND: Kwa mujibu wa mtandao wa “We Are Social’s Digital” mwaka 2018 ilionekana kwamba Facebook ndio mtandao wa pili ambao unafuatiliwa zaidi duniani, ukifuatiwa na mtandao wa Youtube. Kwenye hio orodha mtandao wa Google ndio ulikua unaongoza kwa kufuatiliwa.

Hii ina maanisha kuwa, watu wanatumia muda mwingi mtandaoni. Mitandao hio pia hutumika kama vyanzo vya taarifa kuhusu bidhaa/huduma za biashara/kampuni/shirika fulani. Facebook peke yake ina zaidi ya kurasa (Pages) milioni 60 ambazo hutumika kama Brands za biashara mbalimbali kila siku. Hapa sasa ndipo unapo ijue nguvu ya mitandao ya kijamii katika biashara.

nguvu ya mitandao ya kijamii

Katika mtandao wa twitter pia mambo ni moto. Kwa mujibu wa @Twitter Sababu kuu ya watu kutumia mtandao wa twita ni “kugundua jambo jipya na/au la kusisimua”. Haya hebu tuambie hapa, wewe ni nini kilikufanya kuanza kutumia mtandao wa twita? Ile sababu ya watu kupata kitu kipya imefungwa kwenye design ya twita ambayo inawafanya watu wapate taarifa na mambo mapya na yenye kusisimua ambayo haswa Biashara na makampuni yanavitafuta. Hivyo katika biashara mtandao wa twita unafaida zaidi kulinganisha na mitandao mingine kama Instagram na Quora kutokana na namna yake ilivyobuniwa.

ii. KATIKA KUJENGA UAMINIFU (LOYALTY): Mwaka 2017 utafiti uliofanywa kwa watu wa masoko 5,700 ulionyesha kuwa 69% sawa na watu 3,933 walijenga uaminifu kwa wateja wao kupitia matumizi kibiashara ya mitandao ya kijamii (social media marketing).

Vilevile 66% ya watumiaji wa mitandao wa umri kati ya miaka 18-24 ni waaminifu kwa akaunti wanazozifuatulia kwenye mitandao ya kijamii. 60% ya walio na miaka 25-34 hupendelea kutumia bidhaa/huduma za biashara wanazozifuatilia kupitia Facebook, Twitter na Instagram.

iii. KATIKA MAUZO: Mtandao wa “We Are Social’s Digital” umeripoti kuwa 17% ya idadi nzima ya watu duniani hununua bidhaa na kulipa bills kwa njia ya mtandao. Kwa kuwa % kubwa ya watumiaji ni wa umri kati ya miaka 18-34, hawa hufanya manunuzi kwa ushawishi wa mitandao ya kijamii. Hapa ni muhimu sana ukiwa na website yako. Kwanini, Kwasababu website yako inaelezea kiundani sana kuhusu biashara yako pamoja na bidhaa/huduma zake. Unawezaje sasa kupata website yako? Gusa hapa kujua utaratibu.

FAIDA ZA MITANDAO

Sasa twende kuziona faida ambazo mitandao ya kijamii inaweza kuiletea biashara yako na kuweza kukusaidia kukuunganisha na wateja, kushirikisha, kukuza na kuimarisha biashara yako zaidi.

1. KUKUZA UTAMBULISHO WA BIASHARA: Ikizingatiwa nusu ya idadi ya watu duniani ni watumiaji wa mitandao, kumbe basi matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii ni mbinu bora ya kuhakikisha biashara yako inajulikana zaidi duniani. Mfano tizama ilivyo ngumu kutangaza biashara mtaani katika kulipia gharama za matangazo ya televisheni na redio.

2. KUHUISHA BIASHARA: Siku hizi imekuwa ngumu sana kuamini bidhaa/huduma mpaka upate uthibitisho hai. Yaani uhakikishe hio biashara/kampuni ipo kweli na si matapeli. Hivyo, kupata wateja unatakiwa uonyeshe sehemu inayoishi (human side) ya biashara yako ambayo ni thamani ambayo biashara yako inaitoa kwa jamii. Mfano; hapa unaweza kueleza faida, umuhimu na namna za kutumia bidhaa/huduma yako. Elimu hii inapaswa iwe inatolewa mara kwa mara kupitia akaunti zako za mitandao ya kijamii. Mbinu hii hufanya biashara yako iweze kuishi katika maisha ya watu kila siku.

3. KUONGEZA TRAFFIC: Machapisho ya mitandaoni huchangia kwa kiasi kikubwa kuongeza traffic kwenye tovuti yako. Unaposhirikisha maudhui yaliyo kwenye tovuti kupitia machapisho unayoweka kwenye akaunti za mitandao unaiongezea thamani biashara kwenye shughuli za watu za kila siku kwa wao kuzidi kutembelea tovuti yako.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

4. KUONGEZA WATEJA: Bila shaka dhumuni lako kubwa la kufanya biashara kupitia mitandao ya kijamii ni kuongeza wateja. Sasa mitandao hii inakupa njia nafuu zaidi ya kupata wateja wa bidhaa/huduma yako.

5. KUWASILIANA KWA UKARIBU: Ule msemo wa “Dunia ni kama kijiji” umefanya iwe rahisi zaidi kupitia matumizi ya mitandao ya kijamii. Yaani kupitia mitandao, sasa unao uwezo wa kuwasiliana kwa ukaribu na wateja wako kuhusu ubora wa bidhaa/huduma, kiwango, malipo n.k bila kujali umbali.

Hii imefanya iwe rahisi kutoa Huduma Bora kwa Wateja na kuimarisha uhusiano na ushirikishwaji wa wateja katika kuzalisha bidhaa bora na zenye viwango pamoja na kuhudumu kwa weledi wa hali ya juu zaidi. Unaposhindwa kufanya hivi unajiweka kwenye nafasi mbaya ya kukosa wateja na kushindwa kimbinu na washindani wako katika biashara.

POINT YA ZIADA: Vilevile ni muhimu kujua watu wanasemaje kuhusu washindani wako kwenye biashara. Utajuaje? Ukifuatilia machapisho ya watu mbalimbali kuhusu washindani wako utagundua udhaifu na matamanio ya watu ambayo wewe unaweza kuyatumia ili kuvuta wateja wengi kwako.

Kwa dunia ya leo ya mtandaoni, mambo yanaenda kwa kasi sana. Na huwezi kukubali kuachwa nyuma kizembe. Mitandao imerahisisha kujua kipi watu wanahitaji kwa sasa na kipi watakihitaji kesho. Hivyo kuwa makini kwenye kufuatilia mahitaji ya wateja wako na soko zima kwa ujumla kwa sababu unapo ijue nguvu ya mitandao ya kijamii katika biashara unapata faida ya kushindana na washindani wengine na kuwashinda kirahisi.

Kiufupi kufanya biashara kupitia Mitandao ya Kijamii kunahitaji Mbinu na Ubunifu. Fanya vyote ulivyovipata leo kwenye makala hii katika mtindo wa MBINU na UBUNIFU. Uko na swali? Tafadhali tunakukaribisha kupitia comments hapa chini. Hakikisha una kushare ili makala hii iwafikie wengi zaidi.

Vyanzo: https://www.forbes.com/sites/forbescommunicationscouncil/2018/05/11/how-social-media-can-move-your-business-forward/?sh=60e12c604cf2

https://coschedule.com/blog/benefits-of-social-media-marketing-for-business

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu(website design, logo design, Digital consultacy n.k) BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

FAHAMU KUHUSU MAGEUZI YA ICT KATIKA UWANDA WA SIASA

Ama kwa hakika teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA/ICT) imeendelea kushika kasi katika nyanja mbalimbali za kijamii. Biashara zinazidi kuimarika, Jamii inaunganika, uchumi unainuka na Siasa inapata sura mpya. Muunganiko wa Siasa na Teknolojia unagusa michakato, wasifu za watu, jitihada za kujinasua katika changamoto mbalimbali pamoja na harakati zingine za kijamii zinazohusidha matumizi ya huduma za intaneti na ICT. Katika fumbo hilo wataalamu wa siasa wakagundua njia za kuboresha mifumo ya kisiasa na kuratibu ushawishi wao katika jamii kirahisi zaidi.

Sasa leo tuone maeneo 5 muhimu ambayo ICT imekuwa chachu ya maendeleo katika uwanda wa kisiasa barani Afrika, hususan Kusini mwa jangwa la Sahara:

1. KUBADILI TAWALA

Katika kipindi cha mwaka 2009-2012 katika nchi za kiarabu kulitokea kitu kilichoitwa “Vuguvugu la Kimapinduzi” au “Arab Spring” ambapo serikali nyingi za kiarabu zilijikuta zikipinduliwa kwa nguvu ya wanachi. Kufikia mwaka 2012 dunia ilikua na 61% ya nchi 195 ambazo ndizo zilikua zilitambulika kwa kufanya Chaguzi za Kidemokrasia. Hio ni sawa n nchi 118. Lakini bada ya hapo nchi zinazojiendesha kidemokrasia ziliongezeka kufuatia maandamano nchini Moldovia mwaka 2009, Tunisia (2010/11, Misri (2011) na Iran (2009 mpaka sasa) Mapinduzi hayo ya kubadili tawala hasa zile za Kiimla yalipangwa na kuanzishwa kwa msaada wa kiteknolojia huku mtandao wa Twitter ukihusika kukusanya na kuhamasisha watu kuanzisha vuguvugu la maandamano katika nchi za kiarabu. Hawa waarabu walijua kwelikweli kutumia mitandao.

2. KUTUNGA NA KUENDESHA SERA

Hivi sasa hakuna mtu asiyejua au kutumia mfumo wa malipo ya kiserikali wa eGovernment. Sasa unajua mfumo huo ulianzia wapi? Achana na siasa kabisa. Kwanza tuone hio eGovernment ni kitu gani? Huo ni mfumo wa matumizi ya ICT katika ofisi za umma inazohusisha mifumo ya kiutawala ya kiuweledi inayotumia maarifa na ujuzi wa computer na huduma za intaneti ili kuhakikisha huduma za kijamii zinaimarika na kuchochea demokrasia na nguvu ya ushawishi katika chaguzi za kisiasa na sera za jamii. Umeona siasa imerudi tena apo Wahenga wanakuambia, “Siasa ni kama maji tu, usipoyaoga utayanywa.” Wahenga bwana. Sasa mifumo hii ya eGovernance hutumiwa na taasisi za serikali katika kuhudumia Mashirika mengine ya kiserikali (G2G) mfano Polisi na TRA, Mashirika ya Kiserikali kwa wanachi(G2C) mfano LUKU na Mashirika ya Serikali kwa Biashara (G2B) mfano TRA na Wafanyabiashara. Hii sera ys kuanzishwa kwa mifumo ya eGovernance japo imeanzishwa kwa sera za kisiasa lakini imeleta mapinduzi makubwa sana katika zoezi la ukusanyaji wa mapato na utunzaji wa rekodi za mauzo na manunuzi.

3. SIASA KAMA SIASA

Japokuwa kwenye nchi nyingi haswa zile za kidikteta kumekuwepo na makatazo ya kufanya siasa za wazi, Matumizi ya Teknolojia na mitandao ya kijamii yamewezeshwa kufanyika kwa siasa pasi na haja ya kukusanya watu viwanjani. Matumizi ya mifumo ya computer na mitandao ya kijamii wamewsrahisishia Wanasiasa kutengeneza akaunti zao zinazowapa fursa ya kukutana na wananchi na kufanya siasa kirahisi sana. Hata hivyo hii bado ni changamoto kwa nchi nyingi zinazoendelea kama Tanzania ambapo watumiaji hai wa huduma za internet walikua ni 23.14milioni sawa na 38.7% ya wananchi wote. Pia watumiaji wa mtandao wa facebook wamefikia 4.27milioni. Taarifa hii ni kwa mujibu wa tovuti ya http://internetlivestats.com kufikia mwezi December, 2019. Sasa namba hizi zinakupa picha gani katika uwanda wa siasa nchini? Inaonekana kuwa bado watumiaji hai wa mitandao ya kijamii ni wachache kuwakusanya mtandaoni kwa wakati mmoja, hivyo kufanyika kwa siasa katika mitandao ya kijamii inaonekana bado ni mtihani kwa wanasiasa barani Afrika hasa nchini Tanzania. Licha ya changamoto hizo, bado teknolojia inao mchango wake katika siasa wakati wa kufanya kampeni na uchaguzi ukizingatia Haba na Haba hujaza kibaba. Hivyo katika kampeni za kisasa, ili mwanasiasa apate kuingia katika mfumo wa utoaji wa maamuzi wa Taifa (Legislative level). Hana budi pia awe na ushawishi wa kisiasa katika mitandao ya kijamii. Huko ndipo unakutana na wanachi kirahisi na kusambaziana taarifa mbalimbali kwa wepesi zaidi. Kama afanyavyo Mh. Hamis Kigwangwala tu katika mtandao wa twitter, interractions za mara kwa mara muhimu nyie.

4. ONLINE VOTING (e-Voters System)

Kama ulikua hujui basi mwaka 2005 nchi ya Estonia iliweka rekodi ya kuwa nchi ya kwanza duniani kutumia mfumo wa kimtandao wa upigaji kura (e-Voters System)na kwanzia hapo mfumo huo umekuwa ukisambaa katika nchi na maeneo mbalimbali duniani. Mfumo huu unahusisha sehemu 3 ambazo ni Mpiga Kura, Mamlaka za Usajili na Watu wa Kuhesabu Kura ambao wote hapa sasa hufanya kazi katika mifumo maalum ya kuhakikisha kura zinapigwa kimtandao na kwa usahihi na usalama wa hali ya juu. Hapa bwana usipokua makini wadukuzi wanaweza kupiga tukio uchaguzi ukaharibika ndani ya dakika kadhaa tu.

KWANINI ONLINE VOTING SYSTEM?

Wakati mfumo huu unatengenezwa na kuzinduliwa kwa mara ya kwanza nchini Estonia, lengo kuu lilikua ni kuhakikisha shughuli za uchaguzi zinafanyika kwa haraka, wepesi na kwa usahihi zaidi bila kuathiri shughuli zingine za kiuchumi. Lakini leo hii ambapo dunia inapitia katika changamoto ya Ugonjwa wa #COVID19, ipo haja na hitaji kubwa la matumizi ya e-Voters Systems katika chaguzi za kisiasa sehemu mbalimbali duniani. Wakati mamlaka zikikataza mikusanyiko ya watu, uvaaji wa barakoa, kutogusana na kuzingatia social distance (sijui kiswahili chake kwa kweli), hakuna wakati sahihi wa kuanza kutumia e-Voters Systems kama sasa. Wanaharati na wananchi kwa ujumla hatuna budi kupigia chapuo mgumo huu uanze kutumika mara moja ikiwezekana kuanzia uchaguzi wa Octoba 2020 sio tu kuhakikisha tahadhari dhidi ya Coron zinachukuliwa, lakini zaidi kuongeza Usahihi na Usalama wa kura katika zoezi la Uchaguzi.

5. MATUMIZI NA UCHAMBUZI WA DATA

Teknolojia kwa mapana yake imekua nyenzo muhimu sana katika kukusanya, kuchakata na kuhifanyi data mbalimbali ambazo hutumika maeneo kadha wa kadha katika kufanyia Tafiti, Kupima mwenendo wa mwanasiasa au chama pamoja na kuhifadhi kumbukumbu. Sasa matumizi ya mitandao kama Facebook, Instagram, Twitter pamoja na tovuti/blogu za wanasiasa/vyama, zimekuwa zikichochea sana juhudi na harakati zao katika kuhakikisha wanaboresha nafasi na ushawaishi wao wa kisiasa katika jamii wanazohudumu. Teknolojia imezidi kuwa muhimu sana katika uga huu wa kisiasa.

BONUS POINT:

Matumizi madogo ya teknolojia (hafifu) yameleta madhara makubwa sana katiks mifumo ya siasa hasa barani Afrika. Hizi vita za wenyewe kwa wenyewe, vurugu na wakati mwingine mauaji katika mchakato wa uchaguzi ni matokeo ya siasa mbovu na ufinyu wa teknolojia usiotakiwa.

Pia kuna hizi makala hapa tayari tumekuandalia ambazo zitakupa mwanga zaidi katika kufanya maamuzi na kutumia teknolojia ili kuleta tija zaidi. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/fanya-maamuzi-sahihi-katika-muda-sahihi/ yenye kichwa “FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI”
  2. https://rednet.co.tz/ifahamu-nguvu-ya-mitandao-ya-kijamii/ yenye kichwa “IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO”
  3. https://rednet.co.tz/biashara-yako-inaweza-vipi-kuwa-taasisi-imara/ yenye kichwa “BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA”

KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?

Hebu fikiria wewe ni mgeni mahali fulani, baada ya kushikwa na njaa unaelekezwa migahawa miwili, mmoja ukiutafuta mtandaoni unaweza kupata taarifa zake mwingine hauna taarifa yoyote mtandaoni. Uelekeo wako utakuwa upande gani? Leo sasa tutakwenda kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako. Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Kuishi katika ulimwengu wa kidijitali, tovuti ni zana muhimu sana katika biashara na masoko ya kidijitali. Cha kushangaza inakadiriwa 35% – 50% ya biashara ndogondogo duniani hazina tovuti zao binafsi, jambo linalozinyima fursa ya kuweka taarifa zao kirahisi mtandaoni na kupata wateja wapya kirahisi.

Kuna wanaosema kuwa matumizi ya Tovuti yanamezwa na uwepo wa mitandao ya kijamii ambayo pia watu wanaweza kuweka na kutangaza biashara zao humo. Ni kweli, aghalabu, kwa kutumia Mitandao ya kijamii hauna uhakika wa kumiliki taarifa na maudhui unayoweka humo muda wote. Watengenezaji ambao pia ni wamiliki wa Mitandao hio wanao uwezo wa kusimamisha/kufuta akaunti au maudhui yako muda wowote ikiwa biashara/maudhui yako yanakwenda kunyume na matakwa na masharti yao.

Vile vile Mitandao ya kijamii unayotumia inaweza kupungua umaarufu au kufilisika muda wowote usioutegemea mfano kuna mitandao ilikua maarufu sana zamani kama Hi5 lakini umaarufu wake kwa sasa umepungua au kupotea kabisa. Hivyo, uwezekano wa kudorora kwa biashara yako kunategemea pia umaarufu wa mtandao wa kijamii unaoutumia, jambo linalichangiwa sana na ujio wa mitandao mipya ya kijamii kama Instagram, Whatsapp na TikTok. Hii kwako unaionaje? Nitaeleza Tofauti katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Tovuti wakati Ujao.

Faida ni nyingi sana za matumizi ya website katika kuimarisha biashara yako kupitia ulimwengu wa Teknolojia. Tayari tumekuandalia makala maalum kupitia link hii hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

Leo hii ntakwambia mambo 10 kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika biashara yako:

1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:

Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu huenda wapi kutafuta vitu kama suppliers, bidhaa na huduma mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi. Injini za matafuto mtandaoni zimekuwa kimbilio namba moja huku GOOGLE Ikiziacha mbali Injini zingine kama Yahoo, Bing na Ask. Maana yake hii ni kwamba kama huna tovuti, jua mauzo yako ni 7% tu ya soko zima ambalo hujui kuwa unalo. Upo apo? Yani unapoteza 93% ya mauzo yako kila siku bila hata wewe mwenyewe kujua.

2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)

Kama una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo. Kwa biashara zenye malengo makubwa kuwa na tovuti huwaweka kwenye nafasi za juu katika kupata tenda na wateja, na huonyesha Uweledi bora katika utendaji wa biashara kuanzia katika muonekano na utendaji wa tovuti. Inakadiriwa 80% ya watu duniani huonyesha kutokua na imani na Biashara ambazo hazina tovuti pale wanapotaka huduma/bidhaa fulani mtandaoni.

3. KUPATIKANA KWA URAHISI

Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi, tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako. Ndivyo ilivyo kwa tovuti ambayo inajieleza kwa kila kitu kama ilivyo tovuti maridhawa ya http://rednet.co.tz . Ile raha ya kupata taarifa, huduma au bidhaa kirahisi kupitia simu yako ya mkononi, hufanya wateja waongezeke maradufu na kusambaza sifa bora kwa uharaka sana katika jamii na katika mitandao ya kijamii hali kadhalika.

Hii huongezwa chumvi ya SEO (Search Engine Optimization) ambayo ni teknolojia iliyowekwa katika Injini za matafuto ya kimtandao inayowasiliana na tovuti yako na kuweka taarifa katika Injini hizo na hivyo kufanya taarifa za tovuti yako kuonekana haraka zaidi katika matafuto. Biashara imerahisishwa sana kupitia SEO kuliko kutumia Mitandao ya kijamii. Kama watu wanakwenda Google kutafuta taarifa, basi fahamu taarifa hizo hupelekwa hapo GOOGLE kwa kutumia teknolojia iitwayo S.E.O. Kufahamu zaidi kuhusu SEO gusa hapa chini

4. TANGAZO LA BURE MUDA WOTE

Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo huduma ya internet inapatikana. Tangazo la bure kabisa hili. Kama tovuti yako ina ubora wa kuvutia zaidi katika muonekano, maudhui na utendaji, basi bila shaka biashara yako ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri sokoni na kupata wateja wengi kila siku. Jiulize hivi, unapofunga ofisi/biashara yako wakati wa jioni kila siku, wateja wapya wanaweza vipi kupata taarifa sahihi muda watakaohitaji?turudi kwenye mada yetu, kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Hii pia inawezeshwa sana na teknolojia ya S.E.O.

5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)

Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa. Kupitia tovuti yako, unaweza kuweka testimonials kwa idadi uitakayo bila kurudia rudia na katika mpangilio maalum na watu wakaweza kuona ushahidi utakaowaridhisha kuendelea kutumia huduma/bidhaa zako. Mara nyingi Mitandao ya kijamii huzuia kuoneka kwa biashara kwa urahisi kutokana na wimbi la watumiaji wenye maudhui tofauti tofauti katika ratiba ya saa (timeline) yako unayopitia katika mitandao hio, hivyo kusababisha usumbufu (distractions) katika biashara yako.

6. UAMINIFU (TRUST)

Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza mahusiano na mteja kama UAMINIFU. Ili kupata wateja wa kudumu katika sekta nyingi, kuwa na tovuti hai ni muhimu katika kudumisha mahusianao katika ya mfanyabiashara kwa muda wowte mteja atakaohitaji.

7. POSITIVE ROI

Ikiwa ni Return On Investment (ROI) au Rejesho baada ya Uwekezaji, unapoendesha biashara ambayo ina gharama zake kama umeme, kodi, maji, mafuta n.k, ukijiuliza utaweza vipi kurudisha gharama hizo upate faida? Njia moja nzuri ni matumizi ya tovuti bora yenye uwezo kunasa wateja wapya kwa njia ya mtandao muda wote (24/7) kirahisi kabisa.

8. THAMANI INAYODUMU

Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote itakapohitajika kufanya hivyo. Hivyo thamani ya biashara yako itaendelea kuwepo muda wote tovuti yako inapokuwa hewani.

9. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA

Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei, ushauri nakadhalika. Hivyo kuimarisha mahusiano na ukaribu wako na wateja wako wakiwa popote duniani kwa urahisi kupitia miundombinu mbalimbali unayoweza kuiweka katika tovuti yako kama matumizi ya chatbots na barua pepe maalum za kibiashara (zenye jina/domain name ya tovuti yako).

10. MASIJALA (DATA CENTER) RAHISI YA MTANDAONI

Tovuti yako inaweza pia kuwa masijala rahisi kwa wafanyakazi, wateja na mtu yeyote anayehitaji kujua taarifa kuhusu huduma/bidhaa unazohusika nazo. Mfano mzuri ni tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz ambayo zaidi tu. ya kwamba inatoa taarifa kuhusu huduma tunazohusika nazo za kutengenza websites, softwares, apps n.k, lakini pia tovuti inatoa taarifa muhimu mbalimbali kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia. Taarifa hizi zimetengenzwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha Biashara za wateja wakiwa popote duniani. Pia taarifa hizo zinalenga kuhamasisha matumizi ya Teknolojia katika njanja mabimbali za kiuchumi haswa kwa wafanyabiashara waliopo kusini mwa jangwa la Sahara.

NOTE: Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa muhimu kama jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.

BONUS POINT: Tovuti yako unapoisajili, unashauriwa pia upate kirurushi cha barua pepe yenye jina/domain name sawa na tovuti yako. Mfano, tovuti yako inapatikana katika anwani ya www.mfano.com, hivyo barua pepe yako ya kiofisi unaweza kuchagua kuwa info@mfano.com au maulizo@mfano.com au jinalako@mfano.com. Kwa kutumia barua pepe zenye jina sawa na anwani ya tovuti yako, unajiweka katika nafasi nzuri ya kuimarisha biashara yako na kuongeza wateja wapya na kazi zenya manufaa haraka zaidi katika biashara/kampuni yako. Hii ni sababu muhimu sana unapojiuliza kwanini ni muhimu kuwa na website (tovuti) rasmi ya biashara yako. Website inakufanya unakuwa official kiukweli kweli.

Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna bora za kuimarisha uchumi wa biashara yako kwa kutumia Teknolojia:

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. BRANDING vs MARKETING, KIPI NI KIPI?
  3. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA (AfCFTA), KUNA MANUFAA GANI KWAKO?
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO.

Umejifunza nini kupitia makala hii ya kuhusu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Tafadhali unaweza kuwasilisha maoni yako kupitia sanduku la maoni (comments box) lililo hapo chini au kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yanayopatikana katika Footer Bar chini kabisa ya ukurasa huu. Pia usisite kuwashirikisha wenzako makala haya kwa kushare link yetu ya https://rednet.co.tz mara zote. Karibu!

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

IJUE TEKNOLOJIA NA UMUHIMU WAKE KATIKA SERA YA KULINDA TAARIFA ZA MTEJA

Tarehe 12, August 2019 Benki Kuu ya Tanzania ilitoa rai kwa makampuni yanayotoa huduma za kifedha kwa njia ya kimtandao kuhakikisha wanaweka utaratibu wa kulinda taarifa za wateja wao kuhusu maswala ya kifedha kwa kutumia teknolojia. Akitoa changamoto hio katika hafla ya kufungua mkutano wa 19 wa Mafunzo ya Kibenki kwa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha, Kaimu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Dr. Benard Kibese amesema ” uaminifu wa mteja ndio thamani halisi kwa mtoa huduma wa masuala ya kifedha. Kama hivyo ni kweli, teknolojia peke yake inaweza vipi kulinda uaminifu huu? Kama ni kweli itaweza vipi? Kama hapana, wabobevu wa huduma za kifedha wanatakiwa kufanya nini ili kujenga uaminifu huu? Haya ni baadhi ya maswali mnatakiwa kujiuliza.” alisema Dr. Kibese. Hii ni kwa mujibu wa gazeti za The Citizen.

Sasa swali, huu utaratibu wa kulinda taarifa za mteja (Consumer Protection regulation) ni nini, na unamchango gani katika kukuza uchumi na biashara?

Kufuatia mtikisiko wa kiuchumi duniani mnamo mwaka 2008, wito wa uanzishwaji wa sheria ya kulinda taarifa za mteja kuhusu masoko ya kifedha umezidi kukuwa mkubwa na kupata ushawishi. Watunga sera na sheria duniani wamekuwa wakipewa changamoto za kutafsiri sheria hizo katika namna rahisi na za kiutaratibu ili kuruhusu utoaji huduma za kifedha. Hata hivyo sheria hizi ziko tofauti katika nchi mbalimbali kulingana na viwango vya maendeleo ya kiuchumi, malengo ya ushirikishwaji wa maswala ya kifedha, uwezo wa mamlaka kusimamia na kudhibiti pamoja na uelewa wa wateja.

Sasa mwaka 2009 katika mkutano wa MFW4A (Making Finance Work for Africa) uliofanyika Accra, Ghana, mambo mbalimbali yalijadiliwa katika kutaka kuazishwa kwa utaratibu wa kulinda taarifa za kifedha za wateja walioko katika nchi zinazoendelea. Majadiliano hayo yalilenga maeneo matatu ya kushughulikia katika kufikia lengo. Hii ni kwa mujibu wa ripoti iliyoandaliwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Ushirikiano wa Kiuchumi ya nchini Ujerumani (GIZ) kwa niaba ya Wizara ya Maendeleo na Ushirikiano wa Kiuchumi nchini Ujerumani.

Mambo hayo matatu ni yapi? Baki nasi hapahapa..

1. UWAZI:

Udhaifu wa mawasiliano na uwazi katika kuhifadhi na kufanyia kazi taarifa za wateja umeonekana kukithiri katika masoko ya nchi zinazoendelea jambo linalohitaji mabadiliko chanya ya haraka. Katika masoko ya fedha, taarifa ndio msingi wa shughuli zote nyeti. Hivyo kutokuwa na msawaziko na ulinzi bora wa taarifa katika mamlaka za uendeshaji kwa kutumia teknolojia za kisasa na mifumo ya ulinzi wa kimtandao (network/internet security mechanisms) hudhoofisha masoko haya ya kifedha. Vile vile ufahamu mdogo wa elimu kuhusu maswala ya kifedha kwa watu wengi katika masoko ya nchi zinazoendelea huwapa faida za taarifa watoaji wa huduma za kifedha. Yaani uwazi wa taarifa hutoa maelekezo na mwangaza kwa taratibu zenye lengo la kupangilia bei za bidhaa/huduma, makubaliano na tahadhari kwa wateja na mamlaka za usimamizi.

2. BIASHARA HURU:

Masoko yaliyo huru huchochea utekelezwaji wa usawa katika utendaji bora wa biashara kwa wateja ambao wanatofautiana viwango vya kiuchumi. Hili ni moja kati ya mambo yanayochagiza ulindwaji wa taarifa za wateja ambao wengi hawana uzoefu na mifumo ya kiteknolojia na taarifa zao zipo hatarini kudukuliwa bila ya wao wenyewe kujua. Usawa huu katika biashara huru hujumuisha sheria za kuzuia matangazo yenye lengo la kupotosha na utapeli, miiko ya kibiashara na wafanyakazi na kuzuia bidhaa zenye sumu au madhara kwa afya ya binadamu.

Hivyo huduma zenye usawa kwa wateja pia zinatakiwa kuzuia unyanyasaji kwa wateja na vizuizi visivyo haki vinavyowekwa na watoaji wa huduma za kifedha.

Eneo lingine ni kuhusu matumizi ya data za wateja ambayo inajumuisha ushikishwaji katika taasisi za mikopo na jinsi data hizo zinaweza kutumika kutengeneza vifurushi fulani vya huduma, tahadhari ya bei pamoja na ufanyaji wa minada.

Sheria hizi zinatakiwa kuwekwa ili kulinda haki ya faragha kwa wateja kwa mapana wakati huo huo zielezee kuhusu namna nzuri ya utoani wa taarifa hizo kwa taasisi zingine katika mazingira maalum kama ripoti za madeni na kadhalika. Haya yote ni hufanyika kwa kupitia matumizi ya teknolojia za kisasa za kompyuta katika intaneti na mitandao.

3. MAFUNZO STAHIKI NA NIDHAMU YA KAZI:

Mfumo bora wa mafunzo kwa wafanyakazi na elimu kwa wateja kuhusu haki zao za kuhudumiwa hujenga kujiamini katika kutumia huduma za kifedha. Hii hujumuisha utaratibu wa kutoa malalamiko, uzembe na unyanyasaji ambao unafanywa na wafanyakazi au watoani wa huduma, jambo ambalo litamlinda mteja pindi mambo yatakapokwenda kinyume na utaratibu.

Mifumo hii ya kutoa mafunzo kwa wafanyakazi na elimu kwa mteja inajumuisha usimamiaji wa masanduku ya maoni ambayo yanapatikana kwa wingi katika vituo vya watoaji wa huduma za kifedha kama benki na taasisi za mikopo.

Mpaka sasa utaratibu wa kulinda taarifa za mteja tayari unafanyika, unaandaliwa au kupangwa katika nchi nyingi barani Afrika. Nchi zingine zina vielelezo kuhusu kulinda taarifa za wateja katika vifungu vya sheria zao. Nchi 25 barani tayari zimejumuisha utaratibu au mahitaji ya taasisi za kifedha katika sheria zao. Vile vile wakati huo huo zaidi ya nchi 35 tayari zina mawakala mahsusi wa kusimamia ulinzi wa taarifa za wateja. Lakini bado taratibu hizi ni dhaifu na zinajiendesha bila ya kuwa na msaada muhimu wa sheria mama. Kiukweli mawakala wengi wanaoshughulikia usimamiaji wa taarifa za wateja ni mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s) na hawajajikita sana kwa wateja wa huduma za kifedha.

Nchini Kenya kupitia ripoti ya shirika la Financial Sector Deepening (FSD) Imegundulika kwamba taasisi mpya zote zinazoanzishwa huweka kiapo kulinda taarifa za wateja wao kwa mujibu wa malengo ya nchi hio katika sera zake kufikia mwaka 2030. Pia 25% ya watu wanaokwenda kuweka fedha benki katika mwaka 2010, uchunguzi wa mashirika ya FSD na CGAD wameonyesha “kushtuka” baada ya kukutana na tozo ambazo hawakujifahamu licha ya mwaka 2007 taasisi ya CBK kugundua aina 53 za tozo katika mabenki tofauti tofauti.

Afrika Mashariki tunajiandaa vipi na Ulinzi na Usimamizi wa Taarifa za Wateja katika masuala ya huduma za kifedha? Tujadili..👇👇