Tag: usafirishaji

Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA

Mtandao wa usafiri kwa njia ya nchi kavu barani Africa unajumuisha barabara na reli ambapo kwa wastani umechukua kilomita 6.2 kwa kila eneo la kilomita za mraba 100. Zaidi ya 60% ya mtandao mzima wa barabara haijatengenezwa kwa kiwango cha lami. Zaidi, pungufu ya 40% ya barabara za lami ndizo zilizo kwenye hali nzuri ya kupitika muda wowote. Sasa sekta hii ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika inatoa matumaini gani?

Mtandao wa njia za reli umeundwa kwa njia moja (single-track lines) ambazo huanzia maeneo bandarini kuelekea maeneo mbali mbali ya nchi/bara zikijumuisha viungio vichache tu njiani kuunga njia moja ya reli na nyingine (inter-linkages). Muundo huu wa reli zilizopo barani Afrika uliundwa nyakati za ukoloni na tangu wakati huo, ni marekebisho machache tu yameweza kufanyika ili kuwezesha treni ndefu zaidi zinazotumia dizeli kupita ambapo treni nyingi kati ya hizo hazitumiki tena kwa sasa.

Tukiangazia eneo la bandari, chini ya 50% tu ya matumizi ya bandari hutumika ikiwa ni pungufu ya mahitaji sahihi ya bandari hizo, jambo ambalo huchochewa na ucheleweshwaji wa mizigo na taratibu za forodha. Hali kadhalika, Afrika ndio inaongoza duniani katika ukuaji wa sekta ya viwanja vya ndege haswa kufuatia kuazishwa kwa soko huru lililoanzishwa baada ya makubaliano ya YD (Yamoussoukro Decision) yaliyofanyika mwezi November, 1999. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Afrika AU iliyotolewa mwaka 2014.

USAFIRISHAJI BARANI aFRIKA.
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Sasa changamoto; Je, sekta hii ya Usafirishaji na Miundombinu inaathiri vipi ukuaji wa biashara barani Africa? Na je, matumizi ya Teknolojia yana mchango gani katika kuboresha sekta hii ili kuinua biashara?

Kutokana na hali duni ya miundombinu na huduma za usafirishaji, gharama za kusafiri barani Afrika ni kati ya gharama ghali zaidi duniani, jambo ambalo linadhoofisha ushindani wa kibiashara katika masoko yote, ya ndani ya nchi na yale ya kimataifa.

Ripoti ya Tume inayoshughulikia Uchumi barani Afrika (ECA) imetaja kwamba nchi zisizo na bandari (landlocked countries) gharama za usafiri zinaweza kufikia robo tatu ya thamani ya bidhaa inayosafirishwa. Kwa mfano kusafirisha gari kutoka Japan mpaka Abijdan nchini Ivory Coast hugharimu US $1,500. Lakini kusafirisha gari hilo hilo kutoka kutoka jijini Abidjan hadi Addis Ababa hugharimu US $5,000. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa Teknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi kupitia link hii hapa yenye kichwa MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI. Ukimaliza hapo tuendelee na mada yetu ya leo.

Changamoto za Usafirishaji barani Africa.
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Gharama za usafirishaji zimetajwa kusababishwa na viwango vikubwa vya forodha, tozo za ucheleweshwaji, hasara zitokanazo na ajali pamoja na ukosekanaji wa fursa. Changamoto hizi huchagizwa zaidi na uduni wa miundombinu ya kiuchukuzi pamoja na huduma zinazotokana na nyanja hiyo.

Nayo programu ya maendeleo ya miundombinu barani Afrika (PIDA) katika ripoti yake imeainisha kwamba gharama za kiuchumi zinazosababishwa na changamoto za usafirishaji katika Mtandao wa Miundombinu ya Usafirishaji barani Afrika (ARTIN) zinazidi US $170 bilioni kwa mwaka kufikia mwaka 2014.

Changamoto hizo zimetajwa kusababishwa na;

•Kutokuwa na utendaji wa taratibu za kuwezesha biashara katika majukwaa ya ARTIN (kujumuisha bandari na vituo vya mipakani).

•Sera za nyanja ya usafirishaji ambazo zinapelekea kudhoofika na kuongezeka kwa gharama za usafirshaji kwa njia ya barabara pamoja na viwango duni vya barabara katika nchi nyingi barani Afrika.

• Sera za kiuchumi zinazozuia utendaji mzuri pamoja na utanuzi wa mifumo ya reli.

• Nyanja ya usafiri wa anga na Sera za kiuchumi zinazozuia uanzishwaji wa vituo vya anga vya kikanda, jambo linalotajwa kusababisha kuongezeka kwa gharama za usafiri huo.

Kufuatia changamoto hizo, Je, teknolojia ina mchango gani katika kuimarisha biashara na kupunguza gharama za uendeshaji?

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kuelekea mapinduzi ya nyanja zote za kiuchumi. (Yaani tutaendelea kuwa juu kileleni😁). Mapinduzi katika matumizi ya simu kutoka simu za mezani mpaka simu za rununu (smartphones), huduma za kifedha kielektroniki (fintech), biashara za kielectroniki (ecommerce) na kadhalika vimekuwa sehemu muhimu sana katika kurahisisha utendaji wa kibiashara katika sekta ya miundombinu na usafirishaji.

Benki ya Dunia (WorldBank) inaripoti kwamba ubunifu wa kiteknolojia umewezesha sana muingiliano wa kibiashara kwa kuzingatia ongezeko la watumiaji wa Intaneti huduma za simu. Kipimo cha wiani (density) katika matumizi ya huduma za intaneti kwa kila watu 100 waliopo eneo la Kusini mwa jangwa la Sahara, ni watu 17 tu ndio wameonekana kuwa watumiaji wa intaneti katika mwaka 2015.

website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako?
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika

Utafiti huo unakolezwa wino na shirika la kimataifa linalodhibiti mawasiliano ya simu GSMA ambapo kwenye ripoti yake ya mwaka 2018 limeangazia kwamba, eneo la kusini mwa jangwa la Sahara lilikua na kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu ya 44% kufikia mwishoni mwa mwaka 2017 kukiwa na watumiaji takriban 444 milioni sawa na 9% ya watumiaji wote wa simu duniani. Vile vile katika kipindi cha mwaka 2017-2022 watumiaji wa simu katika eneo hilo wataongezeka katika kiwango cha CAGR cha 4.8% ambayo ni zaidi ya mara mbili ya kiwango cha ongezeko kwa dunia nzima katika kipindi hicho hicho. Pia kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu inatajwa kufikia 50% kufikia mwishoni mwa 2023 na 52% mpaka mwaka 2025.

Kufuatia uchunguzi huo, sekta ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara barani Afrika inatajwa kuongezewa nguvu na maboresho zaidi ili kuendana na kasi hio ya ukuaji katika ICT. Matumizi ya GPS katika usafiri wa taxi yamerahisisha zaidi gharama na muda wa kutoka sehemu moja na nyingine, huku maboresho ya miundombinu kama barabara na viwanja vya ndege yakichagiza kasi ya sekta hio.

Zaidi, mtandao wa huduma za Posta na EMS unajumuisha takriban ofisi 30,000 barani ambazo ni muhimu katika kuwezesha e-commerce trade. Kwa kuliona hilo kampuni kama DHL zimejitosa kuhakikisha teknolojia inabadili huduma za posta kuwa rahisi zaidi.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi na jambo hili?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo kuhusu usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA
mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi

MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI

Ubunifu wa kiteknolojia na zama za Kidijitali huathiri karibu kila mchakato katika utendaji na uendeshaji wa mfumo wa Usafirishaji na Uchukuzi duniani kote. Kuanzia njia na namna ya usafirishaji wa majini/baharini, ardhini na angani, usimamiaji wa mizigo pamoja na shughuli za utawala na ugavi zikiwemo utaratibu/usimamizi wa nyaraka na ufuatiliaji mzuri wa malipo. Leo sasa tuangazie mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi. Kuna nini kinaendelea huko? Makinika..

Idadi wa watu duniani itaongezeka kutoka watu bilioni 7.4 mpaka watu bilioni 10.6 kufikia mwaka 2050, vile vile idadi ya mizigo inayosafirishwa kwa njia ya meli peke yake itaongezeka mpaka mara 4 ambayo inatarajiwa kukua kwa ongezeko la 715% kwa nchi za Africa.

Pia kasi ya ukuaji wa miji itakuwa kwa 56% ya idadi ya watu katika Africa mpaka mwaka huo 2050. Ongezeko hili linatarajiwa kuchagizwa na kasi ya ukuaji wa miji, kukua kwa kipato cha mtu mmoja mmoja, kupenya kwa matumizi ya intaneti pamoja na urahisi wa kupata na kutumia Teknolojia mpya.

Hata hivyo mtindo wa uchukuzi wa mizigo kwa kupitia njia ya meli kwa kutegemea nyaraka peke yake unatarajiwa kupungua kwa kiasi kikubwa kufuatia ujio wa matumizi ya nyaraka za kielektroniki na barua pepe. Hii ni kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la EY.

Kufuatia kasi hio ya ukuaji na mabadiliko, makampuni na biashara zilizopo katika sekta ya Usafiri na Uchukuzi yanahitaji kubadilika ili kumudu kuwepo katika ulimwengu ambao ushindani unakuja kutoka pande zote na teknolojia za kidijitali ndio zitakuwa chachu kuu ya mabadiliko.

Sasa Swali; Teknolojia Inaweza vipi kubadili Kesho ya Sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Leo hii sehemu kubwa ya shughuli za kiuchumi na kijamii hufanyika mtandaoni na haswa haraka zaidi kupitia katika simu janja (smartphones). Ukuaji huu wa kiteknolojia unanufaisha maeneo yote yaliyomo kwenye Sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kama; usafiri wa magari ya mizigo (malori), usafiri wa kimataifa (njia ya anga na majini), usimamiaji wa shughuli za ugavi na kuratibu safari za majini, nchi kavu na angani. Yafuatayo ni mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi barani Afrika;

1. MFUMO WA KURATIBU SAFARI/ONLINE TRACKING SYSTEM (Magari ya mizigo, Meli na Anga): Imezoeleka mteja kuhifadhiwa nafasi ya kusafirisha mizigo yake kwa kujaza fomu fulani ya usafirishaji, halafu anaachwa gizani mpaka siku mzigo wake unamfikia asipoamua kufuatilia kwa kupiga simu. Lakini leo, kwa kutumia huduma za intaneti na programu za kompyuta mteja anao uwezo wa kuagiza na kufuatilia kwa ukaribu zaidi mizigo yake muda wowote akihitaji kufanya hivyo.

Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi

Hii si tu kwamba imerahisisha matumizi ya intaneti kisasa zaidi lakini zaidi teknolojia hii inaokoa muda na gharama za ziada kwa kampuni ya usafirishaji na mtu binafsi.

2. TEKNOLOJIA YA INTERNET OF THINGS (IoT) na RADIO FREQUENCY IDENTIFICATION (RFID): Ulishawahi kufikiria siku fulani una uwezo wa kuwasha feni yako nyumbani kwa kutumia simujanja yako? Sasa leo hii vifaa vingi vya kielektroniki vimeundwa na uwezo wa Wi-Fi na vifaa vya kuhisi mazingira mbalimbali. IoT inafungua nafasi nyingi sana katika kurahisisha shughuli za ugavi kama kupunguza gharama za uendeshaji. Vifaa vya kuhisi mazingira (sensors) pia hufungwa katika magari madogo na makubwa, meli za mizigo, treni na kadhalika. Vifaa hivi hufungwa mfumo wa kengele au mfumo wa GPS ambayo hufuatilia na kuratibu mwenendo wa mzigo kumfikia mteja.

Hali kadhalika teknolojia ya RFID ambayo imeshatumika miaka kadhaa hutumiwa na makampuni ya uchukuzi na usafirishaji kufuatilia mwenendo wa hesabu za bidhaa zao (Inventories). Kwenye teknolojia hii hujumuisha pia matumizi ya barcode za kwenye bidhaa, pamoja na matumizi ya rimoti za televisheni na redio, teknolojia ambayo imetumika kwa miaka mingi zaidi, hivyo kuyafanya makampuni mengi kutumia zaidi RFID’s. Vile vile RFID’s hutumika kusambaza bidhaa katika maghala yao na kuratibu mienendo ya makontena.

3.MAGARI/ MALORI YA KUJIENDESHA NA DRONES: Katika ulimwengu ambao unaendeshwa na matumizi ya kompyuta kutoka mahali fulani kwenda mahali kwingine, utajihisi vipi siku unapokea mzigo kutoka kwenye chombo kinachoruka angali mfano wa helikopta ndogo? Sasa huko ndipo tunapoelekea. Magari ya kujiendesha tayari yanaonekana duniani ambapo kampuni za UBER na EMBARK wametengeneza magari yanayojiendesha japokuwa bado miradi hiyo haijarasimishwa kwa wateja. Ni swala la muda tu kutoka sasa kabla matumizi yake hayajawafikia wateja ulimwenguni kote.

4. MITANDAO YA KIJAMII: Nani ambaye hapitii kwenye mitandao ya kijamii angalau mara moja kwa siku? Nguvu ya mitandao hii ya kijamii inaboresha kwa namna ya kipekee sana sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kwa ujumla wake. Mitandao hii inarahisisha sana katika kutangaza huduma za usafirishaji na uchukuzi pamoja na kampuni kuwasiliana na wateja wake kwa ukaribu na urahisi zaidi katika kutoa taarifa muhimu, dharura na mrejesho kutoka kwa wateja.

Kwa mujibu wa Hootsuite, 59% ya Wamarekani ambao ni watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekubali kwamba huduma kwa wateja kupitia mitandao ya kijamii imerahisisha kujibu maswali na huduma husika.

Zaidi ya yote, miundombinu ya uchukuzi katika nchi za Afrika bado ipo nyuma sana kimaendeleo ukilinganisha na sehemu zingine za dunia. Nchi ya Afrika Kusini ndiyo inaongoza barani kwa kuwa na miundombinu ya kisasa zaidi ya kiuchukuzi ambapo kasi ya ukuaji wa miundombinu kwa mwaka ni ndogo kwa 3% katika kipindi cha mwaka 2012 hadi 2017. Hii ni kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Fedha duniani (IMF).

Kwa upande mwingine nchi za Kenya na Nigeria zinaongoza kwa kuwa na ukuaji mkubwa katika miundombinu yake ya kiuchukuzi na usafirishaji kwa 6.2% na 6.8% katika kipindi hicho hicho (2012-2017). Kwa wafanyabiashara na makampuni ya usafirishaji na uchukuzi; Kuwekeza vema Afrika kunahitaji uelewa mzuri wa maeneo muhimu pamoja na uelewa wa masoko ya wenyeji.

Afrika si tu kwamba ni kubwa mno, lakini zaidi Kuna mtawanyiko mkubwa wa jamii za watu na rasilimali. Hata hivyo, zaidi ya 70% ya makampuni makubwa zaidi duniani yanayozalisha bidhaa za watumiaji tayari zinafanya kazi Afrika. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kimataifa la PwC.

Usipitwe na Ofa Yetu katika msimu huu wa Nane Nane. Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi. Umejifunza nini leo kuhusu mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi? Share nasi mawazo yako kwenye comment au tucheki kwa kugusa WhatsApp namba yetu hii hapa 0765834754.

Makala hizi hapa zitakupa mwanga zaidi katika kuwekeza katika Biashara zinahohusiana na sekta ya Usafiri na Chukuzi hasa katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara:

  1. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  2. USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA
  3. FAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA HABARI NA BURUDANI