Tag: umuhimu wa website

OFA YA MSIMU WA SABASABA

Mwaka 2016 wakati nawaza kufungua kampuni from scratch nilifikiri kupata wateja itakuwa rahisi tu. Nikawaza nikimaliza mchakato wa BRELA, TRA na Leseni basi nikituma proposals zangu kwa watu walau 10 ntakuwa nimeshapata wateja wangu nianze kuingiza pesa.

Sasa nilipoanza kutafuta wateja nikawa nashangaa, kila ninapoenda nasikilizwa tu lakini sitafutwi tufanye kazi. Mteja wangu wa kwanza nilikuja kumpata August, 2018 (mwaka mmoja baada ya kufungua kampuni rasmi mwaka 2017). Sikujua maisha yangekuwa magumu kiasi kile.

ILIKUAJE NIKAPATA MTEJA?

Kutokana na kushamiri kwa vitendo vya Utapeli wa mtandaoni, watu wamekuwa waoga sana katika kufanya biashara mtandaoni. Watu wanatapeliwa jamani, kuweni makini mno na miamala mnayofanya kwenye simu zenu pamoja na humu mtandaoni ndugu zangu.

Ilinichukua muda mrefu, almost miaka miwili mpaka nilipogundua MBINU ya kuchapisha makala zenye maudhui muhimu kwa biashara za wajasiriamali kupitia kurasa zangu za LinkedIn, Instagram na Twitter huku nikiziunga na link ya tovuti ya kampuni ambayo ndipo nilipoweka makala kamili.

Baada ya watu kutembelea kurasa zangu za mtandaoni na tovuti yangu na kuona “Thamani ya maudhui” niliyokua nayatoa ndipo nilipopata mteja wa kwanza wa uhakika ambaye mpaka leo bado tunaendelea kufanya kazi pamoja na wateja wengine wengi kutokea hapo.

NILICHOGUNDUA:

Mpaka mtu afanye kazi/biashara na wewe lazima:

1. Awe anakufahamu au tayari anazo taarifa zako za kutosha.

2. Anakuamini (kwamba utafanya kazi yake kwa viwango anavyotaka na pesa yake haiendi bure).

3. Anakupenda (ni ngumu kufanya biashara na mtu ambaye hampendani).

Jiulize hapo, Unaweza vipi kumshawishi mtu ambaye hakufahamu kabisa (a total stranger) akuamini na akupe kazi zake uwe unamfanyia kwa kiwango anachokitaka? Pitia makala hii hapa kwenye link https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kuweza-kushawishi-wateja-katika-biashara-yako/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUWEZA KUSHAWISHI WATEJA KATIKA BIASHARA YAKO”

Nafahamu kuna muda unapitia wakati mgumu sana katika kutafuta wateja wapya katika biashara yako ili kujitanua zaidi, lakini hujui ufanyeje. Hata hivyo, MBINU BORA ya kutanua biashara yako kwa watu usiofahamiana nao kabisa, hasa watu wa mtandaoni (Digital Neighbors) ni hii hapa:

1. Badili matumizi ya Mitandao ya kijamii kwa kupost maudhui kuhusu Thamani ya bidhaa/huduma yako katika maisha ya mtu ili kumvutia awe mteja wako. Weka tips kama Aina za bidhaa/huduma, Bidhaa feki zinajulikana vipi, bidhaa zako zina utofauti gani na zingine, ubora uko vipi nakadhalika.

2. Fungua website ili kujiweka katika mazingira ya kujulikana kwa Utalaam wako mahsusi. Website ndio CV ya biashara yako mtandaoni. NOTE: Mteja atafanya kazi na wewe kiuhakika kwa kuwa wewe ni Mtaalam katika fani fulani na sio salesperson kama wengine pale akiona website yako.

3. Hakikisha mtu aki-search huduma/bidhaa unazouza kupitia google basi anakupata mara moja. Hii kitaalam inaitwa S.E.O (Search Engine Optimization). Hii inakupa fursa bora ya kutanua biashara yako hasa katika matafuto ya mtandaoni ambayo yatawasaidia wateja kukufikia kirahisi.

Sasa, kwa kufahamu hilo, Natoa OFA YA MSIMU WA SABASABA ambapo utakapofungua website yako kwenye msimu huu tutakufanyia SEO, tutakupa tips za kutoa maudhui ya kuvutia wateja kwenye mitandao yako ya kijamii pamoja na kukufanyia Web maintenance BURE kwa mwaka mzima.

Bei ya OFA hii ni laki tano tu (500,000/-) unapata vyote nilivyokutajia. OFA hii itakapokwisha gharama zitarejea kufikia laki tisa elfu hamsini tu (950,000/-) kwa website peke yake. Hivyo wahi kabla OFA haijakwisha. Karibu Tufanye kazi.

Kwa maswali au maulizo yoyote tafadhali tumia mawasiliano yetu yanayopatikana katika tovuti hii.

OFA YA KUPATA WEBSITE YAKO

OFA YA KUPATA WEBSITE YAKO LEO!

Tarehe 22 June, wakati natangaza maandalizi ya ujio wa OFA hii kupitia Whatsapp, alinijia rafiki yangu mmoja anaitwa Freddy. Yeye ni mfanyabiashara wa viatu pale magomeni. Akaniuliza, “Mimi huwa napost viatu vyangu kupitia whatsapp na Instagram, sasa hio website mimi itanisaidia vipi?”

Ikabidi nirudi kwenye makala mbili nilizowahi kupost kwenye tovuti yetu ya Rednet Technologies kupitia link https://rednet.co.tz/website-inasaidia-vipi-kuimarisha-biashara-yako/?noamp=mobile yenye kichwa “Website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako?”
na link nyingine https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “Kwanini umiliki tovuti (website) rasmi ya biashara yako?”

Kwa uchache nilimweleza haya:

  1. Website inakupa Utambulisho halali na kudumu mtandaoni. Yani website ndio ID muhimu ya biashara yako kama ilivyo ID yako ya NIDA.
  2. Website inawafikia watu wengi zaidi ambao wanaweza kuwa wateja wako kuliko whatsapp ama Instagram.

Kumbuka website ikiwa hewani inapatikana dunia nzima na wengi wataoifungua ni wanakuwa na interests na bidhaa/huduma yako.

Zaidi unaweza kutembelea tovuti yetu kupitia link zilizowekwa hapo juu ili kuzipata makala hizo na kuongeza maarifa.

Fast forward.. Sasa bwana Freddy nilipomueleza hayo akapata shauku sana ya kufungua tovuti yake, lakini bahati mbaya hakua na pesa ya kutosha kupata OFA hii, Hivyo nikaamua yafuatayo;

  1. OFA hii itawafikia wafanyabiashara watano TU kutoka watatu waliopangwa kufikiwa mwanzo.
  2. Muda wa kurequest OFA hii ni kwanzia leo Ijumaa mpaka Jumatatu asubuhi. Baada ya hapo hakutakuwa na OFA tena.
  3. Malipo ya kupata OFA hii yatakuwa katika mtindo wa 300k advance, na 200k italipwa kazi itakapokamilika.

OFA ITAKUPATIA HAYA:

  1. Website kamili ya biashara yako.
  2. Maintenance BURE mwaka mzima.
  3. Business Cards 50 BURE.
  4. Tutakufanyia SEO Bure mwaka mzima ili tovuti yako ipatikane Google mtu yeyote atakapokutafuta..

Kama una swali kuhusu chochote, Tafadhali niulize nami nitakuhudumia kama inavyostahili.

Whatsapp/call: 0765834754
Email: info@rednet.co.tz / fvitalice@gmail.com

Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara

BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA

Biashara nyingi zimekuwa zikiendeshwa katika mtindo wa “Kujiajiri” ambapo wajasiriamali wengi huteseka wakifanya kazi kwa bidii usiku na mchana lakini hujikuta siku moja tu wasipofanya kazi basi biashara inashindwa kuzalisha. Yaani mfanyabiashara unajikuta unakuwa mtumwa kwenye biashara yako mwenyewe? Hio dhana ya kujiajiri inakuwa na maana gani sasa? Leo sasa tuangalie Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara inayojitegemea? Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Septemba 21 kila mwaka ni Siku ya Kimataifa ya Amani. Sasa katika Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (UN), Lengo Na. 16 limekazia katika kudumisha Amani, Haki na Taasisi Imara. Amani ni mbolea muhimu katika ukuaji wa uchumi mahali popote. Mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa uliokaa mwaka 2001 ulithibitisha kuweka Siku maalum ya kutafakari na kudumisha Amani, Haki na Taasisi Imara duniani, ambapo siku hio ni September 21 kila mwaka.

Hii ni kutokana na vitendo vya uvunjifu wa amani, taasisi dhaifu na kukosekana haki si za kidemokrasia katika utendaji, serikali hizi ambazo mara nyingi huwa ni za kidikteta au za kifalme, mara nyingi huendeshwa kwa sheria zinazokandamiza upande mmoja na kuimarisha kikundi kidogo cha watu kwa maslahi yao binafsi.

Jambo hili hutokea pale viongozi (watu wanaopewa dhamana) kushindwa kuwajibika kwa wanachi na hivyo kujiundia sheria ambazo zinawapa mamlaka ya kutumia rasimali za nchi huku zikiwaacha wanachi katika hali ya upofu wasiwe na nguvu ya kuuliza na kusimamia matumizi sahihi ya rasilimali zao. Hili ni jambo baya na linalopaswa kuagamizwa mahali popote kwanzia ngazi ya familia, biashara, kampuni, shirika mpaka serikalini.

Mwandishi mahiri Robert Kiyosaki katika kitabu chake cha CASH FLOW QUADRANT amefafanua kwanini Matajiri huendelea kuwa matajiri huku Watu wa Uchumi wa kati wakiendelea kukimbia mbio za panya na masikini wakizidi kuwa masikini. Kwa haraka haraka, katika Njia 4 za kuingiza mapato ambazo zimeonyeshwa kwa herufi za E, S, B na I, zimetajwa kuwa ndio chanzo kikuu cha mapato ya watu duniani.

SEHEMU ZA KUIFANYA BIASHARA YAKO KUWA TAASISI IMARA?

Waswahili wanakwambia “Kila mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake” lakini katika uwanda wa kiuchumi na biashara duniani, kila mtu anao uwezo wa kubadilika na kufanya uchaguzi ulio bora zaidi kwa maisha yake ya kiuchumi na kijamii. Na hii ni kwa kujifunza na kufanya kazi tu.

E = EMPLOYEE (MWAJIRIWA): Kitu cha kwanza ambacho kipo kichwani kwa mwajiriwa yeyote ni uhakika wa kibarua chake (job security). Mwajiriwa hufanya kazi kwa bidii ili apate mkate wa kila siku na zaidi awe na hakika kuwa ataendelea kupokea mshahara kila mwisho wa mwezi kwa miaka mpaka atakapostaafu au kumaliza mkataba wake. Dhana ya kuwa majiriwa huathiri ubunifu wa mtu katika kutaka kujaribu shughuli nyingine itakayoimarisha uchumi wake zaidi ya ajira.

Mwajiriwa anapohitaji kukua kiuchumi hutafuta ajira itayomlipa zaidi na si fursa za biashara mpya.

udalali wa mtandaoni ongea na watu uvae viatu

Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara

S= SELF-EMPLOYED (KUJIAJIRI): Hii ni njia ya mateso makubwa, japokuwa vijana wengi eti ndio hupenda kufanya shughuli za kujiajiri wakihisi kuwa huko kuna uhuru mkubwa na pesa nyingi. #VijanaWenzangu acheni kujidanganya. Unapojiajiri fahamu kuwa utajinyima uhuru wako binafsi ili biashara yako iweze kuwa hai. Wewe ndio unakua CEO, sales manager, mhasibu wewe, mtu wa masoko wewe, yaani wewe ndio unakuwa kila kitu. Hata hivyo kwa biashara inayoanza si vibaya kupitia katika hatua hii japo hutakiwi kukaa muda mrefu hapa, lazima biashara ivuke hiki kiunzi.

B=BUSINESS OWNER (MMILIKI WA BIASHARA): Tofauti na walio katika Chumba “S” Mtu anayemiliki biashara sio lazima awe anafanya kazi katika biashara hio. Yeye anamiliki mfumo wa utendaji au bidhaa ambayo ndio huzalisha pesa muda wote hata asipokuwepo. Mfano, mtu anayemiliki kiwanda cha kutengeneza nguo. Sio lazima awe ndio mtendaji mkuu wa kutengeneza nguo, hata hivyo yeye anaweza kuajiri watu wa kiwandani na kuwalipa ili waendelee kuzalisha bidhaa zitazoendelea kuingiza pesa.

I=INVESTOR (MUWEKEZAJI): Huyu ndiye mtu mwenye uelewa mkubwa zaidi kati ya wote ambao tumewajadili hapo juu. Mtu huyu hutafuta Mali (Assets) zaidi kuliko madeni (Liabilities). Mara nyingine hutumia pesa za watu wengine (mkopo) ili kuhakikisha anapata Mali itakayozalisha (asset). Ukitaka kufahamu kwa undani kuhusu Uwiano unaofaa wa Mali na Madeni katika biashara gusa link hii Uwiano wa Mali (assets) na Madeni (Liabilities) kwenye biashara.

Mtu huyu hutumia faida anayopata kutoka kwenye assets zake kununua assets nyingine nyingi zaidi, na hujikuta akifurahia maisha ya kuingiza kipato kutoka kwenye assets kuliko vyanzo vya matumizi (liabilities). Kama ulikua hufahamu basi Matajiri unaowajua duniani wote ni Wawekezaji huku wakitumia kanuni ya 70% kwa 30% katika shughuli zote za kifedha. Kiufupi kanuni hio hutumika katika kupanga matumizi ya mapato ambayo hugawanywa katika mafungu matatu ya:

i. 70% Matumizi ya kawaida (Normal Expenses including taxes, rents, food, accomodations etc)

ii. 30% (20% Servings + 10% Charity) Mwekezaji anapohitaji pesa hutafuta assets zaidi kuliko kufanya matumizi yanayofyonza pesa za biashara.

Sasa basi, hayo yote niliyoyaeleza, hayatakuwa na maana kama hayatafanyika katika muundo wa Taasisi Imara.

BIASHARA KAMA TAASISI IMARA INA SIFA ZIPI?

Taasisi Imara ni ile jumuiya ya kiuchumi/Kijamii ambayo inaendeshwa kwa mujibu wa katiba katika utendaji wake wa kila siku. Jumuiya hio inaweza kuwa ni Serikali, Shirika, Kampuni, Chama, Biashara au Familia. Familia (Ndoa) ndio Taasisi ya kwanza kabisa kuwahi kuanzishwa na binadamu duniani. Ndio maana wahenga wanakwambia “Maendeleo yanaanzia nyumbani.

Maendeleo ya taasisi hutegemea uwepo wa sheria zitakazokuwa muongozo wa kila kinachofanyika kila siku ndani ya taasisi hio. Hata hivyo ili iwe taasisi imara inapaswa kuwa na sifa hizi:

1. SHERIA MBELE, MTU NYUMA: Taasisi imara hutambua na kutekeleza matakwa ya kisheria na kamwe si matakwa ya mtu binafsi. Sheria hizi huandikwa katika mfumo wa Katiba (constitution/memorandum/articles of assosciation, Taratibu (regulations) na sheria ndogondogo (by-laws). Taasisi zinazoongozwa vema kwa mujibu wa sheria bila kumuogopa mtu huwa imara sana kiutendaji na hufikia malengo yake kiurahisi zaidi.

2. UTAMADUNI: Katika utendaji bora, Utamaduni huzingatiwa kama silaha bora zaidi katika uzalishaji/utoaji huduma wenye viwango vya juu vinavyitakiwa. Wahenga walishasema “Culture eats strategy for breakfast” yani, hakuna mbinu ambayo itaweza kufanya kazi kwa mafanikio isipofanywa kama sehemu ya utamaduni. Hivyo Taasisi imara hufanya shughuli zake katika Utamaduni uliotengenezwa kwa muda mrefu katika kufikia malengo yaliyowekwa. Mfano, utamaduni wa kupongeza mtendaji bora, utamaduni wa kumhudumia mteja kwa njia ya mtandao na utamaduni wa kuzingatia viwango.

3. UWAJIBIKAJI: Ili iwe Taasisi imara lazima watendaji wawajibike katika majukumu ya kila siku. Watendaji wanapaswa kuwajibika kwa Kupongezwa, Kujiuzulu au Kuongeza kiwango cha uzalishaji/utoaji huduma kwa wateja wao. Taasisi imara haipaswi kufumbia macho swala la uwajibikaji.

Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara

4. KWELI NA HAKIKA: Hakuna Taaasisi Imara ambayo haijiendeshi katika namna ya Ukweli na Uhakika kwa wateja wake. Hata hivyo, hakuna mifumo ya Taasisi inayofanya kazi kwa ubora wa 100%, ni vema kuhakikisha jambo hili linazingatiwa.

Tulizoziona leo ni baadhi ya sifa zinazotengeneza Taasisi Imara. Kwa mujibu wa malengo Endelevu ya kimataifa ya UN, imepangwa kutimiza lengo la kuwa na Taasisi Imara ifikapo mwaka 2030 (#Agenda2030). Tujadili kupitia Replies, Retweets na Share ili watu wengi zaidi wanufaike.

Tuungane kwa pamoja kuhakikisha Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara. Endelea kupata makala muhimu kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia kupitia links hizi hapa:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?
  3. UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA
  4. TEKNOLOJIA KATIKA KUKUZA BIASHARA KUPITIA SEKTA YA UTALII

KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?

Hebu fikiria wewe ni mgeni mahali fulani, baada ya kushikwa na njaa unaelekezwa migahawa miwili, mmoja ukiutafuta mtandaoni unaweza kupata taarifa zake mwingine hauna taarifa yoyote mtandaoni. Uelekeo wako utakuwa upande gani? Leo sasa tutakwenda kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako. Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Kuishi katika ulimwengu wa kidijitali, tovuti ni zana muhimu sana katika biashara na masoko ya kidijitali. Cha kushangaza inakadiriwa 35% – 50% ya biashara ndogondogo duniani hazina tovuti zao binafsi, jambo linalozinyima fursa ya kuweka taarifa zao kirahisi mtandaoni na kupata wateja wapya kirahisi.

Kuna wanaosema kuwa matumizi ya Tovuti yanamezwa na uwepo wa mitandao ya kijamii ambayo pia watu wanaweza kuweka na kutangaza biashara zao humo. Ni kweli, aghalabu, kwa kutumia Mitandao ya kijamii hauna uhakika wa kumiliki taarifa na maudhui unayoweka humo muda wote. Watengenezaji ambao pia ni wamiliki wa Mitandao hio wanao uwezo wa kusimamisha/kufuta akaunti au maudhui yako muda wowote ikiwa biashara/maudhui yako yanakwenda kunyume na matakwa na masharti yao.

Vile vile Mitandao ya kijamii unayotumia inaweza kupungua umaarufu au kufilisika muda wowote usioutegemea mfano kuna mitandao ilikua maarufu sana zamani kama Hi5 lakini umaarufu wake kwa sasa umepungua au kupotea kabisa. Hivyo, uwezekano wa kudorora kwa biashara yako kunategemea pia umaarufu wa mtandao wa kijamii unaoutumia, jambo linalichangiwa sana na ujio wa mitandao mipya ya kijamii kama Instagram, Whatsapp na TikTok. Hii kwako unaionaje? Nitaeleza Tofauti katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Tovuti wakati Ujao.

Faida ni nyingi sana za matumizi ya website katika kuimarisha biashara yako kupitia ulimwengu wa Teknolojia. Tayari tumekuandalia makala maalum kupitia link hii hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

Leo hii ntakwambia mambo 10 kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika biashara yako:

1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:

Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu huenda wapi kutafuta vitu kama suppliers, bidhaa na huduma mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi. Injini za matafuto mtandaoni zimekuwa kimbilio namba moja huku GOOGLE Ikiziacha mbali Injini zingine kama Yahoo, Bing na Ask. Maana yake hii ni kwamba kama huna tovuti, jua mauzo yako ni 7% tu ya soko zima ambalo hujui kuwa unalo. Upo apo? Yani unapoteza 93% ya mauzo yako kila siku bila hata wewe mwenyewe kujua.

2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)

Kama una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo. Kwa biashara zenye malengo makubwa kuwa na tovuti huwaweka kwenye nafasi za juu katika kupata tenda na wateja, na huonyesha Uweledi bora katika utendaji wa biashara kuanzia katika muonekano na utendaji wa tovuti. Inakadiriwa 80% ya watu duniani huonyesha kutokua na imani na Biashara ambazo hazina tovuti pale wanapotaka huduma/bidhaa fulani mtandaoni.

3. KUPATIKANA KWA URAHISI

Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi, tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako. Ndivyo ilivyo kwa tovuti ambayo inajieleza kwa kila kitu kama ilivyo tovuti maridhawa ya http://rednet.co.tz . Ile raha ya kupata taarifa, huduma au bidhaa kirahisi kupitia simu yako ya mkononi, hufanya wateja waongezeke maradufu na kusambaza sifa bora kwa uharaka sana katika jamii na katika mitandao ya kijamii hali kadhalika.

Hii huongezwa chumvi ya SEO (Search Engine Optimization) ambayo ni teknolojia iliyowekwa katika Injini za matafuto ya kimtandao inayowasiliana na tovuti yako na kuweka taarifa katika Injini hizo na hivyo kufanya taarifa za tovuti yako kuonekana haraka zaidi katika matafuto. Biashara imerahisishwa sana kupitia SEO kuliko kutumia Mitandao ya kijamii. Kama watu wanakwenda Google kutafuta taarifa, basi fahamu taarifa hizo hupelekwa hapo GOOGLE kwa kutumia teknolojia iitwayo S.E.O. Kufahamu zaidi kuhusu SEO gusa hapa chini

4. TANGAZO LA BURE MUDA WOTE

Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo huduma ya internet inapatikana. Tangazo la bure kabisa hili. Kama tovuti yako ina ubora wa kuvutia zaidi katika muonekano, maudhui na utendaji, basi bila shaka biashara yako ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri sokoni na kupata wateja wengi kila siku. Jiulize hivi, unapofunga ofisi/biashara yako wakati wa jioni kila siku, wateja wapya wanaweza vipi kupata taarifa sahihi muda watakaohitaji?turudi kwenye mada yetu, kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Hii pia inawezeshwa sana na teknolojia ya S.E.O.

5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)

Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa. Kupitia tovuti yako, unaweza kuweka testimonials kwa idadi uitakayo bila kurudia rudia na katika mpangilio maalum na watu wakaweza kuona ushahidi utakaowaridhisha kuendelea kutumia huduma/bidhaa zako. Mara nyingi Mitandao ya kijamii huzuia kuoneka kwa biashara kwa urahisi kutokana na wimbi la watumiaji wenye maudhui tofauti tofauti katika ratiba ya saa (timeline) yako unayopitia katika mitandao hio, hivyo kusababisha usumbufu (distractions) katika biashara yako.

6. UAMINIFU (TRUST)

Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza mahusiano na mteja kama UAMINIFU. Ili kupata wateja wa kudumu katika sekta nyingi, kuwa na tovuti hai ni muhimu katika kudumisha mahusianao katika ya mfanyabiashara kwa muda wowte mteja atakaohitaji.

7. POSITIVE ROI

Ikiwa ni Return On Investment (ROI) au Rejesho baada ya Uwekezaji, unapoendesha biashara ambayo ina gharama zake kama umeme, kodi, maji, mafuta n.k, ukijiuliza utaweza vipi kurudisha gharama hizo upate faida? Njia moja nzuri ni matumizi ya tovuti bora yenye uwezo kunasa wateja wapya kwa njia ya mtandao muda wote (24/7) kirahisi kabisa.

8. THAMANI INAYODUMU

Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote itakapohitajika kufanya hivyo. Hivyo thamani ya biashara yako itaendelea kuwepo muda wote tovuti yako inapokuwa hewani.

9. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA

Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei, ushauri nakadhalika. Hivyo kuimarisha mahusiano na ukaribu wako na wateja wako wakiwa popote duniani kwa urahisi kupitia miundombinu mbalimbali unayoweza kuiweka katika tovuti yako kama matumizi ya chatbots na barua pepe maalum za kibiashara (zenye jina/domain name ya tovuti yako).

10. MASIJALA (DATA CENTER) RAHISI YA MTANDAONI

Tovuti yako inaweza pia kuwa masijala rahisi kwa wafanyakazi, wateja na mtu yeyote anayehitaji kujua taarifa kuhusu huduma/bidhaa unazohusika nazo. Mfano mzuri ni tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz ambayo zaidi tu. ya kwamba inatoa taarifa kuhusu huduma tunazohusika nazo za kutengenza websites, softwares, apps n.k, lakini pia tovuti inatoa taarifa muhimu mbalimbali kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia. Taarifa hizi zimetengenzwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha Biashara za wateja wakiwa popote duniani. Pia taarifa hizo zinalenga kuhamasisha matumizi ya Teknolojia katika njanja mabimbali za kiuchumi haswa kwa wafanyabiashara waliopo kusini mwa jangwa la Sahara.

NOTE: Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa muhimu kama jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.

BONUS POINT: Tovuti yako unapoisajili, unashauriwa pia upate kirurushi cha barua pepe yenye jina/domain name sawa na tovuti yako. Mfano, tovuti yako inapatikana katika anwani ya www.mfano.com, hivyo barua pepe yako ya kiofisi unaweza kuchagua kuwa info@mfano.com au maulizo@mfano.com au jinalako@mfano.com. Kwa kutumia barua pepe zenye jina sawa na anwani ya tovuti yako, unajiweka katika nafasi nzuri ya kuimarisha biashara yako na kuongeza wateja wapya na kazi zenya manufaa haraka zaidi katika biashara/kampuni yako. Hii ni sababu muhimu sana unapojiuliza kwanini ni muhimu kuwa na website (tovuti) rasmi ya biashara yako. Website inakufanya unakuwa official kiukweli kweli.

Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna bora za kuimarisha uchumi wa biashara yako kwa kutumia Teknolojia:

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. BRANDING vs MARKETING, KIPI NI KIPI?
  3. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA (AfCFTA), KUNA MANUFAA GANI KWAKO?
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO.

Umejifunza nini kupitia makala hii ya kuhusu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Tafadhali unaweza kuwasilisha maoni yako kupitia sanduku la maoni (comments box) lililo hapo chini au kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yanayopatikana katika Footer Bar chini kabisa ya ukurasa huu. Pia usisite kuwashirikisha wenzako makala haya kwa kushare link yetu ya https://rednet.co.tz mara zote. Karibu!

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

FAHAMU KUHUSU UVUVI NA BIASHARA YA SAMAKI BARANI AFRIKA

Japokuwa inafanyika zaidi maeneo ya vijijini na katika hali duni ya zana za utendaji, elimu pamoja na teknolojia, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado inahangaika katika kujiboresha huku ikifichwa katika kivuli cha shughuli za Kilimo na Ufugaji. Mbaya zaidi sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado haijapewa umuhimu inayostahili barani humo. Zaidi sekta hio hutoa chakula cha kuwalisha watu zaidi ya milioni 200 barani humo na nje ya bara la Afrika. Leo sasa fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika. Twende mpaka mwisho.

Benki ya Dunia inaripoti kwamba shughuli za uvuvi na biashara ya samaki huchangia moja kwa moja dola za kimarekani $24 bilioni katika uchumi wa Afrika kwa ujumla, ikiwakilisha 1.3% ya jumla ya pato la ndani (GDP) la Afrika katika mwaka 2011. Vile vile sekta hio imezalisha ajira kwa zaidi ya watu milioni 12 ambapo 58% kati yao ni wavuvi na 42% wanajihusisha na kuandaa samaki waliovuliwa kabla ya kuwapeleka sokoni. Tanzania peke yake, sekta ya uvuvi imetoa ajira kwa watu 183,000 mpaka kufikia mwaka 2014 (chanzo: Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi) Ikionekana kwamba shughuli za uvuvi hufanywa zaidi na wanaume, 59% ya shughuli za kuandaa samaki kabla ya kuwaingiza sokoni hufanywa na wanawake.

Ukiachana na faida za samaki kama chakula katika kupatikana kwa virutubisho muhimu kama vitamini, protini na mafuta, zaidi, sekta ya Uvuvi na biashara ya samaki inachangia sehemu muhimu sana katika kuendesha maisha ya watu haswa vijana ikiwa watachukua angalizo katika fursa zilizopo kwenye sekta hio.

Changamoto; Je, kuna fursa zipi katika kufanya shughuli hii ya uvuvi na biashara ya samaki katika kukuza uchumi? Teknolojia ina mchango gani katika kuboresha uchumi wa mtu mmoja mmoja kupitia setka hii?

Tishio kubwa katika shughuli za uvuvi na biashara ya samaki ni athari zinazotokea katika mazalio ya samaki baharini, mtoni, ziwani au kwenye mabwawa. Umoja wa Mataifa na nchi  jumuishi duniani zimeingia uwoga juu ya upatikanaji wa hazina ya samaki katika soko la dunia. Shirika linaloshughulikia maswala ya Chakula duniani, FAO, limetabiri kwamba zaidi ya 70% ya aina (species) za samaki zinakaribia kuangamia au zimevunwa sana ambapo aina za samaki kama Tuna, Swordfish, Haddock na Flounder zipo katika tishio la kuangamia. Zaidi, uvuvi unaotumia chandarua au baruti huweza kusababisha kunaswa au kuuwawa kabisa kwa samaki na viumbe wengine wa baharini ambao hawajapangwa kuvuliwa kama ngasa, pomboo na papa.

Hata hivyo, shughuli za uvuvi zina faida gani katika maisha ya mwanadamu ikijumuisha?

  1. CHAKULA;  Samaki ni chanzo cha vitamini na protini katika lishe haswa ya mwanadamu ambapo madaktari na wadau wa sekta ya afya hushauri ulaji wa nyama nyeupe mfano samaki zaidi katika mlo. ulaji wa samaki kwa wingi huchochea ukuaji bora wa afya ya akili pamoja na wingi wa protini katika nyama hio huku ikiwa na kiasi kidogo cha lehemu (cholesterol) zaidi kuliko nyama nyekundu mfano ng`ombe, mbuzi na kadhalika.Ripoti zinaonyesha kwamba wakazi wa nchi za ukanda wa bahari ya Pacific peke yake hupata zaidi ya 25% na 69% ya protini za wanyama wanaokula kila siku kutoka katika samaki. Hii imepelekea shughuli za uvuvi na biashara ya samaki kukua kwa kiasi kikubwa kama shughuli rasmi ya kiuchumi ambayo imeajiri watu takribani milioni 200 dunia nzima na ikizalisha pato la dola za kimarekani zaidi ya 80 bilioni kwa mwaka.
  2. UKUAJI WA UCHUMI; Sekta hii ya uvuvi inachangia kwa kiasi kikubwa sana katika ukuaji wa uchumi barani Afrika mpaka dunaini kote ambapo watu zaidi wa milioni 200 wamejipatia ajira kupitia sekta hio. Nchini Uganda kwa mfano, uvuvi wa ziwani umekuwa na thamani ya zaidi ya dola $200 milioni  kwa mwaka ikiwa ni mchango wa 2.2% katika pato la taifa (GDP) la nchi hio. Vile vile watu zaidi ya 135,000 wamepata ajira kama wavuvi katika sekta hio na wengine 700,000 zaidi katika mchakato wa kuandaa samaki kabla hawajafikishwa sokoni na hivyo kuzalisha zaidi ya dola $87.5 milioni kama mapato ya biashara za nje ya nchi (exports earnings). Hapa miundombinu ya barabara na reli ina mchango mkubwa sana katika kuhakikisha kitoweo hiki kinamfikia mlaji kikiwa katika ubora wa hali ya juu. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa miundombinu pitia makala hii hapa;
  1. Vile vile nchini Tanzania kupitia katika mabwawa, maziwa, mito na bahari vilivyomo nchini humo, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki imetoa ajira za moja kwa moja kwa watu takribani 183,800 na wengine zaidi ya 4,000,000 wakijihushisha kama watengenezaji wa vyombo vya uvuvi (ngalawa, boti, ndoano, neti n.k), waaandaaji wa samaki kabla hawajafikishwa sokoni, wachuuzi na wafanyabiashara wa samaki wa jumla na rejareja. Sekta hii ya uvuvi na biashara ya samaki inawapatia watu kipato cha fedha za kigeni, pamoja na kitoweo kwa watu waishio pwani ya bahari ya hindi pamoja wa walaji wa samaki kutoka sehemu zingine katika nchi hio ambapo sekta hio huchangia katika pato la taifa takribani 2.4%. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi katika mwaka 2016.

Kiujumla, mpaka kufikia mwaka 2001 uta fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika katika masoko ya kimataifa ilikuwa na thamani ya dola $2.7 bilioni ambayo ni 5% ya jumla ya thamani ya sekta nzima ya uvuvi na biashara ya smaki duniani ambayo ni dola $56 bilioni. Kwa mujibu wa shirika la FAO, bidhaa za samaki zimejumuisha zaidi ya 10% ya jumla ya biashara za kimataifa (exports) katika nchi 11 barani Afrika.

Sasa Baada ya kuyajua Hayo Yote, Kwanini Ufanye biashara hii ya Uvuvi na samaki?

Mwaka 2019 watumiaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania waliongezeka kufikia milioni 23, ongezeko la watumiaji takribani milioni 1 kutoka mwaka jana 2018. Vile vile watumiaji wa huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi wamefikia takribani milioni 20 hadi kufikia mwaka huu 2019. Hii ni kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA.

Hivyo kupitia ripoti hio ya TCRA mfanyabiashara anaweza kuhamishia shughuli zake kupitia simu mkononi na simu janja (smartphones) katika kuhakikisha biashara yake inawafikia watu wengi zaidi katika muda mfupi kwa njia ya Teknolojia. Hata hivyo mfanyabiashara anaweza kutengeneza majukwaa ya kimtandao kama tovuti za kibiashara (online shops na ecommerce websites) ambayo anaweza kuuza bidhaa zake za samaki kirahisi katika masoko ya ndani na hata yale ya kimataifa kwa gharama nafuu zaidi kuliko ulivyokua hapo kabla.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Kwa kutambua hilo, biashara ya mtandaoni imekuwa ikizidi kufanikiwa sana nyakati hizi huku ikichochewa na maboresho katika miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji. Hivyo ni muhimu kufungua tovuti rasmi ya biashara yako ili kuipa utambulisho usio na shaka ukiwa mtandaoni. Vilevile ni muhimu kufungua akaunti za mitandao ya kijamii ili kusudu uzidi kujiweka karibu na wateja wako na kujua namna nzuri ya kuwahudumia.

Link zifuatazo zitakusaidia sana uweze fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika kupitia mtandaoni iwe na mafanikio zaidi na zaidi:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO

Je umepata nini katika mada ya leo katika ku fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?