Tag: umuhimu wa taarifa

UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-commerce BUSINESSES)?

Japokuwa imechelewa, lakini kwa sasa Africa ndio inaongoza mbio katika kufanya mapinduzi ya kidijitali kuliko sehemu yoyote duniani. Namna ya kufanya biashara inazidi kubadilika ikionyesha nia ya dhati kufanya maendeleo ya kiuchumi, miundombinu na maswala ya kijamii. Mwaka 2018 nchi wanachama wa Umoja wa Africa walipiga hatua kubwa katika mfumo wa kufanya biashara na muingiliano wa kiuchumi baada ya kuanzisha Eneo Huru la Kufanyia Biashara barani (Continental Free Trade Area AfCFTA). Eneo hili lililoanzishwa linashirikisha nchi 22 zilizoweka sahihi tayari na utekelezwaji wake ulipangwa kuanza mwaka 2019 (tayari umeshaanza).

Hata hivyo mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuzishirikisha nchi ambazo bado si wanachama wa eneo hili jipya, inatarajiwa eneo hili kufikia soko la watu takribani bilioni 1.2 barani wakiwa na jumla ya pato la ndani la taifa (GDP) la dola za kimarekani trilioni 2.5 kwa pamoja, kwa mwaka. Hii inatarajiwa kuwa ni mapinduzi makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nyanja ya uchumi wa Afrika.

Sasa, swali linakuja; Afrika(wafanyabiashara, makampuni/mashirika na Serikali) imejiandaa vipi na mapinduzi haya ya uchumi wa kidijitali? Na zaidi, watunga sera/sheria wataangalia vipi biashara za kielektroniki (e-commerce) kama mada muhimu katika eneo hilo jipya la kufanya biashara huru barani?

Tume ya kudhibiti uchumi wa Africa ya Umoja wa Mataifa (ECA) ikishirikiana na Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) pamoja na Baraza la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo ya kibiashara (UNCTAD) mwaka huu 2019 imechapisha ripoti yake ikiangazia maendeleo ya Afrika kiujumla katika nyanja za kiuchumi, siasa na kijamii.

URAHISI: Imeonekana kwamba e-commerce inaweza kufanya biashara ya bidhaa na huduma kwa urahisi zaidi ambapo itarahisisha mwenendo mzuri wa biashara kati ya wazalishaji, wafanyabiashra na walaji pamoja na kumbukumbu zao na miamala ya kifedha.

MITANDAO YA KIJAMII: Pia imeonekana kwamba e-commerce inapatikana na kufanyika kirahisi katika mitandao ya kijamii kama facebook na Instagram ambapo ndipo mahali kuna watumiaji wengi zaidi wa Intaneti duniani (zaidi ya watu bilioni 2 kati ya watumiaji bilioni 4 wa intaneti).

KUTOKUWA NA MIPAKA: Mfumo wa uchumi wa Kidijitali kiasili umetengenezwa kuepuka mipaka ya kijiografia katika kufanya biashara na kubadilishana fedha ambapo mabadiliko haya ya kiteknolojia yataongeza umakini zaidi katika mwenendo wa masoko na gharama. Lakini bado wimbi kubwa la watu watakaoshiriki kwenye soko barani wanaonekana wataachwa nyuma kutokana na kutokuingiliana kwa lugha na vita/ghasia za mara kwa mara katika baadhi ya jamii/nchi.

BIASHARA: Kwa mujibu wa UNCTAD mwaka 2016 kwa dunia nzima e-commerce iliweza kupitisha mauzoya takribani dola trilioni 26 ambapo 90% ilikuwa ni Biashara kwa Biashara (B2B e-commerce) na 10% ilikuwa ni Biashara kwa Mlaji (B2C e-commerce). Hata hivyo kupima mwenendo wa e-commerce katika baadhi ya nchi zinazoendelea imekuwa ni changamoto kupata data na takwimu, haswa katika nchi za Afrika.

IMPORTATION: Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kwamba Biashara kati ya nchi na nchi imekua kwa kiasi kikubwa Afrika ambapo zimechagizwa na vituo vichache vya kiteknolojia (Hubs) ambavyo vimerahisisha mno mwenendo wa biashara. Biashara kati y nchi na nchi (Intraregional import) imekuwa zaidi ya mara 3 katika miongo miwili iliyopita kufikia 12%- 14% sawa na dola bilioni 100 ikichagizwa na uwepo wa jumuiya za kiuchumi barani (Subregional Economic Communities REC‘s).

UZOEFU: Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na umri wa Jumuiya hizi za Kimaendeleo barani Afrika ambapo uzoefu huo hutumika kuongeza jitihada katika kuboresha namna ya ufanyaji biashara kuelekea uchumi wa kidijitali kiteknolojia. Uzoefu huo pia hutumika kuunganisha jumuiya moja na nyingine (mf, SADC na COMESAna EAC) ambapo zitazalishwa nafasi nyingi zaidi za kufanya biashara kati ya nchi wanachama na ripoti zinaonyesha 75% ya biashara hizi ndani ya jumuiya barani Afrika zimefanyika mwaka 2017 peke yake na nusu ya biashara hizo zilifanyika katika jumuiya ya SADC.

Chini ya mwavuli wa AfCFTA nchi wanachama zinatarajia kufuta tozo/ushuru kwa 90% ya bidhaa zote zitakazopitishwa na kufanyiwa biashara katika eneo hilo. Hii itaruhusu uwezekano wa kupunguza mlolongo wa kodi au kuongeza idadi na thamani ya bidhaa na huduma zitakazohusishwa. Matokeo yoyote katika punguzo hilo linalotarajiwa katika muktadha wa biashara kidijitali yataleta picha tofauti. Kupunguza mlolongo wa tozo za mipakani baina ya nchi na nchi kutapungua kwa 15% pekee ikitegemea thamani ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi husika. Hii ni kwa mujibu wa Tume inayoshughulikia Uchumi wa Afrika kutoka Umoja wa Mataifa (UNECA) mwaka 2018.

Sasa mwaka 2018 Jumuiya ya COMESA ilibuni mfumo wa kudhibiti eneo huru la kibiashara kidijitali (Digital Free Trade Area DFTA). Mfumo huu umeundwa na mambo yafuatayo;

•E-trade: Hili ni jukwaa mahsusi kwa ajili ya kufanya biashara za kimtandao na kuwezesha malipo ya kielektroniki, mobile apps kwa ajili ya wafanyabiashara walioko katika Jumuiya hio.

•E-logistics: hili ni jukwaa maalum kwa ajili ya kuwezesha biashara ya usafirishaji wa mizigo baina ya nchi wanachama wa jumuiya.

•E-legislation: huu ni mfumo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara rasmi ambao unawawezesha kufanya miamala na malipo kielektoniki.

Mfumo huu uliobuniwa na Jumuiya ya COMESA umelenga kutangaza biashara za wanajumuiya katika nchi wanachama ikijumuisha kupitia majukwaa ya e-commerce. Mfumo huu ulikuwa ni mfanano wa mfumo uliotengenezwa na kuzinduliw na nchi ya Malaysia mwaka 2017 katika muktadha wa kufanya biashara huru ndani ya eneo maalum.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.

Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana, shuka nazo:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-biashara-ya-fedha-za-kidijitali-cryptocurrency-business/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)”
  2. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia;

e-mail: info@rednet.co.tz

tovuti: https://rednet.co.tz

Simu:+255765834754

fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika

FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA TEKNOLOJIA YA 5G

Dunia ipo mbioni kuelekea zama za matumizi ya teknolojia ya 5G katika kasi ya Intaneti. Mpaka kufikia mwaka 2020 huduma za kibiashara za 5G zilishaanza kupatikana katika nchi zaidi ya 50 kutoka Asia, Ulaya, Mashariki ya Kati na Amerika ya Kaskazini. Muongo wa 2020s’ ndio unatajwa kushuhudiwa kwa usambazaji mkubwa zaidi wa teknolojia hii ya kasi ya intaneti duniani ikijumuisha nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara. Sasa leo kwa uchache uta fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika.

Kufikia mwaka 2022 tu tayari kampuni ya Vodacom Tanzania walishazindua huduma zao za 5G nchini na kuwa kampuni ya kwanza ya mawasiliano kuzindua huduma hizo. Hakika maendeleo ya teknolojia hii yanakwenda kasi sana.

Sasa ili kujua kwa undani kuhusu teknolojia hii pamoja na matarajio yake katika kufanikisha shughuli za kila siku za kibinadamu, kitengo maalum cha kijasusi katika shirika la GSMA kiliendesha ziara iliyohusisha wabia muhimu ili kupata maoni halisi ya watumiaji wa intaneti kuhusu ujio wa 5G katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara. Uchunguzi huo ulijumuisha maeneo sita ambayo ni; matumizi ya mtandao (network deployment), wigo wa mtandao (spectrum), watumiaji (use cases), mifumo ya biashara na fedha (business model and finance), sera na sheria (policy and regulations) pamoja na ushirikiano wa kibiashara na matokeo ya mbeleni.

Katika maeneo hayo walengwa waliojumuishwa walikuwa ni wasimamizi wa mashirika wa mawasiliano katika ukanda huo, kampuni za simu zilizo na hisa zaidi ya 75% kwa pamoja katika ukanda huo pamoja na wauzaji wa vifaa vya mawasiliano ambao wana hisa za zaidi ya 90% ya soko la miundombinu ya kimtandao katika ukanda huo.

Takwimu zilizotolewa na ripoti ya uchunguzi huo ambayo imechapishwa Mwezi July, 2019 zilitokana na uchambuzi wa maoni ya watu mbali mbali kuhusu 5G. Pia matokeo haya yamejumuisha data kutoka vyanzo mbali mbali vinavyohusiana na teknolojia hii ambapo wataalamu waliounda na kendeleza teknolojia hii wataangalia kwa makini watumiaji wa mfumo huu katika ukanda wa kusini mwa Jangwa la Sahara, lengo kuu likiwa ni kujifunza na kujiimarisha zaidi kutoka kwa vinara wa 5G.

Teknolojia za kidijitali zimekuwa muhimu sana katika shughuli za kibinadamu za kila siku. Hii ni muhimu zaidi katika nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo kama teknolojia hizo zisingekuwepo mambo yangekuwa magumu zaidi kutokana na ubovu na uchakavu wa miundombinu, maswala ya fedha pamoja na ujuzi binafsi wa mtu. Sasa ripoti hio iliyotengenzwa kutokana na uchunguzi wa kitengo cha Intelijensia cha shirika la GSMA imekuja na majibu kadha wa kadha;

MAPINDUZI KATIKA KASI YA INTANETI YA 5G YAMEFIKA:

Kufikia mwisho wa mwaka 2019 kulishakuwa na mtandao mkubwa wa kasi ya 3G na 4G zaidi kuliko 2G katika ukanda huo wa kusini mwa Afrika. Hii inaonyesha ukuaji kutoka huduma za sauti mpaka huduma za data. Uwekezaji unaoendelea kufanyika katika 4G umepeleka ukubwa wa huduma za mitandao kufikia robo ya jumla ya watu waishio katika ukanda huo. Vile vile imeonekana kwamba matumizi ya simu za rununu (smartphones) yameongezeka mara mbili ndani ya miaka mitano iliyopita.

jinsi ya kuanzisha website umuhimu wa tehama.

fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika

TEKNOLOJIA YA 5G ITAKUWA NI SEHEMU YA MIUNDOMBINU BORA YA KIMTANDAO, JAPO UENEAJI WAKE HAUTAKUWA WA KASI SANA:

Katika ukanda huu, teknolojia ya 5G haizuiliki. Ni maendeleo ya kiasili kutoka katika teknolojia zilizopita. Japokuwa, kasi ya ueneaji wa teknolojia hii ya 5G si kubwa katika ukanda huu kutokana na uwepo wa teknolojia zingine kama 3G na 4G bado zina uwezo wa kumsaidia mwanadamu kufanya shughuli zake katika kasi inayoridhisha ya intaneti.

Takribani theluthi mbili (2/3) ya walioshiriki kwenye uchunguzi huu wanatarajia huduma za kibiashara za 5G kuwa katika masoko yao kabla ya mwaka 2025. Pia teknolojia hii itasaidia kupevuka na kuweza kutumika katika masoko mengine. Vile vile itaruhusu uchumi kukua kwa kutumia teknolojia ya 5G katika vifaa vya kielektroniki ambavyo vitapunguza gharama za waendeshaji na wateja. Hapa ndipo tuta fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika kwa undani wake kabisa.

UTAYARI WA SOKO NI MUHIMU KATIKA KUKUZA THAMANI YA TEKNOLOJIA YA 5G:

Kwa nchi zote zilizo katika ukanda huu utayari wa soko ni jambo muhimu zaidi kufanikisha mageuzi ya teknolojia ya kasi ya 5G. Hii itasaidia kukuza thamani katika huduma za 5G kwa wateja, waendeshaji na jamii nzima kwa ujumla. Kiwango cha utayari wa soko kinaonyesha kwamba baadhi ya nchi zinakwenda kasi kwenye matumizi ya teknolojia hio kutoka 4G.

Kufikia mwaka 2025 huduma zinazotumia teknolojia yenye kasi ya intaneti ya 5G itafikia nchi 7 zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara ikijumuisha ni Kenya, Nigeria na Afrika Kusini. Pia uchunguzi umetabiri kuwako kwa miunganiko milioni 28 ya simu kwa kutumia 5G, sawasawa na 3% ya jumla nzima ya miunganiko ya kimtandao ya simu katika ukanda huo.

MASHIRIKA NA MAKAMPUNI MAKUBWA YATAONGOZA KUANZA KUTUMIA 5G KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA:

Teknolojia ya 5G itawezesha makampuni ya mawasiliano na mashirika kuhudumu vizuri zaidi kwa wateja wao ambapo watumiaji wa mwanzoni watawezeshwa na huduma ya wireless (Fixed Wireless Access #FWA) ili kutoa changamoto kwenye matumizi, gharama na upatikanaji wa huduma za kimtandao kama huduma za satelaiti na intaneti. Hapa sasa ndipo uta fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika kwa ukaribu zaidi.

KWA WATEJA NA WATUMIAJI ITAKUWA NI ZOEZI LA MUDA MREFU:

Hii ni kutokana na udhaifu katika upatikanaji wa huduma/vifaa(simulaptop..) bora Kwa gharama nafuu pamoja na ujuzi wa matumizi ya teknolojia kama virtual reality (VR) na Augmented Reality (AR). Ubora wa vifaa kama simu za rununu (smartphones) na kompyuta ni muhimu zaidi katika zama za 5G kwa matumizi ya wateja lakini inategemewa malengo ya teknolojia hii ni kufikia vifaa vya nyumbani (Customer Premise Equipment CPE) kama routers ili kupata huduma za uhakika za wireless (FWA).

Hii ni kwa kuwa huduma hizo hupatikana kwa malipo ya kabla kutoka kwa makampuni ya simu, ambapo katika muda huo huo huduma ya kasi ya 4G itaendelea kuhudumu kwa kasi inayoridhisha na kuwafikia watumiaji wengi zaidi ambao watachangia ukuaji mzuri wa uchumi.

KIPAUMBELE KITAWEKWA KATIKA KUPATA UHAKIKA WA HUDUMA YA WIRELESS (FWA):

Ukuaji wa Matumizi ya intaneti katika vifaa kama simu na kompyuta ni mdogo mno ambao ni chini ya 2% katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara, hivyo kufanya ujio wa zama za 5G kuegemea kwanza katika CPE’s. Hii itapunguza gharama za uendeshaji lakini pia itaongeza watumiaji kwa kutumia wireless (FWA). Mbinu hii ya kufikisha teknolojia kwa jamii inalenga kwa suluhu mbadala kwa makampuni ya mawasiliano kulinganisha gharama za kuhudumia/kufikia simu moja moja na uwezo wa watumiaji wengi kuelekea zama za kasi ya 5G.

fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika

Hio ndio mantiki ya mada yetu ya leo katika ku fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika, kwa ufupi. Unataka kujua zaidi? Karibu uwasiliane nami kwa njia ya WhatsApp kupitia namba hii hapa 0765834754 Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo hapa. Zitakusaidia sana ukizipitia:

  1. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  2. TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI
  3. FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA DUNIANI
  4. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?

FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)

Waswahili wanasema “Nyakati ngumu hazidumu bali watu wagumu ndio hudumu.” Na pia “Baada ya dhoruba huja shwari.” Sasa mnamo mwaka 2008 uchumi wa dunia ulikumbwa na mtikisiko mkubwa zaidi kuwahi kutokea baada ya ule Mtikisiko wa kiuchumi wa mwaka 1933. Katika mdororo huo taasisi na mashirika ya kifedha duniani yalijikuta yakishindwa kuzuia hali duni ya uchumi katika bei za bidhaa ghafi kama mafuta na mikopo ya aina mbali mbali ambapo ilipelekea huduma hizo muhimu kupatikana eidha kwa tabu sana au kwa bei isiyokidhi usawa wa soko.

Hivyo ni katika hali hio ya mdororo wa kiuchumi ndipo lilipoibuka jina la Satoshi Nakamoto ambalo linasadikiwa kuwa ni jina la kifumbo la mtu mmoja au kikundi cha watu wasiofahamika hadharani mpaka sasa ambao ndio waliotengeneza sarafu ya kwanza kabisa ya mtandaoni na wakaiita BITCOIN. Pia mtu/watu hao ambao wanasadikiwa kuwa na asili ya Kijapani walitengeneza mfumo wa kwanza wa database ya Teknolojia ya Blockchain kwa kupitia kiunzi (ledger) cha kimtandao ambacho hakitegemei hifadhi moja. Yaani taarifa za miamala ya kifedha katika BITCOIN hufanyika kupitia Miundombinu ya Blockchain ambayo huwa ni ya siri mno na iliyotawanyika duniani kote na hivyo kuzifanya sarafu za mtandaoni zisiweze kudhibitiwa na taasisi na mashirika ya kifedha au hata vyombo vya kiserikali.

Kwanini ikawa hivi? Fuatana nasi kujua zaidi..

Kwa mujibu wa tovuti za study.com na Investopedia, Sarafu za mtandaoni au Cryptocurrency ni sarafu za kidijitali zinazoakisi thamani ya fedha ambapo kukua au kudorora kwa thamani hio hutegemea na uhitaji wa sarafu hio duniani kwa muda huo. Mfano wa sarafu hizi ni kama bitcoin, ethereum, Litecoin, Libra na kadhalika. Mpaka kufikia tarehe 20 June, 2019 BITCOIN thamani yake ilikuwa ni dola za kimarekani 9,259.37 na ETHEREUM ikapatikana kwa dola 269.11, Litecoin ikapatikana kwa dola 136.29 na kadhalika. Inakadiriwa mpaka kufikia February, 2019 tayari mtandaoni kulikuwa na sarafu 2500 tofauti tofauti za kimtandao ambapo pia iliripotiwa kuwa na miamala au mizunguko ya Bitcoin peke yake zaidi ya milioni 17.53 ambayo thamani yake inakadiriwa kuwa ni takribani dola bilioni 63.

Hata hivyo mpaka sasa soko la sarafu za mtandaoni limekua mpaka kufikia zaidi ya dola bilioni 120 huku sarafu ya Bitcoin peke yake ikichukua zaidi ya nusu ya thamani ya soko zima.

DHUMUNI LA KUANZISHWA CRYPTOCURRENCIES:

Neno Cryptocurrency ni mjumuisho wa maneno mawili, ‘Crypto’ na ‘currency’. Yaani sarafu iliyobadilishwa katika ulinzi wa kimtandao uitwao cryptography ambao huipa sarafu thamani yake ya kipekee na pia kuweza kuifanya sarafu hio isiweze kudukuliwa kirahisi.

Kutengeneza urahisi zaidi wa kulipia huduma na bidhaa mtandaoni, huduma za hoteli, migahawa, kurusha fedha kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa uhuru na wepesi zaidi na pia kubadilisha fedha katika masoko ya kimtandao ya kubadili fedha. Hizi ni baadhi ya sababu za kuanzishwa kwa sarafu hizi za mtandaoni, lakini sababu kubwa ni kuhakikisha ulinzi madhubuti na uhuru wa mtu kuhifadhi na kutumia fedha zake katika muda wowote atakaohitaji bila kufuatiliwa na taasisi au mashirika ya kifedha au vyombo vya serikali. Yaani kuwa na uhuru halisi juu ya fedha zako.

ZINAFANYAJE KAZI SARAFU HIZI?

Cryptocurrency zinafanya kazi kwa mfanano kama kadi ya benki ambayo huruhusu kufanyika miamala mbalimbali ya kutuma na kupokea fedha katika mfumo tata wa kielektroniki wa kifedha. Utofauti na utendaji wa kadi ya benki ni inaweza kufuatiliwa na taasisi za kifedha na mashirika ya kiserikali na pia huhifadhi kumbukumbu za wateja mahali pamoja.

Miamala hutumwa baina ya kompyuta washirika kwa kutumia programu ziitwazo “cryptocurrency wallets” ambapo mtu anayefanya muamala hutumia programu hio ya wallet kutuma fedha kutoka akaunti moja kwenda akaunti nyingine. Hata hivyo, ili kuweza kutuma au kupokea fedha katika mfumo huu, huna budi kuwa na nywila(password) au ufunguo binafsi ambayo inahusiana na akaunti yako. Miamala hio inayohusisha kompyuta washirika hufichwa katika msimbo wa kimtandao (encryption) halafu hutumwa katika mtandao wa sarafu hizo duniani ambapo huorodheshwa katika forodha ya jumla iliyohifadhiwa mtandaoni. Kiasi cha miamala inayopitishwa huwa ni wazi, lakini anayetuma muamala huo hufichwa, hii huitwa pseudo-anonymous ambapo ambapo kila muamala huwa na seti ya kipekee ya nywila (keys/passwords) na yeyote anayemiliki nywila hizo ndiye anayemiliki sarafu zote zilizo ndani ya akaunti hio. Kama ilivyo tuu kwamba anayemiliki akaunti ya benki ndiye anamiliki fedha zote zilizo ndani ya akaunti hio.

UNAWEZAJE KUWEKEZA KWENYE CRYPTOCURRENCY?

Sababu kuu ambayo huvutia watu wengi kuwekeza katika cryptocurrency ni kuweza kupata fedha nyingi zaidi muda mchache tuu baada ya kuwekeza mtaji. Hata hivyo kwa mujibu wa mtandao wa Forbes haya hapa chini ni baadhi ya mambo ya msingi zaidi ya kuzingatia kabla hujaamua kuweka fedha zako kama mtaji katika biashara hii:

1. AMUA AINA IPI YA CRYPTOCURRENCY UNGEPENDA KUSHUGHULIKA NAYO ZAIDI: Kama ilivyo muhimu kujua kujua kiasi cha mtaji unachokwenda kuwekeza, vile vile ni busara kuwa na mipango mizuri katika kuelewa misingi ya cryptocurrency hiyo kwa kuwa itachangia kwa kiasi kikubwa jinsi ya kujikinga na matishio yajayo ya kiuchumi.

2. AMUA UTATAKA KUWA NA UWEKEZAJI WA NAMNA GANI: Kwa kawaida utalazimika kuwa na mpango kama unataka kuingia katika masoko ya cryptocurrency. Swali ni mipango yako inaweza kuwa ya muda mrefu, wastani au ya muda mfupi. Hii itategemeana na fedha ulichonacho.

3. KUMBUKA, TAKWIMU ZA SOKO NI MUHIMU ZAIDI: Soko la sarafu za crypto ni tete muda wote. Huweza kubadilika hata kwa asilimia 20 kwa siku, hivyo ni muhimu kufuatilia taarifa za soko kwa ukaribu zaidi.

Umejifunza jambo gani kwenye makala haya? Tafadhali pitia makala tumekuwekea hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala hii ya leo kisha, acha maoni yako chini hapo kwenye sehemu ya comments..

  1. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  2. https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-biashara-za-kielektroniki-e-commerce-businesses/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI?”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-mapinduzi-ya-teknolojia-ya-5g-katika-biashara-na-uchumi-wa-afrika/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA TEKNOLOJIA YA 5G KATIKA BIASHARA NA UCHUMI WA AFRIKA”
  4. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO (BUSINESS INTELLIGENCE)?

FAHAMU KUHUSU MFUMO WA MAWASILIANO YA SIMU (MOBILE ECOSYSTEM) NA FAIDA ZAKE KATIKA BIASHARA

Je Wajua?

Mfumo wa mawasiliano ya simu (mobile ecosystem) huchangia shemu muhimu sana katika uchumi wa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara? Uchumi wa nchi hizo kwa pamoja umefikia thamani ya dola za kimarekani bilioni 110 ($110 b) ambayo ni sawa na 7.1% ya pato la taifa (GDP) katika mwaka 2017. Hii inajumuisha faida za moja kwa moja za mfumo huo, faida zisizo za moja kwa moja (indirect impact) pamoja na ukuaji wa uzalishaji unaoletwa na matumizi ya huduma za simu na teknolojia.

Tukigusia faida za moja kwa moja za mfumo huu wa mawasiliano ambao unajumuisha makampuni ya simu, watengenezaji wa huduma za miundombinu ya kiteknolojia, wasambazaji wa huduma/ bidhaa za simu, wafanyabiashara wa reja reja, watengenezaji wa simu na vifaa vyake pamoja na watengenezaji wa maudhui/applications/huduma za mtandaoni; mchango wao katika uchumi hukadiriwa kwa kupimwa thamani wanayochangia katika uchumi wa nchi husika ambayo hujumuisha bima ya wafanyakazi, faida ya ziada ya biashara pamoja na kodi.

Mwaka 2017, thamani iliyozalishwa na mfumo huu wa mawasiliano katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara ulikuwa dola bilioni 40 ambayo ni sawa na 2.5% ya pato la Taifa (GDP) ambapo makampuni ya simu peke yake yalijumuisha takribani 75% ya mchango huu.

Ukiachana na faida za moja kwa moja, zipo pia faida ambazo si za moja kwa moja (indirect impact) ambapo sekta hii hununua vifaa/huduma mbali mbali kutoka sekta nyingine. Kwa mfano makampuni ya simu hulazimika kununua umeme kutoka sekta ya nishati hali kadhalika wasambazaji na wafanya biashara wa reja reja wa vifaa/huduma za simu huhitaji usafiri kuwafikia wateja wao.

Kwa pamoja uzalishaji huu wa faida isiyo ya moja kwa moja ulitengeneza takribani 60$ mwaka 2017 (ambayo ni takribani 4% ya pato la taifa). Kiujumla ukiongezea na faida za moja kwa moja, sekta hii ya mawasiliano ya simu ilitengeneza 110$ bilioni sawa na 7.1% ya pato la taifa katika ukanda huu.

Hii inaleta picha gani Kibiashara?

Matumizi ya teknolojia ya simu pamoja na maendeleo ya simu za rununu (smartphones) huendesha uchumi kwa kuboresha uzalishaji, kupunguza costs za uendeshaji pamoja na kurahishisha upatikanaji wa huduma/bidhaa za kibinadamu.

Chanzo: Ripoti ya shirika la mawasiliano ya simu duniani la GSMA toleo la mwaka 2019.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”

TEKNOLOJIA KATIKA BIASHARA ZA KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA (TECHNOLOGY IN SUB SAHARAN BUSINESS )

Kwa watumiaji wengi wa simu za mkononi waishio Kusini mwa jangwa la Sahara, simu ya mkononi si kwamba ni kifaa cha mawasiliano tu, lakini zaidi ni kifaa muhimu cha kuperuzi mtandaoni na kupata huduma mbalimbali za msingi za kibinadamu. Ujio wa simu za rununu (Smartphones) eneo hilo umekuwa maradufu katika miaka ya hivi karibuni. Watumiaji wa simu za rununu wameongezeka kutoka 25% mwanzoni mwa muongo huu (2010’s) mpaka kufikia 44% mwishoni mwa mwaka 2017. Hii ni chini ya wastani wa kidunia wa 66% katika ongezeko hilo la watumiaji wa simu za mkononi. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa shirika la kimataifa la mfumo wa mawasiliano ya simu GSMA.

Watumiaji hao wa simu ambao ni 44% ya jumla watu waishio katika eneo hilo sawa na watu milioni 444 ambao pia ni aslimia 9% tu ya watumiaji wote wa simu za mkononi duniani wanatajwa kupatikana katika eneo hilo la kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia inatajwa kwamba ongezeko hilo la watumiaji litakuwa katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) kwa 4.8 katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2022, ambacho ni zaidi ya mara mbili ya CAGR ya dunia nzima katika kipindi hicho hicho.

Moja ya vitu vinavyotoa nguvu katika ongezeko hili ni pamoja na uwezo wa simu za rununu (janja) kuunganisha watu wengi kupitia huduma za intaneti na mitandao ya kijamii ambapo katika mitandao hio ndipo panapotumiwa na watu wengi kama sehemu ya kukutana, kubadilishana mawazo, kuburudika na kufanya biashara. Hivyo kufanya mitandao hio ya kijamii kuzidi kuwa na umuhimu kadiri muda unavyokwenda.

Kibiashara hii ina maana gani?

Ripoti hio ya GSMA iliyochapishwa mwaka 2018 inataja kwamba ukuaji wa teknolojia umerahisisha mambo mengi muhimu yakiwemo utolewaji wa elimu, maswala ya afya na tiba na pia kuwezesha mazingira bora ya kufanyika biashara katika kutunza na kuonyesha kumbukumbu mbalimbali, miamala ya kifedha na jinsi bora ya kumhudumia mteja hata akiwa mbali na mzalishaji kupitia majukwaa ya huduma za kifedha za kimtandao na IoT (Internet of Things). Ripoti hio pia inaakisi kasi ya ukuaji wa matumizi ya simu za rununu (samrtphones) pamoja na vifaa vya kiteknolojia mpaka kufikia mwaka 2025 katika utendaji na utoaji wa huduma mbalimbali za kibinadamu pamoja na shughuli za kibiashara katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”
  5. https://rednet.co.tz/kuanzishwa-kwa-eneo-huru-la-biashara-barani-africa-afcta-kuna-manufaa-gani-kwako/ yenye kichwa “KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?”