Tag: umuhimu wa kuwekeza

Pata huduma za Website, SEO, Social Media Marketing na nyinginezo nyingi kutoka Rednet Technologies Branding vs Marketing. Kipi ni kipi? ukweli kuhusu 'Propaganda' Jinsi ya kutengeneza Attention Mtandaoni.

Jinsi ya Kutengeneza Attention Mtandaoni

Hivi unajua kwamba aliyeshinda vita vya 2 vya Dunia ni Urusi, ndiye aliyepigana na Hitler kwa ground. LAKINI, Leo hii kila mtu anaongelea Bomu la Nyuklia la Marekani lililodondoshwa Hiroshima na Nagasaki. Unajua kwanini? Kwa sababu watu wanapenda ATTENTION duniani na leo hapa utafahamu kiundani kabisa jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni ili uweze kunasa wateja zaidi.

Marekani ni mtaalamu haswa kwenye hilo la kutengeneza attention na kusambaza propaganda zenye manufaa ya nchi yake. Jamaa wamefanikiwa kuujaza Ulimwengu “ukweli wao” kwamba lile Bomu la Nyuklia ndo limeipa ushindi taifa hilo na kwamba kwanzia hapo wao ndo wababe duniani na hakuna mwingine. Ila nyuma ya pazia Urusi ndiye anayemiliki Nyuklia nyingi zaidi.

Kujitangazia Ushindi tu, tayari alishaanza kuteka ATTENTION duniani na mataifa mengi yalianza kuvutika katika Silaha, Siasa, Utamaduni na Biashara zingine za Kimarekani. Leo hii Marekani ndo nchi inayosifika kuuza silaha zaidi duniani, Makampuni makubwa karibu yote yapo USA, Microsoft, Google, Meta, Yahoo, Space X nakadhalika.

Marekani ndo nchi inayotambulika kwa mifumo bora ya Kidemokrasia duniani, na mambo kedekede tayari unayajua kuhusu hao jamaa. Unadhani Marekani alipata wapi sifa zote hizo? Kwamba Urusi hana huo ubavu wa kuuza silaha au teknolojia za kisasa? Jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni is the damn strategy they rely on.

Kwenye Biashara Attention inatengenezwa vipi?

Kwenye biashara Mtandaoni hali ipo hivyo hivyo. Ushindani ni mkali mno kila siku. Ni vita. Mtandao wa Internet Live Stat unaonyesha kuwepo na websites zaidi ya Bilioni 1.9 mpaka sasa duniani. Hebu niambie unachomokaje katikati ya vurugu lote hilo kama hujajua jinsi ya kutengeneza ATTENTION? Leo hii wewe upo hapa kwenye tovuti yetu kwa sababu umeona kuna uwezekano ukaweza kuimarisha biashara yako mtandaoni kwa kutengeneza attention fulani, si ndio?

Utaniuliza; “Sasa Faustine, nawezaje kutengeneza hio ATTENTION ili niweze kusurvive huko mtandaoni?” Zipo njia nyingi, za halali na zile zisizo halali. Hapa tutaongelea zile za halali tu. Habari za kupost utupu, vichupi na makalio hapa hazipo.

Kuijuia Google leo ndo mchongo. Binafsi ningepata nafasi ya kurudi nyuma na kumshauri Faustine wa miaka 15 enzi zile, ningemshauri atie nguvu sana kwenye kuijua jinsi Google inavyofanya kazi na namna anaweza kuitumia kukuza biashara na kunasa wateja zaidi.

Leo hii unaweza kutengeneza ATTENTION ya Biashara yako kule GOOGLE kwa kuhakikisha mtu akitafuta chochote kinachohusiana na bidhaa/huduma unazozitoa kwenye biashara yako basi anakipata mara moja na anakipata kwako chap. Hii inafanyika kwa uzuri kupitia Huduma za SEO (Search Engine Optimization).

Hivi si unajua, kwa siku 1 tu huwa kunafanyika matafuto zaidi ya bilioni 3.5 kule google. Sasa kwanini bidhaa/huduma zako tukizitafuta google kule hatukupati? Kama jibu la hilo swali linakusumbua, wala usiwe na wasiwasi tena, sekunde chache zijazo utakwenda kujua cha kufanya.

Kama unatamani kutengeneza ATTENTION kule Google mpaka ifike mahali mtu akisearch kuhusu bidhaa/huduma zako akupate haraka, basi chukua SIRI hizi hapa. Leo hapa utaziona siri (4) tu;

1. Tengeneza website yako na hakikisha inafanya kazi vizuri na ina load faster. Kwanini website? Kwa sababu ni kupitia website unaweza kutengeneza maudhui mengi ndani ya chanzo kimoja, ukafanya uchambuzi kwa kina na kuelezea kwa mapana kuhusu Faida za bidhaa/huduma zako, Mbinu, Jinsi ya kutumia na taarifa zingine. Hili pia unaweza kulifanya kupitia chaneli yako ya YouTube.

2. Andika maudhui ya kutosha kuhusu Faida za bidhaa/Huduma zako, Jinsi ya kuzitumia, Jinsi ya kupambana na Changamoto, Mbinu za kutumia bidhaa/huduma hizo kwa usahihi, Madhara ya Kutotumia bidhaa/huduma zako n.k Umeona hayo maneno hayo yaliyotumika hapo? Hayo yanaitwa Keywords.

3. Hakikisha unatumia keywords nyingi zinazohusu bidhaa/huduma zako ikiwemo JINA LA BIDHAA/HUDUMA hio. Kwenye keywords hapo ndipo Google hukusanya taarifa na kuzihifadhi kwenye database yake, tayari kwa watu kupata majibu pale watakapotafuta kuhusu bidhaa/huduma hio. Ukiweza kutumia Google kama jukwaa la biashara utafaidi sana biashara yako inapokuwa mtandaoni.

4. Ambatanisha Namba yako inayopatikana katika simu za Kawaida na WhatsApp katika makala unazozichapisha kwenye website yako na mitandao yako ya Kijamii. Hio namba yako ya simu ni muhimu sana iwe hewani muda wote. Hakikisha muda wote ukitafutwa unapatikana. Hapa ndo utajua sasa kwanini Mteja achague kufanya kazi na wewe na sio mtu mwingine.

Ukifanya hivyo, utamtengenezea mteja wako mazingira ya kukupata moja kwa moja pale atakapofikwa na uhitaji wa huduma/bidhaa zako atakazoziona huko Mtandaoni. WhatsApp kupitia Status zako unaweza kuchapisha tips, ushauri, faida nk za bidhaa/huduma zako kila siku.

Sasa, tuishie hapo kwa leo, au unasemaje ndugu yangu?

Anyway, ngoja nisikuache bure, muendelezo wa SIR hizo tayari nimeuweka kwenye eBOOK yako MPYA na BORA ya SEO ambayo nimekuandalia. eBook hio inaitwa TEKNOLOJIA YA SEO; JINSI INAIFANYA BIASHARA YAKO KUWA NA SUMAKU MTANDAONI. Katika Kitabu hiko nimekuwekea SIRI 15 tayari kabisa kukufunulia wewe jinsi SEO inavyofanya kazi na namna unaweza kuitumia kukuletea manufaa zaidi kila siku. Hi ndio kitu unakihitaji sasa.

eBook hii itakusaidia kujua mambo yote muhimu kuhusu SEO, ni nini? inafanya kazi vipi? Faida zake ni zipi? Mambo yapi ya kuzingatia ili uifaidi? Kwanini hupati wateja mtandaoni? Yote hayo na mengine mengi yameelezwa kwa mapana kabisa kwenye eBook hio.

Kama nilivyokutaarifu, kuanzia ukurasa wa 27 wa eBook nimekueleza SIRI 15 ambazo zitakusaidia katika kutengeneza ATTENTION ya biashara yako mtandaoni kupitia SEO. SIRI 15!! Hizi siri wanaojiita wataalam wa SEO unaowafahamu hawawezi kukwambia kwa kuhofia kupoteza wateja ukiwemo wewe, ila mimi nimekwambia.

Utajiuliza, Kwanini nimekwambia? Kwa sababu mteja anayo haki ya kufahamu exactly kila kinachofanyika katika mradi wake. Mfano unapojenga nyumba ukikaa karibu na fundi wako utataka kujua bei ya misumari, aina za misumari, aina za milango, mbao, rangi ipi ipakwe wapi na kwanini, aina za kokoto, mchanga wa plasta ni upi na vitu kama hivyo.

Kadhalika katika SEO, ni muhimu ukafahamu kinachofanyika humo ndani, ili uweze kushiriki kufanya mwenyewe na kupata ujuzi wa ziada. Hii ndio sababu kitabu hiki kipo tayari kwa ajili yako leo.

Sasa ukitaka kuipata hii eBook njia ni hii hapa. Save namba yangu ya WhatsApp kwa kugusa namba hii hapa, 0765834754 Kisha nitumie text yenye jina lako ili niweze kukutumia eBook hio kwa WhatsApp mara moja. Kwa sasa nitaitoa eBook EXCLUSIVELY kwa watu 20 tu.

Hata hivyo eBook yetu hii sio kila mtu ataipata. Wataoweza kuipata eBook hio ni wale tu;

1. Waliopo kwenye contact list yetu ya WhatsApp. Kuingia kwenye list hio save namba yetu hii hapa 0765834754

2. eBook itatoka rasmi Usiku wa kuamkia PASAKA kwa gharama ya shilingi 50,000/-. Lakini leo hii unapouona ujumbe huu, eBook naitoa EXCLUSIVELY kwa shilingi 15,000/- tu.

Hii OFA ni kwa watu 20 tu watakaokuwa wakwanza kulipia. Baada ya hapo OFA itafungwa. Hivyo, ndugu changamka.

LIPA Sasa hivi sh 15,000/- kupitia LIPA NAMBA Yetu ya M-PESA hii hapa 5432715 au scan QR Code unayoiona hapa. Ukishafanya malipo njoo WhatsApp na screenshot ya muamala na hapo hapo utapata eBook yako uanze kuvuta wateja kwa kutumia SIRI za Ajabu za SEO katika Mtandao wa Google.

jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni

Kumbuka Ofa ni EXCLUSIVELY kwa watu 20 tu wa kwanza kulipia. Baada ya hapo eBook itarudi bei yake halisi ya sh 50,000/-.

Kuna mtu aliwahi kuliuliza, “Sasa bro, kwanini unilipishe kufanya SEO wakati kutumia Google ni BURE kabisa?” Ungekuwa wewe ungemjibuje apo?

Sikia nikwambie kitu, Ukiona unapewa mchongo wa bure basi jua wewe ndo bidhaa hapo. Ndo ukweli huo.

Kutumia Google ni BURE. Kutumia Insta, Facebook, WhatsApp na mitandao mingine ya kijamii pia ni BURE kabisa. Kwanini? Kwa sababu kwenye BURE ndo kuna utajiri umejificha hapo.

Umeelewa hapo mchezo unavyochezwa. So nakupa SIRI hii hapa; Toa maudhui yatakayotoa majibu ya changamoto BURE yawafikie watu wengi, wachuje, wachache wawe wateja wa bidhaa/huduma zako. Njoo WhatsApp sasa ufahamu zaidi kuhusu SEO na Tech kwa namba hii 0765834754.

Unatamani ujumbe huu umfikie rafiki yako wa karibu? Umejifunza nini leo katika jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni ili uweze kunasa wateja zaidi. Unaweza kushare makala hii kwa rafiki, ndugu, boss au yeyote unayehisi anahitaji kusikia habari hii. Ni BUREE kabisa, hivyo, sambaza, uliza na comment ili ufahamu zaidi.

Cheers.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni. Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

JINSI YA KUONGEZA MBINU ZA KULIFIKIA SOKO MTANDAONI

Kila mtu atakwambia post insta, facebook, tumia funnels, weka status za kutosha Whatsapp. Mwingine atakwambia kusanya namba za simu uwapigie, tuma emails kila siku nk. Sasa utafanyaje kuongeza mbinu za kulifikia soko? Utakapomaliza makala hii ya leo utafahamu kiundani kuhusu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni. Utafanyaje, twende sambamba mpaka mwisho.

Zama hizi za Internet na huduma za mitandao ya kijamii zimekuja na mgawanyiko wa watu. Kila mtu anatumia mtandao wa kijamii anaoona unampendeza. Sio ajabu uone kuna mtu hana account ya facebook lakini kutwa yupo instagram/twitter. Hata hivyo ukiwa mjasiriamali lazima ufike kote.

UNALIFIAJE SASA HILO SOKO LA MTANDAONI?

1. Kwa kutumia Mitandao kama Whatsapp, Instagram, Twitter na Facebook, sasa unaweza kueneza maudhui yako kote kote kwa mtindo wa Copy & Paste. Ndio sio dhambi kufanya C&P ikiwa maudhui ni yako. Hata hii makala usishangae kuikuta kwa page zatu za LinkedIn na Instagram. Hapa ni muhimu sana Ukaifahamu Nguvu ya Mitandao ya Kijamii katika biashara yako.

Unachotakiwa kufahamu ni kwamba mitandao hii imetofautiana, hivyo maudhui unayopost twitter inabidi UYAHARIRI ili yaendane na aina ya watu katika mitandao mingine kama Website yako, Facebook, Instagram na LinkedIn. So kazi ya kueneza maudhui haiwi ngumu kuvile hapa, sivyo?

2. Pia unaweza kuanzisha kampeni fulani na kisha unaieneza kwa njia ya barua pepe. Kufanikiwa kwenye hili kwanza unapaswa ukusanye anwani za barua pepe nyingi (walau elfu moja) na kisha uifanye kampeni yako kwa uweledi wa hali ya juu ndani muda fulani. Hii ndio Email Marketing.

E-Mail Marketing in Business
mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

NB: Kampeni yako haipaswi kuwa na ujumbe wa kupandikiza chuki au viashiria vya ubaguzi wa namna yoyote kwa sababu kampeni za namna hio huleta hisia mseto kwa watu na kukujengea taswira mbaya. Barua pepe zako unaweza kuzikusanya kwa njia ya Newsletter au kawaida (ile ya kuomba).

3. Tumia Social Media Analytics Tools: Kama unasambaza maudhui yako kupitia mitandao ya kijamii, siku hizi kuna namna ambayo unaweza kupima mwenendo wa machapisho yako kirahisi tu. Katika twita kuna Twitter Analytics na Insta kuna Insights.

social media analytics tools
mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

Hizo tools zitakwambia maudhui yako yamewafikia watu wangapi (impression), wangapi wameshiriki mjadala (engagement), wangapi wameclick links na umepata wafuasi wangapi baada ya kuchapisha maudhui. Ukishajua hayo itakusaidia sana kuboresha zaidi Machapisho yako yajayo.

Mitandao ya kijamii hasa Mtandao wa GOOGLE ina nguvu ya ajabu sana katika kuwafikia watu wengi ndani ya muda mfupi tu. Ni muhimu basi ukajua namna ya kucheza na mitandao hii ambayo kila mtu duniani anatamani awe mtumiaji wa kila siku. Kufahamu zaidi kuhusu nguvu hio gusa hapa;

4. Tumia Web Analytics Tools; Kama tayari unayo website ya biashara au page ya blogu yako, basi ni muhimu sana ukaweza kufuatilia na kujua ufanisi wake kwa watu wanaoitembelea. Unajua watu wangapi wanatembea website yako kila siku? Makala zipi ulizoandika zinafuatiliwa zaidi?

Watu wanaotembelea website yako wanatokea wapi? Katika Injini za Kimtandao, website yako iko katika nafasi gani? Majibu ya maswali yote haya unaweza kuyapata kwa kutumia tools kama Google Search Console, ahrefs, winch, clutch n.k Hivi ndo virutubisho vya website yako mtandaoni.

5. Tumia Content Management System (CMS); Ukiwa muandishi ambaye ungependa maudhui yako yazidi kufanya vizuri mtandaoni basi unapaswa kutumia mbinu mbadala zitakazokusaidia tena na tena. Sikuhizi mambo yamerahisishwa, WordPress ndio CMS maarufu zaidi lakini ukiacha hio kuna Joomla, Drupal, Magento, Shopify na Prestashop (kwa ajili ya e-commerce). Ukiwa na hizo tools inakuwa rahisi kwako kuandika maudhui ambayo yatakuwa rahisi zaidi kunaswa na Injini za Mtandaoni kama Google, Ask na Bing. Umeshawahi kutumia CMS gani? Tuambie hapa leo..

Content Management System
mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

6. Tumia SEO Hapa sitasema mengi kwa sababu tumeshaongea mengi huko nyuma. Kifupi hii SEO (Search Engine Optimization) ni teknolojia iliyopo kwenye software za mtandaoni zenye uwezo wa kukusanya taarifa kutoka vyanzo mbalimbali kama websites, blogs, mitandao ya kijamii n.k

Cha kuzingatia zaidi unapofanya SEO ni matumizi ya Keywords sahihi kwa ajili ya soko lako ulilochagua kuhudumia (niche), Picha unazotumia lazima ziwe na maelezo tambuzi (alt text), matumizi ya links pamoja na ujuzi wa kuuza kwa kupitia maandishi(copywriting skills) Zingatia sana haya kwasababu hii ndio mbinu bora sana katika kufahamu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

Yaani SEO ni SUMAKU inayovuta taarifa kutoka sehemu mbalimbali za watu (open source information) na kuzigawa kwa mtu yeyote ambaye atatafuta taarifa hizo. Umeshaielewa jinsi SEO inavyofanya kazi sasa? Kufahamu zaidi fuatana na makala hii hapa;

7. Fanya Mara kwa Mara; Umeshayaona haya tuliyoyaelezea leo? Sasa kama unataka kufanikiwa katika kuipeleka mbali biashara yako huku mtandaoni, basi SIO LAZIMA uyafanye yote, aghalabu, unaweza kufanya matatu au manne ili ujiweke kwenye nafasi nzuri katika kuimarisha ushawishi wako huku Mtandaoni. Lakini katika kuzifanyia kazi mbinu hizi basi ni muhimu mbinu hizi uzifanye MARA KWA MARA, yaani uwe na consistency. Usifanye mara mbili kisha ukakata tamaa. Andika machapisho 500, tuma emails 2000, rudia na rudia. Njiani utagundua ile njia sahihi zaidi.

Umegundua nini kwenye makala hii ya leo? Umeshafahamu kiundani kuhusu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni? Una la kuongezea, swali au changamoto?

Tafadhali weka maoni yako hapa au kama unahitaji kuwasikiana nasi kupitia emails au Whatsapp, tafadhali fanya hivyo; Whatsapp/Call: +255765834754 Email: info@rednet.co.tz

teknolojia ya S.E.O ina msaada gani katika biashara za mtandaoni?

TEKNOLOJIA YA SEO INA MSAADA GANI KATIKA BIASHARA ZA MTANDAONI?

Je, biashara yako ina uwezo wa kujiendesha hata kama haupo ofisini au pale unapofunga mlango wa ofisi? Kama jibu ni HAPANA, basi wakati wa kuhamisha biashara yako mtandaoni ni SASA kwa sababu Teknolojia haikusubiri wewe ndugu. Leo unapojiuliza teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni? majibu yote muhimu utayapata hapa. Cha kufanya, Fuatana nasi mpaka mwisho wa makala hii.

Imagine wateja wako wanaweza kufanya shopping wakiwa huko huko makwao, wengine wanasoma makala zinazotatua changamoto mbalimbali zinazowakabili na wengine wamepata mawasiliano yako mtandaoni. Yote hayo yanafanyika wewe ukiwa safarini, nyumbani, shambani au ukiwa na mishe zingine nje kabisa ya mtandao.

Faida ni nyingi sana ukiwa unafanya Online Business: Yani ukishakuwa na website inayofanya kazi sawia, ukawa na accounts za mitandao ya kijamii zinazoitambulisha biashara yako kila siku, hapo unafika kwenye hatua ambayo Internet inakufanyia kazi, na sio wewe kuwa Mtumwa wake.

NINI KINAKWAMISHA WATU WENGI SASA?

Watu wengi hudhani kuwa biashara za mtandaoni ni rahisi tu. Kwamba TCRA wameripoti kuwa kuna watumiaji wa internet milioni 29 kufikia October2021, so ukipost biashara yako itawafikia watu milioni29 chap. NO! Maisha si rahisi kiasi hiko asee!

Hii ni kwasababu miundombinu ya kimtandao (websites, blogu na mitandao ya kijamii) imetengenezwa katika namna ambayo inaheshimu Algorithms (mtiririko rasmi) fulani wa maneno, taaluma, mijadala, picha na mahusiano ili kuongeza ufanisi. Ndio maana tunasema kila siku Fuata Ushauri wa kitaalam.

Algorithms hizo huchochewa na mfumo wa kurahisisha utafutaji wa taarifa mtandaoni ujulikanao kama S.E.O (Search Engine Optimization). Mfumo huu huchukua links na maneno(keywords) yanayotumika zaidi katika blogu, websites na social networks na kuyaweka kwenye injini za matafuto kama Google na Bing.

Hivyo, kama unajua ama hujui, chochote unachokiandika sana katika social networks, blogs na websites huchukuliwa na kuwekwa katika Google na Bing. Lakini sio kila kitu unachokitafuta google utakipata kikiwa katika nafasi za juu pale google, Hapana, mambo hayaendi hivyo.

Kuna taarifa ukiitafuta utaipata kutoka kwenye biashara fulani ikiwa juu kabisa ukurasa wa mbele pale google. Taarifa hiohio pia unaweza kuipata kwenye blogu/website ambayo ipo ukurasa ya pili, wa tatu au wa 10.

Ubaya ni kwamba mteja hatatafuta jina la blogu/website yako, bali ataandika changamoto anayotaka kukabiliana nayo au kuhusu taarifa anayotaka kuitafuta mtandaoni. Mfano huandika kupitia google kutafuta “kirefu cha TEHAMA” “Biashara ipi ina faida zaidi Tanzania?” “Siri ya kuwa tajiri Afrika” “Mbinu za kufanikiwa kimaisha/kibiashara” “laptop za bei nafuu Tanzania“, “viatu vikali“, “Faida za TEHAMA“, “Faida za Website“nyimbo za bongo fleva 2022”, “Laptop za bei nafuu zinapatikana wapi?” “Faida za kilimo cha mananasi/tikitimaji” “Chakula kitamu zaidi Tanzania” nakadhalika.

Sasa, kupitia maneno hayo ya S.E.O umegundua nini?

Ngoja nikwambie kitu, Kama unafanya biashara mtandaoni, zingatia maneno ambayo yanatumiwa zaidi na watu wengi au yanayotafutwa zaidi na wateja katika Industry yako. Jiulize, kama wewe ndo ungekuwa mteja unatafuta kujua kuhusu bidhaa/huduma flani, ungeandika nini pale Google?

Sasa hayo maneno ambayo ungeyaandika google ndio chambo ambayo unapoyatumia mara kwa mara katika blogu/website/social media yako, basi unajiweka kwenye nafasi ya kupatikana kirahisi zaidi pale mteja akitaka kutafuta kuhusu huduma/bidhaa zako. Zingatia sana hilo.

Na hio ndio SIRI ambayo wengi wanaojiita “Wataalam wa SEO” hawatakwambia kuhusu teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni. Kuna watu hawaoni sababu ya kuwa na Website/Blog kwasababu vitu hivyo HAVIWAINGIZII pesa direct.

Kuna mmoja nilifanya naye nae kazi akaniambia kilichomkuta mwaka 2018, “Bwana mi nilishawahi kuwa na website ila mwaka ule mzima yani haikunipa hata mia, na niliilipia mnaita ‘Hosting Fee’ sijui. Sikuwahi kuona umuhimu wake, so nikaachana nayo”.

faida za teknolojia ya S.E.O katika biashara

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

Najua hili hata wewe unalihofia Kwanza fahamu haya yafuatayo:

Kuwa na website hakukufanyi kupata wateja wengi kama hutafanya yafuatayo ili ufahamu teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni:

1. Hujatengeneza account ya Google Map: Zamani Google walikuwa wakitumia Application ya Google My Business ili kuwarahisishia wafanyabiashara waweze kuunda profiles zao na ziweze kupatikana kirahisi mtandaoni. Lakini baadaye waliona App ya Google Map inao uwezo wa kubeba taarifa zote muhimu, hivyo App ya Google My Business ikafikia mwisho wake hapo. Stori nzima ipo hapa. Google Map sasa huifanya biashara yako iweze kusajiliwa, kutambulika na kupatikana rasmi na kirahisi katika mtandao wa Google. Yani apa unatengeneza Profile ya biashara yako direct na kumruhusu mteja aweze kuona mpaka mahali biashara yako ilipo.

google Map

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

2. Hujaunganisha blog/website yako na huduma za Search Console: Hii Search Console kazi yake kubwa ni ku-crawl, yani kukusanya taarifa zote za website yako kama huduma/bidhaa unazohusika nazo, links za Menu (Home, contacts etc) Mada unazoziweka, mijadala na maneno unayotumia humo Kutengeneza links ziitwazo SITEMAPS na kuziweka kwnye injini za matafuto ya mtandaoni ili mteja akitafuta anachokitafuta basi google/bing iweze kuileta website yako ukurasa wa mbele kabisa. So ukifanyia kazi vema hiki kipande, Google itai-rank website yako katika nafasi za juu.

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

Google Search Console

3. Huweki maudhui kwenye website/blog yako: Yule jamaa yangu nilikwambia pale juu kuwa hakuona umuhimu wa kuwa na website, changamoto kubwa alikuwa nayo ni kushindwa kuwa na website inayoruhusu kuweka maudhui frequently. Unakuta website ina tabs za Home, Services, About na Contacts peke yake tu, wala haina sehemu ya blog/news au sehemu ya kufanya shopping. Kwa biashara za kisasa hii ni changamoto kubwa sana kama bado hujafahamu teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni.

Fahamu tu kwamba website ambayo haina uwezo wa kuweka maudhui mara kwa mara kupitia Kipengele cha Blog/News ni NGUMU sana kutokea kwenye ukurasa wa kwanza wa google. Hii ni kwasababu Maudhui unayoweka kwenye kipengele cha Blog/News huifanya website yako kuwa ya Kipekee na inayojiboresha kila siku.

Na hivyo ni rahisi google kui-rank website yako katika nafasi za juu pale mtu akitafuta taarifa ambazo pia zinapatikana kwenye website yako. Hii ndo silaha ambayo itaiwezesha biashara yako kuweza kujitangaza yenyewe na kukusanya wateja wengi huku wewe ukiendelea na mishe zingine.

4. Hausambazi Mukhtasari wa taarifa (updates) zinazopatikana kwenye website yako: Ndio, SEO inafanya kazi automatic unapounganisha website yako na huduma ulizozisoma hapo awali, Lakini, ni muhimu pia kusambaza Updates kuhusu taarifa unazoweka kwnye website yako katika social accounts zako za instagram, facebook, twitter nakadhalika.

Hapa unatengeneza kitu kinaitwa BACKLINKS. Tayari nimeshakuwekea elimu ya kutosha kuhusu umuhimu wa Backlinks katika kuhakikisha website yako inafanya vizuri pale Google.. Fahamu tu kuwa ili Website yako iweze kuwa imara mtandaoni lazima links zake zipatikane kwenye media zingine kama Linkedin, Facebook, Twitter, ZoomTanzania, Clutch n.k.

Huko ndo Jikoni kwenye haswa, Kwa sababu, ukiachana na Google, kwenye mitandao hio ndipo watu wengi hushinda wakijadiliana kuhusu mambo mbalimbali ya kijamii, kisiasa, michezo na burudani. So ukiwapelekea solution kuhusu changamoto zao kisha ukawapa link, guess what will happen?

Kujua zaidi namna ya kuongeza traffic kwenye website yako tafadhali tembelea makala hii hapa chini:

KWANINI TUNA-SHARE SIRI HIZI KUHUSU TEKNOLOJIA YA SEO INA MSAADA GANI KATIKA BIASHARA ZA MTANDAONI?

Siku zote maendeleo mazuri ya mgonjwa ndo mafanikio ya daktari. Hivyo wewe mjasiriamali ukifanikiwa ktk website yako, huo ni ushindi pia kwetu developers na wataalam wa SEO. I hope elimu hii inakwenda kutibu changamoto zako katika biashara za mtandaoni?

Kwa makala nyingine nyingi zaidi, endelea kuperuzi ukurasa wetu wa https://rednet.co.tz/blog kila mara ambapo utagundua makala muhimu za kuimarisha uchumi wako binafsi na wa biashara/kampuni yako.

Mjasiriamali anapofanikiwa katika website yake, huo pia ni ushindi kwa web designer na wataalam wa S.E.O.

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

Msaada binafsi tafadhali wasiliana nasi kupitia:

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni
MPESA LIPA NAMBA YETU

MFUMO WA KUWEZESHA MALIPO BARANI AFRIKA (PAPSS)

Umeshawahi kuwaza kufanya biashara na wafanyabiashara wenzako na wateja kutoka nchi yoyote barani Afrika ambapo utaweza kutuma na kupokea fedha bila ya ulazima wa kubadili ziwe za kigeni kwanza? Sasa mfumo wa Kuwezesha malipo barani Afrika(PAPPS) unakwenda kukurahisishia mjasiriamali uwezo wa kutuma na kupokea fedha katika bidhaa/huduma unazotoa kila siku kirahisi zaidi. Leo nakupa fursa ya kufahamu namna mambo yamekuwa mazuri kibiashara barani Afrika. Fuatana nami mpaka mwisho wa makala hii..

Kwetu Moshi bwana ikifika mwezi February mpaka June kila mwaka huwa ni msimu wa parachichi na ndizi ambapo watu huuza sana parachichi ndani na nje ya nchi. Najua umeshawahi kuonja parachichi za Rombo, Marangu, Mwika, Machame nk, right?

Sasa bwana hizo parachichi unazokula ni 20% tu ya parachichi zote zinazovunwa kwenye miteremko ya mlima Kilimanjaro. Zaidi ya 80% ya parachichi hizo huuzwa nchini Kenya na kisha kusafirishwa kwenye barani Ulaya na Asia kupitia bandari ya Mombasa.

Bahati mbaya zaidi pale mpakani Holili kuna madalali wengi sana ambao hununua parachichi kutoka kwa wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali na kuziingiza nchini Kenya. Hawa jamaa bwana wajanja sana. Wao tayari wana vibali vya kuingia na kufanya biashara kati ya Tanzania na Kenya na zaidi wanafanya pia biashara ya kubadilisha fedha hapo mpakani (japo sina uhakika kama wanafanya hivyo kihalali). Kwa kufanya hivyo hawa Madalali wamekuwa wakijipatia faida kubwa sana hapo mpakani japo kuwa wao hawana mashamba wala parachichi zenyewe. Wao wanaconnect dots tu.

Na bahati mbaya zaidi wafanyabiashara wengi wadogo hawawezi kuvuka mpaka wakakutana na wateja wenyewe huko Kenya na kuuza bidhaa zao direct. So unaweza kuona namna hawa ndugu zangu wanapata tabu kufanikiwa kwenye biashara yao japokuwa wao ndo wanamzigo wote wa parachichi.

Huu ni mfano mdogo tu unaowakuta wafanyabiashara ambao wanauza bidhaa/huduma zao nje ya nchi. Hali hio pia inawakumba wale wa Tunduma, Rusumo, Taveta na maeneo mengine ya mpakani ambapo madalali (watu wa kati) wamekuwa wakitumia fursa hio kujinufaisha zaidi kuliko wakulima.

Kupitia changamoto kama hizo ndio maana nchi wanachama wa AU wakaanzisha Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) ili kuhakikisha biashara baina ya nchi wanachama zinafanyika kirahisi, tena bila vikwazo kama kodi na ushuru wa mipakani ambayo imekuwa ikiwaumiza wafanyabiashara.

Kuhusu AfCFTA ni nini na inafanya kazi vipi? tayari nimekuandalia makala murua kabisa kupitia link hii hapa chini:

Ukimalizana na makala hio sasa, tuendelee..

Pia nchi za kusini mwa Afrika kufikia July 2020 zikakubaliana kurasinisha biashara zao ili kuwezesha mazingira ya biashara baina ya nchi wanachama wa SADC kufanya biashara bila mrundikano wa kodi na ushuru. Hapa Prof. Kabudi (waziri wa mambo ya nje) na timu yake walicheza sana.

Kuhusu URASINISHAJI huo wa Kibiashara, ni nini na unafanyika vipi, tayari kuna makala yako kupitia link hii hapa:

Kuna mengi sana ya kujifunza hapo kwenye hio makala hapo.

Lakini licha ya yote hayo, mtaani mambo bado ni magumu kwa wakulima na wafanyabiashara wadogo, kwanini? Kwa sababu taarifa za miamala bado zimetekwa na madalali. Wao ndo wanazuia bidhaa zote pale mpaka na kuzivusha na kufanya biashara nje ya nchi.

Hali hio bado inawatengenezea faida kubwa sana madalali hao na kuwaacha kwenye mataa wakulima na wafanyabiashara wadogo ambao kimsingi ndo wenye mali halisi.

SASA NINI KIFANYIKE ILI KUWEZESHA MALIPO KWA URAHISI?

Wakiwa wanajiuliza serikali, jumuiya za kimataifa na mashirika ya ndani na nje ya nchi, Shirika la African Export-Import Bank (Afreximbank) wakaja na suluhu ambayo inakwenda kumtingisha bwana Dalali na kumtengenezea mazingira mazuri ya kufaidika ndugu Mkulima na mfanyabiashara mdogo. Suluhu hio ni Mfumo wa Kuwezesha Malipo barani Afrika waliouita PAPPS.

Mfumo huu wa PAPSS (Pan-African Payment and Settlement System) ulizinduliwa rasmi tarehe 13 January 2022 katika hafla iliyofanyika nchini Ghana. Kabla ya hapo, mfumo huo ulikua kwenye majaribio tangu mwaka jana 2021 huku ukiwa unatumika ndani ya nchi 6 za Afrika Magharibi. Mtandao wa ICLG unatujuza kwamba mfumo huu unakwenda kuokoa dola bilioni 5 kwa mwaka ambazo hupotea kama makato mbalimbali katika malipo ya kibiashara baina ya wafanyabiashara wa nchi moja na nyingine.

Pia imefahamika kwamba zaidi ya 80% ya miamala inayofanyika maeneo ya mipakani ambayo ilihitaji mifumo ya kimataifa ya kulipa na kubadili fedha, sasa inakwenda kuokolewa na mfumo huu. Imagine wakulima na wafanyabiashara tunavokwenda kunufaika hapa.

UNAJIUNGA VIPI NA MFUMO HUO WA KUWEZESHA MALIPO?

Mfanyabiashara, mteja, mshiriki na mamlaka za serikali ambaye anahitaji kunufaika na mfumo huu kwa sasa anahitajika kujisajili kupitia link hii http://papps.com/connect/ kisha fuata maelekezo.

Changamoto iliyopo ni kwamba mfumo huu bado haujasambaa vya kutosha kiasi cha kuzama katika matumizi ya kila siku ya kibiashara. Hali hio inawalazimu waandaaji kupambana katika kushirikiana na Taasisi za Fedha na Serikali za Mataifa ya Afrika ili kujenga msingi imara wa matumizi.

Mbeleni wafanyabiashara tutaweza kutuma na kupokea fedha ndani ya Jumuiya zetu za kikanda na bara zima kupitia Miundombinu hii ambayo inazidi kuboreshwa katika kutafuta fursa za biashara na maendeleo ya kiuchumi.

Kwa fursa za biashara zinavyofunguka kupitia #AfCFTA pamoja #Urasinishaji unaofanyika katika Jumuiya za Maendeleo (SADC, EAC, COMESA etc) ni wazi mfumo huu wa PAPPS unakwenda kuwezesha malipo yaweze kufanyika kwa haraka na ufanisi wa hali ya juu sana. Hapa hutakiwi kubaki nyuma kabisa ndugu yangu.

NITAIFAIDI VIPI SASA HIO PAPSS NIKIWA MJINI?

Kwanza fahamu mfumo huu ni wa Kimtandao, hivyo, ukiwa popote unaweza kufanya biashara na mteja hasa kupitia ecommerce website yako au Digital Tools zingine kama Instagram, Twita na Whatsapp.

Kufahamu zaidi gusa tweet yetu hii hapa chini

Uzuri wa kuwa na e-commerce website unakuja hapa. Mteja akiwa nchi X anaiona bidhaa kwenye website yako, alipia, kisha wewe mjasiriamali unafanya delivery kupitia Gari, Ndege au Meli na bidhaa inamfikia vema.

Kuna OFA hapa kwa ajili yako. Wasiliana nasi mara moja kuipata:

Umeshawahi kufanya biashara na wateja/wadau walio nje ya nchi yako lakini ndani ya Afrika? Ulipata changamoto gani? Na umejifunza nini? Tushirikishe uzoefu wako kwenye comments Kwa sababu kuna mdau angependa kufahamu kinachoendelea huko nje ya nchi kibiashara, right?

Mfumo huu wa PAPSS unakuja kuleta ushindani katika Kampuni na Mashirika yanayofanya biashara ya fedha kiteknolojia (Fintech) barani Afrika.

Ukiwa kama Mjasiriamali na mdau wa Tech, umejipangaje na ujio wa mfumo huu? Weka majibu na mawazo yako kwenye comments hapo chini.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

MPESA LIPA NAMBA YETU
mbinu ya ufungani (commitment) katika biashara

JITAFUTE KWANZA ILI UFANIKIWE

Mwaka 2017 wakati tunaanzisha Rednet Technologies tulikua na vision kubwa sana, kama ile watoto wadogo wanavyoota kuwa Marubani na Wanasheria. Hata hivyo kuifanyia kazi vision hio haijawahi kuwa rahisi. Jasho, Damu na Machozi haviepukiki. Mwaka 2020 nikagundua kwamba unatakiwa u jitafute kwanza ili ufanikiwe.

Vision ya Rednet Technologies ilikuwa ni “Kuhakikisha Tunawafikia Wafanyabiashara wote wadogo na wale wa kati wanaofanya shughuli zao katika eneo la Afrika Mashariki na Kati, na kuimarisha Biashara zao kwa matumizi ya Teknolijia za kisasa kutoka kwetu”.

Hio Vision inahitaji Maarifa, Ujuzi, Muendelezo (Consistency), Ubunifu na zaidi, Teamwork. Kama wewe ni mfanyabiashara na una ndoto za kufanikiwa katika shughuli zako basi hili la Teamwork unapaswa kulitazama kwa macho matatu. Leo tutachambua kwa undani hapa kwenye TEAMWORK.

Ile Team yetu ya kwanza tulitamani ingeweza kufanikiwa kuifikisha Rednet pale inatakiwa kufika. Lakini haikuweza kufanya hivyo. Hivyo, mwezi March, 2018 kwa huzuni kubwa Rednet Technologies ilisitisha Operations zake kwa kipindi cha Mwaka mzima mpaka May 2019. Kilikua ni kipindi kigumu mno kwangu binafsi kwa sababu mimi ndiye nilikua Visionary Leader.

Nilitamani sana Rednet Ifanikiwe, roho yangu ilikua ikiniuma sana kuona juhudi zangu hazikuwa zikizaa matunda. Kila mbinu niliyokua naitumia haikunipa majibu ya kufurahisha. Nilikata tamaa kabisa. Hata hivyo hio 2019 tulipata kazi chache za kuwahudumia wateja wetu, lakini bado hatukuweza kutanua vizuri mtandao wa wateja wetu na kushirikiana nao kwenye shughuli zao vile inavyotakiwa.

Hali hii ilikwenda mpaka Octoba, 2020, kabla ya ule Uchaguzi Mkuu ndipo ambapo ndugu yangu wa zamani sana, JEOFFREY alinipa idea ya kimapinduzi sana.

JEOFFREY NI NANI?

Huyu Jeoffrey ni rafiki yangu wa zamani sana. Tulisoma wote shule ya msingi japo yeye alinizidi darasa moja. Na zaidi tuliishi wote mtaa mmoja kwa kipindi kirefu sana katika maisha yetu, zaidi ya miaka 18. Kipindi chote icho sikuwahi kujua kuwa mfumo wake wa biashara utanifaa.

Huyu jamaa ana biashara yake ya kusambaza vifaa vya miundombinu ya maji kama koki, elbows, mabomba n.k. Zaidi yeye amejisajili kwenye mfumo wa manunuzi ya serikali (TaNEPS). Huko anapata tenda nyingi sana kuhusu miradi ya maji ya serikali nchi nzima. Kifupi anafanya vizuri sana sokoni.

Hio siku sasa alinijia akihitaji nimtengenezee ecommerce website ili kusudi aweze kuuza bidhaa zake kwa rejareja kwa wateja wake walio nje ya mfumo wa manunuzi. Hivyo akanipatia nyaraka za wasifu wa kampuni (Company Profile) yake. Sasa wakati naifanya hio kazi yake nikawa najiuliza, hivi mimi nashindwaje kutanuka kama jamaa yangu hapa. Hapa kuna kitu muhimu sana, jitafute kwanza ili ufanikiwe.

Najua hata wewe unayesoma unajiuliza hili swali “NAWEZAJE KUTANUA BIASHARA YANGU?” Well, kupitia vikao vichache nilivyokaa na huyu jamaa yangu, nikaweza kugundua namna ambayo tunaweza kusambaza Bidhaa na Huduma zetu kwa watu wengi na kwa haraka zaidi.

Hivyo, tukaanzisha Huduma ya Kusambaza Vifaa vya Ofisini na Computer kama mafile, diaries , flash disks, antivirus na vitu vya stationery unavyovijua. Wateja wetu wakubwa tuloanza nao walikua ni makampuni na taasisi ambazo kimsingi wametupa ushirikiano mkubwa sana.

Tumekuwa tukipokea Oda kutoka sehemu mbalimbali na tumeweza kukuza mtandao wa wateja wetu haraka na kwa ufanisi mkubwa kupitia huduma hii. Jambo hili likatulazimu kwenda mbele zaidi ambapo sasa kupitia tovuti yetu ya https://rednet.co.tz unaweza ku-request oda na tukakufikia.

Urafiki wetu na Jeoffrey ukazidi kuota mizizi ambapo sasa tunashirikiana kwenye mambo mengi sana ya kikazi. #VijanaWenzangu mimi huwa nawaambia “Tutumiane vizuri katika shughuli zetu za kiuchumi. Delegate your tasks kwa kuwa baraka zipo kwenye KUTOA zaidi kuliko kwenye KUPOKEA“.

Mimi rafiki zangu nawapa michongo mingi sana, ya muda mrefu na ile ya muda mfupi. Kadhalika rafiki zangu wananipa michongo mingi sana, ya muda mrefu na ile ya muda mfupi. Wataalam wanakwambia “Your Network is Your Net worth“. Kuna maana kubwa sana kwenye huo msemo ukitafakari.

Kama connections ulizonazo hazikutumii vizuri sasa usilalamike, watumie wewe kwenye mishe zako. Yes, maana hai-make sense kuwajua watu wazuri wanaoweza kuipush biashara yako halafu huwatumii eti kwa kuwa wao hawakutumii kwenye mishe zao. How? Make sure you get upper hand on it.

KARIBU KATIKA HUDUMA MPYA:

Website yetu sasa tumeiweka ili kusudi kukupa wewe uwezo wa kuchagua huduma unayotaka kisha sisi tutapata request yako, tutakutumia Quotation ukiridhia tunakupatia huduma yako katika muda ambao utapanga wewe. Upewe nini zaidi?

Kwa vifaa vya Ofisini (stationeries) kama wino wa printa, flash disks, rim paper, peni (box) n.k gusa link hii https://rednet.co.tz/services/your-order/… Link hio itakupeleka direct kwenye ukurasa utakaokupa nafasi ya kutuambia huduma unayohitaji ukiwa popote Duniani.

Pia tumekuletea huduma mahsusi kwa ajili yako iitwayo “JIHUDUMIE” kupitia link hii https://rednet.co.tz/services/jihudumie-leo/… ambapo humo ndani utajipatia huduma kama zinavyoonekana kwenye picha hapa.

CHANGAMOTO:

1. KUWA RASMI: Najua watu wengi humu mitandaoni biashara zenu si rasmi, kwa maana ya kwamba hazijasajiliwa katika Mamlaka za Kiserikali (BRELA, TRA, HALMASHAURI, BENKI etc). Sasa mtindo huu wa Usambazaji unakutaka kusajili biashara yako kwa kuwa biashara/kampuni yako sasa inakwenda kufanya kazi na biashara/kampuni zingine (B2B). Matumizi ya Quotations, Proforma Invoice, Tax Invoices, EFD receipts na Delivery Notes kwenye mtindo huu wa Biashara ni kama Katiba katika utawala wa Nchi. Eneo hili kama Mjasiriamali unapaswa kuwalo makini sana yani.

Hivyo ifanye biashara/kampuni yako kuwa rasmi kwanza ili kujihakikishia unafanya shughuli zako bila kubughudhiwa na mtu yeyote.

2. UCHELEWESHWAJI WA MALIPO: Kuwa msambazaji/Supplier maana yake ni kwamba unafanya kazi kwa pesa yako na pesa hio utaingiziwa baada ya mwezi mmoja mpaka miezi sita. Hivyo, kukaa muda mrefu bila kuingiziwa pesa si kazi ndogo, uvumilivu lazima uchukue nafasi yake hapa.

3. MTAJI: Kama ulivyoona hizo changamoto zingine hapo juu, kufanya usambazaji lazima uwe na Mtaji wa kutosha kuweza kuhudumia Wateja wako kikamilifu kabla wao hawajakuingizia pesa siku za mbeleni. Hapa lazima uwe na pesa ya kufanya kazi mkononi ili usije ukatolewa katika game.

Hata hivyo, changamoto hizi hazitakiwi kukurudisha nyuma, katika harakati jitafute kwanza ili ufanikiwe lazima uhakikishe unapambana kwa njia zozote ili kusudi mafanikio yako yakapate kujidhihirisha. #VijanaWenzangu muda wa kupambania future zenu ndio sasa. Pambaneni haswa.