Tag: uchumi

thamani vs gharama, nafuu iko wapi? fahamu siri za kuweza kushawishi wateja katika biashara yako.

THAMANI vs GHARAMA, NAFUU IKO WAPI?

Ubora wa kazi una thamani kubwa sana kuliko gharama za kuifanya kazi hio. Unaweza lipia mradi kwa milioni 5, lakini usikupe matokeo yale ulijipangia mwanzoni. Pia unaweza lipa laki 5 ya mradi na ukapata matokeo mazuri zaidi. Ufanyeje? Je kati ya thamani vs gharama nafuu iko wapi? Fuatilia makala hii mpaka mwisho kufahamu zaidi.

Warren Buffet ambaye ni mbuji kabisa katika buruji la uwekezaji duniani amewahi kunukuliwa akisema “Price is what you pay, value is what you get.” akimaanisha, “Gharama ndio unayolipa, thamani ndio unayopata”. Kifupi ni kwamba thamani ndio msingi wa bidhaa/huduma huku gharama ikiwa ni makubaliano ambayo yanatangulizwa na muuzaji.

Kujua tofauti kati ya Gharama na Thamani ni moja kati ya mbinu bora zaidi za kufanya Uwekezaji. Zaidi kuhusu uwekezaji tayari tumeshakufahamisha SIRI ZA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA Ukishazifahamu hapo tuendelee..

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

umuhimu wa tehama

jinsi ya kufanikiwa katika biashara za mtandaoni

Unaposhindwa kutofautisha kati ya Gharama na Thamani kama mfanyabishara unajiweka kwenye mtego wa kukosa wateja, kutoaminika kwa Wawekezaji wakubwa, Kupoteza points dhidi ya washindani wako kibiashara na mwisho kuiweka biashara yako katika majanga ya kudhoofika na hatimaye kufa.

Unawezaje kupata bidhaa zinazouzwa kwa gharama za chini kuliko thamani yake halisi?

Jibu ni kufanya tathmini kwa kutumia viwango vya bei ambazo ni tofauti kabisa na gharama zinazotangazwa sasa. Hapa unaweza kuangalia bei, miaka 3 iliyopita ilikuaje na miaka 3 ijayo itakuwaje.

Bwana Phil Town, ameweka zoezi la kufanya Tathmini makini kwa kupitia hatua nne alizoziita “Four M’s“. Tuzione chap chap:

1. MEANING: Hatua ya kwanza kabla hujawekeza katika bidhaa/huduma fulani lazima ujiridhishe kuwa bidhaa/huduma hio ina maana sana kwako. Ikiwa na maana utapata fursa ya kuichunguza na kuielewa vyema, na kujituma ipasavyo katika kufanya biashara hio.

2. MOAT: (Upekee ambao hauwezi kuigwa na wengine): Unapochagua bishara ya kuwekeza ama bidhaa/huduma, unatakiwa uifanye iwe katika mtindo ambao washindani wako hawawezi kukuiga. Mfano: Duniani kuna makampuni mengi tu ya vinywaji laini (soft drinks) lakini Coca cola ni moja na itaendelea kubaki hivyo.

Hivyo hebu tuambie hapa biashara yako ina utofauti gani ambao washindani wako hawawezi kuiga kamwe?

3. MANAGEMENT: Je wajua kuwa Chanzo kikubwa kwa biashara kufa ni watu wanaoiendesha? Hivyo unapofikiria kuwekeza kwenye biashara lazima eneo ya utawala na uendeshaji wa shughuli linasimamiwa na watu wenye Weledi, Waaminifu na wanaojali maisha ya biashara hio.

4. MARGIN OF SAFETY: Kama umeshajiridhisha na hizo hatua 3 zilizopita, sasa hebu tizama pia namna unaweza kuweka mtaji ama kununua hisa bila kupoteza pesa na uhakika wa pesa yako kurudi.

Kila biashara inahitaji kitu fulani ambacho kitaitofautisha na washindani wake wengine sokoni. Sasa mchakato wa kutafuta tofauti hizo inaitwa “Positioning”. Hii mbinu inaziwezesha biashara kukazia sehemu fulani ya soko/wateja ili kujiimarisha zaidi kwenye sehemu hio. Unafanyaje?

MBINU ZA KUFANYA POSITIONING:

1. KUPUNGUZA GHARAMA: Ukifanya uchunguzi vizuri sokoni hasa kwenye mitaa ambayo wanafanya biashara ya aina moja mf: Kariakoo kila mtaa una shughuli yake maarufu zaidi kama mtaa wa livingstone ni maarufu kwa vyombo vya ndani.

So ukijigundua kuwa upo kwenye aina hii ya biashara, mbinu bora hapo ni kupunguza gharama za bidhaa zako kwa kiwango kidogo kuliko washindani wako. Lengo ni kuhakikisha unakuwa na mzunguko wa haraka wa mauzo ya bidhaa/huduma zako kwa faida ndogo ili mzigo wako uishe mapema.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

2. UBORA: Kama unataka kujitofautisha na washindani wako, basi mbinu bora na ya kuaminika ni kuhakikisha bidhaa/huduma zako ni za Ubora wa hali ya juu. Unapozingatia Ubora unajiweka kwenye nafasi ya kupata wateja wa kuaminika, wateja wa kudumu na wateja wa uhakika katika biashara.

3. MAKUNDI YA KIJAMII (DEMORGRAPHIC): Baadhi ya biashara huamua kujihusisha na makundi fulani tu ya kijamii ili kujiletea faida zaidi. Mfano: kwenye TV na redio vinatengenezwa vipindi mahsusi kwa Vijana, watu wa makamu na watu wa dini fulani kwa siku zao. Umeshawahi fanya hii?

Mbinu hii inafaa sana pale unapoyapata makundi hayo karibu na eneo lako la biashara au watu wanaokufuatilia zaidi mtandaoni wakawa ni wanamna hio. Vinginevyo unajiweka kwenye hatari ya kukosa soko kubwa nje ya hao uliolenga kuwahudumia.

4. HUDUMA BORA: Huwa inatokea kwa baadhi ya biashara ushindani unakuwa mkubwa sana kiasi kwamba mbinu 3 tulizoziona awali haziwezi kufanya kazi. Yani watu wanashikana kooni haswa. Hapa ndipo mbinu ya kutoa Huduma Bora kwa wateja inapokuja kuleta tofauti.

Zoezi la kutoa Huduma Bora ni pana na linahitaji ubunifu mwingi. Na hii inatoa fursa kwa biashara kubuni namna nzuri ya kuhudumia wateja wake ili kuhakikisha wateja wanafurahia bidhaa/huduma na kuzidisha mauzo. Mfano: unaweza kuanzisha dawati la wateja kutoa maoni live ili waweze kuona mawazo yao yakifanyiwa kazi. Unaweza kuanzisha kurasa za mitandao ya kijamii ili kukusanya kero za wateja na kuzifanyia kazi vizuri. Pia unaweza kutengeneza mzunguko kwa wateja wako kushiriki kama mabalozi wa kuitangaza biashara yako kwa watu wengine. Unaionaje hii?

UNAWEZA VIPI KUDADAVUA NA KUWASILISHA THAMANI YA BIASHARA YAKO KWA MTEJA WAKO?

Tafiti zinaonyesha kuwa watu hawapendi kabisa kutangaziwa ama kulazimishwa kununua kitu hasa huku mtandaoni. Mfano: Tizama unavyopata kero pale unapoangalia vidio YouTube mara katikat linakuja Tangazo Ama pale unataka kufungua ukurasa fulani mara unafunguka ukurasa wa tangazo kwanza kabla hujafika pale ulitaka kwenda. Hio kero ndio inatakiwa ikufanye uitazame biashara yako katika jicho la Kitaalamu kwa kutatua changamoto na si la Kibiashara kwa kuuza Bidhaa/huduma yako.

Unapotoa Elimu katika namna ya Utaalam wa kutatua changamoto fulani, unamfanya mteja atake kuondokana na kero zinazomsumbua kwa kutumia Bidhaa/Huduma zako. Hii ni tofauti kabisa pale unapotaka kuuza bidhaa. Ukifanya hivyo hutatui changamoto bali unakuwa kero kwa mteja.

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

gharama vs thamani, kipi kinafaa zaidi?

Thamani ya Biashara yako inaonekana katika kutatua changamoto za mteja wako na Urahisi wa kutumia bidhaa/huduma yako. Hivyo lazima uhakikishe kuwa unachokitangaza ni Ile Namna na hisia ya Bidhaa zako zinaweza kutatua changamoto fulani ya mteja kwa urahisi.

Pia lazima uhakikishe suluhu yako inakwenda sambamba na hisia za mteja wako. Kwa kuwa kitaalam watu hununua bidhaa/huduma kutokana na hisia walizo nazo muda huo. Mfano kuna watu watakwambia kuwa wakiwa na hasira ama furaha sana kwao huo ndo muda wanafanya shopping kubwa zaidi.

Mzazi anapotaka kununua keki ya birthday ya mwanae hanunui tu keki tamu, lazima pia ahakikishe keki hio inakwenda kum-suprise mtoto kwa muonekano wake wa kuvutia. Ni mbinu ya kihisia hapo inatumika. Hivyo unapotaka kuongeza Thamani ya biashara yako unatakiwa kuzingatia hilo pia.

Umejifunza nini kwenye makala hii kuhusu thamani vs gharama, nafuu iko wapi? Tafadhali weka maoni au mtazamo wako katika sehemu ya comments hapo chini..

Vyanzo: https://www.forbes.com/sites/forbesfinancecouncil/2018/01/04/the-important-differences-between-price-and-value/?sh=133fd5c94237

https://www.weebly.com/inspiration/difference-between-value-and-cost/

https://yourbusiness.azcentral.com/different-types-strategies-business-1348.html

Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako (Business Intelligence)?

JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI?

Imagine una ofisi yako (eneo la biashara) na pia unayo akaunti yako ya twita, Instagram au facebook. Lakini hujui namna ya kutengeneza mvuto kwa watu ili wakutafute, wakufollow, wakuamini na wafanye biashara na wewe. Unafanyaje? Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji tosha? Fuatilia makala hii mpaka mwisho kufahamu kiundani.

Imagine hujawahi kutengeneza mahusiano ya kibiashara na followers wako, hata mmoja yani, na kila siku upo mtandaoni kufuatilia habari mpya zinazojiri kwenye Bongo Fleva, Bongo Muvi, Mpira, Umbea, Siasa n.k. Kuna muda unatamani biashara yako iwe kubwa lakini hujui mbinu gani unaweza kutumia ili kuhakikisha biashara yako inazidi kuwa Imara kila siku. LEO hii Nazungumza na wewe hapa.

1. CHANGAMKA KIBIASHARA UWAPO MTANDAONI:

Kabla ya yote, fahamu kuwa biashara inafanyika vizuri katika mazingira yaliyojengwa kwa mahusiano imara, hivyo hebu tizama unahusiana vipi na watu waliokuzunguka na followers wako. Hili ni eneo pana ambapo unatakiwa ufahamu saikolojia ya watu wako hasa wateja na kujua namna ya kukabiliana nao positively. Maana mitandaoni kuna kila aina ya watu na tabia zao, kuna wenye kiburi, kuna wababe, wachechi, wajeuri, wanafunzi, wenye hekima, wapole, wenye lugha chafu na micharuko. Sasa jukumu lako ni kuwajua na kukabiliana nao bila kukwazana. Cha kufanya ni kuhakikisha unatumia vizuri bando lako tu hapa.

Mtandao saidizi jinsi ya kukabiliana na hasara kwenye biashara mbinu za kuwa tajiri

Humu mitandaoni wewe kama sio mtu maarufu basi hakikisha unakuwa mchangamfu kwa kadiri ya inavyowezekana. Kuwa “mchangamfu” haina maana uwe mwenye kiherehere, shobo au mtu wa kujipendekeza, lakini ujue namna kuchangia mijadala mbalimbali na kujihusanisha na watu vizuri.

2. JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI WA KUJIJENGA KUWA MTAALAM?

Kwenye biashara hili ni eneo muhimu sana, yani sawasawa na uti wa mgongo. Watu wengi hudhani biashara ni kuuza na kununua tu, of course wako sawa. Hata hivyo ili biashara yako iweze kunawiri katika mazingira ya mtandaoni yaliyojaa ushindani wa kila aina, unapaswa kujua zaidi ya “kuuza na kununua”. Humu mtandaoni watu hukwepa sasa matangazo, hivyo “unapoweka tangazo lako hakikisha halionekani kama TANGAZO bali lionekane kama HABARI MPYA kwa yeyote anayesoma.”

Mtego ndo upo hapo. Lazima uwe mtaalam wa kuhudumia faida zinazotokana na bidhaa/huduma zako. Usiuze tu ukaishia hapo, hebu kuwa MLEZI wa mteja wako. Binafsi nina LIST ya wateja wangu ambapo huwa nawatumia updates mbalimbali kuhusu hali ya biashara na uchumi katika muktadha wa teknolojia BURE kabisa. Ungependa kuwa kwenye list hio? Nitumie ujumbe kwa WhatsApp sasa hivi kwa kugusa namba hii hapa 0765834754

3. JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI WA KUFUNGUA WEBSITE:

Kwa kasi ambayo teknolojia inakwenda nayo nina uhakika usingependa kupitwa na fursa lukuki zinazokoja na mapinduzi haya ya 4 ya viwanda yanayoendelea duniani. Fikiria, Kusini mwa Jangwa la Sahara kunakadiriwa kuwa na watumiaji wa internet zaidi ya milioni 400. Nchini Tanzania kunaripotiwa kuwa na watumiaji wa internet zaidi ya milioni 29 mpaka kufikia mwaka 2022 Kwa mujibu wa ripoti ya TCRA.

jinsi ya kuanzisha website

Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji

Sasa kwa kutumia hilo Bando lako la internet, unalitumiaje kuwafikishia watu hawa bidhaa/huduma yako? Website ni kifaa (Digital tool) muhimu na mahsusi kwa kuwafikia watu wengi ndani ya muda mchache sana. Kwenye website unao uwezo wa kutoa huduma za kushauri na mafunzo nakdhalika. Zaidi unaweza kujua faida za kuwa na website kupitia hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?

Kuweza kupata website yako wasiliana nasi kupitia namba 0765834754 au email info@rednet.co.tz ili tukusaidia kutatua changamoto zinazokukabili. USIBAKI NYUMA.

4. JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI WA KUWA MKWELI/AMINIKA UKIWA MTANDAONI:

Moja kati ya eneo ambalo linawapa changamoto wafanyabiashara wengi ni hili la kuwa mkweli na Muaminifu. Wateja wengi huwa wanakwazika sana wanapofanya kazi na wafanyabiashara ambao si wakweli/waaminifu. Hiki ni kitu kibaya sana na hata wewe usingependa kikutokee.

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi? gharama vs thamani, kipi kinafaa zaidi?

Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji

Unapojijenga kwa kuwa mkweli unatengeneza mazingira ya kuaminika ambayo yatakufanya upendwe na watu na wao waweze kufanya biashara na wewe bila wasiwasi. Hata wewe mfanyabiashsra, siku ukiwa mteja usingependa kukutana na mtoa huduma ambaye si mkweli/mwaminifu, si ndio?

Ni matumaini yangu umegundua kwamba Bando lako ni Mtaji muhimu sana katika uendeshaji wa biashara yako katika zama hizi za kidijitali? Lazima ujue namna nzuri ya kuendesha akaunti yako ya mtandao wa kijamii ili ilete tija kiuchumi katika biashara yako. Unahitaji mtu wa kuendesha akaunti yako? Wasiliana nasi mara moja.

UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA 2021 – 2025?

Huwa ni kawaida kwa biashara kupata hasara, hasa zile changa/zinazoanza. Lakini inapotokea biashara inapoteza pesa nyingi kuliko inavyoingiza, Juhudi za dhati zinahitajika kujinasua kwenye tabu hio. Sasa jiulize katika kipindi hiki unaweza vipi kukabiliana na hasara katika biashara yako mwaka 2021 – 2025? Makinika mpaka mwisho wa makala hii kufahamu hizo siri.

Hasara inaweza kuwa katika namna ndogo kama kukosa dili fulani ulikua unafukuzia, kupoteza mteja, kupoteza vifaa vya kazi mpaka hasara kubwa kama kushindwa kulipa mahitaji ya biashara kama bili za umeme, mishahara na gharama za mawasiliano. Hali hii ilivyokutokea ulifanyaje?

Hata hivyo, Mjasiriamali bora huwa hatambuliwi kwa uwepo wa hasara katika biashara, bali Ule uwezo wake wa kudili na mazingira yanayoleta hasara mpaka kuhakikisha biashara inatamalaki kwa faida kutoka kwenye kivuli cha Hasara na majanga. Jinsi ya kupenya kwenye nyakati ngumu, ndipo anapopatikana mjasiriamali bora zaidi. Wahenga walishasema “Bahari tulivu haizalishi nahodha hodari.” Kumbe basi ubora upo kwenye Mawimbi, Hofu, Mkazo(pressure), Wasiwasi, Hasara na Woga.

Kwenye mazingira hayo ndipo Tuzo ya Ubora inapopatikana, Ndipo uaminifu kwa mteja unapojileta ndipo Uchumi unapotengeneza misingi yake na ndipo wateja watakapoongezeka kama sisimizi waonapo sukari. Lakini lazima kwanza ujue unatakiwa ufanye nini unapokuwa katka mazingira kama hayo? Na utajuaje kuwa upo kwenye mazingira hayo hatarishi? Lazima kichwa chako kiwe wazi kwanza kwanza kabla hatujasonga mbele.

UTAJUAJE KUWA BIASHARA YAKO INAJIENDESHA KWA HASARA?

Kiufupi Biashara kujiendesha kwa hasara ni pale matumizi yanapokuwa makubwa kuliko fedha inayoingia. Haya matumizi sio lazima yawe mpya, yanaweza kuwa ni yale yale kama bili za umeme, maji, matangazo, mishahara n.k

Mara nyingi matumizi hayo yako hivyo hivyo (constant). Japokuwa mara nyingi fedha inayoingia huwa haitabiriki hasa kwa bishara inayoanza. Hii inaweza kusababishwa na biashara kutokuwa na wateja wa kudumu, mabadiliko katika mahitaji na uelekeo wa masoko pamoja na ujuzi katika kufanya matangazo na mauzo.

Njia ya Kompyuta katika kuhifadhi data
utajuaje pale biashara yako inapojiendesha kwa hasara

Hata hivyo hali hii haipaswi kuwa ya kudumu. Mara nyingi huwa ni ya mpito tu. Lakini kama biashara yako mara kwa mara inajikuta ikijiendesha kwa hasara, my friend unatakiwa ujitafakari upya jinsi unaendesha biashara. Tafuta ushauri wa kitaalam na ikibidi usimamizi wa karibu(mentorship) kutoka kwa wataalam mbali mbali katika maswala ya biashara na usimamizi.

Hizi hapa ni Dalili za biashara inayojiendesha kwa hasara:

•Biashara haina pesa za kulipia gharama za uendeshaji (umeme, maji, mishahara, malighafi/raw materials, matangazo nk). Ukiona umefika hali hii jua ni Red light hio. Jipange.

•Salio lililopo bank/mobile-money ni 0 au negative (una madeni), na bahati mbaya hujui namna gani utaweza kupandisha salio lako kufikia mahali pa kujimudu. Hapa yani ujue kuwa umeshaishiwa mbinu. Rudi vitabuni/mtandaoni, soma, jirekebishe na waone wataalam wakupe direction mpya.

•Hauuzi kwa kiwango kile ambacho kimepangwa kwenye Business Plan. Hii Business Plan ni muhimu sana kuwa nayo kama mfanyabiashara makini. Hii ndio inabeba mipango na malengo yote ambayo biashara inatakiwa kuifikia ndani ya muda uliowekwa (2yrs, 5yrs, 10yrs etc).

Muhimu sana hio document kuwa nayo. Ukihitaji tafadhali wasiliana nasi kupitia mawasiliano haya WhatsApp namba 0765834754 au barua pepe; info@rednet.co.tz

Biashara za kisasa zinafanywa kwa kuzingatia Ujasusi wa Kiuchumi kwa sana. Na hakuna Ujasusi usio na mipango. Na mipango utaikuta katika Business Plan.

Tuendelee, Sasa unapokuwa kwenye mazingira hayo ya hasara, kuna namna nyingi ambazo unaweza kudili nayo. Leo hii tutadiscuss mbinu 9 za kukabiliana na hasara pindi inapotokea kwenye biashara yako. Namba 7 itakushangaza sana.

1. JIANDAE: Huna haja ya kuweka mipango mingi ya namna ya kukabiliana na mazingira ya hasara, hata hivyo jambo la muhimu zaidi ni Kujiandaa kisaikolojia kwamba Hasara ipo kwenye biashara na inaweza kutokea muda wowote. Matarajio yako yasiwe makubwa kuliko uhalisia. Hapo utafeli.

unaweza vipi kukabiliana na hasara katika biashara yako?

Kama unadhani kuwa mambo yatakwenda sawia na mipango yako uliyoiweka kukabiliana na hali ngumu, basi siku mambo yakienda tofauti unaweza kuwa kwenye wakati mgumu zaidi kuliko vile ingetarajiwa. Keep calm and let yourself soar through the storm, like an eagle in the air.

2. TAFUTA NAMNA YA KURUDISHA NGUVU: Nyakati ngumu na hasara kwenye biashara huumiza sana moyo, hudidimiza juhudi na kukatisha tamaa. Lakini kamwe nyakati hizi hazidumu, wanadumu watu imara. Hivyo yakupasa kuwa imara mda wote unakiwa mjasiriamali. Unaweza kujipa mapumziko, likizo ama kujiweka mbali na mazingira ya kazi kwa muda huku ukitafakari kwa kina nini kilikukwamisha na hatua gani unaweza kuzichukua ili kukabiliana na changamoto hizo. Matumizi ya vileo si mazuri hapa kwenye jambo hili.

3. USIAMUE KWA HISIA: Ukiwa kwenye hali ya mkazo huku ukiandamwa na hasara katika biashara, mara nyingi unaweza kujikuta ukiwa na hasira, huzuni, woga na hofu. Huu si wakati wa kufanya maamuzi hasa yahusuyo biashara yako. Tulia na tafuta suluhu kupitia watalaam au marafiki wema.

4. KUWA NA MTANDAO SAIDIZI: Hapa nazungumzia jumla ya watu wote unaokutana nao kila siku katika shughuli za kibiashara na kazi. Hawa watu wanapaswa wawe wasaidizi wako pale utakapowahitaji. Unapaswa kuwa na watu ambao ni assets na uepuke wale ambao ni liabilities (mzigo).

Mtandao saidizi
jinsi ya kukabiliana na hasara kwenye biashara

5. TATHMINI HALI YAKO: Hasara ni funzo moja zuri sana katika maisha ya biashara imara. Ni nafasi yako kujifunza wapi ulikosea na nini unapaswa kufanya ili wakati ujao hasara ipungue au iondoke kabisa biashara izalishe faida tu. Utumie vizuri wakati huu kufanya uchambuzi yakinifu.

6. USIISHI KWENYE HASARA: Katika historia hakuna mtu ambaye alifanikiwa sana na hakupata hasara. Kila shujaa unayemjua, pamoja na mafanikio yake, lakini wakati fulani alishapata hasara. Kinachomfanya mtu kuwa shujaa ni uwezo wa kunyanyuka na kutoruhusu hasara kuathiri utendaji.

7. TENGANISHA HASARA YA BIASHARA NA UTENDAJI WAKO BINAFSI: Ni ngumu mno kutenga mambo ya kibiashara na maisha binafsi. Kama biashara yako imepata hasara, ni biashara sio mkeo nyumbani au watoto au wewe binafsi, ndugu au marafiki. Usijilaumu wala usimlaumu mtu. Focus na biashara na hakikisha utendaji wa biashara hauathiri amani na utulivu ukiwa katika mazingira ya nje ya kazi. Watu wengi wamejikuta wakiingia katika migogoro mikubwa katika ndoa, familia na marafiki kutokana na kuchanganya biashara na undugu. Ni vitu visivyochangamana asilani na umakini mkubwa sana unahitajika kiuweledi katika kusimamia misingi ya kibiashara katika mahusiano ya familia.

8. ELEWA MAZINGIRA UNAYOJIHUSISHA NAYO: Mbinu bora zaidi ya kumshinda adui ni kumjua vizuri adui huyo. Kamwe huwezi kupigana na adui ambaye humjui sawia. Hivyo chukua muda kujua kwanini unapata hasara na ufanyeje ili hatimaye uweze kupata faida.

9. JIFUNZE: Vyovyote itakavyokuwa, maisha lazima yaendelee. Lakini kuendelea kujifunza ndio jambo muhimu ambalo unapaswa kulifanya mara zote. Maisha ya mfanyabiashara ni mfululizo wa mafunzo yasiyokwisha. Hivyo usikaze mishipa ya shingo, jifunze kila inapobidi ili kujiimarisha.

Pamoja na yote, kila mtu ana namna yake ya kukabiliana na hali ngumu na hasara. Hata hivyo mbinu ulizozipata leo zimethibitishwa kitaalam katika kuokoa biashara yoyote katika janga la hasara. Share, reply ili elimu hii iwafikie wafanyabiashara wengi zaidi.

Pitia makala hizi hapa ambazo zinarandana na somo ulilolipata hapa leo. Zitakusaidia sana:

  1. KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?
  2. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  3. BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA?
  4. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?

Umegundua nini baada ya kumaliza makala kuhusu unaweza vipi kukabiliana na hasara katika biashara yako mwaka 2021 – 2025? Share nasi mawazo yako katika comment hapo chini..

focus on your plans and make sure you win.

UKWELI KUHUSU ‘PROPAGANDA’

Wengine watakwambia ni maneno ya uchochezi, wengine “siasa za uhuni hizo”, wengine wanaita figisu, mara fitna. Lakini Propaganda ni mada inayowasilishwa kwa lugha ya picha katika mawasiliano ambayo mara nyingi hubebwa katika kampeni mbalimbali kwa agenda fulani ya kificho. Leo sasa tuone huo ukweli kuhusu ‘Propaganda’. Ni upi? Makinika.

Serikali na mashirika mbalimbali hufanya Propaganda katika kusukuma Agenda zao ambazo zina lengo la kushawishi jamii na kuchochea mapokeo ya kihisa kuhusu jambo fulani. Propaganda zilizokomaa hugeuzwa kuwa utamaduni, mfano Propaganda ya kuagamiza maadui wa “Ujinga, Maradhi na Umasikini” imesababisha watu wengi kwenda shule kupata elimu, kutibiwa kwa tiba za kisasa na kuachana na zile za kizamani pamoja na kufanya kazi kwa lengo la kuboresha hali ya kiuchumi. Ujinga, Maradhi na Umasikini vimeonekana ni adui wa kumuangamiza kabisa mbele ya kila mwananchi sasa na hii imesababishwa na Propaganda za serikali ya awamu ya kwanza katika kufikia lengo hilo.

Kwa upande mwingine Propaganda zimekuwa zikitumika kufanyiana hila za kisiasa katika kumkandamiza mpinzani ili kupata ushindi katika kinyang’anyiro fulani. Mfano kwenye michezo unaweza kumwona @hajismanara ambaye ni mmoja kati ya wana propaganda wazuri sana nchini. Maneno yake, tambo na kampeni anazozifanya kwa kiasi kikubwa ziliisaidia sana @SimbaSCTanzania na Yanga Kupata ushindi hata kabla ya mechi. Propaganda zinapigwa kwa kiwango sana hapa.

Kwingine ni kwenye ulingo wa siasa ambapo huku ndo Propaganda zilipozaliwa (kama wanavyosema Mapenzi yamezaliwa Tanga). Kwenye siasa mara kadhaa Propaganda zimekuwa zikipigwa kukandamizana kisiasa na kuaminisha umma kuwa fulani ni bora zaidi kuliko fulani, na sera hii ni bora zaidi kuliko sera hii. Ili kuweza kujenga ushawishi kwa wapiga kura, wanasiasa wamekuwa wakipiga propaganda za hali ya juu ili kuhakikisha wanapata ushindi. Ukiona mwanasiasa fulani anapendwa sana na ana wafuasi wengi, basi kwa kiasi kikubwa tambua Propaganda zake ni za kiwango cha juu sana.

Hata hivyo kufanya Propaganda si Dhambi, wala hakuna mtu anakatazwa kuzifanya isipokuwa tu usivunje sheria za nchi. Kuna baadhi ya watu huamini kuwa Propaganda ni Maneno ya Uongo na Ulaghai, Hapana. Propaganda ni sanaa ya kushawishi watu wafuate dhana fulani ili kuleta faida kwa mtu au jamii ya watu fulani, kampuni, shirika au serikali.

MBINU ZIPI HUTUMIKA KUFANIKISHA PROPAGANDA?

Mafanikio ya kufanya propaganda huja pale serikali/biashara fulani inapotumia mbinu hizi katika kushawishi jamii kufikia lengo fulani ambalo halionekani wazi kwa mara moja.

i. NJIA YA USHIRIKA (BRANDWAGON): Hii wahenga wanakwambia “Ndege wafananao huruka pamoja” au “Ukitembea na mwizi na wewe utakuwa mwizi”. Njia hii ni ile ambayo mpigapropaganda kujihusanisha na walengwa kwa ukaribu katika kuhakikisha propaganda zake zinakuwa na ushawishi. Najua umeshawahi kuona namna wanasiasa au makampuni wanavyotumia watu wa kitengo cha Masoko katika kuwafikia walengwa wao. Mara nyingi mpigapropaganda hubadili mavazi kuendana na walengwa, wakati mwingine huongea lugha ile inayozungumzwa na walengwa kabisa ili kuhakikisha propaganda zake zinakuwa na ushawishi unaotakiwa.

Pata huduma za Website, SEO, Social Media Marketing na nyinginezo nyingi kutoka Rednet Technologies Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?
ukweli kuhusu 'Propaganda'

ii.KUTAFUTA HURUMA YA JAMII (SNOP APPEAL): Hii ni njia maarufu sana ambayo kwa kiasi kikubwa imekuwa ikitumika katika kutengeneza story ambayo itagusa moyo wa jamii na kuhamasisha watu kukubali Agenda ambayo imebebwa katika propaganda hio. Inakuwa hivi, mtu hueleza story yake ambayo mara nyingi huwa ni ya kusikitisha, kwa lengo (linaloonekana) la kuhamashisha watu kutokata tamaa au kujenga uaminifu juu yao na hivyo kupata lengo (lisiloonekana) la kupata wafuasi, wateja au/na kura. Propaganda hii hufanywa sana na wasanii, wafanyabiashara na kampuni zinazoanza(startups). Umeshaanza kuuona hapa ukweli kuhusu ‘Propaganda’.

iii. MANENO YENYE UJAZO: Wahenga wanasema, “Maneno yanaumba”.Hii ni kwasababu maneno yana nguvu sana linapokuja swala la mahusiano ya kijamii. Ndio maana wanapropaganda hutumia maneneo yenye ujazo kubadili mtazamo wa jamii. Hapa wanapropaganda hutumia maneno matamu sana kushawishi jamii katika kufanya jambo fulani. Hali kadhalika wanapropaganda hutumia maneno ya hasira, chuki, fitna na hila ili kuhakikisha Agenda zao za siri zinafanikiwa. Wakati mwingine agenda hizo huwa na manufaa mema kijamii na wakati mwingine huja na lengo la kubomoa jamii.

Mathalani sisi Rednet Technologies tunakwambia, #WeGiveYouTheWorld hatuna maana kuwa tutakupa dunia kama ilivyo, hapana. Dhima yetu ni kuhakikisha tunakupatia taarifa zote muhimu kuhusu Biashara na Uchumi katika muktadha wa kiteknolojia ikiambatana na ushauri wa kitaalam.

Ili kuhakikisha wajasiriamali wadogo wanaimarisha biashara zao kupitia Matumizi ya teknolojia za kisasa kama Websites bora, softwares na chambuzi zisizokauka za kitaalam kupitia tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz. Tufuatilie uendelee kuimarisha biashara yako.

iv. KULINGANISHA DHANA: Wanapropaganda hutumia njia za kulinganisha dhana zao na matukio ya historia katika kupata kile wanachokidhamiria. Mathalani, katika siasa, watu wengi hupiga propaganda za kulinganisha hotuba za Mwalim Nyerere na matukio yanayoendelea katika kupush agenda zao.

Katika nyanja ya kibiashara, makampuni na mashirika hulinganisha maendeleo ya Kiteknolojia/Uchumi na uwezo wao wa kisasa katika kushawishi na kupata wateja wengi zaidi kila leo. Lakini chumvi ikizidi sana hapa, propaganda hizo hugeuka utapeli na kupoteza wateja kwa haraka sana.

v. NJIA YA SHUHUDA: Katika kufanya propaganda kwa njia hii makampuni na mashirika wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kuongeza wateja wapya na kukuza mauzo kwa viwango vikubwa sana. Makampuni/Mashirika yamekuwa yakiwatumia wasanii na watu mashuhuri kwenye jamii katika kueneza propaganda zao kuhusu huduma wanazotoa, bidhaa, kufungua matawi mapya ya ofisi pamoja na kufungua kampeni zao mbalimbali. Mara nyingi wasanii/watu mashuhuri wanaotumiwa kueneza propaganda hizo hawana elimu/taaluma kuhusu jinsi bidhaa/huduma inayoenezwa ilivyobuniwa/ilivyotengenezwa. Wao kikubwa ni kuhakikisha huduma/bidhaa hio inauzwa na kuketa faida kwenye kampuni/shirika hilo. Hapa ndipo unadhihirika ule ukweli kuhusu ‘Propaganda’.

mteja mshirikishe kwenye maamuzi. Msaidie aweze kununua huduma au bidhaa yako.

ukweli kuhusu 'Propaganda'

Hata hivyo mbinu hio inaweza kutumiwa kwa kupitia Masoko ya kimtandao (Network Marketing) au/na masoko kwa njia ya mitandao ya kijamii (social media marketing) ambapo mtandao wa twitter, facebook na LinkedIn imekuwa ikiongoza kwa kuwafanya watu washirikishane bidhaa/huduma zao. Mathalan kupitia twita, unaweza kusambaza bidhaa/huduma zako kwa kupitia watu ambao hawana ujuzi wa kutengeneza hizo bidhaa/huduma zako. Mfano sisi @RednetCompany tunasambaza huduma zetu kupitia rafiki zetu katika mitandao ya kijamii Ambao hata hivyo wengi kati yao hawana ujuzi kuhusu jinsi ya kutengeneza website, computer maintenance n.k. Lakini Agenda inayobebwa katika propaganda hio ni kuhakikisha tunahudumia Wafanyabiashara na watu wengine wengi zaidi kila leo.

Hivyo ukiwa kama mfanyabiashara hakikisha propaganda zako unazifanya kwa utaalam na weledi bila kufanya ulaghai au kusema uongo ili kujipatia faida. Kwa maana hio si njia bora ya kufanikiwa kipropaganda. Jipange vema kwenye uwanja huu uliosheheni ushindani wa kila namna.

Vile vile tayari hapa tumekuandalia makala ambazo zinarandana na somo ulilojifunza leo. Gusa links hizi kufahamu zaidi:

  1. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021?
  3. FAHAMU SIRI YA KUWEZA KUSHAWISHI WATEJA KATIKA BIASHARA YAKO
  4. UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Umejifunza nini katika makal hii ya leo kuhusiana na ukweli kuhusu ‘Propaganda’? Tafadhali toa maoni yako kupitia comments hapo chini, nasi tutayafanyia kazi mara moja.

UFAHAMU MFUMO WA KODI NA MAPATO YA SERIKALI ZA MITAA

Serikali za mitaa zikiwa ndani ya Halmashauri za miji/Majiji na Wilaya zina mamlaka ya kukusanya mapato na ushuru kutoka vyanzo mbalimbali vya kodi. Pia zina mamlaka ya kutumia mapato hayo kwa mujibu wa sheria.

Kulingana na mipaka ya kisheria inayowekwa na Serikali Kuu, hizi Serikali za mitaa zina uwezo wa kutengeneza sera zake za mapato ili kuleta maendeleo katika shughuli zinazogusa kwa ukaribu maendeleo jamii nzima kama mashule, hospitali, mazingira ya mitaa na ulinzi shirikishi.

Mapato haya yanayokusanywa yanapata Mamlaka kutoka katika Sheria ya Mapato ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1983 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Sasa leo ukimaliza kusoma makala haya, utakuwa umezijua kodi/tozo zote zinazokusanywa pamoja na matumizi yake kwa ujumla.

Idadi ya kodi na ushuru unaokusanywa chini ya Mamlaka ya serikali za mitaa hutofautiana kutoka Halmashauri moja na Halmashauri nyingine. Mambo yanayoleta utofauti huu ni maendeleo katika sekta za Biashara, makazi, Uwepo wa maliasili na shughuli za kiuchumi.

Kuna baadhi ya tozo hukusanywa kwa siku, zingine mlipakodi hutozwa kwa mwaka, na zingine humpa nafasi mlipakodi kuchagua wakati wa kulipa (kwa mwezi, wiki, miezi mitatu/sita au kwa mwaka). Mfano; ushuru wa masoko, huu kawaida hukusanywa kwa siku. Hata hivyo Halmashauri zingine hutoa nafasi kwa mlipakodi kulipia ushuru huu kwa mwezi, miezi 3/6 au kwa mwaka mzima. Mwisho wa mwaka wa fedha kila Halmashauri inatakiwa kuandaa akaunti za kifedha ikiwa na wadau wafuatao:

i. Halmashauri Nzima

ii. Muwakilishi wa wizara (TAMISEMI)

iii. Ofisi ya Waziri Mkuu

iv. Ofisi ya Mdibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG)

v. Umma

Serikali za Mitaa hupata mapato yake kutoka katika vyanzo vikuu vitatu :

1. Mapato yake yenyewe

2. Ruzuku kutoka Serikali Kuu

3. Misaada kutoka mifuko ya Maendeleo ya ndani na nje ya nchi.

MAPATO/KODI ZINAZOTOZWA NI ZIPI?

1. USHURU WA BIDHAA (PRODUCE CESS)

Ushuru huu hutozwa na halmashauri kutoka katika mauzo ya mazao kama mahindi, mchele, kahawa, chai, pamba korosho pamoja na mifugo. Ushuru huu hutozwa kutokana na uzito/ujazo wa bidhaa yenyewe. Hii hufanya thamani ya bidhaa kutokua thabiti ikitegemea uzito/ujazo wa bidhaa (the source to be inelastic unless adjustments become frequent enough to catch up with inflation), hapa watu wa uchumi mtakuwa mmenipata vizuri sana. Viwango vya ushuru huu hubadilika kutegemeana na Halmashauri kutokana na Jiografia ya eneo, misimu ya hali ya hewa pamoja na hadhi ya kiuchumi ya Halmashauri husika.

2. LESENI ZA BIASHARA

Kodi hizi hutozwa kutokana na ukubwa na aina ya biashara, yaani maduka mawili ya rejareja yatatozwa kodi ya leseni sawasawa bila kujali ukubwa wa mitaji yao au hesabu zao wanazowasilisha kwenye mamlaka za mapato (turnovers).

3. ADA YA MASOKO

Aina hii ya Ushuru kwa kawaida hutozwa kwa siku kwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa zao katika maeneo ya sokoni. Viwango vya tozo hii hubadilika kulingana na bidhaa zainazouzwa.

4. KODI YA ARDHI/MAJENGO

Kisheria, Serikali kuu inatakiwa kukusanya kodi kutoka kwenye mali zote zinazohamishika, wakati Serkali za Mitaa zitakusanya kodi katika mali zote zisizohamishika. Hata Hivyo, kodi ya ardhi na majengo haijaweza kutumika ipasavyo katika mambo ya kisiasa na uongozi katika nchi zinazoendelea. Katika kitabu chake kuhusu kodi ya ardhi, Richard Bird (1974:223) anasema, “The administrative constraint on effective land on effective land tax administration is so severe in most developing countries today that virtually all the more refined fiscal devises beloved by theorists can and should be discarded for this reason alone. Not only will they not be well administered, they will in all likelihood be so poorly administered as to produce neither equity, efficiency, nor revenue.” Nadhani hoja yake imeeleweka.

5. USHURU WA HOTELI/NYUMBA ZA WAGENI

Kodi hii kisheria hutegemea na tathmini binafsi kuhusu hesabu za hoteli/nyumba za wageni. Viwango vikubwa vya kodi huhamasisha ukwepaji wa kodi hasa kwa kurekodi hesabu mara mbilimbili. Katika utekelezaji, hasa kwa biashara ndogo ambazo hazitoi risiti, turnover zao hukadiriwa tu na hivyo kupunguza mapato kwenye serikali za mitaa. Hata hivyo, biashara kubwa ambazo pia hazitoi risiti huwekewa utaratibu wa kufanya maridhiano kati ya wakusanya kodi na walipa kodi. Utaratibu huu unaongeza gharama za uendeshaji na kuongeza mianya ya rushwa. Hata hivyo, kutokana na makusanyo haya kuzingatia asilimia za mapato ya biashara, makusanyo yanategemewa kubadilika kadhalika.

6. KODI YA MABANGO/MATANGAZO

Hii kodi wafanyabiashara wengi huilalamikia, wengine wasijui kwanini wanatozwa wakiweka tu mabango katika biashara zao. Viwango vya kodi hii hutegemea ukubwa wa bango, kama linawaka taa usiku na muda bango hilo litakavyokuwa wazi. Mapato ya mabango yanaendelea kukua kutokana na kuongezeka kwa biashara ambazo pia zinahitaji matangazo kujiimarisha.

7. USHURU WA MCHANGA

Unashangaa? Hadi mchanga wa kujengea unalipiwa kodi ndio katika baadhi ya halmashauri. Gharama ndogo za mchanga pamoja na kuongezeka kwa kasi ya watu kujenga kumechochea mmomonyoko wa udongo kwenye machimbo jambo lilifanya serikali kupiga marufuku Uchimbaji holela wa mchanga na kuanzisha utaratibu mpya wa kuchimba mchanga katika maeneo maalum na hivyo kudhibiti mapato yatokanayo na mchanga.

8. USHURU WA MACHINJIO/MAEGESHO

Halmashauri nyingi ambazo zina machinjio ya wanyama na maengesho ya magari hutoza kodi hio vizuri. Mapato yatokanayo na kodi hii yamekuwa yakiongezeka hasa maeneo ya mijini ambapo kumekuwa na uhitaji mkubwa wa maegesho ya magari na pikipiki pamoja na kuongezeka kwa wanyama wanaonmchinjwa katika maeneo maalum. Hii ni kwa kuwa serikali imefanikiwa kudhibiti machinjio zote za mitaani na kulazimisha wanyama wote kuchinjwa maeneo maalum ya machinjio ambayo yana udhibiti wa kiserikali na kuzingatia viwango vya nyama kwa manufaa ya walaji. Wale wanaopajua vingunguti watakuwa wamenipata sawasawa hapa.

9. KODI ZINGINE

Serikali za Mitaa hukusanya kodi nyingine nyingi sana. Unaweza kuzipata kwa ufupi katika tovuti rasmi ya Wizara ya Fedha kupitia link hii https://mof.go.tz/mofdocs/revenue/revlocal.htm…

Serikali za mitaa hazitozi kodi ambazo zipo nje ya zilizopo kwenye listi iliyo kwenye link hio.

Vile vile unaweza kupata maelezo kuhusu Kodi na wajibu wake katika matumizi ya mwaka 2018/2019 kupitia link hii hapa chini

https://rednet.co.tz/download/taxes-and-duties-at-a-glance-2018-2019…

HIZO KODI ZINATUMIKA VIPI?

Kodi zinazokusanywa na Halmashauri za Wilaya/Miji/Majiji hutumi kodi hizo kuimarisha mambo yafuatayo:

i. Ulinzi shirikishi

ii. Barabara za mitaani pamoja na miundombinu yake

iii. Zimamoto na uokoaji

iv. kuimarisha shughuli za kiuchumi (masoko, biashara) nk

Mfumo wa kodi wa serikali za mitaa kwa muda mrefu umekuwa tata sana na usio na uwazi katika makusanyo ya mapato yake mpaka matumizi. Lakini tangu kuzinduliwa kwa mfumo maalum wa makusanyo ya kodi kwa njia ya kielektroniki wa Local Government Revenue Collection Information System (LGRCIS) mnamo mwaka 2014, mfumo huo umekuwa mkombozi katika kurekodi makusanyo sahihi na kudhibiti matumizi katika Halmashauri. Mfumo huo wa kisasa umekuwa bora zaidi katika kukusanya Mapato ambapo unatoa urahisi wa kutumia njia mbalimbali za kulipia kodi kama MPESA, TIGOPESA, AIRTEL MONEY, Njia ya Benki na kadhalika.

Kuna makala hizi hapa chini tumekuwekea kwenye links. Zitakusaidia kufahamu zaidi kuhusu mifumo ya kodi na mapato hasa nchini Tanzania. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-nchini-tanzania/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NCHINI TANZANIA”
  2. https://rednet.co.tz/lipa-kodi-kwa-faida-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “LIPA KODI KWA FAIDA YA BIASHARA YAKO”
  3. https://rednet.co.tz/unaweza-vipi-kukabiliana-na-hasara-katika-biashara-yako-mwaka-huu-2021/ yenye kichwa “UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021”