Tag: Uchumi wa Afrika

mageuzi ya Intaneti (iot) katika biashara na maisha. Jihudumie leo kutoka Rednet Technologies. Kwanini mteja akuchague wewe?

IFAHAMU AINA MPYA YA UDALALI WA MTANDAONI (DROPSHIPPING)

Dunia inakwenda kasi sana na Teknolojia inazidi kusambaa na kuteka sekta za kiuchumi. Mwandishi mmoja alinukuliwa akisema “In this modern world, prepare to change your career.” Umeshafikiria kuwa Dalali smart? Leo sasa ifahamu aina mpya ya udalali wa mtandaoni (Dropshipping) kwa undani. Ni nini na inafanya kazi vipi? Makinika mpaka mwisho wa makala hii..

Kwa Afrika yenye watumiaji wa huduma za internet wanaokadiriwa kuzidi milioni 400, tafiti zinaonyesha fursa za kuongezeka kwa biashara za mtandaoni (e-commerce) sasa ni kubwa kuliko wakati mwingine wowote. Shirika la Statista linakadiria sekta ya e-commerce kufikia thamani ya US 29$ milioni kufikia mwaka 2022.

DROPSHIPPING NI NINI?

Hii ni aina ya Udalali wa kimtandao ambapo Mtu wa kati (Dalali) huchukua Oda kutoka kwa Mteja kisha huituma Oda hio kwa Mwenye Mali (Muuzaji) ambaye hukamilisha mauzo kwa Mteja na kumwachia Dalali Kamisheni yake stahili.

Lakini wakati mwingine hasa barani Afrika huyu Mtu wa Kati huchukua Oda kutoka kwa mteja kisha huenda kwa Mwenye mali na kuchukua Bidhaa na kisha kwenda kuiuza yeye moja kwa moja kwa Mteja. Hii ndio kitu inafanyika sana Afrika kama ulikua hujui.

Hata hivyo msingi Mkuu wa Dropshipping ni kuwa namna hii ya Biashara hufanywa na Mtu wa kati ambaye hana stock kabisa (haihitaji uwe na mtaji wa fedha au bidhaa ili kufanya dropshipping). Kwa hiyo Dropshipping ndiyo kinara katika aina za biashara za mtandaoni (e-commerce).

Hii Dropshipping ni biashara moja ambayo mtu yeyote hasa kijana anaweza kabisa kuifanya kwa kuwa haihitaji uwe na mtaji wa kifedha ama bidhaa (stock). Hata hivyo, kama zilivyo biashara zingine, sio biashara rahisi wala sio biashara ambayo inaweza kukutajirisha mara moja.

Unahitajika kuwa mbunifu, mwenye juhudi na mvumilivu ili uweze kufanikiwa kwenye aina hii ya biashara kwa kuwa:

1. KIWANGO CHA FAIDA NI KIDOGO: Kiwango cha faida hutegemea kamisheni au “cha juu” ambacho mara nyingi hakiwi kiwango kikubwa. Hivyo ili uweze kupata Faida kubwa inakubidi pia uhakikishe bidhaa/huduma nyingi zimemfikia mteja kupitia wewe.

KUMBUKA: Kila mauzo unayoyafanya hapa, kiwango kikubwa cha pesa humwendea Mwenye Mali, kile “Cha juu” ndio hubaki kuwa halali yako.

udalali wa mtandaoni
ongea na watu uvae viatu

ZINGATIA: Waswahili wanasema, “Ongea na watu uvae viatu” Ukitafsiri vizuri hii nafasi ya kufanikiwa ni kubwa kwa sababu kadiri unavyokuwa na watu wengi zaidi katika mtandao wako basi nafasi yako ya kutengeneza faida inazidi kuwa kubwa.

2. USHINDANI NI MKUBWA: Hii ni aina ya bishara ambayo ushindani wake ni mkubwa kweli kweli. Fikiria haihitaji mtaji wa Kifedha wala bidhaa(stock) ili kuanza kuifanya, watu wangapi wanaweza kuifanya? wangapi tayari wanaifanya sasa hivi? Hivyo ili ufanikiwe, lazima ukomae kweli.

3. UHALALI/UBORA WA BIDHAA: Mara nyingi hii sio kesi kubwa lakini huwa inatokea. Ni mara ngapi imetokea mteja ameona bidhaa fulani kupitia ukurasa wako(mtu kati) wa mtandaoni, halafu vile umeenda kwa Mwenye Mali ukakuta ile bidhaa iliyoonekana kwenye picha mtandaoni sio ile halisi uliyoikuta kwa Mwenye Mali. Hili jambo ni baya na linaumiza sana watu wa kati na wakati mwingine hushusha heshima na uaminifu ambao wameutengeneza kwa wateja wao kwa muda mrefu sana.

Wakati mwingine hutokea hata mwenye mali si halali kisheria au/na wewe (dalali) hufahamu hata bidhaa unazozichukua ili kupeleka kwa mteja zinatoka wapi. Swala la bidhaa feki linaathiri sana kipengele hiki ambapo hutokea bidhaa iliyoonekana mtandaoni kuwa na logo fulani inayoaminika, lakini ile iliyo kwa ground inakuwa logo ya kughushi/feki. Hivyo lazima uwe mwangalifu.

4. UGUMU WA KUTENGENEZA BRAND: Ukiwa mfanyabiashara wa aina ya Dropshipping, fahamu kuwa sifa ya ubora wa bidhaa mara zote itakwenda kwa Mwenye Mali tu. Kitachokufanya uendelee kubaki kwenye game ni namna yako nzuri ya kuhudumia wateja wako wote bila ubaguzi na kwa ubora wa juu.

Kutengeneza Brand ni muhimu sana. Brand haijengwi kwa siku moja hata hivyo, ni mchakato wa muda mrefu. Sasa kuelewa zaidi kuhusu Brand (ni nini na inafanyika vipi) gusa link hii hapa Branding vs Marketing, kipi ni kipi?

Kumbuka: sio Logo yako iliyo kwenye bidhaa. Hivyo tengeneza SUMAKU yako kwa kutumia aina ya maneno yanayoweza kuuza bidhaa (copywriting), matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii pamoja na website bora na ambayo imeunganishwa na huduma za S.E.O.

Hizo ni baadhi ya Changamoto ambazo unategemea kukutana nazo katika aina hii ya biashara mtandaoni. Hata hivyo, kuna namna ambayo unatakiwa ujipange ili kuhakikisha Biashara yako inakuwa na mafanikio zaidi na uwezo wa kupambana na changamoto.

Kipi cha kufanya ili ufanikiwe katika Udalali huu wa Mtandaoni (Dropshipping)?:

1. CHAGUA HADHIRA YAKO: Haya ni mazingira na aina ya watu ambao unajihusanisha nao kila siku mtandaoni. Fahamu kuwa aina ya watu unaojihusanisha nao ni muhimu katika kutengeneza Aina ya soko linalofaa kwa bidhaa zako. Pia aina ya watu inaweza kukuambia ni aina gani ya bidhaa itawafaa kulingana na changamoto unaziziona zikiwatatiza kutoka kwao. Hapa lazima uwe na jicho zuri la kuona kile watu wengi hasa wafanyabiashara wenzako hawakioni. Kuwa Mchunguzi kidogo, hala hala usije kuwa mbea tu. Kwa vyovyote unapokua dalali hasa wa mtandaoni lazima ujitangaze, Kwanini ujitangaze sasa fuatana na makala hii hapa kufahamu zaidi..

2. TAFUTA MFANYABIASHARA (MWENYE MALI) WA KUAMINIKA: Hiki ni kipengele muhimu katika kuhakikisha bidhaa zako zinaweza kupatikana kwa wakati bila longolongo wala ujanjaujanja. Mteja mara nyingi hununua kwa uhitaji ambao husukumwa na hisia. Hivyo hisia hizo zinaposhindwa kufikiwa ndani ya muda fulani, basi mteja anaweza kugairi au kununua kwa mtu mwingine.

Hapa ukiwa kama mfanyabiashara lazima ujue namna ya kutengeneza hali ya dharura kwa mteja ili anunue bidhaa yako kwa upesi, lakini zaidi lazima utimize haja ya mteja wako ndani ya muda na kwa uhakika.

3. CHAGUA BIDHAA YA KUUZA: Kabla hujaanza kufanya aina hii ya biashara lazima ujue hizo bidhaa zinazohusika “utamuuzia nani?”. Katika kuchagua unatakiwa uangalie Umri, Elimu, Makundi ya kijamii (wanafunzi, wasomi wa vyuo, wafanyakazi, wazazi, watu wa dini nk). Hivyo lazima ujue ni bidhaa zipi zinawafaa wateja na hadhira yako Kiujumla.

Njia nzuri ya kuchagua bidhaa zinazouzika sana ni kupitia majukwaa kama YouTube kupitia matafuto kama “top 10 products to sell” utajifunza mengi humo.

•Pia unaweza kutumia Majukwaa ya Amazon na AlliExpress kupata bidhaa zinazofaa kufanyia biashara unayotaka kuifanya.

•Chunguza matangazo (sponsored ads) kupitia mitandao kama facebook, instagram na twitter. Kwenye kuchagua aina ya bidhaa jitahidi kuepuka:

•Bidhaa za chakula ambazo zinahitaji uthibitisho wa mamlaka, huna muda wa kupeleka bidhaa ikathibitishwe TMDA/TBS kabla haijamfikia mteja.

•Bidhaa ambazo ni silaha. Hizi mara nyingi soko lake ni la shaka kwa wateja wengi, hivyo kizifanya kutokuwa reliable.

•Mambo ya Fashion: Najua hii ndio watu wengi wanapenda kufanya, lakini jitafakari kuhusu ushindani wake sokoni, Nadhani unawajua wanaouza nguo na viatu katika mitandao ya kijamii.

4. WEKA BIDHAA ZAKO MTANDAONI: Baada yakufanya yote hapo juu, hakikisha bidhaa zako zinaonekana mtandaoni. Njia nzuri zaidi ya kuweka bidhaa mtandaoni ni kupitia Website na Instagram kwa sababu bidhaa inatakiwa kuonekana kwa picha ili kumvutia mteja. Mitandao mingi ya kijamii haikupi nafasi nzuri ya kuonyesha bidhaa zako kwa wateja katika unadhifu unaotakiwa. Hata hivyo ni muhimu pia kutumia mitandao mingine ya kijamii katika kunadi bidhaa zako mara kwa mara kupitia ujuzi wa “Copywriting” vizuri.

Sasa nimekuwekea makala kupitia links hizi hapa chini ili kuhakikisha somo la leo unalielewa vizuri. Zitakusaidia sana ukizimaliza zote.

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO

Nadhani leo ume ifahamu aina mpya ya udalali wa mtandaoni (Dropshipping) katika kiwango chake. Unalo lolote la kushare nasi? Tafadhali tujadili kupitia comment hapo chini.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Ifahamu aina mpya ya udalali wa mtandaoni.

UFAHAMU MFUMO WA KODI NA MAPATO YA SERIKALI ZA MITAA

Serikali za mitaa zikiwa ndani ya Halmashauri za miji/Majiji na Wilaya zina mamlaka ya kukusanya mapato na ushuru kutoka vyanzo mbalimbali vya kodi. Pia zina mamlaka ya kutumia mapato hayo kwa mujibu wa sheria.

Kulingana na mipaka ya kisheria inayowekwa na Serikali Kuu, hizi Serikali za mitaa zina uwezo wa kutengeneza sera zake za mapato ili kuleta maendeleo katika shughuli zinazogusa kwa ukaribu maendeleo jamii nzima kama mashule, hospitali, mazingira ya mitaa na ulinzi shirikishi.

Mapato haya yanayokusanywa yanapata Mamlaka kutoka katika Sheria ya Mapato ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1983 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Sasa leo ukimaliza kusoma makala haya, utakuwa umezijua kodi/tozo zote zinazokusanywa pamoja na matumizi yake kwa ujumla.

Idadi ya kodi na ushuru unaokusanywa chini ya Mamlaka ya serikali za mitaa hutofautiana kutoka Halmashauri moja na Halmashauri nyingine. Mambo yanayoleta utofauti huu ni maendeleo katika sekta za Biashara, makazi, Uwepo wa maliasili na shughuli za kiuchumi.

Kuna baadhi ya tozo hukusanywa kwa siku, zingine mlipakodi hutozwa kwa mwaka, na zingine humpa nafasi mlipakodi kuchagua wakati wa kulipa (kwa mwezi, wiki, miezi mitatu/sita au kwa mwaka). Mfano; ushuru wa masoko, huu kawaida hukusanywa kwa siku. Hata hivyo Halmashauri zingine hutoa nafasi kwa mlipakodi kulipia ushuru huu kwa mwezi, miezi 3/6 au kwa mwaka mzima. Mwisho wa mwaka wa fedha kila Halmashauri inatakiwa kuandaa akaunti za kifedha ikiwa na wadau wafuatao:

i. Halmashauri Nzima

ii. Muwakilishi wa wizara (TAMISEMI)

iii. Ofisi ya Waziri Mkuu

iv. Ofisi ya Mdibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG)

v. Umma

Serikali za Mitaa hupata mapato yake kutoka katika vyanzo vikuu vitatu :

1. Mapato yake yenyewe

2. Ruzuku kutoka Serikali Kuu

3. Misaada kutoka mifuko ya Maendeleo ya ndani na nje ya nchi.

MAPATO/KODI ZINAZOTOZWA NI ZIPI?

1. USHURU WA BIDHAA (PRODUCE CESS)

Ushuru huu hutozwa na halmashauri kutoka katika mauzo ya mazao kama mahindi, mchele, kahawa, chai, pamba korosho pamoja na mifugo. Ushuru huu hutozwa kutokana na uzito/ujazo wa bidhaa yenyewe. Hii hufanya thamani ya bidhaa kutokua thabiti ikitegemea uzito/ujazo wa bidhaa (the source to be inelastic unless adjustments become frequent enough to catch up with inflation), hapa watu wa uchumi mtakuwa mmenipata vizuri sana. Viwango vya ushuru huu hubadilika kutegemeana na Halmashauri kutokana na Jiografia ya eneo, misimu ya hali ya hewa pamoja na hadhi ya kiuchumi ya Halmashauri husika.

2. LESENI ZA BIASHARA

Kodi hizi hutozwa kutokana na ukubwa na aina ya biashara, yaani maduka mawili ya rejareja yatatozwa kodi ya leseni sawasawa bila kujali ukubwa wa mitaji yao au hesabu zao wanazowasilisha kwenye mamlaka za mapato (turnovers).

3. ADA YA MASOKO

Aina hii ya Ushuru kwa kawaida hutozwa kwa siku kwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa zao katika maeneo ya sokoni. Viwango vya tozo hii hubadilika kulingana na bidhaa zainazouzwa.

4. KODI YA ARDHI/MAJENGO

Kisheria, Serikali kuu inatakiwa kukusanya kodi kutoka kwenye mali zote zinazohamishika, wakati Serkali za Mitaa zitakusanya kodi katika mali zote zisizohamishika. Hata Hivyo, kodi ya ardhi na majengo haijaweza kutumika ipasavyo katika mambo ya kisiasa na uongozi katika nchi zinazoendelea. Katika kitabu chake kuhusu kodi ya ardhi, Richard Bird (1974:223) anasema, “The administrative constraint on effective land on effective land tax administration is so severe in most developing countries today that virtually all the more refined fiscal devises beloved by theorists can and should be discarded for this reason alone. Not only will they not be well administered, they will in all likelihood be so poorly administered as to produce neither equity, efficiency, nor revenue.” Nadhani hoja yake imeeleweka.

5. USHURU WA HOTELI/NYUMBA ZA WAGENI

Kodi hii kisheria hutegemea na tathmini binafsi kuhusu hesabu za hoteli/nyumba za wageni. Viwango vikubwa vya kodi huhamasisha ukwepaji wa kodi hasa kwa kurekodi hesabu mara mbilimbili. Katika utekelezaji, hasa kwa biashara ndogo ambazo hazitoi risiti, turnover zao hukadiriwa tu na hivyo kupunguza mapato kwenye serikali za mitaa. Hata hivyo, biashara kubwa ambazo pia hazitoi risiti huwekewa utaratibu wa kufanya maridhiano kati ya wakusanya kodi na walipa kodi. Utaratibu huu unaongeza gharama za uendeshaji na kuongeza mianya ya rushwa. Hata hivyo, kutokana na makusanyo haya kuzingatia asilimia za mapato ya biashara, makusanyo yanategemewa kubadilika kadhalika.

6. KODI YA MABANGO/MATANGAZO

Hii kodi wafanyabiashara wengi huilalamikia, wengine wasijui kwanini wanatozwa wakiweka tu mabango katika biashara zao. Viwango vya kodi hii hutegemea ukubwa wa bango, kama linawaka taa usiku na muda bango hilo litakavyokuwa wazi. Mapato ya mabango yanaendelea kukua kutokana na kuongezeka kwa biashara ambazo pia zinahitaji matangazo kujiimarisha.

7. USHURU WA MCHANGA

Unashangaa? Hadi mchanga wa kujengea unalipiwa kodi ndio katika baadhi ya halmashauri. Gharama ndogo za mchanga pamoja na kuongezeka kwa kasi ya watu kujenga kumechochea mmomonyoko wa udongo kwenye machimbo jambo lilifanya serikali kupiga marufuku Uchimbaji holela wa mchanga na kuanzisha utaratibu mpya wa kuchimba mchanga katika maeneo maalum na hivyo kudhibiti mapato yatokanayo na mchanga.

8. USHURU WA MACHINJIO/MAEGESHO

Halmashauri nyingi ambazo zina machinjio ya wanyama na maengesho ya magari hutoza kodi hio vizuri. Mapato yatokanayo na kodi hii yamekuwa yakiongezeka hasa maeneo ya mijini ambapo kumekuwa na uhitaji mkubwa wa maegesho ya magari na pikipiki pamoja na kuongezeka kwa wanyama wanaonmchinjwa katika maeneo maalum. Hii ni kwa kuwa serikali imefanikiwa kudhibiti machinjio zote za mitaani na kulazimisha wanyama wote kuchinjwa maeneo maalum ya machinjio ambayo yana udhibiti wa kiserikali na kuzingatia viwango vya nyama kwa manufaa ya walaji. Wale wanaopajua vingunguti watakuwa wamenipata sawasawa hapa.

9. KODI ZINGINE

Serikali za Mitaa hukusanya kodi nyingine nyingi sana. Unaweza kuzipata kwa ufupi katika tovuti rasmi ya Wizara ya Fedha kupitia link hii https://mof.go.tz/mofdocs/revenue/revlocal.htm…

Serikali za mitaa hazitozi kodi ambazo zipo nje ya zilizopo kwenye listi iliyo kwenye link hio.

Vile vile unaweza kupata maelezo kuhusu Kodi na wajibu wake katika matumizi ya mwaka 2018/2019 kupitia link hii hapa chini

https://rednet.co.tz/download/taxes-and-duties-at-a-glance-2018-2019…

HIZO KODI ZINATUMIKA VIPI?

Kodi zinazokusanywa na Halmashauri za Wilaya/Miji/Majiji hutumi kodi hizo kuimarisha mambo yafuatayo:

i. Ulinzi shirikishi

ii. Barabara za mitaani pamoja na miundombinu yake

iii. Zimamoto na uokoaji

iv. kuimarisha shughuli za kiuchumi (masoko, biashara) nk

Mfumo wa kodi wa serikali za mitaa kwa muda mrefu umekuwa tata sana na usio na uwazi katika makusanyo ya mapato yake mpaka matumizi. Lakini tangu kuzinduliwa kwa mfumo maalum wa makusanyo ya kodi kwa njia ya kielektroniki wa Local Government Revenue Collection Information System (LGRCIS) mnamo mwaka 2014, mfumo huo umekuwa mkombozi katika kurekodi makusanyo sahihi na kudhibiti matumizi katika Halmashauri. Mfumo huo wa kisasa umekuwa bora zaidi katika kukusanya Mapato ambapo unatoa urahisi wa kutumia njia mbalimbali za kulipia kodi kama MPESA, TIGOPESA, AIRTEL MONEY, Njia ya Benki na kadhalika.

Kuna makala hizi hapa chini tumekuwekea kwenye links. Zitakusaidia kufahamu zaidi kuhusu mifumo ya kodi na mapato hasa nchini Tanzania. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-nchini-tanzania/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NCHINI TANZANIA”
  2. https://rednet.co.tz/lipa-kodi-kwa-faida-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “LIPA KODI KWA FAIDA YA BIASHARA YAKO”
  3. https://rednet.co.tz/unaweza-vipi-kukabiliana-na-hasara-katika-biashara-yako-mwaka-huu-2021/ yenye kichwa “UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021”

FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRICA

Kwa mara ya kwanza katika Historia ya mwanadamu, zaidi ya nusu ya watu wote duniani wanatumia huduma za internet. Na katika maeneo yote, imeonekana huduma hizo zinakua kwa kasi zaidi barani Africa. Idadi ya watu wanaotumia internet imeongezeka sana barani Afrika kutoka 2.1% mwaka 2005 mpaka 24.4% mwaka 2018. Sasa leo nataka u fahamu mchango wa ICT katika maendeleo ya sekta binafsi barani Africa. Twende sambamba.

Huduma hizi za internet zimekuja kurahisisha shughuli za kiuchumi kama kurahisisha njia za malipo (bank, MPESA, tigopesa nk), matumizi ya drones katika matibabu kama inavyofanyika nchini Rwanda, matumizi ya smartphones katika kuongeza maarifa ya kitaaluma na kiufundi stadi na kuongezeka kwa biashara za mtandaoni (e-commerce businesses, network marketing and online businesses). Bill Gates amewahi kuandika katika moja ya tweets zake “If your business is not on the Internet yet, Your are out of the Business.” Mwenye macho haambiwi ona.

SEKTA BINAFSI, INJINI YA UCHUMI AFRIKA

Kama ulikua hufahamu, basi sekta binafsi ndio imetawala Uchumi wa Afrika kwa kuwa zaidi ya 80% ya uzalishaji mali mzima hufanyika katika sekta hio. Zaidi, theluthi mbili (⅔) ya uwekezaji mzima barani na robo tatu (¾) ya jumla ya mitaji katika uchumi kati ya mwaka 1996-2008 imeonekana kutokea katika sekta hio binafsi. Vile vile sekta hio inatoa 90% ya ajira zote kwa vijana walio katika umri wa kufanya kazi. Mchango wa biashara za ndani katika sekta binafsi katika GDP ilikua 59% katika nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara ukilinganisha na 30% ya nchi za Latin America na Caribbean, 32% Asia Kusini na 42% katika Mashariki ya Kati. Hii inaonyesha kiasi gani Afrika sekta binafsi inalipa maradufu. Umeiona nafasi yako hapa ndugu yangu mfanyabiashara.!?

Kujiimarisha katika Sekta binafsi, huna budi kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kila mara unapohitajika kufanya hivyo. Unawezaje kufanya maamuzi sahihi katika changamoto zinazokukabili? Tafadhali fuatana nasi katika makala hii hapa FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI.

Katika nchi za Uchumi wa kati, kampuni binafsi hufanya kazi katika mfumo wa sekta rasmi, ambapo makampuni makubwa na yale madogo (SME’s) huzalisha hisa za thamani katika uwekezaji na zaidi, ajira kwa vijana ambao ndio kundi kubwa zaidi katika nguvu kazi barani Afrika. Lakini zaidi, sekta binafsi katika nchi hizi hufanya ⅔ ya uzalishaji mzima.

Uchumi huwa na ushindani pale kunapokuwa na ushindani mkali wa kibiashara. Na biashara huwa na ushindani pale:

•Sheria zinapokua sawa na haki.

•Wafanyakazi wana maarifa stahiki.

•Gharama za uendeshaji (umeme, maji, mafuta, usafiri) zinakuwa nafuu.

•Wateja wanafikika kila kona.

ICT INAINGIA VIPI HAPO?

Uchumi wa kidijitali umekuwa dhima kuu ya kidunia na Afrika haijabaki nyuma katika hili. Matumizi ya teknolojia yanazidi kushika kasi barani yakichagizwa na kasi ya ueneaji wa huduma za internet ambapo biashara nyingi zinazidi kuhamia mtandaoni kirahisi. Mpaka kufikia mwaka 2015 tu tayari watu 557 barani walikua wanatumia simu ya mkononi ambayo ni 12% ya watumiaji wote wa simu duniani huku idadi hio ikikusanya 6% ya mapato yote yaliyofanyika duniani wakati huo.

Sasa leo wacha tuone maeneo muhimu ya ICT yanayokuza uchumi zaidi;

1. TELECOMUNICATIONS

Eneo hili linajumuisha makampuni makubwa ya mawasiliano. Kwa kiasi kikubwa hufanya shughuli zake katika utaratibu wa sekta rasmi, hivyo kuwafikia watu wengi na kufanya kazi karibu zaidi na mamlaka za serikali. Makampuni kama Vocacom, MTN, Tigo, Airtel na TTCL yapo hapa. Kutokana na kuwa na watumiaji wengi, makampuni haya huchangia kiasi kikubwa katika mapato ya kiserikali kama kodi na gawio huku yakichangia sehemu kubwa katika kukuza uchumi wa watumiaji wake kutokana na fursa zinazopatikana katika huduma wanazozitoa kama uwakala wa huduma, huduma za kifedha nakadhalika.

2. SOFTWARE AND IT CONSULTING

Hapa ndo utatukuta sisi sasa ambao tunakuhudumia wewe muda huu. Zaidi ya kukupatia taarifa hizi ghafi, pia eneo hili la ICT hutoa huduma za kutengeneza mifumo ya computer, Apps za simu, Ushauri na Uchambuzi wa kiteknolojia katika Biashara na Uchumi. Japokuwa sio maarufu sana lakini sehemu hii inachangia uchumi wa mabiashara mbalimbali, makapuni madogo na yale yanayokuwa (SME’s) pamoja na sekta zingine za uma na binafsi kwa kutoa huduma za matengenezo ya tovuti, mifumo mbalimbali ya kibiashara, huduma za afya, elimu, uhifadhi wa data pamoja na uchambuzi na ushauri wa biashara mbalimbali kiteknolojia zaidi.

3. DIGITAL SERVICES

Hapa utawakuta watu wanaotoa huduma za kidijitali ambao wengi wao hufanya kazi kwa ukaribu na makampuni ya mawasiliano. Watoa huduma hawa pia wanahusika kutengeneza mifumo ya makampuni ya mawasiliano pamoja na kutengeneza/kuendesha mitandao ya kijamii zaidi. Watoa huduma hawa wamekuwa wakitengeneza michezo ya video pamoja na kutoa huduma za WebHosting na Cloud services kwa makampuni ya Kiafrika. Kampuni kama Dudumizi Technologies(Tanzania), ISB North Africa (Morocco), Web4Africa (Ghana) na Domains Africa Technologies (Kenya) zipo hapa.

4. INFORMATION SERVICES

Hapa sasa ndio utazikuta redio na televisheni zote unazozifahamu. Hawa kwa jina lingine wanaitwa Watoaji wa Maudhui, ambapo hutafuta habari na maudhui wanayodhani yanafaa kwa wateja wao na hivyo kukusanya jamii ili ipate maudhui hayo huku yenyewe yakijipatia faida yake katika matangazo mbalimbali ya kibiashara yanayoruka sambamba na maudhui yao. Hapa unaweza kunitajia Redio/TV ambayo ina maudhui unayoyapenda yakienda sambamba na matangazo ya wadhamini wa vipindi vyao. Usishangae ukiona hivyo. Kwenye matangazo ndo wanapopatia pesa wenzio, usione unapata bure maudhui hayo.

Kwa uchache haya ndio mambo ya fahamu mchango wa ICT katika maendeleo ya sekta binafsi barani Africa yanayochangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa Uchumi wa Kidijitali na kuboresha biashara nyingi zaidi kila kukicha barani Afrika. Jiulize, unayatumia vipi maeneo haya katika kukuza biashara yako wewe kama mjasiriamali?

Makala hizi hapa chini zitakusaidia kufahamu kwa undani namna sekta binafsi zinachangia uchumi na maendeleo ya wafanyabiashara hasa vijana wa Afrika Mashariki. Gusa links kisha makinika:

  1. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE (TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?
  2. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  3. UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA

Usisahau kutoa maoni yako kuhusu ukichojifunza katika makala hii ya leo na unaweza kusambaza ili kuhakikisha ulichijifunza kinawafikia wengine. Pia unaweza kutembelea tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz kuhakikisha unaendelea kupata taarifa sahihi kuhusu uchumi na biashara yako kiteknolojia. Asante.

Makala hii ni Kwa Heshima ya Hayati B.W. Mkapa aliyekuwa Rais awamu ya 3 nchini Tanzania. Mzee Mkapa aliongoza Taifa kuelekea zama hizi za maendeleo ya Sekta Binafsi kupitia Sera yake ya Ubinafsishaji wa mali za umma zilizokua mzigo kwa serikali, hivyo kuchochea ukuaji wa sekta binafsi kwa kiasi kikubwa mpaka kufikia hivi ilivyo leo. Mzee aliona mbali sana. #RIPMkapa

KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?

Hebu fikiria wewe ni mgeni mahali fulani, baada ya kushikwa na njaa unaelekezwa migahawa miwili, mmoja ukiutafuta mtandaoni unaweza kupata taarifa zake mwingine hauna taarifa yoyote mtandaoni. Uelekeo wako utakuwa upande gani? Leo sasa tutakwenda kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako. Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Kuishi katika ulimwengu wa kidijitali, tovuti ni zana muhimu sana katika biashara na masoko ya kidijitali. Cha kushangaza inakadiriwa 35% – 50% ya biashara ndogondogo duniani hazina tovuti zao binafsi, jambo linalozinyima fursa ya kuweka taarifa zao kirahisi mtandaoni na kupata wateja wapya kirahisi.

Kuna wanaosema kuwa matumizi ya Tovuti yanamezwa na uwepo wa mitandao ya kijamii ambayo pia watu wanaweza kuweka na kutangaza biashara zao humo. Ni kweli, aghalabu, kwa kutumia Mitandao ya kijamii hauna uhakika wa kumiliki taarifa na maudhui unayoweka humo muda wote. Watengenezaji ambao pia ni wamiliki wa Mitandao hio wanao uwezo wa kusimamisha/kufuta akaunti au maudhui yako muda wowote ikiwa biashara/maudhui yako yanakwenda kunyume na matakwa na masharti yao.

Vile vile Mitandao ya kijamii unayotumia inaweza kupungua umaarufu au kufilisika muda wowote usioutegemea mfano kuna mitandao ilikua maarufu sana zamani kama Hi5 lakini umaarufu wake kwa sasa umepungua au kupotea kabisa. Hivyo, uwezekano wa kudorora kwa biashara yako kunategemea pia umaarufu wa mtandao wa kijamii unaoutumia, jambo linalichangiwa sana na ujio wa mitandao mipya ya kijamii kama Instagram, Whatsapp na TikTok. Hii kwako unaionaje? Nitaeleza Tofauti katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Tovuti wakati Ujao.

Faida ni nyingi sana za matumizi ya website katika kuimarisha biashara yako kupitia ulimwengu wa Teknolojia. Tayari tumekuandalia makala maalum kupitia link hii hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

Leo hii ntakwambia mambo 10 kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika biashara yako:

1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:

Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu huenda wapi kutafuta vitu kama suppliers, bidhaa na huduma mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi. Injini za matafuto mtandaoni zimekuwa kimbilio namba moja huku GOOGLE Ikiziacha mbali Injini zingine kama Yahoo, Bing na Ask. Maana yake hii ni kwamba kama huna tovuti, jua mauzo yako ni 7% tu ya soko zima ambalo hujui kuwa unalo. Upo apo? Yani unapoteza 93% ya mauzo yako kila siku bila hata wewe mwenyewe kujua.

2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)

Kama una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo. Kwa biashara zenye malengo makubwa kuwa na tovuti huwaweka kwenye nafasi za juu katika kupata tenda na wateja, na huonyesha Uweledi bora katika utendaji wa biashara kuanzia katika muonekano na utendaji wa tovuti. Inakadiriwa 80% ya watu duniani huonyesha kutokua na imani na Biashara ambazo hazina tovuti pale wanapotaka huduma/bidhaa fulani mtandaoni.

3. KUPATIKANA KWA URAHISI

Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi, tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako. Ndivyo ilivyo kwa tovuti ambayo inajieleza kwa kila kitu kama ilivyo tovuti maridhawa ya http://rednet.co.tz . Ile raha ya kupata taarifa, huduma au bidhaa kirahisi kupitia simu yako ya mkononi, hufanya wateja waongezeke maradufu na kusambaza sifa bora kwa uharaka sana katika jamii na katika mitandao ya kijamii hali kadhalika.

Hii huongezwa chumvi ya SEO (Search Engine Optimization) ambayo ni teknolojia iliyowekwa katika Injini za matafuto ya kimtandao inayowasiliana na tovuti yako na kuweka taarifa katika Injini hizo na hivyo kufanya taarifa za tovuti yako kuonekana haraka zaidi katika matafuto. Biashara imerahisishwa sana kupitia SEO kuliko kutumia Mitandao ya kijamii. Kama watu wanakwenda Google kutafuta taarifa, basi fahamu taarifa hizo hupelekwa hapo GOOGLE kwa kutumia teknolojia iitwayo S.E.O. Kufahamu zaidi kuhusu SEO gusa hapa chini

4. TANGAZO LA BURE MUDA WOTE

Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo huduma ya internet inapatikana. Tangazo la bure kabisa hili. Kama tovuti yako ina ubora wa kuvutia zaidi katika muonekano, maudhui na utendaji, basi bila shaka biashara yako ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri sokoni na kupata wateja wengi kila siku. Jiulize hivi, unapofunga ofisi/biashara yako wakati wa jioni kila siku, wateja wapya wanaweza vipi kupata taarifa sahihi muda watakaohitaji?turudi kwenye mada yetu, kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Hii pia inawezeshwa sana na teknolojia ya S.E.O.

5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)

Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa. Kupitia tovuti yako, unaweza kuweka testimonials kwa idadi uitakayo bila kurudia rudia na katika mpangilio maalum na watu wakaweza kuona ushahidi utakaowaridhisha kuendelea kutumia huduma/bidhaa zako. Mara nyingi Mitandao ya kijamii huzuia kuoneka kwa biashara kwa urahisi kutokana na wimbi la watumiaji wenye maudhui tofauti tofauti katika ratiba ya saa (timeline) yako unayopitia katika mitandao hio, hivyo kusababisha usumbufu (distractions) katika biashara yako.

6. UAMINIFU (TRUST)

Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza mahusiano na mteja kama UAMINIFU. Ili kupata wateja wa kudumu katika sekta nyingi, kuwa na tovuti hai ni muhimu katika kudumisha mahusianao katika ya mfanyabiashara kwa muda wowte mteja atakaohitaji.

7. POSITIVE ROI

Ikiwa ni Return On Investment (ROI) au Rejesho baada ya Uwekezaji, unapoendesha biashara ambayo ina gharama zake kama umeme, kodi, maji, mafuta n.k, ukijiuliza utaweza vipi kurudisha gharama hizo upate faida? Njia moja nzuri ni matumizi ya tovuti bora yenye uwezo kunasa wateja wapya kwa njia ya mtandao muda wote (24/7) kirahisi kabisa.

8. THAMANI INAYODUMU

Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote itakapohitajika kufanya hivyo. Hivyo thamani ya biashara yako itaendelea kuwepo muda wote tovuti yako inapokuwa hewani.

9. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA

Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei, ushauri nakadhalika. Hivyo kuimarisha mahusiano na ukaribu wako na wateja wako wakiwa popote duniani kwa urahisi kupitia miundombinu mbalimbali unayoweza kuiweka katika tovuti yako kama matumizi ya chatbots na barua pepe maalum za kibiashara (zenye jina/domain name ya tovuti yako).

10. MASIJALA (DATA CENTER) RAHISI YA MTANDAONI

Tovuti yako inaweza pia kuwa masijala rahisi kwa wafanyakazi, wateja na mtu yeyote anayehitaji kujua taarifa kuhusu huduma/bidhaa unazohusika nazo. Mfano mzuri ni tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz ambayo zaidi tu. ya kwamba inatoa taarifa kuhusu huduma tunazohusika nazo za kutengenza websites, softwares, apps n.k, lakini pia tovuti inatoa taarifa muhimu mbalimbali kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia. Taarifa hizi zimetengenzwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha Biashara za wateja wakiwa popote duniani. Pia taarifa hizo zinalenga kuhamasisha matumizi ya Teknolojia katika njanja mabimbali za kiuchumi haswa kwa wafanyabiashara waliopo kusini mwa jangwa la Sahara.

NOTE: Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa muhimu kama jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.

BONUS POINT: Tovuti yako unapoisajili, unashauriwa pia upate kirurushi cha barua pepe yenye jina/domain name sawa na tovuti yako. Mfano, tovuti yako inapatikana katika anwani ya www.mfano.com, hivyo barua pepe yako ya kiofisi unaweza kuchagua kuwa info@mfano.com au maulizo@mfano.com au jinalako@mfano.com. Kwa kutumia barua pepe zenye jina sawa na anwani ya tovuti yako, unajiweka katika nafasi nzuri ya kuimarisha biashara yako na kuongeza wateja wapya na kazi zenya manufaa haraka zaidi katika biashara/kampuni yako. Hii ni sababu muhimu sana unapojiuliza kwanini ni muhimu kuwa na website (tovuti) rasmi ya biashara yako. Website inakufanya unakuwa official kiukweli kweli.

Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna bora za kuimarisha uchumi wa biashara yako kwa kutumia Teknolojia:

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. BRANDING vs MARKETING, KIPI NI KIPI?
  3. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA (AfCFTA), KUNA MANUFAA GANI KWAKO?
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO.

Umejifunza nini kupitia makala hii ya kuhusu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Tafadhali unaweza kuwasilisha maoni yako kupitia sanduku la maoni (comments box) lililo hapo chini au kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yanayopatikana katika Footer Bar chini kabisa ya ukurasa huu. Pia usisite kuwashirikisha wenzako makala haya kwa kushare link yetu ya https://rednet.co.tz mara zote. Karibu!

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE

Yaani ni 8% tu ya makampuni ndio wana uwezo wa kugundua wizi wa taarifa zao ndani ya dakika chache. 62% wanaweza kugundua wizi ndani ya siku kadhaa. Wewe unatumia muda gani kugundua upotevu/wizi wa data katika kampuni yako? Makala hii tutaangazia mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) kiundani. Leo, yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake. Makinika mpaka mwisho.

Kama Unavyoona biashara zinavyozidi kushamiri kiteknolojia ndivyo wadukuzi nao wanazidi kutafuta mbinu za kufanya mashambilizi zaidi. Mwaka 2019 peke yake, zaidi ya 2$ billion zilipotelea mikononi mwa wadukuzi duniani. Utafiti wa Juniper unaonesha namba hio inaongezeka kila mwaka.

Unalikumbuka shambulizi lilioitwa NotPetya? Basi jarida la WIRED linalitaja shambulizi hilo kama “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA”. Ndani ya masaa machache tu virusi vya shambulio hilo (malwares) viliathiri kutoka biashara ndogo za Software nchini Ukraine mpaka kusambaa katika vifaa vya kielektroniki dunia nzima. Shambulizi lilidhoofisha mashirika makubwa duniani kama FedEx, TNT, Express na Maersk kwa wiki kadhaa na kusababisha hasara ya zaidi ya $10 bilioni kwa ujumla. Upotevu wa data kwa kiwango hiki unaonyesha namna katili ya dunia tuishiyo ambapo inaonekana hakuna mwenye kinga madhubuti mtandaoni. Kutoka Mashirika makubwa, serikali, mitandao ya kijamii, mifumo ya migahawa na sehemu yoyote unayojua inatumia teknolojia ya IT, Kila mmoja yupo hatarini.

TUMEFIKAJE HAPA?

Ripoti ya mwaka 2019 ya shirika la Accenture Security kuhusu Matishio ya kimtandao (Cyber Threatscape), imeonyesha sababu za wadukuzi kuendelea kuwa tishio dhidi ya taarifa binafsi/za mashirika kwa manufaa yao. Hizi ni baadhi sababu hizo:

1. Wadukuzi wa kimtandao hufaidika zaidi na teknolojia mpya na kukosekana mawasiliano madhubuti katika sheria na tawala za maeneo/nchi mbalimbali duniani.

2. Mitandao ya kihalifu muda wote inakwenda ikibadilika, hasa kuelekea katika makundi ya kihalifu ya siri (syndicates) pasi na kujulikana chanzo chake kwa kutumia nyaraka halali kwa nia halifu.

3. Malengo mseto katika kuimarisha tabia za virusi (kama kujiendesha vyenyewe: self replication)

4. Kuimarika kwa mifumo ya Ulinzi wa Kimtandao (cybersecurity hygiene) inapelekea wadukuzi nao wazidi kujiimarisha kimbinu na maarifa katika uwanda wa kiteknolojia na matumizi ya internet.

Baada ya kujua sababu zinazowasukuma Wadukuzi na wahalifu wa Kimtadao kuendelea kufanya mashambulizi, Leo, uta yafahamu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako, Fuatana nami..

Duniani kunazo aina nyingi za mashambulizi ya kimtandao kulingana na sababu nilizozieleza hapo juu kama ifuatavyo:

1. RANSOMWARE ATTACK: Katika shambulio hili, virusi maalum (specific malware) ambavyo hukusanya na kufunga taarifa/kifaa katika mtandao ili kumnyima mtumiaji haki na uwezo wa kufanyia kazi taarifa zake kama kawaida. Haki na uwezo (access) huo humrudia mtumiaji pale tu matakwa ya mdukuzi yatakapotimizwa ambayo mara nyingi huwa ni pesa au rushwa kwa mapana yake.

Saa ingine wadukuzi wanaweza kugoma kurudisha haki za matumizi kwa mhusika hata wanapotimiziwa matakwa yao, hivyo kuongezea hasara kwa kampuni/biashara. Mbaya zaidi, ripoti ya mwaka 2019 ya Uhalifu wa kimtandao inaonyesha kutokea kwa shambulizi hili kila sekunde11 ya mwaka 2021.

2. ADVANCED PERSISTENT THREATS (APT): Shambulizi hili sio la mojakwamoja (passive attack) ambapo mdukuzi anapata access ya computer/mtandao fulani kwa muda mrefu pasi na kujulikana, hivyo kujichotea taarifa na kuzitumia kwa manufaa yake. Aina hii pia huitwa Trojan Horse attack.

3. PHISHING: Je wajua? Mpaka 32% ya wizi wa data husababishwa na shambulizi hili. Hii ni aina ya shambulizi maarufu sana la kijamii (social engineering) ambapo mdukuzi humtegea mtu adownload file lililo na virusi kupitia SMS, email au link na kuingiza virusi katika kifaa chake.

unawezaje kujilinda dhidi ya shambulizi la kimtandao la phishing katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

4. SQL INJECTION: Umeshawahi kuona ile unaingia kwenye website ukakuta haipo ghafla tu, au kwenye system flani unanashangaa kuna mafiles huyaoni bila sababu ya msingi. Sasa kwa kutumia virusi halifu (malicious codes) shambulizi hufanyika katika servers zinazohifadhi taarifa muhimu za watumiaji na kuzifuta, kuziiba au kuzibadili ili kutimiza azma fulani ya wadukuzi na/au genge lao. Mara nyingi shambulio hili hufanyika kwenye servers zinazohifadhi taarifa ghafi za watu au vitu (personal identifiable information: PII) kama namba ya kadi, username and passwords.

5. DDOS ATTACK: Kirefu huitwa Distributed Denial of Services attack ambapo hutokea pale wadukuzi wanapofurika tovuti au kifaa chako kwa either kupunguza au kondoa kabisa utendaji wa kawaida na hivyo kuiacha kampuni/biashara kuhangaika kurejesha performance ya mifumo yake wakati wao (wadukuzi na virusi vyao) wakitumia mwanya huo kuiba na kufanya uhalifu katika mifumo hio iliyoathirika.

6. MAN IN THE MIDDLE (MITM): Hii hutokea pale mdukuzi anapoingilia mawasiliano halali ya kampuni bila ya wao kujua. Pia shambulio hili hufahamika kama eavesdropping pale linapofanyika baina ya mawasiliano binafsi ya simu kati ya mtu na mtu.

Mawasiliano katika MITM hiungiliwa pia kupitia APN za Wi-Fi za uongo (deceptive wifi). Zaidi ya kuingilia mawasiliano, hapa mdukuzi anaweza pia kuwasiliana akitumia utambulisho (ID) ya wahusika pasi na kufahamika mara moja.

7. PASSWORD ATTACK: Licha ya kuwa shambulizi maarufu zaidi duniani, bado kuna watu huangukia mtego wa kuibiwa nywila zao. Kwa urahisi wake, wadukuzi hutumia mbinu zenye viwango na ujanja kupata nywila dhaifu na kufungua accounts za watumiaji kirahisi. Hapa tunaangukia kwenye usalama wa vifaa vyetu vya mtandaoni. Je viko salama kiasi gani? Fuatana na makala hii hapa kufahamu zaidi..

UNAWEZAJE KUZUIA MASHAMBULIZI HAYO?

Katika yetu iliyopita tumeeleza kwa kirefu kuhusu namna ya kujiepusha na mashambulizi ya kimtandao (Cyber attacks), pitia hapa KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?“. Leo pia, tutaona njia zingine za kuendelea kujiimarisha na kuzuia mashambulizi hayo yasiathiri Biashara/Kampuni yako. Mashambulizi mengi niliyoyaelezea leo yanazuilika kwa njia ambazo tayari tulishaziona katka makala zilizopita isipokuwa:

MITM Attack: •Tumia SSL Certificates za (https) katika website yako. Hii ni boresho la http SSL certificate ambayo ni ya zamani na usalama wake mi mdogo.

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

•Tengeneza VPN yako kama ngao ya ziada dhidi ya wi-fi halifu (deceptive wi-fi). Mashambulizi haya katika biashara yako yana madhara makubwa ikiwemo Kupotea kwa Fedha, faida ya biashara, mauzo, matengenezo, Hadhi ya biashara kushuka au kupotea kabisa na madhara ya kisheria.

Hivyo unapaswa kuwa makini na kufuata ushauri wa kitaalamu kuhusu maboresho ya kimtandao (updates & maintenance) ili kuhakikisha unatumia teknolojia ya kisasa zaidi ambayo ni salama huku ikiwa imeambatana na Passwords zako zilizo bora. Utajuaje kama simu/computer yako ikiwa imedukuliwa? Majibu tayari yanapatikana kwenye makala iliyo hapa UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?.

Usalama wa Kimtandao ni jukumu langu. Ni jukumu lako. Ni jukumu letu sote. Tuchukue tahadhari muda wote tuwapo mtandaoni. Basi ni matumaini yangu leo mengi umeyafahamu kuhusu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako. Ukiwa na swali au nyongeza tafadhali tuandikie katika comments hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo? Umejifunza nini katika ku yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake katika biashara/kampuni yako.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Unawezaje kujikinga dhidi ya mashambulizi ya kimtandao katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake