Tag: teknolojia za kisasa

KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?

Hebu fikiria wewe ni mgeni mahali fulani, baada ya kushikwa na njaa unaelekezwa migahawa miwili, mmoja ukiutafuta mtandaoni unaweza kupata taarifa zake mwingine hauna taarifa yoyote mtandaoni. Uelekeo wako utakuwa upande gani? Leo sasa tutakwenda kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako. Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Kuishi katika ulimwengu wa kidijitali, tovuti ni zana muhimu sana katika biashara na masoko ya kidijitali. Cha kushangaza inakadiriwa 35% – 50% ya biashara ndogondogo duniani hazina tovuti zao binafsi, jambo linalozinyima fursa ya kuweka taarifa zao kirahisi mtandaoni na kupata wateja wapya kirahisi.

Kuna wanaosema kuwa matumizi ya Tovuti yanamezwa na uwepo wa mitandao ya kijamii ambayo pia watu wanaweza kuweka na kutangaza biashara zao humo. Ni kweli, aghalabu, kwa kutumia Mitandao ya kijamii hauna uhakika wa kumiliki taarifa na maudhui unayoweka humo muda wote. Watengenezaji ambao pia ni wamiliki wa Mitandao hio wanao uwezo wa kusimamisha/kufuta akaunti au maudhui yako muda wowote ikiwa biashara/maudhui yako yanakwenda kunyume na matakwa na masharti yao.

Vile vile Mitandao ya kijamii unayotumia inaweza kupungua umaarufu au kufilisika muda wowote usioutegemea mfano kuna mitandao ilikua maarufu sana zamani kama Hi5 lakini umaarufu wake kwa sasa umepungua au kupotea kabisa. Hivyo, uwezekano wa kudorora kwa biashara yako kunategemea pia umaarufu wa mtandao wa kijamii unaoutumia, jambo linalichangiwa sana na ujio wa mitandao mipya ya kijamii kama Instagram, Whatsapp na TikTok. Hii kwako unaionaje? Nitaeleza Tofauti katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Tovuti wakati Ujao.

Faida ni nyingi sana za matumizi ya website katika kuimarisha biashara yako kupitia ulimwengu wa Teknolojia. Tayari tumekuandalia makala maalum kupitia link hii hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

Leo hii ntakwambia mambo 10 kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika biashara yako:

1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:

Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu huenda wapi kutafuta vitu kama suppliers, bidhaa na huduma mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi. Injini za matafuto mtandaoni zimekuwa kimbilio namba moja huku GOOGLE Ikiziacha mbali Injini zingine kama Yahoo, Bing na Ask. Maana yake hii ni kwamba kama huna tovuti, jua mauzo yako ni 7% tu ya soko zima ambalo hujui kuwa unalo. Upo apo? Yani unapoteza 93% ya mauzo yako kila siku bila hata wewe mwenyewe kujua.

2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)

Kama una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo. Kwa biashara zenye malengo makubwa kuwa na tovuti huwaweka kwenye nafasi za juu katika kupata tenda na wateja, na huonyesha Uweledi bora katika utendaji wa biashara kuanzia katika muonekano na utendaji wa tovuti. Inakadiriwa 80% ya watu duniani huonyesha kutokua na imani na Biashara ambazo hazina tovuti pale wanapotaka huduma/bidhaa fulani mtandaoni.

3. KUPATIKANA KWA URAHISI

Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi, tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako. Ndivyo ilivyo kwa tovuti ambayo inajieleza kwa kila kitu kama ilivyo tovuti maridhawa ya http://rednet.co.tz . Ile raha ya kupata taarifa, huduma au bidhaa kirahisi kupitia simu yako ya mkononi, hufanya wateja waongezeke maradufu na kusambaza sifa bora kwa uharaka sana katika jamii na katika mitandao ya kijamii hali kadhalika.

Hii huongezwa chumvi ya SEO (Search Engine Optimization) ambayo ni teknolojia iliyowekwa katika Injini za matafuto ya kimtandao inayowasiliana na tovuti yako na kuweka taarifa katika Injini hizo na hivyo kufanya taarifa za tovuti yako kuonekana haraka zaidi katika matafuto. Biashara imerahisishwa sana kupitia SEO kuliko kutumia Mitandao ya kijamii. Kama watu wanakwenda Google kutafuta taarifa, basi fahamu taarifa hizo hupelekwa hapo GOOGLE kwa kutumia teknolojia iitwayo S.E.O. Kufahamu zaidi kuhusu SEO gusa hapa chini

4. TANGAZO LA BURE MUDA WOTE

Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo huduma ya internet inapatikana. Tangazo la bure kabisa hili. Kama tovuti yako ina ubora wa kuvutia zaidi katika muonekano, maudhui na utendaji, basi bila shaka biashara yako ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri sokoni na kupata wateja wengi kila siku. Jiulize hivi, unapofunga ofisi/biashara yako wakati wa jioni kila siku, wateja wapya wanaweza vipi kupata taarifa sahihi muda watakaohitaji?turudi kwenye mada yetu, kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Hii pia inawezeshwa sana na teknolojia ya S.E.O.

5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)

Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa. Kupitia tovuti yako, unaweza kuweka testimonials kwa idadi uitakayo bila kurudia rudia na katika mpangilio maalum na watu wakaweza kuona ushahidi utakaowaridhisha kuendelea kutumia huduma/bidhaa zako. Mara nyingi Mitandao ya kijamii huzuia kuoneka kwa biashara kwa urahisi kutokana na wimbi la watumiaji wenye maudhui tofauti tofauti katika ratiba ya saa (timeline) yako unayopitia katika mitandao hio, hivyo kusababisha usumbufu (distractions) katika biashara yako.

6. UAMINIFU (TRUST)

Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza mahusiano na mteja kama UAMINIFU. Ili kupata wateja wa kudumu katika sekta nyingi, kuwa na tovuti hai ni muhimu katika kudumisha mahusianao katika ya mfanyabiashara kwa muda wowte mteja atakaohitaji.

7. POSITIVE ROI

Ikiwa ni Return On Investment (ROI) au Rejesho baada ya Uwekezaji, unapoendesha biashara ambayo ina gharama zake kama umeme, kodi, maji, mafuta n.k, ukijiuliza utaweza vipi kurudisha gharama hizo upate faida? Njia moja nzuri ni matumizi ya tovuti bora yenye uwezo kunasa wateja wapya kwa njia ya mtandao muda wote (24/7) kirahisi kabisa.

8. THAMANI INAYODUMU

Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote itakapohitajika kufanya hivyo. Hivyo thamani ya biashara yako itaendelea kuwepo muda wote tovuti yako inapokuwa hewani.

9. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA

Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei, ushauri nakadhalika. Hivyo kuimarisha mahusiano na ukaribu wako na wateja wako wakiwa popote duniani kwa urahisi kupitia miundombinu mbalimbali unayoweza kuiweka katika tovuti yako kama matumizi ya chatbots na barua pepe maalum za kibiashara (zenye jina/domain name ya tovuti yako).

10. MASIJALA (DATA CENTER) RAHISI YA MTANDAONI

Tovuti yako inaweza pia kuwa masijala rahisi kwa wafanyakazi, wateja na mtu yeyote anayehitaji kujua taarifa kuhusu huduma/bidhaa unazohusika nazo. Mfano mzuri ni tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz ambayo zaidi tu. ya kwamba inatoa taarifa kuhusu huduma tunazohusika nazo za kutengenza websites, softwares, apps n.k, lakini pia tovuti inatoa taarifa muhimu mbalimbali kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia. Taarifa hizi zimetengenzwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha Biashara za wateja wakiwa popote duniani. Pia taarifa hizo zinalenga kuhamasisha matumizi ya Teknolojia katika njanja mabimbali za kiuchumi haswa kwa wafanyabiashara waliopo kusini mwa jangwa la Sahara.

NOTE: Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa muhimu kama jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.

BONUS POINT: Tovuti yako unapoisajili, unashauriwa pia upate kirurushi cha barua pepe yenye jina/domain name sawa na tovuti yako. Mfano, tovuti yako inapatikana katika anwani ya www.mfano.com, hivyo barua pepe yako ya kiofisi unaweza kuchagua kuwa info@mfano.com au maulizo@mfano.com au jinalako@mfano.com. Kwa kutumia barua pepe zenye jina sawa na anwani ya tovuti yako, unajiweka katika nafasi nzuri ya kuimarisha biashara yako na kuongeza wateja wapya na kazi zenya manufaa haraka zaidi katika biashara/kampuni yako. Hii ni sababu muhimu sana unapojiuliza kwanini ni muhimu kuwa na website (tovuti) rasmi ya biashara yako. Website inakufanya unakuwa official kiukweli kweli.

Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna bora za kuimarisha uchumi wa biashara yako kwa kutumia Teknolojia:

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. BRANDING vs MARKETING, KIPI NI KIPI?
  3. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA (AfCFTA), KUNA MANUFAA GANI KWAKO?
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO.

Umejifunza nini kupitia makala hii ya kuhusu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Tafadhali unaweza kuwasilisha maoni yako kupitia sanduku la maoni (comments box) lililo hapo chini au kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yanayopatikana katika Footer Bar chini kabisa ya ukurasa huu. Pia usisite kuwashirikisha wenzako makala haya kwa kushare link yetu ya https://rednet.co.tz mara zote. Karibu!

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

FAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA HABARI NA BURUDANI

Baada ya zaidi ya miaka 10 tangu vuguvugu la mapinduzi ya kidijitali lilipoanza kushika kasi barani Africa, sekta ya Habari na Burudani ambayo inawavutia vijana wengi zaidi kwa sasa imeingia katika ukurasa mpya ambapo sasa sekta ya habari imekuwa ikiendeshwa kwa msaada wa teknolojia kwa kiasi kikubwa sana. Leo sasa, uta fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani. Kuna nini humo? Makinika mpaka mwisho..

Sekta hii iliyogawanyika kwenye maeneo kama Matumizi ya IntanetiTelevisheni, Sinema, Video Games, MagazetiMajaridaVitabuMuzikiRedio na kadhalika imechagizwa sana na mapinduzi yasiyozuilika ya Intaneti barani Afrika ambapo matumizi ya simu za rununu yamejenga msingi imara kama chanzo cha maboresho, ubunifu na mapato katika sekta hii.

Changamoto; Je, Teknolojia inabadili vipi sekta hii maarufu ya Habari na Burudani barani Africa?

Kwenye makala hii tutagusia changamoto chache zinazosibibu sekta hii maarufu kabisa. Lakini kwa undani zaidi wa changamoto hizo pamoja na jinsi ya kupambana nazo, tips, ofa mbalimbali na ushauri huwa tunashare kupitia status zetu za WhatsApp, utaipata kwa kugusa namba yeu hii hapa 0765834754. Make sure umeisave kisha nitumie text yenye jina lako ili uanze kufaidi elimu ya BURE kabisa.

Makampuni, Wafanyabiashara, Wasanii na Mashirika ya serikali wanatilia mkazo katika kubuni huduma na bidhaa bora kila siku katika kuboresha utendaji wa sekta hii maarufu na inayopendwa zaidi na vijana barani Afrika ambapo tukianzia nchini Kenya sekta hii ilionyesha ukuaji wa 17.0% katika mwaka 2017, ukuaji ukichagizwa na maendeleo makubwa katika eneo la Matumizi ya Intaneti.

Vile vile ongezeko la watu katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) cha 11.6 litaipaisha sekta hii mpaka kufikia pato la dola za Kimarekani bilioni 2.9 kufikia mwaka 2022 kutoka $ 1.7 bilioni zilizorekodiwa mwaka 2017. Karibu wateja wapya milioni 15 wanatarajiwa kuwa mtandaoni ndani ya miaka 4 ijayo, na zaidi kunatarajiwa kuwepo kwa huduma za kasi ya juu za intaneti.

Katika huduma za kifedha; MPESA imerahisisha sana malipo ya bidhaa/huduma mbalimbali nchi kenya na hivyo kufanya sekta ya Habari na Burudani kuzidi kuimarika.

fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

Huduma za Televisheni; Kenya ni moja ya nchi mwanzo barani kufanikiwa kuhamia katika mfumo wa kidijitali ambao umefungua fursa nyingi zikiwemo huduma za televisheni na utengenezwaji wa mawaidha kidijitali. Hali hii imeibua ushindani mkubwa katika eneo hili ambao unazidi kupeleka mbele na kunogesha maendeleo ya sekta hii ya Habari na burudani.

Kwa kuongezea ujio wa makampuni kama Kwese TV na Startimes ambayo hutoza kiwango kidogo zaidi cha malipo ya huduma zao kwa mwezi, kumeongeza ushindani kwa kiasi kikubwa dhidi ya kampuni kongwe ya Multichoice katika utoaji wa maudhui ya televisheni nchini Kenya.

Redio; ongezeko la huduma na vifurushi katika mashirika ya Redio unakuza kwa kiasi kikubwa sekta hii ambavyo hutoa matangazo ya biashara mbalimbali mtandaoni na katika magazeti. Redio nyingi sasa zinalazimika kuhamia katika mtindo wa mobile applications ili kuwafikia watu wengi zaidi na kuongeza wigo wa mapato yao.

TANZANIA:

Sekta hii ya Habari na Burudani inakuwa kwa kasi sana nchini humo ambapo kwa mwaka 2017 sekta hio iliingiza pato la dola za kimarekani milioni 496 ukiwa ni ukuaji wa 28.2% kwa mwaka. Ongezeko la watu kwa kiwango cha CAGR cha 18.3% utashuhudia mapato ya sekta hio kufikia $1.1 bilioni mwaka hadi mwaka 2022 ambayo ni mara 2.3 zaidi kulinganisha na ilivyorekodiwa mwaka 2017.

Kiujumla ni Nigeria peke yake katika Africa ndio imeizidi Tanzania katika kasi ya ukuaji wa sekta hii ya Habari na Burudani. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Kimataifa la PwC. (Wabongo mnatisha kwa habari na bata 😂).

Internet; Kitakwimu kunatagemewa ongezeko la watumiaji wa huduma za 4G ambapo makampuni ya Vodacom na Zantel tayari yalishazindua huduma zao za 4G LTE tangu robo ya pili ya mwaka 2016. Mwaka 2017 TIGO walitangaza uwekezaji wa $70 million ili kutanua wigo wake wa kimtandao na kujiandaa na matumizi ya kasi ya 5G. Hata hivyo mpaka kufikia mwaka 2022, huduma ya kasi ya intaneti ya 3G bado itaendelea kutumika zaidi kufikia takribani 70% ya watumiaji.

Televisheni; matumizi ya huduma za ving’amuzi na televisheni yatapaa kutoka watumiaji 200,000 waliorekodiwa mwaka 2013 mpaka watumiaji 900,000 kufikia mwaka 2022 kwa huduma za televisheni za majumbani. Watumiaji wengi pia hutumia huduma za ving’amuzi kutoka kwa makampuni ya Multichoice na Startimes.

Magazeti; Ukiachana na matumizi ya intaneti yanayoshika kasi nchini Tanzania. Magazeti pia yanaongeza chachu katika uboreshaji wa sekta hii ya habari na burudani ambapo matumizi rasmi ya lugha za Kiswahili na Kiingereza yamekuwa nguzo muhimu.

Lakini kwa Tanzania nyanja ya magazeti inakwenda ikibadilika kwa kasi, kwa mfano kampuni ya Vodacom imebuni application ya M-Paper ambayo imewezesha kupatikana kwa vichwa vya habari vya magazeti maarufu zaidi nchini na hivyo kufanya upatikanaji wa habari kuwa mkubwa zaidi.

Ikiwa na jumla ya mapatoyaliyotokana na matangazo kufikia dola za kimarekani milioni 91 katika mwaka 2017 na kutabiriwa kufikia $128 milioni mwaka 2022, ni dhahiri sekta ya habari na burudani inakuwa sawia nchini humo na hivyo kuchipusha milango mingi ya kibiashara kuendelea kufanyika.

AFRIKA KUSINI:

Ongezeko la watu katika nchi hii linatajwa kuwa imara kwa kiwango cha CAGR cha 7.6% kwa mapato ya watumiaji wa sekta hii ya habari na burudani kufikia mwaka 2022 ambapo mapato yatapaa kutoka Randi 93.9 bilioni zilizorekodiwa mwaka 2017 mpaka kufikia Randi 135.7 biloni mwaka 2022.

Ukiachana na mapato yanayotokana na matumizi ya Intaneti (ambayo huchagizwa na mapato yatokanayo na applications za simujanja) kuna uwanja mkubwa zaidi wa mapato ambayo huongozwa na michezo ya video (video games). Mapato kutoka kwenye michezo hii nchini SouthAfrica yanazidi maeneo mengine kama vitabu, Business-to-business (B2B) na mauzo ya majarida. Ukuaji huu katika eneo la michezo ya Video umekolezwa na ongezeko la matumizi ya simujanja, uboreshwaji wa huduma za kasi ya intaneti kutoka 3G mpaka 4G kuzidi kuongezeka jambo ambalo linaifanya watumiaji wa Afrika Kusini kuwa ni wacheza games 😁.

Televisheni; Kama ilivyotegemewa, huduma za TV na Video zitaendelea kuongoza katika kuzalisha mapato ya watumiaji, lakini muda mchache ujao Kampuni kama Netflix na Amazon Prime huduma zao zitachukuliwa kama nyongeza kunyongea kwa maudhui yao ya burudani katika soko la Afrika Kusini. Vile vile malipo ta TV yataongeza Randi bilioni 6 mpaka kufikia mwaka 2022 kwa kiwango cha 5% ya CAGR japokuwa ukuaji wa mwaka-kwa-mwaka unategemewa kuoungua kwa 2.6%.

Matangazo; nyanja hii iliathiriwa zaidi katika mwaka 2017 na mazingira ya uchumi wa Afrika Kusini ambapo kulikuwa na ukuaji wa tahadhari wa 2.1% tu mwaka kwa mwaka. Hata hivyo, maboresho yanategemewa mpaka kufikia mwaka 2022, ikiwa na 3.3% ya CAGR ambayo itapaisha mapato zaidi.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.Umejifunza nini leo kwenye ku fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

Makala hizi hapa zitakupa taarifa zaidi kuhusu Teknolojia ya Habari na Burudani katika biashara yako:

  1. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BANDO LAKO NI MTAJI
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Karibu sana REDNET TECHNOLOGIES