Tag: technology

this is why you need backlink for your website

This is why you need backlinks for your website to rank higher and perform better on Google search appearances.

These backlinks are the links to your websites that are mentioned/found on other websites/platforms i.e LinkedIn, Facebook, Instagram, Twitter, Bbc, Aljazeera, government websites, and other organizational and private websites. Today we will learn why you need backlinks for your website to rank higher and perform better on Google search appearances. Get to the bottom of this article.

Why Backlinks?

  1. They give your website a higher Domain Authority: This is the status of Influence in Search Engines. The most influential websites/platforms (LinkedIn, Facebook, BBC, Rednet Technologies) have more Domain Authority than less effective websites.
the domain authority for your website

2. They rank higher your website in Search Engines: If your website has 20 quality backlinks, that means, there are 20 attractive links to your websites that were mentioned by other websites/platforms. That means your website will perform better than the one with 10 poor backlinks.

3. They give your website a Unique Identity: Considering the type of keywords you are using on your website, your backlinks will make sure that the website is very unique on Google Search Appearances. i.e If you have mechanical keywords, don’t expect to appear in food searches.

4. They increase traffic to your website; Since Backlinks are the referral points that other websites endorse for your website, it is likely to increase the number of visitors to your website. This is very powerful in doing #SEO intelligently.

5. Increase Customers for your Services/Products; The easy way of getting customers in Digital Infrastructures is through #SEO and specific Backlinks. Considering the previously mentioned advantages, backlinks will increase your customer base gradually but very surely.

How Do You Get Those Backlinks?

After knowing the advantages of Backlinks, you would want to know how to create them so as to get the benefits out of it asap. Here are a few of what you can do.

  1. Add Internal Links; Internal Links are the links that refer to the topic you’re discussing with the previous topics that you already published before in your older posts. These will give enough details to your visitors on different articles just inside your website.
  2. Add Outbound Links; These are the links coming from other websites that support your points in the article. This gives your readers points of reference, and more is very good in #SEO ranking. The outbound links provide citations to your visitors always. You need them.
  3. Ask other publishers to mention the links from your website in their publications. Here you create the links of your articles as Outbound links on other publishers’ websites. If your links appear in other websites’ content, potential referrals are created to rank it higher.
  4. Publish your articles on other platforms like Linkedin, Facebook, and Medium. If your article has more internal links and outbound links it will be great in Google Search Appearances and #SEO.
  5. Make sure the images that you’re using in your articles have “alt text and meta tags” details with the same words as your topic/keyphrases. This will improve the Image Search in #Google. You know how many images are doing fine in impression nowadays!
alt text and meta tags for your website

6. Update your Articles frequently: The new algorithm of google makes recent posts appear higher on search appearances than old posts. Also if you update your post google will count it as a new article. You want to do this.

Tools to consider

After doing everything that you read in today’s article, please do not forget to check how your website is doing in #SEO and Keyword performance. You can use tools like Google Search Console or Jetpack (for WordPress).

If you will get interested in improving your website in terms of building backlinks and doing SEO for it to perform better on Google Search, please contact me to get your website done today.

Also if you will like to send us a tip to motivate us to prepare great content for you, please use the code below.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

Do you have something to ask or comment on? Please share with me here in the comment section or contact me through the following details:

Call/Whatsapp: +255765834754

Email: info@rednet.co.tz

web: https://rednet.co.tz

Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

Unawezaje kutumia Digital Tools ili kuimarisha biashara yako mtandaoni?

Kama huwezi kuendesha biashara yako ukiwa nyumbani au ukiwa safarini nje ya mkoa/nchi, nakushauri, hii 2022 hakikisha unatumia vema Digital Tools utakazojifunza leo katika kuimarisha biashara yako.

FAQ 1: Digital Tools ndio zipi?

ANS: Website, ecommerce store, twitter account, insta page, facebook, Linkedin, Zoom, CH, Whatsapp na Telegram.

FAQ 2: Nawezaje kuzitumia hizo Digital Tools kuimarisha biashara yangu?

ANS: i. BLOG SECTION:

Kwa website, hakikisha ina kipengele cha “Blog” ambapo utaweza kupost Updates mbalimbali kuhusu biashara yako mara kwa mara ili mteja apate solution ya changamoto zinazomkumba mara kwa mara.

ii. Tumia S.E.O:

Kuhakikisha biashara yako inapatikana google ikitokea mtu yeyote aki-search kuhusu huduma unazotoa. Mfano: ikiwa unauza chakula basi hakikisha katika blogs zako unatumia zaidi maneno kama “Wali, ugali, biriani, juisi ya miwa, chakula kitamu, sambusa za nyama nk”

Kwa sababu maneno hayo kitaalam yanaitwa “Keywords” ambayo ni rahisi kwa mtu yeyote kuyaandika akiwa anatafuta sehemu pa kupata huduma nzuri anazohitaji. So hakikisha unayatumia barabara kabisa kuendana na aina ya biashara yako.

iii. GOOGLE MAP:

Ni changamoto sana kwa wajasiriamali wengi. Unakuta eidha mtu hajui kuitumia au basi tu haoni haja ya kuitumia. Leo nataka nikusanue, hii Google Map inawainua sana watu mtandaoni. Kama unafanya biashara/una ofisi, ingia google map, sajili biashara yako chap.

Ingia google kisha andika (Aina ya biashara unayofanya au unayotaka kutafuta) kisha ikifuatiwa na maneno “near me” Mf: web designer near me, au food provider near me, au kitu chochote kama mifano inavyoonekana hapo. Halafu jiulize kwanini biashara yako haipo kwenye hizo listings?

iii. GOOGLE MY BUSINESS:

Katika jukwaa la Google unao uwezo wa kutengeneza wasifu (profile) wa biashara yako ukaweka details zote kama jina la biashara, mahali ilipo, huduma unazotoa au bidhaa unazouza, offers, mawasiliano yako n.k. Hii ndio njia rahisi zaidi ya kufanya S.E.O.

Hizo details unazoweka kwenye Akaunti yako ya Google My Business zinaisaidia sana biashara yako kuonekana kirahisi pale mtu anapotafuta vitu vinavyofanana na huduma unazotoa kupitia Injini za matafuto kama Google na Bing. Jaribu hii leo uone NGUVU ya SEO. Utanishukuru badae.

iv. SEARCH CONSOLE:

Hii ni Dashboard ya Google ambayo inakuonyesha namna website yako inaperform katika matafuto yanayofanyika huko mitandaoni. Kupitia matafuto hayo, google itai-rank website yako kwa mujibu wa inavyotafutwa na watu mbalimbali duniani kote.

Website zinazotembelewa zaidi na watu hutokea katika page ya kwanza kabisa pale mtu anapo-search kuhusu jambo analotaka mtandaoni. Ukiangalia kwa upande wetu, mpaka kufikia tar1/1/, tovuti yako ya https://rednet.co.tz imepata nafasi ya 7.6. Nia ni kufikia nafasi 3 za juu.

v. Katika matumizi ya Social Media kanuni zipo wazi. Hakikisha maudhui unayoweka kuhusu biashara yako 80% ni kuhusu VALUES ambazo biashara yako inampatia mteja, na 20% ikiwa ni kuhusu MATANGAZO ya bidhaa/huduma unazotoa.

vi. WHATSAPP:

Moja kati ya Tools zenye nguvu zaidi katika kuimarisha biashara kwa njia ya mtandao ni kupitia Whatsapp.

WHY WHATSAPP?

Je wajua kuwa watumiaji wa Whatsapp kwa wastani hufungua App hio mara 23 kwa siku, huku zikitumwa meseji milioni 29 kila dakika katika app hio?

Hii inakuhakikishia kwamba ukiitumia vizuri App ya whatsapp unajiweka kwenye nafasi nzuri ya KUSTAWISHA biashara yako kimtandao na kuongeza MAUZO, tena BILA GHARAMA yoyote ile ya kulipia matangazo.

Pia kupitia features za Whatsapp Status, Whatsapp Broadcast, Groups, Videos and Voicenote, sasa kutoa VALUES za biashara yako kwa wateja imekuwa rahisi. Unaweza kutengeneza Funnels hapo, ukabadili watu unaowasiliana nao kutoka WATU WA KAWAIDA kuwa WATEJA wako kirahisi zaidi.

Muhimu, hakikisha unapotumia hii mitandao ya kijamii basi walau uwe unaweka posts/tweet mbili kwa siku, kila siku (consistently).

Mwaka huu 2022, unao uwezo wa kumanage biashara zaidi ya 1 na zote zikaenda kwa ufanisi unaotakiwa kwa kupitia matumizi SAHIHI ya Digital Tools ulizojifunza leo. Usipoteze nafasi yako LEO sasa kufanya hivyo.

Una changamoto yoyote katika kutumia Digital Tools katika kuimarisha biashara yako? Tucheki kupitia DM yetu au Chati nasi Whatsapp kuitia namba 0765834754 ili kusudi tukushauri BURE kabisa namna ya kutatua changamoto hizo haraka iwezekanavyo.

OFA YA MWAKA MPYA 2022:

OFA YA KUPATA WEBSITE YAKO
OFA YA MWAKA MPYA 2022

Tunayo OFA YA MWAKA MPYA 2022 hapa ambapo, Ukitengeneza website kwetu unapata huduma za SEO kwa Google My Business, Search Console na Google Map BURE KABISA. Pia tutakuwa tunakushauri namna nzuri ya kuendesha website yako ili ikuletee faida kila siku.

Changamkia OFA hii kabla haijakwisha kwa sababu “Biashara asubuhi, jioni mahesabu”. OFA inakwisha tarehe 31/01/2022, hivyo wakati unapanga mipango yako ya kufanyia kazi mwaka huu, weka akilini pia namna utakayoweza kufanikiwa katika biashara zako mtandaoni kwasababu nyakati hizi zinakutaka ujifanyie tathmini binafsi kama kampuni inayofanya tathmini mwenendo wake. Weka mipango ya mwaka kisha igawe katika shughuli za miezi mitatu mitatu, fanya kazi kuifanikisha. Mwisho wa mwaka fanya tathmini uone jinsi umefanikiwa katika mwaka wako.

Cheers.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mpesa lipa namba yetu
website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado?

Website zinazotembelewa na watu wengi kila siku zina nini ambacho hujakifahamu bado?

Unaweza kuwa unajiuliza, “Sasa nimeshafungua website na ninazo akaunti za Twitter, Facebook na Instagram, lakini mbona watu hawatembelei tovuti yangu? nakosea wapi?” Leo nataka nikwambie kuhusu website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado? Makinika hapa.

Ukweli ni kwamba hakuna mtu yeyote ambaye hapendi kufanikiwa. Hakuna mfanyabiashara ambaye hapendi kupata Faida kubwa ya kifedha na wateja. Hakuna mtu ambaye hapendi kuingiza PESA.

Ukweli ambao unaweza usiambiwe na Web-Designer unayempa kazi ya kukutengenezea website ya biashara yako ni kwamba:

“Kumiliki Website na akaunti za mitandao ya kijamii (Zana za kimtandao) hakukufanyi kufanikiwa direct katika biashara hasa za mtandaoni”

-Faustine Kimath

Lakini kwanini umiliki hio website yenyewe, ilhali unaweza kutumia mitandao ya kijamii kuendesha biashara yako izuri tu? Majibu yanapatikana ukifuatilia makala hii hapa Kwanini ni Muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako?

Baada ya hapo utagundua pamoja na kuwa na website bado kuna zana nyingi sana za kimtandao (Digital Tools) ambazo unaweza kuzitumia kuwafikia wateja wako sambamba na website yako kama zana kuu. Sasa uzitumie vipi zana hizo ili ile Kiu yako ya kufanikiwa ikapate kutimilika?

Websites za kisasa zinatengenezwa zikiwa ni chanzo muhimu cha taarifa za kuaminika kuhusu Biashara/Kampuni yako. Hivyo website yako inafanya kazi ya kukutambulisha mtandaoni 24/7.

Sasa leo ukimaliza kusoma makala hii kuhusu website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado? Utapata uelewa hata siku ukifungua website yako ufahamu iwekwe vitu gani vitakavyoongeza idadi ya watu wanaoitembelea pamoja na kunasa wateja:

Kipengele namba 8 kitakufungua kichwa sana. Twende mpaka mwisho:

1. UBUNIFU:

Siku zote hakikisha unawapa wateja wako vitu wanavyopenda wao, sio unavyotaka wewe. Hata unapofikiria kubuni tovuti, hakikisha tovuti hio inafanana na aina ya wateja wako. Hivyo fanya utafiti wa kujua wateja unaowalenga ni wa namna gani kwanza.

Duru zinaonyesha 94% ya vitu vinavyomvutia mteja kwa mara ya kwanza kabisa (first impression) ni ubunifu uliotumika kutengeneza website hio. Ubunifu unajumuisha rangi za tovuti, mijongeo ya picha, aina za maneno (fonts) n.k

2. KASI YA KUFUNGUKA:

Kwa kawaida 94% ya watu huchukua si zaidi ya sekunde 5 kusubiri kurasa ya tovuti ifunguke. Baada ya hapo huachana na ukurasa huo na kuendelea na mambo mengine ya mtandaoni. Imagine tovuti yako inachukua zaidi ya sekunde 10 kufunguka sasa. Nani ataitembelea mara ya pili?

3. MATUMIZI YA ANWANI ZA NDANI

Unapokuwa na tovuti yenye anwani za ndani (internal links) za kutosha katika kurasa mbalimbali, unaiweka tovuti yako kwenye nafasi ya kutembelewa mara kwa mara tena na watu wengi zaidi.

Anwani hizi zinarahisisha kupatikana kwa taarifa kwa haraka na wepesi zaidi ndani ya tovuti yako.

Anwani hizo pia hutumika kama maneno ya msingi (keywords) katika injini za matafuto ya kimtandao kama Google. Hivyo mtu anapo-google inakuwa rahisi kupata majibu, bidhaa au/na huduma zinazotolewa kupitia tovuti yako.

4. MAUDHUI YA VIDEO:

Zamani ilikua si rahisi kurusha maudhui ya video mtandaoni na yakawafikia watu wengi kutokana na uduni wa teknolojia. Lakini siku hizi mambo ni tofauti sana. Maudhui ya video yamekuwa yakiwafikia watu wengi zaidi na kwa haraka sana. Angalia namna YouTube inayoshika kasi pale msanii wako unayempenda akiachia wimbo mpya. Siku hizi hata kukiwa na matukio muhimu ya Kitaifa, watu wengi huyafuatilia kupitia YouTube kuliko televisheni za kawaida.

Kwanini? Kwa sababu YouTube inapatikana kwenye smartphone, stesheni za televisheni hazipatikani kirahisi kwenye smartphones, hivyo nyakati hizi ukiwa popote kwenye mihangaiko yako ni rahisi kufuatilia maudhui ya video kupitia simu yako yenye intaneti kuliko wakati mwingine kwenye historia ya mwanadamu.

Maendeleo ya kiteknolojia yamerahisisha sana usambazwaji wa video mtandaoni. Hivyo unapofikiria kufungua/kuiimarisha website yako, hakikisha pia unaweka maudhui ya video ambayo yatawafanya watu wazidi kumiminika na kufaidi thamani ya maudhui hayo kirahisi.

5. MATUMIZI YA BLOGU

Kwa ulimwengu huu, masoko ya bidhaa na huduma yamehamia mtandaoni na hivyo kusababisha ushindani kuwa mkubwa sana ukiongozwa na uwepo wa maudhui mbalimbali yanayopandishwa kila siku.

Hivyo, tovuti yako inapaswa kuwa na kitu kipya kila leo.

Tovuti yenye Blogu ina nafasi ya kufanya vizuri kwa kuwafikia watu wengi na kutembelewa kila siku tofauti na tovuti ambazo hazina sehemu ya Blogu. Kwenye blogu ndipo unapoweza kuweka maudhui ya kuwasaidia wateja wako kufikia malengo yao na kutatua changamoto wanazokutana nazo kila siku kupitia biashara yako. Hapa utagundua kwanini ni muhimu kuwa na website ya biashara yako?

6. MATUMIZI YA PICHA

Je, wajua kwamba picha ndio kiungo rahisi zaidi katika kuhudumia mteja? Zinamfanya mteja kukumbuka kuhusu huduma/bidhaa yako, ni nyepesi na rahisi kutumia. Maudhui yako yakiwa na picha, 65% ya wanaotembelea tovuti yako watakukumbuka hata wakitoka mtandaoni.

Mfano ukiitizama picha hii hapa chini wazo linalokujia haraka ni kwamba sasa ni wakati wa sikukuu ya Christmass, na kwa kuwa umeiona hapa picha hio bila shaka ukiiona sehemu nyinngine utakumbuka tu kwamba “Faustine alishawahi kuipost pia hii picha“. Unaiona nguvu ya picha hapo sasa? Imagine bidhaa zako unazipiga picha kali za kiubunifu na kuziweka kwenye tovuti yako sasa.

website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado?

7. UMUHIMU WA S.E.O

Kama unahitaji mafuriko ya watu yazidi kumiminika katika tovuti yako kila siku, hiki kipengele cha SEO huwezi kukikwepa. Hii ni Teknolojia inayorahisisha matafuto ya mtandaoni na kuelekeza wapi pa kupata majibu na taarifa zaidi.

Imagine google inawaelekeza wateja waje kwako kupata taarifa, huduma na bidhaa muda wote ambao wewe umelala zako, au muda ambao wewe haupo mtandaoni ikiwa tu tovuti yako utakuwa umeiunga na miundombinu ya SEO. Hii S.E.O inahusisha matafuto katika mifumo ya maneno ya msingi (keywords) ambayo unakuwa ukiyatumia mara kwa mara katika tovuti yako na mifumo yako ya utoaji huduma. Hii imekuja kurahisisha sana maisha. Halafu cha ajabu zaidi, ni rahisi sana kuitumia. Ungependa kufahamu zaidi kuhusu SEO? Njoo WhatsApp sasa hivi kwa kugusa namba hii hapa 0765834754

8. UTATUZI WA KERO/CHANGAMOTO:

Jambo muhimu zaidi linalowavuta watu wengi kutembelea tovuti mbalimbali ni Nafasi ya Kutatua kero/changamoto zinazowakabili. Watu hawatembelei tovuti tu ilimradi, wanatafuta suluhu ya kero zinazowakabili kwenya shughuli zako za kila siku. Hivyo, zingatia hilo.

Hapa tunarudi kwenye SEO ambapo huduma hii itakurahisihia solution unazotoa kupitia website yako ziweze kuwafikia wateja wako haraka sana pale wanapozitafuta huko mtandaoni. Katika hili hakikisha website yako ina ukurasa uitwao Maswali yaulizwayo mara nyingi zaidi au Frequently Asked Questions (FAQs).

Je tovuti yako ina maudhui yanayotatua changamoto gani kwa wateja wako. Tuambie kwenye comments.

Unajiuliza utakuwa unatatua changamoto zipi? 1. Chunguza wateja wako uwafahamu wanapitia changamoto zipi, 2. kisha Jifunze namna ya kutoa huduma bora. 3. Fundisha kwa kuandika kutoka kwa wataalam wa copywriting. Rudia no.1.

-Faustine Kimath

9. MATUMIZI YA FOMU ZA MAULIZO:

Kama unataka tovuti yako ivutie watu wengi zaidi basi moja kati ya SIRI muhimu ni kuweka “fomu ya maulizo” ambayo inampa mtu yeyote anayetembelea tovuti yako nafasi ya kuuliza chochote kuhusu huduma/bidhaa zako. Muhimu sana hii, na siri ya kufanikiwa katika hili ni kuitengeneza fomu yako iwe fupi na ya kufurahisha (yani inatakiwa mtu akiiona tu ajisemee “loh, hebu niulize kuhusu … hapa chap“).

Fomu hii ni kipengele kinachoweza kuwabadili watembeleaji (visitors) kuwa wateja haraka sana.

10. HUDUMA KWA WATEJA:

Hata kama ukiyafanya yote uliyojifunza leo hapa kwanzia 1-9 lakini ukawa huna huduma nzuri kwa wateja wako na watu wanaotembelea tovuti yako na kuuliza maswali kwa lengo la ufafanuzi, ndugu, bado safari ya mafanikio itakuwa ndefu kwako.

Huduma kwa wateja inajumuisha namna unawasikiliza wateja wako, namna unavyojibizana nao (kwa maandishi au kwa sauti), muda unaotumia kuhudumia wateja wako na namna unavyoweza kuhimili hasira na mtazamo hasi kutoka kwa wateja na watu mbalimbali.

thamani vs gharama, nafuu iko wapi? fahamu siri za kuweza kushawishi wateja katika biashara yako.

website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado?
Thamani vs Gharama: Nafuu iko wapi?

Vyote hivyo vinachangia kuongeza au kupunguza idadi ya watu wanaotembelea tovuti yako kwasababu takwimu zinaonyesha 95% ya wateja husambaza maneno kuhusu huduma mbovu walizopata na 89% kati yao huacha kabisa kufanya kazi na yule aliyetoa huduma mbovu zaidi unaweza kupitia makala hii hapa Umuhimu wa Takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa Wateja.

Tovuti ni sehemu muhimu sana katika kuhudumia wateja wa biashara yako pamoja na kujitangaza hasa katika zama hizi za kidijitali.

Huna haja ya kusambaza CV na makaratasi. Tunza mazingira kwa kupunguza matumizi ya karatasi ambazo zinatokana na ukataji wa miti.

ZIADA: Hata ukisema uyafanye hayo yote 10 ambayo umeyaona kwenye makala hii ya leo, bado nature itakudai kitu kimoja cha muhimu zaidi. Nacho ni muendelezo (consistency) katika utendaji wako wa kusimamia biashara katika mazingira yote, mtandaoni na ana kwa ana. Fahamu kuwa hakuna mafanikio ya ghafla au mafanikio ya bahati mbaya. Yeyote unayemwona amefanikiwa (hata kwa bahati nasibu), lazima alistruggle kutengeneza mfumo mzuri wa kiutendaji ili kumsaidia katika kusimamia biashara yake katika viwango vinayotakiwa.

Umejifunza nini kwenye makala hii ya leo kuhusu website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado? Tuambie kwenye comments hapa chini. Pia hakikisha una-share makala hii pamoja na watu wako wa karibu ili kusudi somo hili liwafikie watu wengi zaidi.

website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado?
mpesa lipa namba yetu
thamani vs gharama, nafuu iko wapi? fahamu siri za kuweza kushawishi wateja katika biashara yako.

THAMANI vs GHARAMA, NAFUU IKO WAPI?

Ubora wa kazi una thamani kubwa sana kuliko gharama za kuifanya kazi hio. Unaweza lipia mradi kwa milioni 5, lakini usikupe matokeo yale ulijipangia mwanzoni. Pia unaweza lipa laki 5 ya mradi na ukapata matokeo mazuri zaidi. Ufanyeje? Je kati ya thamani vs gharama nafuu iko wapi? Fuatilia makala hii mpaka mwisho kufahamu zaidi.

Warren Buffet ambaye ni mbuji kabisa katika buruji la uwekezaji duniani amewahi kunukuliwa akisema “Price is what you pay, value is what you get.” akimaanisha, “Gharama ndio unayolipa, thamani ndio unayopata”. Kifupi ni kwamba thamani ndio msingi wa bidhaa/huduma huku gharama ikiwa ni makubaliano ambayo yanatangulizwa na muuzaji.

Kujua tofauti kati ya Gharama na Thamani ni moja kati ya mbinu bora zaidi za kufanya Uwekezaji. Zaidi kuhusu uwekezaji tayari tumeshakufahamisha SIRI ZA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA Ukishazifahamu hapo tuendelee..

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

umuhimu wa tehama

jinsi ya kufanikiwa katika biashara za mtandaoni

Unaposhindwa kutofautisha kati ya Gharama na Thamani kama mfanyabishara unajiweka kwenye mtego wa kukosa wateja, kutoaminika kwa Wawekezaji wakubwa, Kupoteza points dhidi ya washindani wako kibiashara na mwisho kuiweka biashara yako katika majanga ya kudhoofika na hatimaye kufa.

Unawezaje kupata bidhaa zinazouzwa kwa gharama za chini kuliko thamani yake halisi?

Jibu ni kufanya tathmini kwa kutumia viwango vya bei ambazo ni tofauti kabisa na gharama zinazotangazwa sasa. Hapa unaweza kuangalia bei, miaka 3 iliyopita ilikuaje na miaka 3 ijayo itakuwaje.

Bwana Phil Town, ameweka zoezi la kufanya Tathmini makini kwa kupitia hatua nne alizoziita “Four M’s“. Tuzione chap chap:

1. MEANING: Hatua ya kwanza kabla hujawekeza katika bidhaa/huduma fulani lazima ujiridhishe kuwa bidhaa/huduma hio ina maana sana kwako. Ikiwa na maana utapata fursa ya kuichunguza na kuielewa vyema, na kujituma ipasavyo katika kufanya biashara hio.

2. MOAT: (Upekee ambao hauwezi kuigwa na wengine): Unapochagua bishara ya kuwekeza ama bidhaa/huduma, unatakiwa uifanye iwe katika mtindo ambao washindani wako hawawezi kukuiga. Mfano: Duniani kuna makampuni mengi tu ya vinywaji laini (soft drinks) lakini Coca cola ni moja na itaendelea kubaki hivyo.

Hivyo hebu tuambie hapa biashara yako ina utofauti gani ambao washindani wako hawawezi kuiga kamwe?

3. MANAGEMENT: Je wajua kuwa Chanzo kikubwa kwa biashara kufa ni watu wanaoiendesha? Hivyo unapofikiria kuwekeza kwenye biashara lazima eneo ya utawala na uendeshaji wa shughuli linasimamiwa na watu wenye Weledi, Waaminifu na wanaojali maisha ya biashara hio.

4. MARGIN OF SAFETY: Kama umeshajiridhisha na hizo hatua 3 zilizopita, sasa hebu tizama pia namna unaweza kuweka mtaji ama kununua hisa bila kupoteza pesa na uhakika wa pesa yako kurudi.

Kila biashara inahitaji kitu fulani ambacho kitaitofautisha na washindani wake wengine sokoni. Sasa mchakato wa kutafuta tofauti hizo inaitwa “Positioning”. Hii mbinu inaziwezesha biashara kukazia sehemu fulani ya soko/wateja ili kujiimarisha zaidi kwenye sehemu hio. Unafanyaje?

MBINU ZA KUFANYA POSITIONING:

1. KUPUNGUZA GHARAMA: Ukifanya uchunguzi vizuri sokoni hasa kwenye mitaa ambayo wanafanya biashara ya aina moja mf: Kariakoo kila mtaa una shughuli yake maarufu zaidi kama mtaa wa livingstone ni maarufu kwa vyombo vya ndani.

So ukijigundua kuwa upo kwenye aina hii ya biashara, mbinu bora hapo ni kupunguza gharama za bidhaa zako kwa kiwango kidogo kuliko washindani wako. Lengo ni kuhakikisha unakuwa na mzunguko wa haraka wa mauzo ya bidhaa/huduma zako kwa faida ndogo ili mzigo wako uishe mapema.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

2. UBORA: Kama unataka kujitofautisha na washindani wako, basi mbinu bora na ya kuaminika ni kuhakikisha bidhaa/huduma zako ni za Ubora wa hali ya juu. Unapozingatia Ubora unajiweka kwenye nafasi ya kupata wateja wa kuaminika, wateja wa kudumu na wateja wa uhakika katika biashara.

3. MAKUNDI YA KIJAMII (DEMORGRAPHIC): Baadhi ya biashara huamua kujihusisha na makundi fulani tu ya kijamii ili kujiletea faida zaidi. Mfano: kwenye TV na redio vinatengenezwa vipindi mahsusi kwa Vijana, watu wa makamu na watu wa dini fulani kwa siku zao. Umeshawahi fanya hii?

Mbinu hii inafaa sana pale unapoyapata makundi hayo karibu na eneo lako la biashara au watu wanaokufuatilia zaidi mtandaoni wakawa ni wanamna hio. Vinginevyo unajiweka kwenye hatari ya kukosa soko kubwa nje ya hao uliolenga kuwahudumia.

4. HUDUMA BORA: Huwa inatokea kwa baadhi ya biashara ushindani unakuwa mkubwa sana kiasi kwamba mbinu 3 tulizoziona awali haziwezi kufanya kazi. Yani watu wanashikana kooni haswa. Hapa ndipo mbinu ya kutoa Huduma Bora kwa wateja inapokuja kuleta tofauti.

Zoezi la kutoa Huduma Bora ni pana na linahitaji ubunifu mwingi. Na hii inatoa fursa kwa biashara kubuni namna nzuri ya kuhudumia wateja wake ili kuhakikisha wateja wanafurahia bidhaa/huduma na kuzidisha mauzo. Mfano: unaweza kuanzisha dawati la wateja kutoa maoni live ili waweze kuona mawazo yao yakifanyiwa kazi. Unaweza kuanzisha kurasa za mitandao ya kijamii ili kukusanya kero za wateja na kuzifanyia kazi vizuri. Pia unaweza kutengeneza mzunguko kwa wateja wako kushiriki kama mabalozi wa kuitangaza biashara yako kwa watu wengine. Unaionaje hii?

UNAWEZA VIPI KUDADAVUA NA KUWASILISHA THAMANI YA BIASHARA YAKO KWA MTEJA WAKO?

Tafiti zinaonyesha kuwa watu hawapendi kabisa kutangaziwa ama kulazimishwa kununua kitu hasa huku mtandaoni. Mfano: Tizama unavyopata kero pale unapoangalia vidio YouTube mara katikat linakuja Tangazo Ama pale unataka kufungua ukurasa fulani mara unafunguka ukurasa wa tangazo kwanza kabla hujafika pale ulitaka kwenda. Hio kero ndio inatakiwa ikufanye uitazame biashara yako katika jicho la Kitaalamu kwa kutatua changamoto na si la Kibiashara kwa kuuza Bidhaa/huduma yako.

Unapotoa Elimu katika namna ya Utaalam wa kutatua changamoto fulani, unamfanya mteja atake kuondokana na kero zinazomsumbua kwa kutumia Bidhaa/Huduma zako. Hii ni tofauti kabisa pale unapotaka kuuza bidhaa. Ukifanya hivyo hutatui changamoto bali unakuwa kero kwa mteja.

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

gharama vs thamani, kipi kinafaa zaidi?

Thamani ya Biashara yako inaonekana katika kutatua changamoto za mteja wako na Urahisi wa kutumia bidhaa/huduma yako. Hivyo lazima uhakikishe kuwa unachokitangaza ni Ile Namna na hisia ya Bidhaa zako zinaweza kutatua changamoto fulani ya mteja kwa urahisi.

Pia lazima uhakikishe suluhu yako inakwenda sambamba na hisia za mteja wako. Kwa kuwa kitaalam watu hununua bidhaa/huduma kutokana na hisia walizo nazo muda huo. Mfano kuna watu watakwambia kuwa wakiwa na hasira ama furaha sana kwao huo ndo muda wanafanya shopping kubwa zaidi.

Mzazi anapotaka kununua keki ya birthday ya mwanae hanunui tu keki tamu, lazima pia ahakikishe keki hio inakwenda kum-suprise mtoto kwa muonekano wake wa kuvutia. Ni mbinu ya kihisia hapo inatumika. Hivyo unapotaka kuongeza Thamani ya biashara yako unatakiwa kuzingatia hilo pia.

Umejifunza nini kwenye makala hii kuhusu thamani vs gharama, nafuu iko wapi? Tafadhali weka maoni au mtazamo wako katika sehemu ya comments hapo chini..

Vyanzo: https://www.forbes.com/sites/forbesfinancecouncil/2018/01/04/the-important-differences-between-price-and-value/?sh=133fd5c94237

https://www.weebly.com/inspiration/difference-between-value-and-cost/

https://yourbusiness.azcentral.com/different-types-strategies-business-1348.html

IFAHAMU TEKNOLOJIA YA QR-CODE KATIKA BIASHARA YAKO

Kwa kasi ya maendeleo ya kiteknolojia inavyozidi kuchanja mbuga, watu wanatumia sana simu janja kwa matumizi mengi zaidi ukiacha kupiga simu na kutuma ujumbe. Uwezo wa kununua bidhaa na kupata huduma haraka umewezeshwa zaidi kupitia ujio wa QR-Codes. Sasa leo ifahamu teknolojia ya QR-Code katika biashara yako. Makinika.

Hizi QR (Quick Response) codes zinaweza kusomwa na kudadavuliwa vyema kwa kutumia Simu janja na vifaa maalum vya kielektroniki (QR-scanners) na hivyo kujenga wepesi kwa watu wa masoko kuingiza maelezo kuhusu majukwaa yao kupitia hizi QR Codes. Yani maisha ya kibiashara yamekuwa mepesi kweli.

QR-codes hizi huweza kuwekwa katika mabango, magazeti, kurasa za tovuti na vyombo vingine vya kimasoko ili kurahisisha usambazaji wa bidhaa na huduma kwa haraka na wepesi zaidi. Matumizi ya QR-Codes yamekuwa yakizidi kutanuka kila uchwao ambapo katika kipindi cha mwaka 2018/19 peke yake, matumizi ya QR Codes duniani yaliongezeka kwa 28% huku ongezeko la muingiliano katika kipindi hicho likikuwa kwa 26% (chanzo: akaunti ya Blue Bite, mtandao wa medium).

QR CODES ZINA TOFAUTI GANI NA BARCODES?

Japokuwa Barcodes zilianzishwa miongo mingi kabla, QR Codes zimekuja na mapinduzi makubwa ndani ya muda mfupi.

1. Kama ulishawahi kununua bidhaa ya kiwandani hasa zile zinazouzwa katika supermarkets, utagundua bidhaa hizo zina alama fulani za vimistari pamoja na namba. Alama hizo ndio huitwa BARCODES. Sasa hizo Barcodes hutumika kuhifadhi maelezo muhimu kuhusu bidhaa husika kama jina la bidhaa, mtengenezaji, bei, kiwango cha ubora n.k. QR Codes kwa upande wake hufanya kazi sawa sawa na hizo Barcodes, isipokuwa tu katika QR Codes, zina uwezo wa kuhifadhiwa data nyingi kwa mamia zaidi katika nafasi ndogo.

2. MUONEKANO: Hii ndio tofauti kubwa katika ya hizi teknolojia mbili. Kwa kutizama tu unaweza kujua ipi ni QR Code na Ipi ni Barcode. Hebu tizama mifano hii hapa chini.

ifahamu teknolojia ya QR-Code katika biashara yako. Makinika.

3. UWEZO WA KUJISAHIHISHA: Kwa utofauti huu, QR Code inakuwa bora zaidi kuliko Barcode na kujitofautisha katika viwango vya matumizi. Muonekano wa QR Code unaifanya iweze kutoa taarifa kuhusu bidhaa/huduma vizuri hata kama ikitokea sehemu za alama hazionekani vizuri au zimechanika tofauti na Barcode ambapo ukifutika mstari mmoja tu Barcode inashindwa kutoa maelezo kamili kuhusu bidhaa/huduma.

QR CODES HUTUMIKA WAPI NA WAPI?

Kimsingi QR Codes hutumika katika kuhamasisha muingiliano katika ya mteja na huduma kupitia alama za kielektroniki kwa uharaka zaidi kwa kutumia simu janja au QR-Code scanners. Hii ni mbinu bora sana ya kimasoko katika kurahisisha utoaji huduma na uwezeshaji wa malipo/miamala ya kifedha. Sasa tuone maeneo ambayo QR Codes zinatumika:

1. KUELEKEZA WATUMIAJI KATIKA KURASA/TOVUTI:

Unaposcan QR Code, inaweza kukuelekeza katika kurasa fulani maalum au tovuti ambayo maelezo yake yamefichwa katika CODE hio. Zoezi hili unaweza kulifanya kwa wepesi kupitia QRCode iliyopo kwenye tangazo hili ambayo itakuelekeza katika fomu maalum ya kujiandikisha kuhudhuria mafunzo yanayojieleza.

2. KUPIGA SIMU NA KUPATA MAWASILIANO:

Katika mikutano ya kibiashara mara nyingi watu hukutana na kubadilishana mawasiliano kwa wingi. Lakini zoezi hilo hufanywa jepesi kwa kutumia QR Code ambapo kitendo cha kuscan tu hukuwezesha kupata mawasiliano yote muhimu kuhusu mtu fulani.

Kinachofanyika ni kujaza taarifa muhimu katika QR Code kisha CODE hio hupachikwa katika Business Card mara nyingi. Hivyo unaposcan unapata mawasiliano yote pasi na kuhangaika kuandika namba moja moja katika simu yako.

simu za michongo Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

3. KUPAKUWA APPS MTANDAONI:

Unaposcan QRCode katika masijala za Aplikesheni za mitandaoni, basi unakuwa na uwezo wa kupakuwa App husika kirahisi bila ya kuhangaika kutafuta App hio mitandaoni. Unapoikuta QR Code wewe scan tu, mambo mengine yatajiendeleza yenyewe kirahisi.

4. KUJUA MAHALI BIASHARA ILIPO:

Naam, kupitia ramani za kimtandao kama Google Map, mtumiaji anaweza kuscan QR Code ya biashara na mara hio akaweza kuona mpaka mahali/location biashara hio ilipo. NOTE: Location hio lazima iingizwe kwanza katika QR Code na mfanyabiashara husika.

5. KUFANYA MANUNUZI NA MALIPO:

Pengine hii ndio njia maarufu zaidi ambayo QR Code hutumika. Makampuni ya huduma za mitandao yameingiza na kuboresha sana njia hii katika kufanya manunuzi na malipo. Mara nyingi wafanyabiashara hutumia njia hii katika kutoa punguzo la bei au kufanya matangazo (promo) kwa bidhaa/huduma fulani. Ni mwendo wa kuscan tu na malipo yako unakuwa umekamilika mara hio. Unachotakiwa kufanya kama mfanyabiashara ni kuhakikisha QR Code yako inafanya kazi ile uliyoiamuru (Call-To-Action). Mtumiaji hatakiwi ajiulize afanye nini baada ya kuscan hio code.

HIZI QR CODES ZINAFANYA KAZI VIPI?

Ili uweze kutengeneza au kutumia QR Code ukiiona mahali unatakiwa kuwa na vitu vifuatavyo:

>QR Code Generator: Kuna majukwaa mengi sana mtandaoni ambayo unaweza kuyatumia kutengenza QR Code kwa matumizi yako unavyotaka. Baadhi ya majukwaa hayo Ni pamoja na http://qrcode-monkey.com na http://the-qrcode-generator.com . Katika majukwaa haya unaweza kutengeneza QR Code yako, ukaweza na maelezo kama namba ya simu, tovuti, location nakadhalika. Lakini pia yapo majukwaa ambayo unalazimika kulipia ili uweze kutengeneza QR Code yako.

Majukwaa hayo ni pamoja na KAYWA na ni salama zaidi pale unapotaka kutengeneza QR Code ambayo ni mahsusi kwa ajili ya kurahisisha malipo yoyote. Vya bure vina madhara sana hasa katika maswala ya kifedha. Kuwa makini hapo.

>QR Code Readers: Hizi ni Apps ambazo unazipata katika simu yako mahsusi kwa ajili ya kutambua QR Code na kukupeleka kule kunapotakiwa kwenda. Kwa watumiaji wa iPhone unaweza kupakuwa App inaitwa i-nigma ambayo inatajwa kama App bora zaidi duniani katika kuscan hizi QR Codes. Kwa watumiaji wa Android unaweza kupakuwa App iitwayo Barcode Scanner (watumiaji wa tekno nao wamo hapa.)

KWANINI UTUMIE QR CODE KATIKA BIASHARA YAKO LEO?

Mwaka 2019 matumizi ya QR Code katika kufanya malipo ya bidhaa na huduma yalipata umaarufu mkubwa sana duniani huku makampuni makubwa kama Mastercard na Paypal yakithibitisha matumizi katika kutambua account za wateja na kuidhinisha malipo.

Tafiti zinaonyesha kuwa wateja wanaolipia kwa kutumia QR Code hufanya manunuzi makubwa zaidi. Sasa leo hizi ndizo sababu zitakufanya ifahamu teknolojia ya QR-Code katika biashara yako. Mwaka 2013 Adobe mobile consumer uliowahusisha wstumiaji wa simu 3,075 ulionesha majibu haya;

•46% ya wateja waliscan ili kupata discount

•42% walitumia QR Code kama tiketi

•67% walishuhudia huduma za QR Code katika maduka ya mtaani.

Mpaka kufikia mwaka 2020 takwimu hizo zinatajwa kuongezeka maradufu zaidi. Lengo kuu hapa ni kuhakikisha QR Codes zinasaidia wateja kufanya shughuli zao kwa wepesi zaidi.

Makala hizi hapa chini zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana ukizipitia zote. Gusa link kisha makinika:

  1. FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA DUNIANI
  2. UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA
  3. UGUNDUZI WA KITEKNOLOJIA KUELEKEA KATIKA MUSTAKABALI WA SEKTA YA UZALISHAJI MALI

Umejifunza nini kwenye makala ya leo katika ku ifahamu teknolojia ya QR-Code katika biashara yako. Tafadhali toa maoni yako na sambaza hii kwa jirani yako.