Tag: tanzania

simu za michongo Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

FAIDA ZA KUTUMIA GOOGLE KAMA JUKWAA LA BIASHARA YAKO

Je, unaamini kwamba matumizi sahihi ya huduma za internet na mitandao ya kijamii yana uwezo wa kukurahisishia huduma/bidhaa zako zikapatikana kirahisi na wateja wako wakiwa popote duniani? Leo nataka nikupe stori kuhusu Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Tizama hapa, Siku moja asubuhi kabisa ya mwezi April mwaka huu 2022 nikiwa natoka home naelekea ofisini nikapigiwa simu, kutizama ni namba ngeni, nikatafuta utulivu kisha nikapokea;

Mimi: Hello, Habari za asubuhi!

Jamaa: Salama Faustine, I hope uko poa, Bwana mimi ni fulani (jina kapuni) nimekupigia kwa sababu nahitaji website na ningependa ifanywe na kijana mzawa. Nafanya kazi katika shirika (jina kapuni) ambalo ni la kimataifa. Nilikua napitia google pale nikaona kampuni yenu ya Rednet Technologies na nikaona pia kumbe mnajishughulisha na haya mambo. Itawezekana si ndio?

Mimi: Bila shaka hilo linawezekana kabisa, unahitaji lini hii kazi yako iwe imekwisha?

Jamaa: Well, ndani ya wiki 3 ningependa iwe imekwisha, sasa nitampatia namba yako mwenzangu yupo pale ofisini kwetu, yeye sasa atakupa maelezo ya kina. Lakini naomba kujua bei itakuwaje hapo (huku anacheka kwa ufupi)

Mimi: Gharama nitataja nikishajua requirements kaka, wala usiwe na shaka.

Baada ya kuwasiliana na huyo mwenzake akanirudia…

Jamaa: Faustine, naona mmeshaelewana, Sasa the reason tumekuja kwako ni kwasababu kuna mtu tulimpaga kazi ya kutengeneza hii website yetu, lakini hajawahi kutupa ushirikiano, kazi hajamaliza, changes hataki kufanya na tukimpigia simu harespond ndani ya muda, yani ana kiburi sana yule jamaa, kusema ukweli TUMEMCHOKA.

Mimi: (Kiukweli nilijiskia vibaya sana, ndugu zangu ule msemo wa “Mteja ni Mfalme” una maana kubwa sana hapa. Nikamwambia) Kaka, pole sana, utakavyokuwa unafanya kazi kwetu nakuahidi hio kadhia hutakutana nayo.

Jamaa: Kweli? Ok, turudi kwenye bei sasa, utatuchaji kiasi gani?

Mimi: Kwa nature ya Organization yenu hapo mpaka kazi inakamilika itacost 850,000/- tu.

Jamaa: Faustine, mbona bei ipo juu sana, tutaweza kufanya kazi kweli?

Mimi: Kaka, bei iko fair sana hio ukizingatia tutawatengenezea pia business emails BURE na kuwafanyia maintenance BURE kwa mwaka mzima. Anytime hapo mkitaka kufanya changes, tutazifanya BURE kabisa. Hapo unasemaje?

Jamaa: Hapo sio mbaya, walau naona dalili hautakuwa kama jamaa wa mwanzo. Ila bei bado hujashusha..

Mimi: Kaka, lipia 400k leo, baadae utalipa 250k, then finally tutakapomaliza kazi, utalipia 200k ambayo itakuwa imebaki. Hapo je?

Jamaa: Ok, Nataka na hio website pia iwe inapatikana mtu akisearch Google, ili wateja watupate kama sisi tulivyokupata wewe.

Mimi: Ahaa, hio sasa ni huduma nyingine, inaitwa Search Engine Optimization (SEO). Ndo inaiwezesha website kupatikana google.

Jamaa: Na hio utatuchaji au bei yake ndio inakuja na ya website direct?

Mimi: Hio gharama yake ni tofauti kaka.

Jamaa: Ambayo ni ngapi? Usinilalie bwana ndugu yangu.

Mimi: Hio kwa sababu ni kazi ya muendelezo, utakuwa unalipia kila mwezi, ambapo gharama yake ni 100,000/- tu.

Jamaa: sema Faustine mna bei nyie. Ehe niambie, kwenye hio laki 1 mtakuwa mnafanya nini na nini?

Mimi: Hapo tutakuwa tunakuandikia makala (blog posts) mbili kwa mwezi ambazo zitahusu shughuli mnazofanya, tutaweka picha, pamoja na kuzioptimize ili iwe rahisi kupatikana google mtu akiwa anatafuta taarifa zinazowahusu.

Jamaa: Faustine, hapo umeniweza. Basi wacha tuandae contract, halafu next week tutakuita ili tusign, kazi ianze mara moja. Ila usiniangushe bwana.

Mimi: Kaka wala usiwaze, tufanye kazi.

Basi Bwana baada ya simu hio ndio uhusiano ukajengwa na kazi ikaanza kama hivyo.

Na baada ya kazi hio kuisha, jamaa yetu aliweza kutuunganisha kwa watu wengine watano (5) ambao walitamani kupata huduma kama ambayo aliipata kutoka kwetu. Na hatimaye wamekuwa wateja wetu wa kudumu. Unadhani hao walivutiwa na nini? Fuatilia makala hii hapa kufahamu siri za utoaji huduma bora kwa wateja.

Unachoweza kujifunza ili uweze kuzipata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Katika mazingira ya kazi, hasa huku mtandaoni ambapo mara nyingi tunakutana na watu tusiowafahamu (strangers) ni muhimu sana kuzingatia haya yafuatayo;

1. KAULI NJEMA

2. UAMINIFU

3. KUMJALI MTEJA na MAUMIVU YAKE (Mara kwa mara muulize kama anaridhika na huduma anazopata kutoka kwako na nini unaweza kufanya ili kazi yake ifanyike kwa ubora anaotarajia).

Kauli Njema zitakufunulia fursa nyingi na kukuletea wateja wengi sana huku mtandaoni, acha tabia ya kutukana, kudhalilisha au/na kudharau watu. Kumbuka teknolojia haisahau.

Uaminifu utajenga uhusiano mzuri na wa kudumu na mteja wako.

Kumjali mteja kutafanya azidi kukupa kazi nyingi zaidi mbeleni, na hata kukuunganisha kwa watu wake wengine anaowafahamu.

Siri ya kufanya kazi vizuri na mteja ipo kwenye hayo mambo matatu. Ukiyazingatia, hakika huwezi kufeli. Zaidi kama unahisi bado hujajua namna unaweza kushawishi mteja kwenye biashara yako fuatana na makala hii hapa tumekuandalia.

HABARI NJEMA KUELEKEA MSIMU WA SIKUKUU

Sasa kuelekea mwisho wa Mwaka tunakupa ZAWADI ya kuifikisha biashara yako mtandaoni na kukusanya wateja kutoka kila pembe ya nchi. Fungua website leo kwa 500,000/- tu (badala ya 850,000/-) upate na huduma ya SEO BURE (badala ya 100,000/- kwa mwezi) maintenance BURE mwaka mzima pamoja na Ushauri BURE kabisa. Hata hivyo, ZAWADI hii haitamfikia kila mtu. Zawadi hii ni kwa watu 10 tu wa mwanzo, na itadumu mpaka tar 10 December. Baada ya hapo tunakwenda likizo ya Christmas.. So kama unahitaji ZAWADI hii WAHI nafasi mapema ili pia uzipate Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

OFA ya Msimu wa Sikukuu 2022
Sherehe za Christmas na Mwaka Mpya Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Baada ya OFA hii ukihitaji website ni 850,000/-, huduma ya SEO ni 100,000/- kwa mwezi na pia tutafungua group la Whatsapp kwa yeyote atakayehitaji ushauri au atayehitaji kuuliza jambo lolote kuhusu Website, SEO, Social Media Marketing, Digital Marketing na Tech kwa ujumla wake. Kuingia kwenye group hilo itakugharimu 5,000/- tu kwa mwezi.

So ukiliona Tangazo hili, mtaarifu na mwenzako ambaye unahisi atahitaji kunufaika na ZAWADI hii.

Wewe kama unafanya biashara, basi kama unataka kufanya vizuri sokoni, hakikisha unajenga URAFIKI na wateja wako. Hii ni kwa sababu ni rahisi sana MTEJA kuwa RAFIKI yako kama utatengeneza UHUSIANO mzuri kati yenu. Hii ndio SIRI ambayo hakuna mtu atakwambia kirahisi.

Kufanya biashara mtandaoni ni Uwekezaji muhimu sana, na kwa maendeleo yaliyopo kwa sasa duniani, imekuwa ni rahisi mno kutumia huduma za Internet katika kuwafikia wateja popote walipo duniani.

Kuna mtu aliwahi kuniuliza, “Sasa nawezaje kutumia Internet kufanya biashara yangu?”

Jibu: Unaweza fanya haya yafuatayo ili uweze kupata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.:

1. Tumia Website na mitandao ya kijamii kutoa elimu kuhusu bidhaa/huduma zako.

2. Tumia SEO ili kurahisisha maudhui yako yanapatikana kirahisi katika Google.

3. Fanya matangazo (Paid Ads/Sponsored Ads) ili kuwafikia wateja wengi kwa haraka.

4. Jifunze kuuza katika Maandishi (Copywriting). Jaribu kadiri unavyoweza.

5. Tumia WhatsApp yako vizuri kibiashara (Status, Broadcast, Groups n.k).

Ukiona haya yanakuwa magumu kwasababu upo busy au vinginevyo, usikubali sasa biashara yako ife/ishindwe kufanya vizuri mtandaoni.

Tafuta mtaalamu wa kufanya biashara mtandaoni, mpe targets zako, kubaliana nae katika malipo, kisha mpe kazi ili biashara yako izidi kupaa mtandaoni kwa sababu ni muhimu sana ukazipata hizi Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako. Sio lazima kila kitu ukifanye wewe mwenyewe kwa sababu hakuna ajuaje kila kitu.

Ni mategemeo yangu umepata kitu kipya leo. Kumbuka ZAWADI yetu ya kufunga Mwaka inakwisha tarehe 10 December, halafu hii ni maalum kwa watu 10 tu watakaowahi kujinyakulia website zao.

Tutumie ujumbe sasa hivi au tuchek kupitia mawasiliano haya;

Call/WhatsApp: +255765834754

Email: info@rednet.co.tz

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni. Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

JINSI YA KUONGEZA MBINU ZA KULIFIKIA SOKO MTANDAONI

Kila mtu atakwambia post insta, facebook, tumia funnels, weka status za kutosha Whatsapp. Mwingine atakwambia kusanya namba za simu uwapigie, tuma emails kila siku nk. Sasa utafanyaje kuongeza mbinu za kulifikia soko? Utakapomaliza makala hii ya leo utafahamu kiundani kuhusu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni. Utafanyaje, twende sambamba mpaka mwisho.

Zama hizi za Internet na huduma za mitandao ya kijamii zimekuja na mgawanyiko wa watu. Kila mtu anatumia mtandao wa kijamii anaoona unampendeza. Sio ajabu uone kuna mtu hana account ya facebook lakini kutwa yupo instagram/twitter. Hata hivyo ukiwa mjasiriamali lazima ufike kote.

UNALIFIAJE SASA HILO SOKO LA MTANDAONI?

1. Kwa kutumia Mitandao kama Whatsapp, Instagram, Twitter na Facebook, sasa unaweza kueneza maudhui yako kote kote kwa mtindo wa Copy & Paste. Ndio sio dhambi kufanya C&P ikiwa maudhui ni yako. Hata hii makala usishangae kuikuta kwa page zatu za LinkedIn na Instagram. Hapa ni muhimu sana Ukaifahamu Nguvu ya Mitandao ya Kijamii katika biashara yako.

Unachotakiwa kufahamu ni kwamba mitandao hii imetofautiana, hivyo maudhui unayopost twitter inabidi UYAHARIRI ili yaendane na aina ya watu katika mitandao mingine kama Website yako, Facebook, Instagram na LinkedIn. So kazi ya kueneza maudhui haiwi ngumu kuvile hapa, sivyo?

2. Pia unaweza kuanzisha kampeni fulani na kisha unaieneza kwa njia ya barua pepe. Kufanikiwa kwenye hili kwanza unapaswa ukusanye anwani za barua pepe nyingi (walau elfu moja) na kisha uifanye kampeni yako kwa uweledi wa hali ya juu ndani muda fulani. Hii ndio Email Marketing.

E-Mail Marketing in Business
mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

NB: Kampeni yako haipaswi kuwa na ujumbe wa kupandikiza chuki au viashiria vya ubaguzi wa namna yoyote kwa sababu kampeni za namna hio huleta hisia mseto kwa watu na kukujengea taswira mbaya. Barua pepe zako unaweza kuzikusanya kwa njia ya Newsletter au kawaida (ile ya kuomba).

3. Tumia Social Media Analytics Tools: Kama unasambaza maudhui yako kupitia mitandao ya kijamii, siku hizi kuna namna ambayo unaweza kupima mwenendo wa machapisho yako kirahisi tu. Katika twita kuna Twitter Analytics na Insta kuna Insights.

social media analytics tools
mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

Hizo tools zitakwambia maudhui yako yamewafikia watu wangapi (impression), wangapi wameshiriki mjadala (engagement), wangapi wameclick links na umepata wafuasi wangapi baada ya kuchapisha maudhui. Ukishajua hayo itakusaidia sana kuboresha zaidi Machapisho yako yajayo.

Mitandao ya kijamii hasa Mtandao wa GOOGLE ina nguvu ya ajabu sana katika kuwafikia watu wengi ndani ya muda mfupi tu. Ni muhimu basi ukajua namna ya kucheza na mitandao hii ambayo kila mtu duniani anatamani awe mtumiaji wa kila siku. Kufahamu zaidi kuhusu nguvu hio gusa hapa;

4. Tumia Web Analytics Tools; Kama tayari unayo website ya biashara au page ya blogu yako, basi ni muhimu sana ukaweza kufuatilia na kujua ufanisi wake kwa watu wanaoitembelea. Unajua watu wangapi wanatembea website yako kila siku? Makala zipi ulizoandika zinafuatiliwa zaidi?

Watu wanaotembelea website yako wanatokea wapi? Katika Injini za Kimtandao, website yako iko katika nafasi gani? Majibu ya maswali yote haya unaweza kuyapata kwa kutumia tools kama Google Search Console, ahrefs, winch, clutch n.k Hivi ndo virutubisho vya website yako mtandaoni.

5. Tumia Content Management System (CMS); Ukiwa muandishi ambaye ungependa maudhui yako yazidi kufanya vizuri mtandaoni basi unapaswa kutumia mbinu mbadala zitakazokusaidia tena na tena. Sikuhizi mambo yamerahisishwa, WordPress ndio CMS maarufu zaidi lakini ukiacha hio kuna Joomla, Drupal, Magento, Shopify na Prestashop (kwa ajili ya e-commerce). Ukiwa na hizo tools inakuwa rahisi kwako kuandika maudhui ambayo yatakuwa rahisi zaidi kunaswa na Injini za Mtandaoni kama Google, Ask na Bing. Umeshawahi kutumia CMS gani? Tuambie hapa leo..

Content Management System
mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

6. Tumia SEO Hapa sitasema mengi kwa sababu tumeshaongea mengi huko nyuma. Kifupi hii SEO (Search Engine Optimization) ni teknolojia iliyopo kwenye software za mtandaoni zenye uwezo wa kukusanya taarifa kutoka vyanzo mbalimbali kama websites, blogs, mitandao ya kijamii n.k

Cha kuzingatia zaidi unapofanya SEO ni matumizi ya Keywords sahihi kwa ajili ya soko lako ulilochagua kuhudumia (niche), Picha unazotumia lazima ziwe na maelezo tambuzi (alt text), matumizi ya links pamoja na ujuzi wa kuuza kwa kupitia maandishi(copywriting skills) Zingatia sana haya kwasababu hii ndio mbinu bora sana katika kufahamu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

Yaani SEO ni SUMAKU inayovuta taarifa kutoka sehemu mbalimbali za watu (open source information) na kuzigawa kwa mtu yeyote ambaye atatafuta taarifa hizo. Umeshaielewa jinsi SEO inavyofanya kazi sasa? Kufahamu zaidi fuatana na makala hii hapa;

7. Fanya Mara kwa Mara; Umeshayaona haya tuliyoyaelezea leo? Sasa kama unataka kufanikiwa katika kuipeleka mbali biashara yako huku mtandaoni, basi SIO LAZIMA uyafanye yote, aghalabu, unaweza kufanya matatu au manne ili ujiweke kwenye nafasi nzuri katika kuimarisha ushawishi wako huku Mtandaoni. Lakini katika kuzifanyia kazi mbinu hizi basi ni muhimu mbinu hizi uzifanye MARA KWA MARA, yaani uwe na consistency. Usifanye mara mbili kisha ukakata tamaa. Andika machapisho 500, tuma emails 2000, rudia na rudia. Njiani utagundua ile njia sahihi zaidi.

Umegundua nini kwenye makala hii ya leo? Umeshafahamu kiundani kuhusu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni? Una la kuongezea, swali au changamoto?

Tafadhali weka maoni yako hapa au kama unahitaji kuwasikiana nasi kupitia emails au Whatsapp, tafadhali fanya hivyo; Whatsapp/Call: +255765834754 Email: info@rednet.co.tz

D.R.C NDANI YA E.A.C, MFANYABIASHARA ANAFAIDIKA VIPI?

Hatimaye tar29 March Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ilipata kibali cha kuwa mwanajumuiya wa Afrika Mashariki (EAC) na mwezi July mwaka huo 2022 DRC iliingia rasmi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuwasilisha matakwa yote makao makuu ya jumuiya hio jijini Arusha. Hii ni baada ya kuendesha mchakato uliodumu kwa takriban miaka minne. Sasa DRC inapoingia ndani ya EAC mfanyabiashara anafaidika vipi?

DRC inakuwa mwanachama namba 7 wa EAC huku ikiwa ndio nchi kubwa zaidi kijiografia katika ukanda huo. Inasemekana DRC ndio nchi yenye rasilimali (madini, mafuta, misitu n.k) nyingi zaidi duniani. Pia nchi hio ina idadi ya watu takribani milioni 90 ambao ni mtaji muhimu kiuchumi.

MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU D.R.C:

Kukubalika kwa DRC kunamaanisha kwamba soko la Afrika Mashariki linatanuka na kuwafikia watu zaidi ya milioni 300 waishio ndani ya jumuiya hio tu, huku uchumi wa jumla ukiwa na thamani ya 250$ bilioni. Sasa DRC ina nini cha ziada usichokijua?

1. MIPAKA YA KIJIOGRAFIA:

Ikiwa ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa jiografia barani, DRC inapakana na nchi zingine 9. Nchi hizo ni Angola, Burundi, Jumhuri ya Afrika ya Kati, Rwanda, Jamhuri ya Congo (Brazaville), Sudani Kusini, Uganda, Zambia na Tanzania. Muingiliano wa kibiashara ni mkubwa sana hapa.

Zaidi upande wa magharibi mwa jiji la Kinshasha inapakana na bahari ya Atlantiki. Sasa Kongo kupakana na nchi 9 na kuwa na ufukwe wa bahari ya Atlantiki kunaifanya iweze kutanua fursa kwa wafanyabiashara kupitisha mali kwenda nchi nyingi zaidi barani na hata nje ya bara.

DRC na mipaka yake. Milango ya biashara za kimataifa kwa EAC.

2. KUHUSU VIVUTIO VYA UTALII:

Mbuga ya wanyama kongwe zaidi barani ipo DRC, inaitwa Virunga. Hapo utawakuta wale Sokwe wakubwa (Gorillas), simba na tembo. Lakini mbuga hii ipo kwnye tishio la kutoweka kwa sababu kuna mafuta na kampuni ya Uingereza ya Soco tayari imetia timu kuanza kuchimba mafuta hapo mbugani.

Hawa gorilla ni kivutio kizuri sana cha utalii lakini miaka ya hivi karibuni wamekuwa adimu na kutokana na shughuli za mwanadamu, wanyama hawa wapo kwnye tishio la kutoweka kabisa. Je, DRC kuingia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kutadhibiti hatari ya sokwe hawa kutoweka?

Kuhusu namna utalii unaweza kuleta manufaa katika biashara tafadhali fuatana na makala hii hapa chini:

3. KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NA MIUNDOMBINU:

Ni 1.8% tu ya barabara nchini DRC ndio ina kiwango cha lami, huku chini ya 10% ya nyumba za makazi ndio zina umeme. Hii ni hali mbaya sana katika kukuza uchumi wa Taifa. Hata hivyo Benki ya Dunia imetangaza kifurushi za 1$ bilioni kwa ajili ya miundombinu ya DRC.

Moja kati ya vitu vinavyorudisha nyuma juhudi za wajasiriamali na mashirika kuwekeza nchini DRC ni maendeleo duni ya miundombinu. Ukizingatia ukubwa wa nchi hio, imekuwa ni nafuu kusafiri kwa njia ya anga kuliko barabara. Sasa @jumuiya itachangia vipi maendeleo ya miundombinu?

4. BIASHARA ZA NJE YA NCHI (EXPORTS):

Muziki wa DRC ndio mali inayouzwa zaidi nje ya nchi (export). Kuanzia miaka ya 90 muziki wa Bolingo ndio ulikua unasikilizwa na kupendwa zaidi bara zima la Afrika. Ndio maana wasanii kama Fally Ipupa na Koffi Olomide ni matajiri sana. Madini na malighafi zingine zote chali.

5. LUGHA INAYOTUMIKA ZAIDI:

Jiji la Kinshasa ni la pili kwa matumizi ya lugha ya Kifaransa likitanguliwa na jiji la Paris. Yaani Wakongo hawa wanaongea kifaransa zaidi kuliko hata miji ya nchini Ufaransa. Hata hivyo hii inachangiwa na idadi ya watu wanaoishi kwenye jiji hilo, watu milioni 10 mchezo!

Ukiacha Kifaransa raia wa Kongo pia wanazungumza lugha zingine kama Kilingala, Kiingereza, Kiswahili na lugha za makabila asilia. Hivyo ukiwa kama mfanyabiashara na moja kati ya lugha tajwa unazifahamu vyema basi nafasi ni yako kuingia DRC na kutanua biashara zako.

6. KUHUSU UGONJWA WA EBOLA:

Kwamba kupata Ebola nchini DRC ni rahisi kama kupata mafua ukiwa sehemu nyingine? HAPANA. Baada ya ugonjwa huo kufumuka mwaka 1995 na kuua watu zaidi ya 200, milipuko mingine ya ugonjwa huo imekuwa ikidhibitiwa kwa kiwango kikubwa. Hivyo Congo ni salama.

7. KUHUSU MADINI:

Lile bomu la atomiki lililodondoshwa kwenye miji ya Hiroshima na Nagasaki katika WWII lilitengenezwa kwa madini ya Uranium kutoka mgodi wa Shinkolobwe, mkoani Katanga nchini DRC. Hata hivyo mgodi huo ulifungwa mwaka 2004 kutokana na kuishiwa madini ukiiacha DRC patupu.

Kongo imenyonywa sana katika madini yake. Hali kadhalika nchi zingine katika Jumuiya zimepitia hali hio. Hivyo itakapowekwa sera ya pamoja ya kulinda na kusimamia rasilimali zilizopo ndani ya Jumuiya, bila shaka madini na rasilimali ambazo zipo DRC zitakuwa na manufaa sana.

8. HISTORIA YA UNYONYAJI:

Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alijitangazia Kongo kuwa mali yake binafsi kuanzia mwaka 1870. Koloni hilo ndio lilikua mali binafsi kubwa zaidi kuwahi kumilikiwa na mtu mmoja kwenye historia. Umiliki huo ulisababisha vifo vya watu milioni10. Huu ndio mwanzo wa nchi kuharibika.

Mfalme Leopold II aliagiza watu kukusanya zao la mpira ambalo kwa kipindi hiko ndio lilikua zao bora zaidi la kibiashara. Wale walioshindwa kukusanya zao hilo kama kodi waliadhibiwa kwa kunyimwa chakula na kukatwa mikono yao. Ukatili huo ulikua mbaya sana dhidi ya ubinaadam.

9. HALI YA USALAMA NA VITA:

DRC imekuwa ikikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na migogoro isiyokwisha ambayo imepelekea vifo vya watu takriban milioni 6. Hali hio ya vita visivyokwisha imepewa jina la “Vita vya Dunia vya Afrika”.

Vita hivyo kwa sehemu kubwa vimekuwa vikisababishwa na vikundi fulani (kampuni, mashirika na raia wa kawaida) kugombania rasilimali katika eneo fulani. Huyu anataka kuchimba, raia wanataka kunufaika. Je, DRC kuingia kwenye @jumuiya itasaidia kumaliza janga la vita visivyokwisha?

10. KUHUSU MTO CONGO:

Ukiwa na urefu wa kilomita 4,700, mto Congo ndio mto mrefu wa pili barani Afrika ukitanguliwa na mto Nile. Pia huo ndio mto wenye kina kirefu zaidi duniani. Cha kufurahisha zaidi, Mto Congo na Mto Nile yote inapatikana katika EAC. Inakupa picha gani hii kiuchumi?

Je, EAC itaweza kuzalisha umeme wa pamoja kupitia sehemu za mto huo? Je shughuli za kiuchumi kama uvuvi, usafiri, utalii biashara ya mazao ya misitu zitaweza vipi kusimamiwa na Jumuiya kuhakikisha faida zinarudi kwa wanachi wa Kongo na wa jumuiya nzima kiujumla?

ZIADA: MSITU WA CONGO

Msitu wa pili kwa ukubwa duniani, msitu wa Congo unapatikana nchini DRC. Hata hivyo msitu huo ni mkubwa kiasi kwamba umeingia kwenye nchi zingine kama Cameroon, Jamhuri ya Afrika Ya Kati, Jamhuri ya Congo(Brazaville), Guinea ya Ikweta na Gabon. Msitu huu ni utajiri mtupu.

msitu wa mvua wa Congo
Msitu wa Congo

Katika msitu huo kuna fursa nyingi zikiwamo biashara ya magogo, madawa ya kutibu watu, mazao na wanyama, mbao, karatasi na bidhaa zote zitokanazo na misitu. Ukiwa kama mfanyabiashara ambaye sasa una uhuru wa kwenda kuwekeza DRC kirahisi, utaitumiaje fursa hii?

Sasa hayo ni baadhi ya mambo ambayo pengine ulikua huyafahamu kuhusu DRC. Mambo hayo kama yakifanyiwa kazi ipasavyo ndani ya @jumuiya basi ni wazi kutapunguza hali ya umasikini na kuimarisha amani kwa watu wa Kongo na kuimarisha uchumi wa Jumuiya nzima. Mapema mwaka 2021 jumuiya ya nchi za Afrika kwa kauli moja ilianzisha eneo huru la biashara barani (AfCFTA) ambapo nchi wanachama wanaweza kufanya biashara kwa uhuru bila ya vizuizi vya mipakani. Zaidi soma hapa chini

Jumuiya hii inatoa uhuru kwa wanachi wake kuishi na kufanya biashara popote ndani ya nchi wanachama. Jambo hili linatoa fursa kwa Wajasiriamali wa aina zote kuzurura na kutafuta masoko yao kirahisi. Ukiweza vema kutumia majukwaaa ya kimtandao kama websites, mitandao ya kijamii ujue unayo nafasi ya kuwafikia watu milioni 300 waishio ndani ya Afrika Mashariki. Sasa tuambie wewe mtu wa Teknolojia, website designer, mtaalam wa kutengeneza android app, mkulima, engineer nk, unataka ufaidike vipi hapa? Tuambie..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

M-PESA LIPA NAMBA
Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

Unawezaje kutumia Digital Tools ili kuimarisha biashara yako mtandaoni?

Kama huwezi kuendesha biashara yako ukiwa nyumbani au ukiwa safarini nje ya mkoa/nchi, nakushauri, hii 2022 hakikisha unatumia vema Digital Tools utakazojifunza leo katika kuimarisha biashara yako.

FAQ 1: Digital Tools ndio zipi?

ANS: Website, ecommerce store, twitter account, insta page, facebook, Linkedin, Zoom, CH, Whatsapp na Telegram.

FAQ 2: Nawezaje kuzitumia hizo Digital Tools kuimarisha biashara yangu?

ANS: i. BLOG SECTION:

Kwa website, hakikisha ina kipengele cha “Blog” ambapo utaweza kupost Updates mbalimbali kuhusu biashara yako mara kwa mara ili mteja apate solution ya changamoto zinazomkumba mara kwa mara.

ii. Tumia S.E.O:

Kuhakikisha biashara yako inapatikana google ikitokea mtu yeyote aki-search kuhusu huduma unazotoa. Mfano: ikiwa unauza chakula basi hakikisha katika blogs zako unatumia zaidi maneno kama “Wali, ugali, biriani, juisi ya miwa, chakula kitamu, sambusa za nyama nk”

Kwa sababu maneno hayo kitaalam yanaitwa “Keywords” ambayo ni rahisi kwa mtu yeyote kuyaandika akiwa anatafuta sehemu pa kupata huduma nzuri anazohitaji. So hakikisha unayatumia barabara kabisa kuendana na aina ya biashara yako.

iii. GOOGLE MAP:

Ni changamoto sana kwa wajasiriamali wengi. Unakuta eidha mtu hajui kuitumia au basi tu haoni haja ya kuitumia. Leo nataka nikusanue, hii Google Map inawainua sana watu mtandaoni. Kama unafanya biashara/una ofisi, ingia google map, sajili biashara yako chap.

Ingia google kisha andika (Aina ya biashara unayofanya au unayotaka kutafuta) kisha ikifuatiwa na maneno “near me” Mf: web designer near me, au food provider near me, au kitu chochote kama mifano inavyoonekana hapo. Halafu jiulize kwanini biashara yako haipo kwenye hizo listings?

iii. GOOGLE MY BUSINESS:

Katika jukwaa la Google unao uwezo wa kutengeneza wasifu (profile) wa biashara yako ukaweka details zote kama jina la biashara, mahali ilipo, huduma unazotoa au bidhaa unazouza, offers, mawasiliano yako n.k. Hii ndio njia rahisi zaidi ya kufanya S.E.O.

Hizo details unazoweka kwenye Akaunti yako ya Google My Business zinaisaidia sana biashara yako kuonekana kirahisi pale mtu anapotafuta vitu vinavyofanana na huduma unazotoa kupitia Injini za matafuto kama Google na Bing. Jaribu hii leo uone NGUVU ya SEO. Utanishukuru badae.

iv. SEARCH CONSOLE:

Hii ni Dashboard ya Google ambayo inakuonyesha namna website yako inaperform katika matafuto yanayofanyika huko mitandaoni. Kupitia matafuto hayo, google itai-rank website yako kwa mujibu wa inavyotafutwa na watu mbalimbali duniani kote.

Website zinazotembelewa zaidi na watu hutokea katika page ya kwanza kabisa pale mtu anapo-search kuhusu jambo analotaka mtandaoni. Ukiangalia kwa upande wetu, mpaka kufikia tar1/1/, tovuti yako ya https://rednet.co.tz imepata nafasi ya 7.6. Nia ni kufikia nafasi 3 za juu.

v. Katika matumizi ya Social Media kanuni zipo wazi. Hakikisha maudhui unayoweka kuhusu biashara yako 80% ni kuhusu VALUES ambazo biashara yako inampatia mteja, na 20% ikiwa ni kuhusu MATANGAZO ya bidhaa/huduma unazotoa.

vi. WHATSAPP:

Moja kati ya Tools zenye nguvu zaidi katika kuimarisha biashara kwa njia ya mtandao ni kupitia Whatsapp.

WHY WHATSAPP?

Je wajua kuwa watumiaji wa Whatsapp kwa wastani hufungua App hio mara 23 kwa siku, huku zikitumwa meseji milioni 29 kila dakika katika app hio?

Hii inakuhakikishia kwamba ukiitumia vizuri App ya whatsapp unajiweka kwenye nafasi nzuri ya KUSTAWISHA biashara yako kimtandao na kuongeza MAUZO, tena BILA GHARAMA yoyote ile ya kulipia matangazo.

Pia kupitia features za Whatsapp Status, Whatsapp Broadcast, Groups, Videos and Voicenote, sasa kutoa VALUES za biashara yako kwa wateja imekuwa rahisi. Unaweza kutengeneza Funnels hapo, ukabadili watu unaowasiliana nao kutoka WATU WA KAWAIDA kuwa WATEJA wako kirahisi zaidi.

Muhimu, hakikisha unapotumia hii mitandao ya kijamii basi walau uwe unaweka posts/tweet mbili kwa siku, kila siku (consistently).

Mwaka huu 2022, unao uwezo wa kumanage biashara zaidi ya 1 na zote zikaenda kwa ufanisi unaotakiwa kwa kupitia matumizi SAHIHI ya Digital Tools ulizojifunza leo. Usipoteze nafasi yako LEO sasa kufanya hivyo.

Una changamoto yoyote katika kutumia Digital Tools katika kuimarisha biashara yako? Tucheki kupitia DM yetu au Chati nasi Whatsapp kuitia namba 0765834754 ili kusudi tukushauri BURE kabisa namna ya kutatua changamoto hizo haraka iwezekanavyo.

OFA YA MWAKA MPYA 2022:

OFA YA KUPATA WEBSITE YAKO
OFA YA MWAKA MPYA 2022

Tunayo OFA YA MWAKA MPYA 2022 hapa ambapo, Ukitengeneza website kwetu unapata huduma za SEO kwa Google My Business, Search Console na Google Map BURE KABISA. Pia tutakuwa tunakushauri namna nzuri ya kuendesha website yako ili ikuletee faida kila siku.

Changamkia OFA hii kabla haijakwisha kwa sababu “Biashara asubuhi, jioni mahesabu”. OFA inakwisha tarehe 31/01/2022, hivyo wakati unapanga mipango yako ya kufanyia kazi mwaka huu, weka akilini pia namna utakayoweza kufanikiwa katika biashara zako mtandaoni kwasababu nyakati hizi zinakutaka ujifanyie tathmini binafsi kama kampuni inayofanya tathmini mwenendo wake. Weka mipango ya mwaka kisha igawe katika shughuli za miezi mitatu mitatu, fanya kazi kuifanikisha. Mwisho wa mwaka fanya tathmini uone jinsi umefanikiwa katika mwaka wako.

Cheers.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mpesa lipa namba yetu
website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado?

Website zinazotembelewa na watu wengi kila siku zina nini ambacho hujakifahamu bado?

Unaweza kuwa unajiuliza, “Sasa nimeshafungua website na ninazo akaunti za Twitter, Facebook na Instagram, lakini mbona watu hawatembelei tovuti yangu? nakosea wapi?” Leo nataka nikwambie kuhusu website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado? Makinika hapa.

Ukweli ni kwamba hakuna mtu yeyote ambaye hapendi kufanikiwa. Hakuna mfanyabiashara ambaye hapendi kupata Faida kubwa ya kifedha na wateja. Hakuna mtu ambaye hapendi kuingiza PESA.

Ukweli ambao unaweza usiambiwe na Web-Designer unayempa kazi ya kukutengenezea website ya biashara yako ni kwamba:

“Kumiliki Website na akaunti za mitandao ya kijamii (Zana za kimtandao) hakukufanyi kufanikiwa direct katika biashara hasa za mtandaoni”

-Faustine Kimath

Lakini kwanini umiliki hio website yenyewe, ilhali unaweza kutumia mitandao ya kijamii kuendesha biashara yako izuri tu? Majibu yanapatikana ukifuatilia makala hii hapa Kwanini ni Muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako?

Baada ya hapo utagundua pamoja na kuwa na website bado kuna zana nyingi sana za kimtandao (Digital Tools) ambazo unaweza kuzitumia kuwafikia wateja wako sambamba na website yako kama zana kuu. Sasa uzitumie vipi zana hizo ili ile Kiu yako ya kufanikiwa ikapate kutimilika?

Websites za kisasa zinatengenezwa zikiwa ni chanzo muhimu cha taarifa za kuaminika kuhusu Biashara/Kampuni yako. Hivyo website yako inafanya kazi ya kukutambulisha mtandaoni 24/7.

Sasa leo ukimaliza kusoma makala hii kuhusu website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado? Utapata uelewa hata siku ukifungua website yako ufahamu iwekwe vitu gani vitakavyoongeza idadi ya watu wanaoitembelea pamoja na kunasa wateja:

Kipengele namba 8 kitakufungua kichwa sana. Twende mpaka mwisho:

1. UBUNIFU:

Siku zote hakikisha unawapa wateja wako vitu wanavyopenda wao, sio unavyotaka wewe. Hata unapofikiria kubuni tovuti, hakikisha tovuti hio inafanana na aina ya wateja wako. Hivyo fanya utafiti wa kujua wateja unaowalenga ni wa namna gani kwanza.

Duru zinaonyesha 94% ya vitu vinavyomvutia mteja kwa mara ya kwanza kabisa (first impression) ni ubunifu uliotumika kutengeneza website hio. Ubunifu unajumuisha rangi za tovuti, mijongeo ya picha, aina za maneno (fonts) n.k

2. KASI YA KUFUNGUKA:

Kwa kawaida 94% ya watu huchukua si zaidi ya sekunde 5 kusubiri kurasa ya tovuti ifunguke. Baada ya hapo huachana na ukurasa huo na kuendelea na mambo mengine ya mtandaoni. Imagine tovuti yako inachukua zaidi ya sekunde 10 kufunguka sasa. Nani ataitembelea mara ya pili?

3. MATUMIZI YA ANWANI ZA NDANI

Unapokuwa na tovuti yenye anwani za ndani (internal links) za kutosha katika kurasa mbalimbali, unaiweka tovuti yako kwenye nafasi ya kutembelewa mara kwa mara tena na watu wengi zaidi.

Anwani hizi zinarahisisha kupatikana kwa taarifa kwa haraka na wepesi zaidi ndani ya tovuti yako.

Anwani hizo pia hutumika kama maneno ya msingi (keywords) katika injini za matafuto ya kimtandao kama Google. Hivyo mtu anapo-google inakuwa rahisi kupata majibu, bidhaa au/na huduma zinazotolewa kupitia tovuti yako.

4. MAUDHUI YA VIDEO:

Zamani ilikua si rahisi kurusha maudhui ya video mtandaoni na yakawafikia watu wengi kutokana na uduni wa teknolojia. Lakini siku hizi mambo ni tofauti sana. Maudhui ya video yamekuwa yakiwafikia watu wengi zaidi na kwa haraka sana. Angalia namna YouTube inayoshika kasi pale msanii wako unayempenda akiachia wimbo mpya. Siku hizi hata kukiwa na matukio muhimu ya Kitaifa, watu wengi huyafuatilia kupitia YouTube kuliko televisheni za kawaida.

Kwanini? Kwa sababu YouTube inapatikana kwenye smartphone, stesheni za televisheni hazipatikani kirahisi kwenye smartphones, hivyo nyakati hizi ukiwa popote kwenye mihangaiko yako ni rahisi kufuatilia maudhui ya video kupitia simu yako yenye intaneti kuliko wakati mwingine kwenye historia ya mwanadamu.

Maendeleo ya kiteknolojia yamerahisisha sana usambazwaji wa video mtandaoni. Hivyo unapofikiria kufungua/kuiimarisha website yako, hakikisha pia unaweka maudhui ya video ambayo yatawafanya watu wazidi kumiminika na kufaidi thamani ya maudhui hayo kirahisi.

5. MATUMIZI YA BLOGU

Kwa ulimwengu huu, masoko ya bidhaa na huduma yamehamia mtandaoni na hivyo kusababisha ushindani kuwa mkubwa sana ukiongozwa na uwepo wa maudhui mbalimbali yanayopandishwa kila siku.

Hivyo, tovuti yako inapaswa kuwa na kitu kipya kila leo.

Tovuti yenye Blogu ina nafasi ya kufanya vizuri kwa kuwafikia watu wengi na kutembelewa kila siku tofauti na tovuti ambazo hazina sehemu ya Blogu. Kwenye blogu ndipo unapoweza kuweka maudhui ya kuwasaidia wateja wako kufikia malengo yao na kutatua changamoto wanazokutana nazo kila siku kupitia biashara yako. Hapa utagundua kwanini ni muhimu kuwa na website ya biashara yako?

6. MATUMIZI YA PICHA

Je, wajua kwamba picha ndio kiungo rahisi zaidi katika kuhudumia mteja? Zinamfanya mteja kukumbuka kuhusu huduma/bidhaa yako, ni nyepesi na rahisi kutumia. Maudhui yako yakiwa na picha, 65% ya wanaotembelea tovuti yako watakukumbuka hata wakitoka mtandaoni.

Mfano ukiitizama picha hii hapa chini wazo linalokujia haraka ni kwamba sasa ni wakati wa sikukuu ya Christmass, na kwa kuwa umeiona hapa picha hio bila shaka ukiiona sehemu nyinngine utakumbuka tu kwamba “Faustine alishawahi kuipost pia hii picha“. Unaiona nguvu ya picha hapo sasa? Imagine bidhaa zako unazipiga picha kali za kiubunifu na kuziweka kwenye tovuti yako sasa.

website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado?

7. UMUHIMU WA S.E.O

Kama unahitaji mafuriko ya watu yazidi kumiminika katika tovuti yako kila siku, hiki kipengele cha SEO huwezi kukikwepa. Hii ni Teknolojia inayorahisisha matafuto ya mtandaoni na kuelekeza wapi pa kupata majibu na taarifa zaidi.

Imagine google inawaelekeza wateja waje kwako kupata taarifa, huduma na bidhaa muda wote ambao wewe umelala zako, au muda ambao wewe haupo mtandaoni ikiwa tu tovuti yako utakuwa umeiunga na miundombinu ya SEO. Hii S.E.O inahusisha matafuto katika mifumo ya maneno ya msingi (keywords) ambayo unakuwa ukiyatumia mara kwa mara katika tovuti yako na mifumo yako ya utoaji huduma. Hii imekuja kurahisisha sana maisha. Halafu cha ajabu zaidi, ni rahisi sana kuitumia. Ungependa kufahamu zaidi kuhusu SEO? Njoo WhatsApp sasa hivi kwa kugusa namba hii hapa 0765834754

8. UTATUZI WA KERO/CHANGAMOTO:

Jambo muhimu zaidi linalowavuta watu wengi kutembelea tovuti mbalimbali ni Nafasi ya Kutatua kero/changamoto zinazowakabili. Watu hawatembelei tovuti tu ilimradi, wanatafuta suluhu ya kero zinazowakabili kwenya shughuli zako za kila siku. Hivyo, zingatia hilo.

Hapa tunarudi kwenye SEO ambapo huduma hii itakurahisihia solution unazotoa kupitia website yako ziweze kuwafikia wateja wako haraka sana pale wanapozitafuta huko mtandaoni. Katika hili hakikisha website yako ina ukurasa uitwao Maswali yaulizwayo mara nyingi zaidi au Frequently Asked Questions (FAQs).

Je tovuti yako ina maudhui yanayotatua changamoto gani kwa wateja wako. Tuambie kwenye comments.

Unajiuliza utakuwa unatatua changamoto zipi? 1. Chunguza wateja wako uwafahamu wanapitia changamoto zipi, 2. kisha Jifunze namna ya kutoa huduma bora. 3. Fundisha kwa kuandika kutoka kwa wataalam wa copywriting. Rudia no.1.

-Faustine Kimath

9. MATUMIZI YA FOMU ZA MAULIZO:

Kama unataka tovuti yako ivutie watu wengi zaidi basi moja kati ya SIRI muhimu ni kuweka “fomu ya maulizo” ambayo inampa mtu yeyote anayetembelea tovuti yako nafasi ya kuuliza chochote kuhusu huduma/bidhaa zako. Muhimu sana hii, na siri ya kufanikiwa katika hili ni kuitengeneza fomu yako iwe fupi na ya kufurahisha (yani inatakiwa mtu akiiona tu ajisemee “loh, hebu niulize kuhusu … hapa chap“).

Fomu hii ni kipengele kinachoweza kuwabadili watembeleaji (visitors) kuwa wateja haraka sana.

10. HUDUMA KWA WATEJA:

Hata kama ukiyafanya yote uliyojifunza leo hapa kwanzia 1-9 lakini ukawa huna huduma nzuri kwa wateja wako na watu wanaotembelea tovuti yako na kuuliza maswali kwa lengo la ufafanuzi, ndugu, bado safari ya mafanikio itakuwa ndefu kwako.

Huduma kwa wateja inajumuisha namna unawasikiliza wateja wako, namna unavyojibizana nao (kwa maandishi au kwa sauti), muda unaotumia kuhudumia wateja wako na namna unavyoweza kuhimili hasira na mtazamo hasi kutoka kwa wateja na watu mbalimbali.

thamani vs gharama, nafuu iko wapi? fahamu siri za kuweza kushawishi wateja katika biashara yako.

website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado?
Thamani vs Gharama: Nafuu iko wapi?

Vyote hivyo vinachangia kuongeza au kupunguza idadi ya watu wanaotembelea tovuti yako kwasababu takwimu zinaonyesha 95% ya wateja husambaza maneno kuhusu huduma mbovu walizopata na 89% kati yao huacha kabisa kufanya kazi na yule aliyetoa huduma mbovu zaidi unaweza kupitia makala hii hapa Umuhimu wa Takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa Wateja.

Tovuti ni sehemu muhimu sana katika kuhudumia wateja wa biashara yako pamoja na kujitangaza hasa katika zama hizi za kidijitali.

Huna haja ya kusambaza CV na makaratasi. Tunza mazingira kwa kupunguza matumizi ya karatasi ambazo zinatokana na ukataji wa miti.

ZIADA: Hata ukisema uyafanye hayo yote 10 ambayo umeyaona kwenye makala hii ya leo, bado nature itakudai kitu kimoja cha muhimu zaidi. Nacho ni muendelezo (consistency) katika utendaji wako wa kusimamia biashara katika mazingira yote, mtandaoni na ana kwa ana. Fahamu kuwa hakuna mafanikio ya ghafla au mafanikio ya bahati mbaya. Yeyote unayemwona amefanikiwa (hata kwa bahati nasibu), lazima alistruggle kutengeneza mfumo mzuri wa kiutendaji ili kumsaidia katika kusimamia biashara yake katika viwango vinayotakiwa.

Umejifunza nini kwenye makala hii ya leo kuhusu website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado? Tuambie kwenye comments hapa chini. Pia hakikisha una-share makala hii pamoja na watu wako wa karibu ili kusudi somo hili liwafikie watu wengi zaidi.

website zinazotembelewa na watu wengi kila siku, zina nini ambacho hujakifahamu bado?
mpesa lipa namba yetu