Tag: strategy

Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

BRANDING Vs MARKETING, KIPI NI KIPI?

Unapofanya biashara, moja kati ya malengo makubwa ni Kupata/kuendelea kupata wateja kila siku. Wateja ndio Roho ya biashara. Hakuna biashara kama hakuna wateja. Lakini unawapataje wateja hao? Unatumia vipi mbinu za Marketing na Branding? Branding vs Marketing, Kipi ni kipi?

Unapokuwa unaitengeneza biashara yako unatumia mbinu nyingi sana kujitangaza na kuvuta wateja wengi kwa kadiri inavyowezekana. Kuna wanaotumia ndugu, jamaa wa karibu, classmates, colleagues n.k. Ili mradi tu connections zinahusika kwa ukubwa wake. Kuna wengine wanatumia mitandao ya kijamii, kuna wanaofanya company visits na wengine wanatumia mbinu ya Umachinga (Kutembeza Barabarani). Lakini wote hao wanatumia Mbinu mbili tu kimsingi. Ni Either Marketing au Branding.

MARKETING na BRANDING ni nini?

Marketing ni mjumuisho wa vitendea kazi, utaratibu na mbinu za kuhakikisha bidhaa/huduma zako zinapigiwa debe ipasavyo ili ziuzike. Marketing ni mbinu ya kumfanya mteja anunue bidhaa/huduma zako. Ndo kupiga debe kwenye huko. Upande wa pili, Branding ni ile namna unajiweka/unaiweka biashara yako ili iweze kupokea wateja zaidi.

unawezaje kupata wateja mtandaoni unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Branding Vs Marketing. Kipi ni kipi?

Ule unauweka utambulisho wa biashara yako, unavyofanyia kazi Dira, Malengo na Mipango yako na vile vitu vinavyokufanya wewe kuwa tofauti na washindani wako kibiashara. Hio ndio BRAND yako. Kama Marketing ni sumaku ya kuvuta wateja, basi Branding ni sukari ya kuwafanya waendelee kuwepo.

KIPI KINAANZA – BRANDING au MARKETING?

Fahamu, Branding ipo kwenye ule msingi kabisa wa Mbinu zako za kimasoko (marketing strategy), hivyo Branding lazima itangulie. Ukiitengeneza vizuri Brand yako hata kama ni changa, swala la Marketing linakuwa rahisi maradufu. Brand yako unayoitengeneza ndio itawafanya wateja waendelee kukujia na kuongezeka kwa mabalozi wa kujitolea wa bidhaa/huduma zako, ambao ndio wateja wenyewe haohao. Hii inaitwa “Customer’s Loyalty” (nimekosa kiswahili chake). Mfano, tizama Pepsi, pengine ndio soda inayouzika na kunyweka zaidi duniani kwa sasa, nikikuuliza umekunywa pepsi ngapi tangu mwaka huu umeanza pasi na shaka huna jibu, yaani umekunywa nyingi zisizo na idadi. Sasa hio ni kwa kuwa watengenezaji wa soda hio walitengeneza tabia zinazokufanya uendelee kuitumia miaka na miaka. Tabia hizo ni pamoja na Usafi wa chupa, Ubora, ladha n.k.

Pata huduma za Website, SEO, Social Media Marketing na nyinginezo nyingi kutoka Rednet Technologies

Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

Katika biashara za namna bora zaidi ya kuji-Brand ni kutumia mitandao ya kijamii. Sasa unatumiaje mitandao ya kijamii kwa manufaa ya biashara yako? Branding vs Marketing, Kipi ni kipi? Tafadhali songa na makala hii kwenye link IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA

Hivyo linapokuja swala la marketing, ni rahisi zaidi kuipromote Pepsi ikauzika kuliko Fanta passion. Branding ni ile kutengeneza utamaduni, mhenga mmoja alishasema, “Culture eats strategy for breakfast”. Yaani hata uwe na mbinu gani, kama hujazifanya mbinu zako kuwa utamaduni unaoishi, hapo andika maumivu. Ndio maana wanamichezo makini hufanya mazoezi kama utamaduni wao wa kila siku, na ndio hao ambao wanafanikiwa zaidi. Branding vs Marketing, Kipi ni kipi?

Branding vs Marketing, Kipi ni kipi? Tofauti ni ipi?

1. Marketing ni ile mbinu ya kutengeneza mhemko(attention) kwa wateja, Branding ni namna ya kuwafanya wateja waendelee kuwa wateja wako.

2. Marketing ni mbinu ya kufanya mauzo, Branding ni namna ya kutengeneza Jina, Heshima na Ushawishi kwa wateja.

3. Branding ndio inayoanza kuonekana katika biashara yako, Marketing inafuata.

4. Mbinu za kufanya Marketing hubadilika kulingana na wakati na mahitaji, lakini Branding ni Mbinu ya kutengeneza Utamaduni wa kudumu kizazi na kizazi.

5. Branding inahusika sana katika kufanya shughuli za kila siku za ndani ya biashara/kampuni yako, na vile wateja wanaziishi huduma/bidhaa kutoka kwako. Ndio utamaduni wenyewe.

Kwa chochote unachokifanya, fahamu biashara yako ni moja kati ya biashara nyingi duniani ndani ya bahari ya Ushindani wa kimasoko. Unahitaji mbinu bora katika kutengeneza Brand (Recognition) yako pamoja na Marketing (sales) za kila siku.

Kwa maneno mengine mbinu hizi hujieleza kupitia Dira (Vision) na Malengo (Missions) ya biashara yako. Leo nataka useme hapa Vision na Missions ambazo umejiwekea katika biashara yako ni zipi? Ukiweza kuzieleza na kuzisimamia vizuri basi, basi Utakuwa unaiweka pazuri bishara yako. Mfano, Rednet Technologies ilianzishwa ikiwa na Dira(vision) ya “Kuhakikisha Wafanyabishara wadogo na wakati (SME’s) wote nchini Tanzania na Afrika Mashariki wanatumia Teknolojia za kisasa katika utendaji wa biashara zao za kila siku.”

Mipango(Missions) ipo mingi lakini baadhi ni:

i. Kutengeneza websites bora kwa matumizi ya biashara mbalimbali kama ecommerce, corporate, funding na normal profile.

ii. Kutengeneza mifumo ya kuhifandhi na kuendesha mauzo na rekodi mbalimbali za kibiashara.

iii. Kuhakikisha wafanyabiashara wanapata taarifa muhimu kuhusu mbinu, takwimu na habari za Uchumi na mabadiliko ya kibiashara haswa kupitia Mapinduzi ya Viwanda yanayochochewa na mabadiliko ya kiteknolojia yanayotokea duniani kila uchwao. Taarifa hizo unaweza kuzipata kupitia tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz Kupitia Vision na Missions hizo ulizoziona, Niambie ni rahisi kiasi kubuni mbinu ya kufanya Marketing? Je unaweza kuanzisha Marketing strategy gani kwa wakati huu unaosoma makala hii? Majibu yote unayo wewe mwenyewe.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni.

Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

Sasa makala hizi hapa chini zitakupa muendelezo mzuri kuhusu somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana kama ukizisoma zote. Gusa link kisha makinika:

  1. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO
  2. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  3. IFAHAMU TEKNOLOJIA YA QR CODE KATIKA BIASHARA YAKO

Tueleze leo vision ya biashara yako ili tujue utamaduni wako ni upi, watu tuanze kuufuatisha. Hakikisha unasambaza makala hii kwa watu wengi kuhakikisha Biashara zinashamiri na unazidi kupata wateja wapya kupitia hapa. Tuanze.