Tag: SSA

TEKNOLOJIA KATIKA KUKUZA BIASHARA KUPITIA SEKTA YA UTALII

Inasemekana binadamu anajua zaidi mazingira ya mwezini kuliko ajuavyo mazingira ya ndani/chini ya bahari. Sasa kampuni ya usafirishaji ya Uber tarehe 23 May 2019 ilizindua manuwari ndogo iitwayo ScUber kwa ajili ya kutalii ambapo mradi huo umeanzia jijini Queensland, Australia. Moja kati ya sababu ikiwa ni kutoa fursa kwa wageni/watalii kuweza kuzuru eneo maarufu la bahari liitwalo The Great Barrier Reef nchini humo. Sasa tunaweza vipi kutumia teknolojia katika kukuza biashara kupitia sekta ya utalii? Kumbuka Tanzania ina vivutio vingi sana vya utalii na vijana wengi wamejikita katika kuhudumia watalii hao, watumieje teknolojia kujiletea manufaa? Twende sambamba mpaka mwisho wa makala hii kufahamu zaidi.

utalii na teknolojia

Turudi Australia, manuwari hio ndogo yenye uwezo wa kubeba watu watatu kwa wakati mmoja ni ya kwanza kabisa duniani kufanya shughuli za kutalii kwa mtu yeyote anayehitaji kufanya hivyo na ambayo huduma yake inapatikana kirahisi kupitia Application ya Uber inayopatikana Playstore ya Google na Appstore ya iOS (Je, wewe ni mmoja kati ya wale waliozoea kuziona manuwari kwenye muvi na kusikia manuwari za kivita tu? 😂). Haya ni mapinduzi makubwa katika kufanya biashara kupitia nyanja nyingine ya kichumi (kutoka usafirishaji mpaka utalii).

Sekta ya utalii inatajwa kuwa ni sekta muhimu sana katika ukuaji wa uchumi na kutengeneza ajira duniani kote. Sekta hio inatajwa kujumuisha 8.8% ya ajira zote duniani, sawa na watu milioni 258. Vile vile 9.1% ya wastani wa pato la taifa GDP inatokea katika sekta hii ambayo ni sawa na $6 trilioni. Zaidi, 5.8% ya bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi (exports) huhusishwa na sekta hii ambayo ni takribani $1.1 trilioni. Hata hivyo, sekta hii ya utalii huchochea sana uwekezaji ambapo 4.5% ya uwekezaji wote unaofanywa duniani hupitia katika sekta hii ambayo ni sawa na $652 bilioni za kimarekani.

Tukiangazia eneo la kusini mwa jangwa la Sahara inakadiriwa kwamba ajira 3.8 milioni zikijumuisha ajira 2.4 ambazo si za moja kwa moja (indirect jobs) zinakadiriwa kutengenezwa katika miaka 10 ijayo. Hii ni kwa mujibu wa Baraza la usafiri na utalii duniani (WTTC).

Sasa changamoto; Sekta hii ya utalii inachangia vipi katik kukuza biashara barani Afrika? Teknolojia inachangia vipi katika maendeleo haya ya utalii na biashara?

Kutoka ziara za watalii 6.7 milioni mwaka 1990, nchi za ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara zilitembelewa na watalii 33.8 milioni kufikia mwaka 2012 kwa pamoja ambapo stakabadhi za wageni mwaka huo 2012 peke yake zilionyesha zaidi ya dola za kimarekani 36 bilioni zilipatikana huku mchango wa moja kwa moja ukiwa ni 2.8% katika pato la ndani la taifa GDP (Jumla ya mchango ikiwa ni mchango wa moja kwa moja na ule usio wa moja kwa moja, ilifikia 7.3% ya GDP). Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya baraza la WTTC mwaka 2013.

Lakini, ili kufanikiwa zaidi katika kufanya Utalii na kuendeleza biashara, ukanda huo wa SSA (Subsaharan Area) inabidi ujidhatiti katika mambo yafuatayo; upatikanaji wa ardhi, ruhusa ya wawekezaji katika maswala ya fedha, matangazo ya utalii, kodi za uwekezaji katika utalii, utaalamu na ujuzi katika utalii, ulinzi na usalama, maswala ya afya, mahitaji ya viza na ukiritimba. Sasa teknolojia inaleta mchango gani katika kukuza biashara kwa kupitia utalii? Kuhusu namna unavyoweza kuitangaza biashara yako katika nyanja hii ya utalii fuatana na makala hii hapa

Tuzione baadhi ya njia za kiteknolojia zinazotumika katika nyanja hio;

E-TOURISM:

Huduma za intaneti zimeleta mapinduzi makubwa sana kwenye sekta hii ya utalii ambapo watalii na wageni sasa wanaweza kupata taarifa muhimu kuhusu mahali wanapotaka kwenda kutalii kama mbuga za wanyama, bidhaa za kiasili na utamaduni, hoteli, majumba ya makumbusho na historia mbalimbali kwa kutumia vifa vyao vya kielekroniki vilivyoungwa na huduma za intaneti kama simu za rununu na kompyuta mpakato (laptop). Matokeo yake wageni na watalii wamekuwa na mahitaji makubwa kwa bidhaa za kiasili na utamaduni pamoja na kujali thamani ya pesa zao pamoja na thamani ya muda wao. Hii imerahisisha sana ufanyaji wa biashara haswa kupitia majukwaa ya ecommerce (ambayo unaweza kuyapata kwetu Rednet Technologies kirahisi sana., gusa link hii kupata huduma zetu zenye ubora Our Services🙋).

E-HOSPITALITY;

Teknolojia ya ICT imepenya mpaka katika mifumo ya huduma kwa wageni kwa haraka mno, huku ikizama katika utendaji wa hoteli, kuunda upya shughuli za masoko, kukuza huduma kwa wateja, kuimarisha huduma za kifedha, huduma za usafiri wa anga pamoja na huduma za kuwezesha ufanyaji wa biashara mtandaoni. Hii imeleta mafanikio zaidi baada ya kugunduliwa mifumo ya Computerized Reservetion Systems (CRS‘s) kuchukua nafasi ya mfumo wa zamani wa kuandikisha wageni katika mahoteli na katika vituo vya afya.

E-TRAVEL AGENCIES:

Teknolojia ya ICT imeleta maendeleo makubwa katika uendeshaji wa shughuli za taasisi mbalimbali na wakala wa kusafirisha na kutembeza wageni na watalii ambapo imeimarisha sana shughuli za ndani kama uhasibuukaguzi na rasilimali watu pamoja na shughuli za nje kama huduma kwa wateja, mifumo ya tiketi na mawasiliano ya wabia. Licha ya kuwa na 15% ya idadi yota ya watu duniani, Afrika ilikuwa ikihudumia 4% tu ya abiria wa safari za ndege duniani. Hata hivyo huduma hio ilipanda kufikia 6.5% katika kipindi cha mwaka 1998-2009 huku Carpe Verde, Msumbiji, Ethiopia na Tanzania(kabla ya kuimarishwa kwa AirTanzania) zikikuwa kwa makumi ya asilimia (WorldBank report). Maendeleo haya yanaakisi ukuaji wa matumizi ya teknolojia katika eneo hilo ambapo kumekuwepo pia na matumizi ya mifumo ya kudhibiti tiketi (OTS) na mifumo ya kuwasiliana na wateja (CRM‘s). Zaidi mifumo ya kudhibiti tiketi imekuwa muhimu katika kuratibu idadi ya wageni pamoja na kudhibiti maswala ya fedha kiteknolojia.

E-DESTINATION:

Hii ni maalum kwa waendeshaji wa Hoteli, Nyumba za wageni (Guest Houses & Lodges) pamoja na migahawa ya chakula. Sasa teknolojia imeleta mifumo mahsusi kwa ajili ya kurahisisha huduma katika kutafuta soko na kusajili wageni/watalii kirahisi wakiwa popote duniani kwa kutumia simu za rununu au kompyuta. Mfumo wa Destination Management System (DMS) umekuwa muhimu sana licha ya 10% tu ya vyumba vya hoteli 390,000 zinazopatikana katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara kuwa na hadhi ya kimataifa, huku Afrika Kusini ikishikilia nusu ya vyumba hivyo. Hata hivyo Kenya, Mauritius, Shelisheli na Tanzania zinaonyesha kuwekeza zaidi katika huduma za hoteli na teknolojia.

E-COMMERCE:

Jukwaa maarufu zaidi duniani katika kufanya biashara kwa njia ya mtandao kielektroniki. Hii ni muhimu kwa wafanyabiashara wa bidhaa za kiasili na kitamaduni kama shangavinyago na batiki ambapo sasa wanaweza kuweka bidhaa zao katika majukwaa hayo na kufikisha bidhaa zao duniani kote kirahisi zaidi, hivyo kukuza mauzo yao (Majukwaa haya ya ecommerce yanapatikana hapa Rednet Technologies, pitia tovuti yetu kwa kugusa link hii Rednet Technologies).

Kufahamu zaidi kuhusu e-commerce tafadhali fuatilia makala hii hapa kwenye link https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-biashara-za-kielektroniki-e-commerce-businesses/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI?”

Una la zaidi? Tafadhali, weka comment yako hapo chini ili tuweze share mawazo na hoja kuhusu makala haya juu ya unaweza vipi kutumia teknolojia katika kukuza biashara kupitia sekta ya utalii? Kazi kwako mfanyabiashara.

Je umependezwa na makala zetu zilizomo katika website yetu hapa?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) na QR CODE ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA kwenye picha hapa muda wote 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA

Mtandao wa usafiri kwa njia ya nchi kavu barani Africa unajumuisha barabara na reli ambapo kwa wastani umechukua kilomita 6.2 kwa kila eneo la kilomita za mraba 100. Zaidi ya 60% ya mtandao mzima wa barabara haijatengenezwa kwa kiwango cha lami. Zaidi, pungufu ya 40% ya barabara za lami ndizo zilizo kwenye hali nzuri ya kupitika muda wowote. Sasa sekta hii ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika inatoa matumaini gani?

Mtandao wa njia za reli umeundwa kwa njia moja (single-track lines) ambazo huanzia maeneo bandarini kuelekea maeneo mbali mbali ya nchi/bara zikijumuisha viungio vichache tu njiani kuunga njia moja ya reli na nyingine (inter-linkages). Muundo huu wa reli zilizopo barani Afrika uliundwa nyakati za ukoloni na tangu wakati huo, ni marekebisho machache tu yameweza kufanyika ili kuwezesha treni ndefu zaidi zinazotumia dizeli kupita ambapo treni nyingi kati ya hizo hazitumiki tena kwa sasa.

Tukiangazia eneo la bandari, chini ya 50% tu ya matumizi ya bandari hutumika ikiwa ni pungufu ya mahitaji sahihi ya bandari hizo, jambo ambalo huchochewa na ucheleweshwaji wa mizigo na taratibu za forodha. Hali kadhalika, Afrika ndio inaongoza duniani katika ukuaji wa sekta ya viwanja vya ndege haswa kufuatia kuazishwa kwa soko huru lililoanzishwa baada ya makubaliano ya YD (Yamoussoukro Decision) yaliyofanyika mwezi November, 1999. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Afrika AU iliyotolewa mwaka 2014.

USAFIRISHAJI BARANI aFRIKA.Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Sasa changamoto; Je, sekta hii ya Usafirishaji na Miundombinu inaathiri vipi ukuaji wa biashara barani Africa? Na je, matumizi ya Teknolojia yana mchango gani katika kuboresha sekta hii ili kuinua biashara?

Kutokana na hali duni ya miundombinu na huduma za usafirishaji, gharama za kusafiri barani Afrika ni kati ya gharama ghali zaidi duniani, jambo ambalo linadhoofisha ushindani wa kibiashara katika masoko yote, ya ndani ya nchi na yale ya kimataifa.

Ripoti ya Tume inayoshughulikia Uchumi barani Afrika (ECA) imetaja kwamba nchi zisizo na bandari (landlocked countries) gharama za usafiri zinaweza kufikia robo tatu ya thamani ya bidhaa inayosafirishwa. Kwa mfano kusafirisha gari kutoka Japan mpaka Abijdan nchini Ivory Coast hugharimu US $1,500. Lakini kusafirisha gari hilo hilo kutoka kutoka jijini Abidjan hadi Addis Ababa hugharimu US $5,000. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa Teknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi kupitia link hii hapa yenye kichwa MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI. Ukimaliza hapo tuendelee na mada yetu ya leo.

Changamoto za Usafirishaji barani Africa.Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Gharama za usafirishaji zimetajwa kusababishwa na viwango vikubwa vya forodha, tozo za ucheleweshwaji, hasara zitokanazo na ajali pamoja na ukosekanaji wa fursa. Changamoto hizi huchagizwa zaidi na uduni wa miundombinu ya kiuchukuzi pamoja na huduma zinazotokana na nyanja hiyo.

Nayo programu ya maendeleo ya miundombinu barani Afrika (PIDA) katika ripoti yake imeainisha kwamba gharama za kiuchumi zinazosababishwa na changamoto za usafirishaji katika Mtandao wa Miundombinu ya Usafirishaji barani Afrika (ARTIN) zinazidi US $170 bilioni kwa mwaka kufikia mwaka 2014.

Changamoto hizo zimetajwa kusababishwa na;

•Kutokuwa na utendaji wa taratibu za kuwezesha biashara katika majukwaa ya ARTIN (kujumuisha bandari na vituo vya mipakani).

•Sera za nyanja ya usafirishaji ambazo zinapelekea kudhoofika na kuongezeka kwa gharama za usafirshaji kwa njia ya barabara pamoja na viwango duni vya barabara katika nchi nyingi barani Afrika.

• Sera za kiuchumi zinazozuia utendaji mzuri pamoja na utanuzi wa mifumo ya reli.

• Nyanja ya usafiri wa anga na Sera za kiuchumi zinazozuia uanzishwaji wa vituo vya anga vya kikanda, jambo linalotajwa kusababisha kuongezeka kwa gharama za usafiri huo.

Kufuatia changamoto hizo, Je, teknolojia ina mchango gani katika kuimarisha biashara na kupunguza gharama za uendeshaji?

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kuelekea mapinduzi ya nyanja zote za kiuchumi. (Yaani tutaendelea kuwa juu kileleni😁). Mapinduzi katika matumizi ya simu kutoka simu za mezani mpaka simu za rununu (smartphones), huduma za kifedha kielektroniki (fintech), biashara za kielectroniki (ecommerce) na kadhalika vimekuwa sehemu muhimu sana katika kurahisisha utendaji wa kibiashara katika sekta ya miundombinu na usafirishaji.

Benki ya Dunia (WorldBank) inaripoti kwamba ubunifu wa kiteknolojia umewezesha sana muingiliano wa kibiashara kwa kuzingatia ongezeko la watumiaji wa Intaneti huduma za simu. Kipimo cha wiani (density) katika matumizi ya huduma za intaneti kwa kila watu 100 waliopo eneo la Kusini mwa jangwa la Sahara, ni watu 17 tu ndio wameonekana kuwa watumiaji wa intaneti katika mwaka 2015.

website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako?Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika

Utafiti huo unakolezwa wino na shirika la kimataifa linalodhibiti mawasiliano ya simu GSMA ambapo kwenye ripoti yake ya mwaka 2018 limeangazia kwamba, eneo la kusini mwa jangwa la Sahara lilikua na kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu ya 44% kufikia mwishoni mwa mwaka 2017 kukiwa na watumiaji takriban 444 milioni sawa na 9% ya watumiaji wote wa simu duniani. Vile vile katika kipindi cha mwaka 2017-2022 watumiaji wa simu katika eneo hilo wataongezeka katika kiwango cha CAGR cha 4.8% ambayo ni zaidi ya mara mbili ya kiwango cha ongezeko kwa dunia nzima katika kipindi hicho hicho. Pia kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu inatajwa kufikia 50% kufikia mwishoni mwa 2023 na 52% mpaka mwaka 2025.

Kufuatia uchunguzi huo, sekta ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara barani Afrika inatajwa kuongezewa nguvu na maboresho zaidi ili kuendana na kasi hio ya ukuaji katika ICT. Matumizi ya GPS katika usafiri wa taxi yamerahisisha zaidi gharama na muda wa kutoka sehemu moja na nyingine, huku maboresho ya miundombinu kama barabara na viwanja vya ndege yakichagiza kasi ya sekta hio.

Zaidi, mtandao wa huduma za Posta na EMS unajumuisha takriban ofisi 30,000 barani ambazo ni muhimu katika kuwezesha e-commerce trade. Kwa kuliona hilo kampuni kama DHL zimejitosa kuhakikisha teknolojia inabadili huduma za posta kuwa rahisi zaidi.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi na jambo hili?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo kuhusu usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA
teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)

Uchumi wa Africa mpaka sasa hukua kwa kutegemea sekta za asili kama kilimoufugaji na biashara. Hata hivyo ujio wa teknolojia ya huduma za kifedha kwa njia ya kielektroniki (Fintech) utasaidia kwa kiasi kikubwa kuendesha uchumi katika kufanikisha maendeleo kiujumla. Sasa tuangalia teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech), zina mchango gani kwako leo?

Uchunguzi umeonyesha kwamba matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu za mkononi yameongezeka sana ndani ya miaka 10 iliyopita ambapo imeonekana eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara ndio limekuwa kinara wa kubuni na kutumia huduma hizi za kifedha kwa kutumia simu za mkononi duniani kwa sasa.

Utafiti uliofanywa na Shirika la Fedha duniani (IMF) umebaini kwamba takriban 10% ya pato la taifa katika miamala ya kifedha hufanyika kwa huduma za kifedha kupitia simu za mkononi. Hii ni matokeo bora zaidi ukilinganisha na 7% ya GDP katoka bara Asia na chini ya 2% ya GDP kutoka sehemu zingine za dunia.

Sasa swali, hii Fintechs ni nini!? Na ina manufaa gani kwa wafanyabiashara walio Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Shirika la EY linaifafanua FinTech kama Shirika/Kampuni inayojumuisha ubunifu katika utendaji wa biashara pamoja na technolojia ya programu za kompyuta katika kubuni, kuwezesha na kusambaza huduma za kifedha. Hizi FinTechs zinaweza kuwekwa kwenye makundi mawili;

i. FinTechs zinatoa huduma za kifedha e.g TALA App.

ii. FinTech zinazowezesha huduma za kifedha Vodacom na MPESA n.k (tutayajadili zaidi kwenye makala zetu zijazo)

Sekta hii ya FinTech katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara (SSA) inajumuisha zaidi ya makampuni 260 ambapo 80% katika hizo ni kampuni za ndani na 20% ni kampuni za kimataifa. Vile vile imeonekana idadi ya makampuni haya mapya imeongezeka katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) cha 24% ndani ya miaka 10 iliyopita.

Hata hivyo ripoti zinaonyesha kwamba Afrika Mashariki itaendelea kuongoza katika ukuaji wa sekta hii kwa 6.3% ya ukuaji wa uchumi mwaka huu 2019. Hii ni kutokana na Ethiopia, Rwanda, Tanzania na Uganda zote zinatarajia kurekodi pato la Taifa la zaidi ya 6% mwaka huu ambayo ni zaidi ya nchi zilizo maeneo mengine ya Africa. Hii ni kutokana na uwekezaji katika miundombinu na utanuzi wa huduma za kifedha na mawasiliano.

Takriban theluthi moja (1/3) ya michango ya harambee zilizofanyika barani Africa mwaka 2017 iliwezeshwa na kampuni za FinTechs. Hii inatiliwa mkazo kwa kuwa 60% ya akaunti za huduma za kifedha kwa njia ya simu duniani zimegundulika kuwepo katika eneo la SSA. Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliofanya na benki ya Ecobank.

Pia imeonekana sekta hii ya FinTechinaendelea kuwa imara katika muda wa miaka 3 kutoka makadirio ya dola za kimarekani 200 milioni mwaka 2018 hadi 3$ bilioni mwaka 2020. Kiasi kikubwa cha uwekezaji katika muda huu kimeonekana kuelekezwa KenyaNigeria na Afrika Kusini. Vile vile inategemewa kwamba kufanikiwa kwa Fintechs katika nchi hizo kutatanua mafanikio katika nchi zingine za Kiafrika.

MAENDELEO: Ujio wa FinTechs umebadili sana jinsi ya kufanya biashara duniani. Kutoka Crowdsourcing ambayo ni njia inayotumika kufanya usaili wa miradi mbalimbali mtandaoni kupitia intaneti na kupokea ruzuku, mpaka njia ya huduma za kifedha kwa njia ya simu. Wafanyabiashara na wajasiriamali hawajawahi kupata njia rahisi zaidi kwenye utandaji wa biashara zao kwenye maswala ya fedha kuliko hii.

Kupitia Fintechs sasa wafanyabiashara wanaweza kusambaza bidhaa/huduma kwa watu mbali mbali na kupata malipo ndani ya muda mfupi zaidi. teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) inazidi kujisombea watumiaji kwa sababu inaonyesha namna inavyoweza kusaidia katika kujikwamua kwenye maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni.

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH) HAINA MIPAKA:

Kutuma pesa nje ya mipaka ya nchi napo imekuwa rahisi zaidi. Mfumo huu ulioondoa mipaka ya kijiografia kwenye kurusha pesa umepunguza gharama kutoka ilivyokuwa mwanzo kwa njia ya benki ambayo ni ghali mno. Hivyo FinTech imewawezesha wajasiriamali na viwanda vidogo kutuma na kupokea pesa kwa gharama ndogo zaidi.

KUONGEZA THAMANI KATIKA UTOAJI WA HUDUMA ZA KIFEDHA: Eneo hili limetawaliwa na ubunifu ambao unawezesha kuongezeka kwa thamani katika matumizi ya huduma za kifedha. Kwa kuyumia malipo kwa njia ya simu, wateja walioko kusini mwa Jangwa la Sahara wanapata uwezo wa kupata huduma za kibenki kupitia simu za mkononi (mobile banking) pamoja na huduma zingine kama kugungua akaunti, kuchukua mkopo, kupata bima, kupata huduma za mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na masoko ya hisa. Haya yote kupitia FinTech yanawezeshwa kirahisi tuu katika simu yako ya rununu (smartphone) au laptop.

teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi. Umejifunza nini hapa katika teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) leo?

Zaidi unaweza kupitia makala hizi hapa chini ili kupata ufahamu mpana kuhusu biashara za mtandaoni:

  1. MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA
  2. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  3. UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-COMMERCE BUSINESS)?
  4. FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia comments section hapo chini;

UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-commerce BUSINESSES)?

Japokuwa imechelewa, lakini kwa sasa Africa ndio inaongoza mbio katika kufanya mapinduzi ya kidijitali kuliko sehemu yoyote duniani. Namna ya kufanya biashara inazidi kubadilika ikionyesha nia ya dhati kufanya maendeleo ya kiuchumi, miundombinu na maswala ya kijamii. Mwaka 2018 nchi wanachama wa Umoja wa Africa walipiga hatua kubwa katika mfumo wa kufanya biashara na muingiliano wa kiuchumi baada ya kuanzisha Eneo Huru la Kufanyia Biashara barani (Continental Free Trade Area AfCFTA). Eneo hili lililoanzishwa linashirikisha nchi 22 zilizoweka sahihi tayari na utekelezwaji wake ulipangwa kuanza mwaka 2019 (tayari umeshaanza).

Hata hivyo mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuzishirikisha nchi ambazo bado si wanachama wa eneo hili jipya, inatarajiwa eneo hili kufikia soko la watu takribani bilioni 1.2 barani wakiwa na jumla ya pato la ndani la taifa (GDP) la dola za kimarekani trilioni 2.5 kwa pamoja, kwa mwaka. Hii inatarajiwa kuwa ni mapinduzi makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nyanja ya uchumi wa Afrika.

Sasa, swali linakuja; Afrika(wafanyabiashara, makampuni/mashirika na Serikali) imejiandaa vipi na mapinduzi haya ya uchumi wa kidijitali? Na zaidi, watunga sera/sheria wataangalia vipi biashara za kielektroniki (e-commerce) kama mada muhimu katika eneo hilo jipya la kufanya biashara huru barani?

Tume ya kudhibiti uchumi wa Africa ya Umoja wa Mataifa (ECA) ikishirikiana na Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) pamoja na Baraza la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo ya kibiashara (UNCTAD) mwaka huu 2019 imechapisha ripoti yake ikiangazia maendeleo ya Afrika kiujumla katika nyanja za kiuchumi, siasa na kijamii.

URAHISI: Imeonekana kwamba e-commerce inaweza kufanya biashara ya bidhaa na huduma kwa urahisi zaidi ambapo itarahisisha mwenendo mzuri wa biashara kati ya wazalishaji, wafanyabiashra na walaji pamoja na kumbukumbu zao na miamala ya kifedha.

MITANDAO YA KIJAMII: Pia imeonekana kwamba e-commerce inapatikana na kufanyika kirahisi katika mitandao ya kijamii kama facebook na Instagram ambapo ndipo mahali kuna watumiaji wengi zaidi wa Intaneti duniani (zaidi ya watu bilioni 2 kati ya watumiaji bilioni 4 wa intaneti).

KUTOKUWA NA MIPAKA: Mfumo wa uchumi wa Kidijitali kiasili umetengenezwa kuepuka mipaka ya kijiografia katika kufanya biashara na kubadilishana fedha ambapo mabadiliko haya ya kiteknolojia yataongeza umakini zaidi katika mwenendo wa masoko na gharama. Lakini bado wimbi kubwa la watu watakaoshiriki kwenye soko barani wanaonekana wataachwa nyuma kutokana na kutokuingiliana kwa lugha na vita/ghasia za mara kwa mara katika baadhi ya jamii/nchi.

BIASHARA: Kwa mujibu wa UNCTAD mwaka 2016 kwa dunia nzima e-commerce iliweza kupitisha mauzoya takribani dola trilioni 26 ambapo 90% ilikuwa ni Biashara kwa Biashara (B2B e-commerce) na 10% ilikuwa ni Biashara kwa Mlaji (B2C e-commerce). Hata hivyo kupima mwenendo wa e-commerce katika baadhi ya nchi zinazoendelea imekuwa ni changamoto kupata data na takwimu, haswa katika nchi za Afrika.

IMPORTATION: Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kwamba Biashara kati ya nchi na nchi imekua kwa kiasi kikubwa Afrika ambapo zimechagizwa na vituo vichache vya kiteknolojia (Hubs) ambavyo vimerahisisha mno mwenendo wa biashara. Biashara kati y nchi na nchi (Intraregional import) imekuwa zaidi ya mara 3 katika miongo miwili iliyopita kufikia 12%- 14% sawa na dola bilioni 100 ikichagizwa na uwepo wa jumuiya za kiuchumi barani (Subregional Economic Communities REC‘s).

UZOEFU: Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na umri wa Jumuiya hizi za Kimaendeleo barani Afrika ambapo uzoefu huo hutumika kuongeza jitihada katika kuboresha namna ya ufanyaji biashara kuelekea uchumi wa kidijitali kiteknolojia. Uzoefu huo pia hutumika kuunganisha jumuiya moja na nyingine (mf, SADC na COMESAna EAC) ambapo zitazalishwa nafasi nyingi zaidi za kufanya biashara kati ya nchi wanachama na ripoti zinaonyesha 75% ya biashara hizi ndani ya jumuiya barani Afrika zimefanyika mwaka 2017 peke yake na nusu ya biashara hizo zilifanyika katika jumuiya ya SADC.

Chini ya mwavuli wa AfCFTA nchi wanachama zinatarajia kufuta tozo/ushuru kwa 90% ya bidhaa zote zitakazopitishwa na kufanyiwa biashara katika eneo hilo. Hii itaruhusu uwezekano wa kupunguza mlolongo wa kodi au kuongeza idadi na thamani ya bidhaa na huduma zitakazohusishwa. Matokeo yoyote katika punguzo hilo linalotarajiwa katika muktadha wa biashara kidijitali yataleta picha tofauti. Kupunguza mlolongo wa tozo za mipakani baina ya nchi na nchi kutapungua kwa 15% pekee ikitegemea thamani ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi husika. Hii ni kwa mujibu wa Tume inayoshughulikia Uchumi wa Afrika kutoka Umoja wa Mataifa (UNECA) mwaka 2018.

Sasa mwaka 2018 Jumuiya ya COMESA ilibuni mfumo wa kudhibiti eneo huru la kibiashara kidijitali (Digital Free Trade Area DFTA). Mfumo huu umeundwa na mambo yafuatayo;

•E-trade: Hili ni jukwaa mahsusi kwa ajili ya kufanya biashara za kimtandao na kuwezesha malipo ya kielektroniki, mobile apps kwa ajili ya wafanyabiashara walioko katika Jumuiya hio.

•E-logistics: hili ni jukwaa maalum kwa ajili ya kuwezesha biashara ya usafirishaji wa mizigo baina ya nchi wanachama wa jumuiya.

•E-legislation: huu ni mfumo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara rasmi ambao unawawezesha kufanya miamala na malipo kielektoniki.

Mfumo huu uliobuniwa na Jumuiya ya COMESA umelenga kutangaza biashara za wanajumuiya katika nchi wanachama ikijumuisha kupitia majukwaa ya e-commerce. Mfumo huu ulikuwa ni mfanano wa mfumo uliotengenezwa na kuzinduliw na nchi ya Malaysia mwaka 2017 katika muktadha wa kufanya biashara huru ndani ya eneo maalum.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.

Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana, shuka nazo:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-biashara-ya-fedha-za-kidijitali-cryptocurrency-business/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)”
  2. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia;

e-mail: info@rednet.co.tz

tovuti: https://rednet.co.tz

Simu:+255765834754

fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika

FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA TEKNOLOJIA YA 5G

Dunia ipo mbioni kuelekea zama za matumizi ya teknolojia ya 5G katika kasi ya Intaneti. Mpaka kufikia mwaka 2020 huduma za kibiashara za 5G zilishaanza kupatikana katika nchi zaidi ya 50 kutoka Asia, Ulaya, Mashariki ya Kati na Amerika ya Kaskazini. Muongo wa 2020s’ ndio unatajwa kushuhudiwa kwa usambazaji mkubwa zaidi wa teknolojia hii ya kasi ya intaneti duniani ikijumuisha nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara. Sasa leo kwa uchache uta fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika.

Kufikia mwaka 2022 tu tayari kampuni ya Vodacom Tanzania walishazindua huduma zao za 5G nchini na kuwa kampuni ya kwanza ya mawasiliano kuzindua huduma hizo. Hakika maendeleo ya teknolojia hii yanakwenda kasi sana.

Sasa ili kujua kwa undani kuhusu teknolojia hii pamoja na matarajio yake katika kufanikisha shughuli za kila siku za kibinadamu, kitengo maalum cha kijasusi katika shirika la GSMA kiliendesha ziara iliyohusisha wabia muhimu ili kupata maoni halisi ya watumiaji wa intaneti kuhusu ujio wa 5G katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara. Uchunguzi huo ulijumuisha maeneo sita ambayo ni; matumizi ya mtandao (network deployment), wigo wa mtandao (spectrum), watumiaji (use cases), mifumo ya biashara na fedha (business model and finance), sera na sheria (policy and regulations) pamoja na ushirikiano wa kibiashara na matokeo ya mbeleni.

Katika maeneo hayo walengwa waliojumuishwa walikuwa ni wasimamizi wa mashirika wa mawasiliano katika ukanda huo, kampuni za simu zilizo na hisa zaidi ya 75% kwa pamoja katika ukanda huo pamoja na wauzaji wa vifaa vya mawasiliano ambao wana hisa za zaidi ya 90% ya soko la miundombinu ya kimtandao katika ukanda huo.

Takwimu zilizotolewa na ripoti ya uchunguzi huo ambayo imechapishwa Mwezi July, 2019 zilitokana na uchambuzi wa maoni ya watu mbali mbali kuhusu 5G. Pia matokeo haya yamejumuisha data kutoka vyanzo mbali mbali vinavyohusiana na teknolojia hii ambapo wataalamu waliounda na kendeleza teknolojia hii wataangalia kwa makini watumiaji wa mfumo huu katika ukanda wa kusini mwa Jangwa la Sahara, lengo kuu likiwa ni kujifunza na kujiimarisha zaidi kutoka kwa vinara wa 5G.

Teknolojia za kidijitali zimekuwa muhimu sana katika shughuli za kibinadamu za kila siku. Hii ni muhimu zaidi katika nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo kama teknolojia hizo zisingekuwepo mambo yangekuwa magumu zaidi kutokana na ubovu na uchakavu wa miundombinu, maswala ya fedha pamoja na ujuzi binafsi wa mtu. Sasa ripoti hio iliyotengenzwa kutokana na uchunguzi wa kitengo cha Intelijensia cha shirika la GSMA imekuja na majibu kadha wa kadha;

MAPINDUZI KATIKA KASI YA INTANETI YA 5G YAMEFIKA:

Kufikia mwisho wa mwaka 2019 kulishakuwa na mtandao mkubwa wa kasi ya 3G na 4G zaidi kuliko 2G katika ukanda huo wa kusini mwa Afrika. Hii inaonyesha ukuaji kutoka huduma za sauti mpaka huduma za data. Uwekezaji unaoendelea kufanyika katika 4G umepeleka ukubwa wa huduma za mitandao kufikia robo ya jumla ya watu waishio katika ukanda huo. Vile vile imeonekana kwamba matumizi ya simu za rununu (smartphones) yameongezeka mara mbili ndani ya miaka mitano iliyopita.

jinsi ya kuanzisha website umuhimu wa tehama.fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika

TEKNOLOJIA YA 5G ITAKUWA NI SEHEMU YA MIUNDOMBINU BORA YA KIMTANDAO, JAPO UENEAJI WAKE HAUTAKUWA WA KASI SANA:

Katika ukanda huu, teknolojia ya 5G haizuiliki. Ni maendeleo ya kiasili kutoka katika teknolojia zilizopita. Japokuwa, kasi ya ueneaji wa teknolojia hii ya 5G si kubwa katika ukanda huu kutokana na uwepo wa teknolojia zingine kama 3G na 4G bado zina uwezo wa kumsaidia mwanadamu kufanya shughuli zake katika kasi inayoridhisha ya intaneti.

Takribani theluthi mbili (2/3) ya walioshiriki kwenye uchunguzi huu wanatarajia huduma za kibiashara za 5G kuwa katika masoko yao kabla ya mwaka 2025. Pia teknolojia hii itasaidia kupevuka na kuweza kutumika katika masoko mengine. Vile vile itaruhusu uchumi kukua kwa kutumia teknolojia ya 5G katika vifaa vya kielektroniki ambavyo vitapunguza gharama za waendeshaji na wateja. Hapa ndipo tuta fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika kwa undani wake kabisa.

UTAYARI WA SOKO NI MUHIMU KATIKA KUKUZA THAMANI YA TEKNOLOJIA YA 5G:

Kwa nchi zote zilizo katika ukanda huu utayari wa soko ni jambo muhimu zaidi kufanikisha mageuzi ya teknolojia ya kasi ya 5G. Hii itasaidia kukuza thamani katika huduma za 5G kwa wateja, waendeshaji na jamii nzima kwa ujumla. Kiwango cha utayari wa soko kinaonyesha kwamba baadhi ya nchi zinakwenda kasi kwenye matumizi ya teknolojia hio kutoka 4G.

Kufikia mwaka 2025 huduma zinazotumia teknolojia yenye kasi ya intaneti ya 5G itafikia nchi 7 zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara ikijumuisha ni Kenya, Nigeria na Afrika Kusini. Pia uchunguzi umetabiri kuwako kwa miunganiko milioni 28 ya simu kwa kutumia 5G, sawasawa na 3% ya jumla nzima ya miunganiko ya kimtandao ya simu katika ukanda huo.

MASHIRIKA NA MAKAMPUNI MAKUBWA YATAONGOZA KUANZA KUTUMIA 5G KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA:

Teknolojia ya 5G itawezesha makampuni ya mawasiliano na mashirika kuhudumu vizuri zaidi kwa wateja wao ambapo watumiaji wa mwanzoni watawezeshwa na huduma ya wireless (Fixed Wireless Access #FWA) ili kutoa changamoto kwenye matumizi, gharama na upatikanaji wa huduma za kimtandao kama huduma za satelaiti na intaneti. Hapa sasa ndipo uta fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika kwa ukaribu zaidi.

KWA WATEJA NA WATUMIAJI ITAKUWA NI ZOEZI LA MUDA MREFU:

Hii ni kutokana na udhaifu katika upatikanaji wa huduma/vifaa(simulaptop..) bora Kwa gharama nafuu pamoja na ujuzi wa matumizi ya teknolojia kama virtual reality (VR) na Augmented Reality (AR). Ubora wa vifaa kama simu za rununu (smartphones) na kompyuta ni muhimu zaidi katika zama za 5G kwa matumizi ya wateja lakini inategemewa malengo ya teknolojia hii ni kufikia vifaa vya nyumbani (Customer Premise Equipment CPE) kama routers ili kupata huduma za uhakika za wireless (FWA).

Hii ni kwa kuwa huduma hizo hupatikana kwa malipo ya kabla kutoka kwa makampuni ya simu, ambapo katika muda huo huo huduma ya kasi ya 4G itaendelea kuhudumu kwa kasi inayoridhisha na kuwafikia watumiaji wengi zaidi ambao watachangia ukuaji mzuri wa uchumi.

KIPAUMBELE KITAWEKWA KATIKA KUPATA UHAKIKA WA HUDUMA YA WIRELESS (FWA):

Ukuaji wa Matumizi ya intaneti katika vifaa kama simu na kompyuta ni mdogo mno ambao ni chini ya 2% katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara, hivyo kufanya ujio wa zama za 5G kuegemea kwanza katika CPE’s. Hii itapunguza gharama za uendeshaji lakini pia itaongeza watumiaji kwa kutumia wireless (FWA). Mbinu hii ya kufikisha teknolojia kwa jamii inalenga kwa suluhu mbadala kwa makampuni ya mawasiliano kulinganisha gharama za kuhudumia/kufikia simu moja moja na uwezo wa watumiaji wengi kuelekea zama za kasi ya 5G.

fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika

Hio ndio mantiki ya mada yetu ya leo katika ku fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika, kwa ufupi. Unataka kujua zaidi? Karibu uwasiliane nami kwa njia ya WhatsApp kupitia namba hii hapa 0765834754 Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo hapa. Zitakusaidia sana ukizipitia:

  1. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  2. TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI
  3. FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA DUNIANI
  4. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?