Tag: siri ya kufanikiwa katika kuwekeza

jinsi ya kuanzisha website

JINSI YA KUANZISHA WEBSITE

Japokuwa anafanya vizuri mno katika biashara ya kusambaza vifaa vya miundombinu ya maji (mabomba, koki, elbow n.k) huku akipata tenda nyingi kupitia mfumo wa TaNEPS, lakini alitamani sana jinsi ya kuanzisha website na kufikisha bidhaa zake kwa watu binafsi mbali na serikali na mashirika ya kimataifa ambayo amekuwa akifanya nayo kazi. Katika stori hii ya leo utashuhudia siri za kuzingatia jinsi ya kuanzisha website ili biashara yako izidi kushamiri huku mtandaoni. Makinika.

Sasa jamaa yetu huyu yuko busy sana na hio miradi yake kiasi kwamba hana muda wa kuandika makala kwenye mitandao au kupush hashtags au kutweet na kupost mara kwa mara kuhusu huduma anazotoa. Hata hivyo aliazimia kufanya kazi na watu binafsi, mahoteli, shule binafsi, hospitali n.k.

Huwa anazunguka nchi nzima akifanya kazi na serikali na mashirika ya kimataifa kuhakikisha miundombinu ya maji safi na salama inafika kila kijiji. So kwa nature ya kazi yake, tunaweza kusema jamaa hana Time Advantage ya kutumia mitandao ya kijamii ili watu binafsi waweze kumfahamu, kumuamini na kufanya nae kazi. Hata hivyo experience yake imemfanya aaminiwe na serikali pamoja na mashirika yanayotumia mfumo wa TaNEPS. LAKINI; Jamaa yetu huyu bado alitamani kufanya kazi na watu binafsi, afunge mabomba kwenye nyumba binafsi, hoteli, bar n.k hata hivyo bahati mbaya watu binafsi hawatumii mfumo wa TaNEPS katika kutafuta huduma/bidhaa wanazohitaji. So jamaa akafanyaje?

Mwaka 2018 akafungua ecommerce website ambayo baada ya mwaka mmoja website ile ilishindwa kumletea matunda yale aliyotarajia. Akaishia kusema, “Nilifunga website lakini haikuniingizia hata mia kwa mwaka mzima, nikaamua kuachana nayo.” Hii imeshawahi kukukuta wewe? tuambie kwenye comment hapo chini.

faida za teknolojia ya S.E.O katika biashara

Kama unajua uchungu wa kuwekeza na kuvuna hasara nadhani utakuwa umemuelewa jamaa hapo. So mwaka huu 2022 nikakutana na huyu jamaa yangu, anaitwa Steven (tumuite Stivu leo), akanieleza kuhusu kiu yake ya kufanya kazi na watu binafsi na namna alivyopata hasara ya website mwaka 2018.

Katika maongezi yetu alitamani kutumia Nguvu ya Intaneti na Mitandao ya kijamii ili aweze kufanikiwa katika kuwafikia watu binafsi ukizingatia jamaa yupogo busy na TaNEPS + kukusanya materials na kuzifikisha site hivyo kumfanya asiwe na muda na kuweka updates mitandaoni.

Ushauri huu utakufaa hata wewe, zingatia sana:

1. Hakikisha unafahamu ndani nje kuhusu soko la watu wenye njaa na huduma zako: Hapa Stivu ana advantage upande mmoja kwa kuwa tayari anaaminiwa na serikali na mashirika ya nje. Kimbembe ni watu binafsi. So unapaswa kuwajua wateja wako kwa kupost/kutweet kuhusu bidhaa/huduma zako na thamani unayoitoa kwa mteja pindi atakapoamua kufanya kazi na wewe ajue kabisa kwamba bidhaa/huduma yako itakwenda kumtatulia changamoto yake flani. Hii inapaswa kufanywa mara kwa mara ili kusudi kuchuja na kuwapata watu wanaokufuatilia (followers) na kuwafanya wakujue, wakuamini na baadaye wafanye kazi na wewe.

jinsi ya kuanzisha website
umuhimu wa tehama

So hapa Stivu ali #FuataUshauri kwamba anapaswa kutafuta mtu wa kumsaidia kuhakikisha biashara yake inatengeneza ushawishi kwnye mitandao ya kijamii kwasababu yeye mwenyewe hawezi kufanya kila kitu afterall. Hii inaitwa LEVERAGING.

2. Hakikisha jina la biashara yako (Brand Name) ni rahisi kutamkika na kinahusiana na wateja wako:

Hapa kwa Stivu hakukua na shida, lakini kwako wewe inawezekana hujafahamu kuhusu hili. Imagine una mgahawa wa chakula halafu unakuta umeandikwa JOY ELECTRONICS. Imagine yani.

Hii kitu ukitaka kufanikiwa zaidi hakikisha Brand Name yako ipo clear from the beginning, hasa linapokuja swala la Online Business ambapo huku mtandaoni kuna makelele mengi mno. Sema kabisa JOY RESTAURANT (Food Providers in Arusha). Hii itakusaidia kukufanya uwe specific na ujulikane exactly unafanya biashara gani na unapatikana wapi kabla hata mtu hajaanza kujiuliza zaidi.

Hii pia inaipa biashara yako advantage pale mtu anapotaka kufika ofisini kwako kupitia Google Map. Mteja hasumbuki yani kuuliza uliza njiani au kuwa na hofu ya kupotea.

3. Fanya Kazi:

Hata kama tayari biashara yako imeshasimama physically, lakini kama unataka kuihamishia biashara hio mtandaoni; Huna budi kuwekeza muda wako katika kudadisi kuhusu Wateja, Washindani wako ni kina nani, wanafanya nini kufanikiwa kuteka masoko na wewe ufanye nini.

Hivyo, roughly ndani ya miezi 6 ya kwanza unatakiwa kuwekeza masaa 60 kwa wiki (wastani wa masaa 8 kwa siku) ili kuchunguza na kujua namna ya kuandika copies zitakazofanya bidhaa/huduma zako ziuzike mtandaoni. Copies hizo zinaweza kuwa ni makala, tweets, fliers etc.

jinsi ya kuanzisha website
jinsi ya kufanikiwa mtandaoni
umuhimu wa tehama
asiyefanya kazi na asile

Ujuzi huu wa COPYWRITING ni muhimu sana na ukiwa tayari kujifunza huwezi kushindwa kuuweza. Hii ndio sumaku ya kunasa wateja huku mtandaoni sasa. Lazima uhakikishe unaandika kile ambacho mteja wako atakiadika akiwa anatafuta suluhisho la changamoto zake.

Kwenye maandishi yako maneno kama “Faida za Tehama”, “Kirefu cha TEHAMA”, “Jinsi ya kuwa na mwonekano mzuri”, “Jinsi ya kufanikiwa katika biashara ya chakula”, “Faida za website”, “mbinu za kutumia Mitandao ya kijamii”, “jinsi ya kuanzisha website”, “mbinu za kufanikiwa katika kilimo”, “nguo za bei nafuu”, “Ofa ya Sikukuu”, “Makosa 10 usiyotakiwa kufanya katika…” nakadhalika.

Ukitazama hapo utagundua maneno hayo ndio haswa huandikwa kwenye mitandao mbalimbali pale mtu anapotafuta kitu fulani, si ndio? Basi na wewe katika maandiko/copies zako hutakiwi kuyaacha kabisa kwa sababu ndo sumaku yenyewe hio.

4. Zifahamu hatua za awali za kufanya S.E.O:

Kwenye makala zetu zilizopita tumejadili kuhusu Teknolojia hii ya S.E.O inavyoweza kuimarisha biashara yako pindi pale mteja anapotafuta huduma kupitia mtandao wa Google. Pitia hapa kwenye tweet yetu kama ilikupita hii hapa chini.

Awali umeona aina za maneno ambayo unapaswa kuyatumia mara kwa mara katika maandiko yako ili kuwanasa wateja wengi zaidi huku mtandaoni. Katika S.E.O maneno hayo huirahisishia google katika kuchambua keywords na kuzipandisha juu pale mtu anapotafuta tarifa. Hivyo, website yenye keywords nyingi ndio huchaguliwa kirahisi katika mtandao wa google na kuwekwa juu ili mtu anapotafuta basi website hio inatokea kwenye nafasi za juu kabisa. Fikiria mtu ameandika “Jinsi ya kupika chakula kizuri cha ndizi” au “jinsi ya kuanzisha website” na mara links za website yako ya mgahawa wa chakula inatokea ya kwanza kabisa pale google. Inafurahisha eh?

Fahamu kwamba mtu hataandika jina la biashara yako pale google akiwa anatafuta suluhisho kwa changamoto zake. Watu hawajali kuhusu jina la website yako hata, watu wanajali kuhusu namna ya kutatua changamoto zao ndio maana ni rahisi sana mtu kuandika hizo keywords nilizokutajia mifano yake hapo awali na hayo maneno ndio haswa hutumika katika S.E.O kuinua website yako mtandaoni. Unahitaji kuyatumia sana maneno hayo katika website yako.

Kwa kifupi unaweza kufanya S.E.O kwa website ya biashara yako mtandaoni kwa Kuilocate kwenye Google Map, Kusajili akaunti za Google My Business na Search Console. Hii itaifanya website yako iweze kuwa-ranked na Google kwenye nafasi za juu pindi mtu atakapokuwa anatafuta huduma.

5. Fahamu kuwa kufanikiwa kupata watembeleaji wengi kwenye website yako (Organic Traffic) kunachukua muda (walau miezi 6 mpaka mwaka):

Katika muda huu unatakiwa ufanye kazi ya kuweka maudhui, kuandika Keywords zinazovutia wateja (copywriting inaingia hapa), kufanya maintenance ili kuhakikisha website yako ina-run kwa kasi mda wowote mtu akiifungua.

Pia ni muhimu kutengeneza Backlinks. Hizi ni links za website yako ambazo zinaatikana kwenye websites na majukwaa mengine ya mtandaoni mf: umeandika makala halafu unaenda kui-share ZoomTanzania, LinkedIn au unaweza kuomba wadau wako wakashare links zako kwenye accounts zao za twitter, medium, facebook au hata kwenye websites zao kama wanazo. Ndio maana tunasisitiza kujenga Business Relationships, yaani uwe na uhusiano mzuri na wafanyabiashara wenzako humu mtandaoni ndo utatoboa.

Kuhusu namna unavyoweza kuifanya website yako iweze kutembelewa na watu wengi zaidi tumeshakuandalia makala maalum hii hapa chini:

KUMBUKA:

Marekebisho ya website huwa hayaishagi daima. Hii ni kwa sababu Teknolojia inabadilika kwa kasi sana na wewe kama mfanyabiashara hutapenda kuona website yako inaonekana vilevile tangu mwaka juzi. Ndio maana unatakiwa kuzurura mtandaoni na kutizama website zingine uone ziko vipi na ujitathmini unawezaje kuhakikisha website yako inaonekana MPYA, bora na yenye kukidhi matakwa ya wateja wako muda wote ili ufahamu jinsi ya kuanzisha website kabla hujafanya makosa zaidi.

Fahamu tu kwamba hutengenezi website kwa ajili yako, HAPANA. Unatengenza website kwa ajili ya wateja wako wapate kitakachowasaidia. So hudumu kwa nguvu zako zote huku ukiongeza maarifa kila leo.

Website yako ndiyo RECEPTIONIST wa ofisini kwako. Hakikisha anapendeza na ana taarifa zote ambazo unataka mteja wako akija azipate.

We jiulize kwanini mara nyingi Wanaume hawakuwagi Receptionists?

Utagundua “Receptionist LAZIMA awe mrembo haswa. Lazima avutie mteja kutaka kuuliza jambo”.

Hiyo kwanzia leo nategemea utakuwa ukiitizama website yako kwa jicho la tofauti na iliyokuwa hapo kabla. Kufahamu Kwanini umiliki website ya biashara yako tafadhali fuatana na makala hii kwa kugusa alama ya link hapa chini:

Kupata website yako imara na mahsusi kwa ajili ya kuimarisha biashara yako huku mtandaoni tafadhali wasiliana nasi kwa kututumia ujumbe kupitia kitufe cha Whatsapp unachokiona kwenye ukurasa huu.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

M-PESA LIPA NAMBA
thamani vs gharama, nafuu iko wapi? fahamu siri za kuweza kushawishi wateja katika biashara yako.

THAMANI vs GHARAMA, NAFUU IKO WAPI?

Ubora wa kazi una thamani kubwa sana kuliko gharama za kuifanya kazi hio. Unaweza lipia mradi kwa milioni 5, lakini usikupe matokeo yale ulijipangia mwanzoni. Pia unaweza lipa laki 5 ya mradi na ukapata matokeo mazuri zaidi. Ufanyeje? Je kati ya thamani vs gharama nafuu iko wapi? Fuatilia makala hii mpaka mwisho kufahamu zaidi.

Warren Buffet ambaye ni mbuji kabisa katika buruji la uwekezaji duniani amewahi kunukuliwa akisema “Price is what you pay, value is what you get.” akimaanisha, “Gharama ndio unayolipa, thamani ndio unayopata”. Kifupi ni kwamba thamani ndio msingi wa bidhaa/huduma huku gharama ikiwa ni makubaliano ambayo yanatangulizwa na muuzaji.

Kujua tofauti kati ya Gharama na Thamani ni moja kati ya mbinu bora zaidi za kufanya Uwekezaji. Zaidi kuhusu uwekezaji tayari tumeshakufahamisha SIRI ZA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA Ukishazifahamu hapo tuendelee..

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

umuhimu wa tehama

jinsi ya kufanikiwa katika biashara za mtandaoni

Unaposhindwa kutofautisha kati ya Gharama na Thamani kama mfanyabishara unajiweka kwenye mtego wa kukosa wateja, kutoaminika kwa Wawekezaji wakubwa, Kupoteza points dhidi ya washindani wako kibiashara na mwisho kuiweka biashara yako katika majanga ya kudhoofika na hatimaye kufa.

Unawezaje kupata bidhaa zinazouzwa kwa gharama za chini kuliko thamani yake halisi?

Jibu ni kufanya tathmini kwa kutumia viwango vya bei ambazo ni tofauti kabisa na gharama zinazotangazwa sasa. Hapa unaweza kuangalia bei, miaka 3 iliyopita ilikuaje na miaka 3 ijayo itakuwaje.

Bwana Phil Town, ameweka zoezi la kufanya Tathmini makini kwa kupitia hatua nne alizoziita “Four M’s“. Tuzione chap chap:

1. MEANING: Hatua ya kwanza kabla hujawekeza katika bidhaa/huduma fulani lazima ujiridhishe kuwa bidhaa/huduma hio ina maana sana kwako. Ikiwa na maana utapata fursa ya kuichunguza na kuielewa vyema, na kujituma ipasavyo katika kufanya biashara hio.

2. MOAT: (Upekee ambao hauwezi kuigwa na wengine): Unapochagua bishara ya kuwekeza ama bidhaa/huduma, unatakiwa uifanye iwe katika mtindo ambao washindani wako hawawezi kukuiga. Mfano: Duniani kuna makampuni mengi tu ya vinywaji laini (soft drinks) lakini Coca cola ni moja na itaendelea kubaki hivyo.

Hivyo hebu tuambie hapa biashara yako ina utofauti gani ambao washindani wako hawawezi kuiga kamwe?

3. MANAGEMENT: Je wajua kuwa Chanzo kikubwa kwa biashara kufa ni watu wanaoiendesha? Hivyo unapofikiria kuwekeza kwenye biashara lazima eneo ya utawala na uendeshaji wa shughuli linasimamiwa na watu wenye Weledi, Waaminifu na wanaojali maisha ya biashara hio.

4. MARGIN OF SAFETY: Kama umeshajiridhisha na hizo hatua 3 zilizopita, sasa hebu tizama pia namna unaweza kuweka mtaji ama kununua hisa bila kupoteza pesa na uhakika wa pesa yako kurudi.

Kila biashara inahitaji kitu fulani ambacho kitaitofautisha na washindani wake wengine sokoni. Sasa mchakato wa kutafuta tofauti hizo inaitwa “Positioning”. Hii mbinu inaziwezesha biashara kukazia sehemu fulani ya soko/wateja ili kujiimarisha zaidi kwenye sehemu hio. Unafanyaje?

MBINU ZA KUFANYA POSITIONING:

1. KUPUNGUZA GHARAMA: Ukifanya uchunguzi vizuri sokoni hasa kwenye mitaa ambayo wanafanya biashara ya aina moja mf: Kariakoo kila mtaa una shughuli yake maarufu zaidi kama mtaa wa livingstone ni maarufu kwa vyombo vya ndani.

So ukijigundua kuwa upo kwenye aina hii ya biashara, mbinu bora hapo ni kupunguza gharama za bidhaa zako kwa kiwango kidogo kuliko washindani wako. Lengo ni kuhakikisha unakuwa na mzunguko wa haraka wa mauzo ya bidhaa/huduma zako kwa faida ndogo ili mzigo wako uishe mapema.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Je kati ya thamani vs gharama, nafuu iko wapi?

2. UBORA: Kama unataka kujitofautisha na washindani wako, basi mbinu bora na ya kuaminika ni kuhakikisha bidhaa/huduma zako ni za Ubora wa hali ya juu. Unapozingatia Ubora unajiweka kwenye nafasi ya kupata wateja wa kuaminika, wateja wa kudumu na wateja wa uhakika katika biashara.

3. MAKUNDI YA KIJAMII (DEMORGRAPHIC): Baadhi ya biashara huamua kujihusisha na makundi fulani tu ya kijamii ili kujiletea faida zaidi. Mfano: kwenye TV na redio vinatengenezwa vipindi mahsusi kwa Vijana, watu wa makamu na watu wa dini fulani kwa siku zao. Umeshawahi fanya hii?

Mbinu hii inafaa sana pale unapoyapata makundi hayo karibu na eneo lako la biashara au watu wanaokufuatilia zaidi mtandaoni wakawa ni wanamna hio. Vinginevyo unajiweka kwenye hatari ya kukosa soko kubwa nje ya hao uliolenga kuwahudumia.

4. HUDUMA BORA: Huwa inatokea kwa baadhi ya biashara ushindani unakuwa mkubwa sana kiasi kwamba mbinu 3 tulizoziona awali haziwezi kufanya kazi. Yani watu wanashikana kooni haswa. Hapa ndipo mbinu ya kutoa Huduma Bora kwa wateja inapokuja kuleta tofauti.

Zoezi la kutoa Huduma Bora ni pana na linahitaji ubunifu mwingi. Na hii inatoa fursa kwa biashara kubuni namna nzuri ya kuhudumia wateja wake ili kuhakikisha wateja wanafurahia bidhaa/huduma na kuzidisha mauzo. Mfano: unaweza kuanzisha dawati la wateja kutoa maoni live ili waweze kuona mawazo yao yakifanyiwa kazi. Unaweza kuanzisha kurasa za mitandao ya kijamii ili kukusanya kero za wateja na kuzifanyia kazi vizuri. Pia unaweza kutengeneza mzunguko kwa wateja wako kushiriki kama mabalozi wa kuitangaza biashara yako kwa watu wengine. Unaionaje hii?

UNAWEZA VIPI KUDADAVUA NA KUWASILISHA THAMANI YA BIASHARA YAKO KWA MTEJA WAKO?

Tafiti zinaonyesha kuwa watu hawapendi kabisa kutangaziwa ama kulazimishwa kununua kitu hasa huku mtandaoni. Mfano: Tizama unavyopata kero pale unapoangalia vidio YouTube mara katikat linakuja Tangazo Ama pale unataka kufungua ukurasa fulani mara unafunguka ukurasa wa tangazo kwanza kabla hujafika pale ulitaka kwenda. Hio kero ndio inatakiwa ikufanye uitazame biashara yako katika jicho la Kitaalamu kwa kutatua changamoto na si la Kibiashara kwa kuuza Bidhaa/huduma yako.

Unapotoa Elimu katika namna ya Utaalam wa kutatua changamoto fulani, unamfanya mteja atake kuondokana na kero zinazomsumbua kwa kutumia Bidhaa/Huduma zako. Hii ni tofauti kabisa pale unapotaka kuuza bidhaa. Ukifanya hivyo hutatui changamoto bali unakuwa kero kwa mteja.

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

gharama vs thamani, kipi kinafaa zaidi?

Thamani ya Biashara yako inaonekana katika kutatua changamoto za mteja wako na Urahisi wa kutumia bidhaa/huduma yako. Hivyo lazima uhakikishe kuwa unachokitangaza ni Ile Namna na hisia ya Bidhaa zako zinaweza kutatua changamoto fulani ya mteja kwa urahisi.

Pia lazima uhakikishe suluhu yako inakwenda sambamba na hisia za mteja wako. Kwa kuwa kitaalam watu hununua bidhaa/huduma kutokana na hisia walizo nazo muda huo. Mfano kuna watu watakwambia kuwa wakiwa na hasira ama furaha sana kwao huo ndo muda wanafanya shopping kubwa zaidi.

Mzazi anapotaka kununua keki ya birthday ya mwanae hanunui tu keki tamu, lazima pia ahakikishe keki hio inakwenda kum-suprise mtoto kwa muonekano wake wa kuvutia. Ni mbinu ya kihisia hapo inatumika. Hivyo unapotaka kuongeza Thamani ya biashara yako unatakiwa kuzingatia hilo pia.

Umejifunza nini kwenye makala hii kuhusu thamani vs gharama, nafuu iko wapi? Tafadhali weka maoni au mtazamo wako katika sehemu ya comments hapo chini..

Vyanzo: https://www.forbes.com/sites/forbesfinancecouncil/2018/01/04/the-important-differences-between-price-and-value/?sh=133fd5c94237

https://www.weebly.com/inspiration/difference-between-value-and-cost/

https://yourbusiness.azcentral.com/different-types-strategies-business-1348.html

FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRICA

Kwa mara ya kwanza katika Historia ya mwanadamu, zaidi ya nusu ya watu wote duniani wanatumia huduma za internet. Na katika maeneo yote, imeonekana huduma hizo zinakua kwa kasi zaidi barani Africa. Idadi ya watu wanaotumia internet imeongezeka sana barani Afrika kutoka 2.1% mwaka 2005 mpaka 24.4% mwaka 2018. Sasa leo nataka u fahamu mchango wa ICT katika maendeleo ya sekta binafsi barani Africa. Twende sambamba.

Huduma hizi za internet zimekuja kurahisisha shughuli za kiuchumi kama kurahisisha njia za malipo (bank, MPESA, tigopesa nk), matumizi ya drones katika matibabu kama inavyofanyika nchini Rwanda, matumizi ya smartphones katika kuongeza maarifa ya kitaaluma na kiufundi stadi na kuongezeka kwa biashara za mtandaoni (e-commerce businesses, network marketing and online businesses). Bill Gates amewahi kuandika katika moja ya tweets zake “If your business is not on the Internet yet, Your are out of the Business.” Mwenye macho haambiwi ona.

SEKTA BINAFSI, INJINI YA UCHUMI AFRIKA

Kama ulikua hufahamu, basi sekta binafsi ndio imetawala Uchumi wa Afrika kwa kuwa zaidi ya 80% ya uzalishaji mali mzima hufanyika katika sekta hio. Zaidi, theluthi mbili (⅔) ya uwekezaji mzima barani na robo tatu (¾) ya jumla ya mitaji katika uchumi kati ya mwaka 1996-2008 imeonekana kutokea katika sekta hio binafsi. Vile vile sekta hio inatoa 90% ya ajira zote kwa vijana walio katika umri wa kufanya kazi. Mchango wa biashara za ndani katika sekta binafsi katika GDP ilikua 59% katika nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara ukilinganisha na 30% ya nchi za Latin America na Caribbean, 32% Asia Kusini na 42% katika Mashariki ya Kati. Hii inaonyesha kiasi gani Afrika sekta binafsi inalipa maradufu. Umeiona nafasi yako hapa ndugu yangu mfanyabiashara.!?

Kujiimarisha katika Sekta binafsi, huna budi kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kila mara unapohitajika kufanya hivyo. Unawezaje kufanya maamuzi sahihi katika changamoto zinazokukabili? Tafadhali fuatana nasi katika makala hii hapa FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI.

Katika nchi za Uchumi wa kati, kampuni binafsi hufanya kazi katika mfumo wa sekta rasmi, ambapo makampuni makubwa na yale madogo (SME’s) huzalisha hisa za thamani katika uwekezaji na zaidi, ajira kwa vijana ambao ndio kundi kubwa zaidi katika nguvu kazi barani Afrika. Lakini zaidi, sekta binafsi katika nchi hizi hufanya â…” ya uzalishaji mzima.

Uchumi huwa na ushindani pale kunapokuwa na ushindani mkali wa kibiashara. Na biashara huwa na ushindani pale:

•Sheria zinapokua sawa na haki.

•Wafanyakazi wana maarifa stahiki.

•Gharama za uendeshaji (umeme, maji, mafuta, usafiri) zinakuwa nafuu.

•Wateja wanafikika kila kona.

ICT INAINGIA VIPI HAPO?

Uchumi wa kidijitali umekuwa dhima kuu ya kidunia na Afrika haijabaki nyuma katika hili. Matumizi ya teknolojia yanazidi kushika kasi barani yakichagizwa na kasi ya ueneaji wa huduma za internet ambapo biashara nyingi zinazidi kuhamia mtandaoni kirahisi. Mpaka kufikia mwaka 2015 tu tayari watu 557 barani walikua wanatumia simu ya mkononi ambayo ni 12% ya watumiaji wote wa simu duniani huku idadi hio ikikusanya 6% ya mapato yote yaliyofanyika duniani wakati huo.

Sasa leo wacha tuone maeneo muhimu ya ICT yanayokuza uchumi zaidi;

1. TELECOMUNICATIONS

Eneo hili linajumuisha makampuni makubwa ya mawasiliano. Kwa kiasi kikubwa hufanya shughuli zake katika utaratibu wa sekta rasmi, hivyo kuwafikia watu wengi na kufanya kazi karibu zaidi na mamlaka za serikali. Makampuni kama Vocacom, MTN, Tigo, Airtel na TTCL yapo hapa. Kutokana na kuwa na watumiaji wengi, makampuni haya huchangia kiasi kikubwa katika mapato ya kiserikali kama kodi na gawio huku yakichangia sehemu kubwa katika kukuza uchumi wa watumiaji wake kutokana na fursa zinazopatikana katika huduma wanazozitoa kama uwakala wa huduma, huduma za kifedha nakadhalika.

2. SOFTWARE AND IT CONSULTING

Hapa ndo utatukuta sisi sasa ambao tunakuhudumia wewe muda huu. Zaidi ya kukupatia taarifa hizi ghafi, pia eneo hili la ICT hutoa huduma za kutengeneza mifumo ya computer, Apps za simu, Ushauri na Uchambuzi wa kiteknolojia katika Biashara na Uchumi. Japokuwa sio maarufu sana lakini sehemu hii inachangia uchumi wa mabiashara mbalimbali, makapuni madogo na yale yanayokuwa (SME’s) pamoja na sekta zingine za uma na binafsi kwa kutoa huduma za matengenezo ya tovuti, mifumo mbalimbali ya kibiashara, huduma za afya, elimu, uhifadhi wa data pamoja na uchambuzi na ushauri wa biashara mbalimbali kiteknolojia zaidi.

3. DIGITAL SERVICES

Hapa utawakuta watu wanaotoa huduma za kidijitali ambao wengi wao hufanya kazi kwa ukaribu na makampuni ya mawasiliano. Watoa huduma hawa pia wanahusika kutengeneza mifumo ya makampuni ya mawasiliano pamoja na kutengeneza/kuendesha mitandao ya kijamii zaidi. Watoa huduma hawa wamekuwa wakitengeneza michezo ya video pamoja na kutoa huduma za WebHosting na Cloud services kwa makampuni ya Kiafrika. Kampuni kama Dudumizi Technologies(Tanzania), ISB North Africa (Morocco), Web4Africa (Ghana) na Domains Africa Technologies (Kenya) zipo hapa.

4. INFORMATION SERVICES

Hapa sasa ndio utazikuta redio na televisheni zote unazozifahamu. Hawa kwa jina lingine wanaitwa Watoaji wa Maudhui, ambapo hutafuta habari na maudhui wanayodhani yanafaa kwa wateja wao na hivyo kukusanya jamii ili ipate maudhui hayo huku yenyewe yakijipatia faida yake katika matangazo mbalimbali ya kibiashara yanayoruka sambamba na maudhui yao. Hapa unaweza kunitajia Redio/TV ambayo ina maudhui unayoyapenda yakienda sambamba na matangazo ya wadhamini wa vipindi vyao. Usishangae ukiona hivyo. Kwenye matangazo ndo wanapopatia pesa wenzio, usione unapata bure maudhui hayo.

Kwa uchache haya ndio mambo ya fahamu mchango wa ICT katika maendeleo ya sekta binafsi barani Africa yanayochangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa Uchumi wa Kidijitali na kuboresha biashara nyingi zaidi kila kukicha barani Afrika. Jiulize, unayatumia vipi maeneo haya katika kukuza biashara yako wewe kama mjasiriamali?

Makala hizi hapa chini zitakusaidia kufahamu kwa undani namna sekta binafsi zinachangia uchumi na maendeleo ya wafanyabiashara hasa vijana wa Afrika Mashariki. Gusa links kisha makinika:

  1. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE (TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?
  2. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  3. UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA

Usisahau kutoa maoni yako kuhusu ukichojifunza katika makala hii ya leo na unaweza kusambaza ili kuhakikisha ulichijifunza kinawafikia wengine. Pia unaweza kutembelea tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz kuhakikisha unaendelea kupata taarifa sahihi kuhusu uchumi na biashara yako kiteknolojia. Asante.

Makala hii ni Kwa Heshima ya Hayati B.W. Mkapa aliyekuwa Rais awamu ya 3 nchini Tanzania. Mzee Mkapa aliongoza Taifa kuelekea zama hizi za maendeleo ya Sekta Binafsi kupitia Sera yake ya Ubinafsishaji wa mali za umma zilizokua mzigo kwa serikali, hivyo kuchochea ukuaji wa sekta binafsi kwa kiasi kikubwa mpaka kufikia hivi ilivyo leo. Mzee aliona mbali sana. #RIPMkapa

FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA

Watu wengi hufikiri kwamba Kuwekeza ni swala la kupata Utajiri ndani ya muda mfupi, Kustaafu mapema au kupata gawio (interest) kubwa kila baada ya muda fulani kwa haraka. Ukweli ni kwamba Kuwekeza sio chanzo cha kukufanya ushinde unakula upepo wa bahari, kutumia pesa hovyo(kula bata) au kusafiri vile unataka. Usikariri maisha, leo makinika mpaka mwisho wa makala hii ili uweze ku fahamu siri ya kufanikiwa katika kuwekeza.

Watu wanafanya kazi sana ili kupata pesa, na kazi zaidi kutunza pesa. Lakini wachache sana ndio hugundua njia bora zaidi ya kutengeneza na kuzungusha pesa katika biashara zao. Leo hii nitakujuza mambo 10 muhimu ya kuzingatia katika UWEKEZAJI (INVESTING) kwa mafanikio ya biashara yako hio hio unayoifanya/unayotaka kuifanya.

Kuwekeza zaidi katika biashara dhumuni lake ni kuhakikisha biashara yako ina uwezo wa kujiendesha yenyewe hata bila ya wewe kuwepo hapo ofisini kila siku. Sasa ili kuweza kufikia lengo hilo inatakiwa ile energy ambayo mjasiriamali anakuwa nayo wakati anaanza uwekezaji wake wa kwanza ndio hio hio anatakiwa kuwa nayo hata pale anapofanikiwa. Kama misuli inayohitaji mazoezi ili iwe mikubwa na yenye nguvu, the same kwenye biashara yako. Biashara inahitaji muendelezo wa uwekezaji ili kuleta matokeo yenye tija. Vitu kama Mtaji, Masoko, rasilimali watu, connection, wafanyakazi n.k, vinahitaji kukua sana. Hii ni muhimu sana katika ku fahamu siri za kufanikiwa katika kuwekeza popote pale duniani.

Sasa kifupi ni kwamba kuna aina nyingi sana za Uwekezaji duniani (Stocks, Bonds, Real Estate, Commodities n.k). Lakini leo tujadili kuhusu Uwekezaji kwenye Biashara Unayoifanya/Unayowaza kuifanya (kuuza viatu, nguo, chakula, furnitures n.k) Hapa nitakuwa nimekupa kitu unachohitaji sana, si ndio?

Kama umeshawahi kujaribu basi utakubaliana namimi kwamba Kutunza Fedha kwenye kibubu, chini ya godoro, benki, mpesa, tigopesa ni ngumu kweli kweli. Halafu kibaya zaidi, pesa sio kiumbe hai, usitegemee ukiichimbia itazaliana.

Hizi hapa ni njia Bora za kuwekeza na kuzungusha pesa yako vizuri ili uweze fahamu siri ya kufanikiwa katika kuwekeza:

1. FIKIRIA MBALI:

Unapotaka kuwekeza kwenye biashara yako, waza hivi; mwaka 2030 au 2040 nitakuwa katika hatua gani kibiashara? nataka niwafikie watu/wateja/maeneo mangapi mpaka mwaka 2030/2040? Ukiwa na mipango ya mbali katika biashara yako unapata energy ya kusimamia vizuri na kufanikiwa. Kila mafanikio huanzia kwenye fikra na mipango thabiti.

2. ANZA KUWEKEZA KILE ULICHONACHO:

Watu wengi hasa vijana wanapenda kufanya biashara lakini wanalalamika changamoto ni Mtaji. Fahamu, biashara ni kama ile siku mpenzi wako anapokupa taarifa za mimba. Niambie hapa kama ulianza kulea mimba kwa milioni 1 kwa mwezi ule wa kwanza. Utagundua ni ngumu. Hali kadhalika biashara yako inahitaji kulishwa kidogo kidogo kwanzia ingali ndogo.

Unailisha biashara kwa vitu kama Maarifa, aina bora za bidhaa/huduma zinazotakiwa, wapi pa kuzipata, aina za wateja, taarifa sahihi nk. Pesa ni kitendea kazi muhimu lakini tambua pesa ni sehemu ya mtaji tu.

3. WEKEZA PALE UNAPOPAWEZA

“Baba yako hawezi kukufanya uwe tajiri, wala mama yako, wala rafiki yako, wala mwalimu, wala serikali, badala yake ni wewe mwenyewe wa kubadili maisha yako ukianza na namna unavyofikiria (mindset)” Maneno sumu ya jamaa yangu SirJeff Dennis. Hapa nataka kuongelea Uwezo wako specifically. Wewe unaweza kufanya nini katika kiwango kikubwa? Na unaweza vipi kutumia huo uwezo kwa manufaa? Jitambue wewe kwanza.

4. JIFUNZE NA FANYA UCHUNGUZI

Hili swala sio la kufanya mwanzoni wakati unaanza biashara halafu unakuja kuacha mbeleni, Hapana. Kama ilivyo kuwekeza hakuna mwisho kwenye biashara yako, hakikisha pia Unaendelea kujifunza mbinu mpya na kufanya Uchunguzi kuhusu biashara mbalimbali mara zote kabla hujawekeza. Ishi nayo hii kwa sababu Elimu haina mwisho.

5. TENGENEZA NA FANYA KAZI KWENYE TIMU

Kuna mtu mmoja aliwahi kusema “Kama huwezi kutengeneza pesa ukiwa umelala, huwezi kuwa tajiri”, Ni kweli kabisa. Mimi nakuongezea, kama kwenye Uwekezaji wako, wewe ndo kila kitu, hio biashara haiwezi/ni ngumu sana kukua. Gawa majukumu, sio kila kitu unataka kufanya wewe, uzalishaji wewe, marketing wewe, customer care wewe, presentations wewe. Utafeli, hakikisha mfumo wa biashara yako unaweza jiendesha wenyewe hata usipokuwepo.

 fahamu siri za kufanikiwa katika kuwekeza.

fanya kazi kwenye timu

6. KUWA NA MSIMAMO (CONSISTENCE AND RESSILIENCE)

Biashara yako ili iweze kukua na kufanikiwa dhidi ya ushindani wa masoko, dhoruba za kiuchumi, teknolojia nk, Unapaswa kuwa na msimamo/consistency. Wazungu wanasema “Practice makes perfect”. Hutakiwi kukata tamaa, licha ya changamoto ambazo unaweza kukutana nazo kila siku, hakikisha unaendelea kuzalisha/kuhudumu, tafuta wateja wengi zaidi, jisahihishe, jitangaze, pambana. Uwekezaji unakuhitaji uwe na ngozi ngumu kwelikweli kwa sababu katika kuwekeza kuna nyakati za kuanguka na kukata tamaa, sasa hakikisha unao uweza wa kusimama na kuendelea kupambana.

7. KUWA MWOGA PALE WENGI WANAPOKUWA WALAFI

Ulimwengo wa Uwekezaji katika biashara unaendeshwa kiakili na kijasusi sana. Usiwe bendera kufuata upepo, Usiwe mtu wa kufuata mkumbo. Ni afadhali kuwa mwoga na kuishi miaka mingi, kuliko kuingia vitani bila maandalizi, hutachukua raundi. Tulia, changa karata zako vizuri na kwa mipango sahihi.

8. KUWA AGGRESSIVE PALE WENGI WANAPOKUWA WAOGA

Sehemu pazuri zaidi kuwekeza ni pale mahali kuna changamoto nyingi. Uwekezaji wako unapotatua changamoto hapo ndo pakutoboa kabisa. Kuna mahali hamna maji wapelekee hapo, hamna chakula, fungua mgahawa. Pambana na changamoto za wateja wako. Wasikilize wateja wako wanahitaji nini kila wakati kwa sababu kwenye maumivu ya wateja wako ndipo mafanikio ya uwekezaji wako yalipo. Shikilia hapo.

9. PUNGUZA MATUMIZI YASIYO NA ULAZIMA

Fahamu kuwa katika biashara yako kila shilingi ina mchango muhimu katika Uwekezaji endelevu. So hakikisha unazingatia matumizi yale muhimu zaidi katika uwekezaji. Hili zoezi ni gumu lakini linawezekana ukiweka Nia ya Kukuza Biashara yako.

10. TAWANYA UWEKEZAJI/DIVERSIFY

Ili kuhakikisha biashara yako inakuwa na misuli ya kiushindani, lazima Utawanye uwekezaji wako. Unauza nguo kwa sasa, ongeza na viatu, soksi, vipodozi na jitahidi ufungue matawi mikoani. Kama unauza mbao, ongeza karakana za fenicha maeneo mbalimbali, TANUKA.

fahamu siri za kufanikiwa katika kuwekeza.

11. TUMIA VIZURI TEKNOLOJIA

Katika eneo muhimu la kuzingatia katika kufanya uwekezaji wa kibiashara, basi hakikisha unatumia vyema teknolojia katika maana ya kutumia kwa usahihi Mitandao ya kijamii, tovuti bora ya biashara yako, software za kutunza hesabu nakadhalika. Eneo la teknolojia ni pana, hivyo nimekuwekea mambo muhimu ya kuzingatia katika makala hizi hapa chini:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  4. MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA
  5. MBINU ZA KUWEZA KULIFIKIA SOKO LA MTANDAONI

NOTE: Uwekezaji katika biashara ni jambo endelevu, kama mtoto mdogo, “kadiri ya umleavyo ndivyo akuavyo.” wamesema wahenga. Ukizingatia mambo haya bila shaka bishara yako itakuwa na afya tele. Tafadhali sambaza makala haya kwa yeyote aliye karibu yako na usisite kucoment hapa chini.

Je umeweza fahamu siri ya kufanikiwa katika kuwekeza katika biashara yako kupitia makala hii ya leo? Niambie katika comments hapo chini.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) â€“ 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

siri ya kufanikiwa katika kuwekeza.