Tag: siasa

focus on your plans and make sure you win.

UKWELI KUHUSU ‘PROPAGANDA’

Wengine watakwambia ni maneno ya uchochezi, wengine “siasa za uhuni hizo”, wengine wanaita figisu, mara fitna. Lakini Propaganda ni mada inayowasilishwa kwa lugha ya picha katika mawasiliano ambayo mara nyingi hubebwa katika kampeni mbalimbali kwa agenda fulani ya kificho. Leo sasa tuone huo ukweli kuhusu ‘Propaganda’. Ni upi? Makinika.

Serikali na mashirika mbalimbali hufanya Propaganda katika kusukuma Agenda zao ambazo zina lengo la kushawishi jamii na kuchochea mapokeo ya kihisa kuhusu jambo fulani. Propaganda zilizokomaa hugeuzwa kuwa utamaduni, mfano Propaganda ya kuagamiza maadui wa “Ujinga, Maradhi na Umasikini” imesababisha watu wengi kwenda shule kupata elimu, kutibiwa kwa tiba za kisasa na kuachana na zile za kizamani pamoja na kufanya kazi kwa lengo la kuboresha hali ya kiuchumi. Ujinga, Maradhi na Umasikini vimeonekana ni adui wa kumuangamiza kabisa mbele ya kila mwananchi sasa na hii imesababishwa na Propaganda za serikali ya awamu ya kwanza katika kufikia lengo hilo.

Kwa upande mwingine Propaganda zimekuwa zikitumika kufanyiana hila za kisiasa katika kumkandamiza mpinzani ili kupata ushindi katika kinyang’anyiro fulani. Mfano kwenye michezo unaweza kumwona @hajismanara ambaye ni mmoja kati ya wana propaganda wazuri sana nchini. Maneno yake, tambo na kampeni anazozifanya kwa kiasi kikubwa ziliisaidia sana @SimbaSCTanzania na Yanga Kupata ushindi hata kabla ya mechi. Propaganda zinapigwa kwa kiwango sana hapa.

Kwingine ni kwenye ulingo wa siasa ambapo huku ndo Propaganda zilipozaliwa (kama wanavyosema Mapenzi yamezaliwa Tanga). Kwenye siasa mara kadhaa Propaganda zimekuwa zikipigwa kukandamizana kisiasa na kuaminisha umma kuwa fulani ni bora zaidi kuliko fulani, na sera hii ni bora zaidi kuliko sera hii. Ili kuweza kujenga ushawishi kwa wapiga kura, wanasiasa wamekuwa wakipiga propaganda za hali ya juu ili kuhakikisha wanapata ushindi. Ukiona mwanasiasa fulani anapendwa sana na ana wafuasi wengi, basi kwa kiasi kikubwa tambua Propaganda zake ni za kiwango cha juu sana.

Hata hivyo kufanya Propaganda si Dhambi, wala hakuna mtu anakatazwa kuzifanya isipokuwa tu usivunje sheria za nchi. Kuna baadhi ya watu huamini kuwa Propaganda ni Maneno ya Uongo na Ulaghai, Hapana. Propaganda ni sanaa ya kushawishi watu wafuate dhana fulani ili kuleta faida kwa mtu au jamii ya watu fulani, kampuni, shirika au serikali.

MBINU ZIPI HUTUMIKA KUFANIKISHA PROPAGANDA?

Mafanikio ya kufanya propaganda huja pale serikali/biashara fulani inapotumia mbinu hizi katika kushawishi jamii kufikia lengo fulani ambalo halionekani wazi kwa mara moja.

i. NJIA YA USHIRIKA (BRANDWAGON): Hii wahenga wanakwambia “Ndege wafananao huruka pamoja” au “Ukitembea na mwizi na wewe utakuwa mwizi”. Njia hii ni ile ambayo mpigapropaganda kujihusanisha na walengwa kwa ukaribu katika kuhakikisha propaganda zake zinakuwa na ushawishi. Najua umeshawahi kuona namna wanasiasa au makampuni wanavyotumia watu wa kitengo cha Masoko katika kuwafikia walengwa wao. Mara nyingi mpigapropaganda hubadili mavazi kuendana na walengwa, wakati mwingine huongea lugha ile inayozungumzwa na walengwa kabisa ili kuhakikisha propaganda zake zinakuwa na ushawishi unaotakiwa.

Pata huduma za Website, SEO, Social Media Marketing na nyinginezo nyingi kutoka Rednet Technologies Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?
ukweli kuhusu 'Propaganda'

ii.KUTAFUTA HURUMA YA JAMII (SNOP APPEAL): Hii ni njia maarufu sana ambayo kwa kiasi kikubwa imekuwa ikitumika katika kutengeneza story ambayo itagusa moyo wa jamii na kuhamasisha watu kukubali Agenda ambayo imebebwa katika propaganda hio. Inakuwa hivi, mtu hueleza story yake ambayo mara nyingi huwa ni ya kusikitisha, kwa lengo (linaloonekana) la kuhamashisha watu kutokata tamaa au kujenga uaminifu juu yao na hivyo kupata lengo (lisiloonekana) la kupata wafuasi, wateja au/na kura. Propaganda hii hufanywa sana na wasanii, wafanyabiashara na kampuni zinazoanza(startups). Umeshaanza kuuona hapa ukweli kuhusu ‘Propaganda’.

iii. MANENO YENYE UJAZO: Wahenga wanasema, “Maneno yanaumba”.Hii ni kwasababu maneno yana nguvu sana linapokuja swala la mahusiano ya kijamii. Ndio maana wanapropaganda hutumia maneneo yenye ujazo kubadili mtazamo wa jamii. Hapa wanapropaganda hutumia maneno matamu sana kushawishi jamii katika kufanya jambo fulani. Hali kadhalika wanapropaganda hutumia maneno ya hasira, chuki, fitna na hila ili kuhakikisha Agenda zao za siri zinafanikiwa. Wakati mwingine agenda hizo huwa na manufaa mema kijamii na wakati mwingine huja na lengo la kubomoa jamii.

Mathalani sisi Rednet Technologies tunakwambia, #WeGiveYouTheWorld hatuna maana kuwa tutakupa dunia kama ilivyo, hapana. Dhima yetu ni kuhakikisha tunakupatia taarifa zote muhimu kuhusu Biashara na Uchumi katika muktadha wa kiteknolojia ikiambatana na ushauri wa kitaalam.

Ili kuhakikisha wajasiriamali wadogo wanaimarisha biashara zao kupitia Matumizi ya teknolojia za kisasa kama Websites bora, softwares na chambuzi zisizokauka za kitaalam kupitia tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz. Tufuatilie uendelee kuimarisha biashara yako.

iv. KULINGANISHA DHANA: Wanapropaganda hutumia njia za kulinganisha dhana zao na matukio ya historia katika kupata kile wanachokidhamiria. Mathalani, katika siasa, watu wengi hupiga propaganda za kulinganisha hotuba za Mwalim Nyerere na matukio yanayoendelea katika kupush agenda zao.

Katika nyanja ya kibiashara, makampuni na mashirika hulinganisha maendeleo ya Kiteknolojia/Uchumi na uwezo wao wa kisasa katika kushawishi na kupata wateja wengi zaidi kila leo. Lakini chumvi ikizidi sana hapa, propaganda hizo hugeuka utapeli na kupoteza wateja kwa haraka sana.

v. NJIA YA SHUHUDA: Katika kufanya propaganda kwa njia hii makampuni na mashirika wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kuongeza wateja wapya na kukuza mauzo kwa viwango vikubwa sana. Makampuni/Mashirika yamekuwa yakiwatumia wasanii na watu mashuhuri kwenye jamii katika kueneza propaganda zao kuhusu huduma wanazotoa, bidhaa, kufungua matawi mapya ya ofisi pamoja na kufungua kampeni zao mbalimbali. Mara nyingi wasanii/watu mashuhuri wanaotumiwa kueneza propaganda hizo hawana elimu/taaluma kuhusu jinsi bidhaa/huduma inayoenezwa ilivyobuniwa/ilivyotengenezwa. Wao kikubwa ni kuhakikisha huduma/bidhaa hio inauzwa na kuketa faida kwenye kampuni/shirika hilo. Hapa ndipo unadhihirika ule ukweli kuhusu ‘Propaganda’.

mteja mshirikishe kwenye maamuzi. Msaidie aweze kununua huduma au bidhaa yako.

ukweli kuhusu 'Propaganda'

Hata hivyo mbinu hio inaweza kutumiwa kwa kupitia Masoko ya kimtandao (Network Marketing) au/na masoko kwa njia ya mitandao ya kijamii (social media marketing) ambapo mtandao wa twitter, facebook na LinkedIn imekuwa ikiongoza kwa kuwafanya watu washirikishane bidhaa/huduma zao. Mathalan kupitia twita, unaweza kusambaza bidhaa/huduma zako kwa kupitia watu ambao hawana ujuzi wa kutengeneza hizo bidhaa/huduma zako. Mfano sisi @RednetCompany tunasambaza huduma zetu kupitia rafiki zetu katika mitandao ya kijamii Ambao hata hivyo wengi kati yao hawana ujuzi kuhusu jinsi ya kutengeneza website, computer maintenance n.k. Lakini Agenda inayobebwa katika propaganda hio ni kuhakikisha tunahudumia Wafanyabiashara na watu wengine wengi zaidi kila leo.

Hivyo ukiwa kama mfanyabiashara hakikisha propaganda zako unazifanya kwa utaalam na weledi bila kufanya ulaghai au kusema uongo ili kujipatia faida. Kwa maana hio si njia bora ya kufanikiwa kipropaganda. Jipange vema kwenye uwanja huu uliosheheni ushindani wa kila namna.

Vile vile tayari hapa tumekuandalia makala ambazo zinarandana na somo ulilojifunza leo. Gusa links hizi kufahamu zaidi:

  1. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021?
  3. FAHAMU SIRI YA KUWEZA KUSHAWISHI WATEJA KATIKA BIASHARA YAKO
  4. UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Umejifunza nini katika makal hii ya leo kuhusiana na ukweli kuhusu ‘Propaganda’? Tafadhali toa maoni yako kupitia comments hapo chini, nasi tutayafanyia kazi mara moja.

FAHAMU KUHUSU MAGEUZI YA ICT KATIKA UWANDA WA SIASA

Ama kwa hakika teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA/ICT) imeendelea kushika kasi katika nyanja mbalimbali za kijamii. Biashara zinazidi kuimarika, Jamii inaunganika, uchumi unainuka na Siasa inapata sura mpya. Muunganiko wa Siasa na Teknolojia unagusa michakato, wasifu za watu, jitihada za kujinasua katika changamoto mbalimbali pamoja na harakati zingine za kijamii zinazohusidha matumizi ya huduma za intaneti na ICT. Katika fumbo hilo wataalamu wa siasa wakagundua njia za kuboresha mifumo ya kisiasa na kuratibu ushawishi wao katika jamii kirahisi zaidi.

Sasa leo tuone maeneo 5 muhimu ambayo ICT imekuwa chachu ya maendeleo katika uwanda wa kisiasa barani Afrika, hususan Kusini mwa jangwa la Sahara:

1. KUBADILI TAWALA

Katika kipindi cha mwaka 2009-2012 katika nchi za kiarabu kulitokea kitu kilichoitwa “Vuguvugu la Kimapinduzi” au “Arab Spring” ambapo serikali nyingi za kiarabu zilijikuta zikipinduliwa kwa nguvu ya wanachi. Kufikia mwaka 2012 dunia ilikua na 61% ya nchi 195 ambazo ndizo zilikua zilitambulika kwa kufanya Chaguzi za Kidemokrasia. Hio ni sawa n nchi 118. Lakini bada ya hapo nchi zinazojiendesha kidemokrasia ziliongezeka kufuatia maandamano nchini Moldovia mwaka 2009, Tunisia (2010/11, Misri (2011) na Iran (2009 mpaka sasa) Mapinduzi hayo ya kubadili tawala hasa zile za Kiimla yalipangwa na kuanzishwa kwa msaada wa kiteknolojia huku mtandao wa Twitter ukihusika kukusanya na kuhamasisha watu kuanzisha vuguvugu la maandamano katika nchi za kiarabu. Hawa waarabu walijua kwelikweli kutumia mitandao.

2. KUTUNGA NA KUENDESHA SERA

Hivi sasa hakuna mtu asiyejua au kutumia mfumo wa malipo ya kiserikali wa eGovernment. Sasa unajua mfumo huo ulianzia wapi? Achana na siasa kabisa. Kwanza tuone hio eGovernment ni kitu gani? Huo ni mfumo wa matumizi ya ICT katika ofisi za umma inazohusisha mifumo ya kiutawala ya kiuweledi inayotumia maarifa na ujuzi wa computer na huduma za intaneti ili kuhakikisha huduma za kijamii zinaimarika na kuchochea demokrasia na nguvu ya ushawishi katika chaguzi za kisiasa na sera za jamii. Umeona siasa imerudi tena apo Wahenga wanakuambia, “Siasa ni kama maji tu, usipoyaoga utayanywa.” Wahenga bwana. Sasa mifumo hii ya eGovernance hutumiwa na taasisi za serikali katika kuhudumia Mashirika mengine ya kiserikali (G2G) mfano Polisi na TRA, Mashirika ya Kiserikali kwa wanachi(G2C) mfano LUKU na Mashirika ya Serikali kwa Biashara (G2B) mfano TRA na Wafanyabiashara. Hii sera ys kuanzishwa kwa mifumo ya eGovernance japo imeanzishwa kwa sera za kisiasa lakini imeleta mapinduzi makubwa sana katika zoezi la ukusanyaji wa mapato na utunzaji wa rekodi za mauzo na manunuzi.

3. SIASA KAMA SIASA

Japokuwa kwenye nchi nyingi haswa zile za kidikteta kumekuwepo na makatazo ya kufanya siasa za wazi, Matumizi ya Teknolojia na mitandao ya kijamii yamewezeshwa kufanyika kwa siasa pasi na haja ya kukusanya watu viwanjani. Matumizi ya mifumo ya computer na mitandao ya kijamii wamewsrahisishia Wanasiasa kutengeneza akaunti zao zinazowapa fursa ya kukutana na wananchi na kufanya siasa kirahisi sana. Hata hivyo hii bado ni changamoto kwa nchi nyingi zinazoendelea kama Tanzania ambapo watumiaji hai wa huduma za internet walikua ni 23.14milioni sawa na 38.7% ya wananchi wote. Pia watumiaji wa mtandao wa facebook wamefikia 4.27milioni. Taarifa hii ni kwa mujibu wa tovuti ya http://internetlivestats.com kufikia mwezi December, 2019. Sasa namba hizi zinakupa picha gani katika uwanda wa siasa nchini? Inaonekana kuwa bado watumiaji hai wa mitandao ya kijamii ni wachache kuwakusanya mtandaoni kwa wakati mmoja, hivyo kufanyika kwa siasa katika mitandao ya kijamii inaonekana bado ni mtihani kwa wanasiasa barani Afrika hasa nchini Tanzania. Licha ya changamoto hizo, bado teknolojia inao mchango wake katika siasa wakati wa kufanya kampeni na uchaguzi ukizingatia Haba na Haba hujaza kibaba. Hivyo katika kampeni za kisasa, ili mwanasiasa apate kuingia katika mfumo wa utoaji wa maamuzi wa Taifa (Legislative level). Hana budi pia awe na ushawishi wa kisiasa katika mitandao ya kijamii. Huko ndipo unakutana na wanachi kirahisi na kusambaziana taarifa mbalimbali kwa wepesi zaidi. Kama afanyavyo Mh. Hamis Kigwangwala tu katika mtandao wa twitter, interractions za mara kwa mara muhimu nyie.

4. ONLINE VOTING (e-Voters System)

Kama ulikua hujui basi mwaka 2005 nchi ya Estonia iliweka rekodi ya kuwa nchi ya kwanza duniani kutumia mfumo wa kimtandao wa upigaji kura (e-Voters System)na kwanzia hapo mfumo huo umekuwa ukisambaa katika nchi na maeneo mbalimbali duniani. Mfumo huu unahusisha sehemu 3 ambazo ni Mpiga Kura, Mamlaka za Usajili na Watu wa Kuhesabu Kura ambao wote hapa sasa hufanya kazi katika mifumo maalum ya kuhakikisha kura zinapigwa kimtandao na kwa usahihi na usalama wa hali ya juu. Hapa bwana usipokua makini wadukuzi wanaweza kupiga tukio uchaguzi ukaharibika ndani ya dakika kadhaa tu.

KWANINI ONLINE VOTING SYSTEM?

Wakati mfumo huu unatengenezwa na kuzinduliwa kwa mara ya kwanza nchini Estonia, lengo kuu lilikua ni kuhakikisha shughuli za uchaguzi zinafanyika kwa haraka, wepesi na kwa usahihi zaidi bila kuathiri shughuli zingine za kiuchumi. Lakini leo hii ambapo dunia inapitia katika changamoto ya Ugonjwa wa #COVID19, ipo haja na hitaji kubwa la matumizi ya e-Voters Systems katika chaguzi za kisiasa sehemu mbalimbali duniani. Wakati mamlaka zikikataza mikusanyiko ya watu, uvaaji wa barakoa, kutogusana na kuzingatia social distance (sijui kiswahili chake kwa kweli), hakuna wakati sahihi wa kuanza kutumia e-Voters Systems kama sasa. Wanaharati na wananchi kwa ujumla hatuna budi kupigia chapuo mgumo huu uanze kutumika mara moja ikiwezekana kuanzia uchaguzi wa Octoba 2020 sio tu kuhakikisha tahadhari dhidi ya Coron zinachukuliwa, lakini zaidi kuongeza Usahihi na Usalama wa kura katika zoezi la Uchaguzi.

5. MATUMIZI NA UCHAMBUZI WA DATA

Teknolojia kwa mapana yake imekua nyenzo muhimu sana katika kukusanya, kuchakata na kuhifanyi data mbalimbali ambazo hutumika maeneo kadha wa kadha katika kufanyia Tafiti, Kupima mwenendo wa mwanasiasa au chama pamoja na kuhifadhi kumbukumbu. Sasa matumizi ya mitandao kama Facebook, Instagram, Twitter pamoja na tovuti/blogu za wanasiasa/vyama, zimekuwa zikichochea sana juhudi na harakati zao katika kuhakikisha wanaboresha nafasi na ushawaishi wao wa kisiasa katika jamii wanazohudumu. Teknolojia imezidi kuwa muhimu sana katika uga huu wa kisiasa.

BONUS POINT:

Matumizi madogo ya teknolojia (hafifu) yameleta madhara makubwa sana katiks mifumo ya siasa hasa barani Afrika. Hizi vita za wenyewe kwa wenyewe, vurugu na wakati mwingine mauaji katika mchakato wa uchaguzi ni matokeo ya siasa mbovu na ufinyu wa teknolojia usiotakiwa.

Pia kuna hizi makala hapa tayari tumekuandalia ambazo zitakupa mwanga zaidi katika kufanya maamuzi na kutumia teknolojia ili kuleta tija zaidi. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/fanya-maamuzi-sahihi-katika-muda-sahihi/ yenye kichwa “FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI”
  2. https://rednet.co.tz/ifahamu-nguvu-ya-mitandao-ya-kijamii/ yenye kichwa “IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO”
  3. https://rednet.co.tz/biashara-yako-inaweza-vipi-kuwa-taasisi-imara/ yenye kichwa “BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA”