Tag: sekta binafsi

cloud data storage

MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA

Teknolojia ya Internet of Things (IoT) inakuja kwa kasi sana. Mtandao wa Gartner uliripoti kuongezeka kwa vifaa vinavyounganishwa na huduma za internet kufikia 26 bilioni mpaka mwaka 2020. Sasa haya mageuzi ya intaneti (IoT) katika biashara na maisha ya mchango gani? Fuatana na makala hii mpaka mwisho kuahamu zaidi.

Leo hii utakapomaliza kusoma makala hii utafahamu kiundani juu ya namna Teknolojia ya Intaneti katika Vitu (Internet of Things au IoT) inavyoweza kubadili Biashara yako pamoja na vifaa vya kielekroniki unavyotumia nyumbani ama ofisini.

Maeneo kumi (10) muhimu ambapo mageuzi ya intaneti (IoT) katika biashara na maisha, inakwenda kuyagusa na kuleta mabadiliko makubwa katika mazingira ya kazi na jamii. Namba 7 itakushangaza sana:

1. IoT itapofika kwenye ubora wake wa matumizi, biashara nyingi zinazofanyika leo zitapotea sokoni. Mf: biashara za ugavi na usambazaji ambazo kwa sasa hutumia mtu wa tatu katika kufanya usafirishaji/usambazaji, hizi zitaweza kujiendesha kiautomatiki, yaani ukiagiza kitu mtandaoni inakupa namna ya kukufikishia bidhaa/huduma popote bila hata kujieleza. Fikiria upo Magomeni na unaagiza mafuta mtandaoni kutoka Singida, unapotoa oda yako tu, huna haja ya kusema uko wapi, unapokea zako tu ujumbe kuwa “mafuta yako yatakufikia siku fulani saa fulani mahali fulani (Mahali ambapo unakuaga muda mwingi). Life’s Simple.

mageuzi ya Intaneti (iot) katika biashara na maisha.Jihudumie leo kutoka Rednet Technologies.

2. Moja kati ya athari hasi za IoT ni pamoja na kumlazimu mtumiaji kuhakikisha vifaa vyake vinavyotumia intaneti na vilivyoungwa katika teknolojia ya IoT vinakuwa updated muda wote. Hii itaongeza gharama za bando japokuwa “Mtaka cha uvunguni sharti ainame.”

3. Mpaka kufikia 2025 soko la IoT linatarajiwa kuwa na thamani ya kati ya 3.9 $ mpaka 11.1$ trilioni kwa mwaka. Vihisishi (Sensors, RFID na Bluetooth devices) vinatajwa kuchukua zaidi ya 50% ya matumizi ya IoT vikifuatiwa na huduma za Teknolojia ya Habari (IT). hapa ndipo utakapoona sasa mageuzi ya intaneti (iot) katika biashara na maisha kwa ujumla.

4. Soko la Biashara Kwa Biashara (B2B IoT Market size): 2015: soko lilikuwa na thamani ya $195 bilioni na kufikia mwaka 2020 soko lilifikia thamani ya $470 bilioni ikiwa ni ongezeko la zaidi ya dola bilioni 250 ndani ya miaka mitano tu. Yaani IoT imeimarisha sana mapato katika biashara katika nyanja za mifumo ya udhibiti, uchambuzi wa data, vifaa, network na huduma bora. IoT imekuwa mkombozi haswa.

Mfano mzuri hapa ni mifumo ya ukusanyaji kodi ya TRA. Mifumo hio imefanywa imara katika kudhibiti makusanyo ya kodi kupitia mashine za EFD ambazo zimeungwa kielektroniki ili kuwapa TRA data sahihi za kodi.

mageuzi ya intaneti (iot) katika biashara na maisha.

5. Ukuaji wa IoT unaathiriwa kwa kiasi kikubwa na maendeleo ya Teknolojia zingine. Mfano: Teknolojia ya mawingu (cloud tech) inavyokuwa na IoT nayo inakuwa sambamba. Pia IoT inasambaa kwa kasi pale uwezo wa mitandao unaposambaa zaidi. Kifupi ni ngumu kuzuia kasi ukuaji wa IoT duniani.

6. IoT itapofikia ubora wake kwenye matumizi, inatarajiwa kuwezesha kufikia vifaa vingi kwa kutumia kifaa kimoja. Fikiria unarudi zako home, ukifika nje unawasha taa za nyumba, then unawasha feni, TV na sabufa yako na kuzima Friji yote kwa kutumia simujanja yako tu yani.

7. Unazijua RFID’s? Hizi kitaalamu zinaitwa Radio-Frequency Identifications. Yani vifaa vyenye uwezo wa kuratibu utambulisho wa bidhaa/huduma. Mfano vile vitochi unaviona ukienda supamaketi pale kabla hujalipia, bidhaa yako inamulikwa na mwanga flani hivi ili kujua bei. Sasa kile kitochi kinaitwa RFID scanner. Hizi skana zipo za aina nyingi kwa minajili ya kutambua bidhaa/mtu, zingine zipo viwanja vya ndege kukagua mizigo, watu na pasi za kusafiri.

RFID’s zinahusika vipi kwenye IoT?

Teknolojia ya IoT sasa inaziwezesha hizi RFID’s katika sekta ya Ugavi na Usafirishaji ili kutoa data sahihi kuhusu ubora na idadi ya bidhaa zinazosafirishwa na kutumiwa. Kupitia IoT bidhaa inaweza kujulikana ipo wapi na lini imenunuliwa inapopita kwenye skana ambayo hutuma taarifa sahihi za bidhaa kwa mtengenezaji. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa RFID’s katika nyanja ya Biashara na Uchukuzi tafadhali gusa link hii MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI

8. Namba ya Vifaa vya kielektroniki vinavyoweza kuwasiliana pasi na kuingiliwa na mtu M2M (Machine To Machine) inatajwa kuongezeka kwa kasi kubwa ndani ya muda mchache tu. 2018 kulikua na vifaa 1.5 bilioni na mwaka 2020 viliongezeka kufikia 2.6 bilioni. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya mtandao wa Statista.

9. IoT ndio suluhisho sahihi katika kutoa huduma bora zaidi kwa mteja. Yani unapotumia teknolojia ya IoT katika biashara yako, unampa mteja nafasi ya kupata huduma nyingi (mfano: kununua bidhaa/huduma, kujisafirishia na kutoa maoni) ndani ya site moja kirahisi.

10. Kuongeza Mapato: Kwa kutumia IoT matumizi katika biashara yanapungua sana kwa kuwa shughuli nyingi zinafanyika kiautomatiki kupitia mawasiliano baina ya vifaa vinavyotumia huduma za intaneti. Hakuna tena gharama kubwa za usafiri wala kukusanya data. Kifupi, yajayo yanafurahisha sana katika IoT. Makampuni mengi duniani tayari wameshanza kutumia huduma hizi yakiongozwa na makampuni ya Ugavi na Usafirishaji kama DHL, XPO Logistics na FedEx.

Biashara zinazotumia IoT hujikuta zikitumia gharama ndogo na thamani kubwa sana katika kujiendesha, jambo linalowafanya waweze kujitanua zaidi na kupata mapato lukuki. IoT ndio teknolijia ya kibiashara haswa na wajanja ndio wanaoifaidi. Usisubiri uachwe.

Kuna msemo mmoja maarufu katika IoT unasema, “If an electronic device can be connected, it should get connected” yaani, “Kama kifaa kinaweza kuunganishwa, basi na kiunganishwe”. Msemo huu ndio kwa kiasi kikubwa unaipa nguvu kasi ya IoT kuenea duniani. Umegundua nini kwenye makala hii kuhusu mageuzi ya intaneti (iot) katika biashara na maisha? Tuambie kwenye comment hapo chini,..

Vyanzo: https://www.statista.com/statistics/1194677/iot-connected-devices-regionally/

https://www.huffpost.com/entry/8-ways-the-internet-of-th_b_11763836

https://www.newgenapps.com/blog/impact-of-internet-of-things-on-the-business-world/

Njia ya Kompyuta katika kuhifadhi data utajuaje pale biashara yako inapojiendesha kwa hasara changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika

CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.

Bila shaka umeshasikia misemo kama ‘survival for the fittest’ ama ‘Bahari tulivu haizalishi nahodha hodari’, wengine wanakwambia “Mwanzo mgumu”. Sasa kwenye biashara, mambo yapo hivyo hivyo, changamoto haziepukiki. Sasa leo tuazione changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika kabisa. Twende sambamba.

Leo hii, duniani kunaripotiwa kuwapo takriban kampuni/biashara 150 milioni zinazoanza (startups), huku kukiwa na ongezeko la kampuni hizo milioni 50 kila mwaka. Kwa wastani kuna kampuni zinazoanza 137,000 zinaanzishwa kila siku. Hebu niambie, umeshaanzisha biashara ngapi hadi leo? ngapi zimeshakufa? Ngapi upo nazo mpaka leo? tuambie kwenye comments pale chini.

Lakini swali la msingi ni je, hizi kampuni zinazoanza, zinaweza vipi kuhimili mawimbi makali ya changamoto zilizopo katika ulimwengu wa biashara duniani? haswa eneo la Kusini mwa jangwa la Sahara (ambalo linatajwa kuwa na changamoto nyingi zaidi za kibiashara).

unaweza vipi kukabiliana na hasara katika biashara yako?changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika

Takwimu zinaonyesha kuwa 80% ya biashara/kampuni zinazoanza hufa ndani ya mwaka wa kwanza tu tangu kuanzishwa kwake. Na katika hizo 20% zilizobaki 10% hufa ndani ya miaka mitano tangu kuanzishwa. Tatizo ni nini? Wafanyabiashara hawa wanakosea wapi? Ni changamoto gani hizo ambazo pengine wafanyabiashara/waanzilisi wa kampuni hizo hawakuwa wanazijua mpaka zinapelekea biashara/kampuni zao kufa kabla hazijafikia ndoto na malengo yale makubwa ambayo waanzilishi walijiwekea mwanzoni. Hizi changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika kabisa.

Sasa leo tuzione hizo changamoto katika biashara mpya/inayoanza, ni funzo lisiloepukika kweli?;

1. USHINDANI MKALI

Hakuna wakati katika historia ya mwanadamu biashara zimekuwa zikifanyikwa kwa ushindani kama sasa. Yaani usitegemee kuanzisha biashara ambayo haina ushindani. Pia ni ngumu sana kuanzisha biashara ambayo haijawahi kufanyika kabisa hapo kabla. Hivyo jipange na ujiandae kisaikolojia.

Ujio wa matumizi ya intaneti umeongeza sana hali ya ushindani ambapo kwa sasa masoko hutafutwa kwa njia za kidijitali zaidi. Biashara zinahamia mtandaoni na hivyo huna budi kuhakikisha unatafuta wateja kwa nguvu sana kwa njia za Digital marketing, social media marketing, affiliate marketing na nyingine nyingi ili kuhakikisha biashara yako inaendelea kupata wateja wapya na kuwafikia wale ulio nao kirahisi zaidi.

Lakini njia rahisi (japo sio nyepesi) ya kuepuka ushindani sokoni ni kuwa MKIRITIMBA (Being a Monopoly). Hii ni ile hali ya kucontrol soko na kukamata wateja wengi kiasi kwamba washindani wako hawana nguvu ya kupambana na wewe sokoni. Zaidi kuhusu ukiritimba fuatilia makala hii hapa

2. WATU SAHIHI

Waswahili wanasema, Biashara ni watu. Hii haiishii kwa watu kwa maana ya wateja peke yake, watu hawa haswa wanangukia kwenye wabia, wafanyakazi na washauri wako katika biashara. Hawa wana mchango mkubwa na muhimu sana katika kuua au kuendeleza biashara yako.

Hii Rednet ni mfano sahihi katika sehemu hii kwa kuwa mwanzoni Rednet Technologies ilihisusha watu 6. Lakini kutokana na kutoshare vision na sababu zingine, Rednet haikuweza kushamiri katika mwaka wake wa kwanza mpaka tulipoamua kupunguza watu mpaka kupata watu sahihi wa kufanya nao kazi kwa maslahi mapana ya kampuni. Unapoamua kuanzisha biashara/kampuni mpya hakikisha unazungukwa na watu sahihi watakaoimarisha zaidi biashara/kampuni hio. Wahenga wanasema “Ndege wanye manyoya yanayofanana, ndio wanaoruka pamoja”. Take that note.

3. MASWALA YA FEDHA

Moja kati ya vitu vinaua biashara/kampuni nyingi ni Kutokujua kutofautisha maswala ya fedha ya kampuni na yale binafsi. Elewa, ukishaingiza pesa kwenye biashara/kampuni, pesa hio sio Binafsi tena. Inatakiwa izunguke mpaka itoe return/faida ambayo ndio inaweza kutumika kwa matumizi binafsi. Hii ni changamoto kubwa na inayohitaji umakini mkubwa ili kuihimili. Lile gepu la masikini na tajiri kwa kiasi kikubwa huwa linapigwa kutokana na uwezo wa kupambana na changamoto hii.

changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika

4. UFINYU WA RASILIMALI

Miongo michache iliyopita kuanzisha biashara/kampuni mpya ilimlazimu mtu kuwa na mtaji mkubwa ama kuwa na uwezo wa kufanya harambee ya kukuza mfuko wa uwekezaji. Kwa wakati huo mawazo mengi yalishindwa kuwa biashara/kampuni zenye tija.

Lakini leo hii kunakadiriwa kuanzishwa takribani biashara mpya 137,000 kila siku duniani kote. Hii ni kutokana na kukua kwa kasi ya teknolojia katika shughuli za kibiashara ambayo imerahisisha sana upatikanaji wa rasilimali. Lakini swala la maarifa ghafi (softskills) bado limekuwa ni changamoto katika uendeshaji wa biashara nyingi ambapo licha ya kuwa na wazo zuri ama mtaji wa kifedha, bado kuwa na maarifa ya kuendesha biashara/kampuni inabaki kuwa ni changamoto. Hivyo ukitoa Wazo, Vifaa vya kufanyia kazi na Pesa ya uwezeshaji, Maarifa ni rasilimali muhimu zaidi.

5. UWEZO WA KUTOA MAAMUZI SAHIHI

Katika kuanzisha biashara/kampuni mpya, moja kati ya Changamoto kubwa zinazowakabili waanzilishi ni Uwezo wa Kutoa maamuzi sahihi kulingana na wakati na hatua biashara/kampuni inayopitia. Moja kati ya changamoto zinazosumbua sana katika biashara.

Ukiwa mfanyabiashara/mbia wa kampuni unalazimika kufanya maamuzi mengi kila siku. Katika maamuzi hayo utajikuta wakati mwingine unafanya makosa kutokana na maamuzi yako, na pengine maamhzi hayo yanaweza kukukatisha tamaa na hata kuua biashara/kampuni yako ndani ya muda mchache.

Usiogope. Hakikisha unajifunza katika kila maamuzi unayochukua hata kama hayakuleta madhara katika biashara/kampuni yako. Wahenga wanasema “Busara hujengwa katika maamuzi“. Note hio, halafu ifanyie kazi kila siku. Kulifahamu hili kwa undani fuatana na makala hii hapa..

6. KUPATA UAMINIFU WA WATEJA

Hebu niambie, ilikuchukua muda gani kupata mteja wako wa kwanza tangu ulipoanzisha biashara/kampuni yako? Cocacola ilichukua mwaka mzima kuuza chupa moja ya soda katika mwaka wake wa kwanza tangu kuanzishwa.

Rednet ilichukua miezi 8 mpaka kumpata mteja wetu wa kwanza tangu tulipoanza shughuli zetu hapo mwaka 2016. Ni wakati mgumu sana katika biashara, lakini wahenga wanasema “Mteja ni mfalme.” Hivyo kupata mfalme wa kuhudumia kwa vyovyote si rahisi. Siku zote kizuri kinajiuza chenyewe ambapo huduma nzuri huvuta wateja zaidi kwa kutumia mbinu ya “Word of mouth“. Mbinu hii huzalisha wateja wa kudumu zaidi ambao huwa mabalozi wazuri wa biashara/kampuni yako. Jinsi ya utendaji katika biashara yako lazima ijengwe kumzunguka na kuridhisha wateja wako. Mteja asiporidhika, bado hujafanikiwa kibiashara. Zaidi tiririka na makala hii hapa kwa ajili yako..

7. USALAMA WA KIMTANDAO

Wakati huu tunaoishi ni wakati wa Kidijitali. Biashara/kampuni nyingi zinazoanzishwa zama hizi hufanyia shughuli zake mtandaoni, hivyo miundombinu ya utendaji katika biashara za kisasa kwa zaidi ya 75% hutegemea Nguvu ya mtandao.

Hata hivyo, Wadukuzi wa kimtandao wanafanya mazingira ya kiutendaji mtandaoni kuwa magumu na yenye kuhofisha. Matukio ya udukuzi na uhalifu wa kimtandao yanazidi kuongezeka kila uchwao. Tafiti zinaonyesha kufukia mwaka 2021 matukio ya uhalifu wa kimtandao yatakuwa yakitokea kila baada ya sekunde 11 duniani kote. Ili kujilinda dhidi ya uhalifu huu wa kimtandao, biashara zinazoanza hazina budi kuwa na miundombinu ya kimtandao ambayo ni imara zaidi kila wakati.

Zaidi kuhusu Usalama wa kimtandao unaweza kupata makala yetu mahsusi kupitia link hii KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?

Kifupi hizo ni changamoto chache ambazo zinazikabili biashara/kampuni inazoanza, ni funzo lisiloepukika kweli kweli. Je, wewe umepitia changamoto zipi wakati unaanzisha hio biashara yako uliyo nayo? Umeshajaribu kufanya biashara ngapi bila mafanikio mpaka kufikia sasa? Tafadhali tushirikishe ili watu wengine wapate kujifunza zaidi. Karibu.

Pia hakikisha unapitia makala hizi tumekuwekea hapa chini ili kuhakikisha unapata muendelezo mzuri kutokana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Gusa link kisha makinika..

  1. KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?
  2. BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA?
  3. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO

Ni matumaini yangu leo umefahamu kwa undani changamoto katika biashara mpya/inayoanza, funzo lisiloepukika. Utakwenda kukabiliana nazo vipi changamoto hizi za leo? Niambie kwenye comment hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu(website design, logo design, Digital consultacy n.k) BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRICA

Kwa mara ya kwanza katika Historia ya mwanadamu, zaidi ya nusu ya watu wote duniani wanatumia huduma za internet. Na katika maeneo yote, imeonekana huduma hizo zinakua kwa kasi zaidi barani Africa. Idadi ya watu wanaotumia internet imeongezeka sana barani Afrika kutoka 2.1% mwaka 2005 mpaka 24.4% mwaka 2018. Sasa leo nataka u fahamu mchango wa ICT katika maendeleo ya sekta binafsi barani Africa. Twende sambamba.

Huduma hizi za internet zimekuja kurahisisha shughuli za kiuchumi kama kurahisisha njia za malipo (bank, MPESA, tigopesa nk), matumizi ya drones katika matibabu kama inavyofanyika nchini Rwanda, matumizi ya smartphones katika kuongeza maarifa ya kitaaluma na kiufundi stadi na kuongezeka kwa biashara za mtandaoni (e-commerce businesses, network marketing and online businesses). Bill Gates amewahi kuandika katika moja ya tweets zake “If your business is not on the Internet yet, Your are out of the Business.” Mwenye macho haambiwi ona.

SEKTA BINAFSI, INJINI YA UCHUMI AFRIKA

Kama ulikua hufahamu, basi sekta binafsi ndio imetawala Uchumi wa Afrika kwa kuwa zaidi ya 80% ya uzalishaji mali mzima hufanyika katika sekta hio. Zaidi, theluthi mbili (⅔) ya uwekezaji mzima barani na robo tatu (¾) ya jumla ya mitaji katika uchumi kati ya mwaka 1996-2008 imeonekana kutokea katika sekta hio binafsi. Vile vile sekta hio inatoa 90% ya ajira zote kwa vijana walio katika umri wa kufanya kazi. Mchango wa biashara za ndani katika sekta binafsi katika GDP ilikua 59% katika nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara ukilinganisha na 30% ya nchi za Latin America na Caribbean, 32% Asia Kusini na 42% katika Mashariki ya Kati. Hii inaonyesha kiasi gani Afrika sekta binafsi inalipa maradufu. Umeiona nafasi yako hapa ndugu yangu mfanyabiashara.!?

Kujiimarisha katika Sekta binafsi, huna budi kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kila mara unapohitajika kufanya hivyo. Unawezaje kufanya maamuzi sahihi katika changamoto zinazokukabili? Tafadhali fuatana nasi katika makala hii hapa FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI.

Katika nchi za Uchumi wa kati, kampuni binafsi hufanya kazi katika mfumo wa sekta rasmi, ambapo makampuni makubwa na yale madogo (SME’s) huzalisha hisa za thamani katika uwekezaji na zaidi, ajira kwa vijana ambao ndio kundi kubwa zaidi katika nguvu kazi barani Afrika. Lakini zaidi, sekta binafsi katika nchi hizi hufanya ⅔ ya uzalishaji mzima.

Uchumi huwa na ushindani pale kunapokuwa na ushindani mkali wa kibiashara. Na biashara huwa na ushindani pale:

•Sheria zinapokua sawa na haki.

•Wafanyakazi wana maarifa stahiki.

•Gharama za uendeshaji (umeme, maji, mafuta, usafiri) zinakuwa nafuu.

•Wateja wanafikika kila kona.

ICT INAINGIA VIPI HAPO?

Uchumi wa kidijitali umekuwa dhima kuu ya kidunia na Afrika haijabaki nyuma katika hili. Matumizi ya teknolojia yanazidi kushika kasi barani yakichagizwa na kasi ya ueneaji wa huduma za internet ambapo biashara nyingi zinazidi kuhamia mtandaoni kirahisi. Mpaka kufikia mwaka 2015 tu tayari watu 557 barani walikua wanatumia simu ya mkononi ambayo ni 12% ya watumiaji wote wa simu duniani huku idadi hio ikikusanya 6% ya mapato yote yaliyofanyika duniani wakati huo.

Sasa leo wacha tuone maeneo muhimu ya ICT yanayokuza uchumi zaidi;

1. TELECOMUNICATIONS

Eneo hili linajumuisha makampuni makubwa ya mawasiliano. Kwa kiasi kikubwa hufanya shughuli zake katika utaratibu wa sekta rasmi, hivyo kuwafikia watu wengi na kufanya kazi karibu zaidi na mamlaka za serikali. Makampuni kama Vocacom, MTN, Tigo, Airtel na TTCL yapo hapa. Kutokana na kuwa na watumiaji wengi, makampuni haya huchangia kiasi kikubwa katika mapato ya kiserikali kama kodi na gawio huku yakichangia sehemu kubwa katika kukuza uchumi wa watumiaji wake kutokana na fursa zinazopatikana katika huduma wanazozitoa kama uwakala wa huduma, huduma za kifedha nakadhalika.

2. SOFTWARE AND IT CONSULTING

Hapa ndo utatukuta sisi sasa ambao tunakuhudumia wewe muda huu. Zaidi ya kukupatia taarifa hizi ghafi, pia eneo hili la ICT hutoa huduma za kutengeneza mifumo ya computer, Apps za simu, Ushauri na Uchambuzi wa kiteknolojia katika Biashara na Uchumi. Japokuwa sio maarufu sana lakini sehemu hii inachangia uchumi wa mabiashara mbalimbali, makapuni madogo na yale yanayokuwa (SME’s) pamoja na sekta zingine za uma na binafsi kwa kutoa huduma za matengenezo ya tovuti, mifumo mbalimbali ya kibiashara, huduma za afya, elimu, uhifadhi wa data pamoja na uchambuzi na ushauri wa biashara mbalimbali kiteknolojia zaidi.

3. DIGITAL SERVICES

Hapa utawakuta watu wanaotoa huduma za kidijitali ambao wengi wao hufanya kazi kwa ukaribu na makampuni ya mawasiliano. Watoa huduma hawa pia wanahusika kutengeneza mifumo ya makampuni ya mawasiliano pamoja na kutengeneza/kuendesha mitandao ya kijamii zaidi. Watoa huduma hawa wamekuwa wakitengeneza michezo ya video pamoja na kutoa huduma za WebHosting na Cloud services kwa makampuni ya Kiafrika. Kampuni kama Dudumizi Technologies(Tanzania), ISB North Africa (Morocco), Web4Africa (Ghana) na Domains Africa Technologies (Kenya) zipo hapa.

4. INFORMATION SERVICES

Hapa sasa ndio utazikuta redio na televisheni zote unazozifahamu. Hawa kwa jina lingine wanaitwa Watoaji wa Maudhui, ambapo hutafuta habari na maudhui wanayodhani yanafaa kwa wateja wao na hivyo kukusanya jamii ili ipate maudhui hayo huku yenyewe yakijipatia faida yake katika matangazo mbalimbali ya kibiashara yanayoruka sambamba na maudhui yao. Hapa unaweza kunitajia Redio/TV ambayo ina maudhui unayoyapenda yakienda sambamba na matangazo ya wadhamini wa vipindi vyao. Usishangae ukiona hivyo. Kwenye matangazo ndo wanapopatia pesa wenzio, usione unapata bure maudhui hayo.

Kwa uchache haya ndio mambo ya fahamu mchango wa ICT katika maendeleo ya sekta binafsi barani Africa yanayochangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa Uchumi wa Kidijitali na kuboresha biashara nyingi zaidi kila kukicha barani Afrika. Jiulize, unayatumia vipi maeneo haya katika kukuza biashara yako wewe kama mjasiriamali?

Makala hizi hapa chini zitakusaidia kufahamu kwa undani namna sekta binafsi zinachangia uchumi na maendeleo ya wafanyabiashara hasa vijana wa Afrika Mashariki. Gusa links kisha makinika:

  1. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE (TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?
  2. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  3. UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA

Usisahau kutoa maoni yako kuhusu ukichojifunza katika makala hii ya leo na unaweza kusambaza ili kuhakikisha ulichijifunza kinawafikia wengine. Pia unaweza kutembelea tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz kuhakikisha unaendelea kupata taarifa sahihi kuhusu uchumi na biashara yako kiteknolojia. Asante.

Makala hii ni Kwa Heshima ya Hayati B.W. Mkapa aliyekuwa Rais awamu ya 3 nchini Tanzania. Mzee Mkapa aliongoza Taifa kuelekea zama hizi za maendeleo ya Sekta Binafsi kupitia Sera yake ya Ubinafsishaji wa mali za umma zilizokua mzigo kwa serikali, hivyo kuchochea ukuaji wa sekta binafsi kwa kiasi kikubwa mpaka kufikia hivi ilivyo leo. Mzee aliona mbali sana. #RIPMkapa