Tag: sadc

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA

June 23 mwaka huu, Jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika, SADC kwa kauli moja ilipitisha muongozo wa kurasinisha shughuli za kibiashara baina ya nchi wanachama wake. Sasa unajiuliza, huo Urasinishaji ndo nini? Na una manufaa gani katika biashara yako?

Ushindani wa kimasoko ukiongezea, ukiongezea ongezeko la wimbi la wateja wa huduma za kidijtali, hali hii inaongeza changamoto kila leo katika mazingira ya kibiashara hususan barani Afrika ambapo wafanya biashara wengi bado hawatumii mwanya wa teknolojia katika shughuli zao za kiuchumi za kila siku.

Hata hivyo, bado wafanyabiashara wanaamini katika Ubunifu wa mbinu katika kukuza na kuimarisha biashara zao na kunasa wateja wengi zaidi. Hili litawezekana vipi katika mazingira ya kisasa ya Masoko Huru na matumizi makubwa ya kiteknolojia? Jibu mbadala ni Urasinishaji wa shughuli za kibiashara hasa kwa kupitia matumizi mazuri ya teknolojia za mawasiliano na habari.

URASINISHAJI NI NINI?

Ni utaratibu/mchakato wa kuoanisha/kuunganisha shughuli za kibiashara kisheria baina ya maeneo kadhaa/nchi/Jumuiya za maendeleo/Kampuni/Mashirika ili kutanua soko la wafanyabiashara, kuongeza wateja na kukuza uchumi wa washirika. Umenipata apo?

Sasa taratibu zote za kibiashara zinapokuwa sawia pamoja na utekelezaji mzuri wa sera za biashara na maendeleo, basi bila shaka biashara zitashamiri na kuongeza kasi ya kukuza uchumi imara na ongezeko la wateja wa huduma na bidhaa baina ya washirika. Urasinishaji ndio mbinu.

Ili kuweza kurasinisha biashara kwa mafanikio, leo tutajadili hatua 5 muhimu za Kuwezesha Zoezi la Urasinishaji katika Biashara yoyote (hata hio unayoifanya wewe). Hatua hizi huitwa pia Viwezeshaji vya Urasinishaji (Enablers towards Harmonization in Business). Twende nazo sasa.

1. UTAWALA BORA

Nikwambie tu, hakuna biashara ya kiungwana inayoweza kufanyika katikati ya vita na machafuko. Biashara inahitaji mazingira salama ya kufanyika. Biashara ni kama mtoto mdogo, inahitaji malezi bora ili iweze kukua, kushamiri na kurudisha faida mara dufu. Hivyo jukumu la kutunza na kudumisha mazingira ya amani na utulivu ni la kila mmoja, hasa mfanyabiashara, lazima uhakikishe eneo lako la biashara lina amani na ni salama kwa yeyote kufanya biashara na wewe. Serikali kama mlezi mkuu, husimamia amani na usalama wa nchi wakati wote kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama wA nchi kama polisi na jeshi.

2. KUONGEZA MAARIFA

Zoezi la kuoanisha shughuli za biashara mbalimbali linakwenda sambamba na kuongeza maarifa ya kufanya biashara hizo. Hivi wewe mfanyabiashara unaweza vipi kukuza mtandao wa biashara yako kabla hujaongeza maarifa kuhusu biashara yako na biashara zingine ambazo unahitaji kushirikiana nazo? Hakika, huwezi kufanya/kuendelea kufanya biashara pasi na kuwa na maarifa sahihi, utadumaa kibiashara au kuishia kufilisika tu. Maarifa ndio chakula cha biashara. Lazima uwe mjanja, usikubali kuwa hapo ulipo kila siku. Ongeza ujuzi biashara ikue io.

3. UHUSIANO NA WATU

Kama ulikua hujui, Biashara ni mahusiano na mahusiano ni watu. Na watu ndio hao unawaona kila siku na wengine huwaoni ila wapo. Jumuiya ya SADC pekee inakadiriwa kuwa na wakazi takriban milioni 400. Watu wote hawa unawahusisha vipi kwenye biashara yako? una mpango gani wa kuongeza wigo wa watumiaji wa bidhaa/huduma zako? Kama unafanya biashara ambayo haiongezeki wateja, hivi unajua kuwa hio biashara inakwenda kufa muda si mrefu? Waswahili wanasema, “Ongea na watu uvae viatu.” Kalagabaho.

4. MATUMIZI YA TEKNOLOJIA

Mwaka 2018 duniani yalianza mapinduzi ya 4 ya Viwanda ambayo kwa kiasi kikubwa yanahusisha matumizi ya teknolojia ya kompyuta na intaneti katika nyanja mbalimbali ambazo hapo kabla hazikuwa zikitumia teknolojia hio. Matumizi ya smartphones katika kuchakata na kuhifadhi rekodi za kibiashara, matumizi yanayoshika kasi ya mitandao ya kijamii katika kutangaza na kufanya biashara, ujui wa vifaa janja vya kielektroniki (smart devices) pamoja na uanzishwaji wa Maeneo Huru ya kufanyia biashara, kwa mfano, barani Afrika mwaka 2018 ulianzishwa mchakato wa kuanzishwa kwa Eneo Huru la kufanyia Biashara (African Continental Free Trade Area) AfCFTA lenye lengo la kuruhusu nchi wanachama kufanya biashara kwa wepesi na haraka katika kukuza uchumi wao. Kufahamu zaidi kuhusu AfCFTA na faida zake katika mchakato mzima wa urasinishaji wa shughuli za kibiashara barani Afrika, tembelea makala kupitia link hii hapa https://rednet.co.tz/kuanzishwa-kwa-eneo-huru-la-biashara-barani-africa-afcta-kuna-manufaa-gani-kwako/ yenye kichwa “KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?”. Pitia hapo, kisha tuendelee..

Sasa katika njia zote hizi zilizotengenezwa katika msingi wa Kiteknolojia, jiulize, unatumiaje mianya hii iliyotengenezwa kwa ajili ya kukuza na kuimarisha biashara yako? Teknolojia ni uwanda mpana sana na unaweza kuutumia vyovyote vile kuendana na mahitaji ya biashara yako. Kwa taarifa ushauri wa jinsi ya kutumia teknolojia vyema, usisite kuwasiliana nasi sasa kwa kutembelea tovuti yetu maridhawa ya www.rednet.co.tz, tupigie simu au tutumie barua pepe.

5. VIPIMO NA UFUATILIAJI

Ili mambo yote tuliyoyaona yaweze kufanyika kwa usahihi, hakuna budi kila hatua ipimwe na kufuatiliwa vizuri ili kuhakikisha hatua zimefuatwa sawia katika kurasinisha biashara kwa manufaa ya wote. Waswahili wanasema “Biashara haina undugu” Na pia “Kwenye kazi ifanyike Kazi”. Hivyo kwa jinsi hii sheria zilizowekwa wakati wa kuanzishwa kwa urasinishaji lazima zifuatwe ili kuhakikisha kila mshirika wa Urasinishwaji huo anafaidika sawa sawa na juhudi zake.

BONUS POINT:

Urasimishwaji unaweza kufanyika na kuhusisha biashara yoyote. Mfano mfanyabiashara wa viungo vya chakula kama nyanya, karoti, hoho, Anaweza kuungana na mfanyabiashara wa chakula katika migahawa katika biashara zao halafu mambo yakawa safi kabisa. Pia mtunzi wa hadithi na riwaya anaweza kukaa chini na mbunifu wa mitindo ya nguo na fasheni na waongozaji wa filamu na hivyo kufanya kazi bora katika kiwanda cha filamu na maonyesho na watu wote tukasimama kwa heshima. Hata mfanyabiashara wa viatu na nguo akikaa vizuri na mtaalam wa kutengeneza tovuti za mauzo (ecommerce website) wanaweza kutengeneza e-commerce platform moja, kila mtu duniani akanunua viatu na nguo na jamaa wa IT akapata gawio lake safi kabisa.

Pia kuna hizi makala ambazo ukizisoma zote zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna ya kuimarisha biashara kwa kushirikiana na wafanyabiashara na wadau wengine. Cha kufanya, gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/biashara-yako-inaweza-vipi-kuwa-taasisi-imara/ yenye kichwa “BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA?”
  2. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”
  3. https://rednet.co.tz/ukiritimba-katika-biashara-ni-asali-au-shubiri/ yenye kichwa “UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?”

Huo ndo Urasinishaji katika biashara kwa ufupi, moja kati ya mbinu makini sana katika kukuza biashara kwa kutumia biashara ingine. Wazungu wanaita B2B au Business To Business. Ila sisi tunaita Harmonization of Business kama tulivyoiona definition kule juu. Una lolote? Tafadhali maoni yako ni muhimu.

FAHAMU KUHUSU UVUVI NA BIASHARA YA SAMAKI BARANI AFRIKA

Japokuwa inafanyika zaidi maeneo ya vijijini na katika hali duni ya zana za utendaji, elimu pamoja na teknolojia, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado inahangaika katika kujiboresha huku ikifichwa katika kivuli cha shughuli za Kilimo na Ufugaji. Mbaya zaidi sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado haijapewa umuhimu inayostahili barani humo. Zaidi sekta hio hutoa chakula cha kuwalisha watu zaidi ya milioni 200 barani humo na nje ya bara la Afrika. Leo sasa fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika. Twende mpaka mwisho.

Benki ya Dunia inaripoti kwamba shughuli za uvuvi na biashara ya samaki huchangia moja kwa moja dola za kimarekani $24 bilioni katika uchumi wa Afrika kwa ujumla, ikiwakilisha 1.3% ya jumla ya pato la ndani (GDP) la Afrika katika mwaka 2011. Vile vile sekta hio imezalisha ajira kwa zaidi ya watu milioni 12 ambapo 58% kati yao ni wavuvi na 42% wanajihusisha na kuandaa samaki waliovuliwa kabla ya kuwapeleka sokoni. Tanzania peke yake, sekta ya uvuvi imetoa ajira kwa watu 183,000 mpaka kufikia mwaka 2014 (chanzo: Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi) Ikionekana kwamba shughuli za uvuvi hufanywa zaidi na wanaume, 59% ya shughuli za kuandaa samaki kabla ya kuwaingiza sokoni hufanywa na wanawake.

Ukiachana na faida za samaki kama chakula katika kupatikana kwa virutubisho muhimu kama vitamini, protini na mafuta, zaidi, sekta ya Uvuvi na biashara ya samaki inachangia sehemu muhimu sana katika kuendesha maisha ya watu haswa vijana ikiwa watachukua angalizo katika fursa zilizopo kwenye sekta hio.

Changamoto; Je, kuna fursa zipi katika kufanya shughuli hii ya uvuvi na biashara ya samaki katika kukuza uchumi? Teknolojia ina mchango gani katika kuboresha uchumi wa mtu mmoja mmoja kupitia setka hii?

Tishio kubwa katika shughuli za uvuvi na biashara ya samaki ni athari zinazotokea katika mazalio ya samaki baharini, mtoni, ziwani au kwenye mabwawa. Umoja wa Mataifa na nchi  jumuishi duniani zimeingia uwoga juu ya upatikanaji wa hazina ya samaki katika soko la dunia. Shirika linaloshughulikia maswala ya Chakula duniani, FAO, limetabiri kwamba zaidi ya 70% ya aina (species) za samaki zinakaribia kuangamia au zimevunwa sana ambapo aina za samaki kama Tuna, Swordfish, Haddock na Flounder zipo katika tishio la kuangamia. Zaidi, uvuvi unaotumia chandarua au baruti huweza kusababisha kunaswa au kuuwawa kabisa kwa samaki na viumbe wengine wa baharini ambao hawajapangwa kuvuliwa kama ngasa, pomboo na papa.

Hata hivyo, shughuli za uvuvi zina faida gani katika maisha ya mwanadamu ikijumuisha?

  1. CHAKULA;  Samaki ni chanzo cha vitamini na protini katika lishe haswa ya mwanadamu ambapo madaktari na wadau wa sekta ya afya hushauri ulaji wa nyama nyeupe mfano samaki zaidi katika mlo. ulaji wa samaki kwa wingi huchochea ukuaji bora wa afya ya akili pamoja na wingi wa protini katika nyama hio huku ikiwa na kiasi kidogo cha lehemu (cholesterol) zaidi kuliko nyama nyekundu mfano ng`ombe, mbuzi na kadhalika.Ripoti zinaonyesha kwamba wakazi wa nchi za ukanda wa bahari ya Pacific peke yake hupata zaidi ya 25% na 69% ya protini za wanyama wanaokula kila siku kutoka katika samaki. Hii imepelekea shughuli za uvuvi na biashara ya samaki kukua kwa kiasi kikubwa kama shughuli rasmi ya kiuchumi ambayo imeajiri watu takribani milioni 200 dunia nzima na ikizalisha pato la dola za kimarekani zaidi ya 80 bilioni kwa mwaka.
  2. UKUAJI WA UCHUMI; Sekta hii ya uvuvi inachangia kwa kiasi kikubwa sana katika ukuaji wa uchumi barani Afrika mpaka dunaini kote ambapo watu zaidi wa milioni 200 wamejipatia ajira kupitia sekta hio. Nchini Uganda kwa mfano, uvuvi wa ziwani umekuwa na thamani ya zaidi ya dola $200 milioni  kwa mwaka ikiwa ni mchango wa 2.2% katika pato la taifa (GDP) la nchi hio. Vile vile watu zaidi ya 135,000 wamepata ajira kama wavuvi katika sekta hio na wengine 700,000 zaidi katika mchakato wa kuandaa samaki kabla hawajafikishwa sokoni na hivyo kuzalisha zaidi ya dola $87.5 milioni kama mapato ya biashara za nje ya nchi (exports earnings). Hapa miundombinu ya barabara na reli ina mchango mkubwa sana katika kuhakikisha kitoweo hiki kinamfikia mlaji kikiwa katika ubora wa hali ya juu. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa miundombinu pitia makala hii hapa;
  1. Vile vile nchini Tanzania kupitia katika mabwawa, maziwa, mito na bahari vilivyomo nchini humo, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki imetoa ajira za moja kwa moja kwa watu takribani 183,800 na wengine zaidi ya 4,000,000 wakijihushisha kama watengenezaji wa vyombo vya uvuvi (ngalawa, boti, ndoano, neti n.k), waaandaaji wa samaki kabla hawajafikishwa sokoni, wachuuzi na wafanyabiashara wa samaki wa jumla na rejareja. Sekta hii ya uvuvi na biashara ya samaki inawapatia watu kipato cha fedha za kigeni, pamoja na kitoweo kwa watu waishio pwani ya bahari ya hindi pamoja wa walaji wa samaki kutoka sehemu zingine katika nchi hio ambapo sekta hio huchangia katika pato la taifa takribani 2.4%. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi katika mwaka 2016.

Kiujumla, mpaka kufikia mwaka 2001 uta fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika katika masoko ya kimataifa ilikuwa na thamani ya dola $2.7 bilioni ambayo ni 5% ya jumla ya thamani ya sekta nzima ya uvuvi na biashara ya smaki duniani ambayo ni dola $56 bilioni. Kwa mujibu wa shirika la FAO, bidhaa za samaki zimejumuisha zaidi ya 10% ya jumla ya biashara za kimataifa (exports) katika nchi 11 barani Afrika.

Sasa Baada ya kuyajua Hayo Yote, Kwanini Ufanye biashara hii ya Uvuvi na samaki?

Mwaka 2019 watumiaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania waliongezeka kufikia milioni 23, ongezeko la watumiaji takribani milioni 1 kutoka mwaka jana 2018. Vile vile watumiaji wa huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi wamefikia takribani milioni 20 hadi kufikia mwaka huu 2019. Hii ni kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA.

Hivyo kupitia ripoti hio ya TCRA mfanyabiashara anaweza kuhamishia shughuli zake kupitia simu mkononi na simu janja (smartphones) katika kuhakikisha biashara yake inawafikia watu wengi zaidi katika muda mfupi kwa njia ya Teknolojia. Hata hivyo mfanyabiashara anaweza kutengeneza majukwaa ya kimtandao kama tovuti za kibiashara (online shops na ecommerce websites) ambayo anaweza kuuza bidhaa zake za samaki kirahisi katika masoko ya ndani na hata yale ya kimataifa kwa gharama nafuu zaidi kuliko ulivyokua hapo kabla.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Kwa kutambua hilo, biashara ya mtandaoni imekuwa ikizidi kufanikiwa sana nyakati hizi huku ikichochewa na maboresho katika miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji. Hivyo ni muhimu kufungua tovuti rasmi ya biashara yako ili kuipa utambulisho usio na shaka ukiwa mtandaoni. Vilevile ni muhimu kufungua akaunti za mitandao ya kijamii ili kusudu uzidi kujiweka karibu na wateja wako na kujua namna nzuri ya kuwahudumia.

Link zifuatazo zitakusaidia sana uweze fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika kupitia mtandaoni iwe na mafanikio zaidi na zaidi:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO

Je umepata nini katika mada ya leo katika ku fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

TEKNOLOJIA KATIKA KUKUZA BIASHARA KUPITIA SEKTA YA UTALII

Inasemekana binadamu anajua zaidi mazingira ya mwezini kuliko ajuavyo mazingira ya ndani/chini ya bahari. Sasa kampuni ya usafirishaji ya Uber tarehe 23 May 2019 ilizindua manuwari ndogo iitwayo ScUber kwa ajili ya kutalii ambapo mradi huo umeanzia jijini Queensland, Australia. Moja kati ya sababu ikiwa ni kutoa fursa kwa wageni/watalii kuweza kuzuru eneo maarufu la bahari liitwalo The Great Barrier Reef nchini humo. Sasa tunaweza vipi kutumia teknolojia katika kukuza biashara kupitia sekta ya utalii? Kumbuka Tanzania ina vivutio vingi sana vya utalii na vijana wengi wamejikita katika kuhudumia watalii hao, watumieje teknolojia kujiletea manufaa? Twende sambamba mpaka mwisho wa makala hii kufahamu zaidi.

utalii na teknolojia

Turudi Australia, manuwari hio ndogo yenye uwezo wa kubeba watu watatu kwa wakati mmoja ni ya kwanza kabisa duniani kufanya shughuli za kutalii kwa mtu yeyote anayehitaji kufanya hivyo na ambayo huduma yake inapatikana kirahisi kupitia Application ya Uber inayopatikana Playstore ya Google na Appstore ya iOS (Je, wewe ni mmoja kati ya wale waliozoea kuziona manuwari kwenye muvi na kusikia manuwari za kivita tu? 😂). Haya ni mapinduzi makubwa katika kufanya biashara kupitia nyanja nyingine ya kichumi (kutoka usafirishaji mpaka utalii).

Sekta ya utalii inatajwa kuwa ni sekta muhimu sana katika ukuaji wa uchumi na kutengeneza ajira duniani kote. Sekta hio inatajwa kujumuisha 8.8% ya ajira zote duniani, sawa na watu milioni 258. Vile vile 9.1% ya wastani wa pato la taifa GDP inatokea katika sekta hii ambayo ni sawa na $6 trilioni. Zaidi, 5.8% ya bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi (exports) huhusishwa na sekta hii ambayo ni takribani $1.1 trilioni. Hata hivyo, sekta hii ya utalii huchochea sana uwekezaji ambapo 4.5% ya uwekezaji wote unaofanywa duniani hupitia katika sekta hii ambayo ni sawa na $652 bilioni za kimarekani.

Tukiangazia eneo la kusini mwa jangwa la Sahara inakadiriwa kwamba ajira 3.8 milioni zikijumuisha ajira 2.4 ambazo si za moja kwa moja (indirect jobs) zinakadiriwa kutengenezwa katika miaka 10 ijayo. Hii ni kwa mujibu wa Baraza la usafiri na utalii duniani (WTTC).

Sasa changamoto; Sekta hii ya utalii inachangia vipi katik kukuza biashara barani Afrika? Teknolojia inachangia vipi katika maendeleo haya ya utalii na biashara?

Kutoka ziara za watalii 6.7 milioni mwaka 1990, nchi za ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara zilitembelewa na watalii 33.8 milioni kufikia mwaka 2012 kwa pamoja ambapo stakabadhi za wageni mwaka huo 2012 peke yake zilionyesha zaidi ya dola za kimarekani 36 bilioni zilipatikana huku mchango wa moja kwa moja ukiwa ni 2.8% katika pato la ndani la taifa GDP (Jumla ya mchango ikiwa ni mchango wa moja kwa moja na ule usio wa moja kwa moja, ilifikia 7.3% ya GDP). Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya baraza la WTTC mwaka 2013.

Lakini, ili kufanikiwa zaidi katika kufanya Utalii na kuendeleza biashara, ukanda huo wa SSA (Subsaharan Area) inabidi ujidhatiti katika mambo yafuatayo; upatikanaji wa ardhi, ruhusa ya wawekezaji katika maswala ya fedha, matangazo ya utalii, kodi za uwekezaji katika utalii, utaalamu na ujuzi katika utalii, ulinzi na usalama, maswala ya afya, mahitaji ya viza na ukiritimba. Sasa teknolojia inaleta mchango gani katika kukuza biashara kwa kupitia utalii? Kuhusu namna unavyoweza kuitangaza biashara yako katika nyanja hii ya utalii fuatana na makala hii hapa

Tuzione baadhi ya njia za kiteknolojia zinazotumika katika nyanja hio;

E-TOURISM:

Huduma za intaneti zimeleta mapinduzi makubwa sana kwenye sekta hii ya utalii ambapo watalii na wageni sasa wanaweza kupata taarifa muhimu kuhusu mahali wanapotaka kwenda kutalii kama mbuga za wanyama, bidhaa za kiasili na utamaduni, hoteli, majumba ya makumbusho na historia mbalimbali kwa kutumia vifa vyao vya kielekroniki vilivyoungwa na huduma za intaneti kama simu za rununu na kompyuta mpakato (laptop). Matokeo yake wageni na watalii wamekuwa na mahitaji makubwa kwa bidhaa za kiasili na utamaduni pamoja na kujali thamani ya pesa zao pamoja na thamani ya muda wao. Hii imerahisisha sana ufanyaji wa biashara haswa kupitia majukwaa ya ecommerce (ambayo unaweza kuyapata kwetu Rednet Technologies kirahisi sana., gusa link hii kupata huduma zetu zenye ubora Our Services🙋).

E-HOSPITALITY;

Teknolojia ya ICT imepenya mpaka katika mifumo ya huduma kwa wageni kwa haraka mno, huku ikizama katika utendaji wa hoteli, kuunda upya shughuli za masoko, kukuza huduma kwa wateja, kuimarisha huduma za kifedha, huduma za usafiri wa anga pamoja na huduma za kuwezesha ufanyaji wa biashara mtandaoni. Hii imeleta mafanikio zaidi baada ya kugunduliwa mifumo ya Computerized Reservetion Systems (CRS‘s) kuchukua nafasi ya mfumo wa zamani wa kuandikisha wageni katika mahoteli na katika vituo vya afya.

E-TRAVEL AGENCIES:

Teknolojia ya ICT imeleta maendeleo makubwa katika uendeshaji wa shughuli za taasisi mbalimbali na wakala wa kusafirisha na kutembeza wageni na watalii ambapo imeimarisha sana shughuli za ndani kama uhasibuukaguzi na rasilimali watu pamoja na shughuli za nje kama huduma kwa wateja, mifumo ya tiketi na mawasiliano ya wabia. Licha ya kuwa na 15% ya idadi yota ya watu duniani, Afrika ilikuwa ikihudumia 4% tu ya abiria wa safari za ndege duniani. Hata hivyo huduma hio ilipanda kufikia 6.5% katika kipindi cha mwaka 1998-2009 huku Carpe Verde, Msumbiji, Ethiopia na Tanzania(kabla ya kuimarishwa kwa AirTanzania) zikikuwa kwa makumi ya asilimia (WorldBank report). Maendeleo haya yanaakisi ukuaji wa matumizi ya teknolojia katika eneo hilo ambapo kumekuwepo pia na matumizi ya mifumo ya kudhibiti tiketi (OTS) na mifumo ya kuwasiliana na wateja (CRM‘s). Zaidi mifumo ya kudhibiti tiketi imekuwa muhimu katika kuratibu idadi ya wageni pamoja na kudhibiti maswala ya fedha kiteknolojia.

E-DESTINATION:

Hii ni maalum kwa waendeshaji wa Hoteli, Nyumba za wageni (Guest Houses & Lodges) pamoja na migahawa ya chakula. Sasa teknolojia imeleta mifumo mahsusi kwa ajili ya kurahisisha huduma katika kutafuta soko na kusajili wageni/watalii kirahisi wakiwa popote duniani kwa kutumia simu za rununu au kompyuta. Mfumo wa Destination Management System (DMS) umekuwa muhimu sana licha ya 10% tu ya vyumba vya hoteli 390,000 zinazopatikana katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara kuwa na hadhi ya kimataifa, huku Afrika Kusini ikishikilia nusu ya vyumba hivyo. Hata hivyo Kenya, Mauritius, Shelisheli na Tanzania zinaonyesha kuwekeza zaidi katika huduma za hoteli na teknolojia.

E-COMMERCE:

Jukwaa maarufu zaidi duniani katika kufanya biashara kwa njia ya mtandao kielektroniki. Hii ni muhimu kwa wafanyabiashara wa bidhaa za kiasili na kitamaduni kama shangavinyago na batiki ambapo sasa wanaweza kuweka bidhaa zao katika majukwaa hayo na kufikisha bidhaa zao duniani kote kirahisi zaidi, hivyo kukuza mauzo yao (Majukwaa haya ya ecommerce yanapatikana hapa Rednet Technologies, pitia tovuti yetu kwa kugusa link hii Rednet Technologies).

Kufahamu zaidi kuhusu e-commerce tafadhali fuatilia makala hii hapa kwenye link https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-biashara-za-kielektroniki-e-commerce-businesses/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI?”

Una la zaidi? Tafadhali, weka comment yako hapo chini ili tuweze share mawazo na hoja kuhusu makala haya juu ya unaweza vipi kutumia teknolojia katika kukuza biashara kupitia sekta ya utalii? Kazi kwako mfanyabiashara.

Je umependezwa na makala zetu zilizomo katika website yetu hapa?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) na QR CODE ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA kwenye picha hapa muda wote 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-commerce BUSINESSES)?

Japokuwa imechelewa, lakini kwa sasa Africa ndio inaongoza mbio katika kufanya mapinduzi ya kidijitali kuliko sehemu yoyote duniani. Namna ya kufanya biashara inazidi kubadilika ikionyesha nia ya dhati kufanya maendeleo ya kiuchumi, miundombinu na maswala ya kijamii. Mwaka 2018 nchi wanachama wa Umoja wa Africa walipiga hatua kubwa katika mfumo wa kufanya biashara na muingiliano wa kiuchumi baada ya kuanzisha Eneo Huru la Kufanyia Biashara barani (Continental Free Trade Area AfCFTA). Eneo hili lililoanzishwa linashirikisha nchi 22 zilizoweka sahihi tayari na utekelezwaji wake ulipangwa kuanza mwaka 2019 (tayari umeshaanza).

Hata hivyo mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuzishirikisha nchi ambazo bado si wanachama wa eneo hili jipya, inatarajiwa eneo hili kufikia soko la watu takribani bilioni 1.2 barani wakiwa na jumla ya pato la ndani la taifa (GDP) la dola za kimarekani trilioni 2.5 kwa pamoja, kwa mwaka. Hii inatarajiwa kuwa ni mapinduzi makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nyanja ya uchumi wa Afrika.

Sasa, swali linakuja; Afrika(wafanyabiashara, makampuni/mashirika na Serikali) imejiandaa vipi na mapinduzi haya ya uchumi wa kidijitali? Na zaidi, watunga sera/sheria wataangalia vipi biashara za kielektroniki (e-commerce) kama mada muhimu katika eneo hilo jipya la kufanya biashara huru barani?

Tume ya kudhibiti uchumi wa Africa ya Umoja wa Mataifa (ECA) ikishirikiana na Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) pamoja na Baraza la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo ya kibiashara (UNCTAD) mwaka huu 2019 imechapisha ripoti yake ikiangazia maendeleo ya Afrika kiujumla katika nyanja za kiuchumi, siasa na kijamii.

URAHISI: Imeonekana kwamba e-commerce inaweza kufanya biashara ya bidhaa na huduma kwa urahisi zaidi ambapo itarahisisha mwenendo mzuri wa biashara kati ya wazalishaji, wafanyabiashra na walaji pamoja na kumbukumbu zao na miamala ya kifedha.

MITANDAO YA KIJAMII: Pia imeonekana kwamba e-commerce inapatikana na kufanyika kirahisi katika mitandao ya kijamii kama facebook na Instagram ambapo ndipo mahali kuna watumiaji wengi zaidi wa Intaneti duniani (zaidi ya watu bilioni 2 kati ya watumiaji bilioni 4 wa intaneti).

KUTOKUWA NA MIPAKA: Mfumo wa uchumi wa Kidijitali kiasili umetengenezwa kuepuka mipaka ya kijiografia katika kufanya biashara na kubadilishana fedha ambapo mabadiliko haya ya kiteknolojia yataongeza umakini zaidi katika mwenendo wa masoko na gharama. Lakini bado wimbi kubwa la watu watakaoshiriki kwenye soko barani wanaonekana wataachwa nyuma kutokana na kutokuingiliana kwa lugha na vita/ghasia za mara kwa mara katika baadhi ya jamii/nchi.

BIASHARA: Kwa mujibu wa UNCTAD mwaka 2016 kwa dunia nzima e-commerce iliweza kupitisha mauzoya takribani dola trilioni 26 ambapo 90% ilikuwa ni Biashara kwa Biashara (B2B e-commerce) na 10% ilikuwa ni Biashara kwa Mlaji (B2C e-commerce). Hata hivyo kupima mwenendo wa e-commerce katika baadhi ya nchi zinazoendelea imekuwa ni changamoto kupata data na takwimu, haswa katika nchi za Afrika.

IMPORTATION: Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kwamba Biashara kati ya nchi na nchi imekua kwa kiasi kikubwa Afrika ambapo zimechagizwa na vituo vichache vya kiteknolojia (Hubs) ambavyo vimerahisisha mno mwenendo wa biashara. Biashara kati y nchi na nchi (Intraregional import) imekuwa zaidi ya mara 3 katika miongo miwili iliyopita kufikia 12%- 14% sawa na dola bilioni 100 ikichagizwa na uwepo wa jumuiya za kiuchumi barani (Subregional Economic Communities REC‘s).

UZOEFU: Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na umri wa Jumuiya hizi za Kimaendeleo barani Afrika ambapo uzoefu huo hutumika kuongeza jitihada katika kuboresha namna ya ufanyaji biashara kuelekea uchumi wa kidijitali kiteknolojia. Uzoefu huo pia hutumika kuunganisha jumuiya moja na nyingine (mf, SADC na COMESAna EAC) ambapo zitazalishwa nafasi nyingi zaidi za kufanya biashara kati ya nchi wanachama na ripoti zinaonyesha 75% ya biashara hizi ndani ya jumuiya barani Afrika zimefanyika mwaka 2017 peke yake na nusu ya biashara hizo zilifanyika katika jumuiya ya SADC.

Chini ya mwavuli wa AfCFTA nchi wanachama zinatarajia kufuta tozo/ushuru kwa 90% ya bidhaa zote zitakazopitishwa na kufanyiwa biashara katika eneo hilo. Hii itaruhusu uwezekano wa kupunguza mlolongo wa kodi au kuongeza idadi na thamani ya bidhaa na huduma zitakazohusishwa. Matokeo yoyote katika punguzo hilo linalotarajiwa katika muktadha wa biashara kidijitali yataleta picha tofauti. Kupunguza mlolongo wa tozo za mipakani baina ya nchi na nchi kutapungua kwa 15% pekee ikitegemea thamani ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi husika. Hii ni kwa mujibu wa Tume inayoshughulikia Uchumi wa Afrika kutoka Umoja wa Mataifa (UNECA) mwaka 2018.

Sasa mwaka 2018 Jumuiya ya COMESA ilibuni mfumo wa kudhibiti eneo huru la kibiashara kidijitali (Digital Free Trade Area DFTA). Mfumo huu umeundwa na mambo yafuatayo;

•E-trade: Hili ni jukwaa mahsusi kwa ajili ya kufanya biashara za kimtandao na kuwezesha malipo ya kielektroniki, mobile apps kwa ajili ya wafanyabiashara walioko katika Jumuiya hio.

•E-logistics: hili ni jukwaa maalum kwa ajili ya kuwezesha biashara ya usafirishaji wa mizigo baina ya nchi wanachama wa jumuiya.

•E-legislation: huu ni mfumo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara rasmi ambao unawawezesha kufanya miamala na malipo kielektoniki.

Mfumo huu uliobuniwa na Jumuiya ya COMESA umelenga kutangaza biashara za wanajumuiya katika nchi wanachama ikijumuisha kupitia majukwaa ya e-commerce. Mfumo huu ulikuwa ni mfanano wa mfumo uliotengenezwa na kuzinduliw na nchi ya Malaysia mwaka 2017 katika muktadha wa kufanya biashara huru ndani ya eneo maalum.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.

Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana, shuka nazo:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-biashara-ya-fedha-za-kidijitali-cryptocurrency-business/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)”
  2. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia;

e-mail: info@rednet.co.tz

tovuti: https://rednet.co.tz

Simu:+255765834754

TEKNOLOJIA KATIKA BIASHARA ZA KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA (TECHNOLOGY IN SUB SAHARAN BUSINESS )

Kwa watumiaji wengi wa simu za mkononi waishio Kusini mwa jangwa la Sahara, simu ya mkononi si kwamba ni kifaa cha mawasiliano tu, lakini zaidi ni kifaa muhimu cha kuperuzi mtandaoni na kupata huduma mbalimbali za msingi za kibinadamu. Ujio wa simu za rununu (Smartphones) eneo hilo umekuwa maradufu katika miaka ya hivi karibuni. Watumiaji wa simu za rununu wameongezeka kutoka 25% mwanzoni mwa muongo huu (2010’s) mpaka kufikia 44% mwishoni mwa mwaka 2017. Hii ni chini ya wastani wa kidunia wa 66% katika ongezeko hilo la watumiaji wa simu za mkononi. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa shirika la kimataifa la mfumo wa mawasiliano ya simu GSMA.

Watumiaji hao wa simu ambao ni 44% ya jumla watu waishio katika eneo hilo sawa na watu milioni 444 ambao pia ni aslimia 9% tu ya watumiaji wote wa simu za mkononi duniani wanatajwa kupatikana katika eneo hilo la kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia inatajwa kwamba ongezeko hilo la watumiaji litakuwa katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) kwa 4.8 katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2022, ambacho ni zaidi ya mara mbili ya CAGR ya dunia nzima katika kipindi hicho hicho.

Moja ya vitu vinavyotoa nguvu katika ongezeko hili ni pamoja na uwezo wa simu za rununu (janja) kuunganisha watu wengi kupitia huduma za intaneti na mitandao ya kijamii ambapo katika mitandao hio ndipo panapotumiwa na watu wengi kama sehemu ya kukutana, kubadilishana mawazo, kuburudika na kufanya biashara. Hivyo kufanya mitandao hio ya kijamii kuzidi kuwa na umuhimu kadiri muda unavyokwenda.

Kibiashara hii ina maana gani?

Ripoti hio ya GSMA iliyochapishwa mwaka 2018 inataja kwamba ukuaji wa teknolojia umerahisisha mambo mengi muhimu yakiwemo utolewaji wa elimu, maswala ya afya na tiba na pia kuwezesha mazingira bora ya kufanyika biashara katika kutunza na kuonyesha kumbukumbu mbalimbali, miamala ya kifedha na jinsi bora ya kumhudumia mteja hata akiwa mbali na mzalishaji kupitia majukwaa ya huduma za kifedha za kimtandao na IoT (Internet of Things). Ripoti hio pia inaakisi kasi ya ukuaji wa matumizi ya simu za rununu (samrtphones) pamoja na vifaa vya kiteknolojia mpaka kufikia mwaka 2025 katika utendaji na utoaji wa huduma mbalimbali za kibinadamu pamoja na shughuli za kibiashara katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”
  5. https://rednet.co.tz/kuanzishwa-kwa-eneo-huru-la-biashara-barani-africa-afcta-kuna-manufaa-gani-kwako/ yenye kichwa “KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?”