Tag: rfid

mapinduzi ya viwanda

FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA KATIKA BIASHARA DUNIANI

Japokua ilipitwa na zama 3 tayari, lakini sasa Afrika imedhihirisha kwamba haitaki kupitwa tena katika Mapinduzi ya 4 ya viwanda Duniani. Hii ni kutokana na kukua na kuimarika katika sekta za Afya, Elimu, Biashara, Teknolojia pamoja na Mahusiano na Muingiliano wa kijamii ikichagizwa na maendeleo katika miundombinu, usafirishaji na mitandao ya kijamii. Leo tuta fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. Ni nini na yanaashiria nini kwenye maendeleo ya biashara zingine? Makninika mpaka mwisho.

Mwezi September, 2019, jijini Cape Town Afrika Kusini ulifanyika mkutano wa kiuchumi wa WEF (World Economic Forum) ambao unazishirikisha nchi mbali mbali duniani, wafanyabiashara pamoja na wadau wa uchumi.

Mwaka huo 2019 viongozi waliokutana kujadili mustakabali wa Afrika walikua na jambo la msingi sana ambalo linatumainiwa kuleta maendeleo katika uchumi barani ambalo ni Utekelezaji wa Kuanzishwa kwa Eneo Huru la Biashara Barani (African Continental Free Trade Area AfCFTA). Baada ya miaka mingi ya mazungumzo, makubaliano yamefikiwa ya jinsi ya kuvunja vikwazo vya kibiashara, kukuza uchumi na kuunganisha nchi ambazo katika historia zilikuwa na mahusiano mazuri ya kibiashara na bara Ulaya, Amerika na Asia. Kufahamu zaidi gusa hapa chini:

Changamoto; Afrika (wafanyabiashara, kampuni na mashirika) imejifunza nini katika Kongamano hilo la Kiuchumi (WEF)? Na zaidi, Afrika inajiandaa vipi na Mapinduzi ya 4 ya viwanda yanayoendelea duniani?

Kufikia mwaka 2018 Afrika peke yake iliripotiwa kuwa na vijana takribani milioni 200 wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24. Na namba hio inatajwa kuongezeka mara mbili kufikia mwaka 2050.

Sasa “Kuwa na bara lililosheheni vijana ni fursa adhimu sana, lakini vile vile ni tishio kubwa.” alitahadharisha Albert Zeufack, Mchumi Mkuu wa Benki ya Dunia barani Afrika. “Ni tishio kama hatutohakikisha idadi hio ya vijana hawaanzi kufanya kazi inavyotakiwa.” Sasa kufikia Mapinduzi ya 4 ya viwanda, maeneo kadhaa yaliangaziwa na kituo cha mabadiliko ya kiuchumi barani (Africa Center for Economic Transformation, ACET) kwa niaba ya Benki ya maendeleo barani AfDB.

africa na mapinduzi ya viwanda

1. MACHINE LEARNING/ARTIFICIAL INTELLIGENCE/ROBOTICS;

Fikiria kuhusu gari inayojiendesha bila dereva na kufuata sheria na alama za barabarani ipasavyo ikijumuisha foleni. Watu wengi wangesita kupanda katika gari inayojiendesha yenyewe bila dereva, lakini hayo ndio mapinduzi halisi ya viwanda kupitia teknolojia.

Pia eneo hili limeshuhudiwa na ubunifu mwingi ukiwemo; mashine za kisasa za kuvuna na kupembua nafaka na madini, mifumo ya kiautomatiki inayoendesha ndege, meli pamoja na Teknolojia ya kupima udongo. Ni wazi mashine zinaweza kufanya kazi zifanywazo na binadamu katika zama hizi za mapinduzi ya 4 viwanda.

Swali, umejiandaeje kulinda taaluma yako dhidi ya zama hizi za mashine kujifunza (machinelearning) pamoja na teknolojia ya akili isiyo ya asili (ai)?

2. INTERNET OF THINGS (IoT);

Vifaa vingi vya kielektroniki vinavyotumiwa na mwanadamu sasa vinao uwezo wa kuingiliana na vifaa vingine kirahisi katika kurahisisha utendaji. Fikiria pale unarudi nyumbani na kuwasha feni yako kwa kutumia simu yako ya rununu (smartphone). Au kuweza kuendesha jokofu lako kwa kutumia teknolojia ya RFID. Kuunganishwa vifaa vya kielektroniki na huduma za intaneti imerahisisha sana mfumo wa mawasiliano na manunuzi ambao umeinua uchumi japo faida zake bado hazijasambaa sana barani Afrika.

Fikiria vile unaweza nunua bidhaa katika duka bila kumwona hata muuzaji. Hii inawezeshwa na teknolojia za biashara za kielektroniki (ecommerce) ambapo mteja anaweza kulipia kwa kutumia kadi yake ya benki au huduma za kifedha za simu ya mkononi kama MPESA na tigopesa. Katika bara ambalo muingiliano ni mkubwa kama Afrika, hili ni jambo la kutilia maanani sana, haswa wakati huu ambapo unajaribu ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. (Ambapo sisi kama Rednet Technologies ni wadau wakubwa kuhakikisha hupitwi na huduma za kisasa kwa kutumia teknolojia).

Kufahamu mapinduzi ya IoT katika biashara na maisha kwa ujumla tayari tumekuwekea makala maalum kupitia link hii hapa MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA

3. DATA MINING/DATA SCIENCE TECHNOLOGIES;

Kituo cha ACET katika mwaka 2018 kiligundua kwamba “kuvua taarifa nyingi mtandaoni, kwa kutumia kompyuta zenye uwezo mkubwa na kanuni za mifumo ya Akili isiyo ya Asili (AI), huwezeshwa kupatikana kwa ripoti bora ya taarifa sahihi.” Fikiria mifumo ya tiketi za ndege, hoteli, mifumo ya kulipa kodi na taarifa za mteja wa benki.

Sekta ya Takwimu inafurahia sana ujio wa teknolojia ya Kuvua/Kuvuna Taarifa na Sayansi ya Taarifa. Jinsi ya utendaji katika teknolojia hii ni fursa adhimu sana katika kuimarisha biashara kwa kutumia takwimu sahihi zilizovunwa kutokana na taarifa mbalimbali za watu. Mifumo ya tiketi za ndege, Usajili wa vyumba vya Hoteli, taarifa za wateja wa benki na hata mfumo wa Kulipa kodi (Tax returns), hivi ni baadhi ya vyanzo vya ukusanyaji wa taarifa muhimu katika kufanya Uvunaji wa Data na Sayansi ya Data. Serikali za Africa zinamiliki kiwango kikubwa cha taarifa hizi. Je, italeta manufaa kwa Umma au itafanywa kama biashara na wajasiriamali? (Tafiti na ripoti tunazokuwekea kwenye makala zetu hizi zitakupa majibu.😋)

4. 3D PRINTING;

Ama kwa hakika mapinduzi ya viwanda yanakuja na mengi. Hebu buni bidhaa yako kwenye kompyuta halafu ichapishe kama ilivyo. Kutoka ubunifu uliotengenezwa kimchoro mpaka uhalisia katika kuchapisha tu, hii inakwenda kubadili hata namna ya uendeshwaji wa viwanda barani Africa ambapo ugunduzi huu unaleta matumaini katika uwanda wa ubunifu na ujenzi ambao unatazamiwa kuleta maendeleo katika nchi za Afrika. Viwanda vinawezaje kuendana na teknolojia hii ya Uchapishaji? Vimal Shah mkuu wa shirika la viwanda vya BIDCO nchini Kenya mwaka 2017 alinukuliwa akitania, “Tunaweza kuchapisha pizza wakati ujao.”😂

Sasa watunga sera na sheria barani walishaona uhalisia huu kama kuchapisha mfano wa kitu halisi (3D-Printing) katik mipango yao ya muda mrefu?

5. BLOCKCHAIN/TRUST TECHNOLOGIES;

Mwaka 2018 kituo cha ACET kiligundua kwenye uchunguzi wake kwamba teknolojia ya Blockchain inawafanya watu hata wasiaminiana au kujuana, kuweza kushirikiana bila ya kuwa na haja ya kwenda kwenye mamlaka za serikali. Yaani Blockchain ni jalada huru linalosajili miamala ya kifedha kati ya watu wawili au zaidi kwa usahihi na njia bora zaidi. (Tulishaelezea kuhusu Blockchain na cryptocurrencies kwenye makala zetu zilizopita). Sasa itakuaje kwa huduma za kibenki, wanasheria, wakala wa fedha (brokerage firms) na wahusika wa kiserikali katika maswala ya kifedha? Kitawakuta nini, tutajadili kwenye athari ya mapinduzi ya viwanda mbeleni.

mapinduzi ya viwanda

Si ajabu, teknolojia ya Blockchain inaonekana kama mkombozi dhidi ya vitendo vya Rushwa kutokana na undeshwaji wake ulio sahihi na wa haki. Kwa inavyoonekana teknolojia hii ya Blockchain inakwenda kuwa pigo kubwa kwa watu wenye misuli ya kiutawala, madikteta wa waendeshaji wa siasa chafu. Itakapofika siku Teknolojia hii imefikia matumizi yale yaliyonuiwa wakati inaanzishwa, basi wahafidhina na mawakala wa kifedha wa serikali na mashirika binafsi watapoteza nguvu zao. Hakutakuwa na haja ya mihuri, wala sahihi, wala zile nenda urudi kesho tukuhudumie. Blockchain itakwenda kuiweka Afrika huru dhidi ya kero za huduma za kifedha na usalama wake kuwa katika ukuaji mzuri. Haya ndio mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani.

5. BIOPHYSICS AND BIOENGINEERING;

Eneo la 5 ambalo kituo cha ACET imeliacha ni kuhusu mtandao wa mifumo ya kibaolojia na kifizikia. Utahitaji mkono wa bandia unaoweza kuendeshwa na ubongo wako kwa usahihi ikitokea mkono wako halisi umekatika? Hebu fikiria hapo. Tunakubali kwamba asili ni bora sana kuliko sisi, hivyo ni bora kujifunza kwayo, kwasababu mapinduzi haya ya viwanda kwa kuchagizwa na ukuaji wa kiteknolojia duniani yatafanya taaluma ziweze kunyumbulika kwa namna nyingi sana hapo baadaye. Je, mifumo ya elimu imejiandaa na hili katika maandalizi ya mitaala yake ya muda mrefu?

Sasa tumeshajua yanayokuja na Mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani. Afrika, bara ambalo ajira bado ni tatizo kubwa kwa vijana, wataweza vipi kupambana na athari za mapinduzi haya? Kuna nadharia tatu (3) katika kukabiliana na hali hii;

1. Afrika inaweza kuketi chini na kubaki kutizama dunia nzima ikipambana katika Mapinduzi haya. Hii ilishafanyika katika zama 3 zilizopita za Mapinduzi ya viwanda ambapo Mapinduzi ya Kwanza yaliegemea katika kutengeneza mifumo ya Kimekanika na matumizi ya Injini za mvuke katika kutengeneza bidhaa kama nguo.

Mapinduzi ya pili yakiwa ni kuhamasisha Uzalishaji mkubwa (mass production) wa bidhaa viwandani yakichagizwa na Henry Ford na awamu ya 3 ya mapinduzi ikiwa ni zama za kidijitali katika uzalishaji.

Ukitizama elimu ya msingi ya kuunda Injini ni ile ile iliyokuwepo tangu mwanzo, lakini bado Afrika haijaweza kutengeneza magari yake yenyewe.

2. Afrika inaweza kufanya kile ilichokifanya katika kuingia kwenye zama za Kidijitali, mtindo wa kuruka kama chura (leapfrog). Kwa mfano nchini Kenya watu hawakuwa na huduma za simu za mezani miaka ya 1990’s kurudi nyuma, hali kadhalika ilikuwa hivyo nchini Tanzania pamoja na nchi nyingi za kusini mwa jangwa la Sahara katika ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani.

Lakini baada ya mwaka 2000 watu wengi katika eneo hilo wameweza kumiliki simu za mkononi hata kama hawakuwahi kumiliki simu za mezani. Simu za mkononi zimekuja na teknolojia kubwa zaidi baada ya kuunganishwa na huduma za kifedha kama MPESA, huduma za internet, GPS na ramani, huduma za kiafya pamoja na biashara za kielektroniki ecommerce.

Mazingira ya Uchumi jumuishi (social economy) yanafanya iwe rahisi kukaribisha zama za Mapinduzi ya 4 ya viwanda. Watu wengi duniani hawapendi kusoma vitabu, hivyo sasa tunaweza kuziachia mashine kufanya kazi mbalimbali badala yetu. Kama Blockchain inatazamwa kwenda kuangamiza kabisa changamoto ya rushwa, Teknolojia ya 3D-Printing itafanya hata nyumba zetu kuwa viwanda vidogo katika kubuni bidhaa mbalimbali.

Taarifa zote zilizo kwenye mashirika ya Serikali na binafsi ikijumusha taasisi za dini zinaweza kuvunwa kwa ajili ya kupata takwimu mbadala katika chunguzi mbalimbali. Hii inatazamwa kuwa njia mbadala kuyafikia mapinduzi ya viwanda ya 4. Unahitaji kuLeapfrog biashara yako (kuepuka gharama kubwa za matangazo)? Tunalo suluhisho, wasiliana nasi mara moja tukupatie.

3. Vile vile, Afrika inaweza kukuza thamani ya uzalishaji na ubunifu wake ili kuwa mshindani halisi duniani katika kutengeneza na kusambaza bidhaa na huduma za kiteknolojia, kama inavyofanyika mahali kwingine duniani.

Japan imeweza kufanya hivyo katika sekta ya magari na India inafanya vizuri katika sekta ya Famasia na Programu za Kompyuta. Sasa kwanini Tanzania isiwe kinara katika Sayansi ya Data(Data Science) duniani. (maana mbongo mpe picha tuu, vingine utaona atakapovipata😂. Natania.) Sekta hizi za teknolojia zinataka matumizi ya akili zaidi, sio kama viwanda vya saruji na chuma ambavyo vinahitaji mtaji mkubwa wa kifedha.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi kuyapokea Mapinduzi haya ya 4 ya Viwanda katika eneo lako la biashara? Pitia makala hizi ili kupata taarifa zaidi:

  1. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BANDO LAKO NI MTAJI
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  4. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mapinduzi ya 4 viwanda katika biashara duniani
Archiedee Co limited

UMUHIMU WA TEKNOLOJIA BORA KATIKA KILIMO

Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) mpaka mwaka 2050 watu wataongezeka mpaka kufikia bilioni 9.1 na kulisha namba hii ya watu, uzalishaji wa chakula duniani utahitajika kukuwa kwa 70% angalau. Kwa Afrika ambayo inatarajiwa kuwa na jumla ya watu bilioni 2 kufikia 2050, uzalishaji wa chakula kupitia sekta ya kilimo inabidi ukue haraka zaidi ya wastani wa dunia ili kupunguza dalili za baa la njaa. Sasa leo tuangazie umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo. Teknolojia ina mchango gani? Makinika mpaka mwisho wa makala hii kufahamu.

Mpaka nyakati hizi bado sekta ya kilimo inakumbwa na majanga ambayo hayajapatiwa suluhu ya kudumu kama kudhoofu maendeleo maeneo ya vijijini ambapo kilimo ndipo hufanyika kwa kiasi kikubwa, kutokuwa na soko mbadala kwa mazao yatokanayo na kilimo, miundombinu mibovu, vita vya wenyewe kwa wenyewe, magonjwa kama UKIMWI, majanga ya kiasili pamoja na ukataji ovyo wa misitu.

Sasa katika zama hizi za Kidijitali, Teknolojia ina mchango gani katika kukuza sekta ya kilimo na kuboresha uchumi wa mkulima?

Simu za rununu (smartphones), mfumo wa GPS, vifaa vya RFID na barcode scanners ni baadhi ya vifaa vinavyotumika katika sekta ya kilimo katika juhudi za kuboresha uzalishaji ambapo picha za satelaiti kwa mfano, huweza kutumika kupima ukubwa wa eneo sahihi la kufanyia shughuli za kilimo kwa ubora wa hali ya juu. Vile vile vifaa maalum vinavyoweza kuhisi hali ya udongo (soil sensors) hutumika kujua ni aina gani ya mazao inafaa kulimwa kuendana na udongo wa mahala husika. Zaidi mamlaka za hali ya Hewa pia hutoa mrejesho bora kuhusu utabiri wa hali ya hewa kwa kutumia vifaa vya kisasa na teknolojia bora kwenye vipimo vyao.

Ugunduzi wa Programu za kompyuta na Applications za simu unaongeza chachu zaidi katika kufanya kilimo cha kisasa na kudhibiti taarifa muhimu katika utendaji wa hatua kwa hatua, kufanya miamala ya kifedha pamoja na kutafuta masoko. Applications maalum ziitwazo Mobile App for Agriculture and Rural Development (m-ARD) hutumika kwa usahihi katika kufanya miamala na kudhibiti maswala ya kifedha katika ufanyaji wa kilimo. Kupitia MPESA nchini Kenya, taasisi ya kilimo ya Kilimo Salama Agriculture Insurance imeongeza thamani ya bidhaa za wakulima kwa wastani wa 50% kwa bidhaa za kilimo, sawa na $150 kwa mwaka.

CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.
Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) mpaka mwaka 2050 watu wataongezeka mpaka kufikia bilioni 9.1 na kulisha namba hii ya watu, uzalishaji wa chakula duniani utahitajika kukuwa kwa 70% angalau. Kwa Afrika ambayo inatarajiwa kuwa na jumla ya watu bilioni 2 kufikia 2050, uzalishaji wa chakula kupitia sekta ya kilimo inabidi ukue haraka zaidi ya wastani wa dunia ili kupunguza dalili za baa la njaa. Sasa leo tuangazie umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo. Teknolojia ina mchango gani? Makinika mpaka mwisho wa makala hii kufahamu.

Je, wajua kwamba takribani theluthi moja (1/3) ya mazao yote yanayovunwa duniani kwa mwaka hupotea kwa kushambuliwa na wadudu waharibifu, magugu na magonjwa?

Sasa kwa kuligundua hili wataalam walibuni mbegu maalum katika maabara za kisayansi kwa kuboresha vinasaba (DNA) Za mazao na kufanikiwa kupata kitu walichoita Genetic Modified Organism (GMO). Kitaalam mbegu na mimea itokanayo na GMO imekuwa na faida nyingi katika kilimo zikiwemo; kuwa na uhakika wa kupata mazao mengi kwa kutumia mbegu kidogo tu. Vilevile GMO hizi zimetengenezwa zikiwa na ustahimilivu dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa jambo linalozipa uhakika wa kukuwa, kumea na kuzaa ipasavyo. Hata hivyo kinga hio dhidi ya wadudu waharibifu haiwazuii wadudu kama nyuki, vipepeo, minyoo wa ardhini na baadhi ya bakteria ambao huwa na jukumu muhimu katika uchavushaji wa mimea na hivyo kuleta mazao stahiki. Faida zingine ni kutunza na kuboresha rutuba ya udongo pamoja na kusaidia kuhifadhi maji ardhini, mambo ambayo yanaondoa hatari ya kutokea kwa baa la njaa duniani lakini zaidi, kuboresha uchumi wa mkulima.

Je unaamini kwamba wingi ni Faida?

Sasa majibu ya wataalam wa maswala ya kilimo duniani ni kwamba si mara zote wingi unaweza kuleta faida. Hii inajidhihirisha katika matumizi ya mbolea zinazotengenezwa maabara kiteknolojia katika kufanya kilimo ambapo kiasi kikubwa cha mbolea huweza kupelekea kudhoofisha mimea na kutishia kufifia kwa mazao kutokana na mlundikano wa kemikali zilizopo kwenye mbolea ambazo zikizidishwa ni hatari. Hivyo inashauriwa mbolea inayotumika iendane sawia na aina ya udongo, kiasi cha maji katika umwagiliaji na aina ya mazao yanayolimwa ili kuhakikisha mazao yanayotoka yanakuwa bora zaidi. Hata hivyo taarifa nyingi kuhusu matumizi ya mbolea za kisasa hupatikana kupitia applications za simu mahsusi kwa shughuli za kilimo ziitwazo m-ARD’s.

Shirika la maswala ya kilimo la M-Farmer Initiative Fund lilianzishwa mwaka 2011 kwa ushirikiano wa Mfuko wa hifadhi ya jamii wa Bill and Melinda Gates Foundation ili kuratibu, kufadhili na kukuza sekta ya kilimo barani Afrika. Shirika hili limepanga kufikia wakulima walioko katika nchi za Ethiopia, Malawi, Rwanda, Kenya, Zambia na Tanzania.

Hilo ni mojawapo la mashirika makubwa kuonyesha nia ya dhati katika kuendeleza shughuli za kilimo duniani, kuchochea umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo na kupunguza baa la njaa, kuboresha biashara za mazao ya kilimo pamoja na kukuza uchumi wa mkulima mmoja mmoja. Mashirika hayo yanazindua mifumo ya kimtandao ya malipo, mikopo na bima za kidijitali. Kwa mfano shirika la FarmDrive la nchini Kenya limezindua huduma za kifedha mahsusi kwa ajili ya wakulima ambapo kupitia shirika hilo wakulima hata wasio na akaunti za benki na wakulima wadogo kabisa hupata mikopo huku ikisaidia taasisi za kifedha kuongeza huduma za mikopo ya kilimo kwa gharama nafuu.

Kwa wafanyabiashara na kampuni zilipo ukanda wa Afrika Mashariki hii ni fursa kwao kuelekeza macho yao katika sekta ya kilimo kama inavyofanya FarmDrive nchini Kenya na shirika la kimataifa la M-Farmer.

Unalionaje hili? (tafadhali share kwenye comments) Hivyo kupitia jitihada za mashirika hayo, wakulima sasa wanaweza kupata mbolea, mbegu bora na mifumo mizuri ya umwagiliaji ili kukuza shughuli zao. Mchakato huo huboresha kasi ya uzalishaji katika kilimo na kupunguza changamoto kwa kutumia takwimu sahihi katika utendaji wa shughuli za kilimo kwa kutumia data za kisayansi na hivyo, umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo unazidi kuonekana. Kwa mfano matumizi ya vifaa vya umwagiliaji vinavyotumia nishati ya jua kusukuma maji kutoka katika chanzo chake kama mto, ziwa, bwawa au bahari. Vifaa hivi vimerahisisha sana swala zima la umwagiliaji.

Vilevile kwa kuzingatia ukweli kwamba mashamba mengi yapo maeneo ambayo ni mbali na huduma za mitandao ya simu na intaneti, hivyo kufanya huduma hizo kuwa hafifu, nchi kama Ethiopia imerusha satelaiti yake na kufanya wakulima kuwa katika nafasi nzuri kunufaika na mradi huo. Serikali za nchi zingine za Afrika Mashariki zinakwama wapi kwenye hili?

umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo.

matumizi ya TEHAMA katika Satellite

Hata hivyo zama hizi kutokana na kuimarika kwa miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji, pamoja na maendeleo katika sekta ya sayansi na teknolojia ya Habari na mawasiliano, imekuwa rahisi sana kupata taarifa kuhusu Hali ya Hewa, Hali ya soko na ushindani, mazingira ya miundombinu ya uchukuzi, mfumuko wa bei na uelekeo wa mahitaji ya wateja. Kilimo kimeja kufanyika katika namna rahisi sana katika kuuza mazao baada ya kuvuna, shukrani umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo cha kisasa na chenye tija.

Kufahamu zaidi namna unavyoweza kuimarisha shughuli zako za kilimo kwa kutumia teknolojia tafadhali pitia makala zilizomo kwenye links hizi hapa:

  1. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWUWEKEZA
  3. UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021
mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi

MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI

Ubunifu wa kiteknolojia na zama za Kidijitali huathiri karibu kila mchakato katika utendaji na uendeshaji wa mfumo wa Usafirishaji na Uchukuzi duniani kote. Kuanzia njia na namna ya usafirishaji wa majini/baharini, ardhini na angani, usimamiaji wa mizigo pamoja na shughuli za utawala na ugavi zikiwemo utaratibu/usimamizi wa nyaraka na ufuatiliaji mzuri wa malipo. Leo sasa tuangazie mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi. Kuna nini kinaendelea huko? Makinika..

Idadi wa watu duniani itaongezeka kutoka watu bilioni 7.4 mpaka watu bilioni 10.6 kufikia mwaka 2050, vile vile idadi ya mizigo inayosafirishwa kwa njia ya meli peke yake itaongezeka mpaka mara 4 ambayo inatarajiwa kukua kwa ongezeko la 715% kwa nchi za Africa.

Pia kasi ya ukuaji wa miji itakuwa kwa 56% ya idadi ya watu katika Africa mpaka mwaka huo 2050. Ongezeko hili linatarajiwa kuchagizwa na kasi ya ukuaji wa miji, kukua kwa kipato cha mtu mmoja mmoja, kupenya kwa matumizi ya intaneti pamoja na urahisi wa kupata na kutumia Teknolojia mpya.

Hata hivyo mtindo wa uchukuzi wa mizigo kwa kupitia njia ya meli kwa kutegemea nyaraka peke yake unatarajiwa kupungua kwa kiasi kikubwa kufuatia ujio wa matumizi ya nyaraka za kielektroniki na barua pepe. Hii ni kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la EY.

Kufuatia kasi hio ya ukuaji na mabadiliko, makampuni na biashara zilizopo katika sekta ya Usafiri na Uchukuzi yanahitaji kubadilika ili kumudu kuwepo katika ulimwengu ambao ushindani unakuja kutoka pande zote na teknolojia za kidijitali ndio zitakuwa chachu kuu ya mabadiliko.

Sasa Swali; Teknolojia Inaweza vipi kubadili Kesho ya Sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Leo hii sehemu kubwa ya shughuli za kiuchumi na kijamii hufanyika mtandaoni na haswa haraka zaidi kupitia katika simu janja (smartphones). Ukuaji huu wa kiteknolojia unanufaisha maeneo yote yaliyomo kwenye Sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kama; usafiri wa magari ya mizigo (malori), usafiri wa kimataifa (njia ya anga na majini), usimamiaji wa shughuli za ugavi na kuratibu safari za majini, nchi kavu na angani. Yafuatayo ni mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi barani Afrika;

1. MFUMO WA KURATIBU SAFARI/ONLINE TRACKING SYSTEM (Magari ya mizigo, Meli na Anga): Imezoeleka mteja kuhifadhiwa nafasi ya kusafirisha mizigo yake kwa kujaza fomu fulani ya usafirishaji, halafu anaachwa gizani mpaka siku mzigo wake unamfikia asipoamua kufuatilia kwa kupiga simu. Lakini leo, kwa kutumia huduma za intaneti na programu za kompyuta mteja anao uwezo wa kuagiza na kufuatilia kwa ukaribu zaidi mizigo yake muda wowote akihitaji kufanya hivyo.

Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi

Hii si tu kwamba imerahisisha matumizi ya intaneti kisasa zaidi lakini zaidi teknolojia hii inaokoa muda na gharama za ziada kwa kampuni ya usafirishaji na mtu binafsi.

2. TEKNOLOJIA YA INTERNET OF THINGS (IoT) na RADIO FREQUENCY IDENTIFICATION (RFID): Ulishawahi kufikiria siku fulani una uwezo wa kuwasha feni yako nyumbani kwa kutumia simujanja yako? Sasa leo hii vifaa vingi vya kielektroniki vimeundwa na uwezo wa Wi-Fi na vifaa vya kuhisi mazingira mbalimbali. IoT inafungua nafasi nyingi sana katika kurahisisha shughuli za ugavi kama kupunguza gharama za uendeshaji. Vifaa vya kuhisi mazingira (sensors) pia hufungwa katika magari madogo na makubwa, meli za mizigo, treni na kadhalika. Vifaa hivi hufungwa mfumo wa kengele au mfumo wa GPS ambayo hufuatilia na kuratibu mwenendo wa mzigo kumfikia mteja.

Hali kadhalika teknolojia ya RFID ambayo imeshatumika miaka kadhaa hutumiwa na makampuni ya uchukuzi na usafirishaji kufuatilia mwenendo wa hesabu za bidhaa zao (Inventories). Kwenye teknolojia hii hujumuisha pia matumizi ya barcode za kwenye bidhaa, pamoja na matumizi ya rimoti za televisheni na redio, teknolojia ambayo imetumika kwa miaka mingi zaidi, hivyo kuyafanya makampuni mengi kutumia zaidi RFID’s. Vile vile RFID’s hutumika kusambaza bidhaa katika maghala yao na kuratibu mienendo ya makontena.

3.MAGARI/ MALORI YA KUJIENDESHA NA DRONES: Katika ulimwengu ambao unaendeshwa na matumizi ya kompyuta kutoka mahali fulani kwenda mahali kwingine, utajihisi vipi siku unapokea mzigo kutoka kwenye chombo kinachoruka angali mfano wa helikopta ndogo? Sasa huko ndipo tunapoelekea. Magari ya kujiendesha tayari yanaonekana duniani ambapo kampuni za UBER na EMBARK wametengeneza magari yanayojiendesha japokuwa bado miradi hiyo haijarasimishwa kwa wateja. Ni swala la muda tu kutoka sasa kabla matumizi yake hayajawafikia wateja ulimwenguni kote.

4. MITANDAO YA KIJAMII: Nani ambaye hapitii kwenye mitandao ya kijamii angalau mara moja kwa siku? Nguvu ya mitandao hii ya kijamii inaboresha kwa namna ya kipekee sana sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kwa ujumla wake. Mitandao hii inarahisisha sana katika kutangaza huduma za usafirishaji na uchukuzi pamoja na kampuni kuwasiliana na wateja wake kwa ukaribu na urahisi zaidi katika kutoa taarifa muhimu, dharura na mrejesho kutoka kwa wateja.

Kwa mujibu wa Hootsuite, 59% ya Wamarekani ambao ni watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekubali kwamba huduma kwa wateja kupitia mitandao ya kijamii imerahisisha kujibu maswali na huduma husika.

Zaidi ya yote, miundombinu ya uchukuzi katika nchi za Afrika bado ipo nyuma sana kimaendeleo ukilinganisha na sehemu zingine za dunia. Nchi ya Afrika Kusini ndiyo inaongoza barani kwa kuwa na miundombinu ya kisasa zaidi ya kiuchukuzi ambapo kasi ya ukuaji wa miundombinu kwa mwaka ni ndogo kwa 3% katika kipindi cha mwaka 2012 hadi 2017. Hii ni kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Fedha duniani (IMF).

Kwa upande mwingine nchi za Kenya na Nigeria zinaongoza kwa kuwa na ukuaji mkubwa katika miundombinu yake ya kiuchukuzi na usafirishaji kwa 6.2% na 6.8% katika kipindi hicho hicho (2012-2017). Kwa wafanyabiashara na makampuni ya usafirishaji na uchukuzi; Kuwekeza vema Afrika kunahitaji uelewa mzuri wa maeneo muhimu pamoja na uelewa wa masoko ya wenyeji.

Afrika si tu kwamba ni kubwa mno, lakini zaidi Kuna mtawanyiko mkubwa wa jamii za watu na rasilimali. Hata hivyo, zaidi ya 70% ya makampuni makubwa zaidi duniani yanayozalisha bidhaa za watumiaji tayari zinafanya kazi Afrika. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kimataifa la PwC.

Usipitwe na Ofa Yetu katika msimu huu wa Nane Nane. Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi. Umejifunza nini leo kuhusu mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi? Share nasi mawazo yako kwenye comment au tucheki kwa kugusa WhatsApp namba yetu hii hapa 0765834754.

Makala hizi hapa zitakupa mwanga zaidi katika kuwekeza katika Biashara zinahohusiana na sekta ya Usafiri na Chukuzi hasa katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara:

  1. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  2. USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA
  3. FAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA HABARI NA BURUDANI