OFA YA MSIMU WA SABASABA
Mwaka 2016 wakati nawaza kufungua kampuni from scratch nilifikiri kupata wateja itakuwa rahisi tu. Nikawaza nikimaliza mchakato wa BRELA, TRA na Leseni basi nikituma proposals zangu kwa watu walau 10 ntakuwa nimeshapata wateja wangu nianze kuingiza pesa.
Sasa nilipoanza kutafuta wateja nikawa nashangaa, kila ninapoenda nasikilizwa tu lakini sitafutwi tufanye kazi. Mteja wangu wa kwanza nilikuja kumpata August, 2018 (mwaka mmoja baada ya kufungua kampuni rasmi mwaka 2017). Sikujua maisha yangekuwa magumu kiasi kile.
ILIKUAJE NIKAPATA MTEJA?
Kutokana na kushamiri kwa vitendo vya Utapeli wa mtandaoni, watu wamekuwa waoga sana katika kufanya biashara mtandaoni. Watu wanatapeliwa jamani, kuweni makini mno na miamala mnayofanya kwenye simu zenu pamoja na humu mtandaoni ndugu zangu.
Ilinichukua muda mrefu, almost miaka miwili mpaka nilipogundua MBINU ya kuchapisha makala zenye maudhui muhimu kwa biashara za wajasiriamali kupitia kurasa zangu za LinkedIn, Instagram na Twitter huku nikiziunga na link ya tovuti ya kampuni ambayo ndipo nilipoweka makala kamili.
Baada ya watu kutembelea kurasa zangu za mtandaoni na tovuti yangu na kuona “Thamani ya maudhui” niliyokua nayatoa ndipo nilipopata mteja wa kwanza wa uhakika ambaye mpaka leo bado tunaendelea kufanya kazi pamoja na wateja wengine wengi kutokea hapo.
NILICHOGUNDUA:
Mpaka mtu afanye kazi/biashara na wewe lazima:
1. Awe anakufahamu au tayari anazo taarifa zako za kutosha.
2. Anakuamini (kwamba utafanya kazi yake kwa viwango anavyotaka na pesa yake haiendi bure).
3. Anakupenda (ni ngumu kufanya biashara na mtu ambaye hampendani).
Jiulize hapo, Unaweza vipi kumshawishi mtu ambaye hakufahamu kabisa (a total stranger) akuamini na akupe kazi zake uwe unamfanyia kwa kiwango anachokitaka? Pitia makala hii hapa kwenye link https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kuweza-kushawishi-wateja-katika-biashara-yako/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUWEZA KUSHAWISHI WATEJA KATIKA BIASHARA YAKO”
Nafahamu kuna muda unapitia wakati mgumu sana katika kutafuta wateja wapya katika biashara yako ili kujitanua zaidi, lakini hujui ufanyeje. Hata hivyo, MBINU BORA ya kutanua biashara yako kwa watu usiofahamiana nao kabisa, hasa watu wa mtandaoni (Digital Neighbors) ni hii hapa:
1. Badili matumizi ya Mitandao ya kijamii kwa kupost maudhui kuhusu Thamani ya bidhaa/huduma yako katika maisha ya mtu ili kumvutia awe mteja wako. Weka tips kama Aina za bidhaa/huduma, Bidhaa feki zinajulikana vipi, bidhaa zako zina utofauti gani na zingine, ubora uko vipi nakadhalika.
2. Fungua website ili kujiweka katika mazingira ya kujulikana kwa Utalaam wako mahsusi. Website ndio CV ya biashara yako mtandaoni. NOTE: Mteja atafanya kazi na wewe kiuhakika kwa kuwa wewe ni Mtaalam katika fani fulani na sio salesperson kama wengine pale akiona website yako.
3. Hakikisha mtu aki-search huduma/bidhaa unazouza kupitia google basi anakupata mara moja. Hii kitaalam inaitwa S.E.O (Search Engine Optimization). Hii inakupa fursa bora ya kutanua biashara yako hasa katika matafuto ya mtandaoni ambayo yatawasaidia wateja kukufikia kirahisi.
Sasa, kwa kufahamu hilo, Natoa OFA YA MSIMU WA SABASABA ambapo utakapofungua website yako kwenye msimu huu tutakufanyia SEO, tutakupa tips za kutoa maudhui ya kuvutia wateja kwenye mitandao yako ya kijamii pamoja na kukufanyia Web maintenance BURE kwa mwaka mzima.
Bei ya OFA hii ni laki tano tu (500,000/-) unapata vyote nilivyokutajia. OFA hii itakapokwisha gharama zitarejea kufikia laki tisa elfu hamsini tu (950,000/-) kwa website peke yake. Hivyo wahi kabla OFA haijakwisha. Karibu Tufanye kazi.
Kwa maswali au maulizo yoyote tafadhali tumia mawasiliano yetu yanayopatikana katika tovuti hii.