Tag: mitandao ya kijamii

Pata huduma za Website, SEO, Social Media Marketing na nyinginezo nyingi kutoka Rednet Technologies Branding vs Marketing. Kipi ni kipi? ukweli kuhusu 'Propaganda' Jinsi ya kutengeneza Attention Mtandaoni.

Jinsi ya Kutengeneza Attention Mtandaoni

Hivi unajua kwamba aliyeshinda vita vya 2 vya Dunia ni Urusi, ndiye aliyepigana na Hitler kwa ground. LAKINI, Leo hii kila mtu anaongelea Bomu la Nyuklia la Marekani lililodondoshwa Hiroshima na Nagasaki. Unajua kwanini? Kwa sababu watu wanapenda ATTENTION duniani na leo hapa utafahamu kiundani kabisa jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni ili uweze kunasa wateja zaidi.

Marekani ni mtaalamu haswa kwenye hilo la kutengeneza attention na kusambaza propaganda zenye manufaa ya nchi yake. Jamaa wamefanikiwa kuujaza Ulimwengu “ukweli wao” kwamba lile Bomu la Nyuklia ndo limeipa ushindi taifa hilo na kwamba kwanzia hapo wao ndo wababe duniani na hakuna mwingine. Ila nyuma ya pazia Urusi ndiye anayemiliki Nyuklia nyingi zaidi.

Kujitangazia Ushindi tu, tayari alishaanza kuteka ATTENTION duniani na mataifa mengi yalianza kuvutika katika Silaha, Siasa, Utamaduni na Biashara zingine za Kimarekani. Leo hii Marekani ndo nchi inayosifika kuuza silaha zaidi duniani, Makampuni makubwa karibu yote yapo USA, Microsoft, Google, Meta, Yahoo, Space X nakadhalika.

Marekani ndo nchi inayotambulika kwa mifumo bora ya Kidemokrasia duniani, na mambo kedekede tayari unayajua kuhusu hao jamaa. Unadhani Marekani alipata wapi sifa zote hizo? Kwamba Urusi hana huo ubavu wa kuuza silaha au teknolojia za kisasa? Jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni is the damn strategy they rely on.

Kwenye Biashara Attention inatengenezwa vipi?

Kwenye biashara Mtandaoni hali ipo hivyo hivyo. Ushindani ni mkali mno kila siku. Ni vita. Mtandao wa Internet Live Stat unaonyesha kuwepo na websites zaidi ya Bilioni 1.9 mpaka sasa duniani. Hebu niambie unachomokaje katikati ya vurugu lote hilo kama hujajua jinsi ya kutengeneza ATTENTION? Leo hii wewe upo hapa kwenye tovuti yetu kwa sababu umeona kuna uwezekano ukaweza kuimarisha biashara yako mtandaoni kwa kutengeneza attention fulani, si ndio?

Utaniuliza; “Sasa Faustine, nawezaje kutengeneza hio ATTENTION ili niweze kusurvive huko mtandaoni?” Zipo njia nyingi, za halali na zile zisizo halali. Hapa tutaongelea zile za halali tu. Habari za kupost utupu, vichupi na makalio hapa hazipo.

Kuijuia Google leo ndo mchongo. Binafsi ningepata nafasi ya kurudi nyuma na kumshauri Faustine wa miaka 15 enzi zile, ningemshauri atie nguvu sana kwenye kuijua jinsi Google inavyofanya kazi na namna anaweza kuitumia kukuza biashara na kunasa wateja zaidi.

Leo hii unaweza kutengeneza ATTENTION ya Biashara yako kule GOOGLE kwa kuhakikisha mtu akitafuta chochote kinachohusiana na bidhaa/huduma unazozitoa kwenye biashara yako basi anakipata mara moja na anakipata kwako chap. Hii inafanyika kwa uzuri kupitia Huduma za SEO (Search Engine Optimization).

Hivi si unajua, kwa siku 1 tu huwa kunafanyika matafuto zaidi ya bilioni 3.5 kule google. Sasa kwanini bidhaa/huduma zako tukizitafuta google kule hatukupati? Kama jibu la hilo swali linakusumbua, wala usiwe na wasiwasi tena, sekunde chache zijazo utakwenda kujua cha kufanya.

Kama unatamani kutengeneza ATTENTION kule Google mpaka ifike mahali mtu akisearch kuhusu bidhaa/huduma zako akupate haraka, basi chukua SIRI hizi hapa. Leo hapa utaziona siri (4) tu;

1. Tengeneza website yako na hakikisha inafanya kazi vizuri na ina load faster. Kwanini website? Kwa sababu ni kupitia website unaweza kutengeneza maudhui mengi ndani ya chanzo kimoja, ukafanya uchambuzi kwa kina na kuelezea kwa mapana kuhusu Faida za bidhaa/huduma zako, Mbinu, Jinsi ya kutumia na taarifa zingine. Hili pia unaweza kulifanya kupitia chaneli yako ya YouTube.

2. Andika maudhui ya kutosha kuhusu Faida za bidhaa/Huduma zako, Jinsi ya kuzitumia, Jinsi ya kupambana na Changamoto, Mbinu za kutumia bidhaa/huduma hizo kwa usahihi, Madhara ya Kutotumia bidhaa/huduma zako n.k Umeona hayo maneno hayo yaliyotumika hapo? Hayo yanaitwa Keywords.

3. Hakikisha unatumia keywords nyingi zinazohusu bidhaa/huduma zako ikiwemo JINA LA BIDHAA/HUDUMA hio. Kwenye keywords hapo ndipo Google hukusanya taarifa na kuzihifadhi kwenye database yake, tayari kwa watu kupata majibu pale watakapotafuta kuhusu bidhaa/huduma hio. Ukiweza kutumia Google kama jukwaa la biashara utafaidi sana biashara yako inapokuwa mtandaoni.

4. Ambatanisha Namba yako inayopatikana katika simu za Kawaida na WhatsApp katika makala unazozichapisha kwenye website yako na mitandao yako ya Kijamii. Hio namba yako ya simu ni muhimu sana iwe hewani muda wote. Hakikisha muda wote ukitafutwa unapatikana. Hapa ndo utajua sasa kwanini Mteja achague kufanya kazi na wewe na sio mtu mwingine.

Ukifanya hivyo, utamtengenezea mteja wako mazingira ya kukupata moja kwa moja pale atakapofikwa na uhitaji wa huduma/bidhaa zako atakazoziona huko Mtandaoni. WhatsApp kupitia Status zako unaweza kuchapisha tips, ushauri, faida nk za bidhaa/huduma zako kila siku.

Sasa, tuishie hapo kwa leo, au unasemaje ndugu yangu?

Anyway, ngoja nisikuache bure, muendelezo wa SIR hizo tayari nimeuweka kwenye eBOOK yako MPYA na BORA ya SEO ambayo nimekuandalia. eBook hio inaitwa TEKNOLOJIA YA SEO; JINSI INAIFANYA BIASHARA YAKO KUWA NA SUMAKU MTANDAONI. Katika Kitabu hiko nimekuwekea SIRI 15 tayari kabisa kukufunulia wewe jinsi SEO inavyofanya kazi na namna unaweza kuitumia kukuletea manufaa zaidi kila siku. Hi ndio kitu unakihitaji sasa.

eBook hii itakusaidia kujua mambo yote muhimu kuhusu SEO, ni nini? inafanya kazi vipi? Faida zake ni zipi? Mambo yapi ya kuzingatia ili uifaidi? Kwanini hupati wateja mtandaoni? Yote hayo na mengine mengi yameelezwa kwa mapana kabisa kwenye eBook hio.

Kama nilivyokutaarifu, kuanzia ukurasa wa 27 wa eBook nimekueleza SIRI 15 ambazo zitakusaidia katika kutengeneza ATTENTION ya biashara yako mtandaoni kupitia SEO. SIRI 15!! Hizi siri wanaojiita wataalam wa SEO unaowafahamu hawawezi kukwambia kwa kuhofia kupoteza wateja ukiwemo wewe, ila mimi nimekwambia.

Utajiuliza, Kwanini nimekwambia? Kwa sababu mteja anayo haki ya kufahamu exactly kila kinachofanyika katika mradi wake. Mfano unapojenga nyumba ukikaa karibu na fundi wako utataka kujua bei ya misumari, aina za misumari, aina za milango, mbao, rangi ipi ipakwe wapi na kwanini, aina za kokoto, mchanga wa plasta ni upi na vitu kama hivyo.

Kadhalika katika SEO, ni muhimu ukafahamu kinachofanyika humo ndani, ili uweze kushiriki kufanya mwenyewe na kupata ujuzi wa ziada. Hii ndio sababu kitabu hiki kipo tayari kwa ajili yako leo.

Sasa ukitaka kuipata hii eBook njia ni hii hapa. Save namba yangu ya WhatsApp kwa kugusa namba hii hapa, 0765834754 Kisha nitumie text yenye jina lako ili niweze kukutumia eBook hio kwa WhatsApp mara moja. Kwa sasa nitaitoa eBook EXCLUSIVELY kwa watu 20 tu.

Hata hivyo eBook yetu hii sio kila mtu ataipata. Wataoweza kuipata eBook hio ni wale tu;

1. Waliopo kwenye contact list yetu ya WhatsApp. Kuingia kwenye list hio save namba yetu hii hapa 0765834754

2. eBook itatoka rasmi Usiku wa kuamkia PASAKA kwa gharama ya shilingi 50,000/-. Lakini leo hii unapouona ujumbe huu, eBook naitoa EXCLUSIVELY kwa shilingi 15,000/- tu.

Hii OFA ni kwa watu 20 tu watakaokuwa wakwanza kulipia. Baada ya hapo OFA itafungwa. Hivyo, ndugu changamka.

LIPA Sasa hivi sh 15,000/- kupitia LIPA NAMBA Yetu ya M-PESA hii hapa 5432715 au scan QR Code unayoiona hapa. Ukishafanya malipo njoo WhatsApp na screenshot ya muamala na hapo hapo utapata eBook yako uanze kuvuta wateja kwa kutumia SIRI za Ajabu za SEO katika Mtandao wa Google.

jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni

Kumbuka Ofa ni EXCLUSIVELY kwa watu 20 tu wa kwanza kulipia. Baada ya hapo eBook itarudi bei yake halisi ya sh 50,000/-.

Kuna mtu aliwahi kuliuliza, “Sasa bro, kwanini unilipishe kufanya SEO wakati kutumia Google ni BURE kabisa?” Ungekuwa wewe ungemjibuje apo?

Sikia nikwambie kitu, Ukiona unapewa mchongo wa bure basi jua wewe ndo bidhaa hapo. Ndo ukweli huo.

Kutumia Google ni BURE. Kutumia Insta, Facebook, WhatsApp na mitandao mingine ya kijamii pia ni BURE kabisa. Kwanini? Kwa sababu kwenye BURE ndo kuna utajiri umejificha hapo.

Umeelewa hapo mchezo unavyochezwa. So nakupa SIRI hii hapa; Toa maudhui yatakayotoa majibu ya changamoto BURE yawafikie watu wengi, wachuje, wachache wawe wateja wa bidhaa/huduma zako. Njoo WhatsApp sasa ufahamu zaidi kuhusu SEO na Tech kwa namba hii 0765834754.

Unatamani ujumbe huu umfikie rafiki yako wa karibu? Umejifunza nini leo katika jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni ili uweze kunasa wateja zaidi. Unaweza kushare makala hii kwa rafiki, ndugu, boss au yeyote unayehisi anahitaji kusikia habari hii. Ni BUREE kabisa, hivyo, sambaza, uliza na comment ili ufahamu zaidi.

Cheers.

Kwanini mteja akuchague wewe

KWANINI MTEJA AKUCHAGUE WEWE?

Maisha ya biashara za mtandaoni ni marahisi sana kama ukizingatia tabia za wateja mtandaoni, na ni magumu sana ukipuuzia/usipozijua. Kwanza, hakikisha ukitafutwa unapatikana. Swala la kujiuliza ni, Kwanini Mteja akuchague wewe aache watoa huduma na wafanya biashara wengine?

Zipo sababu nyingi sana mtu akiwa mtandaoni anaziangalia ili ajiridhishe kabla hajawa mteja wako. Leo hapa tutaziona 6 tu. Zingine nitaziweka kwa status yangu ya WhatsApp. Ukihitaji kujifunza zaidi gusa hapa 0765834754 nitumie text yenye jina lako ili nikusave chap.

Mwaka 2022, niliweka story hapa kuhusu jamaa yangu fulani ambaye aliona kazi zetu mtandaoni, akashawishika kuchukua namba kisha akanitafuta tufanye kazi yake, na mpaka leo tumejenga uhusiano bora sana. Ile stori ni hii hapa kama ilikupita Faida za Kutumia Google kama Jukwaa la Biashara yako.

Baada ya kupublish stori hio, nilipokea requests nyingi sana kutoka sehemu mbali mbali yakiwemo mashirika ya kiserikali, binafsi ya yale ya kimataifa.

Leo hii sasa nataka nikwambie Kwanini Mteja achague kufanya kazi na wewe na awaache wengine? Fuatilia dondoo hizi hadi mwisho:

1. UBORA WA KAZI/BIDHAA/HUDUMA: Sikufichi, watu wanapenda vitu vizuri bwana. Hakuna anayependa bidhaa/huduma mbovu. Hata utumie mbinu gani za kunasa wateja mtandaoni, kama bidhaa/huduma zako hazina ubora unaotakiwa, jua apo unacheza tu. Utapata tabu yani.

Kama bidhaa/huduma zako zinatolewa na wafanyabiashara wengine, hio ni fursa nzuri kwako. Fanya uchunguzi, angalia wapi unaweza fanya improvements, ongeza ubunifu kidogo upande wako kisha peleka mzigo sokoni. Hakunaga miujiza kwenye hili. Lazima utie juhudi muda wote.

2. UBORA WA HUDUMA UNAYOTOA; Kama kuna kitu kinafanya wafanyabiashara wengi hawakui kibiashara licha ya kuwa na skills au bidhaa/huduma bora, basi ni hili la kushindwa kutoa huduma zinazomridhisha mteja. Angalia, watu wanatofautiana sana kwenye namna ya kutoa na kupokea maoni na changamoto. Wewe sasa kama mtoa huduma lazima ujue jinsi ya kujishusha kwenye kupokea maoni na changamoto na vile vile kwenye kutoa huduma zenye viwango vya hali ya juu. Huduma bora inaenda sambamba na kuijua saikolojia ya mteja wako. Cheza napo vizuri hapo.

Kuna makala hii kuhusu Umuhimu wa Takwimu kwenye utoaji wa huduma bora katika biashara yako. Ifuatilie hapa uelewe kwanini unapaswa kutoa huduma bora muda wote kwa wateja wako.

3. PATIKANA SEHEMU MBALIMBALI MTANDAONI; Katika mitandao ya kijamii, kila mahali watu hujihusanisha kitofauti. Mfano utagundua watu wa facebook na twita ni tofauti kabisa. Lakini sikufichi, wengi ni wale wale tu. So unapaswa kupatikana kwenye majukwaa yote makubwa kama Facebook, Twita, Linkedin, Instagram n.k Patikana huko kote kwasababu kila mtu ana mtandao wake ambao anautumia zaidi na wote hao unawahitaji leo. Na unachokitaka wewe ni kuifikisha biashara yako kwa kila mtu anayetumia smartphone yani. Si ndio? Fanyia kazi hilo.

nguvu ya mitandao ya kijamii unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Kwanini mteja akuchague wewe?

4. TUMIA S.E.O; Hapa sitasema mengi kwasabau kule WhatsApp huwa natupia sana updates, tips, info na najibu maswali mengi sana kuhusu SEO. Pia kuna eBook maalum ambayo inaelezea siri zote unazohitaji kuzifahamu ili SEO iweze kuwa na manufaa kwako siku zote. Kuipata eBook hio pia hakikisha umesave namba yetu ya WhatsApp, kisha tuma ujumbe wenye jina lako na utapatiwa maelekezo.

In short hii SEO inakurajisishia biashara yako kupatikana haraka pale mtu akiwa anasearch taarifa kupitia Google. Yes, unaihitaji google zaidi sawa sawa na Google inavyohitaji taarifa za biashara yako kwa manufaa ya wateja wako duniani kote.

Mteja anayekutafuta ni mzuri sana kuliko yule unayemtafuta, si ndio? Sasa kwanini usijiweke kwenye mazingira ambayo yatamrahisishia mtu akiwa anatafuta bidhaa/huduma kule Google na kumpa majibu Kwanini mteja akuchague wewe kuliko wengine? Ukiitumia SEO vizuri itakujibu vema sana kwenye hili.

Takwimu za Internet Live Stats zinaonyesha kuwa kwa siku 1 tu kule Google huwa kunafanyika matafuto (searches) zaidi ya bilioni 3.5. Sasa linganisha na matangazo (Paid Ads) unayoyaonaga mtandaoni (Youtube, Insta na fb) na kuyaskip. Wapi utatoboa, kwenye Searches (SEO) au Ads?

5. TOA OFA KADHAA; Mwanaume huwezi kuoa ile siku ya kwanza unapokutana na Mwanamke, hali kadhalika, ni ngumu sana mtu akawa mteja wako siku ya kwanza tu amekutana na wewe huku mtandaoni. Ni muhimu sana kumpitisha mteja kwenye hatua kadhaa ili kusudi aweze kukujua zaidi akupende, akuamini na mwishowe sasa ndo aweze kuwa mteja wako wa kudumu.

Hii ni kwakuwa Biashara za Mtandaoni hutegemea sana kujenga Uhusiano Bora na watu usiowafahamu. Ndio maana unaona kuna wasanii wana mashabiki zao wanawapenda mpaka wakiwaona wanazimia japo hawafahamiani.

Hii ni kwasababu wasanii hao waliwapa values/ofa/zawadi nyingi ambazo ziliwafanya mashabiki zao wawapende sana hata kama hawajuani kiundani. Kadhalika, ukiwa unafanya biashara mtandaoni lazima ujifunze kutoa tips, info, updates, ujibu maswali na ujichanganye na wateja wako.

6. DHIHIRISHA KWAMBA BIDHAA/HUDUMA UNAYOTOA NI GHALI KULIKO GHARAMA ANAYOLIPA: Tunaishi kwenye zama ambazo kila mtu anauwezo wa kufanya biashara na akapanga bei itakayompa unafuu. Mfano, kwenye kutengeneza website ukizunguka huku mtandaoni utaona kila mtu ana bei yake.

mageuzi ya Intaneti (iot) katika biashara na maisha. Jihudumie leo kutoka Rednet Technologies.

Kwanini mteja akuchague wewe?

Biashara zimekuwa huru sana. Kila mtu anao uwezo wa kufanya biashara mtandaoni. Sasa unapaswa kujiweka kwenye nafasi ambayo mteja atakuchagua always akikutana nawe mtandaoni. Kwanini mteja akuchague wewe? Tips hizo hapo. Tips nyingine zipo WhatsApp hapa kwa kugusa namba hii 0765834754

Umejifunza nini kwenye makala hii ya leo kuhusu Kwanini mteja akuchague wewe? Kuna mahali hujaelewa? Niulize swali.. Share, Like na ucomment hapo chini maoni na maswali yako.

Cheers.

simu za michongo Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

FAIDA ZA KUTUMIA GOOGLE KAMA JUKWAA LA BIASHARA YAKO

Je, unaamini kwamba matumizi sahihi ya huduma za internet na mitandao ya kijamii yana uwezo wa kukurahisishia huduma/bidhaa zako zikapatikana kirahisi na wateja wako wakiwa popote duniani? Leo nataka nikupe stori kuhusu Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Tizama hapa, Siku moja asubuhi kabisa ya mwezi April mwaka huu 2022 nikiwa natoka home naelekea ofisini nikapigiwa simu, kutizama ni namba ngeni, nikatafuta utulivu kisha nikapokea;

Mimi: Hello, Habari za asubuhi!

Jamaa: Salama Faustine, I hope uko poa, Bwana mimi ni fulani (jina kapuni) nimekupigia kwa sababu nahitaji website na ningependa ifanywe na kijana mzawa. Nafanya kazi katika shirika (jina kapuni) ambalo ni la kimataifa. Nilikua napitia google pale nikaona kampuni yenu ya Rednet Technologies na nikaona pia kumbe mnajishughulisha na haya mambo. Itawezekana si ndio?

Mimi: Bila shaka hilo linawezekana kabisa, unahitaji lini hii kazi yako iwe imekwisha?

Jamaa: Well, ndani ya wiki 3 ningependa iwe imekwisha, sasa nitampatia namba yako mwenzangu yupo pale ofisini kwetu, yeye sasa atakupa maelezo ya kina. Lakini naomba kujua bei itakuwaje hapo (huku anacheka kwa ufupi)

Mimi: Gharama nitataja nikishajua requirements kaka, wala usiwe na shaka.

Baada ya kuwasiliana na huyo mwenzake akanirudia…

Jamaa: Faustine, naona mmeshaelewana, Sasa the reason tumekuja kwako ni kwasababu kuna mtu tulimpaga kazi ya kutengeneza hii website yetu, lakini hajawahi kutupa ushirikiano, kazi hajamaliza, changes hataki kufanya na tukimpigia simu harespond ndani ya muda, yani ana kiburi sana yule jamaa, kusema ukweli TUMEMCHOKA.

Mimi: (Kiukweli nilijiskia vibaya sana, ndugu zangu ule msemo wa “Mteja ni Mfalme” una maana kubwa sana hapa. Nikamwambia) Kaka, pole sana, utakavyokuwa unafanya kazi kwetu nakuahidi hio kadhia hutakutana nayo.

Jamaa: Kweli? Ok, turudi kwenye bei sasa, utatuchaji kiasi gani?

Mimi: Kwa nature ya Organization yenu hapo mpaka kazi inakamilika itacost 850,000/- tu.

Jamaa: Faustine, mbona bei ipo juu sana, tutaweza kufanya kazi kweli?

Mimi: Kaka, bei iko fair sana hio ukizingatia tutawatengenezea pia business emails BURE na kuwafanyia maintenance BURE kwa mwaka mzima. Anytime hapo mkitaka kufanya changes, tutazifanya BURE kabisa. Hapo unasemaje?

Jamaa: Hapo sio mbaya, walau naona dalili hautakuwa kama jamaa wa mwanzo. Ila bei bado hujashusha..

Mimi: Kaka, lipia 400k leo, baadae utalipa 250k, then finally tutakapomaliza kazi, utalipia 200k ambayo itakuwa imebaki. Hapo je?

Jamaa: Ok, Nataka na hio website pia iwe inapatikana mtu akisearch Google, ili wateja watupate kama sisi tulivyokupata wewe.

Mimi: Ahaa, hio sasa ni huduma nyingine, inaitwa Search Engine Optimization (SEO). Ndo inaiwezesha website kupatikana google.

Jamaa: Na hio utatuchaji au bei yake ndio inakuja na ya website direct?

Mimi: Hio gharama yake ni tofauti kaka.

Jamaa: Ambayo ni ngapi? Usinilalie bwana ndugu yangu.

Mimi: Hio kwa sababu ni kazi ya muendelezo, utakuwa unalipia kila mwezi, ambapo gharama yake ni 100,000/- tu.

Jamaa: sema Faustine mna bei nyie. Ehe niambie, kwenye hio laki 1 mtakuwa mnafanya nini na nini?

Mimi: Hapo tutakuwa tunakuandikia makala (blog posts) mbili kwa mwezi ambazo zitahusu shughuli mnazofanya, tutaweka picha, pamoja na kuzioptimize ili iwe rahisi kupatikana google mtu akiwa anatafuta taarifa zinazowahusu.

Jamaa: Faustine, hapo umeniweza. Basi wacha tuandae contract, halafu next week tutakuita ili tusign, kazi ianze mara moja. Ila usiniangushe bwana.

Mimi: Kaka wala usiwaze, tufanye kazi.

Basi Bwana baada ya simu hio ndio uhusiano ukajengwa na kazi ikaanza kama hivyo.

Na baada ya kazi hio kuisha, jamaa yetu aliweza kutuunganisha kwa watu wengine watano (5) ambao walitamani kupata huduma kama ambayo aliipata kutoka kwetu. Na hatimaye wamekuwa wateja wetu wa kudumu. Unadhani hao walivutiwa na nini? Fuatilia makala hii hapa kufahamu siri za utoaji huduma bora kwa wateja.

Unachoweza kujifunza ili uweze kuzipata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Katika mazingira ya kazi, hasa huku mtandaoni ambapo mara nyingi tunakutana na watu tusiowafahamu (strangers) ni muhimu sana kuzingatia haya yafuatayo;

1. KAULI NJEMA

2. UAMINIFU

3. KUMJALI MTEJA na MAUMIVU YAKE (Mara kwa mara muulize kama anaridhika na huduma anazopata kutoka kwako na nini unaweza kufanya ili kazi yake ifanyike kwa ubora anaotarajia).

Kauli Njema zitakufunulia fursa nyingi na kukuletea wateja wengi sana huku mtandaoni, acha tabia ya kutukana, kudhalilisha au/na kudharau watu. Kumbuka teknolojia haisahau.

Uaminifu utajenga uhusiano mzuri na wa kudumu na mteja wako.

Kumjali mteja kutafanya azidi kukupa kazi nyingi zaidi mbeleni, na hata kukuunganisha kwa watu wake wengine anaowafahamu.

Siri ya kufanya kazi vizuri na mteja ipo kwenye hayo mambo matatu. Ukiyazingatia, hakika huwezi kufeli. Zaidi kama unahisi bado hujajua namna unaweza kushawishi mteja kwenye biashara yako fuatana na makala hii hapa tumekuandalia.

HABARI NJEMA KUELEKEA MSIMU WA SIKUKUU

Sasa kuelekea mwisho wa Mwaka tunakupa ZAWADI ya kuifikisha biashara yako mtandaoni na kukusanya wateja kutoka kila pembe ya nchi. Fungua website leo kwa 500,000/- tu (badala ya 850,000/-) upate na huduma ya SEO BURE (badala ya 100,000/- kwa mwezi) maintenance BURE mwaka mzima pamoja na Ushauri BURE kabisa. Hata hivyo, ZAWADI hii haitamfikia kila mtu. Zawadi hii ni kwa watu 10 tu wa mwanzo, na itadumu mpaka tar 10 December. Baada ya hapo tunakwenda likizo ya Christmas.. So kama unahitaji ZAWADI hii WAHI nafasi mapema ili pia uzipate Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

OFA ya Msimu wa Sikukuu 2022
Sherehe za Christmas na Mwaka Mpya Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Baada ya OFA hii ukihitaji website ni 850,000/-, huduma ya SEO ni 100,000/- kwa mwezi na pia tutafungua group la Whatsapp kwa yeyote atakayehitaji ushauri au atayehitaji kuuliza jambo lolote kuhusu Website, SEO, Social Media Marketing, Digital Marketing na Tech kwa ujumla wake. Kuingia kwenye group hilo itakugharimu 5,000/- tu kwa mwezi.

So ukiliona Tangazo hili, mtaarifu na mwenzako ambaye unahisi atahitaji kunufaika na ZAWADI hii.

Wewe kama unafanya biashara, basi kama unataka kufanya vizuri sokoni, hakikisha unajenga URAFIKI na wateja wako. Hii ni kwa sababu ni rahisi sana MTEJA kuwa RAFIKI yako kama utatengeneza UHUSIANO mzuri kati yenu. Hii ndio SIRI ambayo hakuna mtu atakwambia kirahisi.

Kufanya biashara mtandaoni ni Uwekezaji muhimu sana, na kwa maendeleo yaliyopo kwa sasa duniani, imekuwa ni rahisi mno kutumia huduma za Internet katika kuwafikia wateja popote walipo duniani.

Kuna mtu aliwahi kuniuliza, “Sasa nawezaje kutumia Internet kufanya biashara yangu?”

Jibu: Unaweza fanya haya yafuatayo ili uweze kupata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.:

1. Tumia Website na mitandao ya kijamii kutoa elimu kuhusu bidhaa/huduma zako.

2. Tumia SEO ili kurahisisha maudhui yako yanapatikana kirahisi katika Google.

3. Fanya matangazo (Paid Ads/Sponsored Ads) ili kuwafikia wateja wengi kwa haraka.

4. Jifunze kuuza katika Maandishi (Copywriting). Jaribu kadiri unavyoweza.

5. Tumia WhatsApp yako vizuri kibiashara (Status, Broadcast, Groups n.k).

Ukiona haya yanakuwa magumu kwasababu upo busy au vinginevyo, usikubali sasa biashara yako ife/ishindwe kufanya vizuri mtandaoni.

Tafuta mtaalamu wa kufanya biashara mtandaoni, mpe targets zako, kubaliana nae katika malipo, kisha mpe kazi ili biashara yako izidi kupaa mtandaoni kwa sababu ni muhimu sana ukazipata hizi Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako. Sio lazima kila kitu ukifanye wewe mwenyewe kwa sababu hakuna ajuaje kila kitu.

Ni mategemeo yangu umepata kitu kipya leo. Kumbuka ZAWADI yetu ya kufunga Mwaka inakwisha tarehe 10 December, halafu hii ni maalum kwa watu 10 tu watakaowahi kujinyakulia website zao.

Tutumie ujumbe sasa hivi au tuchek kupitia mawasiliano haya;

Call/WhatsApp: +255765834754

Email: info@rednet.co.tz

VITA VYA KIMTANDAO KATI YA URUSI NA UKRAINE (CYBER WARFARE)

VITA VYA KIMTANDAO KATI YA URUSI NA UKRAINE (CYBER WARFARE)

Baada ya kuripotiwa kupatikana kwa kirusi kinachofuta data zote kwenye mifumo ya kopyuta (Wiper) katika shambulizi la hivi karibuni, serikali ya Ukraine inasema “Shambulizi hili ni la kiwango cha tofauti kabisa”. Sasa leo tuone kwa undani vita vya kimtandao kati ya Urusi na Ukraine (Cyber Warfare) kwa sababu ni jambo linaloathiri hali ya uchumi ya kila mwanadamu aishie duniani kwa sasa. Vilianza lini na vinaathiri vipi uchumi na maendeleo ya Teknolojia? Twende sambamba mpaka mwisho wa makala hii.

Jumatano ya tar 23 February, 2022 tovuti (websites) za benki kadhaa na idara za serikali nchini Ukraine hazikupatikana hewani, ambapo kampuni ya usambazaji wa huduma za internet (ISP) ya Netblocks ilidai kutokea kwa shambulizi la DDoS (Distributed Denial of Services). Agalia hii tweet yao hapa..

VITA VYA KIMTANDAO KATI YA URUSI NA UKRAINE (CYBER WARFARE), Shambulizi la DDoS attack.

Lakini hii si mara ya kwanza kuripotiwa mashambukizi ya Kimtandao ambayo yanadaiwa kufanywa na Urusi.

Mashambukizi ya Kimtandao ambayo yalishawahi kufanywa hapo awali na Urusi:

Mwaka 2008 wakati Urusi inaondoa majeshi yake nchini Georgia, Rais Vladimir Putin aliongoza jitihada za kuliimarisha jeshi lake kisasa katika upande wa vita za kimtandao na mbinu zake kijasusi. Ikumbukwe Rais Putin ni ex-KGB. So ni Jasusi mbobevu kabisa kwenye uga huu.

Hivyo kwanzia hapo Urusi imekua ikitumia mashambulizi ya kimtandao kuvuruga na kubomoa taarifa na mifumo ya kimtandao ya adui. Hii imekua ni mbinu mtawalia katika medani za kivita kwanzia hapo na zimekuwa zikiratibiwa na Idara kuu ya Ujasusi jeshini iitwayo GRU.

Hii GRU kwa kifupi ni Glavnoye Razvedyvatelnoye Upravlenie (inasomwa ivyo ivyo kama inavyoandikwa). Jaribu kusoma kwa sauti tuone..

Hii ni Idara ya Ujasusi Jeshini huko Urusi. Kwa huku kwetu tungeiita Millitary Intelligence (MI). Huku ndo Ujasusi haswa unapofanyika.

Idara hii haina uhusiano wa moja kwa moja na shirika kongwe la Ujasusi la KGB kwa kuwa shirika lile lilishakufa na badala yake likazaliwa shirika la FSB ambalo kazi yake kuu kimsingi ni kukusanya taarifa za kijasusi kuhusu watu, miundombinu, usalama ndani ya nchi na mipakani n.k.

Kwa kirefu kuhusu mashirika haya ya kijasusi na namna yanavyofanya kazi tafuta kitabu cha UJASUSI WA KIDOLA NA KIUCHUMI kilichoandikwa na @YerickoNyerereT pamoja na kile cha @habibu_anga kiitwacho OPERESHENI ZA KIJASUSI. Wacha tuendelee na mada yetu tuloanza nayo.

MASHAMBULIZI KATIKA VITA VYA KIMTANDAO KATI YA URUSI NA UKRAINE (CYBER WARFARE)

  1. December 2015, idara ya GRU ilishambulia mitandao ya mifumo ya viwanda nchini Ukraine kwa virusi haribifu (malwares). Hii ilisababisha kukatika kwa umeme kwa zaidi ya masaa 6 katika maeneo ya Magharibi ya Ivano-Frankivsk. Hali hii iliathiri nyumba za makazi takriban 700,000.

Shambulizi hili pia lilifanywa December 2016 ambapo Urusi ilidaiwa kutengeneza kirusi kilichoitwa Crash Override ambacho kilielekezwa kwenye Gridi ya Umeme ya Ukraine. Madhara ya shambulizi hili yaliathiri takriban 1/5 (moja ya tano) ya uwezo wa jiji la Kiev kusambaza umeme.

VITA VYA KIMTANDAO KATI YA URUSI NA UKRAINE (CYBER WARFARE)

Gridi ya Umeme

Sababu inayodhaniwa kusababisha shambulizi hili kutekelezwa inatajwa ni majaribio ya kuharibu vinu vya Nyuklia kwa kutumia mitandao ya kompyuta. Hii ni kwasababu Vinu vya Nyuklia kwa kiasi kikubwa hutumia Nguvu za Umeme na Huduma za Mitandao ya Kompyuta katika kujiendesha kwake.

Hivyo kushambulia Gridi ya Umeme kwa mafanikio kutafanya uwezekano wa kushambulia Kinu cha Nyuklia kuwa rahisi kupitia Shambulizi la Kimtandao. Umeona watu walivyo na akili apo sasa.

2. Mwaka 2020 Marekani iliwakamata maafisa 6 wa GRU kwa tuhuma za kusambaza shambulizi lililoitwa NotPetya ransomware. Shambulizi hili liliathiri mifumo ya kompyuta dunia nzima na lilisababisha hasara ya 1 Billion dola za Kimarekani.

SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA la NOTPETYA

VITA VYA KIMTANDAO KATI YA URUSI NA UKRAINE (CYBER WARFARE)

Shambulizi hilo linatajwa kama “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA” Fuatana na makala kuhusu Mashambulizi ya Kimtandao kufahamu zaidi.

3. Haijatosha hiyo, January 2021, Urusi iliandaa shambulizi lingine ambalo lililenga servers za Microsoft Exchange. Shambulizi hili liliwapa wadukuzi uwezo wa kuingia kwenye akaunti za emails za watu dunia nzima, lakini target yao ilikua ni Ukraine, Marekani na Australia.

KUMBUKA HAYA KATIKA VITA VYA KIMTANDAO KATI YA URUSI NA UKRAINE (CYBER WARFARE):

Katika uwanja wa kivita, wahusika huwa wanajulikana wazi wazi. Lakini katika Vita vya Kimtandao ni ngumu sana wahusika kujitaja hadharani. Hicho ndo kinachoendelea ambapo Urusi mara zote imekuwa ikikana kuhusika katika mashambulizi hayo. Hata China na Marekani huwa hawakubali.

Hii ni kwasababu Wadukuzi hutumia Kifaa kilichodukuliwa kama silaha kuendeleza mashambulizi. So Mdukuzi anaweza kuwa yupo Iringa akadukua compyuta iliyopo NewYork, halafu compyuta hio ikatumika kushambulia mifumo ya kimtandao iliyopo Berlin, Ujerumani. Umeona mambo hayo bwana..

Hivyo ku-trace-back mpaka kumpata mdukuzi halisi ni ngumu sana kwa kuwa mashambulizi haya hufanywa kwa kutumia mbinu za hali ya juu sana ya kijasusi na kiteknolojia. Ndio maana tunasema hapa kila siku, “Security is a myth“. Kwamba usijione upo salama sana uwapo mtandaoni.

Hata hivyo, makampuni ya kiteknolojia duniani huiba na kutumia taarifa za watu kwa sababu za kuimarisha biashara zao kwa kutumia Data Mining na Data Warehousing. Baada ya kupata taarifa hizo hutumia teknolojia mbalimbali mfano Artificial Intelligence katika kuboresha huduma zao.

Ufanyeje sasa ili uwe salama Mtandaoni?

Dunia ya leo inahitaji umakini sana ili kujiepusha na mazingira ambayo yanaweza kukupelekea kudukuliwa. Mazingira hayo ni pamoja na KUACHA tabia ya kuclick links au kufungua picha na video unazotumiwa na watu usiowafahamu, kuwa makini na tovuti unazotembelea pamoja na kuimarisha passwords zako.

Zaidi kuhusu namna bora ya kujilinda uwapo mtandaoni tayari tumeshakuwekea mbinu mbalimbali kupitia makala yatu hii hapa USALAMA WA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI MTANDAONI.

Tumeona Marekani na washirika wake wakiiwekea Russia vikwazo vya kiuchumi na kuwabana matajiri wa Kirusi. Je hatua hii itarudisha nyuma juhudi za Urusi katika kuimarisha ushawishi wake katika eneo la Ulaya Mashariki? vita vya kimtandao kati ya Urusi na Ukraine (Cyber warfare) itakuwa na mchango gani katika mgogoro huu?

Tusubiri tuone itakavyokuwa. Tutaendelea kukupa updates za kinachoendelea kwenye mgogoro huu wa Ukraine na Urusi hasa katika eneo letu mtambuka la Kiteknolojia, Biashara na Uchumi.

Rejea zimetoka https://bbc.com, https://www.theguardian.com/international, https://theconversation.com/global

Je umependezwa na makala zetu zilizomo katika website yetu hapa?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) na QR CODE ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA kwenye picha hapa muda wote 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
Usalamawa vifaa mtandaoni: Ufanyeje kudhibiti mashambulizi?

Usalama wa vifaa vya kielektroniki Mtandaoni

Ndugu yangu, kuwa makini sana uwapo humu mtandaoni hasa kwenye swala la Usalama wa Vifaa vya kielektroniki unavyotumia kila siku kama simu(smartphone) na computer, Kwasababu; Security is a Myth; yaani, Usalama ni hadithi ya kufikirika. Kwamba usijione uko salama sana hapa Mtandaoni. UFANYEJE SASA?

Kwanza kabisa zingatia haya yafuatayo kabla hatujaendelea mbele.

  1. Ule utamaduni wa kuiishi kauli ya “Chako changu, changu chako“, Kuna siku utalizwa kama hutajiepusha na hizo tabia humu mtamdaoni na hutaamini yani. Hapa sichochei watu kuwa wabinafsi, Hapana. Hapa nakuasa kutoshirikiana katika matumizi ya vifaa kama simu (zile tabia za ku logout facebook, insta etc ili rafiki yako aweze kulogin na kwnye account yake) ACHA KABISA hizo tabia.
  2. Jitahidi Kutoazimisha laptop yako. Najua ni ngumu hasa ktk mazingira ya shule, chuoni, ofisini na mtaani. LAKINI; Kumbuka humo kwenye Laptop yako kuna taarifa zako muhimu kama credentials zako, whatsapp web, twitter web, insta, business emails etc. So unapoazima laptop yako ili mtu aende ku-type tu kazi fulani. Una uhakika gani hatachukua nywila (passwords) na credentials zingine kwenye accounts zako, achilia mbali ku-plant malwares?

SHAMBULIZI LA SOCIAL ENGINEERING

Hili ni shambulizi hatari zaidi kwenye kudukua vifaa vya kielektroniki na mawasiliano. Shambulizi hili huanzishwa kwa kuiba taarifa za kuingia accounts za mtandaoni (credentials) zako na kisha Mdukuzi anaingia kwenye accounts zako huku akichunguza mawasiliano yako na kuiba taarifa pasi na wewe kujua. Yani hutajua kinachoendelea kwamba kuna mtu anafuatilia na kujua nyendo zako zote mtandaoni kimya kimya. Accounts zinazoathiriwa zipo nyingi lakini kwa kiasi kikubwa hapa ni email accounts na accounts za mitandao ya kijamii.

Hapa hata kama umeweka 2 Factor Authentication (2FA) ukijiweka kwnye mazingira ya kupigwa Social Engineering attack ni ngumu sana kujilinda. Ndio maana tunasema: “Security is a Myth“. Maana yake ni kwamba, kila njia ambayo unahisi itakupa ulinzi zaidi, basi jua kuna namna nyingine ya kuipindua isifanye kazi yake kwa 100%.

Ukiachana na mashambulizi mengine ya kimtandao, hili la Social Engineering ni kubwa zaidi kwasababu ukipigwa ni ngumu sana kugundua kwa muda huo mpaka pale utakapoanza kuyaona madhara yake. Mbaya zaidi, shambulizi hili linaweza kukaa kwenye kifaa chako kwa miaka likifuatilia na kuchota taarifa kuhusu shughuli zote na mawasiliano yote unayofanya kupitia kifaa hiko bila ufahamu wako.

social engineering attack

Umeona mambo yalivyo mazito sasa. So, unahisi unaweza vipi kujikinga dhidi ya shambulizi kama hili? Utatumia anti-virus? Au Firewalls? NO! Ndio maana tusisitiza #FuataUshauri wa kitaalam mara zote unapotumia huduma za internet katika kifaa chako.

SHAMBULIZI LA PHISHING

Siku moja Rose akiwa nyumbani kwake, akapokea email yenye ujumbe unaomtaka kukagua na kuimarisha taarifa zake za kibenki kupitia link iliyoambatanishwa. Kutokana na dharura hio, Rose akashawishika kufuata link ile na ku-update taarifa zake. LAKINI; baada ya ku-submit, link ile ikamletea ujumbe kuwa “the website is unresponsive. Try sometimes later.” Baadaye kidogo akapokea ujumbe kutoka benki yake ukionyesha amefanya Muamala wa takribani 1 milion TZS. Dada akawa amechanganyikiwa kwa kuwa muamala ule hakuuthibitisha yeye.

So akawasiliana na benki yake ambapo baada ya kutoa maelezo akagundua ule ujumbe aliotumiwa mara ya kwanza kabisa ilikua ni chambo ya kunasa kwenye shambulizi liitwalo Phishing Attack. Hapa mdukuzi hubuni website inayofanana kabisa na websites za taasisi za fedha au mitandao ya kijamii kisha hutuma link kwa watu mbalimbali akitegemea kuna wachache watanasa kwenye mtego huo. Yani hapa mdukuzi hutumia teknik kama ya kuvua samaki kwa ndoano. Ndio chanzo cha kuitwa Phishing (kutokea kwenye neno “fishing“).

shambulizi la phishing lina athiri vipi taarifa zako na usalama wa vifaa vya kielektroniki mtandaoni?
Mashambulizi ya Kimtandao

Shambulizi hili ni aina ya Shambulizi la Social Engineering na huwaathiri watu wengi sana hasa watumiaji wa Mitandao ya kijamii. Nadhani ushuhuda mnao wa watu ambao wamepoteza accounts zao za twitter, facebook au instagram zikaangukia mikononi mwa wadukuzi.

Kwa undani wa mashambulizi haya na mengine mengi kuhusu usalama wa vifaa vya kielekroniki mtandaoni katika uhalisia tunaweza kuyashuhudia katika vita inayoendelea kati ya Urusi na Ukraine ambapo kumekuwa kukiripotiwa mashambulizi ya kimtandao mara kwa mara. Kufahamu zaidi fuatana na makala hii hapa chini:

Hata hivyo, USIOGOPE; zipo Njia bora za kuzua shambulizi hili ikiwa ni pamoja na:

  1. Chunguza link unayotumiwa ambapo link salama LAZIMA iwe na “https://” mwanzoni. Links zenye “http://” ni za kutilia mashaka na za kuchunguza kitaalam sana ili kujiridhisha.
  2. Pia unatakiwa kuchunguza link kama ni sahihi. Wadukuzi hutumia link zinazofanana sana na links halali. Mf: unakuta link ya vodacom imeandikwa kama vodacm au facebook inaandikwa facebok ikiwa imepunguzwa “o” moja hapo, au wakati mwingine hutumia link ya youtube ambayo itakuwa imeandikwa “youtub” bila “e” hapo mwishoni. Kwa harakaharaka unaweza jikuta umezama mtegoni bila kutarajia. Jumbe za namna hii lazima uzichunguze kwa makini mno na uhakikishe imeandikwa kwa usahihi ili Usalama wa vifaa vya kielektroniki mtandaoni uzudi kuimarika zaidi na zaidi.
  3. Pia inashauriwa kutumia anti-phising browser extensions kama Cloudphish ili kuzigundua hizo phishing links pale zinapoingia kwenye kifaa chako. Mtandaoni kuna kila aina ya mitego ya kukuingiza kwenye mashambulizi haya ya Phising. MUHIMU ni kuwa makini muda wote uwapo online.
usalama wa websites unazotembelea mtandaoni una umuhimu gani kwa vifaa vyako vya kielektroniki?

Katika makala yetu ya mwaka 2020 tulieleza kwa kirefu namna ya kujilinda dhidi ya mashambulizi mbalimbali ya kimtandao. Makala yenyewe hii hapa kupitia mtandao wetu wa twita., ipitie hapo uokotepo mbinu mbili tatu zitakakusaidia.

Baada ya kupitia madini hayo tuendelee sasa..

Point ya msingi zaidi ni kwamba; Usalama wa Kimtandao ni kama kazi ya sanaa i.e aliyetengeneza kitasa ndiye anajua Ufunguo o.g wa kitasa hiko upo vipi. Mwingine atakayejua kutengeneza funguo wa mlango lazima aupate ufunguo o.g kwanza.

Anaupataje huo “ufunguo o.g” ndipo tunakuja kuyaona mashambulizi ya kimtandao. Namna bora ya kujiepusha na mashbulizi hayo ni kuilinda ile “funguo o.g” yetu na kuhakikisha kwa namna yoyote hauiweki kwenye mazingira ya mtu yoyote kuifikia (na hapa ndo shughuli ilipo).

Kwa kirefu zaidi mashambukizi ya kimtandao tumeyajadili kupitia makala iliyopo kwenye tovuti yetu maridhawa kabisa kupitia link hii hapa https://rednet.co.tz/yafahamu-mashbulizi-ya-kimtandao-cyber-attacks-na-athari-zake-katika-biashara-kampuni-yako/

ZINGATIA:

Zama hizi kifaa chako (simu/laptop) ni kama ule “ufunguo o.g” wako ambao unautumia kufunga na kufungua kabati lako ulimohifadhia taarifa zako zote za kielektroniki. Hili ni swala muhimu sana kama ulikua hujui ama unajua.

Una wajibu wa kulinda vifaa vyako (hasa smartphones na Laptops) kwa kuviwekea NYWILA (Passwords) ambazo ni ngumu kwa mdukuzi kukisia na rahisi kwako kuzikumbuka. Pia USIHIFADHI nywila zako kwenye daftari/diary ama kwnye Browsers za vifaa vyako kwasababu maeneo hayo ni rahisi kwa mdukuzi ama mtu mwenye nia mbaya kuyafikia na kuanzisha shambulizi la Social Engineering.

Sehemu pekee na Salama zaidi pa kuhifadhi nywila zako ni katika Kichwa chako. Yes! Ndio maana tunahimiza utengeneze nywila ambayo ni rahisi kwako kuikumbuka na ngumu mdukuzi kuikisia.

Njia zingine za kujilinda dhidi ya mashambulizi ya Kimtandao zimeelezewa kwenye makala hii hapa chini kwenye link hii yenye rangi ya bluu:

Umejifunza nini kwmye makala hii ya leo kuhusu usalama wa vifaa vya kielektroniki mtandaoni? Tuandikie ushuhuda wako kwenye comments hapo chini. Kwa changamoto binafsi inayokukumba kwenye biashara yako tafadhali wasiliana nasi kupitia kitufe cha whatsapp hapa chini:

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamalaSasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

usalama wa vifaa vya kielekroniki mtandaoni una faida gani?
MPESA LIPA NAMBA