Tag: mbinu za kufanikiwa katika biashara

jinsi ya kuanzisha website

JINSI YA KUANZISHA WEBSITE

Japokuwa anafanya vizuri mno katika biashara ya kusambaza vifaa vya miundombinu ya maji (mabomba, koki, elbow n.k) huku akipata tenda nyingi kupitia mfumo wa TaNEPS, lakini alitamani sana jinsi ya kuanzisha website na kufikisha bidhaa zake kwa watu binafsi mbali na serikali na mashirika ya kimataifa ambayo amekuwa akifanya nayo kazi. Katika stori hii ya leo utashuhudia siri za kuzingatia jinsi ya kuanzisha website ili biashara yako izidi kushamiri huku mtandaoni. Makinika.

Sasa jamaa yetu huyu yuko busy sana na hio miradi yake kiasi kwamba hana muda wa kuandika makala kwenye mitandao au kupush hashtags au kutweet na kupost mara kwa mara kuhusu huduma anazotoa. Hata hivyo aliazimia kufanya kazi na watu binafsi, mahoteli, shule binafsi, hospitali n.k.

Huwa anazunguka nchi nzima akifanya kazi na serikali na mashirika ya kimataifa kuhakikisha miundombinu ya maji safi na salama inafika kila kijiji. So kwa nature ya kazi yake, tunaweza kusema jamaa hana Time Advantage ya kutumia mitandao ya kijamii ili watu binafsi waweze kumfahamu, kumuamini na kufanya nae kazi. Hata hivyo experience yake imemfanya aaminiwe na serikali pamoja na mashirika yanayotumia mfumo wa TaNEPS. LAKINI; Jamaa yetu huyu bado alitamani kufanya kazi na watu binafsi, afunge mabomba kwenye nyumba binafsi, hoteli, bar n.k hata hivyo bahati mbaya watu binafsi hawatumii mfumo wa TaNEPS katika kutafuta huduma/bidhaa wanazohitaji. So jamaa akafanyaje?

Mwaka 2018 akafungua ecommerce website ambayo baada ya mwaka mmoja website ile ilishindwa kumletea matunda yale aliyotarajia. Akaishia kusema, “Nilifunga website lakini haikuniingizia hata mia kwa mwaka mzima, nikaamua kuachana nayo.” Hii imeshawahi kukukuta wewe? tuambie kwenye comment hapo chini.

faida za teknolojia ya S.E.O katika biashara

Kama unajua uchungu wa kuwekeza na kuvuna hasara nadhani utakuwa umemuelewa jamaa hapo. So mwaka huu 2022 nikakutana na huyu jamaa yangu, anaitwa Steven (tumuite Stivu leo), akanieleza kuhusu kiu yake ya kufanya kazi na watu binafsi na namna alivyopata hasara ya website mwaka 2018.

Katika maongezi yetu alitamani kutumia Nguvu ya Intaneti na Mitandao ya kijamii ili aweze kufanikiwa katika kuwafikia watu binafsi ukizingatia jamaa yupogo busy na TaNEPS + kukusanya materials na kuzifikisha site hivyo kumfanya asiwe na muda na kuweka updates mitandaoni.

Ushauri huu utakufaa hata wewe, zingatia sana:

1. Hakikisha unafahamu ndani nje kuhusu soko la watu wenye njaa na huduma zako: Hapa Stivu ana advantage upande mmoja kwa kuwa tayari anaaminiwa na serikali na mashirika ya nje. Kimbembe ni watu binafsi. So unapaswa kuwajua wateja wako kwa kupost/kutweet kuhusu bidhaa/huduma zako na thamani unayoitoa kwa mteja pindi atakapoamua kufanya kazi na wewe ajue kabisa kwamba bidhaa/huduma yako itakwenda kumtatulia changamoto yake flani. Hii inapaswa kufanywa mara kwa mara ili kusudi kuchuja na kuwapata watu wanaokufuatilia (followers) na kuwafanya wakujue, wakuamini na baadaye wafanye kazi na wewe.

jinsi ya kuanzisha website
umuhimu wa tehama

So hapa Stivu ali #FuataUshauri kwamba anapaswa kutafuta mtu wa kumsaidia kuhakikisha biashara yake inatengeneza ushawishi kwnye mitandao ya kijamii kwasababu yeye mwenyewe hawezi kufanya kila kitu afterall. Hii inaitwa LEVERAGING.

2. Hakikisha jina la biashara yako (Brand Name) ni rahisi kutamkika na kinahusiana na wateja wako:

Hapa kwa Stivu hakukua na shida, lakini kwako wewe inawezekana hujafahamu kuhusu hili. Imagine una mgahawa wa chakula halafu unakuta umeandikwa JOY ELECTRONICS. Imagine yani.

Hii kitu ukitaka kufanikiwa zaidi hakikisha Brand Name yako ipo clear from the beginning, hasa linapokuja swala la Online Business ambapo huku mtandaoni kuna makelele mengi mno. Sema kabisa JOY RESTAURANT (Food Providers in Arusha). Hii itakusaidia kukufanya uwe specific na ujulikane exactly unafanya biashara gani na unapatikana wapi kabla hata mtu hajaanza kujiuliza zaidi.

Hii pia inaipa biashara yako advantage pale mtu anapotaka kufika ofisini kwako kupitia Google Map. Mteja hasumbuki yani kuuliza uliza njiani au kuwa na hofu ya kupotea.

3. Fanya Kazi:

Hata kama tayari biashara yako imeshasimama physically, lakini kama unataka kuihamishia biashara hio mtandaoni; Huna budi kuwekeza muda wako katika kudadisi kuhusu Wateja, Washindani wako ni kina nani, wanafanya nini kufanikiwa kuteka masoko na wewe ufanye nini.

Hivyo, roughly ndani ya miezi 6 ya kwanza unatakiwa kuwekeza masaa 60 kwa wiki (wastani wa masaa 8 kwa siku) ili kuchunguza na kujua namna ya kuandika copies zitakazofanya bidhaa/huduma zako ziuzike mtandaoni. Copies hizo zinaweza kuwa ni makala, tweets, fliers etc.

jinsi ya kuanzisha website
jinsi ya kufanikiwa mtandaoni
umuhimu wa tehama
asiyefanya kazi na asile

Ujuzi huu wa COPYWRITING ni muhimu sana na ukiwa tayari kujifunza huwezi kushindwa kuuweza. Hii ndio sumaku ya kunasa wateja huku mtandaoni sasa. Lazima uhakikishe unaandika kile ambacho mteja wako atakiadika akiwa anatafuta suluhisho la changamoto zake.

Kwenye maandishi yako maneno kama “Faida za Tehama”, “Kirefu cha TEHAMA”, “Jinsi ya kuwa na mwonekano mzuri”, “Jinsi ya kufanikiwa katika biashara ya chakula”, “Faida za website”, “mbinu za kutumia Mitandao ya kijamii”, “jinsi ya kuanzisha website”, “mbinu za kufanikiwa katika kilimo”, “nguo za bei nafuu”, “Ofa ya Sikukuu”, “Makosa 10 usiyotakiwa kufanya katika…” nakadhalika.

Ukitazama hapo utagundua maneno hayo ndio haswa huandikwa kwenye mitandao mbalimbali pale mtu anapotafuta kitu fulani, si ndio? Basi na wewe katika maandiko/copies zako hutakiwi kuyaacha kabisa kwa sababu ndo sumaku yenyewe hio.

4. Zifahamu hatua za awali za kufanya S.E.O:

Kwenye makala zetu zilizopita tumejadili kuhusu Teknolojia hii ya S.E.O inavyoweza kuimarisha biashara yako pindi pale mteja anapotafuta huduma kupitia mtandao wa Google. Pitia hapa kwenye tweet yetu kama ilikupita hii hapa chini.

Awali umeona aina za maneno ambayo unapaswa kuyatumia mara kwa mara katika maandiko yako ili kuwanasa wateja wengi zaidi huku mtandaoni. Katika S.E.O maneno hayo huirahisishia google katika kuchambua keywords na kuzipandisha juu pale mtu anapotafuta tarifa. Hivyo, website yenye keywords nyingi ndio huchaguliwa kirahisi katika mtandao wa google na kuwekwa juu ili mtu anapotafuta basi website hio inatokea kwenye nafasi za juu kabisa. Fikiria mtu ameandika “Jinsi ya kupika chakula kizuri cha ndizi” au “jinsi ya kuanzisha website” na mara links za website yako ya mgahawa wa chakula inatokea ya kwanza kabisa pale google. Inafurahisha eh?

Fahamu kwamba mtu hataandika jina la biashara yako pale google akiwa anatafuta suluhisho kwa changamoto zake. Watu hawajali kuhusu jina la website yako hata, watu wanajali kuhusu namna ya kutatua changamoto zao ndio maana ni rahisi sana mtu kuandika hizo keywords nilizokutajia mifano yake hapo awali na hayo maneno ndio haswa hutumika katika S.E.O kuinua website yako mtandaoni. Unahitaji kuyatumia sana maneno hayo katika website yako.

Kwa kifupi unaweza kufanya S.E.O kwa website ya biashara yako mtandaoni kwa Kuilocate kwenye Google Map, Kusajili akaunti za Google My Business na Search Console. Hii itaifanya website yako iweze kuwa-ranked na Google kwenye nafasi za juu pindi mtu atakapokuwa anatafuta huduma.

5. Fahamu kuwa kufanikiwa kupata watembeleaji wengi kwenye website yako (Organic Traffic) kunachukua muda (walau miezi 6 mpaka mwaka):

Katika muda huu unatakiwa ufanye kazi ya kuweka maudhui, kuandika Keywords zinazovutia wateja (copywriting inaingia hapa), kufanya maintenance ili kuhakikisha website yako ina-run kwa kasi mda wowote mtu akiifungua.

Pia ni muhimu kutengeneza Backlinks. Hizi ni links za website yako ambazo zinaatikana kwenye websites na majukwaa mengine ya mtandaoni mf: umeandika makala halafu unaenda kui-share ZoomTanzania, LinkedIn au unaweza kuomba wadau wako wakashare links zako kwenye accounts zao za twitter, medium, facebook au hata kwenye websites zao kama wanazo. Ndio maana tunasisitiza kujenga Business Relationships, yaani uwe na uhusiano mzuri na wafanyabiashara wenzako humu mtandaoni ndo utatoboa.

Kuhusu namna unavyoweza kuifanya website yako iweze kutembelewa na watu wengi zaidi tumeshakuandalia makala maalum hii hapa chini:

KUMBUKA:

Marekebisho ya website huwa hayaishagi daima. Hii ni kwa sababu Teknolojia inabadilika kwa kasi sana na wewe kama mfanyabiashara hutapenda kuona website yako inaonekana vilevile tangu mwaka juzi. Ndio maana unatakiwa kuzurura mtandaoni na kutizama website zingine uone ziko vipi na ujitathmini unawezaje kuhakikisha website yako inaonekana MPYA, bora na yenye kukidhi matakwa ya wateja wako muda wote ili ufahamu jinsi ya kuanzisha website kabla hujafanya makosa zaidi.

Fahamu tu kwamba hutengenezi website kwa ajili yako, HAPANA. Unatengenza website kwa ajili ya wateja wako wapate kitakachowasaidia. So hudumu kwa nguvu zako zote huku ukiongeza maarifa kila leo.

Website yako ndiyo RECEPTIONIST wa ofisini kwako. Hakikisha anapendeza na ana taarifa zote ambazo unataka mteja wako akija azipate.

We jiulize kwanini mara nyingi Wanaume hawakuwagi Receptionists?

Utagundua “Receptionist LAZIMA awe mrembo haswa. Lazima avutie mteja kutaka kuuliza jambo”.

Hiyo kwanzia leo nategemea utakuwa ukiitizama website yako kwa jicho la tofauti na iliyokuwa hapo kabla. Kufahamu Kwanini umiliki website ya biashara yako tafadhali fuatana na makala hii kwa kugusa alama ya link hapa chini:

Kupata website yako imara na mahsusi kwa ajili ya kuimarisha biashara yako huku mtandaoni tafadhali wasiliana nasi kwa kututumia ujumbe kupitia kitufe cha Whatsapp unachokiona kwenye ukurasa huu.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

M-PESA LIPA NAMBA
teknolojia ya S.E.O ina msaada gani katika biashara za mtandaoni?

TEKNOLOJIA YA SEO INA MSAADA GANI KATIKA BIASHARA ZA MTANDAONI?

Je, biashara yako ina uwezo wa kujiendesha hata kama haupo ofisini au pale unapofunga mlango wa ofisi? Kama jibu ni HAPANA, basi wakati wa kuhamisha biashara yako mtandaoni ni SASA kwa sababu Teknolojia haikusubiri wewe ndugu. Leo unapojiuliza teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni? majibu yote muhimu utayapata hapa. Cha kufanya, Fuatana nasi mpaka mwisho wa makala hii.

Imagine wateja wako wanaweza kufanya shopping wakiwa huko huko makwao, wengine wanasoma makala zinazotatua changamoto mbalimbali zinazowakabili na wengine wamepata mawasiliano yako mtandaoni. Yote hayo yanafanyika wewe ukiwa safarini, nyumbani, shambani au ukiwa na mishe zingine nje kabisa ya mtandao.

Faida ni nyingi sana ukiwa unafanya Online Business: Yani ukishakuwa na website inayofanya kazi sawia, ukawa na accounts za mitandao ya kijamii zinazoitambulisha biashara yako kila siku, hapo unafika kwenye hatua ambayo Internet inakufanyia kazi, na sio wewe kuwa Mtumwa wake.

NINI KINAKWAMISHA WATU WENGI SASA?

Watu wengi hudhani kuwa biashara za mtandaoni ni rahisi tu. Kwamba TCRA wameripoti kuwa kuna watumiaji wa internet milioni 29 kufikia October2021, so ukipost biashara yako itawafikia watu milioni29 chap. NO! Maisha si rahisi kiasi hiko asee!

Hii ni kwasababu miundombinu ya kimtandao (websites, blogu na mitandao ya kijamii) imetengenezwa katika namna ambayo inaheshimu Algorithms (mtiririko rasmi) fulani wa maneno, taaluma, mijadala, picha na mahusiano ili kuongeza ufanisi. Ndio maana tunasema kila siku Fuata Ushauri wa kitaalam.

Algorithms hizo huchochewa na mfumo wa kurahisisha utafutaji wa taarifa mtandaoni ujulikanao kama S.E.O (Search Engine Optimization). Mfumo huu huchukua links na maneno(keywords) yanayotumika zaidi katika blogu, websites na social networks na kuyaweka kwenye injini za matafuto kama Google na Bing.

Hivyo, kama unajua ama hujui, chochote unachokiandika sana katika social networks, blogs na websites huchukuliwa na kuwekwa katika Google na Bing. Lakini sio kila kitu unachokitafuta google utakipata kikiwa katika nafasi za juu pale google, Hapana, mambo hayaendi hivyo.

Kuna taarifa ukiitafuta utaipata kutoka kwenye biashara fulani ikiwa juu kabisa ukurasa wa mbele pale google. Taarifa hiohio pia unaweza kuipata kwenye blogu/website ambayo ipo ukurasa ya pili, wa tatu au wa 10.

Ubaya ni kwamba mteja hatatafuta jina la blogu/website yako, bali ataandika changamoto anayotaka kukabiliana nayo au kuhusu taarifa anayotaka kuitafuta mtandaoni. Mfano huandika kupitia google kutafuta “kirefu cha TEHAMA” “Biashara ipi ina faida zaidi Tanzania?” “Siri ya kuwa tajiri Afrika” “Mbinu za kufanikiwa kimaisha/kibiashara” “laptop za bei nafuu Tanzania“, “viatu vikali“, “Faida za TEHAMA“, “Faida za Website“nyimbo za bongo fleva 2022”, “Laptop za bei nafuu zinapatikana wapi?” “Faida za kilimo cha mananasi/tikitimaji” “Chakula kitamu zaidi Tanzania” nakadhalika.

Sasa, kupitia maneno hayo ya S.E.O umegundua nini?

Ngoja nikwambie kitu, Kama unafanya biashara mtandaoni, zingatia maneno ambayo yanatumiwa zaidi na watu wengi au yanayotafutwa zaidi na wateja katika Industry yako. Jiulize, kama wewe ndo ungekuwa mteja unatafuta kujua kuhusu bidhaa/huduma flani, ungeandika nini pale Google?

Sasa hayo maneno ambayo ungeyaandika google ndio chambo ambayo unapoyatumia mara kwa mara katika blogu/website/social media yako, basi unajiweka kwenye nafasi ya kupatikana kirahisi zaidi pale mteja akitaka kutafuta kuhusu huduma/bidhaa zako. Zingatia sana hilo.

Na hio ndio SIRI ambayo wengi wanaojiita “Wataalam wa SEO” hawatakwambia kuhusu teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni. Kuna watu hawaoni sababu ya kuwa na Website/Blog kwasababu vitu hivyo HAVIWAINGIZII pesa direct.

Kuna mmoja nilifanya naye nae kazi akaniambia kilichomkuta mwaka 2018, “Bwana mi nilishawahi kuwa na website ila mwaka ule mzima yani haikunipa hata mia, na niliilipia mnaita ‘Hosting Fee’ sijui. Sikuwahi kuona umuhimu wake, so nikaachana nayo”.

faida za teknolojia ya S.E.O katika biashara

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

Najua hili hata wewe unalihofia Kwanza fahamu haya yafuatayo:

Kuwa na website hakukufanyi kupata wateja wengi kama hutafanya yafuatayo ili ufahamu teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni:

1. Hujatengeneza account ya Google Map: Zamani Google walikuwa wakitumia Application ya Google My Business ili kuwarahisishia wafanyabiashara waweze kuunda profiles zao na ziweze kupatikana kirahisi mtandaoni. Lakini baadaye waliona App ya Google Map inao uwezo wa kubeba taarifa zote muhimu, hivyo App ya Google My Business ikafikia mwisho wake hapo. Stori nzima ipo hapa. Google Map sasa huifanya biashara yako iweze kusajiliwa, kutambulika na kupatikana rasmi na kirahisi katika mtandao wa Google. Yani apa unatengeneza Profile ya biashara yako direct na kumruhusu mteja aweze kuona mpaka mahali biashara yako ilipo.

google Map

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

2. Hujaunganisha blog/website yako na huduma za Search Console: Hii Search Console kazi yake kubwa ni ku-crawl, yani kukusanya taarifa zote za website yako kama huduma/bidhaa unazohusika nazo, links za Menu (Home, contacts etc) Mada unazoziweka, mijadala na maneno unayotumia humo Kutengeneza links ziitwazo SITEMAPS na kuziweka kwnye injini za matafuto ya mtandaoni ili mteja akitafuta anachokitafuta basi google/bing iweze kuileta website yako ukurasa wa mbele kabisa. So ukifanyia kazi vema hiki kipande, Google itai-rank website yako katika nafasi za juu.

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

Google Search Console

3. Huweki maudhui kwenye website/blog yako: Yule jamaa yangu nilikwambia pale juu kuwa hakuona umuhimu wa kuwa na website, changamoto kubwa alikuwa nayo ni kushindwa kuwa na website inayoruhusu kuweka maudhui frequently. Unakuta website ina tabs za Home, Services, About na Contacts peke yake tu, wala haina sehemu ya blog/news au sehemu ya kufanya shopping. Kwa biashara za kisasa hii ni changamoto kubwa sana kama bado hujafahamu teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni.

Fahamu tu kwamba website ambayo haina uwezo wa kuweka maudhui mara kwa mara kupitia Kipengele cha Blog/News ni NGUMU sana kutokea kwenye ukurasa wa kwanza wa google. Hii ni kwasababu Maudhui unayoweka kwenye kipengele cha Blog/News huifanya website yako kuwa ya Kipekee na inayojiboresha kila siku.

Na hivyo ni rahisi google kui-rank website yako katika nafasi za juu pale mtu akitafuta taarifa ambazo pia zinapatikana kwenye website yako. Hii ndo silaha ambayo itaiwezesha biashara yako kuweza kujitangaza yenyewe na kukusanya wateja wengi huku wewe ukiendelea na mishe zingine.

4. Hausambazi Mukhtasari wa taarifa (updates) zinazopatikana kwenye website yako: Ndio, SEO inafanya kazi automatic unapounganisha website yako na huduma ulizozisoma hapo awali, Lakini, ni muhimu pia kusambaza Updates kuhusu taarifa unazoweka kwnye website yako katika social accounts zako za instagram, facebook, twitter nakadhalika.

Hapa unatengeneza kitu kinaitwa BACKLINKS. Tayari nimeshakuwekea elimu ya kutosha kuhusu umuhimu wa Backlinks katika kuhakikisha website yako inafanya vizuri pale Google.. Fahamu tu kuwa ili Website yako iweze kuwa imara mtandaoni lazima links zake zipatikane kwenye media zingine kama Linkedin, Facebook, Twitter, ZoomTanzania, Clutch n.k.

Huko ndo Jikoni kwenye haswa, Kwa sababu, ukiachana na Google, kwenye mitandao hio ndipo watu wengi hushinda wakijadiliana kuhusu mambo mbalimbali ya kijamii, kisiasa, michezo na burudani. So ukiwapelekea solution kuhusu changamoto zao kisha ukawapa link, guess what will happen?

Kujua zaidi namna ya kuongeza traffic kwenye website yako tafadhali tembelea makala hii hapa chini:

KWANINI TUNA-SHARE SIRI HIZI KUHUSU TEKNOLOJIA YA SEO INA MSAADA GANI KATIKA BIASHARA ZA MTANDAONI?

Siku zote maendeleo mazuri ya mgonjwa ndo mafanikio ya daktari. Hivyo wewe mjasiriamali ukifanikiwa ktk website yako, huo ni ushindi pia kwetu developers na wataalam wa SEO. I hope elimu hii inakwenda kutibu changamoto zako katika biashara za mtandaoni?

Kwa makala nyingine nyingi zaidi, endelea kuperuzi ukurasa wetu wa https://rednet.co.tz/blog kila mara ambapo utagundua makala muhimu za kuimarisha uchumi wako binafsi na wa biashara/kampuni yako.

Mjasiriamali anapofanikiwa katika website yake, huo pia ni ushindi kwa web designer na wataalam wa S.E.O.

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

Msaada binafsi tafadhali wasiliana nasi kupitia:

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni
MPESA LIPA NAMBA YETU

OFA YA MSIMU WA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN

Tunawatakia Ndugu zetu Waislamu wote Ramadhan Kareem! Rehema za Mwenyezi MUNGU zikawe pamoja nanyi katika kipindi hiki. Kwa kutambua umuhimu wa Kipindi Hiki kitakatifu, OFA YA MSIMU WA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN IMEFUNGUKA ambapo sasa utajipatia huduma hizi kwa gharama nafuu ili kuzidi kuimarisha biashara yako:

i. Website Design (500k ✔️ 1.2m❌)

ii. Business Plan + 100 Business cards (350k ✔️ 600k❌)

iii. Ushauri na Usimamizi (mentorship) BURE kabisa.

Kuendana na OFA hio kuna makala hizi hapa ambazo kwa hakika zitakusaidia sana katika kuendesha biashara yako huku mtandaoni. Fuatana nazo mpaka mwisho:

https://rednet.co.tz/yafahamu-mashbulizi-ya-kimtandao-cyber-attacks-na-athari-zake-katika-biashara-kampuni-yako/ yenye kichwa YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO (CYBER ATTACKS) NA ATHARI ZAKE KATIKA BIASHARA/KAMPUNI YAKO.

https://rednet.co.tz/kwanini-uitangaze-biashara-yako/ yenye kichwa KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?

https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-teknolojia-ya-intaneti-na-kompyuta-katika-biashara-yako/ yenye kichwa UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA KATIKA BIASHARA YAKO.

https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE/TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO.

Zaidi, Karibu DM tuwasiliane kwa undani. Muda wa kuimarisha biashara yako ndio huu. Usiache OFA hii ikupite.

Simu/Whatsapp: 0765834754
email: info@rednet.co.tz / fvitalice@gmail.com
Web: https://rednet.co.tz

Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

BRANDING Vs MARKETING, KIPI NI KIPI?

Unapofanya biashara, moja kati ya malengo makubwa ni Kupata/kuendelea kupata wateja kila siku. Wateja ndio Roho ya biashara. Hakuna biashara kama hakuna wateja. Lakini unawapataje wateja hao? Unatumia vipi mbinu za Marketing na Branding? Branding vs Marketing, Kipi ni kipi?

Unapokuwa unaitengeneza biashara yako unatumia mbinu nyingi sana kujitangaza na kuvuta wateja wengi kwa kadiri inavyowezekana. Kuna wanaotumia ndugu, jamaa wa karibu, classmates, colleagues n.k. Ili mradi tu connections zinahusika kwa ukubwa wake. Kuna wengine wanatumia mitandao ya kijamii, kuna wanaofanya company visits na wengine wanatumia mbinu ya Umachinga (Kutembeza Barabarani). Lakini wote hao wanatumia Mbinu mbili tu kimsingi. Ni Either Marketing au Branding.

MARKETING na BRANDING ni nini?

Marketing ni mjumuisho wa vitendea kazi, utaratibu na mbinu za kuhakikisha bidhaa/huduma zako zinapigiwa debe ipasavyo ili ziuzike. Marketing ni mbinu ya kumfanya mteja anunue bidhaa/huduma zako. Ndo kupiga debe kwenye huko. Upande wa pili, Branding ni ile namna unajiweka/unaiweka biashara yako ili iweze kupokea wateja zaidi.

unawezaje kupata wateja mtandaoni unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Branding Vs Marketing. Kipi ni kipi?

Ule unauweka utambulisho wa biashara yako, unavyofanyia kazi Dira, Malengo na Mipango yako na vile vitu vinavyokufanya wewe kuwa tofauti na washindani wako kibiashara. Hio ndio BRAND yako. Kama Marketing ni sumaku ya kuvuta wateja, basi Branding ni sukari ya kuwafanya waendelee kuwepo.

KIPI KINAANZA – BRANDING au MARKETING?

Fahamu, Branding ipo kwenye ule msingi kabisa wa Mbinu zako za kimasoko (marketing strategy), hivyo Branding lazima itangulie. Ukiitengeneza vizuri Brand yako hata kama ni changa, swala la Marketing linakuwa rahisi maradufu. Brand yako unayoitengeneza ndio itawafanya wateja waendelee kukujia na kuongezeka kwa mabalozi wa kujitolea wa bidhaa/huduma zako, ambao ndio wateja wenyewe haohao. Hii inaitwa “Customer’s Loyalty” (nimekosa kiswahili chake). Mfano, tizama Pepsi, pengine ndio soda inayouzika na kunyweka zaidi duniani kwa sasa, nikikuuliza umekunywa pepsi ngapi tangu mwaka huu umeanza pasi na shaka huna jibu, yaani umekunywa nyingi zisizo na idadi. Sasa hio ni kwa kuwa watengenezaji wa soda hio walitengeneza tabia zinazokufanya uendelee kuitumia miaka na miaka. Tabia hizo ni pamoja na Usafi wa chupa, Ubora, ladha n.k.

Pata huduma za Website, SEO, Social Media Marketing na nyinginezo nyingi kutoka Rednet Technologies

Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

Katika biashara za namna bora zaidi ya kuji-Brand ni kutumia mitandao ya kijamii. Sasa unatumiaje mitandao ya kijamii kwa manufaa ya biashara yako? Branding vs Marketing, Kipi ni kipi? Tafadhali songa na makala hii kwenye link IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA

Hivyo linapokuja swala la marketing, ni rahisi zaidi kuipromote Pepsi ikauzika kuliko Fanta passion. Branding ni ile kutengeneza utamaduni, mhenga mmoja alishasema, “Culture eats strategy for breakfast”. Yaani hata uwe na mbinu gani, kama hujazifanya mbinu zako kuwa utamaduni unaoishi, hapo andika maumivu. Ndio maana wanamichezo makini hufanya mazoezi kama utamaduni wao wa kila siku, na ndio hao ambao wanafanikiwa zaidi. Branding vs Marketing, Kipi ni kipi?

Branding vs Marketing, Kipi ni kipi? Tofauti ni ipi?

1. Marketing ni ile mbinu ya kutengeneza mhemko(attention) kwa wateja, Branding ni namna ya kuwafanya wateja waendelee kuwa wateja wako.

2. Marketing ni mbinu ya kufanya mauzo, Branding ni namna ya kutengeneza Jina, Heshima na Ushawishi kwa wateja.

3. Branding ndio inayoanza kuonekana katika biashara yako, Marketing inafuata.

4. Mbinu za kufanya Marketing hubadilika kulingana na wakati na mahitaji, lakini Branding ni Mbinu ya kutengeneza Utamaduni wa kudumu kizazi na kizazi.

5. Branding inahusika sana katika kufanya shughuli za kila siku za ndani ya biashara/kampuni yako, na vile wateja wanaziishi huduma/bidhaa kutoka kwako. Ndio utamaduni wenyewe.

Kwa chochote unachokifanya, fahamu biashara yako ni moja kati ya biashara nyingi duniani ndani ya bahari ya Ushindani wa kimasoko. Unahitaji mbinu bora katika kutengeneza Brand (Recognition) yako pamoja na Marketing (sales) za kila siku.

Kwa maneno mengine mbinu hizi hujieleza kupitia Dira (Vision) na Malengo (Missions) ya biashara yako. Leo nataka useme hapa Vision na Missions ambazo umejiwekea katika biashara yako ni zipi? Ukiweza kuzieleza na kuzisimamia vizuri basi, basi Utakuwa unaiweka pazuri bishara yako. Mfano, Rednet Technologies ilianzishwa ikiwa na Dira(vision) ya “Kuhakikisha Wafanyabishara wadogo na wakati (SME’s) wote nchini Tanzania na Afrika Mashariki wanatumia Teknolojia za kisasa katika utendaji wa biashara zao za kila siku.”

Mipango(Missions) ipo mingi lakini baadhi ni:

i. Kutengeneza websites bora kwa matumizi ya biashara mbalimbali kama ecommerce, corporate, funding na normal profile.

ii. Kutengeneza mifumo ya kuhifandhi na kuendesha mauzo na rekodi mbalimbali za kibiashara.

iii. Kuhakikisha wafanyabiashara wanapata taarifa muhimu kuhusu mbinu, takwimu na habari za Uchumi na mabadiliko ya kibiashara haswa kupitia Mapinduzi ya Viwanda yanayochochewa na mabadiliko ya kiteknolojia yanayotokea duniani kila uchwao. Taarifa hizo unaweza kuzipata kupitia tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz Kupitia Vision na Missions hizo ulizoziona, Niambie ni rahisi kiasi kubuni mbinu ya kufanya Marketing? Je unaweza kuanzisha Marketing strategy gani kwa wakati huu unaosoma makala hii? Majibu yote unayo wewe mwenyewe.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni.

Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

Sasa makala hizi hapa chini zitakupa muendelezo mzuri kuhusu somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana kama ukizisoma zote. Gusa link kisha makinika:

  1. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO
  2. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  3. IFAHAMU TEKNOLOJIA YA QR CODE KATIKA BIASHARA YAKO

Tueleze leo vision ya biashara yako ili tujue utamaduni wako ni upi, watu tuanze kuufuatisha. Hakikisha unasambaza makala hii kwa watu wengi kuhakikisha Biashara zinashamiri na unazidi kupata wateja wapya kupitia hapa. Tuanze.