Tag: mbinu za biashara

teknolojia ya S.E.O ina msaada gani katika biashara za mtandaoni?

TEKNOLOJIA YA SEO INA MSAADA GANI KATIKA BIASHARA ZA MTANDAONI?

Je, biashara yako ina uwezo wa kujiendesha hata kama haupo ofisini au pale unapofunga mlango wa ofisi? Kama jibu ni HAPANA, basi wakati wa kuhamisha biashara yako mtandaoni ni SASA kwa sababu Teknolojia haikusubiri wewe ndugu. Leo unapojiuliza teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni? majibu yote muhimu utayapata hapa. Cha kufanya, Fuatana nasi mpaka mwisho wa makala hii.

Imagine wateja wako wanaweza kufanya shopping wakiwa huko huko makwao, wengine wanasoma makala zinazotatua changamoto mbalimbali zinazowakabili na wengine wamepata mawasiliano yako mtandaoni. Yote hayo yanafanyika wewe ukiwa safarini, nyumbani, shambani au ukiwa na mishe zingine nje kabisa ya mtandao.

Faida ni nyingi sana ukiwa unafanya Online Business: Yani ukishakuwa na website inayofanya kazi sawia, ukawa na accounts za mitandao ya kijamii zinazoitambulisha biashara yako kila siku, hapo unafika kwenye hatua ambayo Internet inakufanyia kazi, na sio wewe kuwa Mtumwa wake.

NINI KINAKWAMISHA WATU WENGI SASA?

Watu wengi hudhani kuwa biashara za mtandaoni ni rahisi tu. Kwamba TCRA wameripoti kuwa kuna watumiaji wa internet milioni 29 kufikia October2021, so ukipost biashara yako itawafikia watu milioni29 chap. NO! Maisha si rahisi kiasi hiko asee!

Hii ni kwasababu miundombinu ya kimtandao (websites, blogu na mitandao ya kijamii) imetengenezwa katika namna ambayo inaheshimu Algorithms (mtiririko rasmi) fulani wa maneno, taaluma, mijadala, picha na mahusiano ili kuongeza ufanisi. Ndio maana tunasema kila siku Fuata Ushauri wa kitaalam.

Algorithms hizo huchochewa na mfumo wa kurahisisha utafutaji wa taarifa mtandaoni ujulikanao kama S.E.O (Search Engine Optimization). Mfumo huu huchukua links na maneno(keywords) yanayotumika zaidi katika blogu, websites na social networks na kuyaweka kwenye injini za matafuto kama Google na Bing.

Hivyo, kama unajua ama hujui, chochote unachokiandika sana katika social networks, blogs na websites huchukuliwa na kuwekwa katika Google na Bing. Lakini sio kila kitu unachokitafuta google utakipata kikiwa katika nafasi za juu pale google, Hapana, mambo hayaendi hivyo.

Kuna taarifa ukiitafuta utaipata kutoka kwenye biashara fulani ikiwa juu kabisa ukurasa wa mbele pale google. Taarifa hiohio pia unaweza kuipata kwenye blogu/website ambayo ipo ukurasa ya pili, wa tatu au wa 10.

Ubaya ni kwamba mteja hatatafuta jina la blogu/website yako, bali ataandika changamoto anayotaka kukabiliana nayo au kuhusu taarifa anayotaka kuitafuta mtandaoni. Mfano huandika kupitia google kutafuta “kirefu cha TEHAMA” “Biashara ipi ina faida zaidi Tanzania?” “Siri ya kuwa tajiri Afrika” “Mbinu za kufanikiwa kimaisha/kibiashara” “laptop za bei nafuu Tanzania“, “viatu vikali“, “Faida za TEHAMA“, “Faida za Website“nyimbo za bongo fleva 2022”, “Laptop za bei nafuu zinapatikana wapi?” “Faida za kilimo cha mananasi/tikitimaji” “Chakula kitamu zaidi Tanzania” nakadhalika.

Sasa, kupitia maneno hayo ya S.E.O umegundua nini?

Ngoja nikwambie kitu, Kama unafanya biashara mtandaoni, zingatia maneno ambayo yanatumiwa zaidi na watu wengi au yanayotafutwa zaidi na wateja katika Industry yako. Jiulize, kama wewe ndo ungekuwa mteja unatafuta kujua kuhusu bidhaa/huduma flani, ungeandika nini pale Google?

Sasa hayo maneno ambayo ungeyaandika google ndio chambo ambayo unapoyatumia mara kwa mara katika blogu/website/social media yako, basi unajiweka kwenye nafasi ya kupatikana kirahisi zaidi pale mteja akitaka kutafuta kuhusu huduma/bidhaa zako. Zingatia sana hilo.

Na hio ndio SIRI ambayo wengi wanaojiita “Wataalam wa SEO” hawatakwambia kuhusu teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni. Kuna watu hawaoni sababu ya kuwa na Website/Blog kwasababu vitu hivyo HAVIWAINGIZII pesa direct.

Kuna mmoja nilifanya naye nae kazi akaniambia kilichomkuta mwaka 2018, “Bwana mi nilishawahi kuwa na website ila mwaka ule mzima yani haikunipa hata mia, na niliilipia mnaita ‘Hosting Fee’ sijui. Sikuwahi kuona umuhimu wake, so nikaachana nayo”.

faida za teknolojia ya S.E.O katika biasharateknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

Najua hili hata wewe unalihofia Kwanza fahamu haya yafuatayo:

Kuwa na website hakukufanyi kupata wateja wengi kama hutafanya yafuatayo ili ufahamu teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni:

1. Hujatengeneza account ya Google Map: Zamani Google walikuwa wakitumia Application ya Google My Business ili kuwarahisishia wafanyabiashara waweze kuunda profiles zao na ziweze kupatikana kirahisi mtandaoni. Lakini baadaye waliona App ya Google Map inao uwezo wa kubeba taarifa zote muhimu, hivyo App ya Google My Business ikafikia mwisho wake hapo. Stori nzima ipo hapa. Google Map sasa huifanya biashara yako iweze kusajiliwa, kutambulika na kupatikana rasmi na kirahisi katika mtandao wa Google. Yani apa unatengeneza Profile ya biashara yako direct na kumruhusu mteja aweze kuona mpaka mahali biashara yako ilipo.

google Mapteknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

2. Hujaunganisha blog/website yako na huduma za Search Console: Hii Search Console kazi yake kubwa ni ku-crawl, yani kukusanya taarifa zote za website yako kama huduma/bidhaa unazohusika nazo, links za Menu (Home, contacts etc) Mada unazoziweka, mijadala na maneno unayotumia humo Kutengeneza links ziitwazo SITEMAPS na kuziweka kwnye injini za matafuto ya mtandaoni ili mteja akitafuta anachokitafuta basi google/bing iweze kuileta website yako ukurasa wa mbele kabisa. So ukifanyia kazi vema hiki kipande, Google itai-rank website yako katika nafasi za juu.

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoniGoogle Search Console

3. Huweki maudhui kwenye website/blog yako: Yule jamaa yangu nilikwambia pale juu kuwa hakuona umuhimu wa kuwa na website, changamoto kubwa alikuwa nayo ni kushindwa kuwa na website inayoruhusu kuweka maudhui frequently. Unakuta website ina tabs za Home, Services, About na Contacts peke yake tu, wala haina sehemu ya blog/news au sehemu ya kufanya shopping. Kwa biashara za kisasa hii ni changamoto kubwa sana kama bado hujafahamu teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni.

Fahamu tu kwamba website ambayo haina uwezo wa kuweka maudhui mara kwa mara kupitia Kipengele cha Blog/News ni NGUMU sana kutokea kwenye ukurasa wa kwanza wa google. Hii ni kwasababu Maudhui unayoweka kwenye kipengele cha Blog/News huifanya website yako kuwa ya Kipekee na inayojiboresha kila siku.

Na hivyo ni rahisi google kui-rank website yako katika nafasi za juu pale mtu akitafuta taarifa ambazo pia zinapatikana kwenye website yako. Hii ndo silaha ambayo itaiwezesha biashara yako kuweza kujitangaza yenyewe na kukusanya wateja wengi huku wewe ukiendelea na mishe zingine.

4. Hausambazi Mukhtasari wa taarifa (updates) zinazopatikana kwenye website yako: Ndio, SEO inafanya kazi automatic unapounganisha website yako na huduma ulizozisoma hapo awali, Lakini, ni muhimu pia kusambaza Updates kuhusu taarifa unazoweka kwnye website yako katika social accounts zako za instagram, facebook, twitter nakadhalika.

Hapa unatengeneza kitu kinaitwa BACKLINKS. Tayari nimeshakuwekea elimu ya kutosha kuhusu umuhimu wa Backlinks katika kuhakikisha website yako inafanya vizuri pale Google.. Fahamu tu kuwa ili Website yako iweze kuwa imara mtandaoni lazima links zake zipatikane kwenye media zingine kama Linkedin, Facebook, Twitter, ZoomTanzania, Clutch n.k.

Huko ndo Jikoni kwenye haswa, Kwa sababu, ukiachana na Google, kwenye mitandao hio ndipo watu wengi hushinda wakijadiliana kuhusu mambo mbalimbali ya kijamii, kisiasa, michezo na burudani. So ukiwapelekea solution kuhusu changamoto zao kisha ukawapa link, guess what will happen?

Kujua zaidi namna ya kuongeza traffic kwenye website yako tafadhali tembelea makala hii hapa chini:

KWANINI TUNA-SHARE SIRI HIZI KUHUSU TEKNOLOJIA YA SEO INA MSAADA GANI KATIKA BIASHARA ZA MTANDAONI?

Siku zote maendeleo mazuri ya mgonjwa ndo mafanikio ya daktari. Hivyo wewe mjasiriamali ukifanikiwa ktk website yako, huo ni ushindi pia kwetu developers na wataalam wa SEO. I hope elimu hii inakwenda kutibu changamoto zako katika biashara za mtandaoni?

Kwa makala nyingine nyingi zaidi, endelea kuperuzi ukurasa wetu wa https://rednet.co.tz/blog kila mara ambapo utagundua makala muhimu za kuimarisha uchumi wako binafsi na wa biashara/kampuni yako.

Mjasiriamali anapofanikiwa katika website yake, huo pia ni ushindi kwa web designer na wataalam wa S.E.O.teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni

Msaada binafsi tafadhali wasiliana nasi kupitia:

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

teknolojia ya SEO ina msaada gani katika biashara za mtandaoni
MPESA LIPA NAMBA YETU
focus on your plans and make sure you win.

UKWELI KUHUSU ‘PROPAGANDA’

Wengine watakwambia ni maneno ya uchochezi, wengine “siasa za uhuni hizo”, wengine wanaita figisu, mara fitna. Lakini Propaganda ni mada inayowasilishwa kwa lugha ya picha katika mawasiliano ambayo mara nyingi hubebwa katika kampeni mbalimbali kwa agenda fulani ya kificho. Leo sasa tuone huo ukweli kuhusu ‘Propaganda’. Ni upi? Makinika.

Serikali na mashirika mbalimbali hufanya Propaganda katika kusukuma Agenda zao ambazo zina lengo la kushawishi jamii na kuchochea mapokeo ya kihisa kuhusu jambo fulani. Propaganda zilizokomaa hugeuzwa kuwa utamaduni, mfano Propaganda ya kuagamiza maadui wa “Ujinga, Maradhi na Umasikini” imesababisha watu wengi kwenda shule kupata elimu, kutibiwa kwa tiba za kisasa na kuachana na zile za kizamani pamoja na kufanya kazi kwa lengo la kuboresha hali ya kiuchumi. Ujinga, Maradhi na Umasikini vimeonekana ni adui wa kumuangamiza kabisa mbele ya kila mwananchi sasa na hii imesababishwa na Propaganda za serikali ya awamu ya kwanza katika kufikia lengo hilo.

Kwa upande mwingine Propaganda zimekuwa zikitumika kufanyiana hila za kisiasa katika kumkandamiza mpinzani ili kupata ushindi katika kinyang’anyiro fulani. Mfano kwenye michezo unaweza kumwona @hajismanara ambaye ni mmoja kati ya wana propaganda wazuri sana nchini. Maneno yake, tambo na kampeni anazozifanya kwa kiasi kikubwa ziliisaidia sana @SimbaSCTanzania na Yanga Kupata ushindi hata kabla ya mechi. Propaganda zinapigwa kwa kiwango sana hapa.

Kwingine ni kwenye ulingo wa siasa ambapo huku ndo Propaganda zilipozaliwa (kama wanavyosema Mapenzi yamezaliwa Tanga). Kwenye siasa mara kadhaa Propaganda zimekuwa zikipigwa kukandamizana kisiasa na kuaminisha umma kuwa fulani ni bora zaidi kuliko fulani, na sera hii ni bora zaidi kuliko sera hii. Ili kuweza kujenga ushawishi kwa wapiga kura, wanasiasa wamekuwa wakipiga propaganda za hali ya juu ili kuhakikisha wanapata ushindi. Ukiona mwanasiasa fulani anapendwa sana na ana wafuasi wengi, basi kwa kiasi kikubwa tambua Propaganda zake ni za kiwango cha juu sana.

Hata hivyo kufanya Propaganda si Dhambi, wala hakuna mtu anakatazwa kuzifanya isipokuwa tu usivunje sheria za nchi. Kuna baadhi ya watu huamini kuwa Propaganda ni Maneno ya Uongo na Ulaghai, Hapana. Propaganda ni sanaa ya kushawishi watu wafuate dhana fulani ili kuleta faida kwa mtu au jamii ya watu fulani, kampuni, shirika au serikali.

MBINU ZIPI HUTUMIKA KUFANIKISHA PROPAGANDA?

Mafanikio ya kufanya propaganda huja pale serikali/biashara fulani inapotumia mbinu hizi katika kushawishi jamii kufikia lengo fulani ambalo halionekani wazi kwa mara moja.

i. NJIA YA USHIRIKA (BRANDWAGON): Hii wahenga wanakwambia “Ndege wafananao huruka pamoja” au “Ukitembea na mwizi na wewe utakuwa mwizi”. Njia hii ni ile ambayo mpigapropaganda kujihusanisha na walengwa kwa ukaribu katika kuhakikisha propaganda zake zinakuwa na ushawishi. Najua umeshawahi kuona namna wanasiasa au makampuni wanavyotumia watu wa kitengo cha Masoko katika kuwafikia walengwa wao. Mara nyingi mpigapropaganda hubadili mavazi kuendana na walengwa, wakati mwingine huongea lugha ile inayozungumzwa na walengwa kabisa ili kuhakikisha propaganda zake zinakuwa na ushawishi unaotakiwa.

Pata huduma za Website, SEO, Social Media Marketing na nyinginezo nyingi kutoka Rednet Technologies Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?ukweli kuhusu 'Propaganda'

ii.KUTAFUTA HURUMA YA JAMII (SNOP APPEAL): Hii ni njia maarufu sana ambayo kwa kiasi kikubwa imekuwa ikitumika katika kutengeneza story ambayo itagusa moyo wa jamii na kuhamasisha watu kukubali Agenda ambayo imebebwa katika propaganda hio. Inakuwa hivi, mtu hueleza story yake ambayo mara nyingi huwa ni ya kusikitisha, kwa lengo (linaloonekana) la kuhamashisha watu kutokata tamaa au kujenga uaminifu juu yao na hivyo kupata lengo (lisiloonekana) la kupata wafuasi, wateja au/na kura. Propaganda hii hufanywa sana na wasanii, wafanyabiashara na kampuni zinazoanza(startups). Umeshaanza kuuona hapa ukweli kuhusu ‘Propaganda’.

iii. MANENO YENYE UJAZO: Wahenga wanasema, “Maneno yanaumba”.Hii ni kwasababu maneno yana nguvu sana linapokuja swala la mahusiano ya kijamii. Ndio maana wanapropaganda hutumia maneneo yenye ujazo kubadili mtazamo wa jamii. Hapa wanapropaganda hutumia maneno matamu sana kushawishi jamii katika kufanya jambo fulani. Hali kadhalika wanapropaganda hutumia maneno ya hasira, chuki, fitna na hila ili kuhakikisha Agenda zao za siri zinafanikiwa. Wakati mwingine agenda hizo huwa na manufaa mema kijamii na wakati mwingine huja na lengo la kubomoa jamii.

Mathalani sisi Rednet Technologies tunakwambia, #WeGiveYouTheWorld hatuna maana kuwa tutakupa dunia kama ilivyo, hapana. Dhima yetu ni kuhakikisha tunakupatia taarifa zote muhimu kuhusu Biashara na Uchumi katika muktadha wa kiteknolojia ikiambatana na ushauri wa kitaalam.

Ili kuhakikisha wajasiriamali wadogo wanaimarisha biashara zao kupitia Matumizi ya teknolojia za kisasa kama Websites bora, softwares na chambuzi zisizokauka za kitaalam kupitia tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz. Tufuatilie uendelee kuimarisha biashara yako.

iv. KULINGANISHA DHANA: Wanapropaganda hutumia njia za kulinganisha dhana zao na matukio ya historia katika kupata kile wanachokidhamiria. Mathalani, katika siasa, watu wengi hupiga propaganda za kulinganisha hotuba za Mwalim Nyerere na matukio yanayoendelea katika kupush agenda zao.

Katika nyanja ya kibiashara, makampuni na mashirika hulinganisha maendeleo ya Kiteknolojia/Uchumi na uwezo wao wa kisasa katika kushawishi na kupata wateja wengi zaidi kila leo. Lakini chumvi ikizidi sana hapa, propaganda hizo hugeuka utapeli na kupoteza wateja kwa haraka sana.

v. NJIA YA SHUHUDA: Katika kufanya propaganda kwa njia hii makampuni na mashirika wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kuongeza wateja wapya na kukuza mauzo kwa viwango vikubwa sana. Makampuni/Mashirika yamekuwa yakiwatumia wasanii na watu mashuhuri kwenye jamii katika kueneza propaganda zao kuhusu huduma wanazotoa, bidhaa, kufungua matawi mapya ya ofisi pamoja na kufungua kampeni zao mbalimbali. Mara nyingi wasanii/watu mashuhuri wanaotumiwa kueneza propaganda hizo hawana elimu/taaluma kuhusu jinsi bidhaa/huduma inayoenezwa ilivyobuniwa/ilivyotengenezwa. Wao kikubwa ni kuhakikisha huduma/bidhaa hio inauzwa na kuketa faida kwenye kampuni/shirika hilo. Hapa ndipo unadhihirika ule ukweli kuhusu ‘Propaganda’.

mteja mshirikishe kwenye maamuzi. Msaidie aweze kununua huduma au bidhaa yako.ukweli kuhusu 'Propaganda'

Hata hivyo mbinu hio inaweza kutumiwa kwa kupitia Masoko ya kimtandao (Network Marketing) au/na masoko kwa njia ya mitandao ya kijamii (social media marketing) ambapo mtandao wa twitter, facebook na LinkedIn imekuwa ikiongoza kwa kuwafanya watu washirikishane bidhaa/huduma zao. Mathalan kupitia twita, unaweza kusambaza bidhaa/huduma zako kwa kupitia watu ambao hawana ujuzi wa kutengeneza hizo bidhaa/huduma zako. Mfano sisi @RednetCompany tunasambaza huduma zetu kupitia rafiki zetu katika mitandao ya kijamii Ambao hata hivyo wengi kati yao hawana ujuzi kuhusu jinsi ya kutengeneza website, computer maintenance n.k. Lakini Agenda inayobebwa katika propaganda hio ni kuhakikisha tunahudumia Wafanyabiashara na watu wengine wengi zaidi kila leo.

Hivyo ukiwa kama mfanyabiashara hakikisha propaganda zako unazifanya kwa utaalam na weledi bila kufanya ulaghai au kusema uongo ili kujipatia faida. Kwa maana hio si njia bora ya kufanikiwa kipropaganda. Jipange vema kwenye uwanja huu uliosheheni ushindani wa kila namna.

Vile vile tayari hapa tumekuandalia makala ambazo zinarandana na somo ulilojifunza leo. Gusa links hizi kufahamu zaidi:

  1. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021?
  3. FAHAMU SIRI YA KUWEZA KUSHAWISHI WATEJA KATIKA BIASHARA YAKO
  4. UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Umejifunza nini katika makal hii ya leo kuhusiana na ukweli kuhusu ‘Propaganda’? Tafadhali toa maoni yako kupitia comments hapo chini, nasi tutayafanyia kazi mara moja.

Mtandao saidizi jinsi ya kukabiliana na hasara kwenye biashara mbinu za kuwa tajiri Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji

UWIANO WA MALI (ASSETS) NA MADENI (LIABILITIES) KATIKA BIASHARA

Watu wengi wanapopata pesa nyingi kwa mkupuo (mara moja) mfano mshahara, pensheni, dili n.k hukimbilia kununua vitu kama mashamba, fenicha za ndani (kitanda, makochi), wakidhani kuwa hapo wamenunua assets. Too bad ni kwamba watu hujiingiza katika hali ya madeni (liabilities) ambayo huwadhoofu sana kiuchumi. Sasa leo tuone uwiano wa Mali (assets) na madeni (liabilities) katika biashara, ukweli ni upi? wapi ukuwekee umakini? Makinika…

Kwanza jiulize, tunaposema hii ni Mali (Asset) maana yake nini? Na tunaposema hili ni deni (liability) maana yake nini. Saa zingine mambo hayako vile ambavyo unaweza kutafsiri kirahisi.

ASSET: Hii ni ile mali ambayo unitumia kuingiza pesa katika biashara yako. Ngoja nikuulize, katika mali zako zote ambazo unazo, ngapi zinakuingizia pesa kila siku/kila baada ya muda fulani? Jibu unalo mwenyewe. Kama una mali (simu, nyumba, gari, laptop, friji n.k) na bado mali hio haikuingizii Pesa, hapo huna Asset bado ndugu.

LIABILITY: Hii ni ile kitu ambayo haikuingizii pesa na badala yake, Kitu hii inafyonza pesa katika mifuko yako. Mfano mzuri ni Simu za vijana wengi, yani unakuta kijana anatumia simu ya gharama, kaiwekea cover la gharama, protector ya kijanja na Bando haliishi. Lakini kijana huyo hajawahi kiutumia simu yake hio anayotamba nayo kuingiza pesa. Kama unahisi nakufokea hapa nisamehe tu. Lakini kufikia hapo simu hio inageuka Deni/Mzigo/Liability. Kwasababu haikusaidii kuingiza pesa, hio ni liability tu. Mfano mwingine wa liability ni nyumba ya kuishi, gari ya kutembelea, mkopo, Kuwa na wanawake wengi (kama wewe ni mwanaume), starehe na maisha ya anasa.

Watu wengi hasa vijana hujikuta wana Liabilities nyingi kuliko Assets, lakini ukimuuliza anakwambia ana assets nyingi kwa kuwa amenunua vitu vingi geto na anatembelea gari nzuri mjini, utamwambia nini apo?

KIBIASHARA IMEKAEJE HII?

Biashara ili iwe imara, inapaswa kuanza kidogo na kisha kukua taratibu bila kuruka stage. Yani kama mtoto mdogo tu, lazima anyonye, atambae, ajifunze kuongea, atembee na kuanguka mara kadhaa kabla hajaanza kukimbia, kutumwa dukani na kuanzishwa shule. Kama ni hivyo kwanini ewe mjasiriamali uliyeanza biashara huna hata miaka miwili ukate tamaa? Hakuna kuruka stage hapa. Na ili uweze kwenda sawa sawa unapaswa kukusanya Assets nilizoelezea leo hapo juu achana na achana na zile ulizokariri shuleni kwenye book-keeping hapo kabla.

Mfano wa assets katika biashara ni Website nzuri iliyounganishwa na teknolojia ya S.E.O, akaunti hai za mitandao ya kijamii kama facebook, instagram, youtube, twitter nk, laptop, simu, printer, jengo la ofisi, connections zako na watu mbalimbali mjini (yes connection ni asset.) pamoja na vifaa vingine unavyovitumia kila siku katika biashara yako. Vipi hapo umeshaanza kupata picha kuhusu uwiano wa Mali (assets) na madeni (liabilities) katika biashara? Tuendelee..

Kufahamu vizuri kuhusu namna ya kutumia teknolojia ya S.E.O kwa manufaa katika biashara yako fuatana na makala hii hapa..

NINAWEZA VIPI KUBADILI MADENI (LIABILITIES) ZANGU KUWA MALI (ASSETS)?

Hili ni swala la ukomavu na maamuzi magumu. Liabilities zako kama smartphone, laptop, gari nakadhalika, unaweza kuzibadili kutoka kuchati, kuangalia muvi na kupigia misele kwa pisi kali mpaka kuweza kukuingizia pesa nzuri.

Mohammed Dewji (@moodewji ) aliwahi kutweet kutushauri vijana kuhusu “Kuongeza Mali na kupunguza Madeni” na bahati nzuri kuna mdau mmoja alinijia nimuelezee, pale Bro alimaanisha nini il’hali pesa ya kujikimu tu bado haitoshi? Nakwambia, hii ndio maana ya ile tweet ya bro Mo Dewji, kwamba hakikisha Assets zinaongezeka kwa kasi zaidi kuliko kasi ya kuongezeka kwa Liabilities. Hapa kuna mtihani mkubwa sikufichi. Maisha ya Watu wengi huongezeka gharama pale kipato kinapozidi kuwa kikubwa.

Angalia mfano huu kutoka katika kitabu maarufu cha Rich Dad Poor Dad

UWIANO WA MALI (ASSETS) NA MADENI (LIABILITIES) KATIKA BIASHARA UKWELI NI UPI?

Ndipo utaelewa kwa nini masikini wanazidi kuwa masikini, Watu wa uchumi wa Kati (mnajijua) wanazidi kukimbizana na mbio za panya, na matajiri wanazidi kuwa matajiri. Narudia ili uweze kubadili Liabilities zako ziwe Assets unahitaji kuwa Mkomavu na Kuchukua Maamuzi Magumu.

Hayo maamuzi magumu yanapaswa kuongozwa na ile Kiu ya kutaka kufanikiwa, sio uchawi na mambo ya kurudishana nyuma. Na pia kuwa Mkomavu unapaswa kuwa misuli katika akili yako. Kama ilivyo misuli ya mwili inahitaji mazoezi ili iweze kuwa Imara na yenye nguvu, kadhalika misuli ya akili yako. Hapa ili akili yako iwe na misuli imara kwanza jiweke kwenye MAZINGIRA ya watu wenye akili na waliofanikiwa kukuzidi. Watoto wa mjini wanaita Koneksheni. Hii ndio asset namba moja.

Ukiweza kubadili na kuimarisha mazingira yanayokuzunguka kwanzia kwa watu wako unaowashirikisha shughuli zako za kila siku, Akili inaanza kukomaa, na automatically unakuwa unao uwezo wa kufanya maamuzi magumu kuhusu hali yako ya Uchumi na Biashara yako. Ukiwa na akili Hasi hapa hutaweza kunielewa kamwe. Hebu fungua hicho kichwa vizuri kabisa kwanza.

IFAHAMU BALANCE SHEET KATIKA KUUTAFUTA UWIANO WA MALI (ASSETS) NA MADENI (LIABILITIES) KATIKA BIASHARA

Licha ya kuwa ni kitabu cha kihasibu, lakini ni muhimu sana katika utendaji wa biashara yoyote na/uchumi binafsi wa mtu yeyote. Kitabu hiki ndicho kinachoweza kukuonyesha afya ya biashara yako au uchumi binafsi. Tizama mfano huu kisha ili uweze kutengeneza Balance Sheet yako binafsi chora alama mfano wa “T” katika karatasi kisha Upande mmoja uite ASSETS kisha orodhesha mali zako zote ambazo zinakuingizia pesa kila siku. Upande wa pili uite LIABILITIES kisha orodhesha mali zote mabazo zinakugharimu pesa bila kuingiza ili kuziendesha.

Ukishafanya hivyo, utakachokipata ndicho kitakupa hali yako kiuchumi ya sasa (kama ni Masikini, mtu wa Uchumi wa kati au Tajiri). Kwa manufaa zaidi zoezi hili unaweza kulifanya kila Unapoanza mwaka mpya. Ule muda watu wamekomaa kuandika Resolutions zao wewe tengeneza Balance sheet yako, kisha ifanyie kazi kwa kuongeza orodha ya Assets na kujitahidi kupunguza/kutoongeza Liabilities zisizo na maana. Kwa hakika kila mwaka mpya ukifanya hivi, matokeo chanya lazima uyaone.

UTAJIRI (NET WORTH) UNAPIMWA VIPI?

Najua umeshawahi mara nyingi tu kuona ile orodha watu matajiri zaidi duniani. Unajua wanapimaje utajiri huo il’hali hawajui hata masalio ya watu hao katika benki wanazohifadhi pesa zao. Leo nakujuza sasa. Hesabu ni ile ile: Orodhesha Assets zote alizonazo mtu fulani unayemfahamu, kumbuka hapa assets tunazoziongelea ni zile mali zinazoingiza pesa tu. Kisha tafuta thamani yake. Halafu orodhesha Liabilities zake zote unazozifahamu (zile mali zinazomfyonza pesa). Ukimaliza fanya hivi; ASSETS – LIABILITIES = NET WORTH

utajiri unapimwa vipi?Watu wengi wanapopata pesa nyingi kwa mkupuo (mara moja) mfano mshahara, pensheni, dili n.k hukimbilia kununua vitu kama mashamba, fenicha za ndani (kitanda, makochi), wakidhani kuwa hapo wamenunua assets. Too bad ni kwamba watu hujiingiza katika hali ya madeni (liabilities) ambayo huwadhoofu sana kiuchumi. Sasa leo tuone uwiano wa Mali (assets) na madeni (liabilities) katika biashara, wapi ukuwekee umakini? Makinika...

Hesabu hii ukitaka iseme ukweli kabisa anza kujipigia wewe mwenyewe, uone jinsi gani unapoteza muda hapa duniani kupiga umbea na kufanya mambo yasiyo na maana. Unavyochora ile Balance sheet yako pale kila mwanzo wa mwaka, piga na hii Net Worth yako, ili ujue kabisa huo mwaka unaoanza unapaswa kuwa serious namna gani. Kifupi hizo ndizo Assets na Liabilities katika uchumi binafsi na uchumi wa kibiashara. Kwa maana ili biashsra iweze kumea vyema basi Mtendaji hana budi kuwa muumini namba moja ws falsafa bora za kibiashara, na falsafa bora ndizo hizi.

Ni matumaini yangu makala hii ya leo kuhusu uwiano wa Mali (assets) na madeni (liabilities) katika biashara, ukweli ni upi? basi umepata majibu ya maswali yaliyokuwa yanakusumbua. Una lolote la kuchangia? Tafadhali comment hapo chini na endelea kufuatilia makala zetu nyingine nyingi kupitia tovuti yetu maridhawa ya Rednet Technologies ili usipitwe daima.

Twende pamoja kidijitali kupitia makala zifuatazo ili upate muendelezo mzuri wa mada hii ya leo. Gusa link kisha makinika.

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

IFAHAMU TEKNOLOJIA YA QR-CODE KATIKA BIASHARA YAKO

Kwa kasi ya maendeleo ya kiteknolojia inavyozidi kuchanja mbuga, watu wanatumia sana simu janja kwa matumizi mengi zaidi ukiacha kupiga simu na kutuma ujumbe. Uwezo wa kununua bidhaa na kupata huduma haraka umewezeshwa zaidi kupitia ujio wa QR-Codes. Sasa leo ifahamu teknolojia ya QR-Code katika biashara yako. Makinika.

Hizi QR (Quick Response) codes zinaweza kusomwa na kudadavuliwa vyema kwa kutumia Simu janja na vifaa maalum vya kielektroniki (QR-scanners) na hivyo kujenga wepesi kwa watu wa masoko kuingiza maelezo kuhusu majukwaa yao kupitia hizi QR Codes. Yani maisha ya kibiashara yamekuwa mepesi kweli.

QR-codes hizi huweza kuwekwa katika mabango, magazeti, kurasa za tovuti na vyombo vingine vya kimasoko ili kurahisisha usambazaji wa bidhaa na huduma kwa haraka na wepesi zaidi. Matumizi ya QR-Codes yamekuwa yakizidi kutanuka kila uchwao ambapo katika kipindi cha mwaka 2018/19 peke yake, matumizi ya QR Codes duniani yaliongezeka kwa 28% huku ongezeko la muingiliano katika kipindi hicho likikuwa kwa 26% (chanzo: akaunti ya Blue Bite, mtandao wa medium).

QR CODES ZINA TOFAUTI GANI NA BARCODES?

Japokuwa Barcodes zilianzishwa miongo mingi kabla, QR Codes zimekuja na mapinduzi makubwa ndani ya muda mfupi.

1. Kama ulishawahi kununua bidhaa ya kiwandani hasa zile zinazouzwa katika supermarkets, utagundua bidhaa hizo zina alama fulani za vimistari pamoja na namba. Alama hizo ndio huitwa BARCODES. Sasa hizo Barcodes hutumika kuhifadhi maelezo muhimu kuhusu bidhaa husika kama jina la bidhaa, mtengenezaji, bei, kiwango cha ubora n.k. QR Codes kwa upande wake hufanya kazi sawa sawa na hizo Barcodes, isipokuwa tu katika QR Codes, zina uwezo wa kuhifadhiwa data nyingi kwa mamia zaidi katika nafasi ndogo.

2. MUONEKANO: Hii ndio tofauti kubwa katika ya hizi teknolojia mbili. Kwa kutizama tu unaweza kujua ipi ni QR Code na Ipi ni Barcode. Hebu tizama mifano hii hapa chini.

ifahamu teknolojia ya QR-Code katika biashara yako. Makinika.

3. UWEZO WA KUJISAHIHISHA: Kwa utofauti huu, QR Code inakuwa bora zaidi kuliko Barcode na kujitofautisha katika viwango vya matumizi. Muonekano wa QR Code unaifanya iweze kutoa taarifa kuhusu bidhaa/huduma vizuri hata kama ikitokea sehemu za alama hazionekani vizuri au zimechanika tofauti na Barcode ambapo ukifutika mstari mmoja tu Barcode inashindwa kutoa maelezo kamili kuhusu bidhaa/huduma.

QR CODES HUTUMIKA WAPI NA WAPI?

Kimsingi QR Codes hutumika katika kuhamasisha muingiliano katika ya mteja na huduma kupitia alama za kielektroniki kwa uharaka zaidi kwa kutumia simu janja au QR-Code scanners. Hii ni mbinu bora sana ya kimasoko katika kurahisisha utoaji huduma na uwezeshaji wa malipo/miamala ya kifedha. Sasa tuone maeneo ambayo QR Codes zinatumika:

1. KUELEKEZA WATUMIAJI KATIKA KURASA/TOVUTI:

Unaposcan QR Code, inaweza kukuelekeza katika kurasa fulani maalum au tovuti ambayo maelezo yake yamefichwa katika CODE hio. Zoezi hili unaweza kulifanya kwa wepesi kupitia QRCode iliyopo kwenye tangazo hili ambayo itakuelekeza katika fomu maalum ya kujiandikisha kuhudhuria mafunzo yanayojieleza.

2. KUPIGA SIMU NA KUPATA MAWASILIANO:

Katika mikutano ya kibiashara mara nyingi watu hukutana na kubadilishana mawasiliano kwa wingi. Lakini zoezi hilo hufanywa jepesi kwa kutumia QR Code ambapo kitendo cha kuscan tu hukuwezesha kupata mawasiliano yote muhimu kuhusu mtu fulani.

Kinachofanyika ni kujaza taarifa muhimu katika QR Code kisha CODE hio hupachikwa katika Business Card mara nyingi. Hivyo unaposcan unapata mawasiliano yote pasi na kuhangaika kuandika namba moja moja katika simu yako.

simu za michongo Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

3. KUPAKUWA APPS MTANDAONI:

Unaposcan QRCode katika masijala za Aplikesheni za mitandaoni, basi unakuwa na uwezo wa kupakuwa App husika kirahisi bila ya kuhangaika kutafuta App hio mitandaoni. Unapoikuta QR Code wewe scan tu, mambo mengine yatajiendeleza yenyewe kirahisi.

4. KUJUA MAHALI BIASHARA ILIPO:

Naam, kupitia ramani za kimtandao kama Google Map, mtumiaji anaweza kuscan QR Code ya biashara na mara hio akaweza kuona mpaka mahali/location biashara hio ilipo. NOTE: Location hio lazima iingizwe kwanza katika QR Code na mfanyabiashara husika.

5. KUFANYA MANUNUZI NA MALIPO:

Pengine hii ndio njia maarufu zaidi ambayo QR Code hutumika. Makampuni ya huduma za mitandao yameingiza na kuboresha sana njia hii katika kufanya manunuzi na malipo. Mara nyingi wafanyabiashara hutumia njia hii katika kutoa punguzo la bei au kufanya matangazo (promo) kwa bidhaa/huduma fulani. Ni mwendo wa kuscan tu na malipo yako unakuwa umekamilika mara hio. Unachotakiwa kufanya kama mfanyabiashara ni kuhakikisha QR Code yako inafanya kazi ile uliyoiamuru (Call-To-Action). Mtumiaji hatakiwi ajiulize afanye nini baada ya kuscan hio code.

HIZI QR CODES ZINAFANYA KAZI VIPI?

Ili uweze kutengeneza au kutumia QR Code ukiiona mahali unatakiwa kuwa na vitu vifuatavyo:

>QR Code Generator: Kuna majukwaa mengi sana mtandaoni ambayo unaweza kuyatumia kutengenza QR Code kwa matumizi yako unavyotaka. Baadhi ya majukwaa hayo Ni pamoja na http://qrcode-monkey.com na http://the-qrcode-generator.com . Katika majukwaa haya unaweza kutengeneza QR Code yako, ukaweza na maelezo kama namba ya simu, tovuti, location nakadhalika. Lakini pia yapo majukwaa ambayo unalazimika kulipia ili uweze kutengeneza QR Code yako.

Majukwaa hayo ni pamoja na KAYWA na ni salama zaidi pale unapotaka kutengeneza QR Code ambayo ni mahsusi kwa ajili ya kurahisisha malipo yoyote. Vya bure vina madhara sana hasa katika maswala ya kifedha. Kuwa makini hapo.

>QR Code Readers: Hizi ni Apps ambazo unazipata katika simu yako mahsusi kwa ajili ya kutambua QR Code na kukupeleka kule kunapotakiwa kwenda. Kwa watumiaji wa iPhone unaweza kupakuwa App inaitwa i-nigma ambayo inatajwa kama App bora zaidi duniani katika kuscan hizi QR Codes. Kwa watumiaji wa Android unaweza kupakuwa App iitwayo Barcode Scanner (watumiaji wa tekno nao wamo hapa.)

KWANINI UTUMIE QR CODE KATIKA BIASHARA YAKO LEO?

Mwaka 2019 matumizi ya QR Code katika kufanya malipo ya bidhaa na huduma yalipata umaarufu mkubwa sana duniani huku makampuni makubwa kama Mastercard na Paypal yakithibitisha matumizi katika kutambua account za wateja na kuidhinisha malipo.

Tafiti zinaonyesha kuwa wateja wanaolipia kwa kutumia QR Code hufanya manunuzi makubwa zaidi. Sasa leo hizi ndizo sababu zitakufanya ifahamu teknolojia ya QR-Code katika biashara yako. Mwaka 2013 Adobe mobile consumer uliowahusisha wstumiaji wa simu 3,075 ulionesha majibu haya;

•46% ya wateja waliscan ili kupata discount

•42% walitumia QR Code kama tiketi

•67% walishuhudia huduma za QR Code katika maduka ya mtaani.

Mpaka kufikia mwaka 2020 takwimu hizo zinatajwa kuongezeka maradufu zaidi. Lengo kuu hapa ni kuhakikisha QR Codes zinasaidia wateja kufanya shughuli zao kwa wepesi zaidi.

Makala hizi hapa chini zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana ukizipitia zote. Gusa link kisha makinika:

  1. FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA DUNIANI
  2. UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA
  3. UGUNDUZI WA KITEKNOLOJIA KUELEKEA KATIKA MUSTAKABALI WA SEKTA YA UZALISHAJI MALI

Umejifunza nini kwenye makala ya leo katika ku ifahamu teknolojia ya QR-Code katika biashara yako. Tafadhali toa maoni yako na sambaza hii kwa jirani yako.

unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako leo?

UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO LEO?

Umeshasikia mara ngapi kampuni inakuwa na vyanzo vingi vya taarifa kuhusu bidhaa/soko/wateja lakini bado haivitumii sawia vyanzo hivyo au haifahamu hata kuwa inavyo vyanzo hivyo? Sasa leo tuangalie unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako leo?

Taarifa ndio kila kitu katika ulimwengu wa leo. Taarifa(Data) zina thamani kubwa ingawa thamani yake hutegemea jinsi unavyozikusanya na kuzichambua. Kama haujafanyika uchambuzi na upembuzi yakinifu, data hukosa maana yake halisi.

Sasa ili uweze kukusanya, kuchambua, kudadavua na kufanya tathmini sahihi hapo ndipo UJASUSI WA KIBIASHARA unapokuja kuhusika. Ujasusi huu unahusika zaidi na data za ndani ya kampuni kuhusu taarifu za wateja, aina za bidhaa/huduma zinazozalishwa, ubora wa bidhaa, huduma kwa wateja, kiwango cha usambazaji, mrejesho kutoka kwa wateja/wabia, Utendaji wa wafanyakazi pamoja na matumizi ya teknolojia.

Kuyafanya yote haya katika kiwango kinachotakiwa na kuleta majibu chanya, Biashara/kampuni haina budi kutengeneza mifumo mizuri ya kukusanya data pamoja na kuwa na wachambuzi (analysts) wazuri wa data hizo. Ndani ya miaka michache iliyopita Ujasusi wa Kibiashara (BI) umebadilika sana na kujumuisha taratibu mbalimbali ili kuhakikisha Utendaji wa Kibiashara Unaimarika.

Taratibu hizo zinajumuisha;

1. DATA MINING (UVUNAJI WA TAARIFA)

Hii ni ile jinsi kampuni hukusanya data kupitia taarifa mbalimbali za wateja wao pale wanapotembelea majukwaa yao, haswa yale ya kimtandao. Taarifa zinazokusanywa hapa ni kama majina na anwani, location, aina ya bidhaa/huduma zinazotumiwa zaidi, tovuti zinazotembelewa zaidi nakadhalika. Makampuni makubwa duniani hutumia sana njia hii kuvuna data za watumiaji wao na kuziuza kwa makampuni mengine kulingana na matakwa ya kibiashara. Kujua zaidi jinsi ya kutumia mitandao ya kijamii katika kukusanya data tafadhali tembelea makala kupitia makala hii IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA.

2. REPORTING

Kiutaratibu kazi ikishafanyika huripotiwa katika mamlaka za juu katika kampuni/biashara ili kutoa maamuzi. Kushirikishana taarifa za uchambuzi katika biashara/kampuni hufanya zoezi la kutoa maamuzi kuwa jepesi na lisilotumia muda mrefu.

3. KULINGANISHA UTENDAJI

Utendaji wa biashara huimarika kirahisi pale kunapokuwa na kumbukumbu katika nyakati tofauti ambazo huonyesha viwango vya utendaji na hivyo kuchochea kufikia malengo ya kampuni kwa wepesi zaidi. Hii ni kama kumbusho kuwa Utendaji unapaswa kuimarika kuliko ulivyokuwa wakati uliopita.

4. UCHAMBUZI WA KITAKWIMU

Data zilizofanyiwa kazi huweza kuwekwa vizuri kupita michoro ya kitakwimu ambayo hutoa picha nzuri kuhusu data zilizokusanywa na hivyo kupatikana maamuzi sahihi kuhusu biashara.

5. UANDAAJI WA DATA

Ujumuishaji wa vyanzo mbalimbali vya taarifu, kutambua vipimo mbalimbali kwa pamoja hufanya zoezi la uchambuzi kuwa rahisi zaidi. Hapa wengine huita ‘Kuunganisha dots’.

UJASUSI UNA FAIDA GANI KWENYE BIASHARA?

Ukusanyaji wa data, uchambuzi, upembuzi mpaka inapofika wakati wa kutoa maamuzi, Ujasusi huleta matokeo chanya pale unapofanyika katika Biashara/Kampuni kwa kuzingatia taratibu zilizoelezwa hapo awali. Hapo ndipo utaelewa unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako (Business Intelligence). Baadhi ya faida zinazoweza kupatikana kutokana na ujasusi huu ni;

i. Kugudua njia za kuongeza faida katika biashara. Likiwa ni lengo kuu la biashara yoyote, kupata faida kunaweza kuongezeka ama kupungua ikiwa utazingatia jinsi Ujasusi wako unavyoufanya katika shughuli za kila siku.

ii. Kuchambua tabia za wateja kuhusu bidhaa/huduma wanazozipenda zaidi na zile wasizozipenda, mtiririko wa manunuzi na mauzo.

iii. Kuwa na uwezo wa kupima, kufuatilia na kutabiri kuhusu mauzo na utendaji imara wa maswala ya kifedha katika biashara/kampuni yako.

iv. Kuimarisha Huduma kwa wateja na utaratibu wa kufikisha bidhaa/huduma kwa wakati.

v. Kutengeneza mipango mizuri ya kifedha, bajeti na makadirio ya kitaalamu zaidi.

vi. Kuwa na uwezo wa kuona fursa katika ushindani mkali wa masoko. Data hukuhakikishia nini cha kufanya ili kupata Soko kubwa katikati ushindani mkali unaoendelea duniani hivi sasa.

UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO (BUSINESS INTELLIGENCE)?

Kampuni na biashara zote hunufaika sana pale zinapotumia ujasusi katika shughuli zao. Lakini kuna vidalili ambavyo ukiviona basi huna budi kuanza kutumia mbinu za kijasusi ili kunusuru biashara/kampuni yako. Wacha tuzione dalili hizo kwa uchache hapa:

i. Kukosekana kwa nidhamu katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji wa kampuni/biashara kama maswala ya fedha, mfumo wa habari na taarifa.

ii. Kampuni/biashara inapokua kwa ghafla kutokana na kupata faida kubwa katika wakati mfupi au kuongezeka kwa uwekezaji. Hapa usipotumia ujasusi vizuri utajikuta unarudi sifuri chap.

iii. Pale unapohitaji kupata taarifa fulani za kiutendaji zilizo sahihi na kwa haraka bila kufanya upembuzi yakinifu au kwa kudhania.

iv. Kuongezeka idadi ya wateja/watumiaji wanaohitaji taarifa/bidhaa/huduma fulani zilizothibitika kiuchambuzi. Hapa ndipo yanapokuja maswala ya ‘zimazoto’ sasa.

Je wajua kuwa bando lako ni Mtajiunawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako leo?

Unapokumbana na dalili hizi katika utendaji wa biashara/kampuni yako, ni dhahiri huna budi kupitia upya mfumo mzima wa kukusanya taarifa mbalimbali katika biashara yako kama aina ya bidhaa/huduma zinazopendwa/zisizopendwa, bidhaa/huduma kulingana na hali ya hewa, aina ya wateja wako wakubwa, wanapopatikana kwa wingi nakadhalika. Baada ya kufahamu hilo hakikisha unaandika na kuandaa ripoti mara kwa mara kwa kadiri inayowezekana (kwa mwezi, miezi3/6, mwaka). Halafu hakikisha unafanya uchambuzi vizuri kila unapoandaa ripoti yako. Jambo hili litakuongezea uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kila wakati unapohitajika kufanya hivyo. Usiache kutumia ujasusi huu.

BIASHARA ZIPI ZINAWEZA KUTUMIA UJASUSI HUU?

Biashara zote zinao uwezo wa kutumia ujasusi katika shughuli zao za kila siku. Utaratibu huu ni msaada mkubwa kwa biashara za aina zote na viwanda kutoka vidogo mpaka vile vikubwa. Ni mbinu inayotumika dunia nzima.

Katika biashara za rejareja, Wal-Mart kwa mfano, hutumia data nyingi sana katika nyanja mbalimbali ili kuhakikisha wanaendelea kuliteka soko. Harrah’s amebadilisha sana ushindani katika michezo ya televisheni kutoka kujenga makasino makubwa mpaka kutengeneza Aplikesheni za kwenye simu zilizotengenezwa kukidhi haja za wateja na zenye huduma bora zaidi. Amazon na Yahoo sio tu tovuti za e-commerce, zimekithiri uchambuzi wa data na hufuata mbinu ya “test and learn” katika kubadili biashara zao kulingana na soko.

TEKNOLOJIA ZINAZOTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA

Microsoft Power BI: Hii ni software ambayo huzalisha data nyingi sana pamoja na uchambuzi katika namna ambayo ni rahisi kutumia ikijumuisha Dashboard yenye ripoti mbalimbali, uchambuzi na utabiri wa kibiashara. Software hii huwasiliana na MS Office na hivyo kukurahisishia zoezi la kuingiza data ambazo hazijachakatwa kutoka vyanzo mbalimbali. Zingine ni Sisense na Zoho Analytics. Zote hizo zinapatikana mtandaoni kirahisi kwa kufuara utaratibu uliowekwa.

Sasa niwaulize wafanya biashara wa humu ndani. Mnatumiaga taratibu zipi za kijasusi kuhakikisha biashara zenu zinashamiri? Tupe maoni yako tafadhali kisha fuatana na makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata leo. Gusa link kisha makinika.

  1. IFAHAMU TEKNOLOJIA YA QR CODE KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BRANDING vs MARKETING. KIPI NI KIPI?
  3. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO?