Tag: matangazo

UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Mteja hakosei na mteja ni mfalme. Hizi ni kauli maarufu sana katika biashara duniani, lakini haswa biashara zinazofanyika kusini mwa jangwa la Sahara. Maana yake ni kwamba, Mteja anatakiwa kusikilizwa na kuridhishwa na huduma/bidhaa zinazotolewa na mfanyabiashara. Je, wewe unatumia mbinu zipi ili kuhakikisha huduma/bidhaa zako zinawaridhisha wateja wako? Katika makala yetu ya leo utakwenda kufahamu kwa undani siri na umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja. Twende pamoja mpaka mwisho.

Sasa ripoti ya mwaka 2019 kutoka shirika la kimataifa la ukaguzi wa mahesabu la PwC imeonyesha kwamba 64% ya Wakurugenzi wa Makampuni na Wafanyabiashara barani Afrika hawana data na takwimu kuhusu mwenendo wa wateja wao. Inashangaza eeh?

Kwa upande mwingine ripoti ya McKinsey imeonyesha kwamba makampuni yanayotumia data na takwimu sahihi kuhusu mwenendo wa wateja wao huyazidi yale yasiyofanya hivyo kwa 85% katika ushindani wa masoko na 25% zaidi katika kuingiza mapato kila mwaka.

Zaidi 95% ya wateja huongelea zaidi huduma mbovu walizokutana nazo katika kampuni/biashara fulani (Mtandao wa American Express), hali kadhalika 89% kati yao huacha kabisa kufanya biashara na kampuni/biashara fulani baada ya kukumbana na huduma/bidhaa zisizokidhi mahitaji/viwango walivyotegemea (ripoti ya Huduma kwa wateja ya mtandao wa RightNow). Kama unaijali biashara yako na ungependa kuona inazidi kukua, makala haya ni kwa ajili yako.

Sasa Changamoto; Kuna umuhimu gani katika kumridhisha mteja wako katika biashara unayofanya baada ya kujua takwimu sahihi kuwahusu?

1. KUONGEZA MAHUSIANO MAZURI NA MTEJA; Mteja aliyeridhishwa na huduma/bidhaa zako atabaki kuwa mteja wako kwa muda mrefu zaidi kutokana na huduma bora anazopata kutoka katika kampuni/biashara yako. Hakikisha unamshirikisha mteja kufanya maamuzi katika mchakato mzima wa kuhudumia. Muulize maswali kama Unaonaje ikiwa hivi au ikionekana vile, Unajiskiaje. Mpeti peti mteja wako muda wote kama unataka aendee kutumia huduma/bidhaa zako.

2. Waswahili wanasema, Kauli Njema ni silaha. Yaani unapokuwa na Kauli njema katika kusambaza huduma/bidhaa zako, unaiweka bishara/kampuni yako katika nafasi nzuri ya kuishindani dhidi ya washindani wako katika soko. Kauli njema ni kama sumaku ambayo inawaleta pamoja wateja na huduma/bidhaa zako na hivyo kufanya wateja wako kuendelea kuwa wako, lakini zaidi kauli njema huwavuta pia wateja wapya kuanza kutumia huduma/bidhaa zitokazo katika biashara/kampuni yako.

umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja

3. KUPUNGUZA GHARAMA ZA MATANGAZO; Kampuni/biashara yako inapotoa huduma bora kwa wateja wake huwafanya wateja hao kuwa mawakala ambao hutangaza huduma bora wanazopata katika kampuni/biashara hio. Kama tulivyoona hapo mwanzo, 95% ya wateja duniani hueleza katika jamii zao jinsi walivyokutana na huduma mbovu/dhaifu walizokutana nazo katika kampuni/biashara fulani. 89% kati yao huacha kabisa kujihusisha na bishara/kampuni ambayo haikuwapatia huduma bora au haujali wateja wake. Hata hivyo bado ni muhimu sana uendelee kuitangaza biashara yako. Gusa hapa kufahamu kwanini.

Na njia bora kabisa ya kutoa huduma bora na kwa wakati huo huo ukipunguza gharama za matangazo ni kwa kutumia teknolojia kama website iliyounganishwa na huduma za S.E.O. Kwanini uwe na website? Majibu yanapatikana kwenye makala hii hapa kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website rasmi ya biashara yako.

4. MAFANIKIO KATIKA BIDHAA/HUDUMA ZIJAZO; Kampuni/biashara hujiweka katika nafasi nzuri ya kufanikiwa katika kusambaza huduma/bidhaa zake mpya pale inapokuwa na kumbukumbu nzuri katika kutoa huduma bora kwa wateja wake.

Matokeo yake, kampuni/biashara hulenga wateja wake wa kudumu katika kusambaza huduma/bidhaa zao mpya ambapo hujihakikishia mafanikio kabla ya kuwasambazia wateja wapya. Hata hivyo wateja wanaoridhishwa na huduma bora zitolewazo hupendelea bidhaa/huduma mpya zitokazo katika kampuni/biashara walizowahi kuhudumiwa vizuri hapo mwanzo.

5. MTEJA WA KUDUMU NI LULU; Kwa mujibu wa Ikulu ya Marekani (#WhiteHouse) Ofisi inayoshughulikia maswala ya wateja, kwa wastani, mteja aliyeridhika na huduma/bidhaa (mteja wa kudumu) katika biashara ana thamani mpaka mara 10 zaidi kuliko thamani ya manunuzi yake ya kwanza.

Tafiti zingine zimeonyesha kwamba ni ghali zaidi ya mara 6 mpaka 7 kumpata mteja mpya kuliko kumtunza mteja wa aliyepo/wa kudumu. Taasisi za kifedha, mabenki na makampuni ya simu kwa mfano, yamejifunza sana katika hili, hivyo hawaoni tabu kuchukua hatua za ziada kuhakikisha mteja ambaye hakuridhishwa na huduma anapatitwa suluhu mbadala haraka sana kuendana na mahitaji yake. Hapa ndio utauona umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja.

6. WANAWEZA KUACHA KUWA WATEJA WAKO MUDA WOWOTE; Si jambo la ajabu hasa katika zama hizi za usasa mteja kuhamia kampuni yoyote atakayopenda kutumia huduma/bidhaa zake. Hii huchochewa zaidi na huduma mbovu/dhaifu za wateja wanazopatiwa zikiwemo kusubirishwa muda mrefu katika kupatiwa huduma/bidhaa/mrejesho/maoni kutoka kwenye kapuni/biashara fulani. Ni jambo lisolopendeza kabisa, lakini bado mambo kama hayo yanaendelea kutukia.

“Mteja anapokwambia hitaji lake, hakwambii tu kuhusu maumivu yake, anakwambia pia jinsi ya kutengeneza bidhaa/huduma itakayomfaa pamoja na biashara yenye ubora. Huduma kwa wateja zinatakiwa kubuniwa katika namna inayotambua changamoto hizo.” Anasema Kristin Smaby katika mtandao wa https://alistapart.com.

Huwezi kupata wateja watakaoridhika na bidhaa/huduma zako milele. Hivyo yakubidi kama mfanyabiashara kuzitafuta changamoto zinazowakabili wateja wako kwa; kuzungumza nao, waulize maswali kuhusu vile wanataka kujiskia ukiwahudumia, wape msaada pale watakapohitaji, wape ofa, punguzo la bei na mambo kama hayo. Utakapowahudumia vizuri wateja wako utakidhi mahitaji ya wote; biashara yako na wateja pia. Wao wanapata huduma bora, biashara inapata mapato na kila mmoja anabaki na furaha.

Njia bora zaidi ya kuhakikisha unazipata changamoto zinazowakabili wateja wako ni Kwa kutumia vizuri mitandao ya kijamii. Mitandao ya kijamii ni kiungo muhimu sana cha kuunganisha mfanyabiashara na wateja wake katika kuimarisha viwango vya utaoji huduma. Sasa unawezaje kuitumia mitando hii kwa usahihi? Tafadhali fuatana na link hii hapa.

Ni matumaini yangu leo umefahamu kwa undani umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja. Utakwenda kuzitumia vipi mbinu hizi za leo? Niambie kwenye comment hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo kuhusu umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu(website design, logo design, Digital consultacy n.k) BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

FAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA HABARI NA BURUDANI

Baada ya zaidi ya miaka 10 tangu vuguvugu la mapinduzi ya kidijitali lilipoanza kushika kasi barani Africa, sekta ya Habari na Burudani ambayo inawavutia vijana wengi zaidi kwa sasa imeingia katika ukurasa mpya ambapo sasa sekta ya habari imekuwa ikiendeshwa kwa msaada wa teknolojia kwa kiasi kikubwa sana. Leo sasa, uta fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani. Kuna nini humo? Makinika mpaka mwisho..

Sekta hii iliyogawanyika kwenye maeneo kama Matumizi ya IntanetiTelevisheni, Sinema, Video Games, MagazetiMajaridaVitabuMuzikiRedio na kadhalika imechagizwa sana na mapinduzi yasiyozuilika ya Intaneti barani Afrika ambapo matumizi ya simu za rununu yamejenga msingi imara kama chanzo cha maboresho, ubunifu na mapato katika sekta hii.

Changamoto; Je, Teknolojia inabadili vipi sekta hii maarufu ya Habari na Burudani barani Africa?

Kwenye makala hii tutagusia changamoto chache zinazosibibu sekta hii maarufu kabisa. Lakini kwa undani zaidi wa changamoto hizo pamoja na jinsi ya kupambana nazo, tips, ofa mbalimbali na ushauri huwa tunashare kupitia status zetu za WhatsApp, utaipata kwa kugusa namba yeu hii hapa 0765834754. Make sure umeisave kisha nitumie text yenye jina lako ili uanze kufaidi elimu ya BURE kabisa.

Makampuni, Wafanyabiashara, Wasanii na Mashirika ya serikali wanatilia mkazo katika kubuni huduma na bidhaa bora kila siku katika kuboresha utendaji wa sekta hii maarufu na inayopendwa zaidi na vijana barani Afrika ambapo tukianzia nchini Kenya sekta hii ilionyesha ukuaji wa 17.0% katika mwaka 2017, ukuaji ukichagizwa na maendeleo makubwa katika eneo la Matumizi ya Intaneti.

Vile vile ongezeko la watu katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) cha 11.6 litaipaisha sekta hii mpaka kufikia pato la dola za Kimarekani bilioni 2.9 kufikia mwaka 2022 kutoka $ 1.7 bilioni zilizorekodiwa mwaka 2017. Karibu wateja wapya milioni 15 wanatarajiwa kuwa mtandaoni ndani ya miaka 4 ijayo, na zaidi kunatarajiwa kuwepo kwa huduma za kasi ya juu za intaneti.

Katika huduma za kifedha; MPESA imerahisisha sana malipo ya bidhaa/huduma mbalimbali nchi kenya na hivyo kufanya sekta ya Habari na Burudani kuzidi kuimarika.

fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

Huduma za Televisheni; Kenya ni moja ya nchi mwanzo barani kufanikiwa kuhamia katika mfumo wa kidijitali ambao umefungua fursa nyingi zikiwemo huduma za televisheni na utengenezwaji wa mawaidha kidijitali. Hali hii imeibua ushindani mkubwa katika eneo hili ambao unazidi kupeleka mbele na kunogesha maendeleo ya sekta hii ya Habari na burudani.

Kwa kuongezea ujio wa makampuni kama Kwese TV na Startimes ambayo hutoza kiwango kidogo zaidi cha malipo ya huduma zao kwa mwezi, kumeongeza ushindani kwa kiasi kikubwa dhidi ya kampuni kongwe ya Multichoice katika utoaji wa maudhui ya televisheni nchini Kenya.

Redio; ongezeko la huduma na vifurushi katika mashirika ya Redio unakuza kwa kiasi kikubwa sekta hii ambavyo hutoa matangazo ya biashara mbalimbali mtandaoni na katika magazeti. Redio nyingi sasa zinalazimika kuhamia katika mtindo wa mobile applications ili kuwafikia watu wengi zaidi na kuongeza wigo wa mapato yao.

TANZANIA:

Sekta hii ya Habari na Burudani inakuwa kwa kasi sana nchini humo ambapo kwa mwaka 2017 sekta hio iliingiza pato la dola za kimarekani milioni 496 ukiwa ni ukuaji wa 28.2% kwa mwaka. Ongezeko la watu kwa kiwango cha CAGR cha 18.3% utashuhudia mapato ya sekta hio kufikia $1.1 bilioni mwaka hadi mwaka 2022 ambayo ni mara 2.3 zaidi kulinganisha na ilivyorekodiwa mwaka 2017.

Kiujumla ni Nigeria peke yake katika Africa ndio imeizidi Tanzania katika kasi ya ukuaji wa sekta hii ya Habari na Burudani. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Kimataifa la PwC. (Wabongo mnatisha kwa habari na bata 😂).

Internet; Kitakwimu kunatagemewa ongezeko la watumiaji wa huduma za 4G ambapo makampuni ya Vodacom na Zantel tayari yalishazindua huduma zao za 4G LTE tangu robo ya pili ya mwaka 2016. Mwaka 2017 TIGO walitangaza uwekezaji wa $70 million ili kutanua wigo wake wa kimtandao na kujiandaa na matumizi ya kasi ya 5G. Hata hivyo mpaka kufikia mwaka 2022, huduma ya kasi ya intaneti ya 3G bado itaendelea kutumika zaidi kufikia takribani 70% ya watumiaji.

Televisheni; matumizi ya huduma za ving’amuzi na televisheni yatapaa kutoka watumiaji 200,000 waliorekodiwa mwaka 2013 mpaka watumiaji 900,000 kufikia mwaka 2022 kwa huduma za televisheni za majumbani. Watumiaji wengi pia hutumia huduma za ving’amuzi kutoka kwa makampuni ya Multichoice na Startimes.

Magazeti; Ukiachana na matumizi ya intaneti yanayoshika kasi nchini Tanzania. Magazeti pia yanaongeza chachu katika uboreshaji wa sekta hii ya habari na burudani ambapo matumizi rasmi ya lugha za Kiswahili na Kiingereza yamekuwa nguzo muhimu.

Lakini kwa Tanzania nyanja ya magazeti inakwenda ikibadilika kwa kasi, kwa mfano kampuni ya Vodacom imebuni application ya M-Paper ambayo imewezesha kupatikana kwa vichwa vya habari vya magazeti maarufu zaidi nchini na hivyo kufanya upatikanaji wa habari kuwa mkubwa zaidi.

Ikiwa na jumla ya mapatoyaliyotokana na matangazo kufikia dola za kimarekani milioni 91 katika mwaka 2017 na kutabiriwa kufikia $128 milioni mwaka 2022, ni dhahiri sekta ya habari na burudani inakuwa sawia nchini humo na hivyo kuchipusha milango mingi ya kibiashara kuendelea kufanyika.

AFRIKA KUSINI:

Ongezeko la watu katika nchi hii linatajwa kuwa imara kwa kiwango cha CAGR cha 7.6% kwa mapato ya watumiaji wa sekta hii ya habari na burudani kufikia mwaka 2022 ambapo mapato yatapaa kutoka Randi 93.9 bilioni zilizorekodiwa mwaka 2017 mpaka kufikia Randi 135.7 biloni mwaka 2022.

Ukiachana na mapato yanayotokana na matumizi ya Intaneti (ambayo huchagizwa na mapato yatokanayo na applications za simujanja) kuna uwanja mkubwa zaidi wa mapato ambayo huongozwa na michezo ya video (video games). Mapato kutoka kwenye michezo hii nchini SouthAfrica yanazidi maeneo mengine kama vitabu, Business-to-business (B2B) na mauzo ya majarida. Ukuaji huu katika eneo la michezo ya Video umekolezwa na ongezeko la matumizi ya simujanja, uboreshwaji wa huduma za kasi ya intaneti kutoka 3G mpaka 4G kuzidi kuongezeka jambo ambalo linaifanya watumiaji wa Afrika Kusini kuwa ni wacheza games 😁.

Televisheni; Kama ilivyotegemewa, huduma za TV na Video zitaendelea kuongoza katika kuzalisha mapato ya watumiaji, lakini muda mchache ujao Kampuni kama Netflix na Amazon Prime huduma zao zitachukuliwa kama nyongeza kunyongea kwa maudhui yao ya burudani katika soko la Afrika Kusini. Vile vile malipo ta TV yataongeza Randi bilioni 6 mpaka kufikia mwaka 2022 kwa kiwango cha 5% ya CAGR japokuwa ukuaji wa mwaka-kwa-mwaka unategemewa kuoungua kwa 2.6%.

Matangazo; nyanja hii iliathiriwa zaidi katika mwaka 2017 na mazingira ya uchumi wa Afrika Kusini ambapo kulikuwa na ukuaji wa tahadhari wa 2.1% tu mwaka kwa mwaka. Hata hivyo, maboresho yanategemewa mpaka kufikia mwaka 2022, ikiwa na 3.3% ya CAGR ambayo itapaisha mapato zaidi.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.Umejifunza nini leo kwenye ku fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

Makala hizi hapa zitakupa taarifa zaidi kuhusu Teknolojia ya Habari na Burudani katika biashara yako:

  1. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BANDO LAKO NI MTAJI
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Karibu sana REDNET TECHNOLOGIES

KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?

Iwe ni shirika binafsi, taasisi za uma(serikali), mashirika ya dini au biashara binafsi, matangazo ni muhimu sana katika maisha ya taasisi au biashara binafsi. Kutuma barua pepe, kuanzisha kurasa katika mitandao ya kijamii au kufikisha taarifa za ana kwa ana kwa uma ni bure (haijumuishi gharama za moja kwa moja). Lakini kutangaza biashara ni gharama zaidi, hata hivyo inakulazimu kuitangaza biashara yako. Makampuni na mashirika duniani hutumia gharama kubwa sana katika kujitangaza japokuwa tayari wana majina makubwa na bidhaa/huduma zao zinajulikana duniani kote. Sasa swali la msingi, kwanini uitangaze biashara yako? Makinika hapa leo kupata majawabu.

Coca cola Company kwa mfano, mwaka 2015 walitumia dola bilioni 3.96, 2016-dola bilioni 4, 2017-dola bilioni 3.96. Kwa upande mwingine Pepsi ambao ni mpinzani wa kibiashara wa Coca cola duniani wao mwaka 2015 walitumia dola bilioni 2.4 kufanya matangazo yao, mwaka 2016- dola bilioni 2.5, mwaka 2017 dola bilioni 2.4. Hii ni kwa mujibu wa tovuti ya Investopedia (http://www.investopedia.com). Sasa, jiulize Kwanini ni muhimu uitangaze biashara yako.!?

1. MASOKO: Katika muktadha wa ulimwengu wa kibiashara, masoko ndiyo moyo wa biashara haswa. Yaani ili biashara yoyote iweze kuendelea kufanya vizuri, haina budi kuwa na soko la kutosha la kuhudumia. Jiulize, bidhaa unazosambaza/unazouza au huduma unayotoa, kuna kampuni au biashara ngapi ambazo zinafanya kitu hicho hicho unachokifanya.!? Kama hauko peke yako, basi hauna budi kutafuta masoko kwa hali na mali ili biashara yako ipate hadhira ya kuhudumia.

2. KUTAMBULISHA BIDHAA/HUDUMA MPYA: Ukuaji wa biashara/kampuni au taasisi yako hujumuisha kwa kiasi kikubwa ubunifu kila siku. Sehemu ya ubunifu huo pia huchagiza utambulisho wa huduma/bidhaa mpya kwa wateja wako. Ili uweze kuwafikishia taarifa wateja wako kuhusu huduma/bidhaa mpya unayoongeza katika biashara/kampuni au taasisi yako, unalazimika kuitangaza huduma/bidhaa hio mpya ili ifike kwa urahisi na usahihi kwa wateja wako.

3. ELIMU KUHUSU BIDHAA/HUDUMA ZITOLEWAZO NA TAASISI:Taasisi yako inapotoa huduma/bidhaa zake kwa mlaji wa mwisho au mteja wako hujumuisha zaidi sana elimu ya jinsi ya kutumia bidhaa/huduma hio. Sio watu wote watajua jinsi au njia za kuipata na kutumia kwa usahihi bidhaa/huduma zinazotolewa na taasisi yako. Vile vile ili elimu hio kuhusu bidhaa/huduma zako ipate kufika kwa mlaji wa mwisho au mteja wako huna budi kufanya tangazo. Hivyo matangazo ya namna hii yenye lengo la kutoa elimu ni muhimu sana katika kuhakikisha huduma/bidhaa zako zinafika kwa wateja lakini zaidi zinatumika kwa usahihi ule unaohitajika.

4.KUTENGENEZA MVUTO WA KIBIASHARA:

Matangazo ni njia bora zaidi kutengeneza mvuto wa kibiashara. Hapa kuna namna nyingi sana katika kutengeneza mvuto huu wa kibiashara kwa kutumia teknolojia ya matangazo. Aina ya mavazi au sare zinazohimizwa kuvaliwa katika taasisi yako, muundo wa rangi rasmi za taasisi, logo ya taasisi pamoja na jina la taasisi linavyohusiana na aina ya bidhaa/taasisi inayotolewa. Mvuto huu wa kibiashara hufanya matangazo ya kiautomatiki yanayokwenda moja kwa moja katika maisha ya kila siku ya mlaji wa mwisho au mteja. Huku mtandaoni tunatumia teknolojia ya SEO kutengeneza mvuto huu. Sasa kufahamu zaidi kuhusu SEO fuatana na makala hii hapa;

5. KUKUZA JINA LA KAMPUNI DUNIANI:

Matangazo ni sauti ya taasisi kuhusu bidhaa/huduma zake kwa wateja wao. Hivyo taasisi inavyofanya matangazo ndivyo inavyozidi kujiongezea wigo wa sauti yake kufika duniani kote. Duniani kuna kadiriwa kuwa na watu zaidi ya bilioni 7, hivyo unapofanya tangazo moja ni ngumu sana kuwafikia watu wote hao zaidi ya bilioni 7 duniani. Hivyo unapofanya matangazo kwa ajili ya wateja wako duniani mara kwa mara, unaimarisha jina la kampuni kitu ambacho huimarisha bidhaa/huduma zako zaidi pia.

6. KUJIKITA KWA WATEJA MAALUM TAASISI INAYODHAMIRIA KUWAPATA:

Kwa kawaida unapojihusisha na biashara ya kuuza nguo kama taasisi, wateja wako wakubwa watakuwa ni wauzaji wa nguo wadogo wadogo, wanamitindo na watu wengine wanaopenda kuvaa nguo za aina mbali mbali kila siku. Hivyo unapofanya matangazo ya taasisi yako, unajiweka kwenye nafasi ya kuwapata wateja haswa wale ambao taasisi imedhamiria kuwafikia.

7. UWEZO WA TAASISI KUHUDUMU:

Kwa kiasi kikubwa matangazo huimarisha uwezo wa taasisi kuhudumu. Hivyo taasisi yako inapofanya matangazo inajiweka kwenye nafasi ya kujiweka tayari kuhudumu kwa wateja wale wote wanaoletwa na matangazo hayo. Hivyo taasisi inayofanya matangazo hujiweka kwenye nafasi ya kuwa na ufanisi zaidi kwenye utendaji wake wa kila siku.

Hivyo kwa ufupi hayo ni baadhi ya mambo muhimu kuhusu Umuhimu wa Ufanyaji wa Matangazo katika taasisi/kampuni au biashara yako. Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi tukupatie usaidizi pale unapohisi kukwama katika biashara zako katika muktadha wa teknolojia ya habari na mawasiliano.

Namna bora ya kuitangaza biashara yako ni kupitia matumizi ya tovuti rasmi ya biashara yako pamoja na matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii ili kuhakikisha biashara yako inabaki katika akili za wateja wako kila siku. Hivyo pitia makala kupitia links hizo hapo chini ili uzidi kufahamu mambo muhimu kwa ajili ya afya ya biashara yako.

  1. https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “KWANINI NI MUHIMU KUWA NA TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/website-inasaidia-vipi-kuimarisha-biashara-yako/ yenye kichwa “WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?” 
  3. https://rednet.co.tz/ifahamu-nguvu-ya-mitandao-ya-kijamii-katika-biashara-yako/ yenye kichwa “IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO”

Una maoni au lolote kuhusu makala hii ya leo? Tafadhali, acha comment yako hapo chini na changia hoja yako. Karibu sana.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uitangaze biashara yako?