Tag: kilimo na teknolojia

MFUMO WA KUWEZESHA MALIPO BARANI AFRIKA (PAPSS)

Umeshawahi kuwaza kufanya biashara na wafanyabiashara wenzako na wateja kutoka nchi yoyote barani Afrika ambapo utaweza kutuma na kupokea fedha bila ya ulazima wa kubadili ziwe za kigeni kwanza? Sasa mfumo wa Kuwezesha malipo barani Afrika(PAPPS) unakwenda kukurahisishia mjasiriamali uwezo wa kutuma na kupokea fedha katika bidhaa/huduma unazotoa kila siku kirahisi zaidi. Leo nakupa fursa ya kufahamu namna mambo yamekuwa mazuri kibiashara barani Afrika. Fuatana nami mpaka mwisho wa makala hii..

Kwetu Moshi bwana ikifika mwezi February mpaka June kila mwaka huwa ni msimu wa parachichi na ndizi ambapo watu huuza sana parachichi ndani na nje ya nchi. Najua umeshawahi kuonja parachichi za Rombo, Marangu, Mwika, Machame nk, right?

Sasa bwana hizo parachichi unazokula ni 20% tu ya parachichi zote zinazovunwa kwenye miteremko ya mlima Kilimanjaro. Zaidi ya 80% ya parachichi hizo huuzwa nchini Kenya na kisha kusafirishwa kwenye barani Ulaya na Asia kupitia bandari ya Mombasa.

Bahati mbaya zaidi pale mpakani Holili kuna madalali wengi sana ambao hununua parachichi kutoka kwa wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali na kuziingiza nchini Kenya. Hawa jamaa bwana wajanja sana. Wao tayari wana vibali vya kuingia na kufanya biashara kati ya Tanzania na Kenya na zaidi wanafanya pia biashara ya kubadilisha fedha hapo mpakani (japo sina uhakika kama wanafanya hivyo kihalali). Kwa kufanya hivyo hawa Madalali wamekuwa wakijipatia faida kubwa sana hapo mpakani japo kuwa wao hawana mashamba wala parachichi zenyewe. Wao wanaconnect dots tu.

Na bahati mbaya zaidi wafanyabiashara wengi wadogo hawawezi kuvuka mpaka wakakutana na wateja wenyewe huko Kenya na kuuza bidhaa zao direct. So unaweza kuona namna hawa ndugu zangu wanapata tabu kufanikiwa kwenye biashara yao japokuwa wao ndo wanamzigo wote wa parachichi.

Huu ni mfano mdogo tu unaowakuta wafanyabiashara ambao wanauza bidhaa/huduma zao nje ya nchi. Hali hio pia inawakumba wale wa Tunduma, Rusumo, Taveta na maeneo mengine ya mpakani ambapo madalali (watu wa kati) wamekuwa wakitumia fursa hio kujinufaisha zaidi kuliko wakulima.

Kupitia changamoto kama hizo ndio maana nchi wanachama wa AU wakaanzisha Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA) ili kuhakikisha biashara baina ya nchi wanachama zinafanyika kirahisi, tena bila vikwazo kama kodi na ushuru wa mipakani ambayo imekuwa ikiwaumiza wafanyabiashara.

Kuhusu AfCFTA ni nini na inafanya kazi vipi? tayari nimekuandalia makala murua kabisa kupitia link hii hapa chini:

Ukimalizana na makala hio sasa, tuendelee..

Pia nchi za kusini mwa Afrika kufikia July 2020 zikakubaliana kurasinisha biashara zao ili kuwezesha mazingira ya biashara baina ya nchi wanachama wa SADC kufanya biashara bila mrundikano wa kodi na ushuru. Hapa Prof. Kabudi (waziri wa mambo ya nje) na timu yake walicheza sana.

Kuhusu URASINISHAJI huo wa Kibiashara, ni nini na unafanyika vipi, tayari kuna makala yako kupitia link hii hapa:

Kuna mengi sana ya kujifunza hapo kwenye hio makala hapo.

Lakini licha ya yote hayo, mtaani mambo bado ni magumu kwa wakulima na wafanyabiashara wadogo, kwanini? Kwa sababu taarifa za miamala bado zimetekwa na madalali. Wao ndo wanazuia bidhaa zote pale mpaka na kuzivusha na kufanya biashara nje ya nchi.

Hali hio bado inawatengenezea faida kubwa sana madalali hao na kuwaacha kwenye mataa wakulima na wafanyabiashara wadogo ambao kimsingi ndo wenye mali halisi.

SASA NINI KIFANYIKE ILI KUWEZESHA MALIPO KWA URAHISI?

Wakiwa wanajiuliza serikali, jumuiya za kimataifa na mashirika ya ndani na nje ya nchi, Shirika la African Export-Import Bank (Afreximbank) wakaja na suluhu ambayo inakwenda kumtingisha bwana Dalali na kumtengenezea mazingira mazuri ya kufaidika ndugu Mkulima na mfanyabiashara mdogo. Suluhu hio ni Mfumo wa Kuwezesha Malipo barani Afrika waliouita PAPPS.

Mfumo huu wa PAPSS (Pan-African Payment and Settlement System) ulizinduliwa rasmi tarehe 13 January 2022 katika hafla iliyofanyika nchini Ghana. Kabla ya hapo, mfumo huo ulikua kwenye majaribio tangu mwaka jana 2021 huku ukiwa unatumika ndani ya nchi 6 za Afrika Magharibi. Mtandao wa ICLG unatujuza kwamba mfumo huu unakwenda kuokoa dola bilioni 5 kwa mwaka ambazo hupotea kama makato mbalimbali katika malipo ya kibiashara baina ya wafanyabiashara wa nchi moja na nyingine.

Pia imefahamika kwamba zaidi ya 80% ya miamala inayofanyika maeneo ya mipakani ambayo ilihitaji mifumo ya kimataifa ya kulipa na kubadili fedha, sasa inakwenda kuokolewa na mfumo huu. Imagine wakulima na wafanyabiashara tunavokwenda kunufaika hapa.

UNAJIUNGA VIPI NA MFUMO HUO WA KUWEZESHA MALIPO?

Mfanyabiashara, mteja, mshiriki na mamlaka za serikali ambaye anahitaji kunufaika na mfumo huu kwa sasa anahitajika kujisajili kupitia link hii http://papps.com/connect/ kisha fuata maelekezo.

Changamoto iliyopo ni kwamba mfumo huu bado haujasambaa vya kutosha kiasi cha kuzama katika matumizi ya kila siku ya kibiashara. Hali hio inawalazimu waandaaji kupambana katika kushirikiana na Taasisi za Fedha na Serikali za Mataifa ya Afrika ili kujenga msingi imara wa matumizi.

Mbeleni wafanyabiashara tutaweza kutuma na kupokea fedha ndani ya Jumuiya zetu za kikanda na bara zima kupitia Miundombinu hii ambayo inazidi kuboreshwa katika kutafuta fursa za biashara na maendeleo ya kiuchumi.

Kwa fursa za biashara zinavyofunguka kupitia #AfCFTA pamoja #Urasinishaji unaofanyika katika Jumuiya za Maendeleo (SADC, EAC, COMESA etc) ni wazi mfumo huu wa PAPPS unakwenda kuwezesha malipo yaweze kufanyika kwa haraka na ufanisi wa hali ya juu sana. Hapa hutakiwi kubaki nyuma kabisa ndugu yangu.

NITAIFAIDI VIPI SASA HIO PAPSS NIKIWA MJINI?

Kwanza fahamu mfumo huu ni wa Kimtandao, hivyo, ukiwa popote unaweza kufanya biashara na mteja hasa kupitia ecommerce website yako au Digital Tools zingine kama Instagram, Twita na Whatsapp.

Kufahamu zaidi gusa tweet yetu hii hapa chini

Uzuri wa kuwa na e-commerce website unakuja hapa. Mteja akiwa nchi X anaiona bidhaa kwenye website yako, alipia, kisha wewe mjasiriamali unafanya delivery kupitia Gari, Ndege au Meli na bidhaa inamfikia vema.

Kuna OFA hapa kwa ajili yako. Wasiliana nasi mara moja kuipata:

Umeshawahi kufanya biashara na wateja/wadau walio nje ya nchi yako lakini ndani ya Afrika? Ulipata changamoto gani? Na umejifunza nini? Tushirikishe uzoefu wako kwenye comments Kwa sababu kuna mdau angependa kufahamu kinachoendelea huko nje ya nchi kibiashara, right?

Mfumo huu wa PAPSS unakuja kuleta ushindani katika Kampuni na Mashirika yanayofanya biashara ya fedha kiteknolojia (Fintech) barani Afrika.

Ukiwa kama Mjasiriamali na mdau wa Tech, umejipangaje na ujio wa mfumo huu? Weka majibu na mawazo yako kwenye comments hapo chini.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

MPESA LIPA NAMBA YETU
Archiedee Co limited

UMUHIMU WA TEKNOLOJIA BORA KATIKA KILIMO

Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) mpaka mwaka 2050 watu wataongezeka mpaka kufikia bilioni 9.1 na kulisha namba hii ya watu, uzalishaji wa chakula duniani utahitajika kukuwa kwa 70% angalau. Kwa Afrika ambayo inatarajiwa kuwa na jumla ya watu bilioni 2 kufikia 2050, uzalishaji wa chakula kupitia sekta ya kilimo inabidi ukue haraka zaidi ya wastani wa dunia ili kupunguza dalili za baa la njaa. Sasa leo tuangazie umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo. Teknolojia ina mchango gani? Makinika mpaka mwisho wa makala hii kufahamu.

Mpaka nyakati hizi bado sekta ya kilimo inakumbwa na majanga ambayo hayajapatiwa suluhu ya kudumu kama kudhoofu maendeleo maeneo ya vijijini ambapo kilimo ndipo hufanyika kwa kiasi kikubwa, kutokuwa na soko mbadala kwa mazao yatokanayo na kilimo, miundombinu mibovu, vita vya wenyewe kwa wenyewe, magonjwa kama UKIMWI, majanga ya kiasili pamoja na ukataji ovyo wa misitu.

Sasa katika zama hizi za Kidijitali, Teknolojia ina mchango gani katika kukuza sekta ya kilimo na kuboresha uchumi wa mkulima?

Simu za rununu (smartphones), mfumo wa GPS, vifaa vya RFID na barcode scanners ni baadhi ya vifaa vinavyotumika katika sekta ya kilimo katika juhudi za kuboresha uzalishaji ambapo picha za satelaiti kwa mfano, huweza kutumika kupima ukubwa wa eneo sahihi la kufanyia shughuli za kilimo kwa ubora wa hali ya juu. Vile vile vifaa maalum vinavyoweza kuhisi hali ya udongo (soil sensors) hutumika kujua ni aina gani ya mazao inafaa kulimwa kuendana na udongo wa mahala husika. Zaidi mamlaka za hali ya Hewa pia hutoa mrejesho bora kuhusu utabiri wa hali ya hewa kwa kutumia vifaa vya kisasa na teknolojia bora kwenye vipimo vyao.

Ugunduzi wa Programu za kompyuta na Applications za simu unaongeza chachu zaidi katika kufanya kilimo cha kisasa na kudhibiti taarifa muhimu katika utendaji wa hatua kwa hatua, kufanya miamala ya kifedha pamoja na kutafuta masoko. Applications maalum ziitwazo Mobile App for Agriculture and Rural Development (m-ARD) hutumika kwa usahihi katika kufanya miamala na kudhibiti maswala ya kifedha katika ufanyaji wa kilimo. Kupitia MPESA nchini Kenya, taasisi ya kilimo ya Kilimo Salama Agriculture Insurance imeongeza thamani ya bidhaa za wakulima kwa wastani wa 50% kwa bidhaa za kilimo, sawa na $150 kwa mwaka.

CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.
Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) mpaka mwaka 2050 watu wataongezeka mpaka kufikia bilioni 9.1 na kulisha namba hii ya watu, uzalishaji wa chakula duniani utahitajika kukuwa kwa 70% angalau. Kwa Afrika ambayo inatarajiwa kuwa na jumla ya watu bilioni 2 kufikia 2050, uzalishaji wa chakula kupitia sekta ya kilimo inabidi ukue haraka zaidi ya wastani wa dunia ili kupunguza dalili za baa la njaa. Sasa leo tuangazie umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo. Teknolojia ina mchango gani? Makinika mpaka mwisho wa makala hii kufahamu.

Je, wajua kwamba takribani theluthi moja (1/3) ya mazao yote yanayovunwa duniani kwa mwaka hupotea kwa kushambuliwa na wadudu waharibifu, magugu na magonjwa?

Sasa kwa kuligundua hili wataalam walibuni mbegu maalum katika maabara za kisayansi kwa kuboresha vinasaba (DNA) Za mazao na kufanikiwa kupata kitu walichoita Genetic Modified Organism (GMO). Kitaalam mbegu na mimea itokanayo na GMO imekuwa na faida nyingi katika kilimo zikiwemo; kuwa na uhakika wa kupata mazao mengi kwa kutumia mbegu kidogo tu. Vilevile GMO hizi zimetengenezwa zikiwa na ustahimilivu dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa jambo linalozipa uhakika wa kukuwa, kumea na kuzaa ipasavyo. Hata hivyo kinga hio dhidi ya wadudu waharibifu haiwazuii wadudu kama nyuki, vipepeo, minyoo wa ardhini na baadhi ya bakteria ambao huwa na jukumu muhimu katika uchavushaji wa mimea na hivyo kuleta mazao stahiki. Faida zingine ni kutunza na kuboresha rutuba ya udongo pamoja na kusaidia kuhifadhi maji ardhini, mambo ambayo yanaondoa hatari ya kutokea kwa baa la njaa duniani lakini zaidi, kuboresha uchumi wa mkulima.

Je unaamini kwamba wingi ni Faida?

Sasa majibu ya wataalam wa maswala ya kilimo duniani ni kwamba si mara zote wingi unaweza kuleta faida. Hii inajidhihirisha katika matumizi ya mbolea zinazotengenezwa maabara kiteknolojia katika kufanya kilimo ambapo kiasi kikubwa cha mbolea huweza kupelekea kudhoofisha mimea na kutishia kufifia kwa mazao kutokana na mlundikano wa kemikali zilizopo kwenye mbolea ambazo zikizidishwa ni hatari. Hivyo inashauriwa mbolea inayotumika iendane sawia na aina ya udongo, kiasi cha maji katika umwagiliaji na aina ya mazao yanayolimwa ili kuhakikisha mazao yanayotoka yanakuwa bora zaidi. Hata hivyo taarifa nyingi kuhusu matumizi ya mbolea za kisasa hupatikana kupitia applications za simu mahsusi kwa shughuli za kilimo ziitwazo m-ARD’s.

Shirika la maswala ya kilimo la M-Farmer Initiative Fund lilianzishwa mwaka 2011 kwa ushirikiano wa Mfuko wa hifadhi ya jamii wa Bill and Melinda Gates Foundation ili kuratibu, kufadhili na kukuza sekta ya kilimo barani Afrika. Shirika hili limepanga kufikia wakulima walioko katika nchi za Ethiopia, Malawi, Rwanda, Kenya, Zambia na Tanzania.

Hilo ni mojawapo la mashirika makubwa kuonyesha nia ya dhati katika kuendeleza shughuli za kilimo duniani, kuchochea umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo na kupunguza baa la njaa, kuboresha biashara za mazao ya kilimo pamoja na kukuza uchumi wa mkulima mmoja mmoja. Mashirika hayo yanazindua mifumo ya kimtandao ya malipo, mikopo na bima za kidijitali. Kwa mfano shirika la FarmDrive la nchini Kenya limezindua huduma za kifedha mahsusi kwa ajili ya wakulima ambapo kupitia shirika hilo wakulima hata wasio na akaunti za benki na wakulima wadogo kabisa hupata mikopo huku ikisaidia taasisi za kifedha kuongeza huduma za mikopo ya kilimo kwa gharama nafuu.

Kwa wafanyabiashara na kampuni zilipo ukanda wa Afrika Mashariki hii ni fursa kwao kuelekeza macho yao katika sekta ya kilimo kama inavyofanya FarmDrive nchini Kenya na shirika la kimataifa la M-Farmer.

Unalionaje hili? (tafadhali share kwenye comments) Hivyo kupitia jitihada za mashirika hayo, wakulima sasa wanaweza kupata mbolea, mbegu bora na mifumo mizuri ya umwagiliaji ili kukuza shughuli zao. Mchakato huo huboresha kasi ya uzalishaji katika kilimo na kupunguza changamoto kwa kutumia takwimu sahihi katika utendaji wa shughuli za kilimo kwa kutumia data za kisayansi na hivyo, umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo unazidi kuonekana. Kwa mfano matumizi ya vifaa vya umwagiliaji vinavyotumia nishati ya jua kusukuma maji kutoka katika chanzo chake kama mto, ziwa, bwawa au bahari. Vifaa hivi vimerahisisha sana swala zima la umwagiliaji.

Vilevile kwa kuzingatia ukweli kwamba mashamba mengi yapo maeneo ambayo ni mbali na huduma za mitandao ya simu na intaneti, hivyo kufanya huduma hizo kuwa hafifu, nchi kama Ethiopia imerusha satelaiti yake na kufanya wakulima kuwa katika nafasi nzuri kunufaika na mradi huo. Serikali za nchi zingine za Afrika Mashariki zinakwama wapi kwenye hili?

umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo.

matumizi ya TEHAMA katika Satellite

Hata hivyo zama hizi kutokana na kuimarika kwa miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji, pamoja na maendeleo katika sekta ya sayansi na teknolojia ya Habari na mawasiliano, imekuwa rahisi sana kupata taarifa kuhusu Hali ya Hewa, Hali ya soko na ushindani, mazingira ya miundombinu ya uchukuzi, mfumuko wa bei na uelekeo wa mahitaji ya wateja. Kilimo kimeja kufanyika katika namna rahisi sana katika kuuza mazao baada ya kuvuna, shukrani umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo cha kisasa na chenye tija.

Kufahamu zaidi namna unavyoweza kuimarisha shughuli zako za kilimo kwa kutumia teknolojia tafadhali pitia makala zilizomo kwenye links hizi hapa:

  1. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWUWEKEZA
  3. UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021