Tag: kenya

D.R.C NDANI YA E.A.C, MFANYABIASHARA ANAFAIDIKA VIPI?

Hatimaye tar29 March Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ilipata kibali cha kuwa mwanajumuiya wa Afrika Mashariki (EAC) na mwezi July mwaka huo 2022 DRC iliingia rasmi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuwasilisha matakwa yote makao makuu ya jumuiya hio jijini Arusha. Hii ni baada ya kuendesha mchakato uliodumu kwa takriban miaka minne. Sasa DRC inapoingia ndani ya EAC mfanyabiashara anafaidika vipi?

DRC inakuwa mwanachama namba 7 wa EAC huku ikiwa ndio nchi kubwa zaidi kijiografia katika ukanda huo. Inasemekana DRC ndio nchi yenye rasilimali (madini, mafuta, misitu n.k) nyingi zaidi duniani. Pia nchi hio ina idadi ya watu takribani milioni 90 ambao ni mtaji muhimu kiuchumi.

MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU D.R.C:

Kukubalika kwa DRC kunamaanisha kwamba soko la Afrika Mashariki linatanuka na kuwafikia watu zaidi ya milioni 300 waishio ndani ya jumuiya hio tu, huku uchumi wa jumla ukiwa na thamani ya 250$ bilioni. Sasa DRC ina nini cha ziada usichokijua?

1. MIPAKA YA KIJIOGRAFIA:

Ikiwa ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa jiografia barani, DRC inapakana na nchi zingine 9. Nchi hizo ni Angola, Burundi, Jumhuri ya Afrika ya Kati, Rwanda, Jamhuri ya Congo (Brazaville), Sudani Kusini, Uganda, Zambia na Tanzania. Muingiliano wa kibiashara ni mkubwa sana hapa.

Zaidi upande wa magharibi mwa jiji la Kinshasha inapakana na bahari ya Atlantiki. Sasa Kongo kupakana na nchi 9 na kuwa na ufukwe wa bahari ya Atlantiki kunaifanya iweze kutanua fursa kwa wafanyabiashara kupitisha mali kwenda nchi nyingi zaidi barani na hata nje ya bara.

DRC na mipaka yake. Milango ya biashara za kimataifa kwa EAC.

2. KUHUSU VIVUTIO VYA UTALII:

Mbuga ya wanyama kongwe zaidi barani ipo DRC, inaitwa Virunga. Hapo utawakuta wale Sokwe wakubwa (Gorillas), simba na tembo. Lakini mbuga hii ipo kwnye tishio la kutoweka kwa sababu kuna mafuta na kampuni ya Uingereza ya Soco tayari imetia timu kuanza kuchimba mafuta hapo mbugani.

Hawa gorilla ni kivutio kizuri sana cha utalii lakini miaka ya hivi karibuni wamekuwa adimu na kutokana na shughuli za mwanadamu, wanyama hawa wapo kwnye tishio la kutoweka kabisa. Je, DRC kuingia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kutadhibiti hatari ya sokwe hawa kutoweka?

Kuhusu namna utalii unaweza kuleta manufaa katika biashara tafadhali fuatana na makala hii hapa chini:

3. KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NA MIUNDOMBINU:

Ni 1.8% tu ya barabara nchini DRC ndio ina kiwango cha lami, huku chini ya 10% ya nyumba za makazi ndio zina umeme. Hii ni hali mbaya sana katika kukuza uchumi wa Taifa. Hata hivyo Benki ya Dunia imetangaza kifurushi za 1$ bilioni kwa ajili ya miundombinu ya DRC.

Moja kati ya vitu vinavyorudisha nyuma juhudi za wajasiriamali na mashirika kuwekeza nchini DRC ni maendeleo duni ya miundombinu. Ukizingatia ukubwa wa nchi hio, imekuwa ni nafuu kusafiri kwa njia ya anga kuliko barabara. Sasa @jumuiya itachangia vipi maendeleo ya miundombinu?

4. BIASHARA ZA NJE YA NCHI (EXPORTS):

Muziki wa DRC ndio mali inayouzwa zaidi nje ya nchi (export). Kuanzia miaka ya 90 muziki wa Bolingo ndio ulikua unasikilizwa na kupendwa zaidi bara zima la Afrika. Ndio maana wasanii kama Fally Ipupa na Koffi Olomide ni matajiri sana. Madini na malighafi zingine zote chali.

5. LUGHA INAYOTUMIKA ZAIDI:

Jiji la Kinshasa ni la pili kwa matumizi ya lugha ya Kifaransa likitanguliwa na jiji la Paris. Yaani Wakongo hawa wanaongea kifaransa zaidi kuliko hata miji ya nchini Ufaransa. Hata hivyo hii inachangiwa na idadi ya watu wanaoishi kwenye jiji hilo, watu milioni 10 mchezo!

Ukiacha Kifaransa raia wa Kongo pia wanazungumza lugha zingine kama Kilingala, Kiingereza, Kiswahili na lugha za makabila asilia. Hivyo ukiwa kama mfanyabiashara na moja kati ya lugha tajwa unazifahamu vyema basi nafasi ni yako kuingia DRC na kutanua biashara zako.

6. KUHUSU UGONJWA WA EBOLA:

Kwamba kupata Ebola nchini DRC ni rahisi kama kupata mafua ukiwa sehemu nyingine? HAPANA. Baada ya ugonjwa huo kufumuka mwaka 1995 na kuua watu zaidi ya 200, milipuko mingine ya ugonjwa huo imekuwa ikidhibitiwa kwa kiwango kikubwa. Hivyo Congo ni salama.

7. KUHUSU MADINI:

Lile bomu la atomiki lililodondoshwa kwenye miji ya Hiroshima na Nagasaki katika WWII lilitengenezwa kwa madini ya Uranium kutoka mgodi wa Shinkolobwe, mkoani Katanga nchini DRC. Hata hivyo mgodi huo ulifungwa mwaka 2004 kutokana na kuishiwa madini ukiiacha DRC patupu.

Kongo imenyonywa sana katika madini yake. Hali kadhalika nchi zingine katika Jumuiya zimepitia hali hio. Hivyo itakapowekwa sera ya pamoja ya kulinda na kusimamia rasilimali zilizopo ndani ya Jumuiya, bila shaka madini na rasilimali ambazo zipo DRC zitakuwa na manufaa sana.

8. HISTORIA YA UNYONYAJI:

Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alijitangazia Kongo kuwa mali yake binafsi kuanzia mwaka 1870. Koloni hilo ndio lilikua mali binafsi kubwa zaidi kuwahi kumilikiwa na mtu mmoja kwenye historia. Umiliki huo ulisababisha vifo vya watu milioni10. Huu ndio mwanzo wa nchi kuharibika.

Mfalme Leopold II aliagiza watu kukusanya zao la mpira ambalo kwa kipindi hiko ndio lilikua zao bora zaidi la kibiashara. Wale walioshindwa kukusanya zao hilo kama kodi waliadhibiwa kwa kunyimwa chakula na kukatwa mikono yao. Ukatili huo ulikua mbaya sana dhidi ya ubinaadam.

9. HALI YA USALAMA NA VITA:

DRC imekuwa ikikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na migogoro isiyokwisha ambayo imepelekea vifo vya watu takriban milioni 6. Hali hio ya vita visivyokwisha imepewa jina la “Vita vya Dunia vya Afrika”.

Vita hivyo kwa sehemu kubwa vimekuwa vikisababishwa na vikundi fulani (kampuni, mashirika na raia wa kawaida) kugombania rasilimali katika eneo fulani. Huyu anataka kuchimba, raia wanataka kunufaika. Je, DRC kuingia kwenye @jumuiya itasaidia kumaliza janga la vita visivyokwisha?

10. KUHUSU MTO CONGO:

Ukiwa na urefu wa kilomita 4,700, mto Congo ndio mto mrefu wa pili barani Afrika ukitanguliwa na mto Nile. Pia huo ndio mto wenye kina kirefu zaidi duniani. Cha kufurahisha zaidi, Mto Congo na Mto Nile yote inapatikana katika EAC. Inakupa picha gani hii kiuchumi?

Je, EAC itaweza kuzalisha umeme wa pamoja kupitia sehemu za mto huo? Je shughuli za kiuchumi kama uvuvi, usafiri, utalii biashara ya mazao ya misitu zitaweza vipi kusimamiwa na Jumuiya kuhakikisha faida zinarudi kwa wanachi wa Kongo na wa jumuiya nzima kiujumla?

ZIADA: MSITU WA CONGO

Msitu wa pili kwa ukubwa duniani, msitu wa Congo unapatikana nchini DRC. Hata hivyo msitu huo ni mkubwa kiasi kwamba umeingia kwenye nchi zingine kama Cameroon, Jamhuri ya Afrika Ya Kati, Jamhuri ya Congo(Brazaville), Guinea ya Ikweta na Gabon. Msitu huu ni utajiri mtupu.

msitu wa mvua wa Congo
Msitu wa Congo

Katika msitu huo kuna fursa nyingi zikiwamo biashara ya magogo, madawa ya kutibu watu, mazao na wanyama, mbao, karatasi na bidhaa zote zitokanazo na misitu. Ukiwa kama mfanyabiashara ambaye sasa una uhuru wa kwenda kuwekeza DRC kirahisi, utaitumiaje fursa hii?

Sasa hayo ni baadhi ya mambo ambayo pengine ulikua huyafahamu kuhusu DRC. Mambo hayo kama yakifanyiwa kazi ipasavyo ndani ya @jumuiya basi ni wazi kutapunguza hali ya umasikini na kuimarisha amani kwa watu wa Kongo na kuimarisha uchumi wa Jumuiya nzima. Mapema mwaka 2021 jumuiya ya nchi za Afrika kwa kauli moja ilianzisha eneo huru la biashara barani (AfCFTA) ambapo nchi wanachama wanaweza kufanya biashara kwa uhuru bila ya vizuizi vya mipakani. Zaidi soma hapa chini

Jumuiya hii inatoa uhuru kwa wanachi wake kuishi na kufanya biashara popote ndani ya nchi wanachama. Jambo hili linatoa fursa kwa Wajasiriamali wa aina zote kuzurura na kutafuta masoko yao kirahisi. Ukiweza vema kutumia majukwaaa ya kimtandao kama websites, mitandao ya kijamii ujue unayo nafasi ya kuwafikia watu milioni 300 waishio ndani ya Afrika Mashariki. Sasa tuambie wewe mtu wa Teknolojia, website designer, mtaalam wa kutengeneza android app, mkulima, engineer nk, unataka ufaidike vipi hapa? Tuambie..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

M-PESA LIPA NAMBA
Archiedee Co limited

UMUHIMU WA TEKNOLOJIA BORA KATIKA KILIMO

Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) mpaka mwaka 2050 watu wataongezeka mpaka kufikia bilioni 9.1 na kulisha namba hii ya watu, uzalishaji wa chakula duniani utahitajika kukuwa kwa 70% angalau. Kwa Afrika ambayo inatarajiwa kuwa na jumla ya watu bilioni 2 kufikia 2050, uzalishaji wa chakula kupitia sekta ya kilimo inabidi ukue haraka zaidi ya wastani wa dunia ili kupunguza dalili za baa la njaa. Sasa leo tuangazie umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo. Teknolojia ina mchango gani? Makinika mpaka mwisho wa makala hii kufahamu.

Mpaka nyakati hizi bado sekta ya kilimo inakumbwa na majanga ambayo hayajapatiwa suluhu ya kudumu kama kudhoofu maendeleo maeneo ya vijijini ambapo kilimo ndipo hufanyika kwa kiasi kikubwa, kutokuwa na soko mbadala kwa mazao yatokanayo na kilimo, miundombinu mibovu, vita vya wenyewe kwa wenyewe, magonjwa kama UKIMWI, majanga ya kiasili pamoja na ukataji ovyo wa misitu.

Sasa katika zama hizi za Kidijitali, Teknolojia ina mchango gani katika kukuza sekta ya kilimo na kuboresha uchumi wa mkulima?

Simu za rununu (smartphones), mfumo wa GPS, vifaa vya RFID na barcode scanners ni baadhi ya vifaa vinavyotumika katika sekta ya kilimo katika juhudi za kuboresha uzalishaji ambapo picha za satelaiti kwa mfano, huweza kutumika kupima ukubwa wa eneo sahihi la kufanyia shughuli za kilimo kwa ubora wa hali ya juu. Vile vile vifaa maalum vinavyoweza kuhisi hali ya udongo (soil sensors) hutumika kujua ni aina gani ya mazao inafaa kulimwa kuendana na udongo wa mahala husika. Zaidi mamlaka za hali ya Hewa pia hutoa mrejesho bora kuhusu utabiri wa hali ya hewa kwa kutumia vifaa vya kisasa na teknolojia bora kwenye vipimo vyao.

Ugunduzi wa Programu za kompyuta na Applications za simu unaongeza chachu zaidi katika kufanya kilimo cha kisasa na kudhibiti taarifa muhimu katika utendaji wa hatua kwa hatua, kufanya miamala ya kifedha pamoja na kutafuta masoko. Applications maalum ziitwazo Mobile App for Agriculture and Rural Development (m-ARD) hutumika kwa usahihi katika kufanya miamala na kudhibiti maswala ya kifedha katika ufanyaji wa kilimo. Kupitia MPESA nchini Kenya, taasisi ya kilimo ya Kilimo Salama Agriculture Insurance imeongeza thamani ya bidhaa za wakulima kwa wastani wa 50% kwa bidhaa za kilimo, sawa na $150 kwa mwaka.

CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.
Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) mpaka mwaka 2050 watu wataongezeka mpaka kufikia bilioni 9.1 na kulisha namba hii ya watu, uzalishaji wa chakula duniani utahitajika kukuwa kwa 70% angalau. Kwa Afrika ambayo inatarajiwa kuwa na jumla ya watu bilioni 2 kufikia 2050, uzalishaji wa chakula kupitia sekta ya kilimo inabidi ukue haraka zaidi ya wastani wa dunia ili kupunguza dalili za baa la njaa. Sasa leo tuangazie umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo. Teknolojia ina mchango gani? Makinika mpaka mwisho wa makala hii kufahamu.

Je, wajua kwamba takribani theluthi moja (1/3) ya mazao yote yanayovunwa duniani kwa mwaka hupotea kwa kushambuliwa na wadudu waharibifu, magugu na magonjwa?

Sasa kwa kuligundua hili wataalam walibuni mbegu maalum katika maabara za kisayansi kwa kuboresha vinasaba (DNA) Za mazao na kufanikiwa kupata kitu walichoita Genetic Modified Organism (GMO). Kitaalam mbegu na mimea itokanayo na GMO imekuwa na faida nyingi katika kilimo zikiwemo; kuwa na uhakika wa kupata mazao mengi kwa kutumia mbegu kidogo tu. Vilevile GMO hizi zimetengenezwa zikiwa na ustahimilivu dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa jambo linalozipa uhakika wa kukuwa, kumea na kuzaa ipasavyo. Hata hivyo kinga hio dhidi ya wadudu waharibifu haiwazuii wadudu kama nyuki, vipepeo, minyoo wa ardhini na baadhi ya bakteria ambao huwa na jukumu muhimu katika uchavushaji wa mimea na hivyo kuleta mazao stahiki. Faida zingine ni kutunza na kuboresha rutuba ya udongo pamoja na kusaidia kuhifadhi maji ardhini, mambo ambayo yanaondoa hatari ya kutokea kwa baa la njaa duniani lakini zaidi, kuboresha uchumi wa mkulima.

Je unaamini kwamba wingi ni Faida?

Sasa majibu ya wataalam wa maswala ya kilimo duniani ni kwamba si mara zote wingi unaweza kuleta faida. Hii inajidhihirisha katika matumizi ya mbolea zinazotengenezwa maabara kiteknolojia katika kufanya kilimo ambapo kiasi kikubwa cha mbolea huweza kupelekea kudhoofisha mimea na kutishia kufifia kwa mazao kutokana na mlundikano wa kemikali zilizopo kwenye mbolea ambazo zikizidishwa ni hatari. Hivyo inashauriwa mbolea inayotumika iendane sawia na aina ya udongo, kiasi cha maji katika umwagiliaji na aina ya mazao yanayolimwa ili kuhakikisha mazao yanayotoka yanakuwa bora zaidi. Hata hivyo taarifa nyingi kuhusu matumizi ya mbolea za kisasa hupatikana kupitia applications za simu mahsusi kwa shughuli za kilimo ziitwazo m-ARD’s.

Shirika la maswala ya kilimo la M-Farmer Initiative Fund lilianzishwa mwaka 2011 kwa ushirikiano wa Mfuko wa hifadhi ya jamii wa Bill and Melinda Gates Foundation ili kuratibu, kufadhili na kukuza sekta ya kilimo barani Afrika. Shirika hili limepanga kufikia wakulima walioko katika nchi za Ethiopia, Malawi, Rwanda, Kenya, Zambia na Tanzania.

Hilo ni mojawapo la mashirika makubwa kuonyesha nia ya dhati katika kuendeleza shughuli za kilimo duniani, kuchochea umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo na kupunguza baa la njaa, kuboresha biashara za mazao ya kilimo pamoja na kukuza uchumi wa mkulima mmoja mmoja. Mashirika hayo yanazindua mifumo ya kimtandao ya malipo, mikopo na bima za kidijitali. Kwa mfano shirika la FarmDrive la nchini Kenya limezindua huduma za kifedha mahsusi kwa ajili ya wakulima ambapo kupitia shirika hilo wakulima hata wasio na akaunti za benki na wakulima wadogo kabisa hupata mikopo huku ikisaidia taasisi za kifedha kuongeza huduma za mikopo ya kilimo kwa gharama nafuu.

Kwa wafanyabiashara na kampuni zilipo ukanda wa Afrika Mashariki hii ni fursa kwao kuelekeza macho yao katika sekta ya kilimo kama inavyofanya FarmDrive nchini Kenya na shirika la kimataifa la M-Farmer.

Unalionaje hili? (tafadhali share kwenye comments) Hivyo kupitia jitihada za mashirika hayo, wakulima sasa wanaweza kupata mbolea, mbegu bora na mifumo mizuri ya umwagiliaji ili kukuza shughuli zao. Mchakato huo huboresha kasi ya uzalishaji katika kilimo na kupunguza changamoto kwa kutumia takwimu sahihi katika utendaji wa shughuli za kilimo kwa kutumia data za kisayansi na hivyo, umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo unazidi kuonekana. Kwa mfano matumizi ya vifaa vya umwagiliaji vinavyotumia nishati ya jua kusukuma maji kutoka katika chanzo chake kama mto, ziwa, bwawa au bahari. Vifaa hivi vimerahisisha sana swala zima la umwagiliaji.

Vilevile kwa kuzingatia ukweli kwamba mashamba mengi yapo maeneo ambayo ni mbali na huduma za mitandao ya simu na intaneti, hivyo kufanya huduma hizo kuwa hafifu, nchi kama Ethiopia imerusha satelaiti yake na kufanya wakulima kuwa katika nafasi nzuri kunufaika na mradi huo. Serikali za nchi zingine za Afrika Mashariki zinakwama wapi kwenye hili?

umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo.

matumizi ya TEHAMA katika Satellite

Hata hivyo zama hizi kutokana na kuimarika kwa miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji, pamoja na maendeleo katika sekta ya sayansi na teknolojia ya Habari na mawasiliano, imekuwa rahisi sana kupata taarifa kuhusu Hali ya Hewa, Hali ya soko na ushindani, mazingira ya miundombinu ya uchukuzi, mfumuko wa bei na uelekeo wa mahitaji ya wateja. Kilimo kimeja kufanyika katika namna rahisi sana katika kuuza mazao baada ya kuvuna, shukrani umuhimu wa teknolojia bora katika kilimo cha kisasa na chenye tija.

Kufahamu zaidi namna unavyoweza kuimarisha shughuli zako za kilimo kwa kutumia teknolojia tafadhali pitia makala zilizomo kwenye links hizi hapa:

  1. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWUWEKEZA
  3. UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021
fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

FAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA HABARI NA BURUDANI

Baada ya zaidi ya miaka 10 tangu vuguvugu la mapinduzi ya kidijitali lilipoanza kushika kasi barani Africa, sekta ya Habari na Burudani ambayo inawavutia vijana wengi zaidi kwa sasa imeingia katika ukurasa mpya ambapo sasa sekta ya habari imekuwa ikiendeshwa kwa msaada wa teknolojia kwa kiasi kikubwa sana. Leo sasa, uta fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani. Kuna nini humo? Makinika mpaka mwisho..

Sekta hii iliyogawanyika kwenye maeneo kama Matumizi ya IntanetiTelevisheni, Sinema, Video Games, MagazetiMajaridaVitabuMuzikiRedio na kadhalika imechagizwa sana na mapinduzi yasiyozuilika ya Intaneti barani Afrika ambapo matumizi ya simu za rununu yamejenga msingi imara kama chanzo cha maboresho, ubunifu na mapato katika sekta hii.

Changamoto; Je, Teknolojia inabadili vipi sekta hii maarufu ya Habari na Burudani barani Africa?

Kwenye makala hii tutagusia changamoto chache zinazosibibu sekta hii maarufu kabisa. Lakini kwa undani zaidi wa changamoto hizo pamoja na jinsi ya kupambana nazo, tips, ofa mbalimbali na ushauri huwa tunashare kupitia status zetu za WhatsApp, utaipata kwa kugusa namba yeu hii hapa 0765834754. Make sure umeisave kisha nitumie text yenye jina lako ili uanze kufaidi elimu ya BURE kabisa.

Makampuni, Wafanyabiashara, Wasanii na Mashirika ya serikali wanatilia mkazo katika kubuni huduma na bidhaa bora kila siku katika kuboresha utendaji wa sekta hii maarufu na inayopendwa zaidi na vijana barani Afrika ambapo tukianzia nchini Kenya sekta hii ilionyesha ukuaji wa 17.0% katika mwaka 2017, ukuaji ukichagizwa na maendeleo makubwa katika eneo la Matumizi ya Intaneti.

Vile vile ongezeko la watu katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) cha 11.6 litaipaisha sekta hii mpaka kufikia pato la dola za Kimarekani bilioni 2.9 kufikia mwaka 2022 kutoka $ 1.7 bilioni zilizorekodiwa mwaka 2017. Karibu wateja wapya milioni 15 wanatarajiwa kuwa mtandaoni ndani ya miaka 4 ijayo, na zaidi kunatarajiwa kuwepo kwa huduma za kasi ya juu za intaneti.

Katika huduma za kifedha; MPESA imerahisisha sana malipo ya bidhaa/huduma mbalimbali nchi kenya na hivyo kufanya sekta ya Habari na Burudani kuzidi kuimarika.

fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

Huduma za Televisheni; Kenya ni moja ya nchi mwanzo barani kufanikiwa kuhamia katika mfumo wa kidijitali ambao umefungua fursa nyingi zikiwemo huduma za televisheni na utengenezwaji wa mawaidha kidijitali. Hali hii imeibua ushindani mkubwa katika eneo hili ambao unazidi kupeleka mbele na kunogesha maendeleo ya sekta hii ya Habari na burudani.

Kwa kuongezea ujio wa makampuni kama Kwese TV na Startimes ambayo hutoza kiwango kidogo zaidi cha malipo ya huduma zao kwa mwezi, kumeongeza ushindani kwa kiasi kikubwa dhidi ya kampuni kongwe ya Multichoice katika utoaji wa maudhui ya televisheni nchini Kenya.

Redio; ongezeko la huduma na vifurushi katika mashirika ya Redio unakuza kwa kiasi kikubwa sekta hii ambavyo hutoa matangazo ya biashara mbalimbali mtandaoni na katika magazeti. Redio nyingi sasa zinalazimika kuhamia katika mtindo wa mobile applications ili kuwafikia watu wengi zaidi na kuongeza wigo wa mapato yao.

TANZANIA:

Sekta hii ya Habari na Burudani inakuwa kwa kasi sana nchini humo ambapo kwa mwaka 2017 sekta hio iliingiza pato la dola za kimarekani milioni 496 ukiwa ni ukuaji wa 28.2% kwa mwaka. Ongezeko la watu kwa kiwango cha CAGR cha 18.3% utashuhudia mapato ya sekta hio kufikia $1.1 bilioni mwaka hadi mwaka 2022 ambayo ni mara 2.3 zaidi kulinganisha na ilivyorekodiwa mwaka 2017.

Kiujumla ni Nigeria peke yake katika Africa ndio imeizidi Tanzania katika kasi ya ukuaji wa sekta hii ya Habari na Burudani. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Kimataifa la PwC. (Wabongo mnatisha kwa habari na bata 😂).

Internet; Kitakwimu kunatagemewa ongezeko la watumiaji wa huduma za 4G ambapo makampuni ya Vodacom na Zantel tayari yalishazindua huduma zao za 4G LTE tangu robo ya pili ya mwaka 2016. Mwaka 2017 TIGO walitangaza uwekezaji wa $70 million ili kutanua wigo wake wa kimtandao na kujiandaa na matumizi ya kasi ya 5G. Hata hivyo mpaka kufikia mwaka 2022, huduma ya kasi ya intaneti ya 3G bado itaendelea kutumika zaidi kufikia takribani 70% ya watumiaji.

Televisheni; matumizi ya huduma za ving’amuzi na televisheni yatapaa kutoka watumiaji 200,000 waliorekodiwa mwaka 2013 mpaka watumiaji 900,000 kufikia mwaka 2022 kwa huduma za televisheni za majumbani. Watumiaji wengi pia hutumia huduma za ving’amuzi kutoka kwa makampuni ya Multichoice na Startimes.

Magazeti; Ukiachana na matumizi ya intaneti yanayoshika kasi nchini Tanzania. Magazeti pia yanaongeza chachu katika uboreshaji wa sekta hii ya habari na burudani ambapo matumizi rasmi ya lugha za Kiswahili na Kiingereza yamekuwa nguzo muhimu.

Lakini kwa Tanzania nyanja ya magazeti inakwenda ikibadilika kwa kasi, kwa mfano kampuni ya Vodacom imebuni application ya M-Paper ambayo imewezesha kupatikana kwa vichwa vya habari vya magazeti maarufu zaidi nchini na hivyo kufanya upatikanaji wa habari kuwa mkubwa zaidi.

Ikiwa na jumla ya mapatoyaliyotokana na matangazo kufikia dola za kimarekani milioni 91 katika mwaka 2017 na kutabiriwa kufikia $128 milioni mwaka 2022, ni dhahiri sekta ya habari na burudani inakuwa sawia nchini humo na hivyo kuchipusha milango mingi ya kibiashara kuendelea kufanyika.

AFRIKA KUSINI:

Ongezeko la watu katika nchi hii linatajwa kuwa imara kwa kiwango cha CAGR cha 7.6% kwa mapato ya watumiaji wa sekta hii ya habari na burudani kufikia mwaka 2022 ambapo mapato yatapaa kutoka Randi 93.9 bilioni zilizorekodiwa mwaka 2017 mpaka kufikia Randi 135.7 biloni mwaka 2022.

Ukiachana na mapato yanayotokana na matumizi ya Intaneti (ambayo huchagizwa na mapato yatokanayo na applications za simujanja) kuna uwanja mkubwa zaidi wa mapato ambayo huongozwa na michezo ya video (video games). Mapato kutoka kwenye michezo hii nchini SouthAfrica yanazidi maeneo mengine kama vitabu, Business-to-business (B2B) na mauzo ya majarida. Ukuaji huu katika eneo la michezo ya Video umekolezwa na ongezeko la matumizi ya simujanja, uboreshwaji wa huduma za kasi ya intaneti kutoka 3G mpaka 4G kuzidi kuongezeka jambo ambalo linaifanya watumiaji wa Afrika Kusini kuwa ni wacheza games 😁.

Televisheni; Kama ilivyotegemewa, huduma za TV na Video zitaendelea kuongoza katika kuzalisha mapato ya watumiaji, lakini muda mchache ujao Kampuni kama Netflix na Amazon Prime huduma zao zitachukuliwa kama nyongeza kunyongea kwa maudhui yao ya burudani katika soko la Afrika Kusini. Vile vile malipo ta TV yataongeza Randi bilioni 6 mpaka kufikia mwaka 2022 kwa kiwango cha 5% ya CAGR japokuwa ukuaji wa mwaka-kwa-mwaka unategemewa kuoungua kwa 2.6%.

Matangazo; nyanja hii iliathiriwa zaidi katika mwaka 2017 na mazingira ya uchumi wa Afrika Kusini ambapo kulikuwa na ukuaji wa tahadhari wa 2.1% tu mwaka kwa mwaka. Hata hivyo, maboresho yanategemewa mpaka kufikia mwaka 2022, ikiwa na 3.3% ya CAGR ambayo itapaisha mapato zaidi.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.Umejifunza nini leo kwenye ku fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

Makala hizi hapa zitakupa taarifa zaidi kuhusu Teknolojia ya Habari na Burudani katika biashara yako:

  1. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BANDO LAKO NI MTAJI
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Karibu sana REDNET TECHNOLOGIES

teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)

Uchumi wa Africa mpaka sasa hukua kwa kutegemea sekta za asili kama kilimoufugaji na biashara. Hata hivyo ujio wa teknolojia ya huduma za kifedha kwa njia ya kielektroniki (Fintech) utasaidia kwa kiasi kikubwa kuendesha uchumi katika kufanikisha maendeleo kiujumla. Sasa tuangalia teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech), zina mchango gani kwako leo?

Uchunguzi umeonyesha kwamba matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu za mkononi yameongezeka sana ndani ya miaka 10 iliyopita ambapo imeonekana eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara ndio limekuwa kinara wa kubuni na kutumia huduma hizi za kifedha kwa kutumia simu za mkononi duniani kwa sasa.

Utafiti uliofanywa na Shirika la Fedha duniani (IMF) umebaini kwamba takriban 10% ya pato la taifa katika miamala ya kifedha hufanyika kwa huduma za kifedha kupitia simu za mkononi. Hii ni matokeo bora zaidi ukilinganisha na 7% ya GDP katoka bara Asia na chini ya 2% ya GDP kutoka sehemu zingine za dunia.

Sasa swali, hii Fintechs ni nini!? Na ina manufaa gani kwa wafanyabiashara walio Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Shirika la EY linaifafanua FinTech kama Shirika/Kampuni inayojumuisha ubunifu katika utendaji wa biashara pamoja na technolojia ya programu za kompyuta katika kubuni, kuwezesha na kusambaza huduma za kifedha. Hizi FinTechs zinaweza kuwekwa kwenye makundi mawili;

i. FinTechs zinatoa huduma za kifedha e.g TALA App.

ii. FinTech zinazowezesha huduma za kifedha Vodacom na MPESA n.k (tutayajadili zaidi kwenye makala zetu zijazo)

Sekta hii ya FinTech katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara (SSA) inajumuisha zaidi ya makampuni 260 ambapo 80% katika hizo ni kampuni za ndani na 20% ni kampuni za kimataifa. Vile vile imeonekana idadi ya makampuni haya mapya imeongezeka katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) cha 24% ndani ya miaka 10 iliyopita.

Hata hivyo ripoti zinaonyesha kwamba Afrika Mashariki itaendelea kuongoza katika ukuaji wa sekta hii kwa 6.3% ya ukuaji wa uchumi mwaka huu 2019. Hii ni kutokana na Ethiopia, Rwanda, Tanzania na Uganda zote zinatarajia kurekodi pato la Taifa la zaidi ya 6% mwaka huu ambayo ni zaidi ya nchi zilizo maeneo mengine ya Africa. Hii ni kutokana na uwekezaji katika miundombinu na utanuzi wa huduma za kifedha na mawasiliano.

Takriban theluthi moja (1/3) ya michango ya harambee zilizofanyika barani Africa mwaka 2017 iliwezeshwa na kampuni za FinTechs. Hii inatiliwa mkazo kwa kuwa 60% ya akaunti za huduma za kifedha kwa njia ya simu duniani zimegundulika kuwepo katika eneo la SSA. Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliofanya na benki ya Ecobank.

Pia imeonekana sekta hii ya FinTechinaendelea kuwa imara katika muda wa miaka 3 kutoka makadirio ya dola za kimarekani 200 milioni mwaka 2018 hadi 3$ bilioni mwaka 2020. Kiasi kikubwa cha uwekezaji katika muda huu kimeonekana kuelekezwa KenyaNigeria na Afrika Kusini. Vile vile inategemewa kwamba kufanikiwa kwa Fintechs katika nchi hizo kutatanua mafanikio katika nchi zingine za Kiafrika.

MAENDELEO: Ujio wa FinTechs umebadili sana jinsi ya kufanya biashara duniani. Kutoka Crowdsourcing ambayo ni njia inayotumika kufanya usaili wa miradi mbalimbali mtandaoni kupitia intaneti na kupokea ruzuku, mpaka njia ya huduma za kifedha kwa njia ya simu. Wafanyabiashara na wajasiriamali hawajawahi kupata njia rahisi zaidi kwenye utandaji wa biashara zao kwenye maswala ya fedha kuliko hii.

Kupitia Fintechs sasa wafanyabiashara wanaweza kusambaza bidhaa/huduma kwa watu mbali mbali na kupata malipo ndani ya muda mfupi zaidi. teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) inazidi kujisombea watumiaji kwa sababu inaonyesha namna inavyoweza kusaidia katika kujikwamua kwenye maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni.

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH) HAINA MIPAKA:

Kutuma pesa nje ya mipaka ya nchi napo imekuwa rahisi zaidi. Mfumo huu ulioondoa mipaka ya kijiografia kwenye kurusha pesa umepunguza gharama kutoka ilivyokuwa mwanzo kwa njia ya benki ambayo ni ghali mno. Hivyo FinTech imewawezesha wajasiriamali na viwanda vidogo kutuma na kupokea pesa kwa gharama ndogo zaidi.

KUONGEZA THAMANI KATIKA UTOAJI WA HUDUMA ZA KIFEDHA: Eneo hili limetawaliwa na ubunifu ambao unawezesha kuongezeka kwa thamani katika matumizi ya huduma za kifedha. Kwa kuyumia malipo kwa njia ya simu, wateja walioko kusini mwa Jangwa la Sahara wanapata uwezo wa kupata huduma za kibenki kupitia simu za mkononi (mobile banking) pamoja na huduma zingine kama kugungua akaunti, kuchukua mkopo, kupata bima, kupata huduma za mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na masoko ya hisa. Haya yote kupitia FinTech yanawezeshwa kirahisi tuu katika simu yako ya rununu (smartphone) au laptop.

teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi. Umejifunza nini hapa katika teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) leo?

Zaidi unaweza kupitia makala hizi hapa chini ili kupata ufahamu mpana kuhusu biashara za mtandaoni:

  1. MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA
  2. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  3. UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-COMMERCE BUSINESS)?
  4. FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia comments section hapo chini;

fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika

FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA TEKNOLOJIA YA 5G

Dunia ipo mbioni kuelekea zama za matumizi ya teknolojia ya 5G katika kasi ya Intaneti. Mpaka kufikia mwaka 2020 huduma za kibiashara za 5G zilishaanza kupatikana katika nchi zaidi ya 50 kutoka Asia, Ulaya, Mashariki ya Kati na Amerika ya Kaskazini. Muongo wa 2020s’ ndio unatajwa kushuhudiwa kwa usambazaji mkubwa zaidi wa teknolojia hii ya kasi ya intaneti duniani ikijumuisha nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara. Sasa leo kwa uchache uta fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika.

Kufikia mwaka 2022 tu tayari kampuni ya Vodacom Tanzania walishazindua huduma zao za 5G nchini na kuwa kampuni ya kwanza ya mawasiliano kuzindua huduma hizo. Hakika maendeleo ya teknolojia hii yanakwenda kasi sana.

Sasa ili kujua kwa undani kuhusu teknolojia hii pamoja na matarajio yake katika kufanikisha shughuli za kila siku za kibinadamu, kitengo maalum cha kijasusi katika shirika la GSMA kiliendesha ziara iliyohusisha wabia muhimu ili kupata maoni halisi ya watumiaji wa intaneti kuhusu ujio wa 5G katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara. Uchunguzi huo ulijumuisha maeneo sita ambayo ni; matumizi ya mtandao (network deployment), wigo wa mtandao (spectrum), watumiaji (use cases), mifumo ya biashara na fedha (business model and finance), sera na sheria (policy and regulations) pamoja na ushirikiano wa kibiashara na matokeo ya mbeleni.

Katika maeneo hayo walengwa waliojumuishwa walikuwa ni wasimamizi wa mashirika wa mawasiliano katika ukanda huo, kampuni za simu zilizo na hisa zaidi ya 75% kwa pamoja katika ukanda huo pamoja na wauzaji wa vifaa vya mawasiliano ambao wana hisa za zaidi ya 90% ya soko la miundombinu ya kimtandao katika ukanda huo.

Takwimu zilizotolewa na ripoti ya uchunguzi huo ambayo imechapishwa Mwezi July, 2019 zilitokana na uchambuzi wa maoni ya watu mbali mbali kuhusu 5G. Pia matokeo haya yamejumuisha data kutoka vyanzo mbali mbali vinavyohusiana na teknolojia hii ambapo wataalamu waliounda na kendeleza teknolojia hii wataangalia kwa makini watumiaji wa mfumo huu katika ukanda wa kusini mwa Jangwa la Sahara, lengo kuu likiwa ni kujifunza na kujiimarisha zaidi kutoka kwa vinara wa 5G.

Teknolojia za kidijitali zimekuwa muhimu sana katika shughuli za kibinadamu za kila siku. Hii ni muhimu zaidi katika nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo kama teknolojia hizo zisingekuwepo mambo yangekuwa magumu zaidi kutokana na ubovu na uchakavu wa miundombinu, maswala ya fedha pamoja na ujuzi binafsi wa mtu. Sasa ripoti hio iliyotengenzwa kutokana na uchunguzi wa kitengo cha Intelijensia cha shirika la GSMA imekuja na majibu kadha wa kadha;

MAPINDUZI KATIKA KASI YA INTANETI YA 5G YAMEFIKA:

Kufikia mwisho wa mwaka 2019 kulishakuwa na mtandao mkubwa wa kasi ya 3G na 4G zaidi kuliko 2G katika ukanda huo wa kusini mwa Afrika. Hii inaonyesha ukuaji kutoka huduma za sauti mpaka huduma za data. Uwekezaji unaoendelea kufanyika katika 4G umepeleka ukubwa wa huduma za mitandao kufikia robo ya jumla ya watu waishio katika ukanda huo. Vile vile imeonekana kwamba matumizi ya simu za rununu (smartphones) yameongezeka mara mbili ndani ya miaka mitano iliyopita.

jinsi ya kuanzisha website umuhimu wa tehama.

fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika

TEKNOLOJIA YA 5G ITAKUWA NI SEHEMU YA MIUNDOMBINU BORA YA KIMTANDAO, JAPO UENEAJI WAKE HAUTAKUWA WA KASI SANA:

Katika ukanda huu, teknolojia ya 5G haizuiliki. Ni maendeleo ya kiasili kutoka katika teknolojia zilizopita. Japokuwa, kasi ya ueneaji wa teknolojia hii ya 5G si kubwa katika ukanda huu kutokana na uwepo wa teknolojia zingine kama 3G na 4G bado zina uwezo wa kumsaidia mwanadamu kufanya shughuli zake katika kasi inayoridhisha ya intaneti.

Takribani theluthi mbili (2/3) ya walioshiriki kwenye uchunguzi huu wanatarajia huduma za kibiashara za 5G kuwa katika masoko yao kabla ya mwaka 2025. Pia teknolojia hii itasaidia kupevuka na kuweza kutumika katika masoko mengine. Vile vile itaruhusu uchumi kukua kwa kutumia teknolojia ya 5G katika vifaa vya kielektroniki ambavyo vitapunguza gharama za waendeshaji na wateja. Hapa ndipo tuta fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika kwa undani wake kabisa.

UTAYARI WA SOKO NI MUHIMU KATIKA KUKUZA THAMANI YA TEKNOLOJIA YA 5G:

Kwa nchi zote zilizo katika ukanda huu utayari wa soko ni jambo muhimu zaidi kufanikisha mageuzi ya teknolojia ya kasi ya 5G. Hii itasaidia kukuza thamani katika huduma za 5G kwa wateja, waendeshaji na jamii nzima kwa ujumla. Kiwango cha utayari wa soko kinaonyesha kwamba baadhi ya nchi zinakwenda kasi kwenye matumizi ya teknolojia hio kutoka 4G.

Kufikia mwaka 2025 huduma zinazotumia teknolojia yenye kasi ya intaneti ya 5G itafikia nchi 7 zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara ikijumuisha ni Kenya, Nigeria na Afrika Kusini. Pia uchunguzi umetabiri kuwako kwa miunganiko milioni 28 ya simu kwa kutumia 5G, sawasawa na 3% ya jumla nzima ya miunganiko ya kimtandao ya simu katika ukanda huo.

MASHIRIKA NA MAKAMPUNI MAKUBWA YATAONGOZA KUANZA KUTUMIA 5G KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA:

Teknolojia ya 5G itawezesha makampuni ya mawasiliano na mashirika kuhudumu vizuri zaidi kwa wateja wao ambapo watumiaji wa mwanzoni watawezeshwa na huduma ya wireless (Fixed Wireless Access #FWA) ili kutoa changamoto kwenye matumizi, gharama na upatikanaji wa huduma za kimtandao kama huduma za satelaiti na intaneti. Hapa sasa ndipo uta fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika kwa ukaribu zaidi.

KWA WATEJA NA WATUMIAJI ITAKUWA NI ZOEZI LA MUDA MREFU:

Hii ni kutokana na udhaifu katika upatikanaji wa huduma/vifaa(simulaptop..) bora Kwa gharama nafuu pamoja na ujuzi wa matumizi ya teknolojia kama virtual reality (VR) na Augmented Reality (AR). Ubora wa vifaa kama simu za rununu (smartphones) na kompyuta ni muhimu zaidi katika zama za 5G kwa matumizi ya wateja lakini inategemewa malengo ya teknolojia hii ni kufikia vifaa vya nyumbani (Customer Premise Equipment CPE) kama routers ili kupata huduma za uhakika za wireless (FWA).

Hii ni kwa kuwa huduma hizo hupatikana kwa malipo ya kabla kutoka kwa makampuni ya simu, ambapo katika muda huo huo huduma ya kasi ya 4G itaendelea kuhudumu kwa kasi inayoridhisha na kuwafikia watumiaji wengi zaidi ambao watachangia ukuaji mzuri wa uchumi.

KIPAUMBELE KITAWEKWA KATIKA KUPATA UHAKIKA WA HUDUMA YA WIRELESS (FWA):

Ukuaji wa Matumizi ya intaneti katika vifaa kama simu na kompyuta ni mdogo mno ambao ni chini ya 2% katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara, hivyo kufanya ujio wa zama za 5G kuegemea kwanza katika CPE’s. Hii itapunguza gharama za uendeshaji lakini pia itaongeza watumiaji kwa kutumia wireless (FWA). Mbinu hii ya kufikisha teknolojia kwa jamii inalenga kwa suluhu mbadala kwa makampuni ya mawasiliano kulinganisha gharama za kuhudumia/kufikia simu moja moja na uwezo wa watumiaji wengi kuelekea zama za kasi ya 5G.

fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika

Hio ndio mantiki ya mada yetu ya leo katika ku fahamu kuhusu mapinduzi ya teknolojia ya 5G katika biashara na uchumi wa Afrika, kwa ufupi. Unataka kujua zaidi? Karibu uwasiliane nami kwa njia ya WhatsApp kupitia namba hii hapa 0765834754 Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo hapa. Zitakusaidia sana ukizipitia:

  1. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  2. TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI
  3. FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA DUNIANI
  4. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?