Tag: jinsi ya kupata wateja

Kwanini mteja akuchague wewe

KWANINI MTEJA AKUCHAGUE WEWE?

Maisha ya biashara za mtandaoni ni marahisi sana kama ukizingatia tabia za wateja mtandaoni, na ni magumu sana ukipuuzia/usipozijua. Kwanza, hakikisha ukitafutwa unapatikana. Swala la kujiuliza ni, Kwanini Mteja akuchague wewe aache watoa huduma na wafanya biashara wengine?

Zipo sababu nyingi sana mtu akiwa mtandaoni anaziangalia ili ajiridhishe kabla hajawa mteja wako. Leo hapa tutaziona 6 tu. Zingine nitaziweka kwa status yangu ya WhatsApp. Ukihitaji kujifunza zaidi gusa hapa 0765834754 nitumie text yenye jina lako ili nikusave chap.

Mwaka 2022, niliweka story hapa kuhusu jamaa yangu fulani ambaye aliona kazi zetu mtandaoni, akashawishika kuchukua namba kisha akanitafuta tufanye kazi yake, na mpaka leo tumejenga uhusiano bora sana. Ile stori ni hii hapa kama ilikupita Faida za Kutumia Google kama Jukwaa la Biashara yako.

Baada ya kupublish stori hio, nilipokea requests nyingi sana kutoka sehemu mbali mbali yakiwemo mashirika ya kiserikali, binafsi ya yale ya kimataifa.

Leo hii sasa nataka nikwambie Kwanini Mteja achague kufanya kazi na wewe na awaache wengine? Fuatilia dondoo hizi hadi mwisho:

1. UBORA WA KAZI/BIDHAA/HUDUMA: Sikufichi, watu wanapenda vitu vizuri bwana. Hakuna anayependa bidhaa/huduma mbovu. Hata utumie mbinu gani za kunasa wateja mtandaoni, kama bidhaa/huduma zako hazina ubora unaotakiwa, jua apo unacheza tu. Utapata tabu yani.

Kama bidhaa/huduma zako zinatolewa na wafanyabiashara wengine, hio ni fursa nzuri kwako. Fanya uchunguzi, angalia wapi unaweza fanya improvements, ongeza ubunifu kidogo upande wako kisha peleka mzigo sokoni. Hakunaga miujiza kwenye hili. Lazima utie juhudi muda wote.

2. UBORA WA HUDUMA UNAYOTOA; Kama kuna kitu kinafanya wafanyabiashara wengi hawakui kibiashara licha ya kuwa na skills au bidhaa/huduma bora, basi ni hili la kushindwa kutoa huduma zinazomridhisha mteja. Angalia, watu wanatofautiana sana kwenye namna ya kutoa na kupokea maoni na changamoto. Wewe sasa kama mtoa huduma lazima ujue jinsi ya kujishusha kwenye kupokea maoni na changamoto na vile vile kwenye kutoa huduma zenye viwango vya hali ya juu. Huduma bora inaenda sambamba na kuijua saikolojia ya mteja wako. Cheza napo vizuri hapo.

Kuna makala hii kuhusu Umuhimu wa Takwimu kwenye utoaji wa huduma bora katika biashara yako. Ifuatilie hapa uelewe kwanini unapaswa kutoa huduma bora muda wote kwa wateja wako.

3. PATIKANA SEHEMU MBALIMBALI MTANDAONI; Katika mitandao ya kijamii, kila mahali watu hujihusanisha kitofauti. Mfano utagundua watu wa facebook na twita ni tofauti kabisa. Lakini sikufichi, wengi ni wale wale tu. So unapaswa kupatikana kwenye majukwaa yote makubwa kama Facebook, Twita, Linkedin, Instagram n.k Patikana huko kote kwasababu kila mtu ana mtandao wake ambao anautumia zaidi na wote hao unawahitaji leo. Na unachokitaka wewe ni kuifikisha biashara yako kwa kila mtu anayetumia smartphone yani. Si ndio? Fanyia kazi hilo.

nguvu ya mitandao ya kijamii unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Kwanini mteja akuchague wewe?

4. TUMIA S.E.O; Hapa sitasema mengi kwasabau kule WhatsApp huwa natupia sana updates, tips, info na najibu maswali mengi sana kuhusu SEO. Pia kuna eBook maalum ambayo inaelezea siri zote unazohitaji kuzifahamu ili SEO iweze kuwa na manufaa kwako siku zote. Kuipata eBook hio pia hakikisha umesave namba yetu ya WhatsApp, kisha tuma ujumbe wenye jina lako na utapatiwa maelekezo.

In short hii SEO inakurajisishia biashara yako kupatikana haraka pale mtu akiwa anasearch taarifa kupitia Google. Yes, unaihitaji google zaidi sawa sawa na Google inavyohitaji taarifa za biashara yako kwa manufaa ya wateja wako duniani kote.

Mteja anayekutafuta ni mzuri sana kuliko yule unayemtafuta, si ndio? Sasa kwanini usijiweke kwenye mazingira ambayo yatamrahisishia mtu akiwa anatafuta bidhaa/huduma kule Google na kumpa majibu Kwanini mteja akuchague wewe kuliko wengine? Ukiitumia SEO vizuri itakujibu vema sana kwenye hili.

Takwimu za Internet Live Stats zinaonyesha kuwa kwa siku 1 tu kule Google huwa kunafanyika matafuto (searches) zaidi ya bilioni 3.5. Sasa linganisha na matangazo (Paid Ads) unayoyaonaga mtandaoni (Youtube, Insta na fb) na kuyaskip. Wapi utatoboa, kwenye Searches (SEO) au Ads?

5. TOA OFA KADHAA; Mwanaume huwezi kuoa ile siku ya kwanza unapokutana na Mwanamke, hali kadhalika, ni ngumu sana mtu akawa mteja wako siku ya kwanza tu amekutana na wewe huku mtandaoni. Ni muhimu sana kumpitisha mteja kwenye hatua kadhaa ili kusudi aweze kukujua zaidi akupende, akuamini na mwishowe sasa ndo aweze kuwa mteja wako wa kudumu.

Hii ni kwakuwa Biashara za Mtandaoni hutegemea sana kujenga Uhusiano Bora na watu usiowafahamu. Ndio maana unaona kuna wasanii wana mashabiki zao wanawapenda mpaka wakiwaona wanazimia japo hawafahamiani.

Hii ni kwasababu wasanii hao waliwapa values/ofa/zawadi nyingi ambazo ziliwafanya mashabiki zao wawapende sana hata kama hawajuani kiundani. Kadhalika, ukiwa unafanya biashara mtandaoni lazima ujifunze kutoa tips, info, updates, ujibu maswali na ujichanganye na wateja wako.

6. DHIHIRISHA KWAMBA BIDHAA/HUDUMA UNAYOTOA NI GHALI KULIKO GHARAMA ANAYOLIPA: Tunaishi kwenye zama ambazo kila mtu anauwezo wa kufanya biashara na akapanga bei itakayompa unafuu. Mfano, kwenye kutengeneza website ukizunguka huku mtandaoni utaona kila mtu ana bei yake.

mageuzi ya Intaneti (iot) katika biashara na maisha. Jihudumie leo kutoka Rednet Technologies.

Kwanini mteja akuchague wewe?

Biashara zimekuwa huru sana. Kila mtu anao uwezo wa kufanya biashara mtandaoni. Sasa unapaswa kujiweka kwenye nafasi ambayo mteja atakuchagua always akikutana nawe mtandaoni. Kwanini mteja akuchague wewe? Tips hizo hapo. Tips nyingine zipo WhatsApp hapa kwa kugusa namba hii 0765834754

Umejifunza nini kwenye makala hii ya leo kuhusu Kwanini mteja akuchague wewe? Kuna mahali hujaelewa? Niulize swali.. Share, Like na ucomment hapo chini maoni na maswali yako.

Cheers.

Kwanini hupati wateja mtandaoni?

KWANINI HUPATI WATEJA MTANDAONI?

Kila mtu anapenda maisha mazuri, kufanikiwa kibiashara, kuwa na amani na uhuru wa kufanya kile kinachokupa furaha muda wowote. Sasa uko tayari kuingia gharama ili kuyapata matamanio yako? Umeshajiuliza Kwanini Hupati Wateja Mtandaoni licha ya Juhudi unazoweka?

Mwaka 2010 wakati nafungua account ya Facebook nilikua nafurahi sana kukutana na rafiki zangu tuliopotezana miaka mingi baada ya kumaliza Primary School na sekondari. Ilikua safi sana kuona picha za washkaji wakiwa na maisha yao baada ya shule.

Baadae tukaanza kupata marafiki wengine katika mtandao pendwa wa facebook. Nyakati hizo Mtandao wa Twita ulionekana kama mtandao wa Wanasiasa, Instagram ya Wasanii na Masuperstar. Ila Facebook kule wote tulionana kuwa ni level moja. So kule ndo tuliona kuna lile vibe la wote.

kwanini hupati wateja mtandaoni?

nguvu ya mitandao ya kijamii 

unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Lakini miaka ilivyozidi kwenda, Matumizi ya Mitandao ya Kijamii yalikua yakibadilika mdogo mdogo, hasa baada ya kushuhudia Wasanii na watu waliokuwa na Followers wengi mitandaoni waliposhindwa kuimarisha Uchumi wao kupitia Nguvu ya Mitandao. Hapa kitu kipya kikatambulishwa.

Ilifika mahali sasa ule utaratibu wa kuwa na urafiki na wale tu uliowahi kusoma nao sasa ulipitwa na wakati na badala yake, Rafiki/Followers/Follows wa mtandaoni wakawa ni wale ambao tunashare nao “Interests” Hapo ndipo mbinu za kufanya biashara mitandaoni zilipoanza kushamiri.

Tayari nimeshakuandalia makala maalum itakayokupa mbinu muhimu za kunasa wateja mtandaoni. Kama unataka kuzifahamu mbinu hizo ili uzitumie kwenye biashara yako basi fuatana na makala hii hapa Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

MAMBO SABA (7) YANAYOKUKOSESHA WATEJA MTANDAONI

Tumeshaona jinsi Mitandao imebadilika kutoka ilipoanza, sasa kuna mambo unayoyafanya kwa kujua au kutokujua yanayokukosesha wateja. Jambo la 5 litakushtusha sana. Hebu tuyaone hapa;

1. Kutokuwa na Bidhaa/Huduma inayokutambulisha;

Hapa unatakiwa kuwa makini na kuelekeza focus yako kwenye bidhaa/huduma fulani specific. Inaweza isiwe bidhaa/huduma moja, lakini hakikisha unakuwa na ile bidhaa/huduma inayokutambulisha. Mfano: Unauza fenicha, shikilia hapo hapo.

kwanini hupati wateja mtandaoni

Zile zama leo unapost fenicha, kesho unapost computers keshokutwa unapost picha uko unasafiri, mara unapost unakula chakula., hivyo ni vitu ambavyo vinakupunguzia mvuto mtandaoni. Sisemi usipost kabisa, hasha, katika post 10, 7 ziwe ni kuhusu fenicha, 3 maisha binafsi.

2. Kushindwa kuingia kwenye Orodha ya Wanaofanya biashara kama yako mtandaoni;

Kuna ile dhana ya kuogopa ushindani au ile kuwekeana mtimanyongo na washindani wako. My friend, huku mtandaoni make sure unajenga uhusiano na kila unayekutana naye. Itakusaidia sana kuendelea kudumu sokoni.

Kuingia kwenye orodha(list) ya wafanyabishara huna budi kuwa support wafanyabiashara wenzako mtandaoni. Ndio, Wasukuma wana msemo wao wanakwambia “Scratch my back, I’ll scratch yours.”

3. Kutokua na muendelezo wa Maudhui kutasema kwanini hupati wateja mtandaoni;

Je wajua kwamba kwa siku huwa kunakuwa na posts zaidi ya milioni 50 katika mitandao mbalimbali duniani. Sasa ndugu unapost mara 1 kwa wiki unategemea nani ataiona hio biashara yako? Hakikisha unapost mara nyingi kadiri iwezekanavyo.

Njia ya Kompyuta katika kuhifadhi data utajuaje pale biashara yako inapojiendesha kwa hasara changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika

4. Kushindwa Kuwasiliana Vema;

Kupost bidhaa/huduma zako mtandaoni ni jambo moja, lakini uwezo wa kuwasiliana ndio muhimu sana. Shuleni tulisoma ile Communication Skills, sasa mtaani unatakiwa uwe na uwezo wa kuwasiliana na kujua wapi, sangapi useme nini. Ni maarifa hayo.

Mtaalam wa mitandao bwana @GillsaInt ana mbinu yake anakwambia katika maudhui yako unayopost mtandaoni, hakikisha 80% ni yanahusu thamani (value) za bidhaa/ huduma zako kama Faida, Jinsi ya Kutumia, Changamoto nk. Na 20% zinazobaki ndo upost sasa Matangazo ya kuuza hio biashara.

5. Kutokuwa na Miundombinu ya Kurahisisha biashara Mtandaoni;

Umeshaona wale wanakwambia No Facebook Acc, No Insta Acc, No twitter etc. Skia, kama unataka kufanya biashara ukafanikiwa mtandaoni USIFUATISHE hizo akili zao. Hakikisha una miundobinu humu mtandaoni.

Mitandao ya kijamii ndipo ilipo NGUVU halisi ya biashara ya mtandaoni. Jifunze namna unavyoweza kuitumia kwa faida ya biashara yako. Kama unataka kuifahamu NGUVU hio ya mitandao, basi fuatana na makala hio hapa kufahamu zaidi.

Lengo la kufanya biashara mtandaoni ni kuhakikisha unakuwa na wateja wengi kadiri iwezekanavyo, si ndio? Kama ni hivyo, fanya research, kisha tambua wateja wako ni kina nani na wako wapi. Fungua website yako, accounts za Insta, Facebook, Linkedin, Twitter n.k Kuwa available.

6. Kukosa Ushawishi na Ujuzi wa Kuuzia wateja Mtandaoni;

Sasa hapa naongelea uwezo wa kumshawishi mtu akapenda bidhaa/huduma zako kabla hajawa mteja wako. Kwenye hili @iamKaga pale twita anakupa funzo gani? Cha kwanza hakikisha watu wanakujua, kisha Wakupende au wapende maudhui yako, hapo ndipo watakujia.

Huo ushawishi hauji tu by default wala haujengwi ndani ya siku moja. Ushawishi ni tabia ya kuhoji na kutoa ufumbuzi juu ya changamoto zinazowakabili watu katika namna bora ya uwasilishaji. Hapa ndipo wanasiasa wanatupiga coz anaijua siri iliyopo kwnye ushawishi.

7. Kutokuwa na Njaa ya Mafanikio;

Tunarudi kulee mwanzo, unapost mara 1 kwa wiki, au mara 2 kwa mwezi halafu unasingizia huna muda wa kuandaa maudhui. Bro, ni vile tu huna njaa ya kufanikiwa. Njaa ya mafanikio ikikushika vizuri huo muda LAZIMA uupate na utautumia vizuri tu.

Kuna nyakati unabanwa na shughuli zako nyingine to the point unashindwa kuendesha biashara yako mtandaoni. Kuna nyakati nyingine unakata tamaa kwa sababu huna followers au huna idea uanzaje kuandaa maudhui ili ufikie yale matamanio yako. Ukifikia hapo wala usiwe na shaka..

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

Hata hivyo, katika biashara sio lazima kila jambo ufanye wewe mwenyewe. Nyakati hizi za mapinduzi ya teknolojia kila siku, ni muhimu kugawa majukumu kwa wataalam wa kuaminika ili kuhakikisha lengo na mipango yako inazidi kwenda kama utakavyo.

Hio ndio sababu sisi Rednet Tech. LEO hii tunakupa nafasi ya kuikuza biashara yako mtandaoni kwa;

1. Kukutengenezea Website bora.

2. Kukufanyia huduma ya SEO. Inafanyeje kazi hii? Gusa hapa kuifahamu zaidi.

3. Kukushauri aina ya maudhui ya kuyatumia kwenye kurasa zako za mitandao. Gusa hapa tuchati pale WhatsApp na upate huduma unayohitaji.

So, mambo haya 7 tuliyoyaona leo kwa uchache wake ndio yanakwambia kwanini hupati wateja mtandaoni. Umeshajua cha kufanya sasa? Hebu niambie wewe ni lipi umegundua leo kuwa ndio linakukosesha wateja? Mtandaoni hamna miujiza. Ni kuwa na maarifa na kuhakikisha unajifunza kila siku. Umependa makala hii? Share..

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni. Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

JINSI YA KUONGEZA MBINU ZA KULIFIKIA SOKO MTANDAONI

Kila mtu atakwambia post insta, facebook, tumia funnels, weka status za kutosha Whatsapp. Mwingine atakwambia kusanya namba za simu uwapigie, tuma emails kila siku nk. Sasa utafanyaje kuongeza mbinu za kulifikia soko? Utakapomaliza makala hii ya leo utafahamu kiundani kuhusu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni. Utafanyaje, twende sambamba mpaka mwisho.

Zama hizi za Internet na huduma za mitandao ya kijamii zimekuja na mgawanyiko wa watu. Kila mtu anatumia mtandao wa kijamii anaoona unampendeza. Sio ajabu uone kuna mtu hana account ya facebook lakini kutwa yupo instagram/twitter. Hata hivyo ukiwa mjasiriamali lazima ufike kote.

UNALIFIAJE SASA HILO SOKO LA MTANDAONI?

1. Kwa kutumia Mitandao kama Whatsapp, Instagram, Twitter na Facebook, sasa unaweza kueneza maudhui yako kote kote kwa mtindo wa Copy & Paste. Ndio sio dhambi kufanya C&P ikiwa maudhui ni yako. Hata hii makala usishangae kuikuta kwa page zatu za LinkedIn na Instagram. Hapa ni muhimu sana Ukaifahamu Nguvu ya Mitandao ya Kijamii katika biashara yako.

Unachotakiwa kufahamu ni kwamba mitandao hii imetofautiana, hivyo maudhui unayopost twitter inabidi UYAHARIRI ili yaendane na aina ya watu katika mitandao mingine kama Website yako, Facebook, Instagram na LinkedIn. So kazi ya kueneza maudhui haiwi ngumu kuvile hapa, sivyo?

2. Pia unaweza kuanzisha kampeni fulani na kisha unaieneza kwa njia ya barua pepe. Kufanikiwa kwenye hili kwanza unapaswa ukusanye anwani za barua pepe nyingi (walau elfu moja) na kisha uifanye kampeni yako kwa uweledi wa hali ya juu ndani muda fulani. Hii ndio Email Marketing.

E-Mail Marketing in Business
mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

NB: Kampeni yako haipaswi kuwa na ujumbe wa kupandikiza chuki au viashiria vya ubaguzi wa namna yoyote kwa sababu kampeni za namna hio huleta hisia mseto kwa watu na kukujengea taswira mbaya. Barua pepe zako unaweza kuzikusanya kwa njia ya Newsletter au kawaida (ile ya kuomba).

3. Tumia Social Media Analytics Tools: Kama unasambaza maudhui yako kupitia mitandao ya kijamii, siku hizi kuna namna ambayo unaweza kupima mwenendo wa machapisho yako kirahisi tu. Katika twita kuna Twitter Analytics na Insta kuna Insights.

social media analytics tools
mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

Hizo tools zitakwambia maudhui yako yamewafikia watu wangapi (impression), wangapi wameshiriki mjadala (engagement), wangapi wameclick links na umepata wafuasi wangapi baada ya kuchapisha maudhui. Ukishajua hayo itakusaidia sana kuboresha zaidi Machapisho yako yajayo.

Mitandao ya kijamii hasa Mtandao wa GOOGLE ina nguvu ya ajabu sana katika kuwafikia watu wengi ndani ya muda mfupi tu. Ni muhimu basi ukajua namna ya kucheza na mitandao hii ambayo kila mtu duniani anatamani awe mtumiaji wa kila siku. Kufahamu zaidi kuhusu nguvu hio gusa hapa;

4. Tumia Web Analytics Tools; Kama tayari unayo website ya biashara au page ya blogu yako, basi ni muhimu sana ukaweza kufuatilia na kujua ufanisi wake kwa watu wanaoitembelea. Unajua watu wangapi wanatembea website yako kila siku? Makala zipi ulizoandika zinafuatiliwa zaidi?

Watu wanaotembelea website yako wanatokea wapi? Katika Injini za Kimtandao, website yako iko katika nafasi gani? Majibu ya maswali yote haya unaweza kuyapata kwa kutumia tools kama Google Search Console, ahrefs, winch, clutch n.k Hivi ndo virutubisho vya website yako mtandaoni.

5. Tumia Content Management System (CMS); Ukiwa muandishi ambaye ungependa maudhui yako yazidi kufanya vizuri mtandaoni basi unapaswa kutumia mbinu mbadala zitakazokusaidia tena na tena. Sikuhizi mambo yamerahisishwa, WordPress ndio CMS maarufu zaidi lakini ukiacha hio kuna Joomla, Drupal, Magento, Shopify na Prestashop (kwa ajili ya e-commerce). Ukiwa na hizo tools inakuwa rahisi kwako kuandika maudhui ambayo yatakuwa rahisi zaidi kunaswa na Injini za Mtandaoni kama Google, Ask na Bing. Umeshawahi kutumia CMS gani? Tuambie hapa leo..

Content Management System
mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

6. Tumia SEO Hapa sitasema mengi kwa sababu tumeshaongea mengi huko nyuma. Kifupi hii SEO (Search Engine Optimization) ni teknolojia iliyopo kwenye software za mtandaoni zenye uwezo wa kukusanya taarifa kutoka vyanzo mbalimbali kama websites, blogs, mitandao ya kijamii n.k

Cha kuzingatia zaidi unapofanya SEO ni matumizi ya Keywords sahihi kwa ajili ya soko lako ulilochagua kuhudumia (niche), Picha unazotumia lazima ziwe na maelezo tambuzi (alt text), matumizi ya links pamoja na ujuzi wa kuuza kwa kupitia maandishi(copywriting skills) Zingatia sana haya kwasababu hii ndio mbinu bora sana katika kufahamu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

Yaani SEO ni SUMAKU inayovuta taarifa kutoka sehemu mbalimbali za watu (open source information) na kuzigawa kwa mtu yeyote ambaye atatafuta taarifa hizo. Umeshaielewa jinsi SEO inavyofanya kazi sasa? Kufahamu zaidi fuatana na makala hii hapa;

7. Fanya Mara kwa Mara; Umeshayaona haya tuliyoyaelezea leo? Sasa kama unataka kufanikiwa katika kuipeleka mbali biashara yako huku mtandaoni, basi SIO LAZIMA uyafanye yote, aghalabu, unaweza kufanya matatu au manne ili ujiweke kwenye nafasi nzuri katika kuimarisha ushawishi wako huku Mtandaoni. Lakini katika kuzifanyia kazi mbinu hizi basi ni muhimu mbinu hizi uzifanye MARA KWA MARA, yaani uwe na consistency. Usifanye mara mbili kisha ukakata tamaa. Andika machapisho 500, tuma emails 2000, rudia na rudia. Njiani utagundua ile njia sahihi zaidi.

Umegundua nini kwenye makala hii ya leo? Umeshafahamu kiundani kuhusu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni? Una la kuongezea, swali au changamoto?

Tafadhali weka maoni yako hapa au kama unahitaji kuwasikiana nasi kupitia emails au Whatsapp, tafadhali fanya hivyo; Whatsapp/Call: +255765834754 Email: info@rednet.co.tz

thamani vs gharama, nafuu iko wapi? fahamu siri za kuweza kushawishi wateja katika biashara yako.

FAHAMU SIRI YA KUWEZA KUSHAWISHI WATEJA KATIKA BIASHARA YAKO

Umeshajiuliza, mtu mmoja anaweza vipi kuweka kitu mtandaoni akapata wateja wengi sana au kuzua mjadala kubwa sana, lakini wewe kila ukijaribu kuweka bidhaa/huduma zako bado hupati muitikio unaotakiwa? Nini huwa kinafanyika? Leo sasa fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako. Uko tayari?

Kuwa na mafanikio katika biashara kuna maana kwamba Mfanyabiashara ambaye ndiye mhusika mkuu ameweza kushawishi wateja kuweza kununua bidhaa/huduma zake kwa wingi. Hivyo mfanyabiashara lazima awe na maarifa/skills za kutosha ili kuweza kushawishi na kuuza kwa mafanikio.

MAARIFA HAYO NI YEPI?

Iwe ni kwenye mitandao ya kijamii, serikalini au mtaani, ili kuweza kuwa na ushawishi popote pale alipo mfanyabiashara, basi hana budi kuhitimu mafunzo katika nyanja ya kushawishi na kuuza (copywriting and closing skills). Mafunzo hayo si lazima uyapate darasani, leo hii utayapata hapa, soma makala hii mpaka mwisho tu:

1. MBINU YA MUITIKIO (RECIPROCITY): Kisaikolojia binadamu hujihisi kuwa na umuhimu pale anapouliza jambo fulani na kupata majibu ya kupendeza. Majibu mazuri humfanya mteja kuhitaji kuuliza/kuchimba zaidi ili aweze kupata hitaji lake ambalo mwishoni huangukia kwenye kununua. Unachotakiwa kukifanya hapa kama mfanyabiashara ni KUMSAIDIA mteja wako KUNUNUA na sio KUMUUZIA tu ilimradi upate pesa. Ukiuza tu unakuwa huna tofauti na wauzaji wengine unaowaona huko barabarani. Wewe unataka kuwa tofauti nao, si ndio?

Mfano: Kwenye mtandao wa twitter kuna watu wanaojiita “mabroo” (wale wenye followers wengi) ambao watumiaji wengi wa kawaida huwalalamikia kwa kushindwa kushiriki kwenye midahalo ya watu wengine isipokuwa wao wenyewe kwa wenyewe.

Sasa ukiwa mfanyabiashara hasa wa mtandaoni, sio lazima uwe na followers wengi ndo uwe na mafanikio, cha msingi ni kuwa na uwezo wa kumjengea mteja aitikie kile unakitoa kwake, na muitikio huo huanzia kwako kwa kujihusanisha nao kwenye mijadala na changamoto wanazokushirikisha kila mara. Hii ni kwasababu silaha kubwa unayoweza kuitumia kunasa wateja wengi zaidi ni kutengeneza MAHUSIANO mazuri na wateja wako. Hapo ndipo unapo fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako sasa.

mbinu ya muitikio katika biashara (reciprocity)
fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako

2. UFUNGANI (Commitment): Mara nyingi mtu akishajifunga kwenye jambo fulani, hubaki hapo akichuma anachokitaka. Sasa lazima uhakikishe biashara yako inakuwa kama Mgodi kwa wateja wako kuendelea kufaidi madini ambayo yamo kwenye biashara. Kwamba, lazima biashara yako itengeneze sumaku ya aina yake ili kuweza kushawishi na kunasa wateja wengi kila siku. Hizi ni zile Mbinu za kuweza kulifikia soko kubwa zaidi mtandaoni. Mfano wa sumaku muhimu ni TAARIFA, yaani ikiwa unauza viazi, basi wape wateja wako taarifa nyingi kuhusu viazi, kama unauza spare za magari waelimishe kuhusu spares mbalimbali za magari, kadhalika kwenye biashara zingine. Hii inapasawa kuwa inafanyika mara kwa mara, tena inaleta tija zaidi ikiwa itakuwa inatolewa BURE.

mbinu ya ufungani (commitment) katika biashara

Yaani hakikisha taarifa kuhusu unachouza au kuhudumu hazikauki kwa wateja wako. Kwa njia hii ndipo unapoweza kutengeneza sumaku ya kushawishi wateja wengi zaidi kujifunga katika biashara yako na kukuletea mafanikio unayoyaota. Na njia bora ya kutoa taarifa ni kupitia Website. Biashara yako ina website? Kama unayo hakikisha unaitumia vyema kwa ukuaji imara wa biashara yako. Zaidi unaweza kujua namna ya kutumia website kikamilifu kupitia hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

3. KUWA NA MAMLAKA: Hii ni siri muhimu sana. Watu hufuata na kusikiliza ushauri kutoka kwa mbobevu/mtaalam katika jambo fulani kuliko mtu yeyote tu asiyefahamika kwa utaalam fulani. Yaani ili uwe mtaalam lazima usome sana, uwe na uelewa mpana juu ya jambo fulani na uwe na confidence katika uwasilishaji wako ambayo itakupa mamlaka ya kutengenezea ushawishi unaotakiwa.

Hivyo, unapoongelea kuhusu bidhaa/huduma zako, ongea kama Mtaalam na sio muuzaji. Ukiongea kama mtaalam kwanza utajiamini zaidi, halafu zaidi utakuwa na mamlaka katika uwasilishaji wako jambo ambalo linavuta watu wengi kufanya biashara na wewe. Jaribu hii utanipa majibu yake.

4. UFANANO: Katika mbinu kongwe zaidi ambayo imetumika kutengeneza ushawishi duniani ni hii. Hata kwa waamini wa dini ya Kikristu mfano, imeandikwa “Neno wa Mungu akatwaa mwili, akakaa kwetu, nasi tukauona utukufu wake“. Yani Neno wa Mungu akajitwalia mwili ili afanane na watu ili lile kusudio lake la kuwaokomboa watu likapate kutimia.

Hali kadhalika katika biashara yako, lazima uhakikishe unatengeneza ufanano kati ya biashara yako, wewe mwenyewe pamoja na wateja wako. Hii hufanyika ili mteja ajiamini na kujihisi huru anapokujia ili aweze kutimiza hitaji lake.

mbinu ya ufanano katika biashara. Unafanana vipi na mteja wako?
fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako

Kumbuka biashara sio sehemu pa kujimwambafai kama wafanyavyo baadhi ya watu wa mitandaoni. Biashara ni watu, na watu lazima ujumuike na ufanane nao katika midahalo yao ya mara kwa mara ili kusudi waweze kukwambia mahitaji yao ambayo wewe ndiye mwenye dhamana ya kuyatimiza.

5. UADIMU (SCARCITY): Mara nyingi watu hupenda kumiliki vitu ambavyo wanavyovipenda na hawana. Mifano ipo mingi tu huko mtaani, jazia hapo. Unapouza bidhaa/kutoa huduma adimu/ambayo itakwenda kuisha baada ya muda fulani, watu hufanya haraka kununua ili wasije wakaikosa pindi itapopotea. Hivyo unapaswa kuzifanya bidhaa/huduma zako kuwa katika kiwango fulani cha uadimu ili kusudi umtengenezee mteja wako kiu ya kutaka kununua haraka iwekanavyo.

6. MKUMBO (BANDWAGON): Nadhani umeshawahi kuona hii. Hutokea pale bidhaa/huduma fulani inapotumiwa sana na watu fulani ambapo husababisha watu wengine kuitumia huduma hio. Mbinu hii imekuwa ikitumiwa sana na makampuni makubwa kwa kuwatumia wasanii/watu wenye ushawishi kwenye jamii ili wawe mabalozi na kutengeneza hali ya “mkumbo” ambao utasaidia bidhaa/huduma yao ikapate kutumika kwa wingi zaidi katika jamii. Kitaalamu mbinu hii hufanya kazi sana kuanzia maeneo ya Uswazi. Kama ulikua hufahamu, yaani fasheni zote kali za mjini huwa zinaanzia uswazi, mitindo ya kusuka, vyakula vizuri vipo huko, misemo, bidhaa nakadhalika.

Aina hii ya ushawishi si wafanyabiashara wote wanaiweza kuifanya na wala si dhambi ila ukiiweza ni moja ya mbinu bora kabisa katika kuhakikisha biashara yako inakuwa na ushawishi wenye tija kwa wateja wako. Unaweza kutengeneza mkumbo ili upate kutengeneza ushawishi wenye tija? Hebu tuone majibu yako..

SASA KWANINI MTEJA AKUCHAGUE WEWE?

Sio siri tena kuwa hisia ni silaha muhimu sana katika kujenga ushawishi katika biashara yako. Lazima uhakikishe unazijua vyema hisia za wateja wako na kuzitendea haki ipasavyo. Ufanyaje sasa ili kutibu hisia za wateja wako? Hakikisha una fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako hizi hapa.

1. WAFANYE WAJIHISI WAKIPEKEE: Kiafrika, mgeni anapokuja kwako hata kama kuna vita humo nyumbani, basi ni muda wa kuzika tofauti zote ili kuhakikisha mgeni anakirimiwa inavyotakiwa. Hii hufanyika ili mgeni huyo ajisikie vizuri na kwenda kutangaza yale mema aliyoyapata kwako.

Kunazo mbinu nyingi za kumfanya mteja akajihisi wa kipekee. Mfano kutabasamu na kusalimiana vizuri na watu kabla ya kwenda direct kwenye mambo ya kuuziana. Lengo ni kuendeleza ukarimu na hali ya urafiki makini katika kuhudumia mteja wako mara zote. Jambo hili ndilo huvutia zaidi.

unawezaje kupata wateja mtandaoni?
fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako

2. MSHIRIKISHE MTEJA KWENYE MAAMUZI: Moja kati ya vitu vinavyoweza kumfanya mtu yeyote awe mteja wako ni kitendo cha kumshirikisha katika maamuzi hasa yale yanayohusu namna ya kumhudumia kwa viwango. Washirikishe kwa njia ya kushikana mikono, bega au simu zenu za mikononi. Maamuzi ni muhimu sana na yanaathiri mwenenedo wa biashara kwa kiasi kikubwa sana. Hakikisha muda wote unafanya maamuzi sahihi. Unawezaje kufanya hivyo? Fuatana na mada hii hapa chini;

Jambo hili hutengeneza hali ya umiliki wa huduma/bidhaa kwa mteja hata kabla manunuzi hayajafanyika, kitu ambacho huchangia kiasi kikubwa mteja kuchagua kufanya biashara nawewe. Unaweza kucomment “viatu hivi unavyoviona vinakwenda sambamba na hio suruali yako, unaonaje ukakichukua hiki?” inachagiza sana mauzo mbinu hii.

mteja mshirikishe kwenye maamuzi. Msaidie aweze kununua huduma au bidhaa yako.
fahamu siri ya kuweza kushawishi wateja katika biashara yako

3. SIMULIA STORI: Mteja angependa kufahamu vitu kama, uliweza vipi kuanzisha hio biashara unayoifanya? Ulianzia wapi? Lini? Mteja wako wa kwanza ulimpata vipi? Umepitia changamoto zipi mpaka sasa na changamoto gani huwezi kuisahau? Stori yako inashawishi kwa kiasi kikubwa sana. Unatakiwa ujifunze namna nzuri ya kusimulia stori ili kuvutia wateja wengi zaidi. Stori hizo unaweza kuwa unazisimulia mara kwa mara kupitia akaunti zako za mitandao ya kijamii.

Kwenye hili mitandao ya kijamii ina nguvu ya ajabu sana. Unaweza vipi kuipata na kuitumia nguvu hio? Fuatana na makala hii hapa mpaka mwisho;

4. TOA AHADI ZA UKWELI: Unapomhudumia mteja ni vema ukamhudumia katika misingi ya uwazi na ukweli katika utoaji huduma zako au bidhaa. Kama kuna kasoro yoyote ni heri ukaiainisha mapema kwa mteja ili ajue namna ya kukabiliana na bidhaa/huduma hio. Haipendezi kutokuwa mkweli.

5. TOA HUDUMA KWA VIWANGO VYA JUU: Siku zote huduma bora huenda sambamba na Heshima kwa mteja, kuzingatia muda na kufuatilia kazi. Wasiliana na mteja wako mara kwa mara ili kujua muda wa kumpatia huduma. Cha msingi ni kutoa taarifa muda wowote inapotakiwa kufanya hivyo.

Hizi ndio siri za kushawishi wateja katika biashara yako wazidi kumiminika kila siku. Hakuna miujiza dunia ya leo. Hata hivyo si lazima utumie mbinu zote ulizozipata leo kwenye biashara yako. Unaweza kutumia mbinu moja au mbili au kadhaa ambazo kwa upande wako utaona zinakufaa zaidi. Ukiwa na swali, ushuhuda au changamoto tafadhali share nasi kupitia comments hapo chini nasi kwa pamoja tutajadili ili kuzitatua. Karibu sana Rednet Technologies.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mrahisishie mteja wako huduma za kifedha. Dunia ya leo si ya jana.