Tag: Je wajua

simu za michongo Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

FAIDA ZA KUTUMIA GOOGLE KAMA JUKWAA LA BIASHARA YAKO

Je, unaamini kwamba matumizi sahihi ya huduma za internet na mitandao ya kijamii yana uwezo wa kukurahisishia huduma/bidhaa zako zikapatikana kirahisi na wateja wako wakiwa popote duniani? Leo nataka nikupe stori kuhusu Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Tizama hapa, Siku moja asubuhi kabisa ya mwezi April mwaka huu 2022 nikiwa natoka home naelekea ofisini nikapigiwa simu, kutizama ni namba ngeni, nikatafuta utulivu kisha nikapokea;

Mimi: Hello, Habari za asubuhi!

Jamaa: Salama Faustine, I hope uko poa, Bwana mimi ni fulani (jina kapuni) nimekupigia kwa sababu nahitaji website na ningependa ifanywe na kijana mzawa. Nafanya kazi katika shirika (jina kapuni) ambalo ni la kimataifa. Nilikua napitia google pale nikaona kampuni yenu ya Rednet Technologies na nikaona pia kumbe mnajishughulisha na haya mambo. Itawezekana si ndio?

Mimi: Bila shaka hilo linawezekana kabisa, unahitaji lini hii kazi yako iwe imekwisha?

Jamaa: Well, ndani ya wiki 3 ningependa iwe imekwisha, sasa nitampatia namba yako mwenzangu yupo pale ofisini kwetu, yeye sasa atakupa maelezo ya kina. Lakini naomba kujua bei itakuwaje hapo (huku anacheka kwa ufupi)

Mimi: Gharama nitataja nikishajua requirements kaka, wala usiwe na shaka.

Baada ya kuwasiliana na huyo mwenzake akanirudia…

Jamaa: Faustine, naona mmeshaelewana, Sasa the reason tumekuja kwako ni kwasababu kuna mtu tulimpaga kazi ya kutengeneza hii website yetu, lakini hajawahi kutupa ushirikiano, kazi hajamaliza, changes hataki kufanya na tukimpigia simu harespond ndani ya muda, yani ana kiburi sana yule jamaa, kusema ukweli TUMEMCHOKA.

Mimi: (Kiukweli nilijiskia vibaya sana, ndugu zangu ule msemo wa “Mteja ni Mfalme” una maana kubwa sana hapa. Nikamwambia) Kaka, pole sana, utakavyokuwa unafanya kazi kwetu nakuahidi hio kadhia hutakutana nayo.

Jamaa: Kweli? Ok, turudi kwenye bei sasa, utatuchaji kiasi gani?

Mimi: Kwa nature ya Organization yenu hapo mpaka kazi inakamilika itacost 850,000/- tu.

Jamaa: Faustine, mbona bei ipo juu sana, tutaweza kufanya kazi kweli?

Mimi: Kaka, bei iko fair sana hio ukizingatia tutawatengenezea pia business emails BURE na kuwafanyia maintenance BURE kwa mwaka mzima. Anytime hapo mkitaka kufanya changes, tutazifanya BURE kabisa. Hapo unasemaje?

Jamaa: Hapo sio mbaya, walau naona dalili hautakuwa kama jamaa wa mwanzo. Ila bei bado hujashusha..

Mimi: Kaka, lipia 400k leo, baadae utalipa 250k, then finally tutakapomaliza kazi, utalipia 200k ambayo itakuwa imebaki. Hapo je?

Jamaa: Ok, Nataka na hio website pia iwe inapatikana mtu akisearch Google, ili wateja watupate kama sisi tulivyokupata wewe.

Mimi: Ahaa, hio sasa ni huduma nyingine, inaitwa Search Engine Optimization (SEO). Ndo inaiwezesha website kupatikana google.

Jamaa: Na hio utatuchaji au bei yake ndio inakuja na ya website direct?

Mimi: Hio gharama yake ni tofauti kaka.

Jamaa: Ambayo ni ngapi? Usinilalie bwana ndugu yangu.

Mimi: Hio kwa sababu ni kazi ya muendelezo, utakuwa unalipia kila mwezi, ambapo gharama yake ni 100,000/- tu.

Jamaa: sema Faustine mna bei nyie. Ehe niambie, kwenye hio laki 1 mtakuwa mnafanya nini na nini?

Mimi: Hapo tutakuwa tunakuandikia makala (blog posts) mbili kwa mwezi ambazo zitahusu shughuli mnazofanya, tutaweka picha, pamoja na kuzioptimize ili iwe rahisi kupatikana google mtu akiwa anatafuta taarifa zinazowahusu.

Jamaa: Faustine, hapo umeniweza. Basi wacha tuandae contract, halafu next week tutakuita ili tusign, kazi ianze mara moja. Ila usiniangushe bwana.

Mimi: Kaka wala usiwaze, tufanye kazi.

Basi Bwana baada ya simu hio ndio uhusiano ukajengwa na kazi ikaanza kama hivyo.

Na baada ya kazi hio kuisha, jamaa yetu aliweza kutuunganisha kwa watu wengine watano (5) ambao walitamani kupata huduma kama ambayo aliipata kutoka kwetu. Na hatimaye wamekuwa wateja wetu wa kudumu. Unadhani hao walivutiwa na nini? Fuatilia makala hii hapa kufahamu siri za utoaji huduma bora kwa wateja.

Unachoweza kujifunza ili uweze kuzipata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Katika mazingira ya kazi, hasa huku mtandaoni ambapo mara nyingi tunakutana na watu tusiowafahamu (strangers) ni muhimu sana kuzingatia haya yafuatayo;

1. KAULI NJEMA

2. UAMINIFU

3. KUMJALI MTEJA na MAUMIVU YAKE (Mara kwa mara muulize kama anaridhika na huduma anazopata kutoka kwako na nini unaweza kufanya ili kazi yake ifanyike kwa ubora anaotarajia).

Kauli Njema zitakufunulia fursa nyingi na kukuletea wateja wengi sana huku mtandaoni, acha tabia ya kutukana, kudhalilisha au/na kudharau watu. Kumbuka teknolojia haisahau.

Uaminifu utajenga uhusiano mzuri na wa kudumu na mteja wako.

Kumjali mteja kutafanya azidi kukupa kazi nyingi zaidi mbeleni, na hata kukuunganisha kwa watu wake wengine anaowafahamu.

Siri ya kufanya kazi vizuri na mteja ipo kwenye hayo mambo matatu. Ukiyazingatia, hakika huwezi kufeli. Zaidi kama unahisi bado hujajua namna unaweza kushawishi mteja kwenye biashara yako fuatana na makala hii hapa tumekuandalia.

HABARI NJEMA KUELEKEA MSIMU WA SIKUKUU

Sasa kuelekea mwisho wa Mwaka tunakupa ZAWADI ya kuifikisha biashara yako mtandaoni na kukusanya wateja kutoka kila pembe ya nchi. Fungua website leo kwa 500,000/- tu (badala ya 850,000/-) upate na huduma ya SEO BURE (badala ya 100,000/- kwa mwezi) maintenance BURE mwaka mzima pamoja na Ushauri BURE kabisa. Hata hivyo, ZAWADI hii haitamfikia kila mtu. Zawadi hii ni kwa watu 10 tu wa mwanzo, na itadumu mpaka tar 10 December. Baada ya hapo tunakwenda likizo ya Christmas.. So kama unahitaji ZAWADI hii WAHI nafasi mapema ili pia uzipate Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

OFA ya Msimu wa Sikukuu 2022
Sherehe za Christmas na Mwaka Mpya Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Baada ya OFA hii ukihitaji website ni 850,000/-, huduma ya SEO ni 100,000/- kwa mwezi na pia tutafungua group la Whatsapp kwa yeyote atakayehitaji ushauri au atayehitaji kuuliza jambo lolote kuhusu Website, SEO, Social Media Marketing, Digital Marketing na Tech kwa ujumla wake. Kuingia kwenye group hilo itakugharimu 5,000/- tu kwa mwezi.

So ukiliona Tangazo hili, mtaarifu na mwenzako ambaye unahisi atahitaji kunufaika na ZAWADI hii.

Wewe kama unafanya biashara, basi kama unataka kufanya vizuri sokoni, hakikisha unajenga URAFIKI na wateja wako. Hii ni kwa sababu ni rahisi sana MTEJA kuwa RAFIKI yako kama utatengeneza UHUSIANO mzuri kati yenu. Hii ndio SIRI ambayo hakuna mtu atakwambia kirahisi.

Kufanya biashara mtandaoni ni Uwekezaji muhimu sana, na kwa maendeleo yaliyopo kwa sasa duniani, imekuwa ni rahisi mno kutumia huduma za Internet katika kuwafikia wateja popote walipo duniani.

Kuna mtu aliwahi kuniuliza, “Sasa nawezaje kutumia Internet kufanya biashara yangu?”

Jibu: Unaweza fanya haya yafuatayo ili uweze kupata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.:

1. Tumia Website na mitandao ya kijamii kutoa elimu kuhusu bidhaa/huduma zako.

2. Tumia SEO ili kurahisisha maudhui yako yanapatikana kirahisi katika Google.

3. Fanya matangazo (Paid Ads/Sponsored Ads) ili kuwafikia wateja wengi kwa haraka.

4. Jifunze kuuza katika Maandishi (Copywriting). Jaribu kadiri unavyoweza.

5. Tumia WhatsApp yako vizuri kibiashara (Status, Broadcast, Groups n.k).

Ukiona haya yanakuwa magumu kwasababu upo busy au vinginevyo, usikubali sasa biashara yako ife/ishindwe kufanya vizuri mtandaoni.

Tafuta mtaalamu wa kufanya biashara mtandaoni, mpe targets zako, kubaliana nae katika malipo, kisha mpe kazi ili biashara yako izidi kupaa mtandaoni kwa sababu ni muhimu sana ukazipata hizi Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako. Sio lazima kila kitu ukifanye wewe mwenyewe kwa sababu hakuna ajuaje kila kitu.

Ni mategemeo yangu umepata kitu kipya leo. Kumbuka ZAWADI yetu ya kufunga Mwaka inakwisha tarehe 10 December, halafu hii ni maalum kwa watu 10 tu watakaowahi kujinyakulia website zao.

Tutumie ujumbe sasa hivi au tuchek kupitia mawasiliano haya;

Call/WhatsApp: +255765834754

Email: info@rednet.co.tz

10 ZA JE WAJUA?

Kama unajua ni kheri, sasa unapata nafasi ya kujua zaidi. Na kama ulikuwa hufahamu basi leo unapata nafasi ya kujua mambo mapya zaidi. Katika jukwaa letu la @ElimikaWikiendi . Sasa leo tuzione zile 10 za je wajua katika Teknolojia na Biashara.

1. Je, wajua kuwa tovuti ya kwanza kabisa kuundwa duniani bado ipo hewani? Hii hapa kwenye link http://info.cern.ch Tovuti hio imetengenezwa kwa kutumia lugha ya HTML na inaonyesha mistari michache tu.

chanzo: https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-teknolojia-ya-intaneti-na-kompyuta-katika-biashara-yako/

2. Ile Teknolojia ya kuongeza uwezekano wa Taarifa kupatikana kwa urahisi na kiwango cha juu katika injini za mitafuto za mtandaoni (Search Engine Optimization, SEO) ilianzishwa mwaka 1991. Teknolojia hii ina umri mkubwa kuliko GOOGLE ilioanzishwa mwaka 1998.

3. Mtandao maarufu wa kutizama mubashara filamu na tamthilia wa NETFLIX ulianzishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1997 huko Carlifonia nchini Marekani. Mtandao huo una umri mkubwa kuliko YouTube ambayo ilianzishwa mwaka 2005. Tuambie, Netflix umeijua lini wewe?

4. Takriban 10% ya pato la Taifa kwa nchi za Kusini mwa Afrika huchangiwa kupitia huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi. Hii ni zaidi ya 7% ya GDP kutoka Asia na chini ya 2% ya GDP kutoka sehemu zingine dubiani.

chanzo: https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/

5. Kusafirisha gari kutoka Japan mpaka Abidjan nchini Ivory Coast (km 14,075) hugharimu $1500. Lakini kusafirisha gari hilihilo kutoka Abidjan hadi Addis Ababa(km 6626) inagharimu takriban $5000. Gharama hii ni ghali mara 3 zaidi ya ile ya kutoka Japan.

Pia kusafirisha gari ndogo kutoka Japan mpaka Dar es salaam (km 11,256) inagharimu $900 bila makato na kodi. Hata hivyo, kusafirisha gari hilo hilo kutoka bandari ya Dar es salaam mpaka jijini Lusaka (km 1937.3), Zambia inafikia $650 bila makato na kodi.

Kutokana na hali duni ya miundombinu, gharama za usafirishaji barani Afrika ni kati ya zile ghali zaidi duniani. Hii pia huletwa na viwango vikubwa vya forodha, tozo za ucheleweshaji, ajali pamoja na ukosekanaji wa fursa zingine.

chanzo: https://rednet.co.tz/usafirishaji-na-miundombinu-katika-ustawi-wa-biashara-afrika/

6. Kufikia Octoba 2018, duniani tovuti bilioni 1.9 zilikuwa zipo hewani (online). Pia kuliripotiwa kuwapo na machapisho mapya (posts) zaidi ya milioni 5 kila siku kutoka kwenye tovuti na blogu mbalimbali duniani. Fikiria leo hali iko vipi..

chanzo: https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-teknolojia-ya-intaneti-na-kompyuta-katika-biashara-yako/

7. Kila siku kunaongezeka watumiaji wapya wa huduma za Intaneti takriban milioni moja duniani kote. Kwa wastani mtumiaji wa kawaida hutumia masaa 6:42 akiwa mtandaoni kwa siku. Kama wewe ni mjasiriamali bila shaka umeshaona fursa hapa.

8. Unalikumbuka shambulizi lililoitwa NOTPETYA? June 27, 2017 malwares hizo ziliathiri kutoka biashara ndogo za software nchini Ukraine mpaka kusambaa duniani kote. Hilo liliitwa “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA DUNIANI”

chanzo: https://rednet.co.tz/yafahamu-mashbulizi-ya-kimtandao-cyber-attacks-na-athari-zake-katika-biashara-kampuni-yako/

9. June 23, 2020 Jumuiya ya SADC ilipitisha muongozo wa kurasinisha(to harmonize) shughuli za kibiashara baina ya nchi wanachama. Sasa mtu akisema watu waende Burundi kutafuta unafuu wa maisha, watu watatumia fursa hio wakaenda Zambia na kwinginepo ndani ya nchi wanachama wa SADC kufanya biashara na maisha yataendelea kama kawaida.

chanzo: https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-urasinishaji-harmonization-katika-biashara/

10. Kufikia mwaka 2022, mwakani tu hapo, 10% ya watu duniani watakuwa wakivaa nguo zilizounganishwa na Intaneti. Imagine nguo yako ina lebo ambayo inaweza kutumika kama tiketi ya kuingia kweny muvi, mpirani au club. Baunsa anascan nguo tu mzigo unajipa.

BONUS: Serikali za duniani zitaanza kutoza kodi katika jukwaa la Blockchain kwa mara ya kwanza mwaka 2023. Sasa wale Traders na Investors wa Bitcoins na Cryptos kupitia Blockchain mjiandae kisaikolojia mkimalizia Tax-holiday yenu huko kwenye Blockchain.

Hayo ndio tuliyotaka kukujuza leo katika 10 za je wajua. Jambo lipi limekushangaza zaidi? Tujuze katika comments hapo chini kisha share makala hii kwa ndugu, rafiki na jamaa zako ili nao wapate kufahamu haya tulokujuza leo.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mpesa lipa namba ya Rednet Technologies.
Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako (Business Intelligence)?

JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI?

Imagine una ofisi yako (eneo la biashara) na pia unayo akaunti yako ya twita, Instagram au facebook. Lakini hujui namna ya kutengeneza mvuto kwa watu ili wakutafute, wakufollow, wakuamini na wafanye biashara na wewe. Unafanyaje? Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji tosha? Fuatilia makala hii mpaka mwisho kufahamu kiundani.

Imagine hujawahi kutengeneza mahusiano ya kibiashara na followers wako, hata mmoja yani, na kila siku upo mtandaoni kufuatilia habari mpya zinazojiri kwenye Bongo Fleva, Bongo Muvi, Mpira, Umbea, Siasa n.k. Kuna muda unatamani biashara yako iwe kubwa lakini hujui mbinu gani unaweza kutumia ili kuhakikisha biashara yako inazidi kuwa Imara kila siku. LEO hii Nazungumza na wewe hapa.

1. CHANGAMKA KIBIASHARA UWAPO MTANDAONI:

Kabla ya yote, fahamu kuwa biashara inafanyika vizuri katika mazingira yaliyojengwa kwa mahusiano imara, hivyo hebu tizama unahusiana vipi na watu waliokuzunguka na followers wako. Hili ni eneo pana ambapo unatakiwa ufahamu saikolojia ya watu wako hasa wateja na kujua namna ya kukabiliana nao positively. Maana mitandaoni kuna kila aina ya watu na tabia zao, kuna wenye kiburi, kuna wababe, wachechi, wajeuri, wanafunzi, wenye hekima, wapole, wenye lugha chafu na micharuko. Sasa jukumu lako ni kuwajua na kukabiliana nao bila kukwazana. Cha kufanya ni kuhakikisha unatumia vizuri bando lako tu hapa.

Mtandao saidizi jinsi ya kukabiliana na hasara kwenye biashara mbinu za kuwa tajiri

Humu mitandaoni wewe kama sio mtu maarufu basi hakikisha unakuwa mchangamfu kwa kadiri ya inavyowezekana. Kuwa “mchangamfu” haina maana uwe mwenye kiherehere, shobo au mtu wa kujipendekeza, lakini ujue namna kuchangia mijadala mbalimbali na kujihusanisha na watu vizuri.

2. JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI WA KUJIJENGA KUWA MTAALAM?

Kwenye biashara hili ni eneo muhimu sana, yani sawasawa na uti wa mgongo. Watu wengi hudhani biashara ni kuuza na kununua tu, of course wako sawa. Hata hivyo ili biashara yako iweze kunawiri katika mazingira ya mtandaoni yaliyojaa ushindani wa kila aina, unapaswa kujua zaidi ya “kuuza na kununua”. Humu mtandaoni watu hukwepa sasa matangazo, hivyo “unapoweka tangazo lako hakikisha halionekani kama TANGAZO bali lionekane kama HABARI MPYA kwa yeyote anayesoma.”

Mtego ndo upo hapo. Lazima uwe mtaalam wa kuhudumia faida zinazotokana na bidhaa/huduma zako. Usiuze tu ukaishia hapo, hebu kuwa MLEZI wa mteja wako. Binafsi nina LIST ya wateja wangu ambapo huwa nawatumia updates mbalimbali kuhusu hali ya biashara na uchumi katika muktadha wa teknolojia BURE kabisa. Ungependa kuwa kwenye list hio? Nitumie ujumbe kwa WhatsApp sasa hivi kwa kugusa namba hii hapa 0765834754

3. JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI WA KUFUNGUA WEBSITE:

Kwa kasi ambayo teknolojia inakwenda nayo nina uhakika usingependa kupitwa na fursa lukuki zinazokoja na mapinduzi haya ya 4 ya viwanda yanayoendelea duniani. Fikiria, Kusini mwa Jangwa la Sahara kunakadiriwa kuwa na watumiaji wa internet zaidi ya milioni 400. Nchini Tanzania kunaripotiwa kuwa na watumiaji wa internet zaidi ya milioni 29 mpaka kufikia mwaka 2022 Kwa mujibu wa ripoti ya TCRA.

jinsi ya kuanzisha website

Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji

Sasa kwa kutumia hilo Bando lako la internet, unalitumiaje kuwafikishia watu hawa bidhaa/huduma yako? Website ni kifaa (Digital tool) muhimu na mahsusi kwa kuwafikia watu wengi ndani ya muda mchache sana. Kwenye website unao uwezo wa kutoa huduma za kushauri na mafunzo nakdhalika. Zaidi unaweza kujua faida za kuwa na website kupitia hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?

Kuweza kupata website yako wasiliana nasi kupitia namba 0765834754 au email info@rednet.co.tz ili tukusaidia kutatua changamoto zinazokukabili. USIBAKI NYUMA.

4. JE WAJUA KUWA BANDO LAKO NI MTAJI WA KUWA MKWELI/AMINIKA UKIWA MTANDAONI:

Moja kati ya eneo ambalo linawapa changamoto wafanyabiashara wengi ni hili la kuwa mkweli na Muaminifu. Wateja wengi huwa wanakwazika sana wanapofanya kazi na wafanyabiashara ambao si wakweli/waaminifu. Hiki ni kitu kibaya sana na hata wewe usingependa kikutokee.

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi? gharama vs thamani, kipi kinafaa zaidi?

Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji

Unapojijenga kwa kuwa mkweli unatengeneza mazingira ya kuaminika ambayo yatakufanya upendwe na watu na wao waweze kufanya biashara na wewe bila wasiwasi. Hata wewe mfanyabiashsra, siku ukiwa mteja usingependa kukutana na mtoa huduma ambaye si mkweli/mwaminifu, si ndio?

Ni matumaini yangu umegundua kwamba Bando lako ni Mtaji muhimu sana katika uendeshaji wa biashara yako katika zama hizi za kidijitali? Lazima ujue namna nzuri ya kuendesha akaunti yako ya mtandao wa kijamii ili ilete tija kiuchumi katika biashara yako. Unahitaji mtu wa kuendesha akaunti yako? Wasiliana nasi mara moja.