Tag: iot

cloud data storage

MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA

Teknolojia ya Internet of Things (IoT) inakuja kwa kasi sana. Mtandao wa Gartner uliripoti kuongezeka kwa vifaa vinavyounganishwa na huduma za internet kufikia 26 bilioni mpaka mwaka 2020. Sasa haya mageuzi ya intaneti (IoT) katika biashara na maisha ya mchango gani? Fuatana na makala hii mpaka mwisho kuahamu zaidi.

Leo hii utakapomaliza kusoma makala hii utafahamu kiundani juu ya namna Teknolojia ya Intaneti katika Vitu (Internet of Things au IoT) inavyoweza kubadili Biashara yako pamoja na vifaa vya kielekroniki unavyotumia nyumbani ama ofisini.

Maeneo kumi (10) muhimu ambapo mageuzi ya intaneti (IoT) katika biashara na maisha, inakwenda kuyagusa na kuleta mabadiliko makubwa katika mazingira ya kazi na jamii. Namba 7 itakushangaza sana:

1. IoT itapofika kwenye ubora wake wa matumizi, biashara nyingi zinazofanyika leo zitapotea sokoni. Mf: biashara za ugavi na usambazaji ambazo kwa sasa hutumia mtu wa tatu katika kufanya usafirishaji/usambazaji, hizi zitaweza kujiendesha kiautomatiki, yaani ukiagiza kitu mtandaoni inakupa namna ya kukufikishia bidhaa/huduma popote bila hata kujieleza. Fikiria upo Magomeni na unaagiza mafuta mtandaoni kutoka Singida, unapotoa oda yako tu, huna haja ya kusema uko wapi, unapokea zako tu ujumbe kuwa “mafuta yako yatakufikia siku fulani saa fulani mahali fulani (Mahali ambapo unakuaga muda mwingi). Life’s Simple.

mageuzi ya Intaneti (iot) katika biashara na maisha.

Jihudumie leo kutoka Rednet Technologies.

2. Moja kati ya athari hasi za IoT ni pamoja na kumlazimu mtumiaji kuhakikisha vifaa vyake vinavyotumia intaneti na vilivyoungwa katika teknolojia ya IoT vinakuwa updated muda wote. Hii itaongeza gharama za bando japokuwa “Mtaka cha uvunguni sharti ainame.”

3. Mpaka kufikia 2025 soko la IoT linatarajiwa kuwa na thamani ya kati ya 3.9 $ mpaka 11.1$ trilioni kwa mwaka. Vihisishi (Sensors, RFID na Bluetooth devices) vinatajwa kuchukua zaidi ya 50% ya matumizi ya IoT vikifuatiwa na huduma za Teknolojia ya Habari (IT). hapa ndipo utakapoona sasa mageuzi ya intaneti (iot) katika biashara na maisha kwa ujumla.

4. Soko la Biashara Kwa Biashara (B2B IoT Market size): 2015: soko lilikuwa na thamani ya $195 bilioni na kufikia mwaka 2020 soko lilifikia thamani ya $470 bilioni ikiwa ni ongezeko la zaidi ya dola bilioni 250 ndani ya miaka mitano tu. Yaani IoT imeimarisha sana mapato katika biashara katika nyanja za mifumo ya udhibiti, uchambuzi wa data, vifaa, network na huduma bora. IoT imekuwa mkombozi haswa.

Mfano mzuri hapa ni mifumo ya ukusanyaji kodi ya TRA. Mifumo hio imefanywa imara katika kudhibiti makusanyo ya kodi kupitia mashine za EFD ambazo zimeungwa kielektroniki ili kuwapa TRA data sahihi za kodi.

mageuzi ya intaneti (iot) katika biashara na maisha.

5. Ukuaji wa IoT unaathiriwa kwa kiasi kikubwa na maendeleo ya Teknolojia zingine. Mfano: Teknolojia ya mawingu (cloud tech) inavyokuwa na IoT nayo inakuwa sambamba. Pia IoT inasambaa kwa kasi pale uwezo wa mitandao unaposambaa zaidi. Kifupi ni ngumu kuzuia kasi ukuaji wa IoT duniani.

6. IoT itapofikia ubora wake kwenye matumizi, inatarajiwa kuwezesha kufikia vifaa vingi kwa kutumia kifaa kimoja. Fikiria unarudi zako home, ukifika nje unawasha taa za nyumba, then unawasha feni, TV na sabufa yako na kuzima Friji yote kwa kutumia simujanja yako tu yani.

7. Unazijua RFID’s? Hizi kitaalamu zinaitwa Radio-Frequency Identifications. Yani vifaa vyenye uwezo wa kuratibu utambulisho wa bidhaa/huduma. Mfano vile vitochi unaviona ukienda supamaketi pale kabla hujalipia, bidhaa yako inamulikwa na mwanga flani hivi ili kujua bei. Sasa kile kitochi kinaitwa RFID scanner. Hizi skana zipo za aina nyingi kwa minajili ya kutambua bidhaa/mtu, zingine zipo viwanja vya ndege kukagua mizigo, watu na pasi za kusafiri.

RFID’s zinahusika vipi kwenye IoT?

Teknolojia ya IoT sasa inaziwezesha hizi RFID’s katika sekta ya Ugavi na Usafirishaji ili kutoa data sahihi kuhusu ubora na idadi ya bidhaa zinazosafirishwa na kutumiwa. Kupitia IoT bidhaa inaweza kujulikana ipo wapi na lini imenunuliwa inapopita kwenye skana ambayo hutuma taarifa sahihi za bidhaa kwa mtengenezaji. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa RFID’s katika nyanja ya Biashara na Uchukuzi tafadhali gusa link hii MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI

8. Namba ya Vifaa vya kielektroniki vinavyoweza kuwasiliana pasi na kuingiliwa na mtu M2M (Machine To Machine) inatajwa kuongezeka kwa kasi kubwa ndani ya muda mchache tu. 2018 kulikua na vifaa 1.5 bilioni na mwaka 2020 viliongezeka kufikia 2.6 bilioni. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya mtandao wa Statista.

9. IoT ndio suluhisho sahihi katika kutoa huduma bora zaidi kwa mteja. Yani unapotumia teknolojia ya IoT katika biashara yako, unampa mteja nafasi ya kupata huduma nyingi (mfano: kununua bidhaa/huduma, kujisafirishia na kutoa maoni) ndani ya site moja kirahisi.

10. Kuongeza Mapato: Kwa kutumia IoT matumizi katika biashara yanapungua sana kwa kuwa shughuli nyingi zinafanyika kiautomatiki kupitia mawasiliano baina ya vifaa vinavyotumia huduma za intaneti. Hakuna tena gharama kubwa za usafiri wala kukusanya data. Kifupi, yajayo yanafurahisha sana katika IoT. Makampuni mengi duniani tayari wameshanza kutumia huduma hizi yakiongozwa na makampuni ya Ugavi na Usafirishaji kama DHL, XPO Logistics na FedEx.

Biashara zinazotumia IoT hujikuta zikitumia gharama ndogo na thamani kubwa sana katika kujiendesha, jambo linalowafanya waweze kujitanua zaidi na kupata mapato lukuki. IoT ndio teknolijia ya kibiashara haswa na wajanja ndio wanaoifaidi. Usisubiri uachwe.

Kuna msemo mmoja maarufu katika IoT unasema, “If an electronic device can be connected, it should get connected” yaani, “Kama kifaa kinaweza kuunganishwa, basi na kiunganishwe”. Msemo huu ndio kwa kiasi kikubwa unaipa nguvu kasi ya IoT kuenea duniani. Umegundua nini kwenye makala hii kuhusu mageuzi ya intaneti (iot) katika biashara na maisha? Tuambie kwenye comment hapo chini,..

Vyanzo: https://www.statista.com/statistics/1194677/iot-connected-devices-regionally/

https://www.huffpost.com/entry/8-ways-the-internet-of-th_b_11763836

https://www.newgenapps.com/blog/impact-of-internet-of-things-on-the-business-world/

mapinduzi ya viwanda

FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA KATIKA BIASHARA DUNIANI

Japokua ilipitwa na zama 3 tayari, lakini sasa Afrika imedhihirisha kwamba haitaki kupitwa tena katika Mapinduzi ya 4 ya viwanda Duniani. Hii ni kutokana na kukua na kuimarika katika sekta za Afya, Elimu, Biashara, Teknolojia pamoja na Mahusiano na Muingiliano wa kijamii ikichagizwa na maendeleo katika miundombinu, usafirishaji na mitandao ya kijamii. Leo tuta fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. Ni nini na yanaashiria nini kwenye maendeleo ya biashara zingine? Makninika mpaka mwisho.

Mwezi September, 2019, jijini Cape Town Afrika Kusini ulifanyika mkutano wa kiuchumi wa WEF (World Economic Forum) ambao unazishirikisha nchi mbali mbali duniani, wafanyabiashara pamoja na wadau wa uchumi.

Mwaka huo 2019 viongozi waliokutana kujadili mustakabali wa Afrika walikua na jambo la msingi sana ambalo linatumainiwa kuleta maendeleo katika uchumi barani ambalo ni Utekelezaji wa Kuanzishwa kwa Eneo Huru la Biashara Barani (African Continental Free Trade Area AfCFTA). Baada ya miaka mingi ya mazungumzo, makubaliano yamefikiwa ya jinsi ya kuvunja vikwazo vya kibiashara, kukuza uchumi na kuunganisha nchi ambazo katika historia zilikuwa na mahusiano mazuri ya kibiashara na bara Ulaya, Amerika na Asia. Kufahamu zaidi gusa hapa chini:

Changamoto; Afrika (wafanyabiashara, kampuni na mashirika) imejifunza nini katika Kongamano hilo la Kiuchumi (WEF)? Na zaidi, Afrika inajiandaa vipi na Mapinduzi ya 4 ya viwanda yanayoendelea duniani?

Kufikia mwaka 2018 Afrika peke yake iliripotiwa kuwa na vijana takribani milioni 200 wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24. Na namba hio inatajwa kuongezeka mara mbili kufikia mwaka 2050.

Sasa “Kuwa na bara lililosheheni vijana ni fursa adhimu sana, lakini vile vile ni tishio kubwa.” alitahadharisha Albert Zeufack, Mchumi Mkuu wa Benki ya Dunia barani Afrika. “Ni tishio kama hatutohakikisha idadi hio ya vijana hawaanzi kufanya kazi inavyotakiwa.” Sasa kufikia Mapinduzi ya 4 ya viwanda, maeneo kadhaa yaliangaziwa na kituo cha mabadiliko ya kiuchumi barani (Africa Center for Economic Transformation, ACET) kwa niaba ya Benki ya maendeleo barani AfDB.

africa na mapinduzi ya viwanda

1. MACHINE LEARNING/ARTIFICIAL INTELLIGENCE/ROBOTICS;

Fikiria kuhusu gari inayojiendesha bila dereva na kufuata sheria na alama za barabarani ipasavyo ikijumuisha foleni. Watu wengi wangesita kupanda katika gari inayojiendesha yenyewe bila dereva, lakini hayo ndio mapinduzi halisi ya viwanda kupitia teknolojia.

Pia eneo hili limeshuhudiwa na ubunifu mwingi ukiwemo; mashine za kisasa za kuvuna na kupembua nafaka na madini, mifumo ya kiautomatiki inayoendesha ndege, meli pamoja na Teknolojia ya kupima udongo. Ni wazi mashine zinaweza kufanya kazi zifanywazo na binadamu katika zama hizi za mapinduzi ya 4 viwanda.

Swali, umejiandaeje kulinda taaluma yako dhidi ya zama hizi za mashine kujifunza (machinelearning) pamoja na teknolojia ya akili isiyo ya asili (ai)?

2. INTERNET OF THINGS (IoT);

Vifaa vingi vya kielektroniki vinavyotumiwa na mwanadamu sasa vinao uwezo wa kuingiliana na vifaa vingine kirahisi katika kurahisisha utendaji. Fikiria pale unarudi nyumbani na kuwasha feni yako kwa kutumia simu yako ya rununu (smartphone). Au kuweza kuendesha jokofu lako kwa kutumia teknolojia ya RFID. Kuunganishwa vifaa vya kielektroniki na huduma za intaneti imerahisisha sana mfumo wa mawasiliano na manunuzi ambao umeinua uchumi japo faida zake bado hazijasambaa sana barani Afrika.

Fikiria vile unaweza nunua bidhaa katika duka bila kumwona hata muuzaji. Hii inawezeshwa na teknolojia za biashara za kielektroniki (ecommerce) ambapo mteja anaweza kulipia kwa kutumia kadi yake ya benki au huduma za kifedha za simu ya mkononi kama MPESA na tigopesa. Katika bara ambalo muingiliano ni mkubwa kama Afrika, hili ni jambo la kutilia maanani sana, haswa wakati huu ambapo unajaribu ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. (Ambapo sisi kama Rednet Technologies ni wadau wakubwa kuhakikisha hupitwi na huduma za kisasa kwa kutumia teknolojia).

Kufahamu mapinduzi ya IoT katika biashara na maisha kwa ujumla tayari tumekuwekea makala maalum kupitia link hii hapa MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA

3. DATA MINING/DATA SCIENCE TECHNOLOGIES;

Kituo cha ACET katika mwaka 2018 kiligundua kwamba “kuvua taarifa nyingi mtandaoni, kwa kutumia kompyuta zenye uwezo mkubwa na kanuni za mifumo ya Akili isiyo ya Asili (AI), huwezeshwa kupatikana kwa ripoti bora ya taarifa sahihi.” Fikiria mifumo ya tiketi za ndege, hoteli, mifumo ya kulipa kodi na taarifa za mteja wa benki.

Sekta ya Takwimu inafurahia sana ujio wa teknolojia ya Kuvua/Kuvuna Taarifa na Sayansi ya Taarifa. Jinsi ya utendaji katika teknolojia hii ni fursa adhimu sana katika kuimarisha biashara kwa kutumia takwimu sahihi zilizovunwa kutokana na taarifa mbalimbali za watu. Mifumo ya tiketi za ndege, Usajili wa vyumba vya Hoteli, taarifa za wateja wa benki na hata mfumo wa Kulipa kodi (Tax returns), hivi ni baadhi ya vyanzo vya ukusanyaji wa taarifa muhimu katika kufanya Uvunaji wa Data na Sayansi ya Data. Serikali za Africa zinamiliki kiwango kikubwa cha taarifa hizi. Je, italeta manufaa kwa Umma au itafanywa kama biashara na wajasiriamali? (Tafiti na ripoti tunazokuwekea kwenye makala zetu hizi zitakupa majibu.😋)

4. 3D PRINTING;

Ama kwa hakika mapinduzi ya viwanda yanakuja na mengi. Hebu buni bidhaa yako kwenye kompyuta halafu ichapishe kama ilivyo. Kutoka ubunifu uliotengenezwa kimchoro mpaka uhalisia katika kuchapisha tu, hii inakwenda kubadili hata namna ya uendeshwaji wa viwanda barani Africa ambapo ugunduzi huu unaleta matumaini katika uwanda wa ubunifu na ujenzi ambao unatazamiwa kuleta maendeleo katika nchi za Afrika. Viwanda vinawezaje kuendana na teknolojia hii ya Uchapishaji? Vimal Shah mkuu wa shirika la viwanda vya BIDCO nchini Kenya mwaka 2017 alinukuliwa akitania, “Tunaweza kuchapisha pizza wakati ujao.”😂

Sasa watunga sera na sheria barani walishaona uhalisia huu kama kuchapisha mfano wa kitu halisi (3D-Printing) katik mipango yao ya muda mrefu?

5. BLOCKCHAIN/TRUST TECHNOLOGIES;

Mwaka 2018 kituo cha ACET kiligundua kwenye uchunguzi wake kwamba teknolojia ya Blockchain inawafanya watu hata wasiaminiana au kujuana, kuweza kushirikiana bila ya kuwa na haja ya kwenda kwenye mamlaka za serikali. Yaani Blockchain ni jalada huru linalosajili miamala ya kifedha kati ya watu wawili au zaidi kwa usahihi na njia bora zaidi. (Tulishaelezea kuhusu Blockchain na cryptocurrencies kwenye makala zetu zilizopita). Sasa itakuaje kwa huduma za kibenki, wanasheria, wakala wa fedha (brokerage firms) na wahusika wa kiserikali katika maswala ya kifedha? Kitawakuta nini, tutajadili kwenye athari ya mapinduzi ya viwanda mbeleni.

mapinduzi ya viwanda

Si ajabu, teknolojia ya Blockchain inaonekana kama mkombozi dhidi ya vitendo vya Rushwa kutokana na undeshwaji wake ulio sahihi na wa haki. Kwa inavyoonekana teknolojia hii ya Blockchain inakwenda kuwa pigo kubwa kwa watu wenye misuli ya kiutawala, madikteta wa waendeshaji wa siasa chafu. Itakapofika siku Teknolojia hii imefikia matumizi yale yaliyonuiwa wakati inaanzishwa, basi wahafidhina na mawakala wa kifedha wa serikali na mashirika binafsi watapoteza nguvu zao. Hakutakuwa na haja ya mihuri, wala sahihi, wala zile nenda urudi kesho tukuhudumie. Blockchain itakwenda kuiweka Afrika huru dhidi ya kero za huduma za kifedha na usalama wake kuwa katika ukuaji mzuri. Haya ndio mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani.

5. BIOPHYSICS AND BIOENGINEERING;

Eneo la 5 ambalo kituo cha ACET imeliacha ni kuhusu mtandao wa mifumo ya kibaolojia na kifizikia. Utahitaji mkono wa bandia unaoweza kuendeshwa na ubongo wako kwa usahihi ikitokea mkono wako halisi umekatika? Hebu fikiria hapo. Tunakubali kwamba asili ni bora sana kuliko sisi, hivyo ni bora kujifunza kwayo, kwasababu mapinduzi haya ya viwanda kwa kuchagizwa na ukuaji wa kiteknolojia duniani yatafanya taaluma ziweze kunyumbulika kwa namna nyingi sana hapo baadaye. Je, mifumo ya elimu imejiandaa na hili katika maandalizi ya mitaala yake ya muda mrefu?

Sasa tumeshajua yanayokuja na Mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani. Afrika, bara ambalo ajira bado ni tatizo kubwa kwa vijana, wataweza vipi kupambana na athari za mapinduzi haya? Kuna nadharia tatu (3) katika kukabiliana na hali hii;

1. Afrika inaweza kuketi chini na kubaki kutizama dunia nzima ikipambana katika Mapinduzi haya. Hii ilishafanyika katika zama 3 zilizopita za Mapinduzi ya viwanda ambapo Mapinduzi ya Kwanza yaliegemea katika kutengeneza mifumo ya Kimekanika na matumizi ya Injini za mvuke katika kutengeneza bidhaa kama nguo.

Mapinduzi ya pili yakiwa ni kuhamasisha Uzalishaji mkubwa (mass production) wa bidhaa viwandani yakichagizwa na Henry Ford na awamu ya 3 ya mapinduzi ikiwa ni zama za kidijitali katika uzalishaji.

Ukitizama elimu ya msingi ya kuunda Injini ni ile ile iliyokuwepo tangu mwanzo, lakini bado Afrika haijaweza kutengeneza magari yake yenyewe.

2. Afrika inaweza kufanya kile ilichokifanya katika kuingia kwenye zama za Kidijitali, mtindo wa kuruka kama chura (leapfrog). Kwa mfano nchini Kenya watu hawakuwa na huduma za simu za mezani miaka ya 1990’s kurudi nyuma, hali kadhalika ilikuwa hivyo nchini Tanzania pamoja na nchi nyingi za kusini mwa jangwa la Sahara katika ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani.

Lakini baada ya mwaka 2000 watu wengi katika eneo hilo wameweza kumiliki simu za mkononi hata kama hawakuwahi kumiliki simu za mezani. Simu za mkononi zimekuja na teknolojia kubwa zaidi baada ya kuunganishwa na huduma za kifedha kama MPESA, huduma za internet, GPS na ramani, huduma za kiafya pamoja na biashara za kielektroniki ecommerce.

Mazingira ya Uchumi jumuishi (social economy) yanafanya iwe rahisi kukaribisha zama za Mapinduzi ya 4 ya viwanda. Watu wengi duniani hawapendi kusoma vitabu, hivyo sasa tunaweza kuziachia mashine kufanya kazi mbalimbali badala yetu. Kama Blockchain inatazamwa kwenda kuangamiza kabisa changamoto ya rushwa, Teknolojia ya 3D-Printing itafanya hata nyumba zetu kuwa viwanda vidogo katika kubuni bidhaa mbalimbali.

Taarifa zote zilizo kwenye mashirika ya Serikali na binafsi ikijumusha taasisi za dini zinaweza kuvunwa kwa ajili ya kupata takwimu mbadala katika chunguzi mbalimbali. Hii inatazamwa kuwa njia mbadala kuyafikia mapinduzi ya viwanda ya 4. Unahitaji kuLeapfrog biashara yako (kuepuka gharama kubwa za matangazo)? Tunalo suluhisho, wasiliana nasi mara moja tukupatie.

3. Vile vile, Afrika inaweza kukuza thamani ya uzalishaji na ubunifu wake ili kuwa mshindani halisi duniani katika kutengeneza na kusambaza bidhaa na huduma za kiteknolojia, kama inavyofanyika mahali kwingine duniani.

Japan imeweza kufanya hivyo katika sekta ya magari na India inafanya vizuri katika sekta ya Famasia na Programu za Kompyuta. Sasa kwanini Tanzania isiwe kinara katika Sayansi ya Data(Data Science) duniani. (maana mbongo mpe picha tuu, vingine utaona atakapovipata😂. Natania.) Sekta hizi za teknolojia zinataka matumizi ya akili zaidi, sio kama viwanda vya saruji na chuma ambavyo vinahitaji mtaji mkubwa wa kifedha.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi kuyapokea Mapinduzi haya ya 4 ya Viwanda katika eneo lako la biashara? Pitia makala hizi ili kupata taarifa zaidi:

  1. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BANDO LAKO NI MTAJI
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  4. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mapinduzi ya 4 viwanda katika biashara duniani
mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi

MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI

Ubunifu wa kiteknolojia na zama za Kidijitali huathiri karibu kila mchakato katika utendaji na uendeshaji wa mfumo wa Usafirishaji na Uchukuzi duniani kote. Kuanzia njia na namna ya usafirishaji wa majini/baharini, ardhini na angani, usimamiaji wa mizigo pamoja na shughuli za utawala na ugavi zikiwemo utaratibu/usimamizi wa nyaraka na ufuatiliaji mzuri wa malipo. Leo sasa tuangazie mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi. Kuna nini kinaendelea huko? Makinika..

Idadi wa watu duniani itaongezeka kutoka watu bilioni 7.4 mpaka watu bilioni 10.6 kufikia mwaka 2050, vile vile idadi ya mizigo inayosafirishwa kwa njia ya meli peke yake itaongezeka mpaka mara 4 ambayo inatarajiwa kukua kwa ongezeko la 715% kwa nchi za Africa.

Pia kasi ya ukuaji wa miji itakuwa kwa 56% ya idadi ya watu katika Africa mpaka mwaka huo 2050. Ongezeko hili linatarajiwa kuchagizwa na kasi ya ukuaji wa miji, kukua kwa kipato cha mtu mmoja mmoja, kupenya kwa matumizi ya intaneti pamoja na urahisi wa kupata na kutumia Teknolojia mpya.

Hata hivyo mtindo wa uchukuzi wa mizigo kwa kupitia njia ya meli kwa kutegemea nyaraka peke yake unatarajiwa kupungua kwa kiasi kikubwa kufuatia ujio wa matumizi ya nyaraka za kielektroniki na barua pepe. Hii ni kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la EY.

Kufuatia kasi hio ya ukuaji na mabadiliko, makampuni na biashara zilizopo katika sekta ya Usafiri na Uchukuzi yanahitaji kubadilika ili kumudu kuwepo katika ulimwengu ambao ushindani unakuja kutoka pande zote na teknolojia za kidijitali ndio zitakuwa chachu kuu ya mabadiliko.

Sasa Swali; Teknolojia Inaweza vipi kubadili Kesho ya Sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Leo hii sehemu kubwa ya shughuli za kiuchumi na kijamii hufanyika mtandaoni na haswa haraka zaidi kupitia katika simu janja (smartphones). Ukuaji huu wa kiteknolojia unanufaisha maeneo yote yaliyomo kwenye Sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kama; usafiri wa magari ya mizigo (malori), usafiri wa kimataifa (njia ya anga na majini), usimamiaji wa shughuli za ugavi na kuratibu safari za majini, nchi kavu na angani. Yafuatayo ni mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi barani Afrika;

1. MFUMO WA KURATIBU SAFARI/ONLINE TRACKING SYSTEM (Magari ya mizigo, Meli na Anga): Imezoeleka mteja kuhifadhiwa nafasi ya kusafirisha mizigo yake kwa kujaza fomu fulani ya usafirishaji, halafu anaachwa gizani mpaka siku mzigo wake unamfikia asipoamua kufuatilia kwa kupiga simu. Lakini leo, kwa kutumia huduma za intaneti na programu za kompyuta mteja anao uwezo wa kuagiza na kufuatilia kwa ukaribu zaidi mizigo yake muda wowote akihitaji kufanya hivyo.

Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi

Hii si tu kwamba imerahisisha matumizi ya intaneti kisasa zaidi lakini zaidi teknolojia hii inaokoa muda na gharama za ziada kwa kampuni ya usafirishaji na mtu binafsi.

2. TEKNOLOJIA YA INTERNET OF THINGS (IoT) na RADIO FREQUENCY IDENTIFICATION (RFID): Ulishawahi kufikiria siku fulani una uwezo wa kuwasha feni yako nyumbani kwa kutumia simujanja yako? Sasa leo hii vifaa vingi vya kielektroniki vimeundwa na uwezo wa Wi-Fi na vifaa vya kuhisi mazingira mbalimbali. IoT inafungua nafasi nyingi sana katika kurahisisha shughuli za ugavi kama kupunguza gharama za uendeshaji. Vifaa vya kuhisi mazingira (sensors) pia hufungwa katika magari madogo na makubwa, meli za mizigo, treni na kadhalika. Vifaa hivi hufungwa mfumo wa kengele au mfumo wa GPS ambayo hufuatilia na kuratibu mwenendo wa mzigo kumfikia mteja.

Hali kadhalika teknolojia ya RFID ambayo imeshatumika miaka kadhaa hutumiwa na makampuni ya uchukuzi na usafirishaji kufuatilia mwenendo wa hesabu za bidhaa zao (Inventories). Kwenye teknolojia hii hujumuisha pia matumizi ya barcode za kwenye bidhaa, pamoja na matumizi ya rimoti za televisheni na redio, teknolojia ambayo imetumika kwa miaka mingi zaidi, hivyo kuyafanya makampuni mengi kutumia zaidi RFID’s. Vile vile RFID’s hutumika kusambaza bidhaa katika maghala yao na kuratibu mienendo ya makontena.

3.MAGARI/ MALORI YA KUJIENDESHA NA DRONES: Katika ulimwengu ambao unaendeshwa na matumizi ya kompyuta kutoka mahali fulani kwenda mahali kwingine, utajihisi vipi siku unapokea mzigo kutoka kwenye chombo kinachoruka angali mfano wa helikopta ndogo? Sasa huko ndipo tunapoelekea. Magari ya kujiendesha tayari yanaonekana duniani ambapo kampuni za UBER na EMBARK wametengeneza magari yanayojiendesha japokuwa bado miradi hiyo haijarasimishwa kwa wateja. Ni swala la muda tu kutoka sasa kabla matumizi yake hayajawafikia wateja ulimwenguni kote.

4. MITANDAO YA KIJAMII: Nani ambaye hapitii kwenye mitandao ya kijamii angalau mara moja kwa siku? Nguvu ya mitandao hii ya kijamii inaboresha kwa namna ya kipekee sana sekta hii ya Usafirishaji na Uchukuzi kwa ujumla wake. Mitandao hii inarahisisha sana katika kutangaza huduma za usafirishaji na uchukuzi pamoja na kampuni kuwasiliana na wateja wake kwa ukaribu na urahisi zaidi katika kutoa taarifa muhimu, dharura na mrejesho kutoka kwa wateja.

Kwa mujibu wa Hootsuite, 59% ya Wamarekani ambao ni watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekubali kwamba huduma kwa wateja kupitia mitandao ya kijamii imerahisisha kujibu maswali na huduma husika.

Zaidi ya yote, miundombinu ya uchukuzi katika nchi za Afrika bado ipo nyuma sana kimaendeleo ukilinganisha na sehemu zingine za dunia. Nchi ya Afrika Kusini ndiyo inaongoza barani kwa kuwa na miundombinu ya kisasa zaidi ya kiuchukuzi ambapo kasi ya ukuaji wa miundombinu kwa mwaka ni ndogo kwa 3% katika kipindi cha mwaka 2012 hadi 2017. Hii ni kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Fedha duniani (IMF).

Kwa upande mwingine nchi za Kenya na Nigeria zinaongoza kwa kuwa na ukuaji mkubwa katika miundombinu yake ya kiuchukuzi na usafirishaji kwa 6.2% na 6.8% katika kipindi hicho hicho (2012-2017). Kwa wafanyabiashara na makampuni ya usafirishaji na uchukuzi; Kuwekeza vema Afrika kunahitaji uelewa mzuri wa maeneo muhimu pamoja na uelewa wa masoko ya wenyeji.

Afrika si tu kwamba ni kubwa mno, lakini zaidi Kuna mtawanyiko mkubwa wa jamii za watu na rasilimali. Hata hivyo, zaidi ya 70% ya makampuni makubwa zaidi duniani yanayozalisha bidhaa za watumiaji tayari zinafanya kazi Afrika. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kimataifa la PwC.

Usipitwe na Ofa Yetu katika msimu huu wa Nane Nane. Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi. Umejifunza nini leo kuhusu mapinduzi ya kiteknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi? Share nasi mawazo yako kwenye comment au tucheki kwa kugusa WhatsApp namba yetu hii hapa 0765834754.

Makala hizi hapa zitakupa mwanga zaidi katika kuwekeza katika Biashara zinahohusiana na sekta ya Usafiri na Chukuzi hasa katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara:

  1. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  2. USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA
  3. FAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA HABARI NA BURUDANI