Tag: IMF

teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)

Uchumi wa Africa mpaka sasa hukua kwa kutegemea sekta za asili kama kilimoufugaji na biashara. Hata hivyo ujio wa teknolojia ya huduma za kifedha kwa njia ya kielektroniki (Fintech) utasaidia kwa kiasi kikubwa kuendesha uchumi katika kufanikisha maendeleo kiujumla. Sasa tuangalia teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech), zina mchango gani kwako leo?

Uchunguzi umeonyesha kwamba matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu za mkononi yameongezeka sana ndani ya miaka 10 iliyopita ambapo imeonekana eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara ndio limekuwa kinara wa kubuni na kutumia huduma hizi za kifedha kwa kutumia simu za mkononi duniani kwa sasa.

Utafiti uliofanywa na Shirika la Fedha duniani (IMF) umebaini kwamba takriban 10% ya pato la taifa katika miamala ya kifedha hufanyika kwa huduma za kifedha kupitia simu za mkononi. Hii ni matokeo bora zaidi ukilinganisha na 7% ya GDP katoka bara Asia na chini ya 2% ya GDP kutoka sehemu zingine za dunia.

Sasa swali, hii Fintechs ni nini!? Na ina manufaa gani kwa wafanyabiashara walio Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Shirika la EY linaifafanua FinTech kama Shirika/Kampuni inayojumuisha ubunifu katika utendaji wa biashara pamoja na technolojia ya programu za kompyuta katika kubuni, kuwezesha na kusambaza huduma za kifedha. Hizi FinTechs zinaweza kuwekwa kwenye makundi mawili;

i. FinTechs zinatoa huduma za kifedha e.g TALA App.

ii. FinTech zinazowezesha huduma za kifedha Vodacom na MPESA n.k (tutayajadili zaidi kwenye makala zetu zijazo)

Sekta hii ya FinTech katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara (SSA) inajumuisha zaidi ya makampuni 260 ambapo 80% katika hizo ni kampuni za ndani na 20% ni kampuni za kimataifa. Vile vile imeonekana idadi ya makampuni haya mapya imeongezeka katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) cha 24% ndani ya miaka 10 iliyopita.

Hata hivyo ripoti zinaonyesha kwamba Afrika Mashariki itaendelea kuongoza katika ukuaji wa sekta hii kwa 6.3% ya ukuaji wa uchumi mwaka huu 2019. Hii ni kutokana na Ethiopia, Rwanda, Tanzania na Uganda zote zinatarajia kurekodi pato la Taifa la zaidi ya 6% mwaka huu ambayo ni zaidi ya nchi zilizo maeneo mengine ya Africa. Hii ni kutokana na uwekezaji katika miundombinu na utanuzi wa huduma za kifedha na mawasiliano.

Takriban theluthi moja (1/3) ya michango ya harambee zilizofanyika barani Africa mwaka 2017 iliwezeshwa na kampuni za FinTechs. Hii inatiliwa mkazo kwa kuwa 60% ya akaunti za huduma za kifedha kwa njia ya simu duniani zimegundulika kuwepo katika eneo la SSA. Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliofanya na benki ya Ecobank.

Pia imeonekana sekta hii ya FinTechinaendelea kuwa imara katika muda wa miaka 3 kutoka makadirio ya dola za kimarekani 200 milioni mwaka 2018 hadi 3$ bilioni mwaka 2020. Kiasi kikubwa cha uwekezaji katika muda huu kimeonekana kuelekezwa KenyaNigeria na Afrika Kusini. Vile vile inategemewa kwamba kufanikiwa kwa Fintechs katika nchi hizo kutatanua mafanikio katika nchi zingine za Kiafrika.

MAENDELEO: Ujio wa FinTechs umebadili sana jinsi ya kufanya biashara duniani. Kutoka Crowdsourcing ambayo ni njia inayotumika kufanya usaili wa miradi mbalimbali mtandaoni kupitia intaneti na kupokea ruzuku, mpaka njia ya huduma za kifedha kwa njia ya simu. Wafanyabiashara na wajasiriamali hawajawahi kupata njia rahisi zaidi kwenye utandaji wa biashara zao kwenye maswala ya fedha kuliko hii.

Kupitia Fintechs sasa wafanyabiashara wanaweza kusambaza bidhaa/huduma kwa watu mbali mbali na kupata malipo ndani ya muda mfupi zaidi. teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) inazidi kujisombea watumiaji kwa sababu inaonyesha namna inavyoweza kusaidia katika kujikwamua kwenye maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni.

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH) HAINA MIPAKA:

Kutuma pesa nje ya mipaka ya nchi napo imekuwa rahisi zaidi. Mfumo huu ulioondoa mipaka ya kijiografia kwenye kurusha pesa umepunguza gharama kutoka ilivyokuwa mwanzo kwa njia ya benki ambayo ni ghali mno. Hivyo FinTech imewawezesha wajasiriamali na viwanda vidogo kutuma na kupokea pesa kwa gharama ndogo zaidi.

KUONGEZA THAMANI KATIKA UTOAJI WA HUDUMA ZA KIFEDHA: Eneo hili limetawaliwa na ubunifu ambao unawezesha kuongezeka kwa thamani katika matumizi ya huduma za kifedha. Kwa kuyumia malipo kwa njia ya simu, wateja walioko kusini mwa Jangwa la Sahara wanapata uwezo wa kupata huduma za kibenki kupitia simu za mkononi (mobile banking) pamoja na huduma zingine kama kugungua akaunti, kuchukua mkopo, kupata bima, kupata huduma za mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na masoko ya hisa. Haya yote kupitia FinTech yanawezeshwa kirahisi tuu katika simu yako ya rununu (smartphone) au laptop.

teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi. Umejifunza nini hapa katika teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) leo?

Zaidi unaweza kupitia makala hizi hapa chini ili kupata ufahamu mpana kuhusu biashara za mtandaoni:

  1. MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA
  2. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  3. UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-COMMERCE BUSINESS)?
  4. FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia comments section hapo chini;

UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-commerce BUSINESSES)?

Japokuwa imechelewa, lakini kwa sasa Africa ndio inaongoza mbio katika kufanya mapinduzi ya kidijitali kuliko sehemu yoyote duniani. Namna ya kufanya biashara inazidi kubadilika ikionyesha nia ya dhati kufanya maendeleo ya kiuchumi, miundombinu na maswala ya kijamii. Mwaka 2018 nchi wanachama wa Umoja wa Africa walipiga hatua kubwa katika mfumo wa kufanya biashara na muingiliano wa kiuchumi baada ya kuanzisha Eneo Huru la Kufanyia Biashara barani (Continental Free Trade Area AfCFTA). Eneo hili lililoanzishwa linashirikisha nchi 22 zilizoweka sahihi tayari na utekelezwaji wake ulipangwa kuanza mwaka 2019 (tayari umeshaanza).

Hata hivyo mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuzishirikisha nchi ambazo bado si wanachama wa eneo hili jipya, inatarajiwa eneo hili kufikia soko la watu takribani bilioni 1.2 barani wakiwa na jumla ya pato la ndani la taifa (GDP) la dola za kimarekani trilioni 2.5 kwa pamoja, kwa mwaka. Hii inatarajiwa kuwa ni mapinduzi makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nyanja ya uchumi wa Afrika.

Sasa, swali linakuja; Afrika(wafanyabiashara, makampuni/mashirika na Serikali) imejiandaa vipi na mapinduzi haya ya uchumi wa kidijitali? Na zaidi, watunga sera/sheria wataangalia vipi biashara za kielektroniki (e-commerce) kama mada muhimu katika eneo hilo jipya la kufanya biashara huru barani?

Tume ya kudhibiti uchumi wa Africa ya Umoja wa Mataifa (ECA) ikishirikiana na Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) pamoja na Baraza la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo ya kibiashara (UNCTAD) mwaka huu 2019 imechapisha ripoti yake ikiangazia maendeleo ya Afrika kiujumla katika nyanja za kiuchumi, siasa na kijamii.

URAHISI: Imeonekana kwamba e-commerce inaweza kufanya biashara ya bidhaa na huduma kwa urahisi zaidi ambapo itarahisisha mwenendo mzuri wa biashara kati ya wazalishaji, wafanyabiashra na walaji pamoja na kumbukumbu zao na miamala ya kifedha.

MITANDAO YA KIJAMII: Pia imeonekana kwamba e-commerce inapatikana na kufanyika kirahisi katika mitandao ya kijamii kama facebook na Instagram ambapo ndipo mahali kuna watumiaji wengi zaidi wa Intaneti duniani (zaidi ya watu bilioni 2 kati ya watumiaji bilioni 4 wa intaneti).

KUTOKUWA NA MIPAKA: Mfumo wa uchumi wa Kidijitali kiasili umetengenezwa kuepuka mipaka ya kijiografia katika kufanya biashara na kubadilishana fedha ambapo mabadiliko haya ya kiteknolojia yataongeza umakini zaidi katika mwenendo wa masoko na gharama. Lakini bado wimbi kubwa la watu watakaoshiriki kwenye soko barani wanaonekana wataachwa nyuma kutokana na kutokuingiliana kwa lugha na vita/ghasia za mara kwa mara katika baadhi ya jamii/nchi.

BIASHARA: Kwa mujibu wa UNCTAD mwaka 2016 kwa dunia nzima e-commerce iliweza kupitisha mauzoya takribani dola trilioni 26 ambapo 90% ilikuwa ni Biashara kwa Biashara (B2B e-commerce) na 10% ilikuwa ni Biashara kwa Mlaji (B2C e-commerce). Hata hivyo kupima mwenendo wa e-commerce katika baadhi ya nchi zinazoendelea imekuwa ni changamoto kupata data na takwimu, haswa katika nchi za Afrika.

IMPORTATION: Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kwamba Biashara kati ya nchi na nchi imekua kwa kiasi kikubwa Afrika ambapo zimechagizwa na vituo vichache vya kiteknolojia (Hubs) ambavyo vimerahisisha mno mwenendo wa biashara. Biashara kati y nchi na nchi (Intraregional import) imekuwa zaidi ya mara 3 katika miongo miwili iliyopita kufikia 12%- 14% sawa na dola bilioni 100 ikichagizwa na uwepo wa jumuiya za kiuchumi barani (Subregional Economic Communities REC‘s).

UZOEFU: Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na umri wa Jumuiya hizi za Kimaendeleo barani Afrika ambapo uzoefu huo hutumika kuongeza jitihada katika kuboresha namna ya ufanyaji biashara kuelekea uchumi wa kidijitali kiteknolojia. Uzoefu huo pia hutumika kuunganisha jumuiya moja na nyingine (mf, SADC na COMESAna EAC) ambapo zitazalishwa nafasi nyingi zaidi za kufanya biashara kati ya nchi wanachama na ripoti zinaonyesha 75% ya biashara hizi ndani ya jumuiya barani Afrika zimefanyika mwaka 2017 peke yake na nusu ya biashara hizo zilifanyika katika jumuiya ya SADC.

Chini ya mwavuli wa AfCFTA nchi wanachama zinatarajia kufuta tozo/ushuru kwa 90% ya bidhaa zote zitakazopitishwa na kufanyiwa biashara katika eneo hilo. Hii itaruhusu uwezekano wa kupunguza mlolongo wa kodi au kuongeza idadi na thamani ya bidhaa na huduma zitakazohusishwa. Matokeo yoyote katika punguzo hilo linalotarajiwa katika muktadha wa biashara kidijitali yataleta picha tofauti. Kupunguza mlolongo wa tozo za mipakani baina ya nchi na nchi kutapungua kwa 15% pekee ikitegemea thamani ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi husika. Hii ni kwa mujibu wa Tume inayoshughulikia Uchumi wa Afrika kutoka Umoja wa Mataifa (UNECA) mwaka 2018.

Sasa mwaka 2018 Jumuiya ya COMESA ilibuni mfumo wa kudhibiti eneo huru la kibiashara kidijitali (Digital Free Trade Area DFTA). Mfumo huu umeundwa na mambo yafuatayo;

•E-trade: Hili ni jukwaa mahsusi kwa ajili ya kufanya biashara za kimtandao na kuwezesha malipo ya kielektroniki, mobile apps kwa ajili ya wafanyabiashara walioko katika Jumuiya hio.

•E-logistics: hili ni jukwaa maalum kwa ajili ya kuwezesha biashara ya usafirishaji wa mizigo baina ya nchi wanachama wa jumuiya.

•E-legislation: huu ni mfumo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara rasmi ambao unawawezesha kufanya miamala na malipo kielektoniki.

Mfumo huu uliobuniwa na Jumuiya ya COMESA umelenga kutangaza biashara za wanajumuiya katika nchi wanachama ikijumuisha kupitia majukwaa ya e-commerce. Mfumo huu ulikuwa ni mfanano wa mfumo uliotengenezwa na kuzinduliw na nchi ya Malaysia mwaka 2017 katika muktadha wa kufanya biashara huru ndani ya eneo maalum.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.

Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana, shuka nazo:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-biashara-ya-fedha-za-kidijitali-cryptocurrency-business/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)”
  2. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia;

e-mail: info@rednet.co.tz

tovuti: https://rednet.co.tz

Simu:+255765834754