Tag: huduma mtandaoni

utajuaje kama kifaa chako (simu/computer) kimedukuliwa?

UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?

Katika makala iliopita kuhusu Kwanini Usalama wa Kimtandao ni muhimu kwako? Mdau mmoja aliuliza, “Sasa nitajuaje kama computer yangu imedukuliwa?” Sasa leo hii nitakujuza dalili 10 muhimu za kutambua kama kifaa chako (simu/computer) kimedukuliwa, utajuaje? Dalili ya 7 itakushangaza sana. Fuatana nami mpaka mwisho wa makala hii katika utajuaje kama kifaa chako (simu/computer) kimedukuliwa? Makinika..

Ngoja nikupe kisa: Mama mmoja alikiri kuwa mumewe alikua akifuatilia nyendo zake na jumbe za kwenye simu kwa kutumia App maalum iliyopandikiza kwenye simu hio. Alipogundua hakulifurahia jambo hilo na kuamua kuripoti polisi kwa kuingiliwa haki yake ya faragha (invasion of privacy) kwa mujibu wa sheria kabla mumewe huyo hajachukuliwa hatua stahiki. Ni kosa la jinai kuingilia faragha ya mtu katika mtandao au mawasiliano pasi na idhini yake. (SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO, 2015).

Kwa sasa duniani kunaongezeka matishio ya kimtandao yakihusisha matumizi ya programu halifu za computer (malwares) na kufanya usalama wa kimtandao kuwa katika hali tete kila uchwao. Hata hivyo, watu lazima watumie huduma za internet licha ya matishio hayo. Sasa itakuaje? utajuaje kama kifaa chako (simu/computer) kimedukuliwa?

Sasa kupambana na hali hio, programu nyingi za kuzuia uhalifu wa kimtandao (antimalware programs) zimekuwa zikitumika kufuatilia utendaji wa vifaa zikiitwa HEURISTICS ili kuhakikisha zinapambana na uhalifu wowote mpya. Lakini, uhalifu mbaya zaidi hufanyika pale kifaa kinapoangukia katika mikono ya mhalifu ambapo anaweza kuhamisha/kubadili taarifa ili uhalifu utendeke katika mfumo mwingine nje ya kifaa bila ufahamu wako. Hivyo njia bora ya kudhibiti hili ni kuhakikisha kifaa chako kipo salama katika uangalizi wako muda wote. Hizi hapa dalili 10 muhimu za kutambua kama kifaa chako (simu/computer) kimedukuliwa, utajuaje? Twende kazi..

Sasa Tuzione Dalili za kukijua Kifaa (simu/computer) kilichodukuliwa:

1. Kutokea kwa Ujumbe wenye Tishio la Kutaka Pesa (Ransomware Message): Kama kuna ujumbe ambao hakuna mtu anautaka kuupata katika kifaa chake ni huu wa kutokea kwa ujumbe au Video ghafla katika kioo cha kifaa ukimtaka kutoa kiasi cha pesa ili kutodhuru/kurudisha data zake ambazo tayari zimedukuliwa bila yeye kujua. Kufahamu zaidi kuhusu shambulizi hili la ransomware tafadhali fuatilia makala hii hapa chini

2. Kutokea kwa Browser Toolbars usizozihitaji: Imeshawahi kukutokea unafungua browser yako ukashangaa inafunguka ikiwa na vitufe/tabs/bookmarks ambazo hujawahi kuziona kabla. Hio ni ishara kwamba kunazo malwares zimepandikizwa katika kifaa chako ambazo tayari zimeanza kufanya kazi..

3. Matafuto na machanguo unayofanya katika Internet yanaelekezwa/redirected katika tovuti usizozitambua: Umeshawahi kuona pale unajaribu kutafuta kitu (mf. gari) ukashangaa unapelekwa kwenye tovuti kuhusu urembo wa nywele. Hii ni njia moja wadukuzi huitumia ili kupata clicks za matangazo na kujipatia pesa, japokuwa njia hii haiathiri sana utendaji wa kifaa chako licha ya kusababisha usumbufu katika matumizi ya huduma za internet.

4. Unapata Matangazo sumbufu ya ghafla ghafla (Pop-ups): Hii ishara maarufu sana pale kifaa chako (simu/computer) kinapokuwa kimedukuliwa.

Matangazo (pop-ups) kutoka tovuti usizozifahamu zinakuja ghafla katika kioo chako bila ya kuziamuru na kusababisha usumbufu. Ukiona hivi ujue kifaa chako kimeathirika tayari na malwares.

•Hakikisha unaziondoa toolbars zote usizozifaham katika browser yako mara tu unapozigundua.

5. Nywila/Password yako haifanyi kazi tena: Hii inawatokea watu wengi sana hasa watumiaji wa mitandao ya kijamii na kupotea/kuibiwa kwa akaunti zao zenye wafuasi wengi, maudhui na kumbukumbu muhimu hivyo kupelekea kuharibika kwa biashara, wawekezaji, hadhi ya mtu katika jamii na usalama binafsi.

kifaa chako kimedukuliwa? Utajuaje?

•Hakikisha akaunti zako zina uthibitisho zaidi ya mmoja kwa kutumia email au namba ya simu, ili isiwezekane kubadili Nywila pasi na kuthibitisha kupitia email au namba yako ya simu. Hii ni njia salama zaidi.

6. Umegundua kuna programu zimepandikizwa katika kifaa bila ya ufahamu wako: Programu hizi mara nyingi huwekwa ili kufuatilia nyendo zako mtandaoni (unawasiliana na nani, uko wapi, nywila zako za benki, mpesa, tigopesa nk) na unaweza kuziona katika Control Panel ya computer yako(kipengele cha Programs) au kwenye simu katika mkusanyiko wa Apps zako.

•Hakikisha simu/computer yako ina programu zile tu umethibitisha ziwepo ndani ya kifaa chako. Vinginevyo, fanya usafi(futa) wa ndani wa kifaa chako mara kwa mara.

7. Kipanya(Mouse pointer) inapotembea yenyewe na kufanya uchaguzi wa programu na mambo mengine bila ushiriki wako: Isipokuwa tu computer yako imepata hitilafu ya vifaa (hardware problems) au pale inapofanyika shughuli maalum katika mtandao kwa kushirikisha kifaa zaidi ya kimoja kupitia programu mf. Teamviewer ambapo unaweza kutumia kipanya cha computer yako katika computer nyingine (ambalo jambo hili ni halali kisheria na huitwa Ethical Hacking), vinginevyo mouse yako inapofanya shughuli zake pasi na ushiriki wako jua hapo kifaa chako kipo mikononi mwa wadukuzi.

Hapa dhumuni kubwa ni kuiba taarifa/fedha kutoka kwenye kifaa chako, hivyo kuwa makini na hakikisha unapozima kifaa chako zima internet/chomoa na waya wa ethernet (kama inatumia waya wa internet) kisha toa taarifa kwa wataalam wa mitandao au mamlaka za serikali. Katika tukio hili unahitaji msaada wa kitaalam ili kuhakikisha shambukizi kama hili haliji kukutokea tena. Usidharau.

8. Antivirus, Task Manager na Registry Editor za kwenye kifaa chako hazifanyi kazi, zimezimwa au zipo slow: Ukiona Antivirus yako ipo OFF wakati hukuwahi kuizima, Task manager/Registry Editor haifunguki (au inafunguka na kufunga gafla), jua hii inaweza kuwa dalili ya kifaa kuwa hatarini.

•Katika tishio hili fanya Complete restoration ya kifaa chako, kwa kuwa mpaka kufikia hatua hio hujui madhara yamefikia kiwango gani.

9. Akaunti zako kifedha ulizoziunga mtandaoni Hazina/zimepungua Pesa: Wadukuzi mara nyingi hujaribu kuiba pesa katika akaunti za watu zinazotumia huduma za internet mtandaoni. Hii hutokea pale wadukuzi wanapopandikiza malwares katika kifaa chako bila ya wewe kujua kwa kupitia picha, link au email (PHISHING ATTACK). Na hivyo kupata taarifa mbalimbali kuhusu akaunti za benki, hivyo kurahisisha uhalifu wao.

utajuaje kama kifaa chako kimedukuliwa?

•Kujiepusha na kadhia hii, hakikisha umewasha alerts/notifications kwa kila muamala unaofanyika kuzidi kiasi fulani (threshold amount) ambapo alert hio itatumwa kwa SMS au email kuthibitisha kabla muamala haujafanyika. Hii ni muhimu sana, wasiliana na mtoa huduma wako(bank, mitandao ya simu nk).

10. Taarifa zako za siri zinapovuja bila ya idhini yako: Hakuna kitu kitakuthibitishia kuwa kifaa chako kimedukuliwa kama pale unaona taarifa nyeti za kampuni/biashara yako zimesambaa mitandaoni au kwa watu wasiostahili kuzipata. Kadhia hii ni hatari sana katika utendaji.

•Hakikisha umethibitisha jambo hilo, kisha taarifu uongozi wa kampuni haswa kitengo cha sheria, kisha fuata utaratibu wa kitaalamu katika kupambana na madhara ya shambulio hilo ili lisije kutokea tena.

NOTE: Siku zote kinga ni bora kuliko Tiba. Hakikisha unatumia njia zaidi ya moja, mfano (two steps verification method) kuhakikisha vifaa vyako vinabaki kuwa salama muda wote. Njia za kujikinga dhidi ya mashambulizi ya kimtandao tayari tumezielezea hapo juu na katika makala zetu zingine kupitia tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz

Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakusaida kuimarisha biashara yako kiuchumi katika kuimarisha Usalama wako uwapo katika mitandao. Cha kufanya, gusa link kisha makinika:

  1. KWANINI UHAMIE WINDOWS 10 KUTOKA WINDOWS 7?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE (TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?

Hizi hapa ndio dalili 10 muhimu za utajuaje kama kifaa chako (simu/computer) kimedukuliwa? Majibu tayari unayo. Ungependa kuuliza swali au kuongezea? tafadhali tuandikie katika comment hapo chini au njoo whatsapp kupitia kitufe cha whatsapp kilichopo katika ukurasa huu.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE

Yaani ni 8% tu ya makampuni ndio wana uwezo wa kugundua wizi wa taarifa zao ndani ya dakika chache. 62% wanaweza kugundua wizi ndani ya siku kadhaa. Wewe unatumia muda gani kugundua upotevu/wizi wa data katika kampuni yako? Makala hii tutaangazia mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) kiundani. Leo, yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake. Makinika mpaka mwisho.

Kama Unavyoona biashara zinavyozidi kushamiri kiteknolojia ndivyo wadukuzi nao wanazidi kutafuta mbinu za kufanya mashambilizi zaidi. Mwaka 2019 peke yake, zaidi ya 2$ billion zilipotelea mikononi mwa wadukuzi duniani. Utafiti wa Juniper unaonesha namba hio inaongezeka kila mwaka.

Unalikumbuka shambulizi lilioitwa NotPetya? Basi jarida la WIRED linalitaja shambulizi hilo kama “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA”. Ndani ya masaa machache tu virusi vya shambulio hilo (malwares) viliathiri kutoka biashara ndogo za Software nchini Ukraine mpaka kusambaa katika vifaa vya kielektroniki dunia nzima. Shambulizi lilidhoofisha mashirika makubwa duniani kama FedEx, TNT, Express na Maersk kwa wiki kadhaa na kusababisha hasara ya zaidi ya $10 bilioni kwa ujumla. Upotevu wa data kwa kiwango hiki unaonyesha namna katili ya dunia tuishiyo ambapo inaonekana hakuna mwenye kinga madhubuti mtandaoni. Kutoka Mashirika makubwa, serikali, mitandao ya kijamii, mifumo ya migahawa na sehemu yoyote unayojua inatumia teknolojia ya IT, Kila mmoja yupo hatarini.

TUMEFIKAJE HAPA?

Ripoti ya mwaka 2019 ya shirika la Accenture Security kuhusu Matishio ya kimtandao (Cyber Threatscape), imeonyesha sababu za wadukuzi kuendelea kuwa tishio dhidi ya taarifa binafsi/za mashirika kwa manufaa yao. Hizi ni baadhi sababu hizo:

1. Wadukuzi wa kimtandao hufaidika zaidi na teknolojia mpya na kukosekana mawasiliano madhubuti katika sheria na tawala za maeneo/nchi mbalimbali duniani.

2. Mitandao ya kihalifu muda wote inakwenda ikibadilika, hasa kuelekea katika makundi ya kihalifu ya siri (syndicates) pasi na kujulikana chanzo chake kwa kutumia nyaraka halali kwa nia halifu.

3. Malengo mseto katika kuimarisha tabia za virusi (kama kujiendesha vyenyewe: self replication)

4. Kuimarika kwa mifumo ya Ulinzi wa Kimtandao (cybersecurity hygiene) inapelekea wadukuzi nao wazidi kujiimarisha kimbinu na maarifa katika uwanda wa kiteknolojia na matumizi ya internet.

Baada ya kujua sababu zinazowasukuma Wadukuzi na wahalifu wa Kimtadao kuendelea kufanya mashambulizi, Leo, uta yafahamu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako, Fuatana nami..

Duniani kunazo aina nyingi za mashambulizi ya kimtandao kulingana na sababu nilizozieleza hapo juu kama ifuatavyo:

1. RANSOMWARE ATTACK: Katika shambulio hili, virusi maalum (specific malware) ambavyo hukusanya na kufunga taarifa/kifaa katika mtandao ili kumnyima mtumiaji haki na uwezo wa kufanyia kazi taarifa zake kama kawaida. Haki na uwezo (access) huo humrudia mtumiaji pale tu matakwa ya mdukuzi yatakapotimizwa ambayo mara nyingi huwa ni pesa au rushwa kwa mapana yake.

Saa ingine wadukuzi wanaweza kugoma kurudisha haki za matumizi kwa mhusika hata wanapotimiziwa matakwa yao, hivyo kuongezea hasara kwa kampuni/biashara. Mbaya zaidi, ripoti ya mwaka 2019 ya Uhalifu wa kimtandao inaonyesha kutokea kwa shambulizi hili kila sekunde11 ya mwaka 2021.

2. ADVANCED PERSISTENT THREATS (APT): Shambulizi hili sio la mojakwamoja (passive attack) ambapo mdukuzi anapata access ya computer/mtandao fulani kwa muda mrefu pasi na kujulikana, hivyo kujichotea taarifa na kuzitumia kwa manufaa yake. Aina hii pia huitwa Trojan Horse attack.

3. PHISHING: Je wajua? Mpaka 32% ya wizi wa data husababishwa na shambulizi hili. Hii ni aina ya shambulizi maarufu sana la kijamii (social engineering) ambapo mdukuzi humtegea mtu adownload file lililo na virusi kupitia SMS, email au link na kuingiza virusi katika kifaa chake.

unawezaje kujilinda dhidi ya shambulizi la kimtandao la phishing katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

4. SQL INJECTION: Umeshawahi kuona ile unaingia kwenye website ukakuta haipo ghafla tu, au kwenye system flani unanashangaa kuna mafiles huyaoni bila sababu ya msingi. Sasa kwa kutumia virusi halifu (malicious codes) shambulizi hufanyika katika servers zinazohifadhi taarifa muhimu za watumiaji na kuzifuta, kuziiba au kuzibadili ili kutimiza azma fulani ya wadukuzi na/au genge lao. Mara nyingi shambulio hili hufanyika kwenye servers zinazohifadhi taarifa ghafi za watu au vitu (personal identifiable information: PII) kama namba ya kadi, username and passwords.

5. DDOS ATTACK: Kirefu huitwa Distributed Denial of Services attack ambapo hutokea pale wadukuzi wanapofurika tovuti au kifaa chako kwa either kupunguza au kondoa kabisa utendaji wa kawaida na hivyo kuiacha kampuni/biashara kuhangaika kurejesha performance ya mifumo yake wakati wao (wadukuzi na virusi vyao) wakitumia mwanya huo kuiba na kufanya uhalifu katika mifumo hio iliyoathirika.

6. MAN IN THE MIDDLE (MITM): Hii hutokea pale mdukuzi anapoingilia mawasiliano halali ya kampuni bila ya wao kujua. Pia shambulio hili hufahamika kama eavesdropping pale linapofanyika baina ya mawasiliano binafsi ya simu kati ya mtu na mtu.

Mawasiliano katika MITM hiungiliwa pia kupitia APN za Wi-Fi za uongo (deceptive wifi). Zaidi ya kuingilia mawasiliano, hapa mdukuzi anaweza pia kuwasiliana akitumia utambulisho (ID) ya wahusika pasi na kufahamika mara moja.

7. PASSWORD ATTACK: Licha ya kuwa shambulizi maarufu zaidi duniani, bado kuna watu huangukia mtego wa kuibiwa nywila zao. Kwa urahisi wake, wadukuzi hutumia mbinu zenye viwango na ujanja kupata nywila dhaifu na kufungua accounts za watumiaji kirahisi. Hapa tunaangukia kwenye usalama wa vifaa vyetu vya mtandaoni. Je viko salama kiasi gani? Fuatana na makala hii hapa kufahamu zaidi..

UNAWEZAJE KUZUIA MASHAMBULIZI HAYO?

Katika yetu iliyopita tumeeleza kwa kirefu kuhusu namna ya kujiepusha na mashambulizi ya kimtandao (Cyber attacks), pitia hapa KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?“. Leo pia, tutaona njia zingine za kuendelea kujiimarisha na kuzuia mashambulizi hayo yasiathiri Biashara/Kampuni yako. Mashambulizi mengi niliyoyaelezea leo yanazuilika kwa njia ambazo tayari tulishaziona katka makala zilizopita isipokuwa:

MITM Attack: •Tumia SSL Certificates za (https) katika website yako. Hii ni boresho la http SSL certificate ambayo ni ya zamani na usalama wake mi mdogo.

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

•Tengeneza VPN yako kama ngao ya ziada dhidi ya wi-fi halifu (deceptive wi-fi). Mashambulizi haya katika biashara yako yana madhara makubwa ikiwemo Kupotea kwa Fedha, faida ya biashara, mauzo, matengenezo, Hadhi ya biashara kushuka au kupotea kabisa na madhara ya kisheria.

Hivyo unapaswa kuwa makini na kufuata ushauri wa kitaalamu kuhusu maboresho ya kimtandao (updates & maintenance) ili kuhakikisha unatumia teknolojia ya kisasa zaidi ambayo ni salama huku ikiwa imeambatana na Passwords zako zilizo bora. Utajuaje kama simu/computer yako ikiwa imedukuliwa? Majibu tayari yanapatikana kwenye makala iliyo hapa UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?.

Usalama wa Kimtandao ni jukumu langu. Ni jukumu lako. Ni jukumu letu sote. Tuchukue tahadhari muda wote tuwapo mtandaoni. Basi ni matumaini yangu leo mengi umeyafahamu kuhusu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako. Ukiwa na swali au nyongeza tafadhali tuandikie katika comments hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo? Umejifunza nini katika ku yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake katika biashara/kampuni yako.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Unawezaje kujikinga dhidi ya mashambulizi ya kimtandao katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Mteja hakosei na mteja ni mfalme. Hizi ni kauli maarufu sana katika biashara duniani, lakini haswa biashara zinazofanyika kusini mwa jangwa la Sahara. Maana yake ni kwamba, Mteja anatakiwa kusikilizwa na kuridhishwa na huduma/bidhaa zinazotolewa na mfanyabiashara. Je, wewe unatumia mbinu zipi ili kuhakikisha huduma/bidhaa zako zinawaridhisha wateja wako? Katika makala yetu ya leo utakwenda kufahamu kwa undani siri na umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja. Twende pamoja mpaka mwisho.

Sasa ripoti ya mwaka 2019 kutoka shirika la kimataifa la ukaguzi wa mahesabu la PwC imeonyesha kwamba 64% ya Wakurugenzi wa Makampuni na Wafanyabiashara barani Afrika hawana data na takwimu kuhusu mwenendo wa wateja wao. Inashangaza eeh?

Kwa upande mwingine ripoti ya McKinsey imeonyesha kwamba makampuni yanayotumia data na takwimu sahihi kuhusu mwenendo wa wateja wao huyazidi yale yasiyofanya hivyo kwa 85% katika ushindani wa masoko na 25% zaidi katika kuingiza mapato kila mwaka.

Zaidi 95% ya wateja huongelea zaidi huduma mbovu walizokutana nazo katika kampuni/biashara fulani (Mtandao wa American Express), hali kadhalika 89% kati yao huacha kabisa kufanya biashara na kampuni/biashara fulani baada ya kukumbana na huduma/bidhaa zisizokidhi mahitaji/viwango walivyotegemea (ripoti ya Huduma kwa wateja ya mtandao wa RightNow). Kama unaijali biashara yako na ungependa kuona inazidi kukua, makala haya ni kwa ajili yako.

Sasa Changamoto; Kuna umuhimu gani katika kumridhisha mteja wako katika biashara unayofanya baada ya kujua takwimu sahihi kuwahusu?

1. KUONGEZA MAHUSIANO MAZURI NA MTEJA; Mteja aliyeridhishwa na huduma/bidhaa zako atabaki kuwa mteja wako kwa muda mrefu zaidi kutokana na huduma bora anazopata kutoka katika kampuni/biashara yako. Hakikisha unamshirikisha mteja kufanya maamuzi katika mchakato mzima wa kuhudumia. Muulize maswali kama Unaonaje ikiwa hivi au ikionekana vile, Unajiskiaje. Mpeti peti mteja wako muda wote kama unataka aendee kutumia huduma/bidhaa zako.

2. Waswahili wanasema, Kauli Njema ni silaha. Yaani unapokuwa na Kauli njema katika kusambaza huduma/bidhaa zako, unaiweka bishara/kampuni yako katika nafasi nzuri ya kuishindani dhidi ya washindani wako katika soko. Kauli njema ni kama sumaku ambayo inawaleta pamoja wateja na huduma/bidhaa zako na hivyo kufanya wateja wako kuendelea kuwa wako, lakini zaidi kauli njema huwavuta pia wateja wapya kuanza kutumia huduma/bidhaa zitokazo katika biashara/kampuni yako.

umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja

3. KUPUNGUZA GHARAMA ZA MATANGAZO; Kampuni/biashara yako inapotoa huduma bora kwa wateja wake huwafanya wateja hao kuwa mawakala ambao hutangaza huduma bora wanazopata katika kampuni/biashara hio. Kama tulivyoona hapo mwanzo, 95% ya wateja duniani hueleza katika jamii zao jinsi walivyokutana na huduma mbovu/dhaifu walizokutana nazo katika kampuni/biashara fulani. 89% kati yao huacha kabisa kujihusisha na bishara/kampuni ambayo haikuwapatia huduma bora au haujali wateja wake. Hata hivyo bado ni muhimu sana uendelee kuitangaza biashara yako. Gusa hapa kufahamu kwanini.

Na njia bora kabisa ya kutoa huduma bora na kwa wakati huo huo ukipunguza gharama za matangazo ni kwa kutumia teknolojia kama website iliyounganishwa na huduma za S.E.O. Kwanini uwe na website? Majibu yanapatikana kwenye makala hii hapa kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website rasmi ya biashara yako.

4. MAFANIKIO KATIKA BIDHAA/HUDUMA ZIJAZO; Kampuni/biashara hujiweka katika nafasi nzuri ya kufanikiwa katika kusambaza huduma/bidhaa zake mpya pale inapokuwa na kumbukumbu nzuri katika kutoa huduma bora kwa wateja wake.

Matokeo yake, kampuni/biashara hulenga wateja wake wa kudumu katika kusambaza huduma/bidhaa zao mpya ambapo hujihakikishia mafanikio kabla ya kuwasambazia wateja wapya. Hata hivyo wateja wanaoridhishwa na huduma bora zitolewazo hupendelea bidhaa/huduma mpya zitokazo katika kampuni/biashara walizowahi kuhudumiwa vizuri hapo mwanzo.

5. MTEJA WA KUDUMU NI LULU; Kwa mujibu wa Ikulu ya Marekani (#WhiteHouse) Ofisi inayoshughulikia maswala ya wateja, kwa wastani, mteja aliyeridhika na huduma/bidhaa (mteja wa kudumu) katika biashara ana thamani mpaka mara 10 zaidi kuliko thamani ya manunuzi yake ya kwanza.

Tafiti zingine zimeonyesha kwamba ni ghali zaidi ya mara 6 mpaka 7 kumpata mteja mpya kuliko kumtunza mteja wa aliyepo/wa kudumu. Taasisi za kifedha, mabenki na makampuni ya simu kwa mfano, yamejifunza sana katika hili, hivyo hawaoni tabu kuchukua hatua za ziada kuhakikisha mteja ambaye hakuridhishwa na huduma anapatitwa suluhu mbadala haraka sana kuendana na mahitaji yake. Hapa ndio utauona umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja.

6. WANAWEZA KUACHA KUWA WATEJA WAKO MUDA WOWOTE; Si jambo la ajabu hasa katika zama hizi za usasa mteja kuhamia kampuni yoyote atakayopenda kutumia huduma/bidhaa zake. Hii huchochewa zaidi na huduma mbovu/dhaifu za wateja wanazopatiwa zikiwemo kusubirishwa muda mrefu katika kupatiwa huduma/bidhaa/mrejesho/maoni kutoka kwenye kapuni/biashara fulani. Ni jambo lisolopendeza kabisa, lakini bado mambo kama hayo yanaendelea kutukia.

“Mteja anapokwambia hitaji lake, hakwambii tu kuhusu maumivu yake, anakwambia pia jinsi ya kutengeneza bidhaa/huduma itakayomfaa pamoja na biashara yenye ubora. Huduma kwa wateja zinatakiwa kubuniwa katika namna inayotambua changamoto hizo.” Anasema Kristin Smaby katika mtandao wa https://alistapart.com.

Huwezi kupata wateja watakaoridhika na bidhaa/huduma zako milele. Hivyo yakubidi kama mfanyabiashara kuzitafuta changamoto zinazowakabili wateja wako kwa; kuzungumza nao, waulize maswali kuhusu vile wanataka kujiskia ukiwahudumia, wape msaada pale watakapohitaji, wape ofa, punguzo la bei na mambo kama hayo. Utakapowahudumia vizuri wateja wako utakidhi mahitaji ya wote; biashara yako na wateja pia. Wao wanapata huduma bora, biashara inapata mapato na kila mmoja anabaki na furaha.

Njia bora zaidi ya kuhakikisha unazipata changamoto zinazowakabili wateja wako ni Kwa kutumia vizuri mitandao ya kijamii. Mitandao ya kijamii ni kiungo muhimu sana cha kuunganisha mfanyabiashara na wateja wake katika kuimarisha viwango vya utaoji huduma. Sasa unawezaje kuitumia mitando hii kwa usahihi? Tafadhali fuatana na link hii hapa.

Ni matumaini yangu leo umefahamu kwa undani umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja. Utakwenda kuzitumia vipi mbinu hizi za leo? Niambie kwenye comment hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo kuhusu umuhimu wa takwimu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu(website design, logo design, Digital consultacy n.k) BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA

Mtandao wa usafiri kwa njia ya nchi kavu barani Africa unajumuisha barabara na reli ambapo kwa wastani umechukua kilomita 6.2 kwa kila eneo la kilomita za mraba 100. Zaidi ya 60% ya mtandao mzima wa barabara haijatengenezwa kwa kiwango cha lami. Zaidi, pungufu ya 40% ya barabara za lami ndizo zilizo kwenye hali nzuri ya kupitika muda wowote. Sasa sekta hii ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika inatoa matumaini gani?

Mtandao wa njia za reli umeundwa kwa njia moja (single-track lines) ambazo huanzia maeneo bandarini kuelekea maeneo mbali mbali ya nchi/bara zikijumuisha viungio vichache tu njiani kuunga njia moja ya reli na nyingine (inter-linkages). Muundo huu wa reli zilizopo barani Afrika uliundwa nyakati za ukoloni na tangu wakati huo, ni marekebisho machache tu yameweza kufanyika ili kuwezesha treni ndefu zaidi zinazotumia dizeli kupita ambapo treni nyingi kati ya hizo hazitumiki tena kwa sasa.

Tukiangazia eneo la bandari, chini ya 50% tu ya matumizi ya bandari hutumika ikiwa ni pungufu ya mahitaji sahihi ya bandari hizo, jambo ambalo huchochewa na ucheleweshwaji wa mizigo na taratibu za forodha. Hali kadhalika, Afrika ndio inaongoza duniani katika ukuaji wa sekta ya viwanja vya ndege haswa kufuatia kuazishwa kwa soko huru lililoanzishwa baada ya makubaliano ya YD (Yamoussoukro Decision) yaliyofanyika mwezi November, 1999. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Afrika AU iliyotolewa mwaka 2014.

USAFIRISHAJI BARANI aFRIKA.
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Sasa changamoto; Je, sekta hii ya Usafirishaji na Miundombinu inaathiri vipi ukuaji wa biashara barani Africa? Na je, matumizi ya Teknolojia yana mchango gani katika kuboresha sekta hii ili kuinua biashara?

Kutokana na hali duni ya miundombinu na huduma za usafirishaji, gharama za kusafiri barani Afrika ni kati ya gharama ghali zaidi duniani, jambo ambalo linadhoofisha ushindani wa kibiashara katika masoko yote, ya ndani ya nchi na yale ya kimataifa.

Ripoti ya Tume inayoshughulikia Uchumi barani Afrika (ECA) imetaja kwamba nchi zisizo na bandari (landlocked countries) gharama za usafiri zinaweza kufikia robo tatu ya thamani ya bidhaa inayosafirishwa. Kwa mfano kusafirisha gari kutoka Japan mpaka Abijdan nchini Ivory Coast hugharimu US $1,500. Lakini kusafirisha gari hilo hilo kutoka kutoka jijini Abidjan hadi Addis Ababa hugharimu US $5,000. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa Teknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi kupitia link hii hapa yenye kichwa MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI. Ukimaliza hapo tuendelee na mada yetu ya leo.

Changamoto za Usafirishaji barani Africa.
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Gharama za usafirishaji zimetajwa kusababishwa na viwango vikubwa vya forodha, tozo za ucheleweshwaji, hasara zitokanazo na ajali pamoja na ukosekanaji wa fursa. Changamoto hizi huchagizwa zaidi na uduni wa miundombinu ya kiuchukuzi pamoja na huduma zinazotokana na nyanja hiyo.

Nayo programu ya maendeleo ya miundombinu barani Afrika (PIDA) katika ripoti yake imeainisha kwamba gharama za kiuchumi zinazosababishwa na changamoto za usafirishaji katika Mtandao wa Miundombinu ya Usafirishaji barani Afrika (ARTIN) zinazidi US $170 bilioni kwa mwaka kufikia mwaka 2014.

Changamoto hizo zimetajwa kusababishwa na;

•Kutokuwa na utendaji wa taratibu za kuwezesha biashara katika majukwaa ya ARTIN (kujumuisha bandari na vituo vya mipakani).

•Sera za nyanja ya usafirishaji ambazo zinapelekea kudhoofika na kuongezeka kwa gharama za usafirshaji kwa njia ya barabara pamoja na viwango duni vya barabara katika nchi nyingi barani Afrika.

• Sera za kiuchumi zinazozuia utendaji mzuri pamoja na utanuzi wa mifumo ya reli.

• Nyanja ya usafiri wa anga na Sera za kiuchumi zinazozuia uanzishwaji wa vituo vya anga vya kikanda, jambo linalotajwa kusababisha kuongezeka kwa gharama za usafiri huo.

Kufuatia changamoto hizo, Je, teknolojia ina mchango gani katika kuimarisha biashara na kupunguza gharama za uendeshaji?

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kuelekea mapinduzi ya nyanja zote za kiuchumi. (Yaani tutaendelea kuwa juu kileleni😁). Mapinduzi katika matumizi ya simu kutoka simu za mezani mpaka simu za rununu (smartphones), huduma za kifedha kielektroniki (fintech), biashara za kielectroniki (ecommerce) na kadhalika vimekuwa sehemu muhimu sana katika kurahisisha utendaji wa kibiashara katika sekta ya miundombinu na usafirishaji.

Benki ya Dunia (WorldBank) inaripoti kwamba ubunifu wa kiteknolojia umewezesha sana muingiliano wa kibiashara kwa kuzingatia ongezeko la watumiaji wa Intaneti huduma za simu. Kipimo cha wiani (density) katika matumizi ya huduma za intaneti kwa kila watu 100 waliopo eneo la Kusini mwa jangwa la Sahara, ni watu 17 tu ndio wameonekana kuwa watumiaji wa intaneti katika mwaka 2015.

website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako?
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika

Utafiti huo unakolezwa wino na shirika la kimataifa linalodhibiti mawasiliano ya simu GSMA ambapo kwenye ripoti yake ya mwaka 2018 limeangazia kwamba, eneo la kusini mwa jangwa la Sahara lilikua na kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu ya 44% kufikia mwishoni mwa mwaka 2017 kukiwa na watumiaji takriban 444 milioni sawa na 9% ya watumiaji wote wa simu duniani. Vile vile katika kipindi cha mwaka 2017-2022 watumiaji wa simu katika eneo hilo wataongezeka katika kiwango cha CAGR cha 4.8% ambayo ni zaidi ya mara mbili ya kiwango cha ongezeko kwa dunia nzima katika kipindi hicho hicho. Pia kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu inatajwa kufikia 50% kufikia mwishoni mwa 2023 na 52% mpaka mwaka 2025.

Kufuatia uchunguzi huo, sekta ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara barani Afrika inatajwa kuongezewa nguvu na maboresho zaidi ili kuendana na kasi hio ya ukuaji katika ICT. Matumizi ya GPS katika usafiri wa taxi yamerahisisha zaidi gharama na muda wa kutoka sehemu moja na nyingine, huku maboresho ya miundombinu kama barabara na viwanja vya ndege yakichagiza kasi ya sekta hio.

Zaidi, mtandao wa huduma za Posta na EMS unajumuisha takriban ofisi 30,000 barani ambazo ni muhimu katika kuwezesha e-commerce trade. Kwa kuliona hilo kampuni kama DHL zimejitosa kuhakikisha teknolojia inabadili huduma za posta kuwa rahisi zaidi.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi na jambo hili?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo kuhusu usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA
fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

FAHAMU KUHUSU TEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA HABARI NA BURUDANI

Baada ya zaidi ya miaka 10 tangu vuguvugu la mapinduzi ya kidijitali lilipoanza kushika kasi barani Africa, sekta ya Habari na Burudani ambayo inawavutia vijana wengi zaidi kwa sasa imeingia katika ukurasa mpya ambapo sasa sekta ya habari imekuwa ikiendeshwa kwa msaada wa teknolojia kwa kiasi kikubwa sana. Leo sasa, uta fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani. Kuna nini humo? Makinika mpaka mwisho..

Sekta hii iliyogawanyika kwenye maeneo kama Matumizi ya IntanetiTelevisheni, Sinema, Video Games, MagazetiMajaridaVitabuMuzikiRedio na kadhalika imechagizwa sana na mapinduzi yasiyozuilika ya Intaneti barani Afrika ambapo matumizi ya simu za rununu yamejenga msingi imara kama chanzo cha maboresho, ubunifu na mapato katika sekta hii.

Changamoto; Je, Teknolojia inabadili vipi sekta hii maarufu ya Habari na Burudani barani Africa?

Kwenye makala hii tutagusia changamoto chache zinazosibibu sekta hii maarufu kabisa. Lakini kwa undani zaidi wa changamoto hizo pamoja na jinsi ya kupambana nazo, tips, ofa mbalimbali na ushauri huwa tunashare kupitia status zetu za WhatsApp, utaipata kwa kugusa namba yeu hii hapa 0765834754. Make sure umeisave kisha nitumie text yenye jina lako ili uanze kufaidi elimu ya BURE kabisa.

Makampuni, Wafanyabiashara, Wasanii na Mashirika ya serikali wanatilia mkazo katika kubuni huduma na bidhaa bora kila siku katika kuboresha utendaji wa sekta hii maarufu na inayopendwa zaidi na vijana barani Afrika ambapo tukianzia nchini Kenya sekta hii ilionyesha ukuaji wa 17.0% katika mwaka 2017, ukuaji ukichagizwa na maendeleo makubwa katika eneo la Matumizi ya Intaneti.

Vile vile ongezeko la watu katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) cha 11.6 litaipaisha sekta hii mpaka kufikia pato la dola za Kimarekani bilioni 2.9 kufikia mwaka 2022 kutoka $ 1.7 bilioni zilizorekodiwa mwaka 2017. Karibu wateja wapya milioni 15 wanatarajiwa kuwa mtandaoni ndani ya miaka 4 ijayo, na zaidi kunatarajiwa kuwepo kwa huduma za kasi ya juu za intaneti.

Katika huduma za kifedha; MPESA imerahisisha sana malipo ya bidhaa/huduma mbalimbali nchi kenya na hivyo kufanya sekta ya Habari na Burudani kuzidi kuimarika.

fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

Huduma za Televisheni; Kenya ni moja ya nchi mwanzo barani kufanikiwa kuhamia katika mfumo wa kidijitali ambao umefungua fursa nyingi zikiwemo huduma za televisheni na utengenezwaji wa mawaidha kidijitali. Hali hii imeibua ushindani mkubwa katika eneo hili ambao unazidi kupeleka mbele na kunogesha maendeleo ya sekta hii ya Habari na burudani.

Kwa kuongezea ujio wa makampuni kama Kwese TV na Startimes ambayo hutoza kiwango kidogo zaidi cha malipo ya huduma zao kwa mwezi, kumeongeza ushindani kwa kiasi kikubwa dhidi ya kampuni kongwe ya Multichoice katika utoaji wa maudhui ya televisheni nchini Kenya.

Redio; ongezeko la huduma na vifurushi katika mashirika ya Redio unakuza kwa kiasi kikubwa sekta hii ambavyo hutoa matangazo ya biashara mbalimbali mtandaoni na katika magazeti. Redio nyingi sasa zinalazimika kuhamia katika mtindo wa mobile applications ili kuwafikia watu wengi zaidi na kuongeza wigo wa mapato yao.

TANZANIA:

Sekta hii ya Habari na Burudani inakuwa kwa kasi sana nchini humo ambapo kwa mwaka 2017 sekta hio iliingiza pato la dola za kimarekani milioni 496 ukiwa ni ukuaji wa 28.2% kwa mwaka. Ongezeko la watu kwa kiwango cha CAGR cha 18.3% utashuhudia mapato ya sekta hio kufikia $1.1 bilioni mwaka hadi mwaka 2022 ambayo ni mara 2.3 zaidi kulinganisha na ilivyorekodiwa mwaka 2017.

Kiujumla ni Nigeria peke yake katika Africa ndio imeizidi Tanzania katika kasi ya ukuaji wa sekta hii ya Habari na Burudani. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Kimataifa la PwC. (Wabongo mnatisha kwa habari na bata 😂).

Internet; Kitakwimu kunatagemewa ongezeko la watumiaji wa huduma za 4G ambapo makampuni ya Vodacom na Zantel tayari yalishazindua huduma zao za 4G LTE tangu robo ya pili ya mwaka 2016. Mwaka 2017 TIGO walitangaza uwekezaji wa $70 million ili kutanua wigo wake wa kimtandao na kujiandaa na matumizi ya kasi ya 5G. Hata hivyo mpaka kufikia mwaka 2022, huduma ya kasi ya intaneti ya 3G bado itaendelea kutumika zaidi kufikia takribani 70% ya watumiaji.

Televisheni; matumizi ya huduma za ving’amuzi na televisheni yatapaa kutoka watumiaji 200,000 waliorekodiwa mwaka 2013 mpaka watumiaji 900,000 kufikia mwaka 2022 kwa huduma za televisheni za majumbani. Watumiaji wengi pia hutumia huduma za ving’amuzi kutoka kwa makampuni ya Multichoice na Startimes.

Magazeti; Ukiachana na matumizi ya intaneti yanayoshika kasi nchini Tanzania. Magazeti pia yanaongeza chachu katika uboreshaji wa sekta hii ya habari na burudani ambapo matumizi rasmi ya lugha za Kiswahili na Kiingereza yamekuwa nguzo muhimu.

Lakini kwa Tanzania nyanja ya magazeti inakwenda ikibadilika kwa kasi, kwa mfano kampuni ya Vodacom imebuni application ya M-Paper ambayo imewezesha kupatikana kwa vichwa vya habari vya magazeti maarufu zaidi nchini na hivyo kufanya upatikanaji wa habari kuwa mkubwa zaidi.

Ikiwa na jumla ya mapatoyaliyotokana na matangazo kufikia dola za kimarekani milioni 91 katika mwaka 2017 na kutabiriwa kufikia $128 milioni mwaka 2022, ni dhahiri sekta ya habari na burudani inakuwa sawia nchini humo na hivyo kuchipusha milango mingi ya kibiashara kuendelea kufanyika.

AFRIKA KUSINI:

Ongezeko la watu katika nchi hii linatajwa kuwa imara kwa kiwango cha CAGR cha 7.6% kwa mapato ya watumiaji wa sekta hii ya habari na burudani kufikia mwaka 2022 ambapo mapato yatapaa kutoka Randi 93.9 bilioni zilizorekodiwa mwaka 2017 mpaka kufikia Randi 135.7 biloni mwaka 2022.

Ukiachana na mapato yanayotokana na matumizi ya Intaneti (ambayo huchagizwa na mapato yatokanayo na applications za simujanja) kuna uwanja mkubwa zaidi wa mapato ambayo huongozwa na michezo ya video (video games). Mapato kutoka kwenye michezo hii nchini SouthAfrica yanazidi maeneo mengine kama vitabu, Business-to-business (B2B) na mauzo ya majarida. Ukuaji huu katika eneo la michezo ya Video umekolezwa na ongezeko la matumizi ya simujanja, uboreshwaji wa huduma za kasi ya intaneti kutoka 3G mpaka 4G kuzidi kuongezeka jambo ambalo linaifanya watumiaji wa Afrika Kusini kuwa ni wacheza games 😁.

Televisheni; Kama ilivyotegemewa, huduma za TV na Video zitaendelea kuongoza katika kuzalisha mapato ya watumiaji, lakini muda mchache ujao Kampuni kama Netflix na Amazon Prime huduma zao zitachukuliwa kama nyongeza kunyongea kwa maudhui yao ya burudani katika soko la Afrika Kusini. Vile vile malipo ta TV yataongeza Randi bilioni 6 mpaka kufikia mwaka 2022 kwa kiwango cha 5% ya CAGR japokuwa ukuaji wa mwaka-kwa-mwaka unategemewa kuoungua kwa 2.6%.

Matangazo; nyanja hii iliathiriwa zaidi katika mwaka 2017 na mazingira ya uchumi wa Afrika Kusini ambapo kulikuwa na ukuaji wa tahadhari wa 2.1% tu mwaka kwa mwaka. Hata hivyo, maboresho yanategemewa mpaka kufikia mwaka 2022, ikiwa na 3.3% ya CAGR ambayo itapaisha mapato zaidi.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.Umejifunza nini leo kwenye ku fahamu kuhusu teknolojia katika sekta ya habari na burudani.

Makala hizi hapa zitakupa taarifa zaidi kuhusu Teknolojia ya Habari na Burudani katika biashara yako:

  1. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BANDO LAKO NI MTAJI
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia; Karibu sana REDNET TECHNOLOGIES