Tag: faida za teknolojia

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA

June 23 mwaka huu, Jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika, SADC kwa kauli moja ilipitisha muongozo wa kurasinisha shughuli za kibiashara baina ya nchi wanachama wake. Sasa unajiuliza, huo Urasinishaji ndo nini? Na una manufaa gani katika biashara yako?

Ushindani wa kimasoko ukiongezea, ukiongezea ongezeko la wimbi la wateja wa huduma za kidijtali, hali hii inaongeza changamoto kila leo katika mazingira ya kibiashara hususan barani Afrika ambapo wafanya biashara wengi bado hawatumii mwanya wa teknolojia katika shughuli zao za kiuchumi za kila siku.

Hata hivyo, bado wafanyabiashara wanaamini katika Ubunifu wa mbinu katika kukuza na kuimarisha biashara zao na kunasa wateja wengi zaidi. Hili litawezekana vipi katika mazingira ya kisasa ya Masoko Huru na matumizi makubwa ya kiteknolojia? Jibu mbadala ni Urasinishaji wa shughuli za kibiashara hasa kwa kupitia matumizi mazuri ya teknolojia za mawasiliano na habari.

URASINISHAJI NI NINI?

Ni utaratibu/mchakato wa kuoanisha/kuunganisha shughuli za kibiashara kisheria baina ya maeneo kadhaa/nchi/Jumuiya za maendeleo/Kampuni/Mashirika ili kutanua soko la wafanyabiashara, kuongeza wateja na kukuza uchumi wa washirika. Umenipata apo?

Sasa taratibu zote za kibiashara zinapokuwa sawia pamoja na utekelezaji mzuri wa sera za biashara na maendeleo, basi bila shaka biashara zitashamiri na kuongeza kasi ya kukuza uchumi imara na ongezeko la wateja wa huduma na bidhaa baina ya washirika. Urasinishaji ndio mbinu.

Ili kuweza kurasinisha biashara kwa mafanikio, leo tutajadili hatua 5 muhimu za Kuwezesha Zoezi la Urasinishaji katika Biashara yoyote (hata hio unayoifanya wewe). Hatua hizi huitwa pia Viwezeshaji vya Urasinishaji (Enablers towards Harmonization in Business). Twende nazo sasa.

1. UTAWALA BORA

Nikwambie tu, hakuna biashara ya kiungwana inayoweza kufanyika katikati ya vita na machafuko. Biashara inahitaji mazingira salama ya kufanyika. Biashara ni kama mtoto mdogo, inahitaji malezi bora ili iweze kukua, kushamiri na kurudisha faida mara dufu. Hivyo jukumu la kutunza na kudumisha mazingira ya amani na utulivu ni la kila mmoja, hasa mfanyabiashara, lazima uhakikishe eneo lako la biashara lina amani na ni salama kwa yeyote kufanya biashara na wewe. Serikali kama mlezi mkuu, husimamia amani na usalama wa nchi wakati wote kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama wA nchi kama polisi na jeshi.

2. KUONGEZA MAARIFA

Zoezi la kuoanisha shughuli za biashara mbalimbali linakwenda sambamba na kuongeza maarifa ya kufanya biashara hizo. Hivi wewe mfanyabiashara unaweza vipi kukuza mtandao wa biashara yako kabla hujaongeza maarifa kuhusu biashara yako na biashara zingine ambazo unahitaji kushirikiana nazo? Hakika, huwezi kufanya/kuendelea kufanya biashara pasi na kuwa na maarifa sahihi, utadumaa kibiashara au kuishia kufilisika tu. Maarifa ndio chakula cha biashara. Lazima uwe mjanja, usikubali kuwa hapo ulipo kila siku. Ongeza ujuzi biashara ikue io.

3. UHUSIANO NA WATU

Kama ulikua hujui, Biashara ni mahusiano na mahusiano ni watu. Na watu ndio hao unawaona kila siku na wengine huwaoni ila wapo. Jumuiya ya SADC pekee inakadiriwa kuwa na wakazi takriban milioni 400. Watu wote hawa unawahusisha vipi kwenye biashara yako? una mpango gani wa kuongeza wigo wa watumiaji wa bidhaa/huduma zako? Kama unafanya biashara ambayo haiongezeki wateja, hivi unajua kuwa hio biashara inakwenda kufa muda si mrefu? Waswahili wanasema, “Ongea na watu uvae viatu.” Kalagabaho.

4. MATUMIZI YA TEKNOLOJIA

Mwaka 2018 duniani yalianza mapinduzi ya 4 ya Viwanda ambayo kwa kiasi kikubwa yanahusisha matumizi ya teknolojia ya kompyuta na intaneti katika nyanja mbalimbali ambazo hapo kabla hazikuwa zikitumia teknolojia hio. Matumizi ya smartphones katika kuchakata na kuhifadhi rekodi za kibiashara, matumizi yanayoshika kasi ya mitandao ya kijamii katika kutangaza na kufanya biashara, ujui wa vifaa janja vya kielektroniki (smart devices) pamoja na uanzishwaji wa Maeneo Huru ya kufanyia biashara, kwa mfano, barani Afrika mwaka 2018 ulianzishwa mchakato wa kuanzishwa kwa Eneo Huru la kufanyia Biashara (African Continental Free Trade Area) AfCFTA lenye lengo la kuruhusu nchi wanachama kufanya biashara kwa wepesi na haraka katika kukuza uchumi wao. Kufahamu zaidi kuhusu AfCFTA na faida zake katika mchakato mzima wa urasinishaji wa shughuli za kibiashara barani Afrika, tembelea makala kupitia link hii hapa https://rednet.co.tz/kuanzishwa-kwa-eneo-huru-la-biashara-barani-africa-afcta-kuna-manufaa-gani-kwako/ yenye kichwa “KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?”. Pitia hapo, kisha tuendelee..

Sasa katika njia zote hizi zilizotengenezwa katika msingi wa Kiteknolojia, jiulize, unatumiaje mianya hii iliyotengenezwa kwa ajili ya kukuza na kuimarisha biashara yako? Teknolojia ni uwanda mpana sana na unaweza kuutumia vyovyote vile kuendana na mahitaji ya biashara yako. Kwa taarifa ushauri wa jinsi ya kutumia teknolojia vyema, usisite kuwasiliana nasi sasa kwa kutembelea tovuti yetu maridhawa ya www.rednet.co.tz, tupigie simu au tutumie barua pepe.

5. VIPIMO NA UFUATILIAJI

Ili mambo yote tuliyoyaona yaweze kufanyika kwa usahihi, hakuna budi kila hatua ipimwe na kufuatiliwa vizuri ili kuhakikisha hatua zimefuatwa sawia katika kurasinisha biashara kwa manufaa ya wote. Waswahili wanasema “Biashara haina undugu” Na pia “Kwenye kazi ifanyike Kazi”. Hivyo kwa jinsi hii sheria zilizowekwa wakati wa kuanzishwa kwa urasinishaji lazima zifuatwe ili kuhakikisha kila mshirika wa Urasinishwaji huo anafaidika sawa sawa na juhudi zake.

BONUS POINT:

Urasimishwaji unaweza kufanyika na kuhusisha biashara yoyote. Mfano mfanyabiashara wa viungo vya chakula kama nyanya, karoti, hoho, Anaweza kuungana na mfanyabiashara wa chakula katika migahawa katika biashara zao halafu mambo yakawa safi kabisa. Pia mtunzi wa hadithi na riwaya anaweza kukaa chini na mbunifu wa mitindo ya nguo na fasheni na waongozaji wa filamu na hivyo kufanya kazi bora katika kiwanda cha filamu na maonyesho na watu wote tukasimama kwa heshima. Hata mfanyabiashara wa viatu na nguo akikaa vizuri na mtaalam wa kutengeneza tovuti za mauzo (ecommerce website) wanaweza kutengeneza e-commerce platform moja, kila mtu duniani akanunua viatu na nguo na jamaa wa IT akapata gawio lake safi kabisa.

Pia kuna hizi makala ambazo ukizisoma zote zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna ya kuimarisha biashara kwa kushirikiana na wafanyabiashara na wadau wengine. Cha kufanya, gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/biashara-yako-inaweza-vipi-kuwa-taasisi-imara/ yenye kichwa “BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA?”
  2. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”
  3. https://rednet.co.tz/ukiritimba-katika-biashara-ni-asali-au-shubiri/ yenye kichwa “UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?”

Huo ndo Urasinishaji katika biashara kwa ufupi, moja kati ya mbinu makini sana katika kukuza biashara kwa kutumia biashara ingine. Wazungu wanaita B2B au Business To Business. Ila sisi tunaita Harmonization of Business kama tulivyoiona definition kule juu. Una lolote? Tafadhali maoni yako ni muhimu.

KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?

Hebu fikiria wewe ni mgeni mahali fulani, baada ya kushikwa na njaa unaelekezwa migahawa miwili, mmoja ukiutafuta mtandaoni unaweza kupata taarifa zake mwingine hauna taarifa yoyote mtandaoni. Uelekeo wako utakuwa upande gani? Leo sasa tutakwenda kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako. Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Kuishi katika ulimwengu wa kidijitali, tovuti ni zana muhimu sana katika biashara na masoko ya kidijitali. Cha kushangaza inakadiriwa 35% – 50% ya biashara ndogondogo duniani hazina tovuti zao binafsi, jambo linalozinyima fursa ya kuweka taarifa zao kirahisi mtandaoni na kupata wateja wapya kirahisi.

Kuna wanaosema kuwa matumizi ya Tovuti yanamezwa na uwepo wa mitandao ya kijamii ambayo pia watu wanaweza kuweka na kutangaza biashara zao humo. Ni kweli, aghalabu, kwa kutumia Mitandao ya kijamii hauna uhakika wa kumiliki taarifa na maudhui unayoweka humo muda wote. Watengenezaji ambao pia ni wamiliki wa Mitandao hio wanao uwezo wa kusimamisha/kufuta akaunti au maudhui yako muda wowote ikiwa biashara/maudhui yako yanakwenda kunyume na matakwa na masharti yao.

Vile vile Mitandao ya kijamii unayotumia inaweza kupungua umaarufu au kufilisika muda wowote usioutegemea mfano kuna mitandao ilikua maarufu sana zamani kama Hi5 lakini umaarufu wake kwa sasa umepungua au kupotea kabisa. Hivyo, uwezekano wa kudorora kwa biashara yako kunategemea pia umaarufu wa mtandao wa kijamii unaoutumia, jambo linalichangiwa sana na ujio wa mitandao mipya ya kijamii kama Instagram, Whatsapp na TikTok. Hii kwako unaionaje? Nitaeleza Tofauti katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Tovuti wakati Ujao.

Faida ni nyingi sana za matumizi ya website katika kuimarisha biashara yako kupitia ulimwengu wa Teknolojia. Tayari tumekuandalia makala maalum kupitia link hii hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

Leo hii ntakwambia mambo 10 kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika biashara yako:

1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:

Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu huenda wapi kutafuta vitu kama suppliers, bidhaa na huduma mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi. Injini za matafuto mtandaoni zimekuwa kimbilio namba moja huku GOOGLE Ikiziacha mbali Injini zingine kama Yahoo, Bing na Ask. Maana yake hii ni kwamba kama huna tovuti, jua mauzo yako ni 7% tu ya soko zima ambalo hujui kuwa unalo. Upo apo? Yani unapoteza 93% ya mauzo yako kila siku bila hata wewe mwenyewe kujua.

2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)

Kama una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo. Kwa biashara zenye malengo makubwa kuwa na tovuti huwaweka kwenye nafasi za juu katika kupata tenda na wateja, na huonyesha Uweledi bora katika utendaji wa biashara kuanzia katika muonekano na utendaji wa tovuti. Inakadiriwa 80% ya watu duniani huonyesha kutokua na imani na Biashara ambazo hazina tovuti pale wanapotaka huduma/bidhaa fulani mtandaoni.

3. KUPATIKANA KWA URAHISI

Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi, tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako. Ndivyo ilivyo kwa tovuti ambayo inajieleza kwa kila kitu kama ilivyo tovuti maridhawa ya http://rednet.co.tz . Ile raha ya kupata taarifa, huduma au bidhaa kirahisi kupitia simu yako ya mkononi, hufanya wateja waongezeke maradufu na kusambaza sifa bora kwa uharaka sana katika jamii na katika mitandao ya kijamii hali kadhalika.

Hii huongezwa chumvi ya SEO (Search Engine Optimization) ambayo ni teknolojia iliyowekwa katika Injini za matafuto ya kimtandao inayowasiliana na tovuti yako na kuweka taarifa katika Injini hizo na hivyo kufanya taarifa za tovuti yako kuonekana haraka zaidi katika matafuto. Biashara imerahisishwa sana kupitia SEO kuliko kutumia Mitandao ya kijamii. Kama watu wanakwenda Google kutafuta taarifa, basi fahamu taarifa hizo hupelekwa hapo GOOGLE kwa kutumia teknolojia iitwayo S.E.O. Kufahamu zaidi kuhusu SEO gusa hapa chini

4. TANGAZO LA BURE MUDA WOTE

Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo huduma ya internet inapatikana. Tangazo la bure kabisa hili. Kama tovuti yako ina ubora wa kuvutia zaidi katika muonekano, maudhui na utendaji, basi bila shaka biashara yako ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri sokoni na kupata wateja wengi kila siku. Jiulize hivi, unapofunga ofisi/biashara yako wakati wa jioni kila siku, wateja wapya wanaweza vipi kupata taarifa sahihi muda watakaohitaji?turudi kwenye mada yetu, kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Hii pia inawezeshwa sana na teknolojia ya S.E.O.

5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)

Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa. Kupitia tovuti yako, unaweza kuweka testimonials kwa idadi uitakayo bila kurudia rudia na katika mpangilio maalum na watu wakaweza kuona ushahidi utakaowaridhisha kuendelea kutumia huduma/bidhaa zako. Mara nyingi Mitandao ya kijamii huzuia kuoneka kwa biashara kwa urahisi kutokana na wimbi la watumiaji wenye maudhui tofauti tofauti katika ratiba ya saa (timeline) yako unayopitia katika mitandao hio, hivyo kusababisha usumbufu (distractions) katika biashara yako.

6. UAMINIFU (TRUST)

Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza mahusiano na mteja kama UAMINIFU. Ili kupata wateja wa kudumu katika sekta nyingi, kuwa na tovuti hai ni muhimu katika kudumisha mahusianao katika ya mfanyabiashara kwa muda wowte mteja atakaohitaji.

7. POSITIVE ROI

Ikiwa ni Return On Investment (ROI) au Rejesho baada ya Uwekezaji, unapoendesha biashara ambayo ina gharama zake kama umeme, kodi, maji, mafuta n.k, ukijiuliza utaweza vipi kurudisha gharama hizo upate faida? Njia moja nzuri ni matumizi ya tovuti bora yenye uwezo kunasa wateja wapya kwa njia ya mtandao muda wote (24/7) kirahisi kabisa.

8. THAMANI INAYODUMU

Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote itakapohitajika kufanya hivyo. Hivyo thamani ya biashara yako itaendelea kuwepo muda wote tovuti yako inapokuwa hewani.

9. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA

Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei, ushauri nakadhalika. Hivyo kuimarisha mahusiano na ukaribu wako na wateja wako wakiwa popote duniani kwa urahisi kupitia miundombinu mbalimbali unayoweza kuiweka katika tovuti yako kama matumizi ya chatbots na barua pepe maalum za kibiashara (zenye jina/domain name ya tovuti yako).

10. MASIJALA (DATA CENTER) RAHISI YA MTANDAONI

Tovuti yako inaweza pia kuwa masijala rahisi kwa wafanyakazi, wateja na mtu yeyote anayehitaji kujua taarifa kuhusu huduma/bidhaa unazohusika nazo. Mfano mzuri ni tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz ambayo zaidi tu. ya kwamba inatoa taarifa kuhusu huduma tunazohusika nazo za kutengenza websites, softwares, apps n.k, lakini pia tovuti inatoa taarifa muhimu mbalimbali kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia. Taarifa hizi zimetengenzwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha Biashara za wateja wakiwa popote duniani. Pia taarifa hizo zinalenga kuhamasisha matumizi ya Teknolojia katika njanja mabimbali za kiuchumi haswa kwa wafanyabiashara waliopo kusini mwa jangwa la Sahara.

NOTE: Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa muhimu kama jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.

BONUS POINT: Tovuti yako unapoisajili, unashauriwa pia upate kirurushi cha barua pepe yenye jina/domain name sawa na tovuti yako. Mfano, tovuti yako inapatikana katika anwani ya www.mfano.com, hivyo barua pepe yako ya kiofisi unaweza kuchagua kuwa info@mfano.com au maulizo@mfano.com au jinalako@mfano.com. Kwa kutumia barua pepe zenye jina sawa na anwani ya tovuti yako, unajiweka katika nafasi nzuri ya kuimarisha biashara yako na kuongeza wateja wapya na kazi zenya manufaa haraka zaidi katika biashara/kampuni yako. Hii ni sababu muhimu sana unapojiuliza kwanini ni muhimu kuwa na website (tovuti) rasmi ya biashara yako. Website inakufanya unakuwa official kiukweli kweli.

Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna bora za kuimarisha uchumi wa biashara yako kwa kutumia Teknolojia:

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. BRANDING vs MARKETING, KIPI NI KIPI?
  3. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA (AfCFTA), KUNA MANUFAA GANI KWAKO?
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO.

Umejifunza nini kupitia makala hii ya kuhusu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Tafadhali unaweza kuwasilisha maoni yako kupitia sanduku la maoni (comments box) lililo hapo chini au kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yanayopatikana katika Footer Bar chini kabisa ya ukurasa huu. Pia usisite kuwashirikisha wenzako makala haya kwa kushare link yetu ya https://rednet.co.tz mara zote. Karibu!

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) â€“ 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE

Yaani ni 8% tu ya makampuni ndio wana uwezo wa kugundua wizi wa taarifa zao ndani ya dakika chache. 62% wanaweza kugundua wizi ndani ya siku kadhaa. Wewe unatumia muda gani kugundua upotevu/wizi wa data katika kampuni yako? Makala hii tutaangazia mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) kiundani. Leo, yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake. Makinika mpaka mwisho.

Kama Unavyoona biashara zinavyozidi kushamiri kiteknolojia ndivyo wadukuzi nao wanazidi kutafuta mbinu za kufanya mashambilizi zaidi. Mwaka 2019 peke yake, zaidi ya 2$ billion zilipotelea mikononi mwa wadukuzi duniani. Utafiti wa Juniper unaonesha namba hio inaongezeka kila mwaka.

Unalikumbuka shambulizi lilioitwa NotPetya? Basi jarida la WIRED linalitaja shambulizi hilo kama “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA”. Ndani ya masaa machache tu virusi vya shambulio hilo (malwares) viliathiri kutoka biashara ndogo za Software nchini Ukraine mpaka kusambaa katika vifaa vya kielektroniki dunia nzima. Shambulizi lilidhoofisha mashirika makubwa duniani kama FedEx, TNT, Express na Maersk kwa wiki kadhaa na kusababisha hasara ya zaidi ya $10 bilioni kwa ujumla. Upotevu wa data kwa kiwango hiki unaonyesha namna katili ya dunia tuishiyo ambapo inaonekana hakuna mwenye kinga madhubuti mtandaoni. Kutoka Mashirika makubwa, serikali, mitandao ya kijamii, mifumo ya migahawa na sehemu yoyote unayojua inatumia teknolojia ya IT, Kila mmoja yupo hatarini.

TUMEFIKAJE HAPA?

Ripoti ya mwaka 2019 ya shirika la Accenture Security kuhusu Matishio ya kimtandao (Cyber Threatscape), imeonyesha sababu za wadukuzi kuendelea kuwa tishio dhidi ya taarifa binafsi/za mashirika kwa manufaa yao. Hizi ni baadhi sababu hizo:

1. Wadukuzi wa kimtandao hufaidika zaidi na teknolojia mpya na kukosekana mawasiliano madhubuti katika sheria na tawala za maeneo/nchi mbalimbali duniani.

2. Mitandao ya kihalifu muda wote inakwenda ikibadilika, hasa kuelekea katika makundi ya kihalifu ya siri (syndicates) pasi na kujulikana chanzo chake kwa kutumia nyaraka halali kwa nia halifu.

3. Malengo mseto katika kuimarisha tabia za virusi (kama kujiendesha vyenyewe: self replication)

4. Kuimarika kwa mifumo ya Ulinzi wa Kimtandao (cybersecurity hygiene) inapelekea wadukuzi nao wazidi kujiimarisha kimbinu na maarifa katika uwanda wa kiteknolojia na matumizi ya internet.

Baada ya kujua sababu zinazowasukuma Wadukuzi na wahalifu wa Kimtadao kuendelea kufanya mashambulizi, Leo, uta yafahamu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako, Fuatana nami..

Duniani kunazo aina nyingi za mashambulizi ya kimtandao kulingana na sababu nilizozieleza hapo juu kama ifuatavyo:

1. RANSOMWARE ATTACK: Katika shambulio hili, virusi maalum (specific malware) ambavyo hukusanya na kufunga taarifa/kifaa katika mtandao ili kumnyima mtumiaji haki na uwezo wa kufanyia kazi taarifa zake kama kawaida. Haki na uwezo (access) huo humrudia mtumiaji pale tu matakwa ya mdukuzi yatakapotimizwa ambayo mara nyingi huwa ni pesa au rushwa kwa mapana yake.

Saa ingine wadukuzi wanaweza kugoma kurudisha haki za matumizi kwa mhusika hata wanapotimiziwa matakwa yao, hivyo kuongezea hasara kwa kampuni/biashara. Mbaya zaidi, ripoti ya mwaka 2019 ya Uhalifu wa kimtandao inaonyesha kutokea kwa shambulizi hili kila sekunde11 ya mwaka 2021.

2. ADVANCED PERSISTENT THREATS (APT): Shambulizi hili sio la mojakwamoja (passive attack) ambapo mdukuzi anapata access ya computer/mtandao fulani kwa muda mrefu pasi na kujulikana, hivyo kujichotea taarifa na kuzitumia kwa manufaa yake. Aina hii pia huitwa Trojan Horse attack.

3. PHISHING: Je wajua? Mpaka 32% ya wizi wa data husababishwa na shambulizi hili. Hii ni aina ya shambulizi maarufu sana la kijamii (social engineering) ambapo mdukuzi humtegea mtu adownload file lililo na virusi kupitia SMS, email au link na kuingiza virusi katika kifaa chake.

unawezaje kujilinda dhidi ya shambulizi la kimtandao la phishing katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

4. SQL INJECTION: Umeshawahi kuona ile unaingia kwenye website ukakuta haipo ghafla tu, au kwenye system flani unanashangaa kuna mafiles huyaoni bila sababu ya msingi. Sasa kwa kutumia virusi halifu (malicious codes) shambulizi hufanyika katika servers zinazohifadhi taarifa muhimu za watumiaji na kuzifuta, kuziiba au kuzibadili ili kutimiza azma fulani ya wadukuzi na/au genge lao. Mara nyingi shambulio hili hufanyika kwenye servers zinazohifadhi taarifa ghafi za watu au vitu (personal identifiable information: PII) kama namba ya kadi, username and passwords.

5. DDOS ATTACK: Kirefu huitwa Distributed Denial of Services attack ambapo hutokea pale wadukuzi wanapofurika tovuti au kifaa chako kwa either kupunguza au kondoa kabisa utendaji wa kawaida na hivyo kuiacha kampuni/biashara kuhangaika kurejesha performance ya mifumo yake wakati wao (wadukuzi na virusi vyao) wakitumia mwanya huo kuiba na kufanya uhalifu katika mifumo hio iliyoathirika.

6. MAN IN THE MIDDLE (MITM): Hii hutokea pale mdukuzi anapoingilia mawasiliano halali ya kampuni bila ya wao kujua. Pia shambulio hili hufahamika kama eavesdropping pale linapofanyika baina ya mawasiliano binafsi ya simu kati ya mtu na mtu.

Mawasiliano katika MITM hiungiliwa pia kupitia APN za Wi-Fi za uongo (deceptive wifi). Zaidi ya kuingilia mawasiliano, hapa mdukuzi anaweza pia kuwasiliana akitumia utambulisho (ID) ya wahusika pasi na kufahamika mara moja.

7. PASSWORD ATTACK: Licha ya kuwa shambulizi maarufu zaidi duniani, bado kuna watu huangukia mtego wa kuibiwa nywila zao. Kwa urahisi wake, wadukuzi hutumia mbinu zenye viwango na ujanja kupata nywila dhaifu na kufungua accounts za watumiaji kirahisi. Hapa tunaangukia kwenye usalama wa vifaa vyetu vya mtandaoni. Je viko salama kiasi gani? Fuatana na makala hii hapa kufahamu zaidi..

UNAWEZAJE KUZUIA MASHAMBULIZI HAYO?

Katika yetu iliyopita tumeeleza kwa kirefu kuhusu namna ya kujiepusha na mashambulizi ya kimtandao (Cyber attacks), pitia hapa KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?“. Leo pia, tutaona njia zingine za kuendelea kujiimarisha na kuzuia mashambulizi hayo yasiathiri Biashara/Kampuni yako. Mashambulizi mengi niliyoyaelezea leo yanazuilika kwa njia ambazo tayari tulishaziona katka makala zilizopita isipokuwa:

MITM Attack: •Tumia SSL Certificates za (https) katika website yako. Hii ni boresho la http SSL certificate ambayo ni ya zamani na usalama wake mi mdogo.

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

•Tengeneza VPN yako kama ngao ya ziada dhidi ya wi-fi halifu (deceptive wi-fi). Mashambulizi haya katika biashara yako yana madhara makubwa ikiwemo Kupotea kwa Fedha, faida ya biashara, mauzo, matengenezo, Hadhi ya biashara kushuka au kupotea kabisa na madhara ya kisheria.

Hivyo unapaswa kuwa makini na kufuata ushauri wa kitaalamu kuhusu maboresho ya kimtandao (updates & maintenance) ili kuhakikisha unatumia teknolojia ya kisasa zaidi ambayo ni salama huku ikiwa imeambatana na Passwords zako zilizo bora. Utajuaje kama simu/computer yako ikiwa imedukuliwa? Majibu tayari yanapatikana kwenye makala iliyo hapa UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?.

Usalama wa Kimtandao ni jukumu langu. Ni jukumu lako. Ni jukumu letu sote. Tuchukue tahadhari muda wote tuwapo mtandaoni. Basi ni matumaini yangu leo mengi umeyafahamu kuhusu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako. Ukiwa na swali au nyongeza tafadhali tuandikie katika comments hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo? Umejifunza nini katika ku yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake katika biashara/kampuni yako.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) â€“ 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Unawezaje kujikinga dhidi ya mashambulizi ya kimtandao katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?

Imeibuka kuwa issue muhimu sana ya kuzingatia katika zama hizi za kiteknolojia ambapo kumekuwepo na wimbi la mashambulizi ya kimtandao kwa watumiaji duniani kote. Kama unatumia Android, iOS, Windows7, 8, 10, Ubuntu na OS zingine unazozijua basi fahamu tayari upo katika hatari ya kushambuliwa na wadukuzi wenye nia ovu na uhalifu katika kuiba taarifa zako, mali na hadhi yako katika jamii inayokuzunguka. Sasa utafanyaje ili ujikinge na hatari za mashambulizi hayo? Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako? Fuatana nami leo mpaka mwisho nitakufahamisha.

Mwaka 1988, Robert Morris akiwa nguli wa mitandao alitengeneza shambulio la kimtandao lilioitwa CHRISTMASS TREE WORM katika internet ambapo mifumo zaidi ya 2000 iliharibika na computer zaidi ya 6000 ziliathirika kwa siku moja tu nchini Marekani. Kwa kuwa alikua ni afisa wa Shirika la NSA (National Security Agency) alikamatwa na kupigwa faini ya 10,000$.

Japokuwa faini ilionekana ndogo kwake lakini dunia ilipata funzo muhimu sana kuhusu Usalama wa Data za watumiaji wa internet wawappo mtandaoni. Hata hivyo, katika muongo wa 1980’s mpaka 1990’s, wadukuzi wa mitandao Hawakuwa tishio sana duniani moja ya sababu ikitajwa ni kutokuwa na matumizi makubwa ya internet na kuwa na watumiaji wachache.

Lakini mambo yalikuja kubadilika mwishoni mwa miaka ya 1990’s na mwanzoni mwa 2000’s ambapo Udukuzi ulianza kutumika kama biashara na kuwa silaha ya kimbinu Katika idara mbalimbali za kiserikali, kibiashara au kibinafsi ambapo ujasusi wa taarifa umechochea kwa kiasi kikubwa katika kutafuta, kuchakata na kutumia taarifu mbalimbali kwa manufaa ya kiuchumi au kibinafsi..

Wanafanyaje Mpaka kuifikia Computer/kifaa chako? Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

Mashambulizi haya ya kimtandao yalianzia katika matukio ya Uhuni wa mtaani katika kuibiana taarifa, mpaka kufikia Oparesheni za kidunia zinazohusu Mashirika makubwa, majeshi, Idara za kiresikali na Magaidi. Mwaka 2008, Mike Cloppert mchambuzi wa mifumo ya kimtandao aligundua na kubaini mbinu wanazotumia wadukuzi katika kufanya misheni zao ambazo aliziweka katika utaratibu huu.

1. Reconnaissance (Utambuzi, Ufahamu)

2. Weaponization (matumizi ya silaha)

3. Delivery (jinsi ya kufikisha Botnet, virusi kwa victim)

4. Exploitation (uvunaji wa taarifa za muathirika)

5. Installation (jinsi botnet na malwares zinafanya kazi katika kifaa chako)

6. Command and Control

7. Actions (athari za udukuzi katika kifaa chako)

Tuiruke hatua ya kwanza as inaeleweka kirahisi, WEAPONIZATION au matumizi ya Silaha sio lazima mara zote silaha iwe Bunduki na Mabomu. Silaha muhimu inayotumika ni Software za kidukuzi (Malwares, Botnets nk). Kuna kisa kilionekana katika mtandao wa twitter kuhusu “wakala wa simu na mtu mmoja“.

Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

Hizi Malwares zinamfikia victim/target kupitia picha, USB, email, pdf au link iliyobeba Botnets ambazo hudukua taarifa muhimu katika kifaa cha victim (DELIVERY). Shambulizi hili huitwa Phishing. Wadukuzi hupendelea kununua hizi Malware katika masoko yasiyo rasmi mtandaoni (black market). Baada ya Botnet kuingia katika kifaa cha Victim huanza kufanya kazi pasi na idhini au ufahamu wa mtumiaji ambapo huvuna taarifa nakuzituma kwa wadukuzi muda wowote watakaohitaji taarifa hizo automatically(EXPLOITATION AND INSTALLATION). Taarifa hizo zinazoibiwa humuathiri kwa kiasi kikubwa mtumiaji ambaye hana ufahamu wa shambulizi katika kifaa chake, jambo linaloweza kumfanya akapoteza fedha, taarifa muhimu na mali (COMMAND, CONTROL AND ACTIONS). Sasa Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

UFANYEJE SASA ILI USALAMA WA KIMTADAO UWE MUHIMU KWAKO?

Hakikisha kifaa chako kipo salama muda wote. Tumia password bora. Hakikisha password unayotumia inajumuisha mambo yafuatayo: Herufi ndogo, herufi kubwa, namba pamoja na alama za uandishi. Mfano wa Password bora unaweza kuwa (HJas876?2). Somo la Password nimelielezea kwa kirefu kupitia link HIFADHI MBADALA YA NYARAKA. Pia, epuka kushiriki matumizi ya kifaa chako na watu wengine.

Lakini zaidi epuka kutembelea tovuti usizozifahamu ambazo zinaweza kubeba shambulizi. Lakini zaidi Epuka kufungua email kutoka kwa mtu usiyemfahamu au ambaye hujawahi kufanya nae mazungumzo kabisa. Email za wadukuzi zinaweza kuja kama email ya kawaida tu lakini imebeba Malwares ambazo hutajua zimeingia sangapi kwenye kifaa chako Ukihisi kwamba kifaa chako kimeingiliwa na Malwares au Botnets, kwanza Hutakiwi kupanic. Fanya yafuatayo ili kuhakikisha unabaki kuwa salama:

1. Tumia Antivirus Software katika kifaa chako: Hapa sizungumzii zile antivirus za kudownload, Antivirus bora kanunue dukani ikiwa mpya kabisa. Kwa 95% antivirus huzuia mashambulizi yanayokuja katika mfumo wa Spywares and Adwares (Pop ups), virus, Botnets. Ili kuongeza ubora katika utendaji wa Antivirus yako, hakikisha unaiUpdate mara kwa mara kupata latest security protocols katika kifaa chako.

2. Matumizi ya Windows Defender (WD): Kama unatumia computer yenye OS ya windows make sure Windows Defender yako ipo ON in Real Time protection na Automatic Updates zipo ON kama inavyohitajika.

Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

3. Pia hakikisha FIREWALLS zako zipo ON and active: Hizi ni security protocols zinazozuia any software Au App ambayo haitambuliki na Watengenezaji wa Windows OS kama Activators, Softwares from Unrecognized sources n.k Kama Firewalls zako zipo okutaona ukiweka any mentioned Software inaliwa hapo hapo. Kupitia LINUX OS, Iptables firewalls hutumika na zinafanya kazi just like windows

4. Matumizi ya VPN Virtual Private Network (VPN): Ni mwamvuli wa kimtandao unaokuwezesha kutumia huduma za internet bila kufuatiliwa na either Mtoa huduma wako (Network Operator) au mashirika ya kiserikali. VPN inakufanya uwe free kufanya shughuli zako katika usalama zaidi Si watu wote wana uwezo wa kumiliki/kutumia VPN’s, lakini kwa matumizi binafsi na salama zaidi mtandaoni, huna budi kutafuta VPN yako ili kujilinda.

NOTE: Usalama wako na kifaa chako katika huduma za internet mtandaoni unaanza na wewe mwenyewe. Hakikisha kifaa chako ni chako. Umejifunza jambo katika makala haya kuhusu Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako? Tafadhali tujulishe na sambaza kwa mwenzako ili kuhakikisha makala haya yanawafikia watu wengi zaidi.

Kuhusu usalama uwapo mtandaoni nimeshakuwekea makala zingine kupitia links hizi hapa chini:

  1. UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?
  2. YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE KATIKA BIASHARA/KAMPUNI YAKO

UGUNDUZI WA KITEKNOLOJIA KUELEKEA KATIKA MUSTAKABALI WA SEKTA YA UZALISHAJI

Katika zama hizi za mapinduzi ya 4 ya Viwanda duniani, teknolojia inakuja na mapinduzi makubwa katika kuunganisha nyanja mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kidijitali katika mifumo ya uzalishaji duniani (mass production). Kasi ya maendeleo ya kiteknolojia inatajwa kuchochea mabadiliko katika namna watu wanaishi na kufanya kazi katika nyanja zote za uzalishaji, uchumi na viwanda, pengine na zaidi ili kuhakikisha bidhaa zinazalishwa katika ubora unaotakiwa, kujali muda pamoja na matakwa/mahitaji ya watumiaji. kufahamu zaidi kuhusu mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani tayari tumekuwekea makala maalum kupitia link hii hapa https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-mapinduzi-ya-4-ya-viwanda-duniani/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA DUNIANI” kisha tuendelee na mada yetu ya leo.

Katika nyanja tano (5) za kiteknolojia hatua mbalimbali za kiufundi huja na viwango mbalimbali katika kutafuta mustakabali wa uzalishaji. Kwa kuangazia;

Teknolojia ya Roboti (Advanced Robotics): Ni teknolojia kubwa duniani yenye soko la takribani dola za kimarekani 35 bilioni na Teknolojia ya 3D Printing yenye soko la ukubwa wa dola bilioni 5. Teknolojia hizi zenye historia kubwa katika maendeleo ya Viwanda zinatajwa kuwa na mahitaji makubwa ya soko haswa katika nyanja ya jiografia na viwanda.

Teknilojia zingine kama Akili Isiyo ya Asili (Artificial Intelligence) na Enterprise Wearables, Ambazo kwa pamoja zina soko la thamani ya takribani dola 700milioni zipo kwenye hatua nzuri zaidi ya kufanikiwa na kuwafikia watu wengi zaidi. Kwa sasa Amerika ya Kaskazini, Ulaya na sehemu za Asia (China, Japan na Korea Kusini) zinaongoza kwa matumizi ya Teknolojia hizi tajwa huku maeneo mengine ya dunia yakishika mkia.

Changamoto; Nchi za Afrika, haswa zile zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara, zinaweza vipi kuongeza uzalishaji wa bidhaa na huduma zake kwa kutumia Teknolojia na kufaidika na Mapinduzi ya 4 ya Viwanda Duniani?

Ili kufikia kasi inayotakiwa katika kutafuta fursa mbalimbali katika zama za mpinduzi ya 4 ya kidijitali Duniani, Kampuni na wadau wanapaswa kubadili mtindo wa kufanya Biashara zao kutoka Kushawishi Wateja Wanunue Bidhaa/Huduma (Push into the Market) kuelekea Kubuni Bidhaa maalum kwa matakwa ya Mteja mmoja mmoja katika muktadha wa Kiteknolojia. (Pull from the Customer).

Kiasili dunia imeumbwa katika mifumo ya kufanya kazi, ikijumuisha vitendea kazi (assets) na maarifa/ujuzi yenye kuleta ufanisi. Hata hivyo, Maarifa ya Kiinjinia ya Hali ya Juu, mipango na mabadiliko ya kiteknolojia huleta gharama za juu katika utekelezwaji wa miradi ya kufikia mapinduzi ya kidijitali haswa barani Africa. Je, suluhu ya changamoto hii ni nini?

Ili kufaidika na ukuaji wa kasi katika mabadiliko chanya ya kidijitali kuelekea mapinduzi ya 4, Kampuni zilizo katika nyanja Uzalishaji mali zinahitaji malengo ya muda mrefu (long-term vision), kujenga na kuimarisha jumuiya baina ya nchi/kampuni zenye nguvu zaidi ya kidijitali, kuongeza ujuzi na maarifa katika ubunifu wa bidhaa/huduma, kuongeza vitendea kazi (computer, smartphones, huduma za internet, masomo ya sayansi ya computer), kuongeza ujuzi na mbinu za kuongeza/kutanua masoko, viwanda na mahitaji ya wateja.

Kama unahitaji kuendelea kufanikiwa na kuwa na uwezo wa kushindana katika zama hizi za mapinduzi ya kidijitali, huna budi kujiweka tayari kukabiliana na kasi kubwa ya mabadiliko, kuipanga biashara yako katika mtindo wa ‘Kuvuta’ Wateja zaidi kuliko ‘Kushawishi’. Na zaidi huna budi kukuza Biashara yako kwa namna ya kufikisha Bidhaa/Huduma zako kwa wateja wengi na maeneo tofauti tofauti kila siku bila kuchoka. Hili ni somo muhimu sana katika kubuni mbinu mbadaka ya kuendesha Biashara yako kisasa zaidi.

Uwekezaji unaofanywa katika sekta ya uzalishaji mali unaakisi malengo makubwa ambayo yanalenga katika kufikisha bidhaa na huduma kwa soko la watu duniani kote. Zaidi kuhusu uwekezaji unaweza kusoma makala maalum kupitia link hii hapa https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Umejifunza kitu gani kipya leo. Tafadhali tuambie.