Tag: faida za mitandao

Pata huduma za Website, SEO, Social Media Marketing na nyinginezo nyingi kutoka Rednet Technologies Branding vs Marketing. Kipi ni kipi? ukweli kuhusu 'Propaganda' Jinsi ya kutengeneza Attention Mtandaoni.

Jinsi ya Kutengeneza Attention Mtandaoni

Hivi unajua kwamba aliyeshinda vita vya 2 vya Dunia ni Urusi, ndiye aliyepigana na Hitler kwa ground. LAKINI, Leo hii kila mtu anaongelea Bomu la Nyuklia la Marekani lililodondoshwa Hiroshima na Nagasaki. Unajua kwanini? Kwa sababu watu wanapenda ATTENTION duniani na leo hapa utafahamu kiundani kabisa jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni ili uweze kunasa wateja zaidi.

Marekani ni mtaalamu haswa kwenye hilo la kutengeneza attention na kusambaza propaganda zenye manufaa ya nchi yake. Jamaa wamefanikiwa kuujaza Ulimwengu “ukweli wao” kwamba lile Bomu la Nyuklia ndo limeipa ushindi taifa hilo na kwamba kwanzia hapo wao ndo wababe duniani na hakuna mwingine. Ila nyuma ya pazia Urusi ndiye anayemiliki Nyuklia nyingi zaidi.

Kujitangazia Ushindi tu, tayari alishaanza kuteka ATTENTION duniani na mataifa mengi yalianza kuvutika katika Silaha, Siasa, Utamaduni na Biashara zingine za Kimarekani. Leo hii Marekani ndo nchi inayosifika kuuza silaha zaidi duniani, Makampuni makubwa karibu yote yapo USA, Microsoft, Google, Meta, Yahoo, Space X nakadhalika.

Marekani ndo nchi inayotambulika kwa mifumo bora ya Kidemokrasia duniani, na mambo kedekede tayari unayajua kuhusu hao jamaa. Unadhani Marekani alipata wapi sifa zote hizo? Kwamba Urusi hana huo ubavu wa kuuza silaha au teknolojia za kisasa? Jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni is the damn strategy they rely on.

Kwenye Biashara Attention inatengenezwa vipi?

Kwenye biashara Mtandaoni hali ipo hivyo hivyo. Ushindani ni mkali mno kila siku. Ni vita. Mtandao wa Internet Live Stat unaonyesha kuwepo na websites zaidi ya Bilioni 1.9 mpaka sasa duniani. Hebu niambie unachomokaje katikati ya vurugu lote hilo kama hujajua jinsi ya kutengeneza ATTENTION? Leo hii wewe upo hapa kwenye tovuti yetu kwa sababu umeona kuna uwezekano ukaweza kuimarisha biashara yako mtandaoni kwa kutengeneza attention fulani, si ndio?

Utaniuliza; “Sasa Faustine, nawezaje kutengeneza hio ATTENTION ili niweze kusurvive huko mtandaoni?” Zipo njia nyingi, za halali na zile zisizo halali. Hapa tutaongelea zile za halali tu. Habari za kupost utupu, vichupi na makalio hapa hazipo.

Kuijuia Google leo ndo mchongo. Binafsi ningepata nafasi ya kurudi nyuma na kumshauri Faustine wa miaka 15 enzi zile, ningemshauri atie nguvu sana kwenye kuijua jinsi Google inavyofanya kazi na namna anaweza kuitumia kukuza biashara na kunasa wateja zaidi.

Leo hii unaweza kutengeneza ATTENTION ya Biashara yako kule GOOGLE kwa kuhakikisha mtu akitafuta chochote kinachohusiana na bidhaa/huduma unazozitoa kwenye biashara yako basi anakipata mara moja na anakipata kwako chap. Hii inafanyika kwa uzuri kupitia Huduma za SEO (Search Engine Optimization).

Hivi si unajua, kwa siku 1 tu huwa kunafanyika matafuto zaidi ya bilioni 3.5 kule google. Sasa kwanini bidhaa/huduma zako tukizitafuta google kule hatukupati? Kama jibu la hilo swali linakusumbua, wala usiwe na wasiwasi tena, sekunde chache zijazo utakwenda kujua cha kufanya.

Kama unatamani kutengeneza ATTENTION kule Google mpaka ifike mahali mtu akisearch kuhusu bidhaa/huduma zako akupate haraka, basi chukua SIRI hizi hapa. Leo hapa utaziona siri (4) tu;

1. Tengeneza website yako na hakikisha inafanya kazi vizuri na ina load faster. Kwanini website? Kwa sababu ni kupitia website unaweza kutengeneza maudhui mengi ndani ya chanzo kimoja, ukafanya uchambuzi kwa kina na kuelezea kwa mapana kuhusu Faida za bidhaa/huduma zako, Mbinu, Jinsi ya kutumia na taarifa zingine. Hili pia unaweza kulifanya kupitia chaneli yako ya YouTube.

2. Andika maudhui ya kutosha kuhusu Faida za bidhaa/Huduma zako, Jinsi ya kuzitumia, Jinsi ya kupambana na Changamoto, Mbinu za kutumia bidhaa/huduma hizo kwa usahihi, Madhara ya Kutotumia bidhaa/huduma zako n.k Umeona hayo maneno hayo yaliyotumika hapo? Hayo yanaitwa Keywords.

3. Hakikisha unatumia keywords nyingi zinazohusu bidhaa/huduma zako ikiwemo JINA LA BIDHAA/HUDUMA hio. Kwenye keywords hapo ndipo Google hukusanya taarifa na kuzihifadhi kwenye database yake, tayari kwa watu kupata majibu pale watakapotafuta kuhusu bidhaa/huduma hio. Ukiweza kutumia Google kama jukwaa la biashara utafaidi sana biashara yako inapokuwa mtandaoni.

4. Ambatanisha Namba yako inayopatikana katika simu za Kawaida na WhatsApp katika makala unazozichapisha kwenye website yako na mitandao yako ya Kijamii. Hio namba yako ya simu ni muhimu sana iwe hewani muda wote. Hakikisha muda wote ukitafutwa unapatikana. Hapa ndo utajua sasa kwanini Mteja achague kufanya kazi na wewe na sio mtu mwingine.

Ukifanya hivyo, utamtengenezea mteja wako mazingira ya kukupata moja kwa moja pale atakapofikwa na uhitaji wa huduma/bidhaa zako atakazoziona huko Mtandaoni. WhatsApp kupitia Status zako unaweza kuchapisha tips, ushauri, faida nk za bidhaa/huduma zako kila siku.

Sasa, tuishie hapo kwa leo, au unasemaje ndugu yangu?

Anyway, ngoja nisikuache bure, muendelezo wa SIR hizo tayari nimeuweka kwenye eBOOK yako MPYA na BORA ya SEO ambayo nimekuandalia. eBook hio inaitwa TEKNOLOJIA YA SEO; JINSI INAIFANYA BIASHARA YAKO KUWA NA SUMAKU MTANDAONI. Katika Kitabu hiko nimekuwekea SIRI 15 tayari kabisa kukufunulia wewe jinsi SEO inavyofanya kazi na namna unaweza kuitumia kukuletea manufaa zaidi kila siku. Hi ndio kitu unakihitaji sasa.

eBook hii itakusaidia kujua mambo yote muhimu kuhusu SEO, ni nini? inafanya kazi vipi? Faida zake ni zipi? Mambo yapi ya kuzingatia ili uifaidi? Kwanini hupati wateja mtandaoni? Yote hayo na mengine mengi yameelezwa kwa mapana kabisa kwenye eBook hio.

Kama nilivyokutaarifu, kuanzia ukurasa wa 27 wa eBook nimekueleza SIRI 15 ambazo zitakusaidia katika kutengeneza ATTENTION ya biashara yako mtandaoni kupitia SEO. SIRI 15!! Hizi siri wanaojiita wataalam wa SEO unaowafahamu hawawezi kukwambia kwa kuhofia kupoteza wateja ukiwemo wewe, ila mimi nimekwambia.

Utajiuliza, Kwanini nimekwambia? Kwa sababu mteja anayo haki ya kufahamu exactly kila kinachofanyika katika mradi wake. Mfano unapojenga nyumba ukikaa karibu na fundi wako utataka kujua bei ya misumari, aina za misumari, aina za milango, mbao, rangi ipi ipakwe wapi na kwanini, aina za kokoto, mchanga wa plasta ni upi na vitu kama hivyo.

Kadhalika katika SEO, ni muhimu ukafahamu kinachofanyika humo ndani, ili uweze kushiriki kufanya mwenyewe na kupata ujuzi wa ziada. Hii ndio sababu kitabu hiki kipo tayari kwa ajili yako leo.

Sasa ukitaka kuipata hii eBook njia ni hii hapa. Save namba yangu ya WhatsApp kwa kugusa namba hii hapa, 0765834754 Kisha nitumie text yenye jina lako ili niweze kukutumia eBook hio kwa WhatsApp mara moja. Kwa sasa nitaitoa eBook EXCLUSIVELY kwa watu 20 tu.

Hata hivyo eBook yetu hii sio kila mtu ataipata. Wataoweza kuipata eBook hio ni wale tu;

1. Waliopo kwenye contact list yetu ya WhatsApp. Kuingia kwenye list hio save namba yetu hii hapa 0765834754

2. eBook itatoka rasmi Usiku wa kuamkia PASAKA kwa gharama ya shilingi 50,000/-. Lakini leo hii unapouona ujumbe huu, eBook naitoa EXCLUSIVELY kwa shilingi 15,000/- tu.

Hii OFA ni kwa watu 20 tu watakaokuwa wakwanza kulipia. Baada ya hapo OFA itafungwa. Hivyo, ndugu changamka.

LIPA Sasa hivi sh 15,000/- kupitia LIPA NAMBA Yetu ya M-PESA hii hapa 5432715 au scan QR Code unayoiona hapa. Ukishafanya malipo njoo WhatsApp na screenshot ya muamala na hapo hapo utapata eBook yako uanze kuvuta wateja kwa kutumia SIRI za Ajabu za SEO katika Mtandao wa Google.

jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni

Kumbuka Ofa ni EXCLUSIVELY kwa watu 20 tu wa kwanza kulipia. Baada ya hapo eBook itarudi bei yake halisi ya sh 50,000/-.

Kuna mtu aliwahi kuliuliza, “Sasa bro, kwanini unilipishe kufanya SEO wakati kutumia Google ni BURE kabisa?” Ungekuwa wewe ungemjibuje apo?

Sikia nikwambie kitu, Ukiona unapewa mchongo wa bure basi jua wewe ndo bidhaa hapo. Ndo ukweli huo.

Kutumia Google ni BURE. Kutumia Insta, Facebook, WhatsApp na mitandao mingine ya kijamii pia ni BURE kabisa. Kwanini? Kwa sababu kwenye BURE ndo kuna utajiri umejificha hapo.

Umeelewa hapo mchezo unavyochezwa. So nakupa SIRI hii hapa; Toa maudhui yatakayotoa majibu ya changamoto BURE yawafikie watu wengi, wachuje, wachache wawe wateja wa bidhaa/huduma zako. Njoo WhatsApp sasa ufahamu zaidi kuhusu SEO na Tech kwa namba hii 0765834754.

Unatamani ujumbe huu umfikie rafiki yako wa karibu? Umejifunza nini leo katika jinsi ya kutengeneza attention mtandaoni ili uweze kunasa wateja zaidi. Unaweza kushare makala hii kwa rafiki, ndugu, boss au yeyote unayehisi anahitaji kusikia habari hii. Ni BUREE kabisa, hivyo, sambaza, uliza na comment ili ufahamu zaidi.

Cheers.

Kwanini mteja akuchague wewe

KWANINI MTEJA AKUCHAGUE WEWE?

Maisha ya biashara za mtandaoni ni marahisi sana kama ukizingatia tabia za wateja mtandaoni, na ni magumu sana ukipuuzia/usipozijua. Kwanza, hakikisha ukitafutwa unapatikana. Swala la kujiuliza ni, Kwanini Mteja akuchague wewe aache watoa huduma na wafanya biashara wengine?

Zipo sababu nyingi sana mtu akiwa mtandaoni anaziangalia ili ajiridhishe kabla hajawa mteja wako. Leo hapa tutaziona 6 tu. Zingine nitaziweka kwa status yangu ya WhatsApp. Ukihitaji kujifunza zaidi gusa hapa 0765834754 nitumie text yenye jina lako ili nikusave chap.

Mwaka 2022, niliweka story hapa kuhusu jamaa yangu fulani ambaye aliona kazi zetu mtandaoni, akashawishika kuchukua namba kisha akanitafuta tufanye kazi yake, na mpaka leo tumejenga uhusiano bora sana. Ile stori ni hii hapa kama ilikupita Faida za Kutumia Google kama Jukwaa la Biashara yako.

Baada ya kupublish stori hio, nilipokea requests nyingi sana kutoka sehemu mbali mbali yakiwemo mashirika ya kiserikali, binafsi ya yale ya kimataifa.

Leo hii sasa nataka nikwambie Kwanini Mteja achague kufanya kazi na wewe na awaache wengine? Fuatilia dondoo hizi hadi mwisho:

1. UBORA WA KAZI/BIDHAA/HUDUMA: Sikufichi, watu wanapenda vitu vizuri bwana. Hakuna anayependa bidhaa/huduma mbovu. Hata utumie mbinu gani za kunasa wateja mtandaoni, kama bidhaa/huduma zako hazina ubora unaotakiwa, jua apo unacheza tu. Utapata tabu yani.

Kama bidhaa/huduma zako zinatolewa na wafanyabiashara wengine, hio ni fursa nzuri kwako. Fanya uchunguzi, angalia wapi unaweza fanya improvements, ongeza ubunifu kidogo upande wako kisha peleka mzigo sokoni. Hakunaga miujiza kwenye hili. Lazima utie juhudi muda wote.

2. UBORA WA HUDUMA UNAYOTOA; Kama kuna kitu kinafanya wafanyabiashara wengi hawakui kibiashara licha ya kuwa na skills au bidhaa/huduma bora, basi ni hili la kushindwa kutoa huduma zinazomridhisha mteja. Angalia, watu wanatofautiana sana kwenye namna ya kutoa na kupokea maoni na changamoto. Wewe sasa kama mtoa huduma lazima ujue jinsi ya kujishusha kwenye kupokea maoni na changamoto na vile vile kwenye kutoa huduma zenye viwango vya hali ya juu. Huduma bora inaenda sambamba na kuijua saikolojia ya mteja wako. Cheza napo vizuri hapo.

Kuna makala hii kuhusu Umuhimu wa Takwimu kwenye utoaji wa huduma bora katika biashara yako. Ifuatilie hapa uelewe kwanini unapaswa kutoa huduma bora muda wote kwa wateja wako.

3. PATIKANA SEHEMU MBALIMBALI MTANDAONI; Katika mitandao ya kijamii, kila mahali watu hujihusanisha kitofauti. Mfano utagundua watu wa facebook na twita ni tofauti kabisa. Lakini sikufichi, wengi ni wale wale tu. So unapaswa kupatikana kwenye majukwaa yote makubwa kama Facebook, Twita, Linkedin, Instagram n.k Patikana huko kote kwasababu kila mtu ana mtandao wake ambao anautumia zaidi na wote hao unawahitaji leo. Na unachokitaka wewe ni kuifikisha biashara yako kwa kila mtu anayetumia smartphone yani. Si ndio? Fanyia kazi hilo.

nguvu ya mitandao ya kijamii unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?Kwanini mteja akuchague wewe?

4. TUMIA S.E.O; Hapa sitasema mengi kwasabau kule WhatsApp huwa natupia sana updates, tips, info na najibu maswali mengi sana kuhusu SEO. Pia kuna eBook maalum ambayo inaelezea siri zote unazohitaji kuzifahamu ili SEO iweze kuwa na manufaa kwako siku zote. Kuipata eBook hio pia hakikisha umesave namba yetu ya WhatsApp, kisha tuma ujumbe wenye jina lako na utapatiwa maelekezo.

In short hii SEO inakurajisishia biashara yako kupatikana haraka pale mtu akiwa anasearch taarifa kupitia Google. Yes, unaihitaji google zaidi sawa sawa na Google inavyohitaji taarifa za biashara yako kwa manufaa ya wateja wako duniani kote.

Mteja anayekutafuta ni mzuri sana kuliko yule unayemtafuta, si ndio? Sasa kwanini usijiweke kwenye mazingira ambayo yatamrahisishia mtu akiwa anatafuta bidhaa/huduma kule Google na kumpa majibu Kwanini mteja akuchague wewe kuliko wengine? Ukiitumia SEO vizuri itakujibu vema sana kwenye hili.

Takwimu za Internet Live Stats zinaonyesha kuwa kwa siku 1 tu kule Google huwa kunafanyika matafuto (searches) zaidi ya bilioni 3.5. Sasa linganisha na matangazo (Paid Ads) unayoyaonaga mtandaoni (Youtube, Insta na fb) na kuyaskip. Wapi utatoboa, kwenye Searches (SEO) au Ads?

5. TOA OFA KADHAA; Mwanaume huwezi kuoa ile siku ya kwanza unapokutana na Mwanamke, hali kadhalika, ni ngumu sana mtu akawa mteja wako siku ya kwanza tu amekutana na wewe huku mtandaoni. Ni muhimu sana kumpitisha mteja kwenye hatua kadhaa ili kusudi aweze kukujua zaidi akupende, akuamini na mwishowe sasa ndo aweze kuwa mteja wako wa kudumu.

Hii ni kwakuwa Biashara za Mtandaoni hutegemea sana kujenga Uhusiano Bora na watu usiowafahamu. Ndio maana unaona kuna wasanii wana mashabiki zao wanawapenda mpaka wakiwaona wanazimia japo hawafahamiani.

Hii ni kwasababu wasanii hao waliwapa values/ofa/zawadi nyingi ambazo ziliwafanya mashabiki zao wawapende sana hata kama hawajuani kiundani. Kadhalika, ukiwa unafanya biashara mtandaoni lazima ujifunze kutoa tips, info, updates, ujibu maswali na ujichanganye na wateja wako.

6. DHIHIRISHA KWAMBA BIDHAA/HUDUMA UNAYOTOA NI GHALI KULIKO GHARAMA ANAYOLIPA: Tunaishi kwenye zama ambazo kila mtu anauwezo wa kufanya biashara na akapanga bei itakayompa unafuu. Mfano, kwenye kutengeneza website ukizunguka huku mtandaoni utaona kila mtu ana bei yake.

mageuzi ya Intaneti (iot) katika biashara na maisha. Jihudumie leo kutoka Rednet Technologies.Kwanini mteja akuchague wewe?

Biashara zimekuwa huru sana. Kila mtu anao uwezo wa kufanya biashara mtandaoni. Sasa unapaswa kujiweka kwenye nafasi ambayo mteja atakuchagua always akikutana nawe mtandaoni. Kwanini mteja akuchague wewe? Tips hizo hapo. Tips nyingine zipo WhatsApp hapa kwa kugusa namba hii 0765834754

Umejifunza nini kwenye makala hii ya leo kuhusu Kwanini mteja akuchague wewe? Kuna mahali hujaelewa? Niulize swali.. Share, Like na ucomment hapo chini maoni na maswali yako.

Cheers.

Kwanini hupati wateja mtandaoni?

KWANINI HUPATI WATEJA MTANDAONI?

Kila mtu anapenda maisha mazuri, kufanikiwa kibiashara, kuwa na amani na uhuru wa kufanya kile kinachokupa furaha muda wowote. Sasa uko tayari kuingia gharama ili kuyapata matamanio yako? Umeshajiuliza Kwanini Hupati Wateja Mtandaoni licha ya Juhudi unazoweka?

Mwaka 2010 wakati nafungua account ya Facebook nilikua nafurahi sana kukutana na rafiki zangu tuliopotezana miaka mingi baada ya kumaliza Primary School na sekondari. Ilikua safi sana kuona picha za washkaji wakiwa na maisha yao baada ya shule.

Baadae tukaanza kupata marafiki wengine katika mtandao pendwa wa facebook. Nyakati hizo Mtandao wa Twita ulionekana kama mtandao wa Wanasiasa, Instagram ya Wasanii na Masuperstar. Ila Facebook kule wote tulionana kuwa ni level moja. So kule ndo tuliona kuna lile vibe la wote.

kwanini hupati wateja mtandaoni?nguvu ya mitandao ya kijamii unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Lakini miaka ilivyozidi kwenda, Matumizi ya Mitandao ya Kijamii yalikua yakibadilika mdogo mdogo, hasa baada ya kushuhudia Wasanii na watu waliokuwa na Followers wengi mitandaoni waliposhindwa kuimarisha Uchumi wao kupitia Nguvu ya Mitandao. Hapa kitu kipya kikatambulishwa.

Ilifika mahali sasa ule utaratibu wa kuwa na urafiki na wale tu uliowahi kusoma nao sasa ulipitwa na wakati na badala yake, Rafiki/Followers/Follows wa mtandaoni wakawa ni wale ambao tunashare nao “Interests” Hapo ndipo mbinu za kufanya biashara mitandaoni zilipoanza kushamiri.

Tayari nimeshakuandalia makala maalum itakayokupa mbinu muhimu za kunasa wateja mtandaoni. Kama unataka kuzifahamu mbinu hizo ili uzitumie kwenye biashara yako basi fuatana na makala hii hapa Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

MAMBO SABA (7) YANAYOKUKOSESHA WATEJA MTANDAONI

Tumeshaona jinsi Mitandao imebadilika kutoka ilipoanza, sasa kuna mambo unayoyafanya kwa kujua au kutokujua yanayokukosesha wateja. Jambo la 5 litakushtusha sana. Hebu tuyaone hapa;

1. Kutokuwa na Bidhaa/Huduma inayokutambulisha;

Hapa unatakiwa kuwa makini na kuelekeza focus yako kwenye bidhaa/huduma fulani specific. Inaweza isiwe bidhaa/huduma moja, lakini hakikisha unakuwa na ile bidhaa/huduma inayokutambulisha. Mfano: Unauza fenicha, shikilia hapo hapo.

kwanini hupati wateja mtandaoni

Zile zama leo unapost fenicha, kesho unapost computers keshokutwa unapost picha uko unasafiri, mara unapost unakula chakula., hivyo ni vitu ambavyo vinakupunguzia mvuto mtandaoni. Sisemi usipost kabisa, hasha, katika post 10, 7 ziwe ni kuhusu fenicha, 3 maisha binafsi.

2. Kushindwa kuingia kwenye Orodha ya Wanaofanya biashara kama yako mtandaoni;

Kuna ile dhana ya kuogopa ushindani au ile kuwekeana mtimanyongo na washindani wako. My friend, huku mtandaoni make sure unajenga uhusiano na kila unayekutana naye. Itakusaidia sana kuendelea kudumu sokoni.

Kuingia kwenye orodha(list) ya wafanyabishara huna budi kuwa support wafanyabiashara wenzako mtandaoni. Ndio, Wasukuma wana msemo wao wanakwambia “Scratch my back, I’ll scratch yours.”

3. Kutokua na muendelezo wa Maudhui kutasema kwanini hupati wateja mtandaoni;

Je wajua kwamba kwa siku huwa kunakuwa na posts zaidi ya milioni 50 katika mitandao mbalimbali duniani. Sasa ndugu unapost mara 1 kwa wiki unategemea nani ataiona hio biashara yako? Hakikisha unapost mara nyingi kadiri iwezekanavyo.

Njia ya Kompyuta katika kuhifadhi data utajuaje pale biashara yako inapojiendesha kwa hasara changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika

4. Kushindwa Kuwasiliana Vema;

Kupost bidhaa/huduma zako mtandaoni ni jambo moja, lakini uwezo wa kuwasiliana ndio muhimu sana. Shuleni tulisoma ile Communication Skills, sasa mtaani unatakiwa uwe na uwezo wa kuwasiliana na kujua wapi, sangapi useme nini. Ni maarifa hayo.

Mtaalam wa mitandao bwana @GillsaInt ana mbinu yake anakwambia katika maudhui yako unayopost mtandaoni, hakikisha 80% ni yanahusu thamani (value) za bidhaa/ huduma zako kama Faida, Jinsi ya Kutumia, Changamoto nk. Na 20% zinazobaki ndo upost sasa Matangazo ya kuuza hio biashara.

5. Kutokuwa na Miundombinu ya Kurahisisha biashara Mtandaoni;

Umeshaona wale wanakwambia No Facebook Acc, No Insta Acc, No twitter etc. Skia, kama unataka kufanya biashara ukafanikiwa mtandaoni USIFUATISHE hizo akili zao. Hakikisha una miundobinu humu mtandaoni.

Mitandao ya kijamii ndipo ilipo NGUVU halisi ya biashara ya mtandaoni. Jifunze namna unavyoweza kuitumia kwa faida ya biashara yako. Kama unataka kuifahamu NGUVU hio ya mitandao, basi fuatana na makala hio hapa kufahamu zaidi.

Lengo la kufanya biashara mtandaoni ni kuhakikisha unakuwa na wateja wengi kadiri iwezekanavyo, si ndio? Kama ni hivyo, fanya research, kisha tambua wateja wako ni kina nani na wako wapi. Fungua website yako, accounts za Insta, Facebook, Linkedin, Twitter n.k Kuwa available.

6. Kukosa Ushawishi na Ujuzi wa Kuuzia wateja Mtandaoni;

Sasa hapa naongelea uwezo wa kumshawishi mtu akapenda bidhaa/huduma zako kabla hajawa mteja wako. Kwenye hili @iamKaga pale twita anakupa funzo gani? Cha kwanza hakikisha watu wanakujua, kisha Wakupende au wapende maudhui yako, hapo ndipo watakujia.

Huo ushawishi hauji tu by default wala haujengwi ndani ya siku moja. Ushawishi ni tabia ya kuhoji na kutoa ufumbuzi juu ya changamoto zinazowakabili watu katika namna bora ya uwasilishaji. Hapa ndipo wanasiasa wanatupiga coz anaijua siri iliyopo kwnye ushawishi.

7. Kutokuwa na Njaa ya Mafanikio;

Tunarudi kulee mwanzo, unapost mara 1 kwa wiki, au mara 2 kwa mwezi halafu unasingizia huna muda wa kuandaa maudhui. Bro, ni vile tu huna njaa ya kufanikiwa. Njaa ya mafanikio ikikushika vizuri huo muda LAZIMA uupate na utautumia vizuri tu.

Kuna nyakati unabanwa na shughuli zako nyingine to the point unashindwa kuendesha biashara yako mtandaoni. Kuna nyakati nyingine unakata tamaa kwa sababu huna followers au huna idea uanzaje kuandaa maudhui ili ufikie yale matamanio yako. Ukifikia hapo wala usiwe na shaka..

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

Hata hivyo, katika biashara sio lazima kila jambo ufanye wewe mwenyewe. Nyakati hizi za mapinduzi ya teknolojia kila siku, ni muhimu kugawa majukumu kwa wataalam wa kuaminika ili kuhakikisha lengo na mipango yako inazidi kwenda kama utakavyo.

Hio ndio sababu sisi Rednet Tech. LEO hii tunakupa nafasi ya kuikuza biashara yako mtandaoni kwa;

1. Kukutengenezea Website bora.

2. Kukufanyia huduma ya SEO. Inafanyeje kazi hii? Gusa hapa kuifahamu zaidi.

3. Kukushauri aina ya maudhui ya kuyatumia kwenye kurasa zako za mitandao. Gusa hapa tuchati pale WhatsApp na upate huduma unayohitaji.

So, mambo haya 7 tuliyoyaona leo kwa uchache wake ndio yanakwambia kwanini hupati wateja mtandaoni. Umeshajua cha kufanya sasa? Hebu niambie wewe ni lipi umegundua leo kuwa ndio linakukosesha wateja? Mtandaoni hamna miujiza. Ni kuwa na maarifa na kuhakikisha unajifunza kila siku. Umependa makala hii? Share..

simu za michongo Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

FAIDA ZA KUTUMIA GOOGLE KAMA JUKWAA LA BIASHARA YAKO

Je, unaamini kwamba matumizi sahihi ya huduma za internet na mitandao ya kijamii yana uwezo wa kukurahisishia huduma/bidhaa zako zikapatikana kirahisi na wateja wako wakiwa popote duniani? Leo nataka nikupe stori kuhusu Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Tizama hapa, Siku moja asubuhi kabisa ya mwezi April mwaka huu 2022 nikiwa natoka home naelekea ofisini nikapigiwa simu, kutizama ni namba ngeni, nikatafuta utulivu kisha nikapokea;

Mimi: Hello, Habari za asubuhi!

Jamaa: Salama Faustine, I hope uko poa, Bwana mimi ni fulani (jina kapuni) nimekupigia kwa sababu nahitaji website na ningependa ifanywe na kijana mzawa. Nafanya kazi katika shirika (jina kapuni) ambalo ni la kimataifa. Nilikua napitia google pale nikaona kampuni yenu ya Rednet Technologies na nikaona pia kumbe mnajishughulisha na haya mambo. Itawezekana si ndio?

Mimi: Bila shaka hilo linawezekana kabisa, unahitaji lini hii kazi yako iwe imekwisha?

Jamaa: Well, ndani ya wiki 3 ningependa iwe imekwisha, sasa nitampatia namba yako mwenzangu yupo pale ofisini kwetu, yeye sasa atakupa maelezo ya kina. Lakini naomba kujua bei itakuwaje hapo (huku anacheka kwa ufupi)

Mimi: Gharama nitataja nikishajua requirements kaka, wala usiwe na shaka.

Baada ya kuwasiliana na huyo mwenzake akanirudia…

Jamaa: Faustine, naona mmeshaelewana, Sasa the reason tumekuja kwako ni kwasababu kuna mtu tulimpaga kazi ya kutengeneza hii website yetu, lakini hajawahi kutupa ushirikiano, kazi hajamaliza, changes hataki kufanya na tukimpigia simu harespond ndani ya muda, yani ana kiburi sana yule jamaa, kusema ukweli TUMEMCHOKA.

Mimi: (Kiukweli nilijiskia vibaya sana, ndugu zangu ule msemo wa “Mteja ni Mfalme” una maana kubwa sana hapa. Nikamwambia) Kaka, pole sana, utakavyokuwa unafanya kazi kwetu nakuahidi hio kadhia hutakutana nayo.

Jamaa: Kweli? Ok, turudi kwenye bei sasa, utatuchaji kiasi gani?

Mimi: Kwa nature ya Organization yenu hapo mpaka kazi inakamilika itacost 850,000/- tu.

Jamaa: Faustine, mbona bei ipo juu sana, tutaweza kufanya kazi kweli?

Mimi: Kaka, bei iko fair sana hio ukizingatia tutawatengenezea pia business emails BURE na kuwafanyia maintenance BURE kwa mwaka mzima. Anytime hapo mkitaka kufanya changes, tutazifanya BURE kabisa. Hapo unasemaje?

Jamaa: Hapo sio mbaya, walau naona dalili hautakuwa kama jamaa wa mwanzo. Ila bei bado hujashusha..

Mimi: Kaka, lipia 400k leo, baadae utalipa 250k, then finally tutakapomaliza kazi, utalipia 200k ambayo itakuwa imebaki. Hapo je?

Jamaa: Ok, Nataka na hio website pia iwe inapatikana mtu akisearch Google, ili wateja watupate kama sisi tulivyokupata wewe.

Mimi: Ahaa, hio sasa ni huduma nyingine, inaitwa Search Engine Optimization (SEO). Ndo inaiwezesha website kupatikana google.

Jamaa: Na hio utatuchaji au bei yake ndio inakuja na ya website direct?

Mimi: Hio gharama yake ni tofauti kaka.

Jamaa: Ambayo ni ngapi? Usinilalie bwana ndugu yangu.

Mimi: Hio kwa sababu ni kazi ya muendelezo, utakuwa unalipia kila mwezi, ambapo gharama yake ni 100,000/- tu.

Jamaa: sema Faustine mna bei nyie. Ehe niambie, kwenye hio laki 1 mtakuwa mnafanya nini na nini?

Mimi: Hapo tutakuwa tunakuandikia makala (blog posts) mbili kwa mwezi ambazo zitahusu shughuli mnazofanya, tutaweka picha, pamoja na kuzioptimize ili iwe rahisi kupatikana google mtu akiwa anatafuta taarifa zinazowahusu.

Jamaa: Faustine, hapo umeniweza. Basi wacha tuandae contract, halafu next week tutakuita ili tusign, kazi ianze mara moja. Ila usiniangushe bwana.

Mimi: Kaka wala usiwaze, tufanye kazi.

Basi Bwana baada ya simu hio ndio uhusiano ukajengwa na kazi ikaanza kama hivyo.

Na baada ya kazi hio kuisha, jamaa yetu aliweza kutuunganisha kwa watu wengine watano (5) ambao walitamani kupata huduma kama ambayo aliipata kutoka kwetu. Na hatimaye wamekuwa wateja wetu wa kudumu. Unadhani hao walivutiwa na nini? Fuatilia makala hii hapa kufahamu siri za utoaji huduma bora kwa wateja.

Unachoweza kujifunza ili uweze kuzipata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Katika mazingira ya kazi, hasa huku mtandaoni ambapo mara nyingi tunakutana na watu tusiowafahamu (strangers) ni muhimu sana kuzingatia haya yafuatayo;

1. KAULI NJEMA

2. UAMINIFU

3. KUMJALI MTEJA na MAUMIVU YAKE (Mara kwa mara muulize kama anaridhika na huduma anazopata kutoka kwako na nini unaweza kufanya ili kazi yake ifanyike kwa ubora anaotarajia).

Kauli Njema zitakufunulia fursa nyingi na kukuletea wateja wengi sana huku mtandaoni, acha tabia ya kutukana, kudhalilisha au/na kudharau watu. Kumbuka teknolojia haisahau.

Uaminifu utajenga uhusiano mzuri na wa kudumu na mteja wako.

Kumjali mteja kutafanya azidi kukupa kazi nyingi zaidi mbeleni, na hata kukuunganisha kwa watu wake wengine anaowafahamu.

Siri ya kufanya kazi vizuri na mteja ipo kwenye hayo mambo matatu. Ukiyazingatia, hakika huwezi kufeli. Zaidi kama unahisi bado hujajua namna unaweza kushawishi mteja kwenye biashara yako fuatana na makala hii hapa tumekuandalia.

HABARI NJEMA KUELEKEA MSIMU WA SIKUKUU

Sasa kuelekea mwisho wa Mwaka tunakupa ZAWADI ya kuifikisha biashara yako mtandaoni na kukusanya wateja kutoka kila pembe ya nchi. Fungua website leo kwa 500,000/- tu (badala ya 850,000/-) upate na huduma ya SEO BURE (badala ya 100,000/- kwa mwezi) maintenance BURE mwaka mzima pamoja na Ushauri BURE kabisa. Hata hivyo, ZAWADI hii haitamfikia kila mtu. Zawadi hii ni kwa watu 10 tu wa mwanzo, na itadumu mpaka tar 10 December. Baada ya hapo tunakwenda likizo ya Christmas.. So kama unahitaji ZAWADI hii WAHI nafasi mapema ili pia uzipate Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

OFA ya Msimu wa Sikukuu 2022Sherehe za Christmas na Mwaka Mpya Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Baada ya OFA hii ukihitaji website ni 850,000/-, huduma ya SEO ni 100,000/- kwa mwezi na pia tutafungua group la Whatsapp kwa yeyote atakayehitaji ushauri au atayehitaji kuuliza jambo lolote kuhusu Website, SEO, Social Media Marketing, Digital Marketing na Tech kwa ujumla wake. Kuingia kwenye group hilo itakugharimu 5,000/- tu kwa mwezi.

So ukiliona Tangazo hili, mtaarifu na mwenzako ambaye unahisi atahitaji kunufaika na ZAWADI hii.

Wewe kama unafanya biashara, basi kama unataka kufanya vizuri sokoni, hakikisha unajenga URAFIKI na wateja wako. Hii ni kwa sababu ni rahisi sana MTEJA kuwa RAFIKI yako kama utatengeneza UHUSIANO mzuri kati yenu. Hii ndio SIRI ambayo hakuna mtu atakwambia kirahisi.

Kufanya biashara mtandaoni ni Uwekezaji muhimu sana, na kwa maendeleo yaliyopo kwa sasa duniani, imekuwa ni rahisi mno kutumia huduma za Internet katika kuwafikia wateja popote walipo duniani.

Kuna mtu aliwahi kuniuliza, “Sasa nawezaje kutumia Internet kufanya biashara yangu?”

Jibu: Unaweza fanya haya yafuatayo ili uweze kupata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.:

1. Tumia Website na mitandao ya kijamii kutoa elimu kuhusu bidhaa/huduma zako.

2. Tumia SEO ili kurahisisha maudhui yako yanapatikana kirahisi katika Google.

3. Fanya matangazo (Paid Ads/Sponsored Ads) ili kuwafikia wateja wengi kwa haraka.

4. Jifunze kuuza katika Maandishi (Copywriting). Jaribu kadiri unavyoweza.

5. Tumia WhatsApp yako vizuri kibiashara (Status, Broadcast, Groups n.k).

Ukiona haya yanakuwa magumu kwasababu upo busy au vinginevyo, usikubali sasa biashara yako ife/ishindwe kufanya vizuri mtandaoni.

Tafuta mtaalamu wa kufanya biashara mtandaoni, mpe targets zako, kubaliana nae katika malipo, kisha mpe kazi ili biashara yako izidi kupaa mtandaoni kwa sababu ni muhimu sana ukazipata hizi Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako. Sio lazima kila kitu ukifanye wewe mwenyewe kwa sababu hakuna ajuaje kila kitu.

Ni mategemeo yangu umepata kitu kipya leo. Kumbuka ZAWADI yetu ya kufunga Mwaka inakwisha tarehe 10 December, halafu hii ni maalum kwa watu 10 tu watakaowahi kujinyakulia website zao.

Tutumie ujumbe sasa hivi au tuchek kupitia mawasiliano haya;

Call/WhatsApp: +255765834754

Email: info@rednet.co.tz

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni. Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

JINSI YA KUONGEZA MBINU ZA KULIFIKIA SOKO MTANDAONI

Kila mtu atakwambia post insta, facebook, tumia funnels, weka status za kutosha Whatsapp. Mwingine atakwambia kusanya namba za simu uwapigie, tuma emails kila siku nk. Sasa utafanyaje kuongeza mbinu za kulifikia soko? Utakapomaliza makala hii ya leo utafahamu kiundani kuhusu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni. Utafanyaje, twende sambamba mpaka mwisho.

Zama hizi za Internet na huduma za mitandao ya kijamii zimekuja na mgawanyiko wa watu. Kila mtu anatumia mtandao wa kijamii anaoona unampendeza. Sio ajabu uone kuna mtu hana account ya facebook lakini kutwa yupo instagram/twitter. Hata hivyo ukiwa mjasiriamali lazima ufike kote.

UNALIFIAJE SASA HILO SOKO LA MTANDAONI?

1. Kwa kutumia Mitandao kama Whatsapp, Instagram, Twitter na Facebook, sasa unaweza kueneza maudhui yako kote kote kwa mtindo wa Copy & Paste. Ndio sio dhambi kufanya C&P ikiwa maudhui ni yako. Hata hii makala usishangae kuikuta kwa page zatu za LinkedIn na Instagram. Hapa ni muhimu sana Ukaifahamu Nguvu ya Mitandao ya Kijamii katika biashara yako.

Unachotakiwa kufahamu ni kwamba mitandao hii imetofautiana, hivyo maudhui unayopost twitter inabidi UYAHARIRI ili yaendane na aina ya watu katika mitandao mingine kama Website yako, Facebook, Instagram na LinkedIn. So kazi ya kueneza maudhui haiwi ngumu kuvile hapa, sivyo?

2. Pia unaweza kuanzisha kampeni fulani na kisha unaieneza kwa njia ya barua pepe. Kufanikiwa kwenye hili kwanza unapaswa ukusanye anwani za barua pepe nyingi (walau elfu moja) na kisha uifanye kampeni yako kwa uweledi wa hali ya juu ndani muda fulani. Hii ndio Email Marketing.

E-Mail Marketing in Businessmbinu za kulifikia soko mtandaoni.

NB: Kampeni yako haipaswi kuwa na ujumbe wa kupandikiza chuki au viashiria vya ubaguzi wa namna yoyote kwa sababu kampeni za namna hio huleta hisia mseto kwa watu na kukujengea taswira mbaya. Barua pepe zako unaweza kuzikusanya kwa njia ya Newsletter au kawaida (ile ya kuomba).

3. Tumia Social Media Analytics Tools: Kama unasambaza maudhui yako kupitia mitandao ya kijamii, siku hizi kuna namna ambayo unaweza kupima mwenendo wa machapisho yako kirahisi tu. Katika twita kuna Twitter Analytics na Insta kuna Insights.

social media analytics toolsmbinu za kulifikia soko mtandaoni.

Hizo tools zitakwambia maudhui yako yamewafikia watu wangapi (impression), wangapi wameshiriki mjadala (engagement), wangapi wameclick links na umepata wafuasi wangapi baada ya kuchapisha maudhui. Ukishajua hayo itakusaidia sana kuboresha zaidi Machapisho yako yajayo.

Mitandao ya kijamii hasa Mtandao wa GOOGLE ina nguvu ya ajabu sana katika kuwafikia watu wengi ndani ya muda mfupi tu. Ni muhimu basi ukajua namna ya kucheza na mitandao hii ambayo kila mtu duniani anatamani awe mtumiaji wa kila siku. Kufahamu zaidi kuhusu nguvu hio gusa hapa;

4. Tumia Web Analytics Tools; Kama tayari unayo website ya biashara au page ya blogu yako, basi ni muhimu sana ukaweza kufuatilia na kujua ufanisi wake kwa watu wanaoitembelea. Unajua watu wangapi wanatembea website yako kila siku? Makala zipi ulizoandika zinafuatiliwa zaidi?

Watu wanaotembelea website yako wanatokea wapi? Katika Injini za Kimtandao, website yako iko katika nafasi gani? Majibu ya maswali yote haya unaweza kuyapata kwa kutumia tools kama Google Search Console, ahrefs, winch, clutch n.k Hivi ndo virutubisho vya website yako mtandaoni.

5. Tumia Content Management System (CMS); Ukiwa muandishi ambaye ungependa maudhui yako yazidi kufanya vizuri mtandaoni basi unapaswa kutumia mbinu mbadala zitakazokusaidia tena na tena. Sikuhizi mambo yamerahisishwa, WordPress ndio CMS maarufu zaidi lakini ukiacha hio kuna Joomla, Drupal, Magento, Shopify na Prestashop (kwa ajili ya e-commerce). Ukiwa na hizo tools inakuwa rahisi kwako kuandika maudhui ambayo yatakuwa rahisi zaidi kunaswa na Injini za Mtandaoni kama Google, Ask na Bing. Umeshawahi kutumia CMS gani? Tuambie hapa leo..

Content Management Systemmbinu za kulifikia soko mtandaoni.

6. Tumia SEO Hapa sitasema mengi kwa sababu tumeshaongea mengi huko nyuma. Kifupi hii SEO (Search Engine Optimization) ni teknolojia iliyopo kwenye software za mtandaoni zenye uwezo wa kukusanya taarifa kutoka vyanzo mbalimbali kama websites, blogs, mitandao ya kijamii n.k

Cha kuzingatia zaidi unapofanya SEO ni matumizi ya Keywords sahihi kwa ajili ya soko lako ulilochagua kuhudumia (niche), Picha unazotumia lazima ziwe na maelezo tambuzi (alt text), matumizi ya links pamoja na ujuzi wa kuuza kwa kupitia maandishi(copywriting skills) Zingatia sana haya kwasababu hii ndio mbinu bora sana katika kufahamu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni.

Yaani SEO ni SUMAKU inayovuta taarifa kutoka sehemu mbalimbali za watu (open source information) na kuzigawa kwa mtu yeyote ambaye atatafuta taarifa hizo. Umeshaielewa jinsi SEO inavyofanya kazi sasa? Kufahamu zaidi fuatana na makala hii hapa;

7. Fanya Mara kwa Mara; Umeshayaona haya tuliyoyaelezea leo? Sasa kama unataka kufanikiwa katika kuipeleka mbali biashara yako huku mtandaoni, basi SIO LAZIMA uyafanye yote, aghalabu, unaweza kufanya matatu au manne ili ujiweke kwenye nafasi nzuri katika kuimarisha ushawishi wako huku Mtandaoni. Lakini katika kuzifanyia kazi mbinu hizi basi ni muhimu mbinu hizi uzifanye MARA KWA MARA, yaani uwe na consistency. Usifanye mara mbili kisha ukakata tamaa. Andika machapisho 500, tuma emails 2000, rudia na rudia. Njiani utagundua ile njia sahihi zaidi.

Umegundua nini kwenye makala hii ya leo? Umeshafahamu kiundani kuhusu jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko mtandaoni? Una la kuongezea, swali au changamoto?

Tafadhali weka maoni yako hapa au kama unahitaji kuwasikiana nasi kupitia emails au Whatsapp, tafadhali fanya hivyo; Whatsapp/Call: +255765834754 Email: info@rednet.co.tz