Tag: faida za iot

KWANINI UHAMIE WINDOWS 10?

Inawezekana unaipenda sana windows7. Inawezekana pia computer yako ina taarifu nyingi ambazo usingependa uzipoteze. Lakini mifumo ya uendeshaji (OS) kutoka kampuni ya Microsoft hukamilisha muda wa huduma zake kila baada ya miaka 10. Sasa leo nataka nikujuze, kwanini uhamie windows 10?

Sasa kufikia January 14 mwaka 2020, kampuni ya Microsoft iliacha kutoa matoleo (updates) mbalimbali kuhusu windows7. Hivyo, matoleo ya kiusalama, speed n.k yalikomea hapo na kufanya kama unatumia Windows7 baada ya tarehe hio, basi computer yako ipo hatarini kushambuliwa kimtandao kwa kuwa hakuna uimara wa kiusalama tena katika mifumo ya uendeshaji (OS) ya computer yako.

JE, COMPUTER ITAZIMA BAADA YA UKOMO HUO?

Hapana, computer yako yenye windows7 itaendelea kufanya kazi kama kawaida isipokuwa, Microsoft hawatakupa updates za kuisalama wala marekebisho yoyote ya kiautomatiki yaliyokua yakitolewa hapo kabla. Hii itaifanya computer yako kuwa katila hatari kubwa ya kuvamiwa na virusi au mashambulio ya kimtandao yatakayoelekezwa kwako muda wowote upenyo ukipatikana.

KWANI LAZIMA KUWEKA WINDOWS 10?

Sio lazima, wala hakuna mtu atakulazimisha kuanza kutumia windows10. Lakini ni jambo muhimu na la busara zaidi kuimarisha mifumo tendaji (OS) ya computer yako kwa kuwa windows10 imetengenezwa kwa uimara zaidi katika matoleo ya kiusalama, antivirus iliyojishikiza (built-in antivirus) na Windows defender ambazo hukulinda zaidi dhidi ya shambulio lolote la kimtandao.

KWANINI MICROSOFT WAMEIACHA WINDOWS 7?

Microsoft wana utaratibu wao wa kisera (Fixed Lifestyle Policy) ambao unazipa muda wa kuhudumu bidhaa zao mbalimbali. Mfano, Windows 7 ilitoka kwa mara ya kwanza October 2009, hivyo miaka yake 10 ya kuhudumu imehitimishwa January 14 mwaka huu (japo imechelewa kidogo kufikia ukomo wake). Hii windows 10 inayopigiwa chapuo ilizinduliwa mwaka 2015 na inatarajiwa kuhudumu kwa miaka 10 mpaka 2025. Sasa windows 10 ilikua ni bure kabisa kuinstall mpaka kufikia majira ya kiangazi cha mwaka 2016. Lakini, ofa hio iliishia hapo ambapo kwa sasa itakulazimu kulipia gharama za kufanya installation kama unatumia matoleo ya zamani ya mifumo tendaji. Windows10 ya kawaida (Home edition) hugharimu dola za kimarekani $ 139.99 na ile ya kiuweledi (Pro edition) itakugharimu dola za kimarekani $ 199.99 kuipata katika majukwaa ya kimtandao ya Microsoft.

Sasa Leo tukiacha yote hayo, nataka nikupe faida 10 za kutumia windows10 kama mfumo tendaji katika computer yako:

1. USALAMA

Windows10 imerithi mifumo ya kiusalama kutokea kwenye toleo la nyuma yake la windows8, hivyo kuifanya windows10 kuwa salama zaidi. Hii ni kwa kuwa code yoyote ambayo huanza kufanya kazi pale computer inapowaka, basi code hio ni lazima ipewe kibali na Microsoft au watengenezaji wa Hardware (Dell, hp n.k). Lakini zaidi ya windows8, windows10 imetengenezwa kuhakikisha codes zake haziwezi kuvukwa (kuwa bypassed). Kuboresha huduma, hivi karibuni Microsoft wameongeza features katika usalama zaidi za Ransomware Protection na Threat Protection. Zaidi katika kuzingatia usalama wako uwapo mtandaoni hakikisha unapitia makala katika link hii KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO NI MUHIMU KWAKO? huu ni ukweli muhimu sana kuufahamu unapojiuliza kwanini uhamie windows 10?

2. SPEED

Kuanzia pale unapowasha computer yako, Windows10 hufunguka kwa spidi zaidi pengine kuliko computer zenye MacOS japokuwa mifumo tendaji ys Mac imeonekana muda mrefu kuwa ipo fasta zaidi. Safari hii imekula kwao. Injini ya 3D iitwayo DirectX 12, ambayo watengenezaji wa michezo ya video (video games) huitumia kurahisisha matengenezo na viwango vya michezo hio, hufanya kazi vizuri zaidi katika windows10 kuliko katika matoleo mengine.

3. CORTANA

Ebwana eeh, nna uhakika hata wewe huwa unafurahi sana pale unapoweza kuzungumza/kukiamuru kifaa chako kufanya jambo unalolitaka kwa sauti tu. Hapa watumiaji wa iPhone na yule “Siri” wao watakuwa wananipata vizuri sana. Sasa kwenye Windows10 kuna feature inaitwa “Cortana” ambayo ni teknolojia ya Sauti ambayo unaweza kuiamuru ifanye shughuli mbalimbali zilizopo kwenye computer yako kama “Hey Cortana, Cheza muvi ya Ray Kigosi, Imba wimbo wa Ray C, Onyesha picha ya Mr. Blue, zima computer.” nakadhalika. Hivyo vyote vinaweza kufanyika kwa sauti yako tu kupitia Kipengele hicho ndani ya computer yako yenye Windows10. Kumbe mambo ni murua bwana.

4. START MENU

Kama ulikua hufahamu basi Windows95 ambayo ilitoka mwaka 1995 ilikua na kipengele cha menu ambayo inafanana na menu ya windows8. Lakini watu waliilalamikia sana kuwa menu ile ilikua na mambo mengi hivyo kulazimisha Microsoft kuiondoa katika matoleo yake yaliyofuata. Lakini ajabu ni kwamba baada ya kubuni start menu ambayo ilitumika kwenye matoleo ya windows98 mpaka windows7 bado watu wengi walikua wakilalamika kuwa menu haijakaa vizuri mpaka ilipotoka windows8 na start screen yake. Hivyo toleo la Windows10 limeboreshwa zaidi na kuipa muonekano bora Start Menu yake na kuifanya yenye kuvutia na rahisi kutumia. Mudhui yake yameifanya iwe bora zaidi kwa kufanya Apps muhimu zaidi ziweze kuongezeka ukubwa na zile zenye umuhimu kidogo zinaweza kufanywa ndogo ili iwe rahisi hata kuchagua kwa kutumia kipanya (mouse).

kwanini uhamie windows 10?

5. TOUCH

Kama kila kifaa unachotumia kimetengenezwa kuruhusu teknolojia ya “Touch screen” kuanzia simu janja, redio za gari, tablet mpaka mifumo ya ramani elekezi (navigation systems). Sasa kwanini isiwezekane katika computer yako pia? Kuna watu watasema “oh kioo cha Pc ukiwa unakigusa gusa kinachafuka na kuharibika mapema” Sasa hilo linakuaje tatizo kwenye Pc na lisiwe kwenye simu yako ambayo kioo chake ni kidogo zaidi na unaitumia muda mwingi zaidi kwa siku. Basi kama ulikua hujui, computer zilizotengenezwa kupokea teknolojia ya “Touch screen” hufanya kazi kwa ufanisi zaidi pale zinapokuwa na Windows10 kuliko zile zinazokua na mifumo tendaji mingine. Pc kama Lenovo IdeaCenter Yoga A940, The Surface Pro7, Convertible Tablet na Acer T232HL ambazo zimewezeshwa na Touch screen hufanya kazi kwa ufanisi zikiwa na Windows10 kuliko hata Tablet za iOS katika mambo mengi.

6. KIVINJARI BORA

Hakuna tena mambo ya Internet Explorer. Sasa hivi ni mwendo wa Microsoft Edge ambayo ni balaa. Hii Microsoft Edge imefanywa kuwa bora sana katika speed, vipengele (features) kama web page markup na reading mode. Vile vile hii Edge inatajwa kuwa inatumia kiasi kidogo cha umeme (Power use) kuliko kiasi kinachohitajika katika kivinjari cha Google Chrome. Huu ndio ukweli muhimu sana kuufahamu unapojiuliza kwanini uhamie windows 10? Sasa Inategemewa katika maboresho yajayo kutakuwa na matafuto ya mtandaoni kupitia “Cortana” katika hii Microsoft Edge. Watu wamejipanga bwana.

7. KUCHAPA(TYPING) KWA SAUTI

Kirahisi kabisa, bonyeza alama ya Windows na kitufe H (Ili kuiamuru computer yako ianze kukusikiliza). Halafu anza kuongea kila unachotaka kichapishwe kwenye nyaraka yako. Hakuna haja ya kutatanisha mambo hapa. Wale wavivu wa kuchapa hapa ndo kwenyewe.

8. VIUNGANISHI VYA SIMU (SMARTPHONE TIE-INS)

Windows 10 bwana imeundwa kitaalamu sana. Yaani sasa unaweza kuunganisha smarphone yako na computer yako ili kuhakikisha shughuli zako unazofanya baina ya vifaa vyako zinakuwa zikishirikiana na kuungana (synchronized). Kuna App imeundwa katika Windows10 inaitwa “Continue on PC App“, Hii sasa hutuma kurasa za tovuti ulizopitia au nyaraka ulizozihifadhi katika computer yako moja kwa moja zinafika kwa simu yako na hivyo unapata wepesi wa kufanya shughuli zako kirahisi hivyo yani. Unaweza kutumia kivinjari cha Microsoft Edge kuunganisha shughuli zako za mtandaoni na kipengele cha Cortana kuunganisha kumbukizi (reminders) baina ya vifaa vyako. Watumiaji wa Android hapa ndo wanafaidi zaidi, nyie wengine wa iOS ebu tulieni kwanza. Kwa kutumia kipengele cha “Your Phone App” sasa unaweza kuona picha zako na video mara tu unapopiga kutokea katika camera ya simu yako. Hivi karibuni kutakuwa na toleo la Voice calling hata katika computer yako yenye Windows10. Mambo ni mazito.

9. DARK AND LIGHT MODES

Sikuizi bwana kila kitu ni Dark mode. Sio Whatsapp, Telegram, Instagram, kote kote yani ni mwendo wa Dark mode. Sasa Windows10 nayo haiko nyuma, toleo la mwezi May, 2019, kampuni ya Microsoft walisambaza upendo kwa “wapenda giza” pia ambapo sasa unaweza Kwenda kwenye Settings>Personalization>Colors. Halafu hapo unachagua rangi uipendayo halafu mambo yanakuwa safi kabisa. Kuna baadhi ya vivinjari (browsers) huheshimu aina ya rangi unayotumia katika windows10 yako mfano Microsoft Edge. Hii ndio raha ya kuufahamu utamu unapojiuliza kwanini uhamie windows 10?

10. GAMING BAR

Yes, kwa kubofya kitufe cha Windows kikifuatiwa na kitufe G (kama haiko active nenda kwa Settings>Gaming>Game Bar). Hapo sasa unaweza kupiga screenshot, kurekodi video, audio na mambo kibao kuhusu game unayocheza hapo. Ikiwa tu computer yako ina RAM ya kutosha pamoja na Processor nzuri. Basi hiki kipengele kinakuhusu vilivyo.

BONUS: Kuna watu wanahisi Windows10 ni nzito, ngumu kutumia na ina mambo mengi ambayo sio muhimu. FYI, kampuni ya Microsoft imefanya marekebisho ili kuhakikisha mtumiaji anafanya kazi zake kirahisi bila shida yoyote ya kiufundi. Na zaidi, wa wataalam (coders and gamers) wameongezewa vipengele ili kuhakikisha kazi zao zinapatiwa msaada stahiki kupitia matoleo ya Windows10.

Zaidi, hakikisha unapotumia Windows10 unapata huduma ya Internet (wi-fi) ili kuhakikisha matoleo muhimu ya kiusalama (security updates) unayapata kwa wakati. Tumia wifi nzuri ili usije ukapata gharama za ziada unapotumia bando lako la simu (ambalo kwa watu wengi hupigiwa bajeti kali).

Sasa tumekuwekea makala zingine kwa ajili ya kukupa maarifa na taarifa zaidi kuhusu namna nzuri ya kutumia teknolojia hizi kwa manufaa yako binafsi na manufaa ya uchumi wa biashara yako binafsi. Gusa link kisha makinika:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO KIMEDUKULIWA
  3. YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO (CYBER ATTACK) NA ATAHARI ZAKE KATIKA BIASHARA YAKO

Kiufupi hii ndo Windows10 na umuhimu wake. Kama hujawahi kutumia OS zingine, hii inakufaa. Ukiwa na maoni yoyote ama ushauri kuhusu kufanya installation ya Windows10 katika computer yako, tafadhali wasiliana nasi kupitia namba yetu ya simu ya 0765834754 au barua pepe info@rednet.co.tz. Karibu sana.

KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?

Hebu fikiria wewe ni mgeni mahali fulani, baada ya kushikwa na njaa unaelekezwa migahawa miwili, mmoja ukiutafuta mtandaoni unaweza kupata taarifa zake mwingine hauna taarifa yoyote mtandaoni. Uelekeo wako utakuwa upande gani? Leo sasa tutakwenda kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako. Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Kuishi katika ulimwengu wa kidijitali, tovuti ni zana muhimu sana katika biashara na masoko ya kidijitali. Cha kushangaza inakadiriwa 35% – 50% ya biashara ndogondogo duniani hazina tovuti zao binafsi, jambo linalozinyima fursa ya kuweka taarifa zao kirahisi mtandaoni na kupata wateja wapya kirahisi.

Kuna wanaosema kuwa matumizi ya Tovuti yanamezwa na uwepo wa mitandao ya kijamii ambayo pia watu wanaweza kuweka na kutangaza biashara zao humo. Ni kweli, aghalabu, kwa kutumia Mitandao ya kijamii hauna uhakika wa kumiliki taarifa na maudhui unayoweka humo muda wote. Watengenezaji ambao pia ni wamiliki wa Mitandao hio wanao uwezo wa kusimamisha/kufuta akaunti au maudhui yako muda wowote ikiwa biashara/maudhui yako yanakwenda kunyume na matakwa na masharti yao.

Vile vile Mitandao ya kijamii unayotumia inaweza kupungua umaarufu au kufilisika muda wowote usioutegemea mfano kuna mitandao ilikua maarufu sana zamani kama Hi5 lakini umaarufu wake kwa sasa umepungua au kupotea kabisa. Hivyo, uwezekano wa kudorora kwa biashara yako kunategemea pia umaarufu wa mtandao wa kijamii unaoutumia, jambo linalichangiwa sana na ujio wa mitandao mipya ya kijamii kama Instagram, Whatsapp na TikTok. Hii kwako unaionaje? Nitaeleza Tofauti katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Tovuti wakati Ujao.

Faida ni nyingi sana za matumizi ya website katika kuimarisha biashara yako kupitia ulimwengu wa Teknolojia. Tayari tumekuandalia makala maalum kupitia link hii hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

Leo hii ntakwambia mambo 10 kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika biashara yako:

1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:

Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu huenda wapi kutafuta vitu kama suppliers, bidhaa na huduma mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi. Injini za matafuto mtandaoni zimekuwa kimbilio namba moja huku GOOGLE Ikiziacha mbali Injini zingine kama Yahoo, Bing na Ask. Maana yake hii ni kwamba kama huna tovuti, jua mauzo yako ni 7% tu ya soko zima ambalo hujui kuwa unalo. Upo apo? Yani unapoteza 93% ya mauzo yako kila siku bila hata wewe mwenyewe kujua.

2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)

Kama una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo. Kwa biashara zenye malengo makubwa kuwa na tovuti huwaweka kwenye nafasi za juu katika kupata tenda na wateja, na huonyesha Uweledi bora katika utendaji wa biashara kuanzia katika muonekano na utendaji wa tovuti. Inakadiriwa 80% ya watu duniani huonyesha kutokua na imani na Biashara ambazo hazina tovuti pale wanapotaka huduma/bidhaa fulani mtandaoni.

3. KUPATIKANA KWA URAHISI

Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi, tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako. Ndivyo ilivyo kwa tovuti ambayo inajieleza kwa kila kitu kama ilivyo tovuti maridhawa ya http://rednet.co.tz . Ile raha ya kupata taarifa, huduma au bidhaa kirahisi kupitia simu yako ya mkononi, hufanya wateja waongezeke maradufu na kusambaza sifa bora kwa uharaka sana katika jamii na katika mitandao ya kijamii hali kadhalika.

Hii huongezwa chumvi ya SEO (Search Engine Optimization) ambayo ni teknolojia iliyowekwa katika Injini za matafuto ya kimtandao inayowasiliana na tovuti yako na kuweka taarifa katika Injini hizo na hivyo kufanya taarifa za tovuti yako kuonekana haraka zaidi katika matafuto. Biashara imerahisishwa sana kupitia SEO kuliko kutumia Mitandao ya kijamii. Kama watu wanakwenda Google kutafuta taarifa, basi fahamu taarifa hizo hupelekwa hapo GOOGLE kwa kutumia teknolojia iitwayo S.E.O. Kufahamu zaidi kuhusu SEO gusa hapa chini

4. TANGAZO LA BURE MUDA WOTE

Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo huduma ya internet inapatikana. Tangazo la bure kabisa hili. Kama tovuti yako ina ubora wa kuvutia zaidi katika muonekano, maudhui na utendaji, basi bila shaka biashara yako ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri sokoni na kupata wateja wengi kila siku. Jiulize hivi, unapofunga ofisi/biashara yako wakati wa jioni kila siku, wateja wapya wanaweza vipi kupata taarifa sahihi muda watakaohitaji?turudi kwenye mada yetu, kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Hii pia inawezeshwa sana na teknolojia ya S.E.O.

5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)

Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa. Kupitia tovuti yako, unaweza kuweka testimonials kwa idadi uitakayo bila kurudia rudia na katika mpangilio maalum na watu wakaweza kuona ushahidi utakaowaridhisha kuendelea kutumia huduma/bidhaa zako. Mara nyingi Mitandao ya kijamii huzuia kuoneka kwa biashara kwa urahisi kutokana na wimbi la watumiaji wenye maudhui tofauti tofauti katika ratiba ya saa (timeline) yako unayopitia katika mitandao hio, hivyo kusababisha usumbufu (distractions) katika biashara yako.

6. UAMINIFU (TRUST)

Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza mahusiano na mteja kama UAMINIFU. Ili kupata wateja wa kudumu katika sekta nyingi, kuwa na tovuti hai ni muhimu katika kudumisha mahusianao katika ya mfanyabiashara kwa muda wowte mteja atakaohitaji.

7. POSITIVE ROI

Ikiwa ni Return On Investment (ROI) au Rejesho baada ya Uwekezaji, unapoendesha biashara ambayo ina gharama zake kama umeme, kodi, maji, mafuta n.k, ukijiuliza utaweza vipi kurudisha gharama hizo upate faida? Njia moja nzuri ni matumizi ya tovuti bora yenye uwezo kunasa wateja wapya kwa njia ya mtandao muda wote (24/7) kirahisi kabisa.

8. THAMANI INAYODUMU

Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote itakapohitajika kufanya hivyo. Hivyo thamani ya biashara yako itaendelea kuwepo muda wote tovuti yako inapokuwa hewani.

9. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA

Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei, ushauri nakadhalika. Hivyo kuimarisha mahusiano na ukaribu wako na wateja wako wakiwa popote duniani kwa urahisi kupitia miundombinu mbalimbali unayoweza kuiweka katika tovuti yako kama matumizi ya chatbots na barua pepe maalum za kibiashara (zenye jina/domain name ya tovuti yako).

10. MASIJALA (DATA CENTER) RAHISI YA MTANDAONI

Tovuti yako inaweza pia kuwa masijala rahisi kwa wafanyakazi, wateja na mtu yeyote anayehitaji kujua taarifa kuhusu huduma/bidhaa unazohusika nazo. Mfano mzuri ni tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz ambayo zaidi tu. ya kwamba inatoa taarifa kuhusu huduma tunazohusika nazo za kutengenza websites, softwares, apps n.k, lakini pia tovuti inatoa taarifa muhimu mbalimbali kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia. Taarifa hizi zimetengenzwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha Biashara za wateja wakiwa popote duniani. Pia taarifa hizo zinalenga kuhamasisha matumizi ya Teknolojia katika njanja mabimbali za kiuchumi haswa kwa wafanyabiashara waliopo kusini mwa jangwa la Sahara.

NOTE: Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa muhimu kama jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.

BONUS POINT: Tovuti yako unapoisajili, unashauriwa pia upate kirurushi cha barua pepe yenye jina/domain name sawa na tovuti yako. Mfano, tovuti yako inapatikana katika anwani ya www.mfano.com, hivyo barua pepe yako ya kiofisi unaweza kuchagua kuwa info@mfano.com au maulizo@mfano.com au jinalako@mfano.com. Kwa kutumia barua pepe zenye jina sawa na anwani ya tovuti yako, unajiweka katika nafasi nzuri ya kuimarisha biashara yako na kuongeza wateja wapya na kazi zenya manufaa haraka zaidi katika biashara/kampuni yako. Hii ni sababu muhimu sana unapojiuliza kwanini ni muhimu kuwa na website (tovuti) rasmi ya biashara yako. Website inakufanya unakuwa official kiukweli kweli.

Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna bora za kuimarisha uchumi wa biashara yako kwa kutumia Teknolojia:

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. BRANDING vs MARKETING, KIPI NI KIPI?
  3. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA (AfCFTA), KUNA MANUFAA GANI KWAKO?
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO.

Umejifunza nini kupitia makala hii ya kuhusu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Tafadhali unaweza kuwasilisha maoni yako kupitia sanduku la maoni (comments box) lililo hapo chini au kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yanayopatikana katika Footer Bar chini kabisa ya ukurasa huu. Pia usisite kuwashirikisha wenzako makala haya kwa kushare link yetu ya https://rednet.co.tz mara zote. Karibu!

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE

Yaani ni 8% tu ya makampuni ndio wana uwezo wa kugundua wizi wa taarifa zao ndani ya dakika chache. 62% wanaweza kugundua wizi ndani ya siku kadhaa. Wewe unatumia muda gani kugundua upotevu/wizi wa data katika kampuni yako? Makala hii tutaangazia mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) kiundani. Leo, yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake. Makinika mpaka mwisho.

Kama Unavyoona biashara zinavyozidi kushamiri kiteknolojia ndivyo wadukuzi nao wanazidi kutafuta mbinu za kufanya mashambilizi zaidi. Mwaka 2019 peke yake, zaidi ya 2$ billion zilipotelea mikononi mwa wadukuzi duniani. Utafiti wa Juniper unaonesha namba hio inaongezeka kila mwaka.

Unalikumbuka shambulizi lilioitwa NotPetya? Basi jarida la WIRED linalitaja shambulizi hilo kama “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA”. Ndani ya masaa machache tu virusi vya shambulio hilo (malwares) viliathiri kutoka biashara ndogo za Software nchini Ukraine mpaka kusambaa katika vifaa vya kielektroniki dunia nzima. Shambulizi lilidhoofisha mashirika makubwa duniani kama FedEx, TNT, Express na Maersk kwa wiki kadhaa na kusababisha hasara ya zaidi ya $10 bilioni kwa ujumla. Upotevu wa data kwa kiwango hiki unaonyesha namna katili ya dunia tuishiyo ambapo inaonekana hakuna mwenye kinga madhubuti mtandaoni. Kutoka Mashirika makubwa, serikali, mitandao ya kijamii, mifumo ya migahawa na sehemu yoyote unayojua inatumia teknolojia ya IT, Kila mmoja yupo hatarini.

TUMEFIKAJE HAPA?

Ripoti ya mwaka 2019 ya shirika la Accenture Security kuhusu Matishio ya kimtandao (Cyber Threatscape), imeonyesha sababu za wadukuzi kuendelea kuwa tishio dhidi ya taarifa binafsi/za mashirika kwa manufaa yao. Hizi ni baadhi sababu hizo:

1. Wadukuzi wa kimtandao hufaidika zaidi na teknolojia mpya na kukosekana mawasiliano madhubuti katika sheria na tawala za maeneo/nchi mbalimbali duniani.

2. Mitandao ya kihalifu muda wote inakwenda ikibadilika, hasa kuelekea katika makundi ya kihalifu ya siri (syndicates) pasi na kujulikana chanzo chake kwa kutumia nyaraka halali kwa nia halifu.

3. Malengo mseto katika kuimarisha tabia za virusi (kama kujiendesha vyenyewe: self replication)

4. Kuimarika kwa mifumo ya Ulinzi wa Kimtandao (cybersecurity hygiene) inapelekea wadukuzi nao wazidi kujiimarisha kimbinu na maarifa katika uwanda wa kiteknolojia na matumizi ya internet.

Baada ya kujua sababu zinazowasukuma Wadukuzi na wahalifu wa Kimtadao kuendelea kufanya mashambulizi, Leo, uta yafahamu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako, Fuatana nami..

Duniani kunazo aina nyingi za mashambulizi ya kimtandao kulingana na sababu nilizozieleza hapo juu kama ifuatavyo:

1. RANSOMWARE ATTACK: Katika shambulio hili, virusi maalum (specific malware) ambavyo hukusanya na kufunga taarifa/kifaa katika mtandao ili kumnyima mtumiaji haki na uwezo wa kufanyia kazi taarifa zake kama kawaida. Haki na uwezo (access) huo humrudia mtumiaji pale tu matakwa ya mdukuzi yatakapotimizwa ambayo mara nyingi huwa ni pesa au rushwa kwa mapana yake.

Saa ingine wadukuzi wanaweza kugoma kurudisha haki za matumizi kwa mhusika hata wanapotimiziwa matakwa yao, hivyo kuongezea hasara kwa kampuni/biashara. Mbaya zaidi, ripoti ya mwaka 2019 ya Uhalifu wa kimtandao inaonyesha kutokea kwa shambulizi hili kila sekunde11 ya mwaka 2021.

2. ADVANCED PERSISTENT THREATS (APT): Shambulizi hili sio la mojakwamoja (passive attack) ambapo mdukuzi anapata access ya computer/mtandao fulani kwa muda mrefu pasi na kujulikana, hivyo kujichotea taarifa na kuzitumia kwa manufaa yake. Aina hii pia huitwa Trojan Horse attack.

3. PHISHING: Je wajua? Mpaka 32% ya wizi wa data husababishwa na shambulizi hili. Hii ni aina ya shambulizi maarufu sana la kijamii (social engineering) ambapo mdukuzi humtegea mtu adownload file lililo na virusi kupitia SMS, email au link na kuingiza virusi katika kifaa chake.

unawezaje kujilinda dhidi ya shambulizi la kimtandao la phishing katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

4. SQL INJECTION: Umeshawahi kuona ile unaingia kwenye website ukakuta haipo ghafla tu, au kwenye system flani unanashangaa kuna mafiles huyaoni bila sababu ya msingi. Sasa kwa kutumia virusi halifu (malicious codes) shambulizi hufanyika katika servers zinazohifadhi taarifa muhimu za watumiaji na kuzifuta, kuziiba au kuzibadili ili kutimiza azma fulani ya wadukuzi na/au genge lao. Mara nyingi shambulio hili hufanyika kwenye servers zinazohifadhi taarifa ghafi za watu au vitu (personal identifiable information: PII) kama namba ya kadi, username and passwords.

5. DDOS ATTACK: Kirefu huitwa Distributed Denial of Services attack ambapo hutokea pale wadukuzi wanapofurika tovuti au kifaa chako kwa either kupunguza au kondoa kabisa utendaji wa kawaida na hivyo kuiacha kampuni/biashara kuhangaika kurejesha performance ya mifumo yake wakati wao (wadukuzi na virusi vyao) wakitumia mwanya huo kuiba na kufanya uhalifu katika mifumo hio iliyoathirika.

6. MAN IN THE MIDDLE (MITM): Hii hutokea pale mdukuzi anapoingilia mawasiliano halali ya kampuni bila ya wao kujua. Pia shambulio hili hufahamika kama eavesdropping pale linapofanyika baina ya mawasiliano binafsi ya simu kati ya mtu na mtu.

Mawasiliano katika MITM hiungiliwa pia kupitia APN za Wi-Fi za uongo (deceptive wifi). Zaidi ya kuingilia mawasiliano, hapa mdukuzi anaweza pia kuwasiliana akitumia utambulisho (ID) ya wahusika pasi na kufahamika mara moja.

7. PASSWORD ATTACK: Licha ya kuwa shambulizi maarufu zaidi duniani, bado kuna watu huangukia mtego wa kuibiwa nywila zao. Kwa urahisi wake, wadukuzi hutumia mbinu zenye viwango na ujanja kupata nywila dhaifu na kufungua accounts za watumiaji kirahisi. Hapa tunaangukia kwenye usalama wa vifaa vyetu vya mtandaoni. Je viko salama kiasi gani? Fuatana na makala hii hapa kufahamu zaidi..

UNAWEZAJE KUZUIA MASHAMBULIZI HAYO?

Katika yetu iliyopita tumeeleza kwa kirefu kuhusu namna ya kujiepusha na mashambulizi ya kimtandao (Cyber attacks), pitia hapa KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?“. Leo pia, tutaona njia zingine za kuendelea kujiimarisha na kuzuia mashambulizi hayo yasiathiri Biashara/Kampuni yako. Mashambulizi mengi niliyoyaelezea leo yanazuilika kwa njia ambazo tayari tulishaziona katka makala zilizopita isipokuwa:

MITM Attack: •Tumia SSL Certificates za (https) katika website yako. Hii ni boresho la http SSL certificate ambayo ni ya zamani na usalama wake mi mdogo.

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

•Tengeneza VPN yako kama ngao ya ziada dhidi ya wi-fi halifu (deceptive wi-fi). Mashambulizi haya katika biashara yako yana madhara makubwa ikiwemo Kupotea kwa Fedha, faida ya biashara, mauzo, matengenezo, Hadhi ya biashara kushuka au kupotea kabisa na madhara ya kisheria.

Hivyo unapaswa kuwa makini na kufuata ushauri wa kitaalamu kuhusu maboresho ya kimtandao (updates & maintenance) ili kuhakikisha unatumia teknolojia ya kisasa zaidi ambayo ni salama huku ikiwa imeambatana na Passwords zako zilizo bora. Utajuaje kama simu/computer yako ikiwa imedukuliwa? Majibu tayari yanapatikana kwenye makala iliyo hapa UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?.

Usalama wa Kimtandao ni jukumu langu. Ni jukumu lako. Ni jukumu letu sote. Tuchukue tahadhari muda wote tuwapo mtandaoni. Basi ni matumaini yangu leo mengi umeyafahamu kuhusu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako. Ukiwa na swali au nyongeza tafadhali tuandikie katika comments hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo? Umejifunza nini katika ku yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake katika biashara/kampuni yako.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Unawezaje kujikinga dhidi ya mashambulizi ya kimtandao katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake
mapinduzi ya viwanda

FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA KATIKA BIASHARA DUNIANI

Japokua ilipitwa na zama 3 tayari, lakini sasa Afrika imedhihirisha kwamba haitaki kupitwa tena katika Mapinduzi ya 4 ya viwanda Duniani. Hii ni kutokana na kukua na kuimarika katika sekta za Afya, Elimu, Biashara, Teknolojia pamoja na Mahusiano na Muingiliano wa kijamii ikichagizwa na maendeleo katika miundombinu, usafirishaji na mitandao ya kijamii. Leo tuta fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. Ni nini na yanaashiria nini kwenye maendeleo ya biashara zingine? Makninika mpaka mwisho.

Mwezi September, 2019, jijini Cape Town Afrika Kusini ulifanyika mkutano wa kiuchumi wa WEF (World Economic Forum) ambao unazishirikisha nchi mbali mbali duniani, wafanyabiashara pamoja na wadau wa uchumi.

Mwaka huo 2019 viongozi waliokutana kujadili mustakabali wa Afrika walikua na jambo la msingi sana ambalo linatumainiwa kuleta maendeleo katika uchumi barani ambalo ni Utekelezaji wa Kuanzishwa kwa Eneo Huru la Biashara Barani (African Continental Free Trade Area AfCFTA). Baada ya miaka mingi ya mazungumzo, makubaliano yamefikiwa ya jinsi ya kuvunja vikwazo vya kibiashara, kukuza uchumi na kuunganisha nchi ambazo katika historia zilikuwa na mahusiano mazuri ya kibiashara na bara Ulaya, Amerika na Asia. Kufahamu zaidi gusa hapa chini:

Changamoto; Afrika (wafanyabiashara, kampuni na mashirika) imejifunza nini katika Kongamano hilo la Kiuchumi (WEF)? Na zaidi, Afrika inajiandaa vipi na Mapinduzi ya 4 ya viwanda yanayoendelea duniani?

Kufikia mwaka 2018 Afrika peke yake iliripotiwa kuwa na vijana takribani milioni 200 wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24. Na namba hio inatajwa kuongezeka mara mbili kufikia mwaka 2050.

Sasa “Kuwa na bara lililosheheni vijana ni fursa adhimu sana, lakini vile vile ni tishio kubwa.” alitahadharisha Albert Zeufack, Mchumi Mkuu wa Benki ya Dunia barani Afrika. “Ni tishio kama hatutohakikisha idadi hio ya vijana hawaanzi kufanya kazi inavyotakiwa.” Sasa kufikia Mapinduzi ya 4 ya viwanda, maeneo kadhaa yaliangaziwa na kituo cha mabadiliko ya kiuchumi barani (Africa Center for Economic Transformation, ACET) kwa niaba ya Benki ya maendeleo barani AfDB.

africa na mapinduzi ya viwanda

1. MACHINE LEARNING/ARTIFICIAL INTELLIGENCE/ROBOTICS;

Fikiria kuhusu gari inayojiendesha bila dereva na kufuata sheria na alama za barabarani ipasavyo ikijumuisha foleni. Watu wengi wangesita kupanda katika gari inayojiendesha yenyewe bila dereva, lakini hayo ndio mapinduzi halisi ya viwanda kupitia teknolojia.

Pia eneo hili limeshuhudiwa na ubunifu mwingi ukiwemo; mashine za kisasa za kuvuna na kupembua nafaka na madini, mifumo ya kiautomatiki inayoendesha ndege, meli pamoja na Teknolojia ya kupima udongo. Ni wazi mashine zinaweza kufanya kazi zifanywazo na binadamu katika zama hizi za mapinduzi ya 4 viwanda.

Swali, umejiandaeje kulinda taaluma yako dhidi ya zama hizi za mashine kujifunza (machinelearning) pamoja na teknolojia ya akili isiyo ya asili (ai)?

2. INTERNET OF THINGS (IoT);

Vifaa vingi vya kielektroniki vinavyotumiwa na mwanadamu sasa vinao uwezo wa kuingiliana na vifaa vingine kirahisi katika kurahisisha utendaji. Fikiria pale unarudi nyumbani na kuwasha feni yako kwa kutumia simu yako ya rununu (smartphone). Au kuweza kuendesha jokofu lako kwa kutumia teknolojia ya RFID. Kuunganishwa vifaa vya kielektroniki na huduma za intaneti imerahisisha sana mfumo wa mawasiliano na manunuzi ambao umeinua uchumi japo faida zake bado hazijasambaa sana barani Afrika.

Fikiria vile unaweza nunua bidhaa katika duka bila kumwona hata muuzaji. Hii inawezeshwa na teknolojia za biashara za kielektroniki (ecommerce) ambapo mteja anaweza kulipia kwa kutumia kadi yake ya benki au huduma za kifedha za simu ya mkononi kama MPESA na tigopesa. Katika bara ambalo muingiliano ni mkubwa kama Afrika, hili ni jambo la kutilia maanani sana, haswa wakati huu ambapo unajaribu ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. (Ambapo sisi kama Rednet Technologies ni wadau wakubwa kuhakikisha hupitwi na huduma za kisasa kwa kutumia teknolojia).

Kufahamu mapinduzi ya IoT katika biashara na maisha kwa ujumla tayari tumekuwekea makala maalum kupitia link hii hapa MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA

3. DATA MINING/DATA SCIENCE TECHNOLOGIES;

Kituo cha ACET katika mwaka 2018 kiligundua kwamba “kuvua taarifa nyingi mtandaoni, kwa kutumia kompyuta zenye uwezo mkubwa na kanuni za mifumo ya Akili isiyo ya Asili (AI), huwezeshwa kupatikana kwa ripoti bora ya taarifa sahihi.” Fikiria mifumo ya tiketi za ndege, hoteli, mifumo ya kulipa kodi na taarifa za mteja wa benki.

Sekta ya Takwimu inafurahia sana ujio wa teknolojia ya Kuvua/Kuvuna Taarifa na Sayansi ya Taarifa. Jinsi ya utendaji katika teknolojia hii ni fursa adhimu sana katika kuimarisha biashara kwa kutumia takwimu sahihi zilizovunwa kutokana na taarifa mbalimbali za watu. Mifumo ya tiketi za ndege, Usajili wa vyumba vya Hoteli, taarifa za wateja wa benki na hata mfumo wa Kulipa kodi (Tax returns), hivi ni baadhi ya vyanzo vya ukusanyaji wa taarifa muhimu katika kufanya Uvunaji wa Data na Sayansi ya Data. Serikali za Africa zinamiliki kiwango kikubwa cha taarifa hizi. Je, italeta manufaa kwa Umma au itafanywa kama biashara na wajasiriamali? (Tafiti na ripoti tunazokuwekea kwenye makala zetu hizi zitakupa majibu.😋)

4. 3D PRINTING;

Ama kwa hakika mapinduzi ya viwanda yanakuja na mengi. Hebu buni bidhaa yako kwenye kompyuta halafu ichapishe kama ilivyo. Kutoka ubunifu uliotengenezwa kimchoro mpaka uhalisia katika kuchapisha tu, hii inakwenda kubadili hata namna ya uendeshwaji wa viwanda barani Africa ambapo ugunduzi huu unaleta matumaini katika uwanda wa ubunifu na ujenzi ambao unatazamiwa kuleta maendeleo katika nchi za Afrika. Viwanda vinawezaje kuendana na teknolojia hii ya Uchapishaji? Vimal Shah mkuu wa shirika la viwanda vya BIDCO nchini Kenya mwaka 2017 alinukuliwa akitania, “Tunaweza kuchapisha pizza wakati ujao.”😂

Sasa watunga sera na sheria barani walishaona uhalisia huu kama kuchapisha mfano wa kitu halisi (3D-Printing) katik mipango yao ya muda mrefu?

5. BLOCKCHAIN/TRUST TECHNOLOGIES;

Mwaka 2018 kituo cha ACET kiligundua kwenye uchunguzi wake kwamba teknolojia ya Blockchain inawafanya watu hata wasiaminiana au kujuana, kuweza kushirikiana bila ya kuwa na haja ya kwenda kwenye mamlaka za serikali. Yaani Blockchain ni jalada huru linalosajili miamala ya kifedha kati ya watu wawili au zaidi kwa usahihi na njia bora zaidi. (Tulishaelezea kuhusu Blockchain na cryptocurrencies kwenye makala zetu zilizopita). Sasa itakuaje kwa huduma za kibenki, wanasheria, wakala wa fedha (brokerage firms) na wahusika wa kiserikali katika maswala ya kifedha? Kitawakuta nini, tutajadili kwenye athari ya mapinduzi ya viwanda mbeleni.

mapinduzi ya viwanda

Si ajabu, teknolojia ya Blockchain inaonekana kama mkombozi dhidi ya vitendo vya Rushwa kutokana na undeshwaji wake ulio sahihi na wa haki. Kwa inavyoonekana teknolojia hii ya Blockchain inakwenda kuwa pigo kubwa kwa watu wenye misuli ya kiutawala, madikteta wa waendeshaji wa siasa chafu. Itakapofika siku Teknolojia hii imefikia matumizi yale yaliyonuiwa wakati inaanzishwa, basi wahafidhina na mawakala wa kifedha wa serikali na mashirika binafsi watapoteza nguvu zao. Hakutakuwa na haja ya mihuri, wala sahihi, wala zile nenda urudi kesho tukuhudumie. Blockchain itakwenda kuiweka Afrika huru dhidi ya kero za huduma za kifedha na usalama wake kuwa katika ukuaji mzuri. Haya ndio mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani.

5. BIOPHYSICS AND BIOENGINEERING;

Eneo la 5 ambalo kituo cha ACET imeliacha ni kuhusu mtandao wa mifumo ya kibaolojia na kifizikia. Utahitaji mkono wa bandia unaoweza kuendeshwa na ubongo wako kwa usahihi ikitokea mkono wako halisi umekatika? Hebu fikiria hapo. Tunakubali kwamba asili ni bora sana kuliko sisi, hivyo ni bora kujifunza kwayo, kwasababu mapinduzi haya ya viwanda kwa kuchagizwa na ukuaji wa kiteknolojia duniani yatafanya taaluma ziweze kunyumbulika kwa namna nyingi sana hapo baadaye. Je, mifumo ya elimu imejiandaa na hili katika maandalizi ya mitaala yake ya muda mrefu?

Sasa tumeshajua yanayokuja na Mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani. Afrika, bara ambalo ajira bado ni tatizo kubwa kwa vijana, wataweza vipi kupambana na athari za mapinduzi haya? Kuna nadharia tatu (3) katika kukabiliana na hali hii;

1. Afrika inaweza kuketi chini na kubaki kutizama dunia nzima ikipambana katika Mapinduzi haya. Hii ilishafanyika katika zama 3 zilizopita za Mapinduzi ya viwanda ambapo Mapinduzi ya Kwanza yaliegemea katika kutengeneza mifumo ya Kimekanika na matumizi ya Injini za mvuke katika kutengeneza bidhaa kama nguo.

Mapinduzi ya pili yakiwa ni kuhamasisha Uzalishaji mkubwa (mass production) wa bidhaa viwandani yakichagizwa na Henry Ford na awamu ya 3 ya mapinduzi ikiwa ni zama za kidijitali katika uzalishaji.

Ukitizama elimu ya msingi ya kuunda Injini ni ile ile iliyokuwepo tangu mwanzo, lakini bado Afrika haijaweza kutengeneza magari yake yenyewe.

2. Afrika inaweza kufanya kile ilichokifanya katika kuingia kwenye zama za Kidijitali, mtindo wa kuruka kama chura (leapfrog). Kwa mfano nchini Kenya watu hawakuwa na huduma za simu za mezani miaka ya 1990’s kurudi nyuma, hali kadhalika ilikuwa hivyo nchini Tanzania pamoja na nchi nyingi za kusini mwa jangwa la Sahara katika ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani.

Lakini baada ya mwaka 2000 watu wengi katika eneo hilo wameweza kumiliki simu za mkononi hata kama hawakuwahi kumiliki simu za mezani. Simu za mkononi zimekuja na teknolojia kubwa zaidi baada ya kuunganishwa na huduma za kifedha kama MPESA, huduma za internet, GPS na ramani, huduma za kiafya pamoja na biashara za kielektroniki ecommerce.

Mazingira ya Uchumi jumuishi (social economy) yanafanya iwe rahisi kukaribisha zama za Mapinduzi ya 4 ya viwanda. Watu wengi duniani hawapendi kusoma vitabu, hivyo sasa tunaweza kuziachia mashine kufanya kazi mbalimbali badala yetu. Kama Blockchain inatazamwa kwenda kuangamiza kabisa changamoto ya rushwa, Teknolojia ya 3D-Printing itafanya hata nyumba zetu kuwa viwanda vidogo katika kubuni bidhaa mbalimbali.

Taarifa zote zilizo kwenye mashirika ya Serikali na binafsi ikijumusha taasisi za dini zinaweza kuvunwa kwa ajili ya kupata takwimu mbadala katika chunguzi mbalimbali. Hii inatazamwa kuwa njia mbadala kuyafikia mapinduzi ya viwanda ya 4. Unahitaji kuLeapfrog biashara yako (kuepuka gharama kubwa za matangazo)? Tunalo suluhisho, wasiliana nasi mara moja tukupatie.

3. Vile vile, Afrika inaweza kukuza thamani ya uzalishaji na ubunifu wake ili kuwa mshindani halisi duniani katika kutengeneza na kusambaza bidhaa na huduma za kiteknolojia, kama inavyofanyika mahali kwingine duniani.

Japan imeweza kufanya hivyo katika sekta ya magari na India inafanya vizuri katika sekta ya Famasia na Programu za Kompyuta. Sasa kwanini Tanzania isiwe kinara katika Sayansi ya Data(Data Science) duniani. (maana mbongo mpe picha tuu, vingine utaona atakapovipata😂. Natania.) Sekta hizi za teknolojia zinataka matumizi ya akili zaidi, sio kama viwanda vya saruji na chuma ambavyo vinahitaji mtaji mkubwa wa kifedha.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi kuyapokea Mapinduzi haya ya 4 ya Viwanda katika eneo lako la biashara? Pitia makala hizi ili kupata taarifa zaidi:

  1. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BANDO LAKO NI MTAJI
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  4. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mapinduzi ya 4 viwanda katika biashara duniani
Unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA KATIKA BIASHARA YAKO?

Bila kujali unafanya biashara ya aina gani, teknolojia ya intaneti na kompyuta imekuwa kwa kiwango kikubwa sana duniani hivyo kupelekea kuathiri mfumo mzima wa uendeshaji biashara duniani. Mwaka 2011 mwandishi Marc Andreessen alinukuliwa akisema, “Softwares are eating the world” akiwa na maana ugunduzi wa programu za kompyuta unarahisisha shughuli nyingi za kibinadamu kufanyika kwa haraka, kwa unafuu na kwa ufanisi zaidi kila siku zinavyozidi kwenda mbele. Sasa unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Leo tufahamu kwa undani.

Kufikia Octoba, mwaka 2018 tovuti ya Lifehacks (lifehacks.io) iliripoti kwamba jumla ya tovuti bilioni 1.9 zilithibitika uwepo wake kwenye intaneti pamoja na kuripotiwa kuwepo kwa machapisho (posts) zaidi ya milioni tano (5) ya blogu mbali mbali duniani kila siku. Tafiti hii ya kimtandao inakupa sababu mbali mbali za kukuwezesha kufanya biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta. Fuatana nasi.,

1. KUWA NA MPANGO WA BIASHARA ILI KUJUA KIUNDANI UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA:

Ukiwa na ndoto za kufanya biashara yako iwe na mafanikio maradufu, huna budi kuwa na mpango madhubuti wa kibiashara ambao utaainisha aina ya biashara unayoifanya, Jina la biashara linaloendana na aina ya bidhaa/huduma unayotoa, maudhui bora ya tovuti, soko unalolilenga na mbinu stahiki za kulikamata soko la kudumu.

Unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

MPANGO WA BIASHARA

2. TAFUTA NA CHAGUA JINA ZURI LA TOVUTI YA BIASHARA YAKO MTANDAONI:

Unapofikiria kuanzisha biashara, fikiria soko kwanza kabla ya aina ya biashara unayoitaka. Yaani tizama kwenye jamii, changamoto zilizopo ambazo hazijatatuliwa au hazionekani kama ni changamoto sana kwa muda huo, halafu tafuta suluhisho la changamoto hizo. Suluhisho hilo liendane na Jina zuri la kuwasilisha kile unachotaka kutatua kwenye jamii.

Uza suluhisho na si bidhaa kama bidhaa. Ukishapata Jina zuri, tengeneza tovuti yako au tafuta wataalamu waliobobea kwenye ujenzi na uendelezaji wa tovuti bora za kibiashara. KUMBUKA Tovuti sio Bidhaa bali ni Jukwaa la kufanyia biashara zako kama ilivyo ofisi yako, Fremu au Meza ya kuuzia bidhaa zako kila siku. Tofauti na ofisi, fremu au meza., tovuti ni jukwaa la kimtandao linalokuwezesha kuonyesha bidhaa/huduma zako dunia nzima kiurahisi zaidi mara moja. Kuhusu Umuhimu na faida za tovuti (website) katika biashara yako tayari nimekuwekea makala hizi hapa. Zitakufaa sana katika kuimarisha biashara yako ukizipitia zote.

3. TANGAZA NA WEKA UTARATIBU WA KUFUATILIA BIASHARA YAKO:

Dunia inakadiriwa kuwa na watu zaidi ya bilioni 7 mpaka sasa. Kati ya hao watumiaji wa mitandao ya kompyuta wanakadiriwa kufika bilioni 4 ikiwa ni takwimu zilizowasilishwa na yovuti ya lifehacks. Katika watu zaidi ya bilioni 4 ambao ni watumiaji mubashara wa mitandao ya kompyuta na simu, zaidi ya watu bilioni 2.234 wamegundulika kuwa ni watumiaji wa mtandao wa kijamii wa facebook peke yake.

Mfumo wa kimtandao wa kompyuta uitwao Internet Live Stats (ILS) unatumika kufuatilia watumiaji mubashara wa watumiaji wa Intaneti duniani kote kila siku. Hii ina maana kwamba zaidi ya nusu ya jumla ya watumiaji wote wa mitandao ya kompyuta na simu duniani wanapatikana facebook. Vilevile asilimia thelathini (30%) ya jumla ya idadi nzima ya watu wanaoishi duniani ni watumiaji wa facebook.

Kwa kusema hivyo, tayari tumekuwekea makala maalum itakueleza kwanini ni muhimu uitangaze biashara yako kila siku. Tafadhali ipitie makala hio mpaka mwisho kupitia link hii hapa yenye kichwa KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO.

unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Hivyo kwa kuutumia vyema mtandao wa facebook peke yake kibiashara unajiweka kwenye nafasi ya kuwafikia zaidi ya watu bilioni 2 ambao wanaweza kuwa wateja wazuri katika biashara unayoifanya. Vile vile watu zaidi ya bilioni 1 wamefahamika kuwa ni watumiaji wa mtandao unaoshika kasi wa Instagram.

Zaidi ya hayo pia kama mfanyabiashara mwenye kiu ya mafanikio una wajibu wa kufuatilia maendeleo ya biashara/kampuni/taasisi yako katika muktadha wa kuichumi na masoko. Biashara inabidi iwe inakua katika viwango vinavyohitajika kulingana na kasi ya soko la dunia.

Hivyo baada ya kujiuliza unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?, sasa unao uwezo wa kufuatilia biashara yako kwa kutumia takwimu sahihi kama ongezeko la wateja ndani ya muda fulani (wiki, mwezi au mwaka), ongezeko la faida, taarifa za mapato na matumizi na zaidi, usalama wa taarifa zako kibiashara.

Pia katika ufuatiliaji unaweza kuongeza njia kusambaza taarifa kuhusu biashara yako. Moja ya njia hizo ni Search Engine Optimization ambayo ni huduma inayotolewa na makampuni ya programu za kompyuta na mitandao. Huduma hii hukupatia nafasi ya kusambaza links za tovuti au mifumo yako ya kompyuta ambapo mtu yeyote anapotafuta bidhaa au huduma zako katika mtandao, basi inakuwa rahisi zaidi kukupata kwa kuandika maneno yanayohusu huduma hio unayotoa.

4. JIBU KWA WAKATI NA KWA UWELEDI ILI UNAPOJIULIZA UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA MTANDAONI UPATE ULE MVUTO WA KIBIASHARA

Unapokuwa mfanyabiashara au mhusika katika kampuni/taasisi fulani maana yake upo hapo kwa ajili ya wateja wako, hivyo unapaswa kutoa majibu na ufafanuzi wowote unaofika kwako kutokea kwa wateja wako. Aina ya majibu au ufafanuzi wako huchangia kwa kiasi kikubwa kupata wateja wapya kila siku au kupoteza wateja kila siku. Waswahili wanasema “Kauli Njema ni Silaha.” Hivyo kwenye kauli zako za kuhudumu ni lazima uweke uweledi wa hali ya juu ili kumvutia na kumridhisha mteja na bidhaa/huduma zako.

Kulingana na elimu ya wanasaikolojia mtu yeyote hupenda kujibiwa mara moja pale anapokuwa na shauku ya kujua jambo fulani. Hivyo unaposhindwa kujibu au kutoa ufafanuzi wa jambo fulani kuhusu bidhaa/huduma kwa wakati, unajiweka kwenye nafasi mbaya ya kupoteza wateja wengi kila siku.

5. BADILIKA KULINGANA NA SOKO LINAVYOKUHITAJI KUBADILIKA:

Dhana ya Biashara na masoko inafanana na dhana ya muziki na mtu anayeucheza muziki huo. Yaani unapaswa kuendana na mdundo wa muziki pale unapokuhitaji. Hali kadhalika unapokuwa katika ulimwengu wa biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta soko lako linakuwa ni kuwafikia watu bilioni 7 waliopo duniani.

unawezaje kupata wateja mtandaoni unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Na bahati ni kwamba duniani wapo watu/kampuni/taasisi nyingi ambazo zinafanya biashara unayoifanya wewe, hivyo unapaswa kuwa mbunifu kila siku, unapaswa kuongeza ubora wa bidhaa na huduma, kuongeza mtandao wa washirika wako duniani, bidhaa/huduma mpya na mambo mengi ambayo hujitokeza kila siku kulingana na uhitaji wa wateja. Hapa inakubidi uwe mwanafunzi mwenye uwezo wa kunyumbulika wakati wowote kwa ajili ya wateja wako.

Kwanini ufanye hivyo? Majibu zaidi yanapatikana kupitia makala hizi hapa:

Zaidi, tambua Tovuti ya kwanza kabisa kuundwa duniani bado ipo hewani (info.cern.ch). Tovuti hii ilitengezwa kwa lugha ya kuundia mifumo ya kimtandao ya HTML na inaonyesha mistari michache tuu. Lakini sasa mambo ni tofauti sana katika uwanda wa usanifu na uendelezaji wa programu za kompyuta na tovuti. Kama mwandishi Marc Andreessen alivyonukuliwa mwaka 2011 akisema programu za kopyuta zinaila dunia.

Je unajiandaa vipi kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Tafadhali toa maoni yako kupitia comments hapo chini..