FAIDA ZA KUTUMIA GOOGLE KAMA JUKWAA LA BIASHARA YAKO
Je, unaamini kwamba matumizi sahihi ya huduma za internet na mitandao ya kijamii yana uwezo wa kukurahisishia huduma/bidhaa zako zikapatikana kirahisi na wateja wako wakiwa popote duniani? Leo nataka nikupe stori kuhusu Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.
Tizama hapa, Siku moja asubuhi kabisa ya mwezi April mwaka huu 2022 nikiwa natoka home naelekea ofisini nikapigiwa simu, kutizama ni namba ngeni, nikatafuta utulivu kisha nikapokea;
Mimi: Hello, Habari za asubuhi!
Jamaa: Salama Faustine, I hope uko poa, Bwana mimi ni fulani (jina kapuni) nimekupigia kwa sababu nahitaji website na ningependa ifanywe na kijana mzawa. Nafanya kazi katika shirika (jina kapuni) ambalo ni la kimataifa. Nilikua napitia google pale nikaona kampuni yenu ya Rednet Technologies na nikaona pia kumbe mnajishughulisha na haya mambo. Itawezekana si ndio?
Mimi: Bila shaka hilo linawezekana kabisa, unahitaji lini hii kazi yako iwe imekwisha?
Jamaa: Well, ndani ya wiki 3 ningependa iwe imekwisha, sasa nitampatia namba yako mwenzangu yupo pale ofisini kwetu, yeye sasa atakupa maelezo ya kina. Lakini naomba kujua bei itakuwaje hapo (huku anacheka kwa ufupi)
Mimi: Gharama nitataja nikishajua requirements kaka, wala usiwe na shaka.
Baada ya kuwasiliana na huyo mwenzake akanirudia…
Jamaa: Faustine, naona mmeshaelewana, Sasa the reason tumekuja kwako ni kwasababu kuna mtu tulimpaga kazi ya kutengeneza hii website yetu, lakini hajawahi kutupa ushirikiano, kazi hajamaliza, changes hataki kufanya na tukimpigia simu harespond ndani ya muda, yani ana kiburi sana yule jamaa, kusema ukweli TUMEMCHOKA.
Mimi: (Kiukweli nilijiskia vibaya sana, ndugu zangu ule msemo wa “Mteja ni Mfalme” una maana kubwa sana hapa. Nikamwambia) Kaka, pole sana, utakavyokuwa unafanya kazi kwetu nakuahidi hio kadhia hutakutana nayo.
Jamaa: Kweli? Ok, turudi kwenye bei sasa, utatuchaji kiasi gani?
Mimi: Kwa nature ya Organization yenu hapo mpaka kazi inakamilika itacost 850,000/- tu.
Jamaa: Faustine, mbona bei ipo juu sana, tutaweza kufanya kazi kweli?
Mimi: Kaka, bei iko fair sana hio ukizingatia tutawatengenezea pia business emails BURE na kuwafanyia maintenance BURE kwa mwaka mzima. Anytime hapo mkitaka kufanya changes, tutazifanya BURE kabisa. Hapo unasemaje?
Jamaa: Hapo sio mbaya, walau naona dalili hautakuwa kama jamaa wa mwanzo. Ila bei bado hujashusha..
Mimi: Kaka, lipia 400k leo, baadae utalipa 250k, then finally tutakapomaliza kazi, utalipia 200k ambayo itakuwa imebaki. Hapo je?
Jamaa: Ok, Nataka na hio website pia iwe inapatikana mtu akisearch Google, ili wateja watupate kama sisi tulivyokupata wewe.
Mimi: Ahaa, hio sasa ni huduma nyingine, inaitwa Search Engine Optimization (SEO). Ndo inaiwezesha website kupatikana google.
Jamaa: Na hio utatuchaji au bei yake ndio inakuja na ya website direct?
Mimi: Hio gharama yake ni tofauti kaka.
Jamaa: Ambayo ni ngapi? Usinilalie bwana ndugu yangu.
Mimi: Hio kwa sababu ni kazi ya muendelezo, utakuwa unalipia kila mwezi, ambapo gharama yake ni 100,000/- tu.
Jamaa: sema Faustine mna bei nyie. Ehe niambie, kwenye hio laki 1 mtakuwa mnafanya nini na nini?
Mimi: Hapo tutakuwa tunakuandikia makala (blog posts) mbili kwa mwezi ambazo zitahusu shughuli mnazofanya, tutaweka picha, pamoja na kuzioptimize ili iwe rahisi kupatikana google mtu akiwa anatafuta taarifa zinazowahusu.
Jamaa: Faustine, hapo umeniweza. Basi wacha tuandae contract, halafu next week tutakuita ili tusign, kazi ianze mara moja. Ila usiniangushe bwana.
Mimi: Kaka wala usiwaze, tufanye kazi.
Basi Bwana baada ya simu hio ndio uhusiano ukajengwa na kazi ikaanza kama hivyo.
Na baada ya kazi hio kuisha, jamaa yetu aliweza kutuunganisha kwa watu wengine watano (5) ambao walitamani kupata huduma kama ambayo aliipata kutoka kwetu. Na hatimaye wamekuwa wateja wetu wa kudumu. Unadhani hao walivutiwa na nini? Fuatilia makala hii hapa kufahamu siri za utoaji huduma bora kwa wateja.
Unachoweza kujifunza ili uweze kuzipata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.
Katika mazingira ya kazi, hasa huku mtandaoni ambapo mara nyingi tunakutana na watu tusiowafahamu (strangers) ni muhimu sana kuzingatia haya yafuatayo;
1. KAULI NJEMA
2. UAMINIFU
3. KUMJALI MTEJA na MAUMIVU YAKE (Mara kwa mara muulize kama anaridhika na huduma anazopata kutoka kwako na nini unaweza kufanya ili kazi yake ifanyike kwa ubora anaotarajia).
Kauli Njema zitakufunulia fursa nyingi na kukuletea wateja wengi sana huku mtandaoni, acha tabia ya kutukana, kudhalilisha au/na kudharau watu. Kumbuka teknolojia haisahau.
Uaminifu utajenga uhusiano mzuri na wa kudumu na mteja wako.
Kumjali mteja kutafanya azidi kukupa kazi nyingi zaidi mbeleni, na hata kukuunganisha kwa watu wake wengine anaowafahamu.
Siri ya kufanya kazi vizuri na mteja ipo kwenye hayo mambo matatu. Ukiyazingatia, hakika huwezi kufeli. Zaidi kama unahisi bado hujajua namna unaweza kushawishi mteja kwenye biashara yako fuatana na makala hii hapa tumekuandalia.
HABARI NJEMA KUELEKEA MSIMU WA SIKUKUU
Sasa kuelekea mwisho wa Mwaka tunakupa ZAWADI ya kuifikisha biashara yako mtandaoni na kukusanya wateja kutoka kila pembe ya nchi. Fungua website leo kwa 500,000/- tu (badala ya 850,000/-) upate na huduma ya SEO BURE (badala ya 100,000/- kwa mwezi) maintenance BURE mwaka mzima pamoja na Ushauri BURE kabisa. Hata hivyo, ZAWADI hii haitamfikia kila mtu. Zawadi hii ni kwa watu 10 tu wa mwanzo, na itadumu mpaka tar 10 December. Baada ya hapo tunakwenda likizo ya Christmas.. So kama unahitaji ZAWADI hii WAHI nafasi mapema ili pia uzipate Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.

Baada ya OFA hii ukihitaji website ni 850,000/-, huduma ya SEO ni 100,000/- kwa mwezi na pia tutafungua group la Whatsapp kwa yeyote atakayehitaji ushauri au atayehitaji kuuliza jambo lolote kuhusu Website, SEO, Social Media Marketing, Digital Marketing na Tech kwa ujumla wake. Kuingia kwenye group hilo itakugharimu 5,000/- tu kwa mwezi.
So ukiliona Tangazo hili, mtaarifu na mwenzako ambaye unahisi atahitaji kunufaika na ZAWADI hii.
Wewe kama unafanya biashara, basi kama unataka kufanya vizuri sokoni, hakikisha unajenga URAFIKI na wateja wako. Hii ni kwa sababu ni rahisi sana MTEJA kuwa RAFIKI yako kama utatengeneza UHUSIANO mzuri kati yenu. Hii ndio SIRI ambayo hakuna mtu atakwambia kirahisi.
Kufanya biashara mtandaoni ni Uwekezaji muhimu sana, na kwa maendeleo yaliyopo kwa sasa duniani, imekuwa ni rahisi mno kutumia huduma za Internet katika kuwafikia wateja popote walipo duniani.
Kuna mtu aliwahi kuniuliza, “Sasa nawezaje kutumia Internet kufanya biashara yangu?”
Jibu: Unaweza fanya haya yafuatayo ili uweze kupata Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako.:
1. Tumia Website na mitandao ya kijamii kutoa elimu kuhusu bidhaa/huduma zako.
2. Tumia SEO ili kurahisisha maudhui yako yanapatikana kirahisi katika Google.
3. Fanya matangazo (Paid Ads/Sponsored Ads) ili kuwafikia wateja wengi kwa haraka.
4. Jifunze kuuza katika Maandishi (Copywriting). Jaribu kadiri unavyoweza.
5. Tumia WhatsApp yako vizuri kibiashara (Status, Broadcast, Groups n.k).
Ukiona haya yanakuwa magumu kwasababu upo busy au vinginevyo, usikubali sasa biashara yako ife/ishindwe kufanya vizuri mtandaoni.
Tafuta mtaalamu wa kufanya biashara mtandaoni, mpe targets zako, kubaliana nae katika malipo, kisha mpe kazi ili biashara yako izidi kupaa mtandaoni kwa sababu ni muhimu sana ukazipata hizi Faida za kutumia Google kama Jukwaa la biashara yako. Sio lazima kila kitu ukifanye wewe mwenyewe kwa sababu hakuna ajuaje kila kitu.
Ni mategemeo yangu umepata kitu kipya leo. Kumbuka ZAWADI yetu ya kufunga Mwaka inakwisha tarehe 10 December, halafu hii ni maalum kwa watu 10 tu watakaowahi kujinyakulia website zao.
Tutumie ujumbe sasa hivi au tuchek kupitia mawasiliano haya;
Call/WhatsApp: +255765834754
Email: info@rednet.co.tz