Tag: elimu ya biashara

FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA

Watu wengi hufikiri kwamba Kuwekeza ni swala la kupata Utajiri ndani ya muda mfupi, Kustaafu mapema au kupata gawio (interest) kubwa kila baada ya muda fulani kwa haraka. Ukweli ni kwamba Kuwekeza sio chanzo cha kukufanya ushinde unakula upepo wa bahari, kutumia pesa hovyo(kula bata) au kusafiri vile unataka. Usikariri maisha, leo makinika mpaka mwisho wa makala hii ili uweze ku fahamu siri ya kufanikiwa katika kuwekeza.

Watu wanafanya kazi sana ili kupata pesa, na kazi zaidi kutunza pesa. Lakini wachache sana ndio hugundua njia bora zaidi ya kutengeneza na kuzungusha pesa katika biashara zao. Leo hii nitakujuza mambo 10 muhimu ya kuzingatia katika UWEKEZAJI (INVESTING) kwa mafanikio ya biashara yako hio hio unayoifanya/unayotaka kuifanya.

Kuwekeza zaidi katika biashara dhumuni lake ni kuhakikisha biashara yako ina uwezo wa kujiendesha yenyewe hata bila ya wewe kuwepo hapo ofisini kila siku. Sasa ili kuweza kufikia lengo hilo inatakiwa ile energy ambayo mjasiriamali anakuwa nayo wakati anaanza uwekezaji wake wa kwanza ndio hio hio anatakiwa kuwa nayo hata pale anapofanikiwa. Kama misuli inayohitaji mazoezi ili iwe mikubwa na yenye nguvu, the same kwenye biashara yako. Biashara inahitaji muendelezo wa uwekezaji ili kuleta matokeo yenye tija. Vitu kama Mtaji, Masoko, rasilimali watu, connection, wafanyakazi n.k, vinahitaji kukua sana. Hii ni muhimu sana katika ku fahamu siri za kufanikiwa katika kuwekeza popote pale duniani.

Sasa kifupi ni kwamba kuna aina nyingi sana za Uwekezaji duniani (Stocks, Bonds, Real Estate, Commodities n.k). Lakini leo tujadili kuhusu Uwekezaji kwenye Biashara Unayoifanya/Unayowaza kuifanya (kuuza viatu, nguo, chakula, furnitures n.k) Hapa nitakuwa nimekupa kitu unachohitaji sana, si ndio?

Kama umeshawahi kujaribu basi utakubaliana namimi kwamba Kutunza Fedha kwenye kibubu, chini ya godoro, benki, mpesa, tigopesa ni ngumu kweli kweli. Halafu kibaya zaidi, pesa sio kiumbe hai, usitegemee ukiichimbia itazaliana.

Hizi hapa ni njia Bora za kuwekeza na kuzungusha pesa yako vizuri ili uweze fahamu siri ya kufanikiwa katika kuwekeza:

1. FIKIRIA MBALI:

Unapotaka kuwekeza kwenye biashara yako, waza hivi; mwaka 2030 au 2040 nitakuwa katika hatua gani kibiashara? nataka niwafikie watu/wateja/maeneo mangapi mpaka mwaka 2030/2040? Ukiwa na mipango ya mbali katika biashara yako unapata energy ya kusimamia vizuri na kufanikiwa. Kila mafanikio huanzia kwenye fikra na mipango thabiti.

2. ANZA KUWEKEZA KILE ULICHONACHO:

Watu wengi hasa vijana wanapenda kufanya biashara lakini wanalalamika changamoto ni Mtaji. Fahamu, biashara ni kama ile siku mpenzi wako anapokupa taarifa za mimba. Niambie hapa kama ulianza kulea mimba kwa milioni 1 kwa mwezi ule wa kwanza. Utagundua ni ngumu. Hali kadhalika biashara yako inahitaji kulishwa kidogo kidogo kwanzia ingali ndogo.

Unailisha biashara kwa vitu kama Maarifa, aina bora za bidhaa/huduma zinazotakiwa, wapi pa kuzipata, aina za wateja, taarifa sahihi nk. Pesa ni kitendea kazi muhimu lakini tambua pesa ni sehemu ya mtaji tu.

3. WEKEZA PALE UNAPOPAWEZA

“Baba yako hawezi kukufanya uwe tajiri, wala mama yako, wala rafiki yako, wala mwalimu, wala serikali, badala yake ni wewe mwenyewe wa kubadili maisha yako ukianza na namna unavyofikiria (mindset)” Maneno sumu ya jamaa yangu SirJeff Dennis. Hapa nataka kuongelea Uwezo wako specifically. Wewe unaweza kufanya nini katika kiwango kikubwa? Na unaweza vipi kutumia huo uwezo kwa manufaa? Jitambue wewe kwanza.

4. JIFUNZE NA FANYA UCHUNGUZI

Hili swala sio la kufanya mwanzoni wakati unaanza biashara halafu unakuja kuacha mbeleni, Hapana. Kama ilivyo kuwekeza hakuna mwisho kwenye biashara yako, hakikisha pia Unaendelea kujifunza mbinu mpya na kufanya Uchunguzi kuhusu biashara mbalimbali mara zote kabla hujawekeza. Ishi nayo hii kwa sababu Elimu haina mwisho.

5. TENGENEZA NA FANYA KAZI KWENYE TIMU

Kuna mtu mmoja aliwahi kusema “Kama huwezi kutengeneza pesa ukiwa umelala, huwezi kuwa tajiri”, Ni kweli kabisa. Mimi nakuongezea, kama kwenye Uwekezaji wako, wewe ndo kila kitu, hio biashara haiwezi/ni ngumu sana kukua. Gawa majukumu, sio kila kitu unataka kufanya wewe, uzalishaji wewe, marketing wewe, customer care wewe, presentations wewe. Utafeli, hakikisha mfumo wa biashara yako unaweza jiendesha wenyewe hata usipokuwepo.

 fahamu siri za kufanikiwa katika kuwekeza.

fanya kazi kwenye timu

6. KUWA NA MSIMAMO (CONSISTENCE AND RESSILIENCE)

Biashara yako ili iweze kukua na kufanikiwa dhidi ya ushindani wa masoko, dhoruba za kiuchumi, teknolojia nk, Unapaswa kuwa na msimamo/consistency. Wazungu wanasema “Practice makes perfect”. Hutakiwi kukata tamaa, licha ya changamoto ambazo unaweza kukutana nazo kila siku, hakikisha unaendelea kuzalisha/kuhudumu, tafuta wateja wengi zaidi, jisahihishe, jitangaze, pambana. Uwekezaji unakuhitaji uwe na ngozi ngumu kwelikweli kwa sababu katika kuwekeza kuna nyakati za kuanguka na kukata tamaa, sasa hakikisha unao uweza wa kusimama na kuendelea kupambana.

7. KUWA MWOGA PALE WENGI WANAPOKUWA WALAFI

Ulimwengo wa Uwekezaji katika biashara unaendeshwa kiakili na kijasusi sana. Usiwe bendera kufuata upepo, Usiwe mtu wa kufuata mkumbo. Ni afadhali kuwa mwoga na kuishi miaka mingi, kuliko kuingia vitani bila maandalizi, hutachukua raundi. Tulia, changa karata zako vizuri na kwa mipango sahihi.

8. KUWA AGGRESSIVE PALE WENGI WANAPOKUWA WAOGA

Sehemu pazuri zaidi kuwekeza ni pale mahali kuna changamoto nyingi. Uwekezaji wako unapotatua changamoto hapo ndo pakutoboa kabisa. Kuna mahali hamna maji wapelekee hapo, hamna chakula, fungua mgahawa. Pambana na changamoto za wateja wako. Wasikilize wateja wako wanahitaji nini kila wakati kwa sababu kwenye maumivu ya wateja wako ndipo mafanikio ya uwekezaji wako yalipo. Shikilia hapo.

9. PUNGUZA MATUMIZI YASIYO NA ULAZIMA

Fahamu kuwa katika biashara yako kila shilingi ina mchango muhimu katika Uwekezaji endelevu. So hakikisha unazingatia matumizi yale muhimu zaidi katika uwekezaji. Hili zoezi ni gumu lakini linawezekana ukiweka Nia ya Kukuza Biashara yako.

10. TAWANYA UWEKEZAJI/DIVERSIFY

Ili kuhakikisha biashara yako inakuwa na misuli ya kiushindani, lazima Utawanye uwekezaji wako. Unauza nguo kwa sasa, ongeza na viatu, soksi, vipodozi na jitahidi ufungue matawi mikoani. Kama unauza mbao, ongeza karakana za fenicha maeneo mbalimbali, TANUKA.

fahamu siri za kufanikiwa katika kuwekeza.

11. TUMIA VIZURI TEKNOLOJIA

Katika eneo muhimu la kuzingatia katika kufanya uwekezaji wa kibiashara, basi hakikisha unatumia vyema teknolojia katika maana ya kutumia kwa usahihi Mitandao ya kijamii, tovuti bora ya biashara yako, software za kutunza hesabu nakadhalika. Eneo la teknolojia ni pana, hivyo nimekuwekea mambo muhimu ya kuzingatia katika makala hizi hapa chini:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  4. MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA
  5. MBINU ZA KUWEZA KULIFIKIA SOKO LA MTANDAONI

NOTE: Uwekezaji katika biashara ni jambo endelevu, kama mtoto mdogo, “kadiri ya umleavyo ndivyo akuavyo.” wamesema wahenga. Ukizingatia mambo haya bila shaka bishara yako itakuwa na afya tele. Tafadhali sambaza makala haya kwa yeyote aliye karibu yako na usisite kucoment hapa chini.

Je umeweza fahamu siri ya kufanikiwa katika kuwekeza katika biashara yako kupitia makala hii ya leo? Niambie katika comments hapo chini.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

siri ya kufanikiwa katika kuwekeza.

KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?

Imeibuka kuwa issue muhimu sana ya kuzingatia katika zama hizi za kiteknolojia ambapo kumekuwepo na wimbi la mashambulizi ya kimtandao kwa watumiaji duniani kote. Kama unatumia Android, iOS, Windows7, 8, 10, Ubuntu na OS zingine unazozijua basi fahamu tayari upo katika hatari ya kushambuliwa na wadukuzi wenye nia ovu na uhalifu katika kuiba taarifa zako, mali na hadhi yako katika jamii inayokuzunguka. Sasa utafanyaje ili ujikinge na hatari za mashambulizi hayo? Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako? Fuatana nami leo mpaka mwisho nitakufahamisha.

Mwaka 1988, Robert Morris akiwa nguli wa mitandao alitengeneza shambulio la kimtandao lilioitwa CHRISTMASS TREE WORM katika internet ambapo mifumo zaidi ya 2000 iliharibika na computer zaidi ya 6000 ziliathirika kwa siku moja tu nchini Marekani. Kwa kuwa alikua ni afisa wa Shirika la NSA (National Security Agency) alikamatwa na kupigwa faini ya 10,000$.

Japokuwa faini ilionekana ndogo kwake lakini dunia ilipata funzo muhimu sana kuhusu Usalama wa Data za watumiaji wa internet wawappo mtandaoni. Hata hivyo, katika muongo wa 1980’s mpaka 1990’s, wadukuzi wa mitandao Hawakuwa tishio sana duniani moja ya sababu ikitajwa ni kutokuwa na matumizi makubwa ya internet na kuwa na watumiaji wachache.

Lakini mambo yalikuja kubadilika mwishoni mwa miaka ya 1990’s na mwanzoni mwa 2000’s ambapo Udukuzi ulianza kutumika kama biashara na kuwa silaha ya kimbinu Katika idara mbalimbali za kiserikali, kibiashara au kibinafsi ambapo ujasusi wa taarifa umechochea kwa kiasi kikubwa katika kutafuta, kuchakata na kutumia taarifu mbalimbali kwa manufaa ya kiuchumi au kibinafsi..

Wanafanyaje Mpaka kuifikia Computer/kifaa chako? Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

Mashambulizi haya ya kimtandao yalianzia katika matukio ya Uhuni wa mtaani katika kuibiana taarifa, mpaka kufikia Oparesheni za kidunia zinazohusu Mashirika makubwa, majeshi, Idara za kiresikali na Magaidi. Mwaka 2008, Mike Cloppert mchambuzi wa mifumo ya kimtandao aligundua na kubaini mbinu wanazotumia wadukuzi katika kufanya misheni zao ambazo aliziweka katika utaratibu huu.

1. Reconnaissance (Utambuzi, Ufahamu)

2. Weaponization (matumizi ya silaha)

3. Delivery (jinsi ya kufikisha Botnet, virusi kwa victim)

4. Exploitation (uvunaji wa taarifa za muathirika)

5. Installation (jinsi botnet na malwares zinafanya kazi katika kifaa chako)

6. Command and Control

7. Actions (athari za udukuzi katika kifaa chako)

Tuiruke hatua ya kwanza as inaeleweka kirahisi, WEAPONIZATION au matumizi ya Silaha sio lazima mara zote silaha iwe Bunduki na Mabomu. Silaha muhimu inayotumika ni Software za kidukuzi (Malwares, Botnets nk). Kuna kisa kilionekana katika mtandao wa twitter kuhusu “wakala wa simu na mtu mmoja“.

Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

Hizi Malwares zinamfikia victim/target kupitia picha, USB, email, pdf au link iliyobeba Botnets ambazo hudukua taarifa muhimu katika kifaa cha victim (DELIVERY). Shambulizi hili huitwa Phishing. Wadukuzi hupendelea kununua hizi Malware katika masoko yasiyo rasmi mtandaoni (black market). Baada ya Botnet kuingia katika kifaa cha Victim huanza kufanya kazi pasi na idhini au ufahamu wa mtumiaji ambapo huvuna taarifa nakuzituma kwa wadukuzi muda wowote watakaohitaji taarifa hizo automatically(EXPLOITATION AND INSTALLATION). Taarifa hizo zinazoibiwa humuathiri kwa kiasi kikubwa mtumiaji ambaye hana ufahamu wa shambulizi katika kifaa chake, jambo linaloweza kumfanya akapoteza fedha, taarifa muhimu na mali (COMMAND, CONTROL AND ACTIONS). Sasa Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

UFANYEJE SASA ILI USALAMA WA KIMTADAO UWE MUHIMU KWAKO?

Hakikisha kifaa chako kipo salama muda wote. Tumia password bora. Hakikisha password unayotumia inajumuisha mambo yafuatayo: Herufi ndogo, herufi kubwa, namba pamoja na alama za uandishi. Mfano wa Password bora unaweza kuwa (HJas876?2). Somo la Password nimelielezea kwa kirefu kupitia link HIFADHI MBADALA YA NYARAKA. Pia, epuka kushiriki matumizi ya kifaa chako na watu wengine.

Lakini zaidi epuka kutembelea tovuti usizozifahamu ambazo zinaweza kubeba shambulizi. Lakini zaidi Epuka kufungua email kutoka kwa mtu usiyemfahamu au ambaye hujawahi kufanya nae mazungumzo kabisa. Email za wadukuzi zinaweza kuja kama email ya kawaida tu lakini imebeba Malwares ambazo hutajua zimeingia sangapi kwenye kifaa chako Ukihisi kwamba kifaa chako kimeingiliwa na Malwares au Botnets, kwanza Hutakiwi kupanic. Fanya yafuatayo ili kuhakikisha unabaki kuwa salama:

1. Tumia Antivirus Software katika kifaa chako: Hapa sizungumzii zile antivirus za kudownload, Antivirus bora kanunue dukani ikiwa mpya kabisa. Kwa 95% antivirus huzuia mashambulizi yanayokuja katika mfumo wa Spywares and Adwares (Pop ups), virus, Botnets. Ili kuongeza ubora katika utendaji wa Antivirus yako, hakikisha unaiUpdate mara kwa mara kupata latest security protocols katika kifaa chako.

2. Matumizi ya Windows Defender (WD): Kama unatumia computer yenye OS ya windows make sure Windows Defender yako ipo ON in Real Time protection na Automatic Updates zipo ON kama inavyohitajika.

Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

3. Pia hakikisha FIREWALLS zako zipo ON and active: Hizi ni security protocols zinazozuia any software Au App ambayo haitambuliki na Watengenezaji wa Windows OS kama Activators, Softwares from Unrecognized sources n.k Kama Firewalls zako zipo okutaona ukiweka any mentioned Software inaliwa hapo hapo. Kupitia LINUX OS, Iptables firewalls hutumika na zinafanya kazi just like windows

4. Matumizi ya VPN Virtual Private Network (VPN): Ni mwamvuli wa kimtandao unaokuwezesha kutumia huduma za internet bila kufuatiliwa na either Mtoa huduma wako (Network Operator) au mashirika ya kiserikali. VPN inakufanya uwe free kufanya shughuli zako katika usalama zaidi Si watu wote wana uwezo wa kumiliki/kutumia VPN’s, lakini kwa matumizi binafsi na salama zaidi mtandaoni, huna budi kutafuta VPN yako ili kujilinda.

NOTE: Usalama wako na kifaa chako katika huduma za internet mtandaoni unaanza na wewe mwenyewe. Hakikisha kifaa chako ni chako. Umejifunza jambo katika makala haya kuhusu Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako? Tafadhali tujulishe na sambaza kwa mwenzako ili kuhakikisha makala haya yanawafikia watu wengi zaidi.

Kuhusu usalama uwapo mtandaoni nimeshakuwekea makala zingine kupitia links hizi hapa chini:

  1. UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?
  2. YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE KATIKA BIASHARA/KAMPUNI YAKO

THIS IS THE ONLINE BUSINESS MONITORY SYSTEM (BIMOS)

Je, Ungependa kuwa na uwezo wa kuhifadhi na kufuatilia rekodi za biashara yako ukiwa popote duniani? Kwa kutumia Online Business Monitory System (BIMOS) unaweza kuweka rekodi mbalimbali kuhusu biashara yako kama mapato, matumizi, orodha ya wateja, suppliers, nyaraka za kiashara (documents) kama PO’s, orodha mbalimbali na wafanyakazi (cashiers) wako kirahisi sana.

Vilevile mfumo huu wa BIMOS unakuwezesha kupata ripoti sahihi kuhusu mwenendo wa Biashara yako, hivyo kukuwezesha katika kuimarisha biashara yako zaidi na zaidi.

Ungependa kutumia mfumo huu? fungua link ifuatayo kisha weka credentials as;

Username: admin

Passwords: admin123

www.bimos.sil.co.tz

Wasiliana nasi muda huu ili kuimarisha Biashara yako leo:

0765834754 / 0713497275

http://www.rednet.co.tz

 

Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA

Mtandao wa usafiri kwa njia ya nchi kavu barani Africa unajumuisha barabara na reli ambapo kwa wastani umechukua kilomita 6.2 kwa kila eneo la kilomita za mraba 100. Zaidi ya 60% ya mtandao mzima wa barabara haijatengenezwa kwa kiwango cha lami. Zaidi, pungufu ya 40% ya barabara za lami ndizo zilizo kwenye hali nzuri ya kupitika muda wowote. Sasa sekta hii ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika inatoa matumaini gani?

Mtandao wa njia za reli umeundwa kwa njia moja (single-track lines) ambazo huanzia maeneo bandarini kuelekea maeneo mbali mbali ya nchi/bara zikijumuisha viungio vichache tu njiani kuunga njia moja ya reli na nyingine (inter-linkages). Muundo huu wa reli zilizopo barani Afrika uliundwa nyakati za ukoloni na tangu wakati huo, ni marekebisho machache tu yameweza kufanyika ili kuwezesha treni ndefu zaidi zinazotumia dizeli kupita ambapo treni nyingi kati ya hizo hazitumiki tena kwa sasa.

Tukiangazia eneo la bandari, chini ya 50% tu ya matumizi ya bandari hutumika ikiwa ni pungufu ya mahitaji sahihi ya bandari hizo, jambo ambalo huchochewa na ucheleweshwaji wa mizigo na taratibu za forodha. Hali kadhalika, Afrika ndio inaongoza duniani katika ukuaji wa sekta ya viwanja vya ndege haswa kufuatia kuazishwa kwa soko huru lililoanzishwa baada ya makubaliano ya YD (Yamoussoukro Decision) yaliyofanyika mwezi November, 1999. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Afrika AU iliyotolewa mwaka 2014.

USAFIRISHAJI BARANI aFRIKA.
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Sasa changamoto; Je, sekta hii ya Usafirishaji na Miundombinu inaathiri vipi ukuaji wa biashara barani Africa? Na je, matumizi ya Teknolojia yana mchango gani katika kuboresha sekta hii ili kuinua biashara?

Kutokana na hali duni ya miundombinu na huduma za usafirishaji, gharama za kusafiri barani Afrika ni kati ya gharama ghali zaidi duniani, jambo ambalo linadhoofisha ushindani wa kibiashara katika masoko yote, ya ndani ya nchi na yale ya kimataifa.

Ripoti ya Tume inayoshughulikia Uchumi barani Afrika (ECA) imetaja kwamba nchi zisizo na bandari (landlocked countries) gharama za usafiri zinaweza kufikia robo tatu ya thamani ya bidhaa inayosafirishwa. Kwa mfano kusafirisha gari kutoka Japan mpaka Abijdan nchini Ivory Coast hugharimu US $1,500. Lakini kusafirisha gari hilo hilo kutoka kutoka jijini Abidjan hadi Addis Ababa hugharimu US $5,000. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa Teknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi kupitia link hii hapa yenye kichwa MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI. Ukimaliza hapo tuendelee na mada yetu ya leo.

Changamoto za Usafirishaji barani Africa.
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Gharama za usafirishaji zimetajwa kusababishwa na viwango vikubwa vya forodha, tozo za ucheleweshwaji, hasara zitokanazo na ajali pamoja na ukosekanaji wa fursa. Changamoto hizi huchagizwa zaidi na uduni wa miundombinu ya kiuchukuzi pamoja na huduma zinazotokana na nyanja hiyo.

Nayo programu ya maendeleo ya miundombinu barani Afrika (PIDA) katika ripoti yake imeainisha kwamba gharama za kiuchumi zinazosababishwa na changamoto za usafirishaji katika Mtandao wa Miundombinu ya Usafirishaji barani Afrika (ARTIN) zinazidi US $170 bilioni kwa mwaka kufikia mwaka 2014.

Changamoto hizo zimetajwa kusababishwa na;

•Kutokuwa na utendaji wa taratibu za kuwezesha biashara katika majukwaa ya ARTIN (kujumuisha bandari na vituo vya mipakani).

•Sera za nyanja ya usafirishaji ambazo zinapelekea kudhoofika na kuongezeka kwa gharama za usafirshaji kwa njia ya barabara pamoja na viwango duni vya barabara katika nchi nyingi barani Afrika.

• Sera za kiuchumi zinazozuia utendaji mzuri pamoja na utanuzi wa mifumo ya reli.

• Nyanja ya usafiri wa anga na Sera za kiuchumi zinazozuia uanzishwaji wa vituo vya anga vya kikanda, jambo linalotajwa kusababisha kuongezeka kwa gharama za usafiri huo.

Kufuatia changamoto hizo, Je, teknolojia ina mchango gani katika kuimarisha biashara na kupunguza gharama za uendeshaji?

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kuelekea mapinduzi ya nyanja zote za kiuchumi. (Yaani tutaendelea kuwa juu kileleni😁). Mapinduzi katika matumizi ya simu kutoka simu za mezani mpaka simu za rununu (smartphones), huduma za kifedha kielektroniki (fintech), biashara za kielectroniki (ecommerce) na kadhalika vimekuwa sehemu muhimu sana katika kurahisisha utendaji wa kibiashara katika sekta ya miundombinu na usafirishaji.

Benki ya Dunia (WorldBank) inaripoti kwamba ubunifu wa kiteknolojia umewezesha sana muingiliano wa kibiashara kwa kuzingatia ongezeko la watumiaji wa Intaneti huduma za simu. Kipimo cha wiani (density) katika matumizi ya huduma za intaneti kwa kila watu 100 waliopo eneo la Kusini mwa jangwa la Sahara, ni watu 17 tu ndio wameonekana kuwa watumiaji wa intaneti katika mwaka 2015.

website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako?
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika

Utafiti huo unakolezwa wino na shirika la kimataifa linalodhibiti mawasiliano ya simu GSMA ambapo kwenye ripoti yake ya mwaka 2018 limeangazia kwamba, eneo la kusini mwa jangwa la Sahara lilikua na kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu ya 44% kufikia mwishoni mwa mwaka 2017 kukiwa na watumiaji takriban 444 milioni sawa na 9% ya watumiaji wote wa simu duniani. Vile vile katika kipindi cha mwaka 2017-2022 watumiaji wa simu katika eneo hilo wataongezeka katika kiwango cha CAGR cha 4.8% ambayo ni zaidi ya mara mbili ya kiwango cha ongezeko kwa dunia nzima katika kipindi hicho hicho. Pia kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu inatajwa kufikia 50% kufikia mwishoni mwa 2023 na 52% mpaka mwaka 2025.

Kufuatia uchunguzi huo, sekta ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara barani Afrika inatajwa kuongezewa nguvu na maboresho zaidi ili kuendana na kasi hio ya ukuaji katika ICT. Matumizi ya GPS katika usafiri wa taxi yamerahisisha zaidi gharama na muda wa kutoka sehemu moja na nyingine, huku maboresho ya miundombinu kama barabara na viwanja vya ndege yakichagiza kasi ya sekta hio.

Zaidi, mtandao wa huduma za Posta na EMS unajumuisha takriban ofisi 30,000 barani ambazo ni muhimu katika kuwezesha e-commerce trade. Kwa kuliona hilo kampuni kama DHL zimejitosa kuhakikisha teknolojia inabadili huduma za posta kuwa rahisi zaidi.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi na jambo hili?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo kuhusu usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA

UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-commerce BUSINESSES)?

Japokuwa imechelewa, lakini kwa sasa Africa ndio inaongoza mbio katika kufanya mapinduzi ya kidijitali kuliko sehemu yoyote duniani. Namna ya kufanya biashara inazidi kubadilika ikionyesha nia ya dhati kufanya maendeleo ya kiuchumi, miundombinu na maswala ya kijamii. Mwaka 2018 nchi wanachama wa Umoja wa Africa walipiga hatua kubwa katika mfumo wa kufanya biashara na muingiliano wa kiuchumi baada ya kuanzisha Eneo Huru la Kufanyia Biashara barani (Continental Free Trade Area AfCFTA). Eneo hili lililoanzishwa linashirikisha nchi 22 zilizoweka sahihi tayari na utekelezwaji wake ulipangwa kuanza mwaka 2019 (tayari umeshaanza).

Hata hivyo mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuzishirikisha nchi ambazo bado si wanachama wa eneo hili jipya, inatarajiwa eneo hili kufikia soko la watu takribani bilioni 1.2 barani wakiwa na jumla ya pato la ndani la taifa (GDP) la dola za kimarekani trilioni 2.5 kwa pamoja, kwa mwaka. Hii inatarajiwa kuwa ni mapinduzi makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nyanja ya uchumi wa Afrika.

Sasa, swali linakuja; Afrika(wafanyabiashara, makampuni/mashirika na Serikali) imejiandaa vipi na mapinduzi haya ya uchumi wa kidijitali? Na zaidi, watunga sera/sheria wataangalia vipi biashara za kielektroniki (e-commerce) kama mada muhimu katika eneo hilo jipya la kufanya biashara huru barani?

Tume ya kudhibiti uchumi wa Africa ya Umoja wa Mataifa (ECA) ikishirikiana na Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) pamoja na Baraza la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo ya kibiashara (UNCTAD) mwaka huu 2019 imechapisha ripoti yake ikiangazia maendeleo ya Afrika kiujumla katika nyanja za kiuchumi, siasa na kijamii.

URAHISI: Imeonekana kwamba e-commerce inaweza kufanya biashara ya bidhaa na huduma kwa urahisi zaidi ambapo itarahisisha mwenendo mzuri wa biashara kati ya wazalishaji, wafanyabiashra na walaji pamoja na kumbukumbu zao na miamala ya kifedha.

MITANDAO YA KIJAMII: Pia imeonekana kwamba e-commerce inapatikana na kufanyika kirahisi katika mitandao ya kijamii kama facebook na Instagram ambapo ndipo mahali kuna watumiaji wengi zaidi wa Intaneti duniani (zaidi ya watu bilioni 2 kati ya watumiaji bilioni 4 wa intaneti).

KUTOKUWA NA MIPAKA: Mfumo wa uchumi wa Kidijitali kiasili umetengenezwa kuepuka mipaka ya kijiografia katika kufanya biashara na kubadilishana fedha ambapo mabadiliko haya ya kiteknolojia yataongeza umakini zaidi katika mwenendo wa masoko na gharama. Lakini bado wimbi kubwa la watu watakaoshiriki kwenye soko barani wanaonekana wataachwa nyuma kutokana na kutokuingiliana kwa lugha na vita/ghasia za mara kwa mara katika baadhi ya jamii/nchi.

BIASHARA: Kwa mujibu wa UNCTAD mwaka 2016 kwa dunia nzima e-commerce iliweza kupitisha mauzoya takribani dola trilioni 26 ambapo 90% ilikuwa ni Biashara kwa Biashara (B2B e-commerce) na 10% ilikuwa ni Biashara kwa Mlaji (B2C e-commerce). Hata hivyo kupima mwenendo wa e-commerce katika baadhi ya nchi zinazoendelea imekuwa ni changamoto kupata data na takwimu, haswa katika nchi za Afrika.

IMPORTATION: Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kwamba Biashara kati ya nchi na nchi imekua kwa kiasi kikubwa Afrika ambapo zimechagizwa na vituo vichache vya kiteknolojia (Hubs) ambavyo vimerahisisha mno mwenendo wa biashara. Biashara kati y nchi na nchi (Intraregional import) imekuwa zaidi ya mara 3 katika miongo miwili iliyopita kufikia 12%- 14% sawa na dola bilioni 100 ikichagizwa na uwepo wa jumuiya za kiuchumi barani (Subregional Economic Communities REC‘s).

UZOEFU: Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na umri wa Jumuiya hizi za Kimaendeleo barani Afrika ambapo uzoefu huo hutumika kuongeza jitihada katika kuboresha namna ya ufanyaji biashara kuelekea uchumi wa kidijitali kiteknolojia. Uzoefu huo pia hutumika kuunganisha jumuiya moja na nyingine (mf, SADC na COMESAna EAC) ambapo zitazalishwa nafasi nyingi zaidi za kufanya biashara kati ya nchi wanachama na ripoti zinaonyesha 75% ya biashara hizi ndani ya jumuiya barani Afrika zimefanyika mwaka 2017 peke yake na nusu ya biashara hizo zilifanyika katika jumuiya ya SADC.

Chini ya mwavuli wa AfCFTA nchi wanachama zinatarajia kufuta tozo/ushuru kwa 90% ya bidhaa zote zitakazopitishwa na kufanyiwa biashara katika eneo hilo. Hii itaruhusu uwezekano wa kupunguza mlolongo wa kodi au kuongeza idadi na thamani ya bidhaa na huduma zitakazohusishwa. Matokeo yoyote katika punguzo hilo linalotarajiwa katika muktadha wa biashara kidijitali yataleta picha tofauti. Kupunguza mlolongo wa tozo za mipakani baina ya nchi na nchi kutapungua kwa 15% pekee ikitegemea thamani ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi husika. Hii ni kwa mujibu wa Tume inayoshughulikia Uchumi wa Afrika kutoka Umoja wa Mataifa (UNECA) mwaka 2018.

Sasa mwaka 2018 Jumuiya ya COMESA ilibuni mfumo wa kudhibiti eneo huru la kibiashara kidijitali (Digital Free Trade Area DFTA). Mfumo huu umeundwa na mambo yafuatayo;

•E-trade: Hili ni jukwaa mahsusi kwa ajili ya kufanya biashara za kimtandao na kuwezesha malipo ya kielektroniki, mobile apps kwa ajili ya wafanyabiashara walioko katika Jumuiya hio.

•E-logistics: hili ni jukwaa maalum kwa ajili ya kuwezesha biashara ya usafirishaji wa mizigo baina ya nchi wanachama wa jumuiya.

•E-legislation: huu ni mfumo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara rasmi ambao unawawezesha kufanya miamala na malipo kielektoniki.

Mfumo huu uliobuniwa na Jumuiya ya COMESA umelenga kutangaza biashara za wanajumuiya katika nchi wanachama ikijumuisha kupitia majukwaa ya e-commerce. Mfumo huu ulikuwa ni mfanano wa mfumo uliotengenezwa na kuzinduliw na nchi ya Malaysia mwaka 2017 katika muktadha wa kufanya biashara huru ndani ya eneo maalum.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.

Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana, shuka nazo:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-biashara-ya-fedha-za-kidijitali-cryptocurrency-business/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)”
  2. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia;

e-mail: info@rednet.co.tz

tovuti: https://rednet.co.tz

Simu:+255765834754