Tag: ECA

Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA

Mtandao wa usafiri kwa njia ya nchi kavu barani Africa unajumuisha barabara na reli ambapo kwa wastani umechukua kilomita 6.2 kwa kila eneo la kilomita za mraba 100. Zaidi ya 60% ya mtandao mzima wa barabara haijatengenezwa kwa kiwango cha lami. Zaidi, pungufu ya 40% ya barabara za lami ndizo zilizo kwenye hali nzuri ya kupitika muda wowote. Sasa sekta hii ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika inatoa matumaini gani?

Mtandao wa njia za reli umeundwa kwa njia moja (single-track lines) ambazo huanzia maeneo bandarini kuelekea maeneo mbali mbali ya nchi/bara zikijumuisha viungio vichache tu njiani kuunga njia moja ya reli na nyingine (inter-linkages). Muundo huu wa reli zilizopo barani Afrika uliundwa nyakati za ukoloni na tangu wakati huo, ni marekebisho machache tu yameweza kufanyika ili kuwezesha treni ndefu zaidi zinazotumia dizeli kupita ambapo treni nyingi kati ya hizo hazitumiki tena kwa sasa.

Tukiangazia eneo la bandari, chini ya 50% tu ya matumizi ya bandari hutumika ikiwa ni pungufu ya mahitaji sahihi ya bandari hizo, jambo ambalo huchochewa na ucheleweshwaji wa mizigo na taratibu za forodha. Hali kadhalika, Afrika ndio inaongoza duniani katika ukuaji wa sekta ya viwanja vya ndege haswa kufuatia kuazishwa kwa soko huru lililoanzishwa baada ya makubaliano ya YD (Yamoussoukro Decision) yaliyofanyika mwezi November, 1999. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Afrika AU iliyotolewa mwaka 2014.

USAFIRISHAJI BARANI aFRIKA.
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Sasa changamoto; Je, sekta hii ya Usafirishaji na Miundombinu inaathiri vipi ukuaji wa biashara barani Africa? Na je, matumizi ya Teknolojia yana mchango gani katika kuboresha sekta hii ili kuinua biashara?

Kutokana na hali duni ya miundombinu na huduma za usafirishaji, gharama za kusafiri barani Afrika ni kati ya gharama ghali zaidi duniani, jambo ambalo linadhoofisha ushindani wa kibiashara katika masoko yote, ya ndani ya nchi na yale ya kimataifa.

Ripoti ya Tume inayoshughulikia Uchumi barani Afrika (ECA) imetaja kwamba nchi zisizo na bandari (landlocked countries) gharama za usafiri zinaweza kufikia robo tatu ya thamani ya bidhaa inayosafirishwa. Kwa mfano kusafirisha gari kutoka Japan mpaka Abijdan nchini Ivory Coast hugharimu US $1,500. Lakini kusafirisha gari hilo hilo kutoka kutoka jijini Abidjan hadi Addis Ababa hugharimu US $5,000. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa Teknolojia katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi kupitia link hii hapa yenye kichwa MAPINDUZI YA KITEKNOLOJIA KATIKA SEKTA YA USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI. Ukimaliza hapo tuendelee na mada yetu ya leo.

Changamoto za Usafirishaji barani Africa.
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika.

Gharama za usafirishaji zimetajwa kusababishwa na viwango vikubwa vya forodha, tozo za ucheleweshwaji, hasara zitokanazo na ajali pamoja na ukosekanaji wa fursa. Changamoto hizi huchagizwa zaidi na uduni wa miundombinu ya kiuchukuzi pamoja na huduma zinazotokana na nyanja hiyo.

Nayo programu ya maendeleo ya miundombinu barani Afrika (PIDA) katika ripoti yake imeainisha kwamba gharama za kiuchumi zinazosababishwa na changamoto za usafirishaji katika Mtandao wa Miundombinu ya Usafirishaji barani Afrika (ARTIN) zinazidi US $170 bilioni kwa mwaka kufikia mwaka 2014.

Changamoto hizo zimetajwa kusababishwa na;

•Kutokuwa na utendaji wa taratibu za kuwezesha biashara katika majukwaa ya ARTIN (kujumuisha bandari na vituo vya mipakani).

•Sera za nyanja ya usafirishaji ambazo zinapelekea kudhoofika na kuongezeka kwa gharama za usafirshaji kwa njia ya barabara pamoja na viwango duni vya barabara katika nchi nyingi barani Afrika.

• Sera za kiuchumi zinazozuia utendaji mzuri pamoja na utanuzi wa mifumo ya reli.

• Nyanja ya usafiri wa anga na Sera za kiuchumi zinazozuia uanzishwaji wa vituo vya anga vya kikanda, jambo linalotajwa kusababisha kuongezeka kwa gharama za usafiri huo.

Kufuatia changamoto hizo, Je, teknolojia ina mchango gani katika kuimarisha biashara na kupunguza gharama za uendeshaji?

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kuelekea mapinduzi ya nyanja zote za kiuchumi. (Yaani tutaendelea kuwa juu kileleni😁). Mapinduzi katika matumizi ya simu kutoka simu za mezani mpaka simu za rununu (smartphones), huduma za kifedha kielektroniki (fintech), biashara za kielectroniki (ecommerce) na kadhalika vimekuwa sehemu muhimu sana katika kurahisisha utendaji wa kibiashara katika sekta ya miundombinu na usafirishaji.

Benki ya Dunia (WorldBank) inaripoti kwamba ubunifu wa kiteknolojia umewezesha sana muingiliano wa kibiashara kwa kuzingatia ongezeko la watumiaji wa Intaneti huduma za simu. Kipimo cha wiani (density) katika matumizi ya huduma za intaneti kwa kila watu 100 waliopo eneo la Kusini mwa jangwa la Sahara, ni watu 17 tu ndio wameonekana kuwa watumiaji wa intaneti katika mwaka 2015.

website inasaidia vipi kuimarisha biashara yako?
Usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika

Utafiti huo unakolezwa wino na shirika la kimataifa linalodhibiti mawasiliano ya simu GSMA ambapo kwenye ripoti yake ya mwaka 2018 limeangazia kwamba, eneo la kusini mwa jangwa la Sahara lilikua na kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu ya 44% kufikia mwishoni mwa mwaka 2017 kukiwa na watumiaji takriban 444 milioni sawa na 9% ya watumiaji wote wa simu duniani. Vile vile katika kipindi cha mwaka 2017-2022 watumiaji wa simu katika eneo hilo wataongezeka katika kiwango cha CAGR cha 4.8% ambayo ni zaidi ya mara mbili ya kiwango cha ongezeko kwa dunia nzima katika kipindi hicho hicho. Pia kasi ya kupenya kwa matumizi ya simu inatajwa kufikia 50% kufikia mwishoni mwa 2023 na 52% mpaka mwaka 2025.

Kufuatia uchunguzi huo, sekta ya usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara barani Afrika inatajwa kuongezewa nguvu na maboresho zaidi ili kuendana na kasi hio ya ukuaji katika ICT. Matumizi ya GPS katika usafiri wa taxi yamerahisisha zaidi gharama na muda wa kutoka sehemu moja na nyingine, huku maboresho ya miundombinu kama barabara na viwanja vya ndege yakichagiza kasi ya sekta hio.

Zaidi, mtandao wa huduma za Posta na EMS unajumuisha takriban ofisi 30,000 barani ambazo ni muhimu katika kuwezesha e-commerce trade. Kwa kuliona hilo kampuni kama DHL zimejitosa kuhakikisha teknolojia inabadili huduma za posta kuwa rahisi zaidi.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi na jambo hili?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo kuhusu usafirishaji na miundombinu katika ustawi wa biashara Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA

UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-commerce BUSINESSES)?

Japokuwa imechelewa, lakini kwa sasa Africa ndio inaongoza mbio katika kufanya mapinduzi ya kidijitali kuliko sehemu yoyote duniani. Namna ya kufanya biashara inazidi kubadilika ikionyesha nia ya dhati kufanya maendeleo ya kiuchumi, miundombinu na maswala ya kijamii. Mwaka 2018 nchi wanachama wa Umoja wa Africa walipiga hatua kubwa katika mfumo wa kufanya biashara na muingiliano wa kiuchumi baada ya kuanzisha Eneo Huru la Kufanyia Biashara barani (Continental Free Trade Area AfCFTA). Eneo hili lililoanzishwa linashirikisha nchi 22 zilizoweka sahihi tayari na utekelezwaji wake ulipangwa kuanza mwaka 2019 (tayari umeshaanza).

Hata hivyo mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuzishirikisha nchi ambazo bado si wanachama wa eneo hili jipya, inatarajiwa eneo hili kufikia soko la watu takribani bilioni 1.2 barani wakiwa na jumla ya pato la ndani la taifa (GDP) la dola za kimarekani trilioni 2.5 kwa pamoja, kwa mwaka. Hii inatarajiwa kuwa ni mapinduzi makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nyanja ya uchumi wa Afrika.

Sasa, swali linakuja; Afrika(wafanyabiashara, makampuni/mashirika na Serikali) imejiandaa vipi na mapinduzi haya ya uchumi wa kidijitali? Na zaidi, watunga sera/sheria wataangalia vipi biashara za kielektroniki (e-commerce) kama mada muhimu katika eneo hilo jipya la kufanya biashara huru barani?

Tume ya kudhibiti uchumi wa Africa ya Umoja wa Mataifa (ECA) ikishirikiana na Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) pamoja na Baraza la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo ya kibiashara (UNCTAD) mwaka huu 2019 imechapisha ripoti yake ikiangazia maendeleo ya Afrika kiujumla katika nyanja za kiuchumi, siasa na kijamii.

URAHISI: Imeonekana kwamba e-commerce inaweza kufanya biashara ya bidhaa na huduma kwa urahisi zaidi ambapo itarahisisha mwenendo mzuri wa biashara kati ya wazalishaji, wafanyabiashra na walaji pamoja na kumbukumbu zao na miamala ya kifedha.

MITANDAO YA KIJAMII: Pia imeonekana kwamba e-commerce inapatikana na kufanyika kirahisi katika mitandao ya kijamii kama facebook na Instagram ambapo ndipo mahali kuna watumiaji wengi zaidi wa Intaneti duniani (zaidi ya watu bilioni 2 kati ya watumiaji bilioni 4 wa intaneti).

KUTOKUWA NA MIPAKA: Mfumo wa uchumi wa Kidijitali kiasili umetengenezwa kuepuka mipaka ya kijiografia katika kufanya biashara na kubadilishana fedha ambapo mabadiliko haya ya kiteknolojia yataongeza umakini zaidi katika mwenendo wa masoko na gharama. Lakini bado wimbi kubwa la watu watakaoshiriki kwenye soko barani wanaonekana wataachwa nyuma kutokana na kutokuingiliana kwa lugha na vita/ghasia za mara kwa mara katika baadhi ya jamii/nchi.

BIASHARA: Kwa mujibu wa UNCTAD mwaka 2016 kwa dunia nzima e-commerce iliweza kupitisha mauzoya takribani dola trilioni 26 ambapo 90% ilikuwa ni Biashara kwa Biashara (B2B e-commerce) na 10% ilikuwa ni Biashara kwa Mlaji (B2C e-commerce). Hata hivyo kupima mwenendo wa e-commerce katika baadhi ya nchi zinazoendelea imekuwa ni changamoto kupata data na takwimu, haswa katika nchi za Afrika.

IMPORTATION: Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kwamba Biashara kati ya nchi na nchi imekua kwa kiasi kikubwa Afrika ambapo zimechagizwa na vituo vichache vya kiteknolojia (Hubs) ambavyo vimerahisisha mno mwenendo wa biashara. Biashara kati y nchi na nchi (Intraregional import) imekuwa zaidi ya mara 3 katika miongo miwili iliyopita kufikia 12%- 14% sawa na dola bilioni 100 ikichagizwa na uwepo wa jumuiya za kiuchumi barani (Subregional Economic Communities REC‘s).

UZOEFU: Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na umri wa Jumuiya hizi za Kimaendeleo barani Afrika ambapo uzoefu huo hutumika kuongeza jitihada katika kuboresha namna ya ufanyaji biashara kuelekea uchumi wa kidijitali kiteknolojia. Uzoefu huo pia hutumika kuunganisha jumuiya moja na nyingine (mf, SADC na COMESAna EAC) ambapo zitazalishwa nafasi nyingi zaidi za kufanya biashara kati ya nchi wanachama na ripoti zinaonyesha 75% ya biashara hizi ndani ya jumuiya barani Afrika zimefanyika mwaka 2017 peke yake na nusu ya biashara hizo zilifanyika katika jumuiya ya SADC.

Chini ya mwavuli wa AfCFTA nchi wanachama zinatarajia kufuta tozo/ushuru kwa 90% ya bidhaa zote zitakazopitishwa na kufanyiwa biashara katika eneo hilo. Hii itaruhusu uwezekano wa kupunguza mlolongo wa kodi au kuongeza idadi na thamani ya bidhaa na huduma zitakazohusishwa. Matokeo yoyote katika punguzo hilo linalotarajiwa katika muktadha wa biashara kidijitali yataleta picha tofauti. Kupunguza mlolongo wa tozo za mipakani baina ya nchi na nchi kutapungua kwa 15% pekee ikitegemea thamani ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi husika. Hii ni kwa mujibu wa Tume inayoshughulikia Uchumi wa Afrika kutoka Umoja wa Mataifa (UNECA) mwaka 2018.

Sasa mwaka 2018 Jumuiya ya COMESA ilibuni mfumo wa kudhibiti eneo huru la kibiashara kidijitali (Digital Free Trade Area DFTA). Mfumo huu umeundwa na mambo yafuatayo;

•E-trade: Hili ni jukwaa mahsusi kwa ajili ya kufanya biashara za kimtandao na kuwezesha malipo ya kielektroniki, mobile apps kwa ajili ya wafanyabiashara walioko katika Jumuiya hio.

•E-logistics: hili ni jukwaa maalum kwa ajili ya kuwezesha biashara ya usafirishaji wa mizigo baina ya nchi wanachama wa jumuiya.

•E-legislation: huu ni mfumo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara rasmi ambao unawawezesha kufanya miamala na malipo kielektoniki.

Mfumo huu uliobuniwa na Jumuiya ya COMESA umelenga kutangaza biashara za wanajumuiya katika nchi wanachama ikijumuisha kupitia majukwaa ya e-commerce. Mfumo huu ulikuwa ni mfanano wa mfumo uliotengenezwa na kuzinduliw na nchi ya Malaysia mwaka 2017 katika muktadha wa kufanya biashara huru ndani ya eneo maalum.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.

Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana, shuka nazo:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-biashara-ya-fedha-za-kidijitali-cryptocurrency-business/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)”
  2. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia;

e-mail: info@rednet.co.tz

tovuti: https://rednet.co.tz

Simu:+255765834754