Tag: east africa

Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara

BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA

Biashara nyingi zimekuwa zikiendeshwa katika mtindo wa “Kujiajiri” ambapo wajasiriamali wengi huteseka wakifanya kazi kwa bidii usiku na mchana lakini hujikuta siku moja tu wasipofanya kazi basi biashara inashindwa kuzalisha. Yaani mfanyabiashara unajikuta unakuwa mtumwa kwenye biashara yako mwenyewe? Hio dhana ya kujiajiri inakuwa na maana gani sasa? Leo sasa tuangalie Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara inayojitegemea? Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Septemba 21 kila mwaka ni Siku ya Kimataifa ya Amani. Sasa katika Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (UN), Lengo Na. 16 limekazia katika kudumisha Amani, Haki na Taasisi Imara. Amani ni mbolea muhimu katika ukuaji wa uchumi mahali popote. Mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa uliokaa mwaka 2001 ulithibitisha kuweka Siku maalum ya kutafakari na kudumisha Amani, Haki na Taasisi Imara duniani, ambapo siku hio ni September 21 kila mwaka.

Hii ni kutokana na vitendo vya uvunjifu wa amani, taasisi dhaifu na kukosekana haki si za kidemokrasia katika utendaji, serikali hizi ambazo mara nyingi huwa ni za kidikteta au za kifalme, mara nyingi huendeshwa kwa sheria zinazokandamiza upande mmoja na kuimarisha kikundi kidogo cha watu kwa maslahi yao binafsi.

Jambo hili hutokea pale viongozi (watu wanaopewa dhamana) kushindwa kuwajibika kwa wanachi na hivyo kujiundia sheria ambazo zinawapa mamlaka ya kutumia rasimali za nchi huku zikiwaacha wanachi katika hali ya upofu wasiwe na nguvu ya kuuliza na kusimamia matumizi sahihi ya rasilimali zao. Hili ni jambo baya na linalopaswa kuagamizwa mahali popote kwanzia ngazi ya familia, biashara, kampuni, shirika mpaka serikalini.

Mwandishi mahiri Robert Kiyosaki katika kitabu chake cha CASH FLOW QUADRANT amefafanua kwanini Matajiri huendelea kuwa matajiri huku Watu wa Uchumi wa kati wakiendelea kukimbia mbio za panya na masikini wakizidi kuwa masikini. Kwa haraka haraka, katika Njia 4 za kuingiza mapato ambazo zimeonyeshwa kwa herufi za E, S, B na I, zimetajwa kuwa ndio chanzo kikuu cha mapato ya watu duniani.

SEHEMU ZA KUIFANYA BIASHARA YAKO KUWA TAASISI IMARA?

Waswahili wanakwambia “Kila mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake” lakini katika uwanda wa kiuchumi na biashara duniani, kila mtu anao uwezo wa kubadilika na kufanya uchaguzi ulio bora zaidi kwa maisha yake ya kiuchumi na kijamii. Na hii ni kwa kujifunza na kufanya kazi tu.

E = EMPLOYEE (MWAJIRIWA): Kitu cha kwanza ambacho kipo kichwani kwa mwajiriwa yeyote ni uhakika wa kibarua chake (job security). Mwajiriwa hufanya kazi kwa bidii ili apate mkate wa kila siku na zaidi awe na hakika kuwa ataendelea kupokea mshahara kila mwisho wa mwezi kwa miaka mpaka atakapostaafu au kumaliza mkataba wake. Dhana ya kuwa majiriwa huathiri ubunifu wa mtu katika kutaka kujaribu shughuli nyingine itakayoimarisha uchumi wake zaidi ya ajira.

Mwajiriwa anapohitaji kukua kiuchumi hutafuta ajira itayomlipa zaidi na si fursa za biashara mpya.

udalali wa mtandaoni ongea na watu uvae viatuBiashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara

S= SELF-EMPLOYED (KUJIAJIRI): Hii ni njia ya mateso makubwa, japokuwa vijana wengi eti ndio hupenda kufanya shughuli za kujiajiri wakihisi kuwa huko kuna uhuru mkubwa na pesa nyingi. #VijanaWenzangu acheni kujidanganya. Unapojiajiri fahamu kuwa utajinyima uhuru wako binafsi ili biashara yako iweze kuwa hai. Wewe ndio unakua CEO, sales manager, mhasibu wewe, mtu wa masoko wewe, yaani wewe ndio unakuwa kila kitu. Hata hivyo kwa biashara inayoanza si vibaya kupitia katika hatua hii japo hutakiwi kukaa muda mrefu hapa, lazima biashara ivuke hiki kiunzi.

B=BUSINESS OWNER (MMILIKI WA BIASHARA): Tofauti na walio katika Chumba “S” Mtu anayemiliki biashara sio lazima awe anafanya kazi katika biashara hio. Yeye anamiliki mfumo wa utendaji au bidhaa ambayo ndio huzalisha pesa muda wote hata asipokuwepo. Mfano, mtu anayemiliki kiwanda cha kutengeneza nguo. Sio lazima awe ndio mtendaji mkuu wa kutengeneza nguo, hata hivyo yeye anaweza kuajiri watu wa kiwandani na kuwalipa ili waendelee kuzalisha bidhaa zitazoendelea kuingiza pesa.

I=INVESTOR (MUWEKEZAJI): Huyu ndiye mtu mwenye uelewa mkubwa zaidi kati ya wote ambao tumewajadili hapo juu. Mtu huyu hutafuta Mali (Assets) zaidi kuliko madeni (Liabilities). Mara nyingine hutumia pesa za watu wengine (mkopo) ili kuhakikisha anapata Mali itakayozalisha (asset). Ukitaka kufahamu kwa undani kuhusu Uwiano unaofaa wa Mali na Madeni katika biashara gusa link hii Uwiano wa Mali (assets) na Madeni (Liabilities) kwenye biashara.

Mtu huyu hutumia faida anayopata kutoka kwenye assets zake kununua assets nyingine nyingi zaidi, na hujikuta akifurahia maisha ya kuingiza kipato kutoka kwenye assets kuliko vyanzo vya matumizi (liabilities). Kama ulikua hufahamu basi Matajiri unaowajua duniani wote ni Wawekezaji huku wakitumia kanuni ya 70% kwa 30% katika shughuli zote za kifedha. Kiufupi kanuni hio hutumika katika kupanga matumizi ya mapato ambayo hugawanywa katika mafungu matatu ya:

i. 70% Matumizi ya kawaida (Normal Expenses including taxes, rents, food, accomodations etc)

ii. 30% (20% Servings + 10% Charity) Mwekezaji anapohitaji pesa hutafuta assets zaidi kuliko kufanya matumizi yanayofyonza pesa za biashara.

Sasa basi, hayo yote niliyoyaeleza, hayatakuwa na maana kama hayatafanyika katika muundo wa Taasisi Imara.

BIASHARA KAMA TAASISI IMARA INA SIFA ZIPI?

Taasisi Imara ni ile jumuiya ya kiuchumi/Kijamii ambayo inaendeshwa kwa mujibu wa katiba katika utendaji wake wa kila siku. Jumuiya hio inaweza kuwa ni Serikali, Shirika, Kampuni, Chama, Biashara au Familia. Familia (Ndoa) ndio Taasisi ya kwanza kabisa kuwahi kuanzishwa na binadamu duniani. Ndio maana wahenga wanakwambia “Maendeleo yanaanzia nyumbani.

Maendeleo ya taasisi hutegemea uwepo wa sheria zitakazokuwa muongozo wa kila kinachofanyika kila siku ndani ya taasisi hio. Hata hivyo ili iwe taasisi imara inapaswa kuwa na sifa hizi:

1. SHERIA MBELE, MTU NYUMA: Taasisi imara hutambua na kutekeleza matakwa ya kisheria na kamwe si matakwa ya mtu binafsi. Sheria hizi huandikwa katika mfumo wa Katiba (constitution/memorandum/articles of assosciation, Taratibu (regulations) na sheria ndogondogo (by-laws). Taasisi zinazoongozwa vema kwa mujibu wa sheria bila kumuogopa mtu huwa imara sana kiutendaji na hufikia malengo yake kiurahisi zaidi.

2. UTAMADUNI: Katika utendaji bora, Utamaduni huzingatiwa kama silaha bora zaidi katika uzalishaji/utoaji huduma wenye viwango vya juu vinavyitakiwa. Wahenga walishasema “Culture eats strategy for breakfast” yani, hakuna mbinu ambayo itaweza kufanya kazi kwa mafanikio isipofanywa kama sehemu ya utamaduni. Hivyo Taasisi imara hufanya shughuli zake katika Utamaduni uliotengenezwa kwa muda mrefu katika kufikia malengo yaliyowekwa. Mfano, utamaduni wa kupongeza mtendaji bora, utamaduni wa kumhudumia mteja kwa njia ya mtandao na utamaduni wa kuzingatia viwango.

3. UWAJIBIKAJI: Ili iwe Taasisi imara lazima watendaji wawajibike katika majukumu ya kila siku. Watendaji wanapaswa kuwajibika kwa Kupongezwa, Kujiuzulu au Kuongeza kiwango cha uzalishaji/utoaji huduma kwa wateja wao. Taasisi imara haipaswi kufumbia macho swala la uwajibikaji.

Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara

4. KWELI NA HAKIKA: Hakuna Taaasisi Imara ambayo haijiendeshi katika namna ya Ukweli na Uhakika kwa wateja wake. Hata hivyo, hakuna mifumo ya Taasisi inayofanya kazi kwa ubora wa 100%, ni vema kuhakikisha jambo hili linazingatiwa.

Tulizoziona leo ni baadhi ya sifa zinazotengeneza Taasisi Imara. Kwa mujibu wa malengo Endelevu ya kimataifa ya UN, imepangwa kutimiza lengo la kuwa na Taasisi Imara ifikapo mwaka 2030 (#Agenda2030). Tujadili kupitia Replies, Retweets na Share ili watu wengi zaidi wanufaike.

Tuungane kwa pamoja kuhakikisha Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara. Endelea kupata makala muhimu kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia kupitia links hizi hapa:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?
  3. UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA
  4. TEKNOLOJIA KATIKA KUKUZA BIASHARA KUPITIA SEKTA YA UTALII

KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRICA (AfCTA), KUNA MANUFAA GANI KWAKO?

January 1, 2021 ilikua ndio siku rasmi ya kuanza kwa shughuli huru za kibiashara na uchumi baina ya nchi wanachama wa Umoja wa Afrika waliokubaliana kuanzisha AfCTA. Ni furaha ilioje.

Hata hivyo kuanzishwa kwa eneo hilo (African Continental Free Trade Area) kumekuja baada ya makubaliano rasmi baina ya nchi wanachama kusainiwa ambapo ilihitajika nchi 22 walau ili eneo hilo liweze kuanzishwa rasmi (kifungu na23 cha mkataba wa makubaliano). Hivyo tar30 May 2019 nchi 24 zilisaini hati za kuwa washiriki wa kwanza kabisa wa Eneo hilo la kibiashara.

Kufikia leo hii, nchi 35 za AU tayari zimeshatia saini kujiunga katika AfCTA ambapo jiji la Accra, Ghana limewekwa kuwa Makao Makuu rasmi.

AfCTA INA MAANA GANI?

Hili ni eneo la kinadharia, yaani hakuna soko linaloonekana kama Kariakoo ndo useme AfCTA inafanyika hapa, Hapana.

Eneo hili ni Jumuiya ya Kibiashara na maendeleo kama zilivyo Jumuiya za kikanda kama EAC na SADC, isipokuwa hii AfCTA imepangwa mahsusi kujumuisha nchi zote za Afrika kwa malengo ya kiuchumi na Biashara. Hivyo nchi zinazohitaji kujiunga zitapewa mkataba wa makubaliano kabla ya kujiunga rasmi.

Kupata Waraka wa makubaliano ambao wakuu wa nchi Washiriki waliafikiana gusa link hii itakupeleka kwenda kuuona waraka huo na kuupakua ili uusome na kujua kwa undani Mambo yaliyokubaliwa, Malengo na kadhalika: https://rednet.co.tz/download/agreement-establishing-the-african-continental-free-trade-area-afcta

Kuwa mshiriki na mnufaika wa faida za eneo hili kunamtaka mwanachama wa AU kukubali na kusaini makubaliano hayo. Hivyo inawezekana nchi ikawa ni mwanachama wa AU lakini isiwe mshirika wa AfCTA kwa kuwa ni hiari kwa nchi yeyote ya Africa kuingia katika eneo hili la kibiashara.

FAIDA NI ZIPI KUWA MWANA AfCTA?

AfCTA inatajwa kuibua eneo huru kubwa zaidi la kibiashara duniani likijumuisha idadi kubwa ya washiriki. Inatarajiwa eneo hilo litawafikia watu 1.3 bilioni waishio barani Afrika lenye pato la ndani (GDP) la pamoja linalofikia $3.4 trillioni.

Makubaliano ya kuanzisha AfCTA yalilenga kuleta faida zifuatazo:

i. Kukuza Uchumi wa nchi washiriki, Kupunguza umasikini na kupanua wigo wa uchumi shirikishi ambapo:

•Watu milioni 30 watatolewa katika wimbi la umasikini uliokithiri, na wengize zaidi ya milioni 68 wanaoishi chini ya dola 5.50 kwa siku (hapa bila shaka na wewe pia umo) watapandishwa hali zao za kiuchumi.

•Bidhaa zinazouzwa nje (Exports) zinapangwa kuongezeka kufikia thamani ya dola 600 bilioni, hasa katika sekta ya viwanda na uzalishaji.

•Kutakuwa na Ongezeko la Kipato kwa watu wenye taaluma (skilled workers) na wale wasio na taaluma (unskilled workers) kwa 10.3% na 9.8% respectfully.

•Kutakuwa na ongezeko la kipato kwa Afrika kwa dola 450 bilioni kufikia mwaka 2035, ikiwa ni ongezeko la 7%. Hivyo kuongeza pato la dunia nzima kwa dola 76 bilioni.

ii. Urahisi wa watu kusafiri na kufanya biashara baina ya nchi wanachama. Hebu imagine leo hii unaweza kufikisha bidhaa/huduma zako ndani ya nchi 35 barani Afrika bila yavikwazo vya kibiashara ikiwa mtaji unao na rasilimali za kukuwezesha kusafiri pia zipo. Upewe nini tena?

iii. Kukuza/kuchochea ushindani wa kiuchumi na biashara baina ya nchi wanachama, jambo ambalo linatajwa kuboresha mazingira ya uzalishaji wa bidhaa bora na huduma zinazokidhi mahitaji ya wateja kwa gharama nafuu zaidi.

iii. Kuondoa vikwazo vya mipakani (trade tariffs) ambavyo vinatajwa kuleta changamoto kubwa na kufanya wafanyabiasha washindwe kuvusha bidhaa/huduma zao kwenda nje ya nchi kwa urahisi. Sasa leo AfCTA inakuwezesha kupitisha bidhaa/huduma zako ndani ya nchi 35 bila tabu yoyote.

iv. Kuchochea maendeleo ya viwanda kupitia mgawanyo wa maendeleo na upatikanaji wa rasilimali ndani ya maeneo husika. Pia kukuza sekta ya kilimo kwa kuboresha pembejeo za uzalishaji, masoko na upatikaji wa chakula. Imagine wakulima wadogo wataokolewaje hapa na hii fursa!

v. Kuweza kupambana na athari za majanga mbalimbali ya kiasili na magonjwa ya mlipuko mfano #COVID19 ambao unatajwa kusababisha hasara ya dola 79 bilioni barani Afrika katika mwaka 2020 pekee. Ugonjwa wa Korona umesababisha hasara kubwa katika utendaji wa kibiashara ikijumuisha upatikani adimu wa bidhaa, huduma za afya pamoja na chakula. Hivyo kwa kuchochea biashara za kikanda kwa kupunguza kodi na makato/taratibu za mipakani baina ya nchi washiriki, uwepo wa AfCTA unatajwa kusaidia nchi za Afrika kuchochea uchumi na kuongeza uwezo wa kupambana na majanga mbalimbali pamoja na magonjwa ya mlipuko. Mkakati wa kuanzishwa kwa AfCTA unalenga kuzipa nguvu za kiuchumi za muda mrefu nchi washiriki, hivyo eneo hilo linatajwa kuwa ni eneo muhimu zana la kimbinu za Ujasusi wa Kiuchumi.

AfCTA ni moja ya mradi wa kimkakati wa Agenda 2063 ambao ni mpango wa kimaendeleo wa miaka 50 kutoka mwaka 2023 – 2063 uliowekwa na nchi wanachama wa Jumuiya Umoja wa Afrika (AU). Mpango huo ulilenga kuimarisha hali za kiuchumi, biashara na maendeleo baina ya nchi wanachama.

Eneo hili pia linatajwa pia kuwa muhimu sana kwa jumuiya za maendeleo barani Afrika na nchi zingine kwa kuruhusu Makubaliano ya kibiashara kama Economic Partnership Agreement (EPA, sio ile mnayoijua nyie). Makubaliano hayo yanatajwa kuimarisha kuimarisha biashara za Jumuiya kimataifa kama EU, Jumuiya ya Nchi za Asia kusini (ASEAN) na Marekani. Ama kwa Hakika Eneo hili la AfCTA lina mchango mkubwa sana wa kuimarisha biashara ndogo ndogo barani Afrika. Ni wakati wako sasa kutumia vyema kila fursa inayojitokeza kwenye eneo hili. GET IT DONE!

Zaidi pata makala hizi zinazorandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana ukizimaliza zote. Gusa links zifuatazo:

  1. https://rednet.co.tz/umuhimu-wa-takwimu-katika-utoaji-wa-huduma-bora-kwa-wateja/ yenye kichwa “UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA
  2. https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  4. https://rednet.co.tz/teknolojia-katika-kukuza-biashara-kupitia-sekta-ya-utalii/ yenye kichwaTEKNOLOJIA KATIKA KUKUZA BIASHARA KUPITIA SEKTA YA UTALII

Marejeo:

https://au.int/en/treaties/agreement-establishing-african-continental-free-trade-area

https://www.tralac.org/resources/our-resources/6730-continental-free-trade-area-cfta.html

https://www.worldbank.org/en/topic/trade/publication/the-african-continental-free-trade-area

Photo curtesy of the “Digital Tools on Business Performance” iliyofanyika jijini Dodoma mwaka 2020.

teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)

Uchumi wa Africa mpaka sasa hukua kwa kutegemea sekta za asili kama kilimoufugaji na biashara. Hata hivyo ujio wa teknolojia ya huduma za kifedha kwa njia ya kielektroniki (Fintech) utasaidia kwa kiasi kikubwa kuendesha uchumi katika kufanikisha maendeleo kiujumla. Sasa tuangalia teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech), zina mchango gani kwako leo?

Uchunguzi umeonyesha kwamba matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu za mkononi yameongezeka sana ndani ya miaka 10 iliyopita ambapo imeonekana eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara ndio limekuwa kinara wa kubuni na kutumia huduma hizi za kifedha kwa kutumia simu za mkononi duniani kwa sasa.

Utafiti uliofanywa na Shirika la Fedha duniani (IMF) umebaini kwamba takriban 10% ya pato la taifa katika miamala ya kifedha hufanyika kwa huduma za kifedha kupitia simu za mkononi. Hii ni matokeo bora zaidi ukilinganisha na 7% ya GDP katoka bara Asia na chini ya 2% ya GDP kutoka sehemu zingine za dunia.

Sasa swali, hii Fintechs ni nini!? Na ina manufaa gani kwa wafanyabiashara walio Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Shirika la EY linaifafanua FinTech kama Shirika/Kampuni inayojumuisha ubunifu katika utendaji wa biashara pamoja na technolojia ya programu za kompyuta katika kubuni, kuwezesha na kusambaza huduma za kifedha. Hizi FinTechs zinaweza kuwekwa kwenye makundi mawili;

i. FinTechs zinatoa huduma za kifedha e.g TALA App.

ii. FinTech zinazowezesha huduma za kifedha Vodacom na MPESA n.k (tutayajadili zaidi kwenye makala zetu zijazo)

Sekta hii ya FinTech katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara (SSA) inajumuisha zaidi ya makampuni 260 ambapo 80% katika hizo ni kampuni za ndani na 20% ni kampuni za kimataifa. Vile vile imeonekana idadi ya makampuni haya mapya imeongezeka katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) cha 24% ndani ya miaka 10 iliyopita.

Hata hivyo ripoti zinaonyesha kwamba Afrika Mashariki itaendelea kuongoza katika ukuaji wa sekta hii kwa 6.3% ya ukuaji wa uchumi mwaka huu 2019. Hii ni kutokana na Ethiopia, Rwanda, Tanzania na Uganda zote zinatarajia kurekodi pato la Taifa la zaidi ya 6% mwaka huu ambayo ni zaidi ya nchi zilizo maeneo mengine ya Africa. Hii ni kutokana na uwekezaji katika miundombinu na utanuzi wa huduma za kifedha na mawasiliano.

Takriban theluthi moja (1/3) ya michango ya harambee zilizofanyika barani Africa mwaka 2017 iliwezeshwa na kampuni za FinTechs. Hii inatiliwa mkazo kwa kuwa 60% ya akaunti za huduma za kifedha kwa njia ya simu duniani zimegundulika kuwepo katika eneo la SSA. Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliofanya na benki ya Ecobank.

Pia imeonekana sekta hii ya FinTechinaendelea kuwa imara katika muda wa miaka 3 kutoka makadirio ya dola za kimarekani 200 milioni mwaka 2018 hadi 3$ bilioni mwaka 2020. Kiasi kikubwa cha uwekezaji katika muda huu kimeonekana kuelekezwa KenyaNigeria na Afrika Kusini. Vile vile inategemewa kwamba kufanikiwa kwa Fintechs katika nchi hizo kutatanua mafanikio katika nchi zingine za Kiafrika.

MAENDELEO: Ujio wa FinTechs umebadili sana jinsi ya kufanya biashara duniani. Kutoka Crowdsourcing ambayo ni njia inayotumika kufanya usaili wa miradi mbalimbali mtandaoni kupitia intaneti na kupokea ruzuku, mpaka njia ya huduma za kifedha kwa njia ya simu. Wafanyabiashara na wajasiriamali hawajawahi kupata njia rahisi zaidi kwenye utandaji wa biashara zao kwenye maswala ya fedha kuliko hii.

Kupitia Fintechs sasa wafanyabiashara wanaweza kusambaza bidhaa/huduma kwa watu mbali mbali na kupata malipo ndani ya muda mfupi zaidi. teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) inazidi kujisombea watumiaji kwa sababu inaonyesha namna inavyoweza kusaidia katika kujikwamua kwenye maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni.

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH) HAINA MIPAKA:

Kutuma pesa nje ya mipaka ya nchi napo imekuwa rahisi zaidi. Mfumo huu ulioondoa mipaka ya kijiografia kwenye kurusha pesa umepunguza gharama kutoka ilivyokuwa mwanzo kwa njia ya benki ambayo ni ghali mno. Hivyo FinTech imewawezesha wajasiriamali na viwanda vidogo kutuma na kupokea pesa kwa gharama ndogo zaidi.

KUONGEZA THAMANI KATIKA UTOAJI WA HUDUMA ZA KIFEDHA: Eneo hili limetawaliwa na ubunifu ambao unawezesha kuongezeka kwa thamani katika matumizi ya huduma za kifedha. Kwa kuyumia malipo kwa njia ya simu, wateja walioko kusini mwa Jangwa la Sahara wanapata uwezo wa kupata huduma za kibenki kupitia simu za mkononi (mobile banking) pamoja na huduma zingine kama kugungua akaunti, kuchukua mkopo, kupata bima, kupata huduma za mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na masoko ya hisa. Haya yote kupitia FinTech yanawezeshwa kirahisi tuu katika simu yako ya rununu (smartphone) au laptop.

teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi. Umejifunza nini hapa katika teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) leo?

Zaidi unaweza kupitia makala hizi hapa chini ili kupata ufahamu mpana kuhusu biashara za mtandaoni:

  1. MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA
  2. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  3. UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-COMMERCE BUSINESS)?
  4. FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia comments section hapo chini;