Tag: digital economy

LIPA KODI KWA FAIDA YA BIASHARA YAKO

Wamiliki wengi wa biashara huanza katika Biashara binafsi (machinga/sole proprietor). Baadae hukua kufikia partnerships, wabia wa kampuni mpaka mashirika. Kadiri unavyotengeneza mifumo ya biashara yako ndivyo inakuwa rahisi kulipa kodi.

Kodi huja katika namna nyingi, unapofanya kazi, unalipwa ujira/mshahara, hapo utalipa “Income Tax”. Kutegemea na kiasi cha pesa unacholipwa, asilimia fulani hukatwa na muajiri wako na kulipwa kwenye Mamlaka za Kodi, % hio huitwa “Withholding Tax”, hii hutaiona kwenye paycheck yako kwani hulipwa na mwajiri moja kwa moja kwenda kwa Mamlaka za kodi.

Ukinunua bidhaa, fahamu kuna kodi pale unalipa ambayo inajumuishwa katika bei ya bidhaa hio. Kodi hio huitwa “VAT” ambayo ni kodi maarufu na yenye kuingiza mapato makubwa sana katika mamlaka za Kodi. Kama unamiliki mali/ardhi unalipa Kodi iitwayo “Property Tax” kulingana na thamani ya mali/ardhi yako hio.

Kulipa kodi ni wajibu wa kizalendo, lakini zaidi ni matakwa ya kisheria. Usipolipa kodi unajiweka kwenye mazingira ya kulipishwa faini au adhabu kwa mujibu wa sheria. Kodi unayolipa inakwenda sehemu mbalimbali za kiserikali kama mishahara ya watumishi wa serikali, polisi, jeshi la zimamoto na uokoaji, kuimarisha miundombinu, sekta ys afya n.k.

UNAEPUKA VIPI RUNDO LA KODI KWA MANUFAA?

Kuendesha biashara kunajumuisha gharama nyingi sana. Na katika kila gharama kuna kiasi cha kodi unatozwa. Fahamu, Ukinunua unalipa kodi, Ukiuza unamlipisha mtu kodi. Jambo hili linafanyika ukiwa unajua na hata bila ya wewe kujua.

1. MANUNUZI

Kodi ya VAT (Value of Added Tax/Kodi ya Ongezeko la Thamani) ambapo unaponunua bidhaa/huduma yoyote unakuwa unanunua kitu chako pamoja na kukilipia kodi yake ya VAT hapo hapo. Kodi hiyo huwa ni 18% ya thamani kamili ya bidhaa/huduma inayouzwa. Mfano unaponunua umeme wa 2,000/-, hapo unakuwa umelipia na kodi yake ambayo imejumlishiwa kwenye hio 2,000/- (indirect tax). Hali kadhalika katika bidhaa/huduma zingine kama mafuta, vocha, computer, chakula, gesi n.k. Kila unachonunua kina kodi yake, Hivyo kama mfanyabiashara hakikisha manunuzi yako yote yahusuyo gharama za uendeshaji (umeme, maji, chakula, mafuta, maintenance, usafi) yanakuwa na risiti zake halali. Risiti zako hueleza kodi zile ulizokatwa “withheld” katika manunuzi/matumizi ya biashara yako. Hivyo jambo hili litakupa unafuu katika kulipa kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).

2. MAUZO

Wafanyabiashara huwalipisha wateja wao VAT lakini wengi hawapendi kulipa kiasi hiko cha kodi katika Mamlaka ya Kodi. Jambo hili ni kinyume na sheria na linaweza kukuweka kwenye mikono ya kisheria yanayoweza kukufilisi mali, kukupeleka gerezani au vyote vikakupata.

Hivyo unapofanya mauzo katika biashara yako hakikisha unatoa risiti halali ili bidhaa unazouza ziwe kwenye uwiano mzuri wa thamani na Mamlaka za kodi

CHANGAMOTO:

i. Tafiti zinaonyesha kuwa zaidi ya 70% biashara hazilipi kodi. Hii inachochewa na upungufu wa elimu ya kodi pamoja na morali ya wananchi katika kulipa kodi.

ii. Pia kumekuwepo na sekta ambazo hazilipi kodi ipasavyo, mfano sekta ya madini, uvuvi, misitu na utalii. Hii imetokana na kutokuwepo na njia bora za ukusanyaji wa kodi katika maeneo hayo, hivyo kudidimisha mapato yao katika kodi.

iii. Kuwepo kwa misamaha mikubwa ya kodi (tax exemptions) kwa wawekezaji wa ndani na wale wa nje. Mbinu hii iliwekwa ili kuwavutia wawekezaji wazidi kumininika lakini matokeo yake yamekuja kudhoofisha sekta zingine za biashara kutokana na kutokuwepo kwa usawa katika makusanyo.

iv. UFISADI: Inarudisha maendeleo nyuma sana hali ya kutokuwepo kwa makusanyo ya kodi. Hali hii kwa kiasi kikubwa huchochewa na kukithiri kwa vitendo vya Ufisadi katika Mashirika ya Umma pamoja na Mamlaka za Kodi. Watu huishiwa morari ya kulipa kodi pale wakiona kodi zao zinaishia mifukoni mwa watu wachache tena kwa manufaa binafsi. Jambo hili ni baya sana katika maendeleo ya biashara. Likemewe kwa nguvu zote.

MATUMIZI YA ICT KATIKA MFUMO WA KODI:

Teknolojia ya ICT imekuja kuwa mkombozi katika mifumo ya mapato na kodi katika biashara na Mamlaka za Kodi katika kutunza kumbukumbu za walipa kodi. Teknolojia imeleta afadhali katika kukusanya kodi kupitia matumizi ya mashine za EFD ambayo hutumika kukusanya taarifa za kodi, mauzo na manunuzi katika biashara.

Mashine hizi za EFD zilianza rasmi kutumika mwaka 2013 zikiwa na lengo la kusajili wafanyabiashara wote pamoja na miamala yote ya mauzo na manunuzi nchini Tanzania. Mwaka 2014/15 Halmashauri ya manispaa ya jiji la Arusha ilianza kutumia mfumo wa LGRCIS (Local Government Revenue Collection Information System). Zaidi kuhusu mfumo wa mapato ya serikali za mitaa unaweza kupata kupitia makala kwenye link hii https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-na-mapato-ya-serikali-za-mitaa/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NA MAPATO YA SERIKALI ZA MITAA”

Kuanzia hapo Halmashauri 8 nchini Tanzania zilianza kutumia mfumo huo wa LGRCIS kama mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi katika Halmashauri zao. Hata hivyo mwaka 2016 mifumo yote ya makusanyo iliunganishwa katika mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi wa TRA.

Lakini bado mpaka sasa mfumo wa LGRCIS unaendelea kutumika ktika kukusanya mapato ya halmashauri ikijumuisha Ushuru, Tozo na kodi za leseni za biashara. Mfumo huo umerahisisha malipo ya kodi kupitia njia za malipo ya kielektroniki kama MPESA, Bank transfer, Tigopesa n.k.

Hivyo, katika mifumo ya kodi kupitia makala haya ni matumaini yangu umejifunza kitu muhimu katika namna unavyoendesha biashara yako kwa faida bila kukwaruzana na Mamlaka za Kodi. Una maoni yoyote? Tafadhali weka comment yako hapa chini. Pia unaweza kushare link ya makala hii ili kuhakikisha inawafikia watu wengi zaidi kwa faida ya biashara zetu.

Sasa tumekuandalia makala hizi hapa chini zenye lengo la kukuimarisha katika namna ya kulipa kodi na kuifahamu mifumo yake zaidi. Zitakusaidia sana ukizisoma zote. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-nchini-tanzania/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NCHINI TANZANIA”
  2. https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-urasinishaji-harmonization-katika-biashara/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA”
  3. https://rednet.co.tz/ukiritimba-katika-biashara-ni-asali-au-shubiri/ yenye kichwa “UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI”

KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?

Hebu fikiria wewe ni mgeni mahali fulani, baada ya kushikwa na njaa unaelekezwa migahawa miwili, mmoja ukiutafuta mtandaoni unaweza kupata taarifa zake mwingine hauna taarifa yoyote mtandaoni. Uelekeo wako utakuwa upande gani? Leo sasa tutakwenda kufahamu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako. Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Kuishi katika ulimwengu wa kidijitali, tovuti ni zana muhimu sana katika biashara na masoko ya kidijitali. Cha kushangaza inakadiriwa 35% – 50% ya biashara ndogondogo duniani hazina tovuti zao binafsi, jambo linalozinyima fursa ya kuweka taarifa zao kirahisi mtandaoni na kupata wateja wapya kirahisi.

Kuna wanaosema kuwa matumizi ya Tovuti yanamezwa na uwepo wa mitandao ya kijamii ambayo pia watu wanaweza kuweka na kutangaza biashara zao humo. Ni kweli, aghalabu, kwa kutumia Mitandao ya kijamii hauna uhakika wa kumiliki taarifa na maudhui unayoweka humo muda wote. Watengenezaji ambao pia ni wamiliki wa Mitandao hio wanao uwezo wa kusimamisha/kufuta akaunti au maudhui yako muda wowote ikiwa biashara/maudhui yako yanakwenda kunyume na matakwa na masharti yao.

Vile vile Mitandao ya kijamii unayotumia inaweza kupungua umaarufu au kufilisika muda wowote usioutegemea mfano kuna mitandao ilikua maarufu sana zamani kama Hi5 lakini umaarufu wake kwa sasa umepungua au kupotea kabisa. Hivyo, uwezekano wa kudorora kwa biashara yako kunategemea pia umaarufu wa mtandao wa kijamii unaoutumia, jambo linalichangiwa sana na ujio wa mitandao mipya ya kijamii kama Instagram, Whatsapp na TikTok. Hii kwako unaionaje? Nitaeleza Tofauti katika matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Tovuti wakati Ujao.

Faida ni nyingi sana za matumizi ya website katika kuimarisha biashara yako kupitia ulimwengu wa Teknolojia. Tayari tumekuandalia makala maalum kupitia link hii hapa WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?.

Leo hii ntakwambia mambo 10 kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika biashara yako:

1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:

Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu huenda wapi kutafuta vitu kama suppliers, bidhaa na huduma mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi. Injini za matafuto mtandaoni zimekuwa kimbilio namba moja huku GOOGLE Ikiziacha mbali Injini zingine kama Yahoo, Bing na Ask. Maana yake hii ni kwamba kama huna tovuti, jua mauzo yako ni 7% tu ya soko zima ambalo hujui kuwa unalo. Upo apo? Yani unapoteza 93% ya mauzo yako kila siku bila hata wewe mwenyewe kujua.

2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)

Kama una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo. Kwa biashara zenye malengo makubwa kuwa na tovuti huwaweka kwenye nafasi za juu katika kupata tenda na wateja, na huonyesha Uweledi bora katika utendaji wa biashara kuanzia katika muonekano na utendaji wa tovuti. Inakadiriwa 80% ya watu duniani huonyesha kutokua na imani na Biashara ambazo hazina tovuti pale wanapotaka huduma/bidhaa fulani mtandaoni.

3. KUPATIKANA KWA URAHISI

Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi, tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako. Ndivyo ilivyo kwa tovuti ambayo inajieleza kwa kila kitu kama ilivyo tovuti maridhawa ya http://rednet.co.tz . Ile raha ya kupata taarifa, huduma au bidhaa kirahisi kupitia simu yako ya mkononi, hufanya wateja waongezeke maradufu na kusambaza sifa bora kwa uharaka sana katika jamii na katika mitandao ya kijamii hali kadhalika.

Hii huongezwa chumvi ya SEO (Search Engine Optimization) ambayo ni teknolojia iliyowekwa katika Injini za matafuto ya kimtandao inayowasiliana na tovuti yako na kuweka taarifa katika Injini hizo na hivyo kufanya taarifa za tovuti yako kuonekana haraka zaidi katika matafuto. Biashara imerahisishwa sana kupitia SEO kuliko kutumia Mitandao ya kijamii. Kama watu wanakwenda Google kutafuta taarifa, basi fahamu taarifa hizo hupelekwa hapo GOOGLE kwa kutumia teknolojia iitwayo S.E.O. Kufahamu zaidi kuhusu SEO gusa hapa chini

4. TANGAZO LA BURE MUDA WOTE

Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo huduma ya internet inapatikana. Tangazo la bure kabisa hili. Kama tovuti yako ina ubora wa kuvutia zaidi katika muonekano, maudhui na utendaji, basi bila shaka biashara yako ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri sokoni na kupata wateja wengi kila siku. Jiulize hivi, unapofunga ofisi/biashara yako wakati wa jioni kila siku, wateja wapya wanaweza vipi kupata taarifa sahihi muda watakaohitaji?turudi kwenye mada yetu, kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Hii pia inawezeshwa sana na teknolojia ya S.E.O.

5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)

Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa. Kupitia tovuti yako, unaweza kuweka testimonials kwa idadi uitakayo bila kurudia rudia na katika mpangilio maalum na watu wakaweza kuona ushahidi utakaowaridhisha kuendelea kutumia huduma/bidhaa zako. Mara nyingi Mitandao ya kijamii huzuia kuoneka kwa biashara kwa urahisi kutokana na wimbi la watumiaji wenye maudhui tofauti tofauti katika ratiba ya saa (timeline) yako unayopitia katika mitandao hio, hivyo kusababisha usumbufu (distractions) katika biashara yako.

6. UAMINIFU (TRUST)

Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza mahusiano na mteja kama UAMINIFU. Ili kupata wateja wa kudumu katika sekta nyingi, kuwa na tovuti hai ni muhimu katika kudumisha mahusianao katika ya mfanyabiashara kwa muda wowte mteja atakaohitaji.

7. POSITIVE ROI

Ikiwa ni Return On Investment (ROI) au Rejesho baada ya Uwekezaji, unapoendesha biashara ambayo ina gharama zake kama umeme, kodi, maji, mafuta n.k, ukijiuliza utaweza vipi kurudisha gharama hizo upate faida? Njia moja nzuri ni matumizi ya tovuti bora yenye uwezo kunasa wateja wapya kwa njia ya mtandao muda wote (24/7) kirahisi kabisa.

8. THAMANI INAYODUMU

Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote itakapohitajika kufanya hivyo. Hivyo thamani ya biashara yako itaendelea kuwepo muda wote tovuti yako inapokuwa hewani.

9. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA

Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei, ushauri nakadhalika. Hivyo kuimarisha mahusiano na ukaribu wako na wateja wako wakiwa popote duniani kwa urahisi kupitia miundombinu mbalimbali unayoweza kuiweka katika tovuti yako kama matumizi ya chatbots na barua pepe maalum za kibiashara (zenye jina/domain name ya tovuti yako).

10. MASIJALA (DATA CENTER) RAHISI YA MTANDAONI

Tovuti yako inaweza pia kuwa masijala rahisi kwa wafanyakazi, wateja na mtu yeyote anayehitaji kujua taarifa kuhusu huduma/bidhaa unazohusika nazo. Mfano mzuri ni tovuti yetu maridhawa ya http://rednet.co.tz ambayo zaidi tu. ya kwamba inatoa taarifa kuhusu huduma tunazohusika nazo za kutengenza websites, softwares, apps n.k, lakini pia tovuti inatoa taarifa muhimu mbalimbali kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia. Taarifa hizi zimetengenzwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha Biashara za wateja wakiwa popote duniani. Pia taarifa hizo zinalenga kuhamasisha matumizi ya Teknolojia katika njanja mabimbali za kiuchumi haswa kwa wafanyabiashara waliopo kusini mwa jangwa la Sahara.

NOTE: Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa muhimu kama jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.

BONUS POINT: Tovuti yako unapoisajili, unashauriwa pia upate kirurushi cha barua pepe yenye jina/domain name sawa na tovuti yako. Mfano, tovuti yako inapatikana katika anwani ya www.mfano.com, hivyo barua pepe yako ya kiofisi unaweza kuchagua kuwa info@mfano.com au maulizo@mfano.com au jinalako@mfano.com. Kwa kutumia barua pepe zenye jina sawa na anwani ya tovuti yako, unajiweka katika nafasi nzuri ya kuimarisha biashara yako na kuongeza wateja wapya na kazi zenya manufaa haraka zaidi katika biashara/kampuni yako. Hii ni sababu muhimu sana unapojiuliza kwanini ni muhimu kuwa na website (tovuti) rasmi ya biashara yako. Website inakufanya unakuwa official kiukweli kweli.

Pia kuna makala hizi hapa ambazo zitakupa mwanga zaidi kuhusu namna bora za kuimarisha uchumi wa biashara yako kwa kutumia Teknolojia:

  1. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  2. BRANDING vs MARKETING, KIPI NI KIPI?
  3. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA (AfCFTA), KUNA MANUFAA GANI KWAKO?
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO.

Umejifunza nini kupitia makala hii ya kuhusu kwanini ni muhimu kuwa na website(tovuti) rasmi ya biashara yako? Tafadhali unaweza kuwasilisha maoni yako kupitia sanduku la maoni (comments box) lililo hapo chini au kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yanayopatikana katika Footer Bar chini kabisa ya ukurasa huu. Pia usisite kuwashirikisha wenzako makala haya kwa kushare link yetu ya https://rednet.co.tz mara zote. Karibu!

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?
yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE

Yaani ni 8% tu ya makampuni ndio wana uwezo wa kugundua wizi wa taarifa zao ndani ya dakika chache. 62% wanaweza kugundua wizi ndani ya siku kadhaa. Wewe unatumia muda gani kugundua upotevu/wizi wa data katika kampuni yako? Makala hii tutaangazia mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) kiundani. Leo, yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake. Makinika mpaka mwisho.

Kama Unavyoona biashara zinavyozidi kushamiri kiteknolojia ndivyo wadukuzi nao wanazidi kutafuta mbinu za kufanya mashambilizi zaidi. Mwaka 2019 peke yake, zaidi ya 2$ billion zilipotelea mikononi mwa wadukuzi duniani. Utafiti wa Juniper unaonesha namba hio inaongezeka kila mwaka.

Unalikumbuka shambulizi lilioitwa NotPetya? Basi jarida la WIRED linalitaja shambulizi hilo kama “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA”. Ndani ya masaa machache tu virusi vya shambulio hilo (malwares) viliathiri kutoka biashara ndogo za Software nchini Ukraine mpaka kusambaa katika vifaa vya kielektroniki dunia nzima. Shambulizi lilidhoofisha mashirika makubwa duniani kama FedEx, TNT, Express na Maersk kwa wiki kadhaa na kusababisha hasara ya zaidi ya $10 bilioni kwa ujumla. Upotevu wa data kwa kiwango hiki unaonyesha namna katili ya dunia tuishiyo ambapo inaonekana hakuna mwenye kinga madhubuti mtandaoni. Kutoka Mashirika makubwa, serikali, mitandao ya kijamii, mifumo ya migahawa na sehemu yoyote unayojua inatumia teknolojia ya IT, Kila mmoja yupo hatarini.

TUMEFIKAJE HAPA?

Ripoti ya mwaka 2019 ya shirika la Accenture Security kuhusu Matishio ya kimtandao (Cyber Threatscape), imeonyesha sababu za wadukuzi kuendelea kuwa tishio dhidi ya taarifa binafsi/za mashirika kwa manufaa yao. Hizi ni baadhi sababu hizo:

1. Wadukuzi wa kimtandao hufaidika zaidi na teknolojia mpya na kukosekana mawasiliano madhubuti katika sheria na tawala za maeneo/nchi mbalimbali duniani.

2. Mitandao ya kihalifu muda wote inakwenda ikibadilika, hasa kuelekea katika makundi ya kihalifu ya siri (syndicates) pasi na kujulikana chanzo chake kwa kutumia nyaraka halali kwa nia halifu.

3. Malengo mseto katika kuimarisha tabia za virusi (kama kujiendesha vyenyewe: self replication)

4. Kuimarika kwa mifumo ya Ulinzi wa Kimtandao (cybersecurity hygiene) inapelekea wadukuzi nao wazidi kujiimarisha kimbinu na maarifa katika uwanda wa kiteknolojia na matumizi ya internet.

Baada ya kujua sababu zinazowasukuma Wadukuzi na wahalifu wa Kimtadao kuendelea kufanya mashambulizi, Leo, uta yafahamu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako, Fuatana nami..

Duniani kunazo aina nyingi za mashambulizi ya kimtandao kulingana na sababu nilizozieleza hapo juu kama ifuatavyo:

1. RANSOMWARE ATTACK: Katika shambulio hili, virusi maalum (specific malware) ambavyo hukusanya na kufunga taarifa/kifaa katika mtandao ili kumnyima mtumiaji haki na uwezo wa kufanyia kazi taarifa zake kama kawaida. Haki na uwezo (access) huo humrudia mtumiaji pale tu matakwa ya mdukuzi yatakapotimizwa ambayo mara nyingi huwa ni pesa au rushwa kwa mapana yake.

Saa ingine wadukuzi wanaweza kugoma kurudisha haki za matumizi kwa mhusika hata wanapotimiziwa matakwa yao, hivyo kuongezea hasara kwa kampuni/biashara. Mbaya zaidi, ripoti ya mwaka 2019 ya Uhalifu wa kimtandao inaonyesha kutokea kwa shambulizi hili kila sekunde11 ya mwaka 2021.

2. ADVANCED PERSISTENT THREATS (APT): Shambulizi hili sio la mojakwamoja (passive attack) ambapo mdukuzi anapata access ya computer/mtandao fulani kwa muda mrefu pasi na kujulikana, hivyo kujichotea taarifa na kuzitumia kwa manufaa yake. Aina hii pia huitwa Trojan Horse attack.

3. PHISHING: Je wajua? Mpaka 32% ya wizi wa data husababishwa na shambulizi hili. Hii ni aina ya shambulizi maarufu sana la kijamii (social engineering) ambapo mdukuzi humtegea mtu adownload file lililo na virusi kupitia SMS, email au link na kuingiza virusi katika kifaa chake.

unawezaje kujilinda dhidi ya shambulizi la kimtandao la phishing katika biashara yako?yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

4. SQL INJECTION: Umeshawahi kuona ile unaingia kwenye website ukakuta haipo ghafla tu, au kwenye system flani unanashangaa kuna mafiles huyaoni bila sababu ya msingi. Sasa kwa kutumia virusi halifu (malicious codes) shambulizi hufanyika katika servers zinazohifadhi taarifa muhimu za watumiaji na kuzifuta, kuziiba au kuzibadili ili kutimiza azma fulani ya wadukuzi na/au genge lao. Mara nyingi shambulio hili hufanyika kwenye servers zinazohifadhi taarifa ghafi za watu au vitu (personal identifiable information: PII) kama namba ya kadi, username and passwords.

5. DDOS ATTACK: Kirefu huitwa Distributed Denial of Services attack ambapo hutokea pale wadukuzi wanapofurika tovuti au kifaa chako kwa either kupunguza au kondoa kabisa utendaji wa kawaida na hivyo kuiacha kampuni/biashara kuhangaika kurejesha performance ya mifumo yake wakati wao (wadukuzi na virusi vyao) wakitumia mwanya huo kuiba na kufanya uhalifu katika mifumo hio iliyoathirika.

6. MAN IN THE MIDDLE (MITM): Hii hutokea pale mdukuzi anapoingilia mawasiliano halali ya kampuni bila ya wao kujua. Pia shambulio hili hufahamika kama eavesdropping pale linapofanyika baina ya mawasiliano binafsi ya simu kati ya mtu na mtu.

Mawasiliano katika MITM hiungiliwa pia kupitia APN za Wi-Fi za uongo (deceptive wifi). Zaidi ya kuingilia mawasiliano, hapa mdukuzi anaweza pia kuwasiliana akitumia utambulisho (ID) ya wahusika pasi na kufahamika mara moja.

7. PASSWORD ATTACK: Licha ya kuwa shambulizi maarufu zaidi duniani, bado kuna watu huangukia mtego wa kuibiwa nywila zao. Kwa urahisi wake, wadukuzi hutumia mbinu zenye viwango na ujanja kupata nywila dhaifu na kufungua accounts za watumiaji kirahisi. Hapa tunaangukia kwenye usalama wa vifaa vyetu vya mtandaoni. Je viko salama kiasi gani? Fuatana na makala hii hapa kufahamu zaidi..

UNAWEZAJE KUZUIA MASHAMBULIZI HAYO?

Katika yetu iliyopita tumeeleza kwa kirefu kuhusu namna ya kujiepusha na mashambulizi ya kimtandao (Cyber attacks), pitia hapa KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?“. Leo pia, tutaona njia zingine za kuendelea kujiimarisha na kuzuia mashambulizi hayo yasiathiri Biashara/Kampuni yako. Mashambulizi mengi niliyoyaelezea leo yanazuilika kwa njia ambazo tayari tulishaziona katka makala zilizopita isipokuwa:

MITM Attack: •Tumia SSL Certificates za (https) katika website yako. Hii ni boresho la http SSL certificate ambayo ni ya zamani na usalama wake mi mdogo.

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

•Tengeneza VPN yako kama ngao ya ziada dhidi ya wi-fi halifu (deceptive wi-fi). Mashambulizi haya katika biashara yako yana madhara makubwa ikiwemo Kupotea kwa Fedha, faida ya biashara, mauzo, matengenezo, Hadhi ya biashara kushuka au kupotea kabisa na madhara ya kisheria.

Hivyo unapaswa kuwa makini na kufuata ushauri wa kitaalamu kuhusu maboresho ya kimtandao (updates & maintenance) ili kuhakikisha unatumia teknolojia ya kisasa zaidi ambayo ni salama huku ikiwa imeambatana na Passwords zako zilizo bora. Utajuaje kama simu/computer yako ikiwa imedukuliwa? Majibu tayari yanapatikana kwenye makala iliyo hapa UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?.

Usalama wa Kimtandao ni jukumu langu. Ni jukumu lako. Ni jukumu letu sote. Tuchukue tahadhari muda wote tuwapo mtandaoni. Basi ni matumaini yangu leo mengi umeyafahamu kuhusu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako. Ukiwa na swali au nyongeza tafadhali tuandikie katika comments hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo? Umejifunza nini katika ku yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake katika biashara/kampuni yako.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Unawezaje kujikinga dhidi ya mashambulizi ya kimtandao katika biashara yako?yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

FAHAMU KUHUSU UVUVI NA BIASHARA YA SAMAKI BARANI AFRIKA

Japokuwa inafanyika zaidi maeneo ya vijijini na katika hali duni ya zana za utendaji, elimu pamoja na teknolojia, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado inahangaika katika kujiboresha huku ikifichwa katika kivuli cha shughuli za Kilimo na Ufugaji. Mbaya zaidi sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado haijapewa umuhimu inayostahili barani humo. Zaidi sekta hio hutoa chakula cha kuwalisha watu zaidi ya milioni 200 barani humo na nje ya bara la Afrika. Leo sasa fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika. Twende mpaka mwisho.

Benki ya Dunia inaripoti kwamba shughuli za uvuvi na biashara ya samaki huchangia moja kwa moja dola za kimarekani $24 bilioni katika uchumi wa Afrika kwa ujumla, ikiwakilisha 1.3% ya jumla ya pato la ndani (GDP) la Afrika katika mwaka 2011. Vile vile sekta hio imezalisha ajira kwa zaidi ya watu milioni 12 ambapo 58% kati yao ni wavuvi na 42% wanajihusisha na kuandaa samaki waliovuliwa kabla ya kuwapeleka sokoni. Tanzania peke yake, sekta ya uvuvi imetoa ajira kwa watu 183,000 mpaka kufikia mwaka 2014 (chanzo: Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi) Ikionekana kwamba shughuli za uvuvi hufanywa zaidi na wanaume, 59% ya shughuli za kuandaa samaki kabla ya kuwaingiza sokoni hufanywa na wanawake.

Ukiachana na faida za samaki kama chakula katika kupatikana kwa virutubisho muhimu kama vitamini, protini na mafuta, zaidi, sekta ya Uvuvi na biashara ya samaki inachangia sehemu muhimu sana katika kuendesha maisha ya watu haswa vijana ikiwa watachukua angalizo katika fursa zilizopo kwenye sekta hio.

Changamoto; Je, kuna fursa zipi katika kufanya shughuli hii ya uvuvi na biashara ya samaki katika kukuza uchumi? Teknolojia ina mchango gani katika kuboresha uchumi wa mtu mmoja mmoja kupitia setka hii?

Tishio kubwa katika shughuli za uvuvi na biashara ya samaki ni athari zinazotokea katika mazalio ya samaki baharini, mtoni, ziwani au kwenye mabwawa. Umoja wa Mataifa na nchi  jumuishi duniani zimeingia uwoga juu ya upatikanaji wa hazina ya samaki katika soko la dunia. Shirika linaloshughulikia maswala ya Chakula duniani, FAO, limetabiri kwamba zaidi ya 70% ya aina (species) za samaki zinakaribia kuangamia au zimevunwa sana ambapo aina za samaki kama Tuna, Swordfish, Haddock na Flounder zipo katika tishio la kuangamia. Zaidi, uvuvi unaotumia chandarua au baruti huweza kusababisha kunaswa au kuuwawa kabisa kwa samaki na viumbe wengine wa baharini ambao hawajapangwa kuvuliwa kama ngasa, pomboo na papa.

Hata hivyo, shughuli za uvuvi zina faida gani katika maisha ya mwanadamu ikijumuisha?

  1. CHAKULA;  Samaki ni chanzo cha vitamini na protini katika lishe haswa ya mwanadamu ambapo madaktari na wadau wa sekta ya afya hushauri ulaji wa nyama nyeupe mfano samaki zaidi katika mlo. ulaji wa samaki kwa wingi huchochea ukuaji bora wa afya ya akili pamoja na wingi wa protini katika nyama hio huku ikiwa na kiasi kidogo cha lehemu (cholesterol) zaidi kuliko nyama nyekundu mfano ng`ombe, mbuzi na kadhalika.Ripoti zinaonyesha kwamba wakazi wa nchi za ukanda wa bahari ya Pacific peke yake hupata zaidi ya 25% na 69% ya protini za wanyama wanaokula kila siku kutoka katika samaki. Hii imepelekea shughuli za uvuvi na biashara ya samaki kukua kwa kiasi kikubwa kama shughuli rasmi ya kiuchumi ambayo imeajiri watu takribani milioni 200 dunia nzima na ikizalisha pato la dola za kimarekani zaidi ya 80 bilioni kwa mwaka.
  2. UKUAJI WA UCHUMI; Sekta hii ya uvuvi inachangia kwa kiasi kikubwa sana katika ukuaji wa uchumi barani Afrika mpaka dunaini kote ambapo watu zaidi wa milioni 200 wamejipatia ajira kupitia sekta hio. Nchini Uganda kwa mfano, uvuvi wa ziwani umekuwa na thamani ya zaidi ya dola $200 milioni  kwa mwaka ikiwa ni mchango wa 2.2% katika pato la taifa (GDP) la nchi hio. Vile vile watu zaidi ya 135,000 wamepata ajira kama wavuvi katika sekta hio na wengine 700,000 zaidi katika mchakato wa kuandaa samaki kabla hawajafikishwa sokoni na hivyo kuzalisha zaidi ya dola $87.5 milioni kama mapato ya biashara za nje ya nchi (exports earnings). Hapa miundombinu ya barabara na reli ina mchango mkubwa sana katika kuhakikisha kitoweo hiki kinamfikia mlaji kikiwa katika ubora wa hali ya juu. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa miundombinu pitia makala hii hapa;
  1. Vile vile nchini Tanzania kupitia katika mabwawa, maziwa, mito na bahari vilivyomo nchini humo, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki imetoa ajira za moja kwa moja kwa watu takribani 183,800 na wengine zaidi ya 4,000,000 wakijihushisha kama watengenezaji wa vyombo vya uvuvi (ngalawa, boti, ndoano, neti n.k), waaandaaji wa samaki kabla hawajafikishwa sokoni, wachuuzi na wafanyabiashara wa samaki wa jumla na rejareja. Sekta hii ya uvuvi na biashara ya samaki inawapatia watu kipato cha fedha za kigeni, pamoja na kitoweo kwa watu waishio pwani ya bahari ya hindi pamoja wa walaji wa samaki kutoka sehemu zingine katika nchi hio ambapo sekta hio huchangia katika pato la taifa takribani 2.4%. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi katika mwaka 2016.

Kiujumla, mpaka kufikia mwaka 2001 uta fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika katika masoko ya kimataifa ilikuwa na thamani ya dola $2.7 bilioni ambayo ni 5% ya jumla ya thamani ya sekta nzima ya uvuvi na biashara ya smaki duniani ambayo ni dola $56 bilioni. Kwa mujibu wa shirika la FAO, bidhaa za samaki zimejumuisha zaidi ya 10% ya jumla ya biashara za kimataifa (exports) katika nchi 11 barani Afrika.

Sasa Baada ya kuyajua Hayo Yote, Kwanini Ufanye biashara hii ya Uvuvi na samaki?

Mwaka 2019 watumiaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania waliongezeka kufikia milioni 23, ongezeko la watumiaji takribani milioni 1 kutoka mwaka jana 2018. Vile vile watumiaji wa huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi wamefikia takribani milioni 20 hadi kufikia mwaka huu 2019. Hii ni kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA.

Hivyo kupitia ripoti hio ya TCRA mfanyabiashara anaweza kuhamishia shughuli zake kupitia simu mkononi na simu janja (smartphones) katika kuhakikisha biashara yake inawafikia watu wengi zaidi katika muda mfupi kwa njia ya Teknolojia. Hata hivyo mfanyabiashara anaweza kutengeneza majukwaa ya kimtandao kama tovuti za kibiashara (online shops na ecommerce websites) ambayo anaweza kuuza bidhaa zake za samaki kirahisi katika masoko ya ndani na hata yale ya kimataifa kwa gharama nafuu zaidi kuliko ulivyokua hapo kabla.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Kwa kutambua hilo, biashara ya mtandaoni imekuwa ikizidi kufanikiwa sana nyakati hizi huku ikichochewa na maboresho katika miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji. Hivyo ni muhimu kufungua tovuti rasmi ya biashara yako ili kuipa utambulisho usio na shaka ukiwa mtandaoni. Vilevile ni muhimu kufungua akaunti za mitandao ya kijamii ili kusudu uzidi kujiweka karibu na wateja wako na kujua namna nzuri ya kuwahudumia.

Link zifuatazo zitakusaidia sana uweze fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika kupitia mtandaoni iwe na mafanikio zaidi na zaidi:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO

Je umepata nini katika mada ya leo katika ku fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-commerce BUSINESSES)?

Japokuwa imechelewa, lakini kwa sasa Africa ndio inaongoza mbio katika kufanya mapinduzi ya kidijitali kuliko sehemu yoyote duniani. Namna ya kufanya biashara inazidi kubadilika ikionyesha nia ya dhati kufanya maendeleo ya kiuchumi, miundombinu na maswala ya kijamii. Mwaka 2018 nchi wanachama wa Umoja wa Africa walipiga hatua kubwa katika mfumo wa kufanya biashara na muingiliano wa kiuchumi baada ya kuanzisha Eneo Huru la Kufanyia Biashara barani (Continental Free Trade Area AfCFTA). Eneo hili lililoanzishwa linashirikisha nchi 22 zilizoweka sahihi tayari na utekelezwaji wake ulipangwa kuanza mwaka 2019 (tayari umeshaanza).

Hata hivyo mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuzishirikisha nchi ambazo bado si wanachama wa eneo hili jipya, inatarajiwa eneo hili kufikia soko la watu takribani bilioni 1.2 barani wakiwa na jumla ya pato la ndani la taifa (GDP) la dola za kimarekani trilioni 2.5 kwa pamoja, kwa mwaka. Hii inatarajiwa kuwa ni mapinduzi makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nyanja ya uchumi wa Afrika.

Sasa, swali linakuja; Afrika(wafanyabiashara, makampuni/mashirika na Serikali) imejiandaa vipi na mapinduzi haya ya uchumi wa kidijitali? Na zaidi, watunga sera/sheria wataangalia vipi biashara za kielektroniki (e-commerce) kama mada muhimu katika eneo hilo jipya la kufanya biashara huru barani?

Tume ya kudhibiti uchumi wa Africa ya Umoja wa Mataifa (ECA) ikishirikiana na Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) pamoja na Baraza la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo ya kibiashara (UNCTAD) mwaka huu 2019 imechapisha ripoti yake ikiangazia maendeleo ya Afrika kiujumla katika nyanja za kiuchumi, siasa na kijamii.

URAHISI: Imeonekana kwamba e-commerce inaweza kufanya biashara ya bidhaa na huduma kwa urahisi zaidi ambapo itarahisisha mwenendo mzuri wa biashara kati ya wazalishaji, wafanyabiashra na walaji pamoja na kumbukumbu zao na miamala ya kifedha.

MITANDAO YA KIJAMII: Pia imeonekana kwamba e-commerce inapatikana na kufanyika kirahisi katika mitandao ya kijamii kama facebook na Instagram ambapo ndipo mahali kuna watumiaji wengi zaidi wa Intaneti duniani (zaidi ya watu bilioni 2 kati ya watumiaji bilioni 4 wa intaneti).

KUTOKUWA NA MIPAKA: Mfumo wa uchumi wa Kidijitali kiasili umetengenezwa kuepuka mipaka ya kijiografia katika kufanya biashara na kubadilishana fedha ambapo mabadiliko haya ya kiteknolojia yataongeza umakini zaidi katika mwenendo wa masoko na gharama. Lakini bado wimbi kubwa la watu watakaoshiriki kwenye soko barani wanaonekana wataachwa nyuma kutokana na kutokuingiliana kwa lugha na vita/ghasia za mara kwa mara katika baadhi ya jamii/nchi.

BIASHARA: Kwa mujibu wa UNCTAD mwaka 2016 kwa dunia nzima e-commerce iliweza kupitisha mauzoya takribani dola trilioni 26 ambapo 90% ilikuwa ni Biashara kwa Biashara (B2B e-commerce) na 10% ilikuwa ni Biashara kwa Mlaji (B2C e-commerce). Hata hivyo kupima mwenendo wa e-commerce katika baadhi ya nchi zinazoendelea imekuwa ni changamoto kupata data na takwimu, haswa katika nchi za Afrika.

IMPORTATION: Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kwamba Biashara kati ya nchi na nchi imekua kwa kiasi kikubwa Afrika ambapo zimechagizwa na vituo vichache vya kiteknolojia (Hubs) ambavyo vimerahisisha mno mwenendo wa biashara. Biashara kati y nchi na nchi (Intraregional import) imekuwa zaidi ya mara 3 katika miongo miwili iliyopita kufikia 12%- 14% sawa na dola bilioni 100 ikichagizwa na uwepo wa jumuiya za kiuchumi barani (Subregional Economic Communities REC‘s).

UZOEFU: Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na umri wa Jumuiya hizi za Kimaendeleo barani Afrika ambapo uzoefu huo hutumika kuongeza jitihada katika kuboresha namna ya ufanyaji biashara kuelekea uchumi wa kidijitali kiteknolojia. Uzoefu huo pia hutumika kuunganisha jumuiya moja na nyingine (mf, SADC na COMESAna EAC) ambapo zitazalishwa nafasi nyingi zaidi za kufanya biashara kati ya nchi wanachama na ripoti zinaonyesha 75% ya biashara hizi ndani ya jumuiya barani Afrika zimefanyika mwaka 2017 peke yake na nusu ya biashara hizo zilifanyika katika jumuiya ya SADC.

Chini ya mwavuli wa AfCFTA nchi wanachama zinatarajia kufuta tozo/ushuru kwa 90% ya bidhaa zote zitakazopitishwa na kufanyiwa biashara katika eneo hilo. Hii itaruhusu uwezekano wa kupunguza mlolongo wa kodi au kuongeza idadi na thamani ya bidhaa na huduma zitakazohusishwa. Matokeo yoyote katika punguzo hilo linalotarajiwa katika muktadha wa biashara kidijitali yataleta picha tofauti. Kupunguza mlolongo wa tozo za mipakani baina ya nchi na nchi kutapungua kwa 15% pekee ikitegemea thamani ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi husika. Hii ni kwa mujibu wa Tume inayoshughulikia Uchumi wa Afrika kutoka Umoja wa Mataifa (UNECA) mwaka 2018.

Sasa mwaka 2018 Jumuiya ya COMESA ilibuni mfumo wa kudhibiti eneo huru la kibiashara kidijitali (Digital Free Trade Area DFTA). Mfumo huu umeundwa na mambo yafuatayo;

•E-trade: Hili ni jukwaa mahsusi kwa ajili ya kufanya biashara za kimtandao na kuwezesha malipo ya kielektroniki, mobile apps kwa ajili ya wafanyabiashara walioko katika Jumuiya hio.

•E-logistics: hili ni jukwaa maalum kwa ajili ya kuwezesha biashara ya usafirishaji wa mizigo baina ya nchi wanachama wa jumuiya.

•E-legislation: huu ni mfumo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara rasmi ambao unawawezesha kufanya miamala na malipo kielektoniki.

Mfumo huu uliobuniwa na Jumuiya ya COMESA umelenga kutangaza biashara za wanajumuiya katika nchi wanachama ikijumuisha kupitia majukwaa ya e-commerce. Mfumo huu ulikuwa ni mfanano wa mfumo uliotengenezwa na kuzinduliw na nchi ya Malaysia mwaka 2017 katika muktadha wa kufanya biashara huru ndani ya eneo maalum.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.

Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana, shuka nazo:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-biashara-ya-fedha-za-kidijitali-cryptocurrency-business/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)”
  2. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia;

e-mail: info@rednet.co.tz

tovuti: https://rednet.co.tz

Simu:+255765834754