Tag: cyber

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE

Yaani ni 8% tu ya makampuni ndio wana uwezo wa kugundua wizi wa taarifa zao ndani ya dakika chache. 62% wanaweza kugundua wizi ndani ya siku kadhaa. Wewe unatumia muda gani kugundua upotevu/wizi wa data katika kampuni yako? Makala hii tutaangazia mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) kiundani. Leo, yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake. Makinika mpaka mwisho.

Kama Unavyoona biashara zinavyozidi kushamiri kiteknolojia ndivyo wadukuzi nao wanazidi kutafuta mbinu za kufanya mashambilizi zaidi. Mwaka 2019 peke yake, zaidi ya 2$ billion zilipotelea mikononi mwa wadukuzi duniani. Utafiti wa Juniper unaonesha namba hio inaongezeka kila mwaka.

Unalikumbuka shambulizi lilioitwa NotPetya? Basi jarida la WIRED linalitaja shambulizi hilo kama “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA”. Ndani ya masaa machache tu virusi vya shambulio hilo (malwares) viliathiri kutoka biashara ndogo za Software nchini Ukraine mpaka kusambaa katika vifaa vya kielektroniki dunia nzima. Shambulizi lilidhoofisha mashirika makubwa duniani kama FedEx, TNT, Express na Maersk kwa wiki kadhaa na kusababisha hasara ya zaidi ya $10 bilioni kwa ujumla. Upotevu wa data kwa kiwango hiki unaonyesha namna katili ya dunia tuishiyo ambapo inaonekana hakuna mwenye kinga madhubuti mtandaoni. Kutoka Mashirika makubwa, serikali, mitandao ya kijamii, mifumo ya migahawa na sehemu yoyote unayojua inatumia teknolojia ya IT, Kila mmoja yupo hatarini.

TUMEFIKAJE HAPA?

Ripoti ya mwaka 2019 ya shirika la Accenture Security kuhusu Matishio ya kimtandao (Cyber Threatscape), imeonyesha sababu za wadukuzi kuendelea kuwa tishio dhidi ya taarifa binafsi/za mashirika kwa manufaa yao. Hizi ni baadhi sababu hizo:

1. Wadukuzi wa kimtandao hufaidika zaidi na teknolojia mpya na kukosekana mawasiliano madhubuti katika sheria na tawala za maeneo/nchi mbalimbali duniani.

2. Mitandao ya kihalifu muda wote inakwenda ikibadilika, hasa kuelekea katika makundi ya kihalifu ya siri (syndicates) pasi na kujulikana chanzo chake kwa kutumia nyaraka halali kwa nia halifu.

3. Malengo mseto katika kuimarisha tabia za virusi (kama kujiendesha vyenyewe: self replication)

4. Kuimarika kwa mifumo ya Ulinzi wa Kimtandao (cybersecurity hygiene) inapelekea wadukuzi nao wazidi kujiimarisha kimbinu na maarifa katika uwanda wa kiteknolojia na matumizi ya internet.

Baada ya kujua sababu zinazowasukuma Wadukuzi na wahalifu wa Kimtadao kuendelea kufanya mashambulizi, Leo, uta yafahamu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako, Fuatana nami..

Duniani kunazo aina nyingi za mashambulizi ya kimtandao kulingana na sababu nilizozieleza hapo juu kama ifuatavyo:

1. RANSOMWARE ATTACK: Katika shambulio hili, virusi maalum (specific malware) ambavyo hukusanya na kufunga taarifa/kifaa katika mtandao ili kumnyima mtumiaji haki na uwezo wa kufanyia kazi taarifa zake kama kawaida. Haki na uwezo (access) huo humrudia mtumiaji pale tu matakwa ya mdukuzi yatakapotimizwa ambayo mara nyingi huwa ni pesa au rushwa kwa mapana yake.

Saa ingine wadukuzi wanaweza kugoma kurudisha haki za matumizi kwa mhusika hata wanapotimiziwa matakwa yao, hivyo kuongezea hasara kwa kampuni/biashara. Mbaya zaidi, ripoti ya mwaka 2019 ya Uhalifu wa kimtandao inaonyesha kutokea kwa shambulizi hili kila sekunde11 ya mwaka 2021.

2. ADVANCED PERSISTENT THREATS (APT): Shambulizi hili sio la mojakwamoja (passive attack) ambapo mdukuzi anapata access ya computer/mtandao fulani kwa muda mrefu pasi na kujulikana, hivyo kujichotea taarifa na kuzitumia kwa manufaa yake. Aina hii pia huitwa Trojan Horse attack.

3. PHISHING: Je wajua? Mpaka 32% ya wizi wa data husababishwa na shambulizi hili. Hii ni aina ya shambulizi maarufu sana la kijamii (social engineering) ambapo mdukuzi humtegea mtu adownload file lililo na virusi kupitia SMS, email au link na kuingiza virusi katika kifaa chake.

unawezaje kujilinda dhidi ya shambulizi la kimtandao la phishing katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

4. SQL INJECTION: Umeshawahi kuona ile unaingia kwenye website ukakuta haipo ghafla tu, au kwenye system flani unanashangaa kuna mafiles huyaoni bila sababu ya msingi. Sasa kwa kutumia virusi halifu (malicious codes) shambulizi hufanyika katika servers zinazohifadhi taarifa muhimu za watumiaji na kuzifuta, kuziiba au kuzibadili ili kutimiza azma fulani ya wadukuzi na/au genge lao. Mara nyingi shambulio hili hufanyika kwenye servers zinazohifadhi taarifa ghafi za watu au vitu (personal identifiable information: PII) kama namba ya kadi, username and passwords.

5. DDOS ATTACK: Kirefu huitwa Distributed Denial of Services attack ambapo hutokea pale wadukuzi wanapofurika tovuti au kifaa chako kwa either kupunguza au kondoa kabisa utendaji wa kawaida na hivyo kuiacha kampuni/biashara kuhangaika kurejesha performance ya mifumo yake wakati wao (wadukuzi na virusi vyao) wakitumia mwanya huo kuiba na kufanya uhalifu katika mifumo hio iliyoathirika.

6. MAN IN THE MIDDLE (MITM): Hii hutokea pale mdukuzi anapoingilia mawasiliano halali ya kampuni bila ya wao kujua. Pia shambulio hili hufahamika kama eavesdropping pale linapofanyika baina ya mawasiliano binafsi ya simu kati ya mtu na mtu.

Mawasiliano katika MITM hiungiliwa pia kupitia APN za Wi-Fi za uongo (deceptive wifi). Zaidi ya kuingilia mawasiliano, hapa mdukuzi anaweza pia kuwasiliana akitumia utambulisho (ID) ya wahusika pasi na kufahamika mara moja.

7. PASSWORD ATTACK: Licha ya kuwa shambulizi maarufu zaidi duniani, bado kuna watu huangukia mtego wa kuibiwa nywila zao. Kwa urahisi wake, wadukuzi hutumia mbinu zenye viwango na ujanja kupata nywila dhaifu na kufungua accounts za watumiaji kirahisi. Hapa tunaangukia kwenye usalama wa vifaa vyetu vya mtandaoni. Je viko salama kiasi gani? Fuatana na makala hii hapa kufahamu zaidi..

UNAWEZAJE KUZUIA MASHAMBULIZI HAYO?

Katika yetu iliyopita tumeeleza kwa kirefu kuhusu namna ya kujiepusha na mashambulizi ya kimtandao (Cyber attacks), pitia hapa KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?“. Leo pia, tutaona njia zingine za kuendelea kujiimarisha na kuzuia mashambulizi hayo yasiathiri Biashara/Kampuni yako. Mashambulizi mengi niliyoyaelezea leo yanazuilika kwa njia ambazo tayari tulishaziona katka makala zilizopita isipokuwa:

MITM Attack: •Tumia SSL Certificates za (https) katika website yako. Hii ni boresho la http SSL certificate ambayo ni ya zamani na usalama wake mi mdogo.

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

•Tengeneza VPN yako kama ngao ya ziada dhidi ya wi-fi halifu (deceptive wi-fi). Mashambulizi haya katika biashara yako yana madhara makubwa ikiwemo Kupotea kwa Fedha, faida ya biashara, mauzo, matengenezo, Hadhi ya biashara kushuka au kupotea kabisa na madhara ya kisheria.

Hivyo unapaswa kuwa makini na kufuata ushauri wa kitaalamu kuhusu maboresho ya kimtandao (updates & maintenance) ili kuhakikisha unatumia teknolojia ya kisasa zaidi ambayo ni salama huku ikiwa imeambatana na Passwords zako zilizo bora. Utajuaje kama simu/computer yako ikiwa imedukuliwa? Majibu tayari yanapatikana kwenye makala iliyo hapa UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?.

Usalama wa Kimtandao ni jukumu langu. Ni jukumu lako. Ni jukumu letu sote. Tuchukue tahadhari muda wote tuwapo mtandaoni. Basi ni matumaini yangu leo mengi umeyafahamu kuhusu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako. Ukiwa na swali au nyongeza tafadhali tuandikie katika comments hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo? Umejifunza nini katika ku yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake katika biashara/kampuni yako.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Unawezaje kujikinga dhidi ya mashambulizi ya kimtandao katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?

Imeibuka kuwa issue muhimu sana ya kuzingatia katika zama hizi za kiteknolojia ambapo kumekuwepo na wimbi la mashambulizi ya kimtandao kwa watumiaji duniani kote. Kama unatumia Android, iOS, Windows7, 8, 10, Ubuntu na OS zingine unazozijua basi fahamu tayari upo katika hatari ya kushambuliwa na wadukuzi wenye nia ovu na uhalifu katika kuiba taarifa zako, mali na hadhi yako katika jamii inayokuzunguka. Sasa utafanyaje ili ujikinge na hatari za mashambulizi hayo? Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako? Fuatana nami leo mpaka mwisho nitakufahamisha.

Mwaka 1988, Robert Morris akiwa nguli wa mitandao alitengeneza shambulio la kimtandao lilioitwa CHRISTMASS TREE WORM katika internet ambapo mifumo zaidi ya 2000 iliharibika na computer zaidi ya 6000 ziliathirika kwa siku moja tu nchini Marekani. Kwa kuwa alikua ni afisa wa Shirika la NSA (National Security Agency) alikamatwa na kupigwa faini ya 10,000$.

Japokuwa faini ilionekana ndogo kwake lakini dunia ilipata funzo muhimu sana kuhusu Usalama wa Data za watumiaji wa internet wawappo mtandaoni. Hata hivyo, katika muongo wa 1980’s mpaka 1990’s, wadukuzi wa mitandao Hawakuwa tishio sana duniani moja ya sababu ikitajwa ni kutokuwa na matumizi makubwa ya internet na kuwa na watumiaji wachache.

Lakini mambo yalikuja kubadilika mwishoni mwa miaka ya 1990’s na mwanzoni mwa 2000’s ambapo Udukuzi ulianza kutumika kama biashara na kuwa silaha ya kimbinu Katika idara mbalimbali za kiserikali, kibiashara au kibinafsi ambapo ujasusi wa taarifa umechochea kwa kiasi kikubwa katika kutafuta, kuchakata na kutumia taarifu mbalimbali kwa manufaa ya kiuchumi au kibinafsi..

Wanafanyaje Mpaka kuifikia Computer/kifaa chako? Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

Mashambulizi haya ya kimtandao yalianzia katika matukio ya Uhuni wa mtaani katika kuibiana taarifa, mpaka kufikia Oparesheni za kidunia zinazohusu Mashirika makubwa, majeshi, Idara za kiresikali na Magaidi. Mwaka 2008, Mike Cloppert mchambuzi wa mifumo ya kimtandao aligundua na kubaini mbinu wanazotumia wadukuzi katika kufanya misheni zao ambazo aliziweka katika utaratibu huu.

1. Reconnaissance (Utambuzi, Ufahamu)

2. Weaponization (matumizi ya silaha)

3. Delivery (jinsi ya kufikisha Botnet, virusi kwa victim)

4. Exploitation (uvunaji wa taarifa za muathirika)

5. Installation (jinsi botnet na malwares zinafanya kazi katika kifaa chako)

6. Command and Control

7. Actions (athari za udukuzi katika kifaa chako)

Tuiruke hatua ya kwanza as inaeleweka kirahisi, WEAPONIZATION au matumizi ya Silaha sio lazima mara zote silaha iwe Bunduki na Mabomu. Silaha muhimu inayotumika ni Software za kidukuzi (Malwares, Botnets nk). Kuna kisa kilionekana katika mtandao wa twitter kuhusu “wakala wa simu na mtu mmoja“.

Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

Hizi Malwares zinamfikia victim/target kupitia picha, USB, email, pdf au link iliyobeba Botnets ambazo hudukua taarifa muhimu katika kifaa cha victim (DELIVERY). Shambulizi hili huitwa Phishing. Wadukuzi hupendelea kununua hizi Malware katika masoko yasiyo rasmi mtandaoni (black market). Baada ya Botnet kuingia katika kifaa cha Victim huanza kufanya kazi pasi na idhini au ufahamu wa mtumiaji ambapo huvuna taarifa nakuzituma kwa wadukuzi muda wowote watakaohitaji taarifa hizo automatically(EXPLOITATION AND INSTALLATION). Taarifa hizo zinazoibiwa humuathiri kwa kiasi kikubwa mtumiaji ambaye hana ufahamu wa shambulizi katika kifaa chake, jambo linaloweza kumfanya akapoteza fedha, taarifa muhimu na mali (COMMAND, CONTROL AND ACTIONS). Sasa Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

UFANYEJE SASA ILI USALAMA WA KIMTADAO UWE MUHIMU KWAKO?

Hakikisha kifaa chako kipo salama muda wote. Tumia password bora. Hakikisha password unayotumia inajumuisha mambo yafuatayo: Herufi ndogo, herufi kubwa, namba pamoja na alama za uandishi. Mfano wa Password bora unaweza kuwa (HJas876?2). Somo la Password nimelielezea kwa kirefu kupitia link HIFADHI MBADALA YA NYARAKA. Pia, epuka kushiriki matumizi ya kifaa chako na watu wengine.

Lakini zaidi epuka kutembelea tovuti usizozifahamu ambazo zinaweza kubeba shambulizi. Lakini zaidi Epuka kufungua email kutoka kwa mtu usiyemfahamu au ambaye hujawahi kufanya nae mazungumzo kabisa. Email za wadukuzi zinaweza kuja kama email ya kawaida tu lakini imebeba Malwares ambazo hutajua zimeingia sangapi kwenye kifaa chako Ukihisi kwamba kifaa chako kimeingiliwa na Malwares au Botnets, kwanza Hutakiwi kupanic. Fanya yafuatayo ili kuhakikisha unabaki kuwa salama:

1. Tumia Antivirus Software katika kifaa chako: Hapa sizungumzii zile antivirus za kudownload, Antivirus bora kanunue dukani ikiwa mpya kabisa. Kwa 95% antivirus huzuia mashambulizi yanayokuja katika mfumo wa Spywares and Adwares (Pop ups), virus, Botnets. Ili kuongeza ubora katika utendaji wa Antivirus yako, hakikisha unaiUpdate mara kwa mara kupata latest security protocols katika kifaa chako.

2. Matumizi ya Windows Defender (WD): Kama unatumia computer yenye OS ya windows make sure Windows Defender yako ipo ON in Real Time protection na Automatic Updates zipo ON kama inavyohitajika.

Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako?

3. Pia hakikisha FIREWALLS zako zipo ON and active: Hizi ni security protocols zinazozuia any software Au App ambayo haitambuliki na Watengenezaji wa Windows OS kama Activators, Softwares from Unrecognized sources n.k Kama Firewalls zako zipo okutaona ukiweka any mentioned Software inaliwa hapo hapo. Kupitia LINUX OS, Iptables firewalls hutumika na zinafanya kazi just like windows

4. Matumizi ya VPN Virtual Private Network (VPN): Ni mwamvuli wa kimtandao unaokuwezesha kutumia huduma za internet bila kufuatiliwa na either Mtoa huduma wako (Network Operator) au mashirika ya kiserikali. VPN inakufanya uwe free kufanya shughuli zako katika usalama zaidi Si watu wote wana uwezo wa kumiliki/kutumia VPN’s, lakini kwa matumizi binafsi na salama zaidi mtandaoni, huna budi kutafuta VPN yako ili kujilinda.

NOTE: Usalama wako na kifaa chako katika huduma za internet mtandaoni unaanza na wewe mwenyewe. Hakikisha kifaa chako ni chako. Umejifunza jambo katika makala haya kuhusu Kwanini usalama wa kimtandao (cyber security) ni muhimu kwako? Tafadhali tujulishe na sambaza kwa mwenzako ili kuhakikisha makala haya yanawafikia watu wengi zaidi.

Kuhusu usalama uwapo mtandaoni nimeshakuwekea makala zingine kupitia links hizi hapa chini:

  1. UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?
  2. YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE KATIKA BIASHARA/KAMPUNI YAKO