Tag: cryptocurrency

mapinduzi ya viwanda

FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA 4 YA VIWANDA KATIKA BIASHARA DUNIANI

Japokua ilipitwa na zama 3 tayari, lakini sasa Afrika imedhihirisha kwamba haitaki kupitwa tena katika Mapinduzi ya 4 ya viwanda Duniani. Hii ni kutokana na kukua na kuimarika katika sekta za Afya, Elimu, Biashara, Teknolojia pamoja na Mahusiano na Muingiliano wa kijamii ikichagizwa na maendeleo katika miundombinu, usafirishaji na mitandao ya kijamii. Leo tuta fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. Ni nini na yanaashiria nini kwenye maendeleo ya biashara zingine? Makninika mpaka mwisho.

Mwezi September, 2019, jijini Cape Town Afrika Kusini ulifanyika mkutano wa kiuchumi wa WEF (World Economic Forum) ambao unazishirikisha nchi mbali mbali duniani, wafanyabiashara pamoja na wadau wa uchumi.

Mwaka huo 2019 viongozi waliokutana kujadili mustakabali wa Afrika walikua na jambo la msingi sana ambalo linatumainiwa kuleta maendeleo katika uchumi barani ambalo ni Utekelezaji wa Kuanzishwa kwa Eneo Huru la Biashara Barani (African Continental Free Trade Area AfCFTA). Baada ya miaka mingi ya mazungumzo, makubaliano yamefikiwa ya jinsi ya kuvunja vikwazo vya kibiashara, kukuza uchumi na kuunganisha nchi ambazo katika historia zilikuwa na mahusiano mazuri ya kibiashara na bara Ulaya, Amerika na Asia. Kufahamu zaidi gusa hapa chini:

Changamoto; Afrika (wafanyabiashara, kampuni na mashirika) imejifunza nini katika Kongamano hilo la Kiuchumi (WEF)? Na zaidi, Afrika inajiandaa vipi na Mapinduzi ya 4 ya viwanda yanayoendelea duniani?

Kufikia mwaka 2018 Afrika peke yake iliripotiwa kuwa na vijana takribani milioni 200 wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24. Na namba hio inatajwa kuongezeka mara mbili kufikia mwaka 2050.

Sasa “Kuwa na bara lililosheheni vijana ni fursa adhimu sana, lakini vile vile ni tishio kubwa.” alitahadharisha Albert Zeufack, Mchumi Mkuu wa Benki ya Dunia barani Afrika. “Ni tishio kama hatutohakikisha idadi hio ya vijana hawaanzi kufanya kazi inavyotakiwa.” Sasa kufikia Mapinduzi ya 4 ya viwanda, maeneo kadhaa yaliangaziwa na kituo cha mabadiliko ya kiuchumi barani (Africa Center for Economic Transformation, ACET) kwa niaba ya Benki ya maendeleo barani AfDB.

africa na mapinduzi ya viwanda

1. MACHINE LEARNING/ARTIFICIAL INTELLIGENCE/ROBOTICS;

Fikiria kuhusu gari inayojiendesha bila dereva na kufuata sheria na alama za barabarani ipasavyo ikijumuisha foleni. Watu wengi wangesita kupanda katika gari inayojiendesha yenyewe bila dereva, lakini hayo ndio mapinduzi halisi ya viwanda kupitia teknolojia.

Pia eneo hili limeshuhudiwa na ubunifu mwingi ukiwemo; mashine za kisasa za kuvuna na kupembua nafaka na madini, mifumo ya kiautomatiki inayoendesha ndege, meli pamoja na Teknolojia ya kupima udongo. Ni wazi mashine zinaweza kufanya kazi zifanywazo na binadamu katika zama hizi za mapinduzi ya 4 viwanda.

Swali, umejiandaeje kulinda taaluma yako dhidi ya zama hizi za mashine kujifunza (machinelearning) pamoja na teknolojia ya akili isiyo ya asili (ai)?

2. INTERNET OF THINGS (IoT);

Vifaa vingi vya kielektroniki vinavyotumiwa na mwanadamu sasa vinao uwezo wa kuingiliana na vifaa vingine kirahisi katika kurahisisha utendaji. Fikiria pale unarudi nyumbani na kuwasha feni yako kwa kutumia simu yako ya rununu (smartphone). Au kuweza kuendesha jokofu lako kwa kutumia teknolojia ya RFID. Kuunganishwa vifaa vya kielektroniki na huduma za intaneti imerahisisha sana mfumo wa mawasiliano na manunuzi ambao umeinua uchumi japo faida zake bado hazijasambaa sana barani Afrika.

Fikiria vile unaweza nunua bidhaa katika duka bila kumwona hata muuzaji. Hii inawezeshwa na teknolojia za biashara za kielektroniki (ecommerce) ambapo mteja anaweza kulipia kwa kutumia kadi yake ya benki au huduma za kifedha za simu ya mkononi kama MPESA na tigopesa. Katika bara ambalo muingiliano ni mkubwa kama Afrika, hili ni jambo la kutilia maanani sana, haswa wakati huu ambapo unajaribu ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani. (Ambapo sisi kama Rednet Technologies ni wadau wakubwa kuhakikisha hupitwi na huduma za kisasa kwa kutumia teknolojia).

Kufahamu mapinduzi ya IoT katika biashara na maisha kwa ujumla tayari tumekuwekea makala maalum kupitia link hii hapa MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA

3. DATA MINING/DATA SCIENCE TECHNOLOGIES;

Kituo cha ACET katika mwaka 2018 kiligundua kwamba “kuvua taarifa nyingi mtandaoni, kwa kutumia kompyuta zenye uwezo mkubwa na kanuni za mifumo ya Akili isiyo ya Asili (AI), huwezeshwa kupatikana kwa ripoti bora ya taarifa sahihi.” Fikiria mifumo ya tiketi za ndege, hoteli, mifumo ya kulipa kodi na taarifa za mteja wa benki.

Sekta ya Takwimu inafurahia sana ujio wa teknolojia ya Kuvua/Kuvuna Taarifa na Sayansi ya Taarifa. Jinsi ya utendaji katika teknolojia hii ni fursa adhimu sana katika kuimarisha biashara kwa kutumia takwimu sahihi zilizovunwa kutokana na taarifa mbalimbali za watu. Mifumo ya tiketi za ndege, Usajili wa vyumba vya Hoteli, taarifa za wateja wa benki na hata mfumo wa Kulipa kodi (Tax returns), hivi ni baadhi ya vyanzo vya ukusanyaji wa taarifa muhimu katika kufanya Uvunaji wa Data na Sayansi ya Data. Serikali za Africa zinamiliki kiwango kikubwa cha taarifa hizi. Je, italeta manufaa kwa Umma au itafanywa kama biashara na wajasiriamali? (Tafiti na ripoti tunazokuwekea kwenye makala zetu hizi zitakupa majibu.😋)

4. 3D PRINTING;

Ama kwa hakika mapinduzi ya viwanda yanakuja na mengi. Hebu buni bidhaa yako kwenye kompyuta halafu ichapishe kama ilivyo. Kutoka ubunifu uliotengenezwa kimchoro mpaka uhalisia katika kuchapisha tu, hii inakwenda kubadili hata namna ya uendeshwaji wa viwanda barani Africa ambapo ugunduzi huu unaleta matumaini katika uwanda wa ubunifu na ujenzi ambao unatazamiwa kuleta maendeleo katika nchi za Afrika. Viwanda vinawezaje kuendana na teknolojia hii ya Uchapishaji? Vimal Shah mkuu wa shirika la viwanda vya BIDCO nchini Kenya mwaka 2017 alinukuliwa akitania, “Tunaweza kuchapisha pizza wakati ujao.”😂

Sasa watunga sera na sheria barani walishaona uhalisia huu kama kuchapisha mfano wa kitu halisi (3D-Printing) katik mipango yao ya muda mrefu?

5. BLOCKCHAIN/TRUST TECHNOLOGIES;

Mwaka 2018 kituo cha ACET kiligundua kwenye uchunguzi wake kwamba teknolojia ya Blockchain inawafanya watu hata wasiaminiana au kujuana, kuweza kushirikiana bila ya kuwa na haja ya kwenda kwenye mamlaka za serikali. Yaani Blockchain ni jalada huru linalosajili miamala ya kifedha kati ya watu wawili au zaidi kwa usahihi na njia bora zaidi. (Tulishaelezea kuhusu Blockchain na cryptocurrencies kwenye makala zetu zilizopita). Sasa itakuaje kwa huduma za kibenki, wanasheria, wakala wa fedha (brokerage firms) na wahusika wa kiserikali katika maswala ya kifedha? Kitawakuta nini, tutajadili kwenye athari ya mapinduzi ya viwanda mbeleni.

mapinduzi ya viwanda

Si ajabu, teknolojia ya Blockchain inaonekana kama mkombozi dhidi ya vitendo vya Rushwa kutokana na undeshwaji wake ulio sahihi na wa haki. Kwa inavyoonekana teknolojia hii ya Blockchain inakwenda kuwa pigo kubwa kwa watu wenye misuli ya kiutawala, madikteta wa waendeshaji wa siasa chafu. Itakapofika siku Teknolojia hii imefikia matumizi yale yaliyonuiwa wakati inaanzishwa, basi wahafidhina na mawakala wa kifedha wa serikali na mashirika binafsi watapoteza nguvu zao. Hakutakuwa na haja ya mihuri, wala sahihi, wala zile nenda urudi kesho tukuhudumie. Blockchain itakwenda kuiweka Afrika huru dhidi ya kero za huduma za kifedha na usalama wake kuwa katika ukuaji mzuri. Haya ndio mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani.

5. BIOPHYSICS AND BIOENGINEERING;

Eneo la 5 ambalo kituo cha ACET imeliacha ni kuhusu mtandao wa mifumo ya kibaolojia na kifizikia. Utahitaji mkono wa bandia unaoweza kuendeshwa na ubongo wako kwa usahihi ikitokea mkono wako halisi umekatika? Hebu fikiria hapo. Tunakubali kwamba asili ni bora sana kuliko sisi, hivyo ni bora kujifunza kwayo, kwasababu mapinduzi haya ya viwanda kwa kuchagizwa na ukuaji wa kiteknolojia duniani yatafanya taaluma ziweze kunyumbulika kwa namna nyingi sana hapo baadaye. Je, mifumo ya elimu imejiandaa na hili katika maandalizi ya mitaala yake ya muda mrefu?

Sasa tumeshajua yanayokuja na Mapinduzi ya 4 ya viwanda duniani. Afrika, bara ambalo ajira bado ni tatizo kubwa kwa vijana, wataweza vipi kupambana na athari za mapinduzi haya? Kuna nadharia tatu (3) katika kukabiliana na hali hii;

1. Afrika inaweza kuketi chini na kubaki kutizama dunia nzima ikipambana katika Mapinduzi haya. Hii ilishafanyika katika zama 3 zilizopita za Mapinduzi ya viwanda ambapo Mapinduzi ya Kwanza yaliegemea katika kutengeneza mifumo ya Kimekanika na matumizi ya Injini za mvuke katika kutengeneza bidhaa kama nguo.

Mapinduzi ya pili yakiwa ni kuhamasisha Uzalishaji mkubwa (mass production) wa bidhaa viwandani yakichagizwa na Henry Ford na awamu ya 3 ya mapinduzi ikiwa ni zama za kidijitali katika uzalishaji.

Ukitizama elimu ya msingi ya kuunda Injini ni ile ile iliyokuwepo tangu mwanzo, lakini bado Afrika haijaweza kutengeneza magari yake yenyewe.

2. Afrika inaweza kufanya kile ilichokifanya katika kuingia kwenye zama za Kidijitali, mtindo wa kuruka kama chura (leapfrog). Kwa mfano nchini Kenya watu hawakuwa na huduma za simu za mezani miaka ya 1990’s kurudi nyuma, hali kadhalika ilikuwa hivyo nchini Tanzania pamoja na nchi nyingi za kusini mwa jangwa la Sahara katika ku fahamu kuhusu Mapinduzi ya 4 ya viwanda katika biashara duniani.

Lakini baada ya mwaka 2000 watu wengi katika eneo hilo wameweza kumiliki simu za mkononi hata kama hawakuwahi kumiliki simu za mezani. Simu za mkononi zimekuja na teknolojia kubwa zaidi baada ya kuunganishwa na huduma za kifedha kama MPESA, huduma za internet, GPS na ramani, huduma za kiafya pamoja na biashara za kielektroniki ecommerce.

Mazingira ya Uchumi jumuishi (social economy) yanafanya iwe rahisi kukaribisha zama za Mapinduzi ya 4 ya viwanda. Watu wengi duniani hawapendi kusoma vitabu, hivyo sasa tunaweza kuziachia mashine kufanya kazi mbalimbali badala yetu. Kama Blockchain inatazamwa kwenda kuangamiza kabisa changamoto ya rushwa, Teknolojia ya 3D-Printing itafanya hata nyumba zetu kuwa viwanda vidogo katika kubuni bidhaa mbalimbali.

Taarifa zote zilizo kwenye mashirika ya Serikali na binafsi ikijumusha taasisi za dini zinaweza kuvunwa kwa ajili ya kupata takwimu mbadala katika chunguzi mbalimbali. Hii inatazamwa kuwa njia mbadala kuyafikia mapinduzi ya viwanda ya 4. Unahitaji kuLeapfrog biashara yako (kuepuka gharama kubwa za matangazo)? Tunalo suluhisho, wasiliana nasi mara moja tukupatie.

3. Vile vile, Afrika inaweza kukuza thamani ya uzalishaji na ubunifu wake ili kuwa mshindani halisi duniani katika kutengeneza na kusambaza bidhaa na huduma za kiteknolojia, kama inavyofanyika mahali kwingine duniani.

Japan imeweza kufanya hivyo katika sekta ya magari na India inafanya vizuri katika sekta ya Famasia na Programu za Kompyuta. Sasa kwanini Tanzania isiwe kinara katika Sayansi ya Data(Data Science) duniani. (maana mbongo mpe picha tuu, vingine utaona atakapovipata😂. Natania.) Sekta hizi za teknolojia zinataka matumizi ya akili zaidi, sio kama viwanda vya saruji na chuma ambavyo vinahitaji mtaji mkubwa wa kifedha.

Mfanyabiashara, umejiandaa vipi kuyapokea Mapinduzi haya ya 4 ya Viwanda katika eneo lako la biashara? Pitia makala hizi ili kupata taarifa zaidi:

  1. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BANDO LAKO NI MTAJI
  3. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  4. KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mapinduzi ya 4 viwanda katika biashara duniani

FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)

Waswahili wanasema “Nyakati ngumu hazidumu bali watu wagumu ndio hudumu.” Na pia “Baada ya dhoruba huja shwari.” Sasa mnamo mwaka 2008 uchumi wa dunia ulikumbwa na mtikisiko mkubwa zaidi kuwahi kutokea baada ya ule Mtikisiko wa kiuchumi wa mwaka 1933. Katika mdororo huo taasisi na mashirika ya kifedha duniani yalijikuta yakishindwa kuzuia hali duni ya uchumi katika bei za bidhaa ghafi kama mafuta na mikopo ya aina mbali mbali ambapo ilipelekea huduma hizo muhimu kupatikana eidha kwa tabu sana au kwa bei isiyokidhi usawa wa soko.

Hivyo ni katika hali hio ya mdororo wa kiuchumi ndipo lilipoibuka jina la Satoshi Nakamoto ambalo linasadikiwa kuwa ni jina la kifumbo la mtu mmoja au kikundi cha watu wasiofahamika hadharani mpaka sasa ambao ndio waliotengeneza sarafu ya kwanza kabisa ya mtandaoni na wakaiita BITCOIN. Pia mtu/watu hao ambao wanasadikiwa kuwa na asili ya Kijapani walitengeneza mfumo wa kwanza wa database ya Teknolojia ya Blockchain kwa kupitia kiunzi (ledger) cha kimtandao ambacho hakitegemei hifadhi moja. Yaani taarifa za miamala ya kifedha katika BITCOIN hufanyika kupitia Miundombinu ya Blockchain ambayo huwa ni ya siri mno na iliyotawanyika duniani kote na hivyo kuzifanya sarafu za mtandaoni zisiweze kudhibitiwa na taasisi na mashirika ya kifedha au hata vyombo vya kiserikali.

Kwanini ikawa hivi? Fuatana nasi kujua zaidi..

Kwa mujibu wa tovuti za study.com na Investopedia, Sarafu za mtandaoni au Cryptocurrency ni sarafu za kidijitali zinazoakisi thamani ya fedha ambapo kukua au kudorora kwa thamani hio hutegemea na uhitaji wa sarafu hio duniani kwa muda huo. Mfano wa sarafu hizi ni kama bitcoin, ethereum, Litecoin, Libra na kadhalika. Mpaka kufikia tarehe 20 June, 2019 BITCOIN thamani yake ilikuwa ni dola za kimarekani 9,259.37 na ETHEREUM ikapatikana kwa dola 269.11, Litecoin ikapatikana kwa dola 136.29 na kadhalika. Inakadiriwa mpaka kufikia February, 2019 tayari mtandaoni kulikuwa na sarafu 2500 tofauti tofauti za kimtandao ambapo pia iliripotiwa kuwa na miamala au mizunguko ya Bitcoin peke yake zaidi ya milioni 17.53 ambayo thamani yake inakadiriwa kuwa ni takribani dola bilioni 63.

Hata hivyo mpaka sasa soko la sarafu za mtandaoni limekua mpaka kufikia zaidi ya dola bilioni 120 huku sarafu ya Bitcoin peke yake ikichukua zaidi ya nusu ya thamani ya soko zima.

DHUMUNI LA KUANZISHWA CRYPTOCURRENCIES:

Neno Cryptocurrency ni mjumuisho wa maneno mawili, ‘Crypto’ na ‘currency’. Yaani sarafu iliyobadilishwa katika ulinzi wa kimtandao uitwao cryptography ambao huipa sarafu thamani yake ya kipekee na pia kuweza kuifanya sarafu hio isiweze kudukuliwa kirahisi.

Kutengeneza urahisi zaidi wa kulipia huduma na bidhaa mtandaoni, huduma za hoteli, migahawa, kurusha fedha kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa uhuru na wepesi zaidi na pia kubadilisha fedha katika masoko ya kimtandao ya kubadili fedha. Hizi ni baadhi ya sababu za kuanzishwa kwa sarafu hizi za mtandaoni, lakini sababu kubwa ni kuhakikisha ulinzi madhubuti na uhuru wa mtu kuhifadhi na kutumia fedha zake katika muda wowote atakaohitaji bila kufuatiliwa na taasisi au mashirika ya kifedha au vyombo vya serikali. Yaani kuwa na uhuru halisi juu ya fedha zako.

ZINAFANYAJE KAZI SARAFU HIZI?

Cryptocurrency zinafanya kazi kwa mfanano kama kadi ya benki ambayo huruhusu kufanyika miamala mbalimbali ya kutuma na kupokea fedha katika mfumo tata wa kielektroniki wa kifedha. Utofauti na utendaji wa kadi ya benki ni inaweza kufuatiliwa na taasisi za kifedha na mashirika ya kiserikali na pia huhifadhi kumbukumbu za wateja mahali pamoja.

Miamala hutumwa baina ya kompyuta washirika kwa kutumia programu ziitwazo “cryptocurrency wallets” ambapo mtu anayefanya muamala hutumia programu hio ya wallet kutuma fedha kutoka akaunti moja kwenda akaunti nyingine. Hata hivyo, ili kuweza kutuma au kupokea fedha katika mfumo huu, huna budi kuwa na nywila(password) au ufunguo binafsi ambayo inahusiana na akaunti yako. Miamala hio inayohusisha kompyuta washirika hufichwa katika msimbo wa kimtandao (encryption) halafu hutumwa katika mtandao wa sarafu hizo duniani ambapo huorodheshwa katika forodha ya jumla iliyohifadhiwa mtandaoni. Kiasi cha miamala inayopitishwa huwa ni wazi, lakini anayetuma muamala huo hufichwa, hii huitwa pseudo-anonymous ambapo ambapo kila muamala huwa na seti ya kipekee ya nywila (keys/passwords) na yeyote anayemiliki nywila hizo ndiye anayemiliki sarafu zote zilizo ndani ya akaunti hio. Kama ilivyo tuu kwamba anayemiliki akaunti ya benki ndiye anamiliki fedha zote zilizo ndani ya akaunti hio.

UNAWEZAJE KUWEKEZA KWENYE CRYPTOCURRENCY?

Sababu kuu ambayo huvutia watu wengi kuwekeza katika cryptocurrency ni kuweza kupata fedha nyingi zaidi muda mchache tuu baada ya kuwekeza mtaji. Hata hivyo kwa mujibu wa mtandao wa Forbes haya hapa chini ni baadhi ya mambo ya msingi zaidi ya kuzingatia kabla hujaamua kuweka fedha zako kama mtaji katika biashara hii:

1. AMUA AINA IPI YA CRYPTOCURRENCY UNGEPENDA KUSHUGHULIKA NAYO ZAIDI: Kama ilivyo muhimu kujua kujua kiasi cha mtaji unachokwenda kuwekeza, vile vile ni busara kuwa na mipango mizuri katika kuelewa misingi ya cryptocurrency hiyo kwa kuwa itachangia kwa kiasi kikubwa jinsi ya kujikinga na matishio yajayo ya kiuchumi.

2. AMUA UTATAKA KUWA NA UWEKEZAJI WA NAMNA GANI: Kwa kawaida utalazimika kuwa na mpango kama unataka kuingia katika masoko ya cryptocurrency. Swali ni mipango yako inaweza kuwa ya muda mrefu, wastani au ya muda mfupi. Hii itategemeana na fedha ulichonacho.

3. KUMBUKA, TAKWIMU ZA SOKO NI MUHIMU ZAIDI: Soko la sarafu za crypto ni tete muda wote. Huweza kubadilika hata kwa asilimia 20 kwa siku, hivyo ni muhimu kufuatilia taarifa za soko kwa ukaribu zaidi.

Umejifunza jambo gani kwenye makala haya? Tafadhali pitia makala tumekuwekea hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala hii ya leo kisha, acha maoni yako chini hapo kwenye sehemu ya comments..

  1. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  2. https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-biashara-za-kielektroniki-e-commerce-businesses/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI?”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-mapinduzi-ya-teknolojia-ya-5g-katika-biashara-na-uchumi-wa-afrika/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA TEKNOLOJIA YA 5G KATIKA BIASHARA NA UCHUMI WA AFRIKA”
  4. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO (BUSINESS INTELLIGENCE)?