Tag: cloud

FAHAMU KUHUSU UVUVI NA BIASHARA YA SAMAKI BARANI AFRIKA

Japokuwa inafanyika zaidi maeneo ya vijijini na katika hali duni ya zana za utendaji, elimu pamoja na teknolojia, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado inahangaika katika kujiboresha huku ikifichwa katika kivuli cha shughuli za Kilimo na Ufugaji. Mbaya zaidi sekta ya uvuvi na biashara ya samaki bado haijapewa umuhimu inayostahili barani humo. Zaidi sekta hio hutoa chakula cha kuwalisha watu zaidi ya milioni 200 barani humo na nje ya bara la Afrika. Leo sasa fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika. Twende mpaka mwisho.

Benki ya Dunia inaripoti kwamba shughuli za uvuvi na biashara ya samaki huchangia moja kwa moja dola za kimarekani $24 bilioni katika uchumi wa Afrika kwa ujumla, ikiwakilisha 1.3% ya jumla ya pato la ndani (GDP) la Afrika katika mwaka 2011. Vile vile sekta hio imezalisha ajira kwa zaidi ya watu milioni 12 ambapo 58% kati yao ni wavuvi na 42% wanajihusisha na kuandaa samaki waliovuliwa kabla ya kuwapeleka sokoni. Tanzania peke yake, sekta ya uvuvi imetoa ajira kwa watu 183,000 mpaka kufikia mwaka 2014 (chanzo: Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi) Ikionekana kwamba shughuli za uvuvi hufanywa zaidi na wanaume, 59% ya shughuli za kuandaa samaki kabla ya kuwaingiza sokoni hufanywa na wanawake.

Ukiachana na faida za samaki kama chakula katika kupatikana kwa virutubisho muhimu kama vitamini, protini na mafuta, zaidi, sekta ya Uvuvi na biashara ya samaki inachangia sehemu muhimu sana katika kuendesha maisha ya watu haswa vijana ikiwa watachukua angalizo katika fursa zilizopo kwenye sekta hio.

Changamoto; Je, kuna fursa zipi katika kufanya shughuli hii ya uvuvi na biashara ya samaki katika kukuza uchumi? Teknolojia ina mchango gani katika kuboresha uchumi wa mtu mmoja mmoja kupitia setka hii?

Tishio kubwa katika shughuli za uvuvi na biashara ya samaki ni athari zinazotokea katika mazalio ya samaki baharini, mtoni, ziwani au kwenye mabwawa. Umoja wa Mataifa na nchi  jumuishi duniani zimeingia uwoga juu ya upatikanaji wa hazina ya samaki katika soko la dunia. Shirika linaloshughulikia maswala ya Chakula duniani, FAO, limetabiri kwamba zaidi ya 70% ya aina (species) za samaki zinakaribia kuangamia au zimevunwa sana ambapo aina za samaki kama Tuna, Swordfish, Haddock na Flounder zipo katika tishio la kuangamia. Zaidi, uvuvi unaotumia chandarua au baruti huweza kusababisha kunaswa au kuuwawa kabisa kwa samaki na viumbe wengine wa baharini ambao hawajapangwa kuvuliwa kama ngasa, pomboo na papa.

Hata hivyo, shughuli za uvuvi zina faida gani katika maisha ya mwanadamu ikijumuisha?

  1. CHAKULA;  Samaki ni chanzo cha vitamini na protini katika lishe haswa ya mwanadamu ambapo madaktari na wadau wa sekta ya afya hushauri ulaji wa nyama nyeupe mfano samaki zaidi katika mlo. ulaji wa samaki kwa wingi huchochea ukuaji bora wa afya ya akili pamoja na wingi wa protini katika nyama hio huku ikiwa na kiasi kidogo cha lehemu (cholesterol) zaidi kuliko nyama nyekundu mfano ng`ombe, mbuzi na kadhalika.Ripoti zinaonyesha kwamba wakazi wa nchi za ukanda wa bahari ya Pacific peke yake hupata zaidi ya 25% na 69% ya protini za wanyama wanaokula kila siku kutoka katika samaki. Hii imepelekea shughuli za uvuvi na biashara ya samaki kukua kwa kiasi kikubwa kama shughuli rasmi ya kiuchumi ambayo imeajiri watu takribani milioni 200 dunia nzima na ikizalisha pato la dola za kimarekani zaidi ya 80 bilioni kwa mwaka.
  2. UKUAJI WA UCHUMI; Sekta hii ya uvuvi inachangia kwa kiasi kikubwa sana katika ukuaji wa uchumi barani Afrika mpaka dunaini kote ambapo watu zaidi wa milioni 200 wamejipatia ajira kupitia sekta hio. Nchini Uganda kwa mfano, uvuvi wa ziwani umekuwa na thamani ya zaidi ya dola $200 milioni  kwa mwaka ikiwa ni mchango wa 2.2% katika pato la taifa (GDP) la nchi hio. Vile vile watu zaidi ya 135,000 wamepata ajira kama wavuvi katika sekta hio na wengine 700,000 zaidi katika mchakato wa kuandaa samaki kabla hawajafikishwa sokoni na hivyo kuzalisha zaidi ya dola $87.5 milioni kama mapato ya biashara za nje ya nchi (exports earnings). Hapa miundombinu ya barabara na reli ina mchango mkubwa sana katika kuhakikisha kitoweo hiki kinamfikia mlaji kikiwa katika ubora wa hali ya juu. Kufahamu zaidi kuhusu mchango wa miundombinu pitia makala hii hapa;
  1. Vile vile nchini Tanzania kupitia katika mabwawa, maziwa, mito na bahari vilivyomo nchini humo, sekta ya uvuvi na biashara ya samaki imetoa ajira za moja kwa moja kwa watu takribani 183,800 na wengine zaidi ya 4,000,000 wakijihushisha kama watengenezaji wa vyombo vya uvuvi (ngalawa, boti, ndoano, neti n.k), waaandaaji wa samaki kabla hawajafikishwa sokoni, wachuuzi na wafanyabiashara wa samaki wa jumla na rejareja. Sekta hii ya uvuvi na biashara ya samaki inawapatia watu kipato cha fedha za kigeni, pamoja na kitoweo kwa watu waishio pwani ya bahari ya hindi pamoja wa walaji wa samaki kutoka sehemu zingine katika nchi hio ambapo sekta hio huchangia katika pato la taifa takribani 2.4%. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Wizara ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi katika mwaka 2016.

Kiujumla, mpaka kufikia mwaka 2001 uta fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika katika masoko ya kimataifa ilikuwa na thamani ya dola $2.7 bilioni ambayo ni 5% ya jumla ya thamani ya sekta nzima ya uvuvi na biashara ya smaki duniani ambayo ni dola $56 bilioni. Kwa mujibu wa shirika la FAO, bidhaa za samaki zimejumuisha zaidi ya 10% ya jumla ya biashara za kimataifa (exports) katika nchi 11 barani Afrika.

Sasa Baada ya kuyajua Hayo Yote, Kwanini Ufanye biashara hii ya Uvuvi na samaki?

Mwaka 2019 watumiaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania waliongezeka kufikia milioni 23, ongezeko la watumiaji takribani milioni 1 kutoka mwaka jana 2018. Vile vile watumiaji wa huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi wamefikia takribani milioni 20 hadi kufikia mwaka huu 2019. Hii ni kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA.

Hivyo kupitia ripoti hio ya TCRA mfanyabiashara anaweza kuhamishia shughuli zake kupitia simu mkononi na simu janja (smartphones) katika kuhakikisha biashara yake inawafikia watu wengi zaidi katika muda mfupi kwa njia ya Teknolojia. Hata hivyo mfanyabiashara anaweza kutengeneza majukwaa ya kimtandao kama tovuti za kibiashara (online shops na ecommerce websites) ambayo anaweza kuuza bidhaa zake za samaki kirahisi katika masoko ya ndani na hata yale ya kimataifa kwa gharama nafuu zaidi kuliko ulivyokua hapo kabla.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni

Kwa kutambua hilo, biashara ya mtandaoni imekuwa ikizidi kufanikiwa sana nyakati hizi huku ikichochewa na maboresho katika miundombinu ya uchukuzi na usafirishaji. Hivyo ni muhimu kufungua tovuti rasmi ya biashara yako ili kuipa utambulisho usio na shaka ukiwa mtandaoni. Vilevile ni muhimu kufungua akaunti za mitandao ya kijamii ili kusudu uzidi kujiweka karibu na wateja wako na kujua namna nzuri ya kuwahudumia.

Link zifuatazo zitakusaidia sana uweze fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika kupitia mtandaoni iwe na mafanikio zaidi na zaidi:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO

Je umepata nini katika mada ya leo katika ku fahamu kuhusu Uvuvi na biashara ya samaki barani Afrika?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)

Waswahili wanasema “Nyakati ngumu hazidumu bali watu wagumu ndio hudumu.” Na pia “Baada ya dhoruba huja shwari.” Sasa mnamo mwaka 2008 uchumi wa dunia ulikumbwa na mtikisiko mkubwa zaidi kuwahi kutokea baada ya ule Mtikisiko wa kiuchumi wa mwaka 1933. Katika mdororo huo taasisi na mashirika ya kifedha duniani yalijikuta yakishindwa kuzuia hali duni ya uchumi katika bei za bidhaa ghafi kama mafuta na mikopo ya aina mbali mbali ambapo ilipelekea huduma hizo muhimu kupatikana eidha kwa tabu sana au kwa bei isiyokidhi usawa wa soko.

Hivyo ni katika hali hio ya mdororo wa kiuchumi ndipo lilipoibuka jina la Satoshi Nakamoto ambalo linasadikiwa kuwa ni jina la kifumbo la mtu mmoja au kikundi cha watu wasiofahamika hadharani mpaka sasa ambao ndio waliotengeneza sarafu ya kwanza kabisa ya mtandaoni na wakaiita BITCOIN. Pia mtu/watu hao ambao wanasadikiwa kuwa na asili ya Kijapani walitengeneza mfumo wa kwanza wa database ya Teknolojia ya Blockchain kwa kupitia kiunzi (ledger) cha kimtandao ambacho hakitegemei hifadhi moja. Yaani taarifa za miamala ya kifedha katika BITCOIN hufanyika kupitia Miundombinu ya Blockchain ambayo huwa ni ya siri mno na iliyotawanyika duniani kote na hivyo kuzifanya sarafu za mtandaoni zisiweze kudhibitiwa na taasisi na mashirika ya kifedha au hata vyombo vya kiserikali.

Kwanini ikawa hivi? Fuatana nasi kujua zaidi..

Kwa mujibu wa tovuti za study.com na Investopedia, Sarafu za mtandaoni au Cryptocurrency ni sarafu za kidijitali zinazoakisi thamani ya fedha ambapo kukua au kudorora kwa thamani hio hutegemea na uhitaji wa sarafu hio duniani kwa muda huo. Mfano wa sarafu hizi ni kama bitcoin, ethereum, Litecoin, Libra na kadhalika. Mpaka kufikia tarehe 20 June, 2019 BITCOIN thamani yake ilikuwa ni dola za kimarekani 9,259.37 na ETHEREUM ikapatikana kwa dola 269.11, Litecoin ikapatikana kwa dola 136.29 na kadhalika. Inakadiriwa mpaka kufikia February, 2019 tayari mtandaoni kulikuwa na sarafu 2500 tofauti tofauti za kimtandao ambapo pia iliripotiwa kuwa na miamala au mizunguko ya Bitcoin peke yake zaidi ya milioni 17.53 ambayo thamani yake inakadiriwa kuwa ni takribani dola bilioni 63.

Hata hivyo mpaka sasa soko la sarafu za mtandaoni limekua mpaka kufikia zaidi ya dola bilioni 120 huku sarafu ya Bitcoin peke yake ikichukua zaidi ya nusu ya thamani ya soko zima.

DHUMUNI LA KUANZISHWA CRYPTOCURRENCIES:

Neno Cryptocurrency ni mjumuisho wa maneno mawili, ‘Crypto’ na ‘currency’. Yaani sarafu iliyobadilishwa katika ulinzi wa kimtandao uitwao cryptography ambao huipa sarafu thamani yake ya kipekee na pia kuweza kuifanya sarafu hio isiweze kudukuliwa kirahisi.

Kutengeneza urahisi zaidi wa kulipia huduma na bidhaa mtandaoni, huduma za hoteli, migahawa, kurusha fedha kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa uhuru na wepesi zaidi na pia kubadilisha fedha katika masoko ya kimtandao ya kubadili fedha. Hizi ni baadhi ya sababu za kuanzishwa kwa sarafu hizi za mtandaoni, lakini sababu kubwa ni kuhakikisha ulinzi madhubuti na uhuru wa mtu kuhifadhi na kutumia fedha zake katika muda wowote atakaohitaji bila kufuatiliwa na taasisi au mashirika ya kifedha au vyombo vya serikali. Yaani kuwa na uhuru halisi juu ya fedha zako.

ZINAFANYAJE KAZI SARAFU HIZI?

Cryptocurrency zinafanya kazi kwa mfanano kama kadi ya benki ambayo huruhusu kufanyika miamala mbalimbali ya kutuma na kupokea fedha katika mfumo tata wa kielektroniki wa kifedha. Utofauti na utendaji wa kadi ya benki ni inaweza kufuatiliwa na taasisi za kifedha na mashirika ya kiserikali na pia huhifadhi kumbukumbu za wateja mahali pamoja.

Miamala hutumwa baina ya kompyuta washirika kwa kutumia programu ziitwazo “cryptocurrency wallets” ambapo mtu anayefanya muamala hutumia programu hio ya wallet kutuma fedha kutoka akaunti moja kwenda akaunti nyingine. Hata hivyo, ili kuweza kutuma au kupokea fedha katika mfumo huu, huna budi kuwa na nywila(password) au ufunguo binafsi ambayo inahusiana na akaunti yako. Miamala hio inayohusisha kompyuta washirika hufichwa katika msimbo wa kimtandao (encryption) halafu hutumwa katika mtandao wa sarafu hizo duniani ambapo huorodheshwa katika forodha ya jumla iliyohifadhiwa mtandaoni. Kiasi cha miamala inayopitishwa huwa ni wazi, lakini anayetuma muamala huo hufichwa, hii huitwa pseudo-anonymous ambapo ambapo kila muamala huwa na seti ya kipekee ya nywila (keys/passwords) na yeyote anayemiliki nywila hizo ndiye anayemiliki sarafu zote zilizo ndani ya akaunti hio. Kama ilivyo tuu kwamba anayemiliki akaunti ya benki ndiye anamiliki fedha zote zilizo ndani ya akaunti hio.

UNAWEZAJE KUWEKEZA KWENYE CRYPTOCURRENCY?

Sababu kuu ambayo huvutia watu wengi kuwekeza katika cryptocurrency ni kuweza kupata fedha nyingi zaidi muda mchache tuu baada ya kuwekeza mtaji. Hata hivyo kwa mujibu wa mtandao wa Forbes haya hapa chini ni baadhi ya mambo ya msingi zaidi ya kuzingatia kabla hujaamua kuweka fedha zako kama mtaji katika biashara hii:

1. AMUA AINA IPI YA CRYPTOCURRENCY UNGEPENDA KUSHUGHULIKA NAYO ZAIDI: Kama ilivyo muhimu kujua kujua kiasi cha mtaji unachokwenda kuwekeza, vile vile ni busara kuwa na mipango mizuri katika kuelewa misingi ya cryptocurrency hiyo kwa kuwa itachangia kwa kiasi kikubwa jinsi ya kujikinga na matishio yajayo ya kiuchumi.

2. AMUA UTATAKA KUWA NA UWEKEZAJI WA NAMNA GANI: Kwa kawaida utalazimika kuwa na mpango kama unataka kuingia katika masoko ya cryptocurrency. Swali ni mipango yako inaweza kuwa ya muda mrefu, wastani au ya muda mfupi. Hii itategemeana na fedha ulichonacho.

3. KUMBUKA, TAKWIMU ZA SOKO NI MUHIMU ZAIDI: Soko la sarafu za crypto ni tete muda wote. Huweza kubadilika hata kwa asilimia 20 kwa siku, hivyo ni muhimu kufuatilia taarifa za soko kwa ukaribu zaidi.

Umejifunza jambo gani kwenye makala haya? Tafadhali pitia makala tumekuwekea hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala hii ya leo kisha, acha maoni yako chini hapo kwenye sehemu ya comments..

  1. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  2. https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-biashara-za-kielektroniki-e-commerce-businesses/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI?”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-mapinduzi-ya-teknolojia-ya-5g-katika-biashara-na-uchumi-wa-afrika/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA TEKNOLOJIA YA 5G KATIKA BIASHARA NA UCHUMI WA AFRIKA”
  4. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO (BUSINESS INTELLIGENCE)?
Hifadhi mbadala ya nyaraka (Data backup strategies)

HIFADHI MBADALA YA NYARAKA (DATA BACK UP)

Mwaka 2017 Makampuni ya CISCO na Microsoft yalitoa ripoti yao ya mwaka kuhusu Usalama wa masuala ya Kimtandao ambapo ilionekana kwamba matukio ya udukuzi yaliongezeka maradufu katika maeneo ya kibiashara/kampuni na taasisi mbali mbali. Zaidi ya hayo iligundulika kwamba biashara nyingi licha ya kuingia katika majanga ya kudukuliwa taarifa zao, zilijikuta zikipoteza vitu vingine vingi kwa wadukuzi wa kimtandao na wezi zaidi hata ya pesa na taarifa zao.Sasa leo tuone kuhusu hifadhi mbadala ya nyaraka (Data Backup), ni nini na inafanya kazi vipi. Fuatana na makala hii mpaka mwisho.

Kulingana na Shirika la Acromis, zaidi ya nusu ya biashara zote duniani ni muhanga wa matukio ya udukuzi wa kimtandao na wizi wa taarifa muhimu za taasisi. Matukio hayo yanahofiwa kusababisha hasara kwa kampuni kutokana na kuharibu taswira ya taasisi katika jamii, kushusha heshima ya wateja kwa taasisi na kupunguza uaminifu wa taasisi kwa wateja wake na jamii kwa ujumla. Kuhusiana na udukuzi na namna unavyoweza kupambana nao bila shaka utataka kujifunza kupitia makala hii hapa chini.

Ripoti hiyo ya CISCO na Microsoft pia imetaja kwamba zaidi ya aslimia ishirini na tisa (29%) ya biashara ambazo ni muhanga wa mashambulio ya udukuzi hupoteza mapato yao na takribani asilimia arobaini (40%) ya biashara hizo hupoteza asilimia ishirini (20%) ya jumla ya mapato yao kwa mwaka.

Kati ya biashara zilizopo duniani, takribani robo ya biashara hizo hupoteza nafasi muhimu sana za kuongeza wigo wa kibiashara kufuatia kupotea kwa taarifa zake kuishia mikononi mwa wadukuzi na matukio ya wizi wa nyaraka. Na zaidi ya 20% ya biashara zinazopitia katika janga ya kupotea kwa nyaraka zao muhimu hupoteza pia wateja wao. Na 40% kati yao hupoteza zaidi ya 20% ya wateja wao kila mwaka.

Sasa unaweza vipi kuhakikisha wateja wako wanaendelea kuwa kwako bila ya kuwapoteza? Hakikisha unapitia makala hii hapa ili ujue  UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA .

Zaidi ya wadukuzi wa kimtandao na matukio ya wizi wa nyaraka, Majanga ya kiasili yanayotokea duniani pia huchangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa nyaraka muhimu za taasisi. Mafuriko, Majanga ya Moto, Hali ya unyevu unyevu, Kimbunga na Tetemeko la ardhi husababisha athari kubwa zaidi katika uhifadhi wa taarifa muhimu za taasisi. Kutokana na kuongezeka kwa matukio ya upotevu wa taarifu hizo muhimu za taasisi na biashara mbalimbali, wataalamu wa masuala ya uhifadhi wa taarifu na nyaraka muhimu za kibaishara na taasisi duniani kupitia katika ripoti ya mwaka ya makampuni ya CISCO na Microsoft, njia mbali mbali za hifadhi mbadala ya nyaraka (Data Backup) zilishauriwa:

1. NJIA YA 3-2-1:

Njia hii ni kanuni bora sana ya kuhifadhi nyaraka na taarifu za kampuni/taasisi au biashara kwa urahisi na wepesi zaidi. Inafanya kazi kama ifuatavyo., • Tengeneza nakala tatu (3 copies) kaika kila nyaraka zako unazozifanyia kazi kila siku. Hapa unajihakikishia kwamba hakuna tukio lolote ambalo litaweza kuziharibu nakala zote tatu kwa urahisi.

• Katika nakala zako tatu, mbili (2) zihifadhi katika mitindo (formats) tofauti ambayo inaweza kuwa disk format, tape, cloud na kadhalika.

• Nakala moja (1) iweke mbali kabisa na mahali unafanyia kazi (inaweza kuwa nyumbani, mkoani, nchi nyingine n.k) ili kuepuka hatari ya majanga ya moto, unyevu unyevu, mafuriko, vimbunga na wezi.

2. NJIA YA MTANDAO WA KOMPYUTA:

Njia hii pia imethibitika kuwa na ubora katika uhifadhi mzuri wa nyaraka. Hapa nyaraka zinahifadhiwa katika kompyuta zaidi ya moja ambazo zimeunganishwa katika mtandao fulani( inaweza kuwa LAN, MAN au WAN). Njia hii huhakikisha usalama wa nyaraka za taasisi au biashara yako kuongeza uwezo wa upatikanaji wa nyaraka kwa wahusika wale tuu waliokusudiwa kushirikiana katika kufanyia kazi na kuhifadhi nyaraka hizo katika muda muafaka.

Njia ya Kompyuta katika kuhifadhi data

3. NJIA YA INTANETI (CLOUD BACK UP):

Hii ni njia rahisi na ya kisasa zaidi katika nyanja ya uhifadhi mbadala wa Nyaraka za taasisi/kampuni au biashara yako. Katika njia hii kanuni kubwa inayotumika ni kupandisha nyaraka zako katika majukwaa ya kimtandao ambayo yanatoa huduma hio ya uhifadhi kwa njia ya Intaneti.

Mpaka kufikia mwaka 2022 katika intaneti inakadiriwa kutakuwa na zaidi ya Terabite (TB) bilioni 2 za nyaraka zitakazohifadhiwa. Mashirika na Makampuni ya kimataifa ya NASA na GOOGLE yanajipanga kila siku kuongeza nafasi ya uhifadhi katika majukwaa yao ya huduma za intaneti. Hali kadhalika makampuni mengi zaidi yanaibuka duniani na kutoa huduma hii ya uhifadhi wa nyaraka kwa intaneti ambapo huduma hii inazidi kuboreshwa kila siku.

cloud data storage

Kampuni la Microsoft kwa mfano, limeanzisha huduma ya Office 365 ambayo ni mageuzi ya Programu ya Microsoft Office ambayo watu wengi duniani wamezoea kuitumia katika kazi zao za kila siku. Hata hivyo huduma hii ya office 365 ni ya kimtandao zaidi ambapo sasa mtu unaweza kufanya kazi zako ukiwa popote na katika vifaa mbali mbali vya kielektroniki kama simu janja na kompyuta mpakato ikiwa tuu tayari umeshajipatia huduma hii kutoka Microsoft. Hali kadhalika kampuni ya Google nayo imeanzisha huduma ya Google Drive ambapo inawezesha kuhifadhi nyaraka zako vizuri, kwa muda mrefu na kwa usalama wa hali ya juu. Vile vile duniani yameanzishwa majukwaa mengine mengi ya huduma za uhifadhi nyaraka kwa intaneti kama Dropbox, Acronis Data Backup na kadhalika.

Lengo kuu la huduma hizi za hifadhi mbadala ya nyaraka (Data Backup) zako ni kuhakikisha Usalama wa taarifa zako za kibiashara au taasisi/kampuni unakuwa wa hali ya juu na hivyo kuongeza ufanisi wa huduma/bidhaa zako kila siku.

Kama una la ziada usisite kuwasiliana nasi kuweza kupata huduma bora na za kisasa za kimtandao ili kuimarisha biashara yako ili iweze kuendana na kasi ya kidunia. Wasiliana nasi kupitia mawasiliano yetu hapa au komenti hapa chini. Karibu sana.

Call/WhatsApp: +255765834754

Email: info@rednet.co.tz