Tag: business

KWANINI UHAMIE WINDOWS 10?

Inawezekana unaipenda sana windows7. Inawezekana pia computer yako ina taarifu nyingi ambazo usingependa uzipoteze. Lakini mifumo ya uendeshaji (OS) kutoka kampuni ya Microsoft hukamilisha muda wa huduma zake kila baada ya miaka 10. Sasa leo nataka nikujuze, kwanini uhamie windows 10?

Sasa kufikia January 14 mwaka 2020, kampuni ya Microsoft iliacha kutoa matoleo (updates) mbalimbali kuhusu windows7. Hivyo, matoleo ya kiusalama, speed n.k yalikomea hapo na kufanya kama unatumia Windows7 baada ya tarehe hio, basi computer yako ipo hatarini kushambuliwa kimtandao kwa kuwa hakuna uimara wa kiusalama tena katika mifumo ya uendeshaji (OS) ya computer yako.

JE, COMPUTER ITAZIMA BAADA YA UKOMO HUO?

Hapana, computer yako yenye windows7 itaendelea kufanya kazi kama kawaida isipokuwa, Microsoft hawatakupa updates za kuisalama wala marekebisho yoyote ya kiautomatiki yaliyokua yakitolewa hapo kabla. Hii itaifanya computer yako kuwa katila hatari kubwa ya kuvamiwa na virusi au mashambulio ya kimtandao yatakayoelekezwa kwako muda wowote upenyo ukipatikana.

KWANI LAZIMA KUWEKA WINDOWS 10?

Sio lazima, wala hakuna mtu atakulazimisha kuanza kutumia windows10. Lakini ni jambo muhimu na la busara zaidi kuimarisha mifumo tendaji (OS) ya computer yako kwa kuwa windows10 imetengenezwa kwa uimara zaidi katika matoleo ya kiusalama, antivirus iliyojishikiza (built-in antivirus) na Windows defender ambazo hukulinda zaidi dhidi ya shambulio lolote la kimtandao.

KWANINI MICROSOFT WAMEIACHA WINDOWS 7?

Microsoft wana utaratibu wao wa kisera (Fixed Lifestyle Policy) ambao unazipa muda wa kuhudumu bidhaa zao mbalimbali. Mfano, Windows 7 ilitoka kwa mara ya kwanza October 2009, hivyo miaka yake 10 ya kuhudumu imehitimishwa January 14 mwaka huu (japo imechelewa kidogo kufikia ukomo wake). Hii windows 10 inayopigiwa chapuo ilizinduliwa mwaka 2015 na inatarajiwa kuhudumu kwa miaka 10 mpaka 2025. Sasa windows 10 ilikua ni bure kabisa kuinstall mpaka kufikia majira ya kiangazi cha mwaka 2016. Lakini, ofa hio iliishia hapo ambapo kwa sasa itakulazimu kulipia gharama za kufanya installation kama unatumia matoleo ya zamani ya mifumo tendaji. Windows10 ya kawaida (Home edition) hugharimu dola za kimarekani $ 139.99 na ile ya kiuweledi (Pro edition) itakugharimu dola za kimarekani $ 199.99 kuipata katika majukwaa ya kimtandao ya Microsoft.

Sasa Leo tukiacha yote hayo, nataka nikupe faida 10 za kutumia windows10 kama mfumo tendaji katika computer yako:

1. USALAMA

Windows10 imerithi mifumo ya kiusalama kutokea kwenye toleo la nyuma yake la windows8, hivyo kuifanya windows10 kuwa salama zaidi. Hii ni kwa kuwa code yoyote ambayo huanza kufanya kazi pale computer inapowaka, basi code hio ni lazima ipewe kibali na Microsoft au watengenezaji wa Hardware (Dell, hp n.k). Lakini zaidi ya windows8, windows10 imetengenezwa kuhakikisha codes zake haziwezi kuvukwa (kuwa bypassed). Kuboresha huduma, hivi karibuni Microsoft wameongeza features katika usalama zaidi za Ransomware Protection na Threat Protection. Zaidi katika kuzingatia usalama wako uwapo mtandaoni hakikisha unapitia makala katika link hii KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO NI MUHIMU KWAKO? huu ni ukweli muhimu sana kuufahamu unapojiuliza kwanini uhamie windows 10?

2. SPEED

Kuanzia pale unapowasha computer yako, Windows10 hufunguka kwa spidi zaidi pengine kuliko computer zenye MacOS japokuwa mifumo tendaji ys Mac imeonekana muda mrefu kuwa ipo fasta zaidi. Safari hii imekula kwao. Injini ya 3D iitwayo DirectX 12, ambayo watengenezaji wa michezo ya video (video games) huitumia kurahisisha matengenezo na viwango vya michezo hio, hufanya kazi vizuri zaidi katika windows10 kuliko katika matoleo mengine.

3. CORTANA

Ebwana eeh, nna uhakika hata wewe huwa unafurahi sana pale unapoweza kuzungumza/kukiamuru kifaa chako kufanya jambo unalolitaka kwa sauti tu. Hapa watumiaji wa iPhone na yule “Siri” wao watakuwa wananipata vizuri sana. Sasa kwenye Windows10 kuna feature inaitwa “Cortana” ambayo ni teknolojia ya Sauti ambayo unaweza kuiamuru ifanye shughuli mbalimbali zilizopo kwenye computer yako kama “Hey Cortana, Cheza muvi ya Ray Kigosi, Imba wimbo wa Ray C, Onyesha picha ya Mr. Blue, zima computer.” nakadhalika. Hivyo vyote vinaweza kufanyika kwa sauti yako tu kupitia Kipengele hicho ndani ya computer yako yenye Windows10. Kumbe mambo ni murua bwana.

4. START MENU

Kama ulikua hufahamu basi Windows95 ambayo ilitoka mwaka 1995 ilikua na kipengele cha menu ambayo inafanana na menu ya windows8. Lakini watu waliilalamikia sana kuwa menu ile ilikua na mambo mengi hivyo kulazimisha Microsoft kuiondoa katika matoleo yake yaliyofuata. Lakini ajabu ni kwamba baada ya kubuni start menu ambayo ilitumika kwenye matoleo ya windows98 mpaka windows7 bado watu wengi walikua wakilalamika kuwa menu haijakaa vizuri mpaka ilipotoka windows8 na start screen yake. Hivyo toleo la Windows10 limeboreshwa zaidi na kuipa muonekano bora Start Menu yake na kuifanya yenye kuvutia na rahisi kutumia. Mudhui yake yameifanya iwe bora zaidi kwa kufanya Apps muhimu zaidi ziweze kuongezeka ukubwa na zile zenye umuhimu kidogo zinaweza kufanywa ndogo ili iwe rahisi hata kuchagua kwa kutumia kipanya (mouse).

kwanini uhamie windows 10?

5. TOUCH

Kama kila kifaa unachotumia kimetengenezwa kuruhusu teknolojia ya “Touch screen” kuanzia simu janja, redio za gari, tablet mpaka mifumo ya ramani elekezi (navigation systems). Sasa kwanini isiwezekane katika computer yako pia? Kuna watu watasema “oh kioo cha Pc ukiwa unakigusa gusa kinachafuka na kuharibika mapema” Sasa hilo linakuaje tatizo kwenye Pc na lisiwe kwenye simu yako ambayo kioo chake ni kidogo zaidi na unaitumia muda mwingi zaidi kwa siku. Basi kama ulikua hujui, computer zilizotengenezwa kupokea teknolojia ya “Touch screen” hufanya kazi kwa ufanisi zaidi pale zinapokuwa na Windows10 kuliko zile zinazokua na mifumo tendaji mingine. Pc kama Lenovo IdeaCenter Yoga A940, The Surface Pro7, Convertible Tablet na Acer T232HL ambazo zimewezeshwa na Touch screen hufanya kazi kwa ufanisi zikiwa na Windows10 kuliko hata Tablet za iOS katika mambo mengi.

6. KIVINJARI BORA

Hakuna tena mambo ya Internet Explorer. Sasa hivi ni mwendo wa Microsoft Edge ambayo ni balaa. Hii Microsoft Edge imefanywa kuwa bora sana katika speed, vipengele (features) kama web page markup na reading mode. Vile vile hii Edge inatajwa kuwa inatumia kiasi kidogo cha umeme (Power use) kuliko kiasi kinachohitajika katika kivinjari cha Google Chrome. Huu ndio ukweli muhimu sana kuufahamu unapojiuliza kwanini uhamie windows 10? Sasa Inategemewa katika maboresho yajayo kutakuwa na matafuto ya mtandaoni kupitia “Cortana” katika hii Microsoft Edge. Watu wamejipanga bwana.

7. KUCHAPA(TYPING) KWA SAUTI

Kirahisi kabisa, bonyeza alama ya Windows na kitufe H (Ili kuiamuru computer yako ianze kukusikiliza). Halafu anza kuongea kila unachotaka kichapishwe kwenye nyaraka yako. Hakuna haja ya kutatanisha mambo hapa. Wale wavivu wa kuchapa hapa ndo kwenyewe.

8. VIUNGANISHI VYA SIMU (SMARTPHONE TIE-INS)

Windows 10 bwana imeundwa kitaalamu sana. Yaani sasa unaweza kuunganisha smarphone yako na computer yako ili kuhakikisha shughuli zako unazofanya baina ya vifaa vyako zinakuwa zikishirikiana na kuungana (synchronized). Kuna App imeundwa katika Windows10 inaitwa “Continue on PC App“, Hii sasa hutuma kurasa za tovuti ulizopitia au nyaraka ulizozihifadhi katika computer yako moja kwa moja zinafika kwa simu yako na hivyo unapata wepesi wa kufanya shughuli zako kirahisi hivyo yani. Unaweza kutumia kivinjari cha Microsoft Edge kuunganisha shughuli zako za mtandaoni na kipengele cha Cortana kuunganisha kumbukizi (reminders) baina ya vifaa vyako. Watumiaji wa Android hapa ndo wanafaidi zaidi, nyie wengine wa iOS ebu tulieni kwanza. Kwa kutumia kipengele cha “Your Phone App” sasa unaweza kuona picha zako na video mara tu unapopiga kutokea katika camera ya simu yako. Hivi karibuni kutakuwa na toleo la Voice calling hata katika computer yako yenye Windows10. Mambo ni mazito.

9. DARK AND LIGHT MODES

Sikuizi bwana kila kitu ni Dark mode. Sio Whatsapp, Telegram, Instagram, kote kote yani ni mwendo wa Dark mode. Sasa Windows10 nayo haiko nyuma, toleo la mwezi May, 2019, kampuni ya Microsoft walisambaza upendo kwa “wapenda giza” pia ambapo sasa unaweza Kwenda kwenye Settings>Personalization>Colors. Halafu hapo unachagua rangi uipendayo halafu mambo yanakuwa safi kabisa. Kuna baadhi ya vivinjari (browsers) huheshimu aina ya rangi unayotumia katika windows10 yako mfano Microsoft Edge. Hii ndio raha ya kuufahamu utamu unapojiuliza kwanini uhamie windows 10?

10. GAMING BAR

Yes, kwa kubofya kitufe cha Windows kikifuatiwa na kitufe G (kama haiko active nenda kwa Settings>Gaming>Game Bar). Hapo sasa unaweza kupiga screenshot, kurekodi video, audio na mambo kibao kuhusu game unayocheza hapo. Ikiwa tu computer yako ina RAM ya kutosha pamoja na Processor nzuri. Basi hiki kipengele kinakuhusu vilivyo.

BONUS: Kuna watu wanahisi Windows10 ni nzito, ngumu kutumia na ina mambo mengi ambayo sio muhimu. FYI, kampuni ya Microsoft imefanya marekebisho ili kuhakikisha mtumiaji anafanya kazi zake kirahisi bila shida yoyote ya kiufundi. Na zaidi, wa wataalam (coders and gamers) wameongezewa vipengele ili kuhakikisha kazi zao zinapatiwa msaada stahiki kupitia matoleo ya Windows10.

Zaidi, hakikisha unapotumia Windows10 unapata huduma ya Internet (wi-fi) ili kuhakikisha matoleo muhimu ya kiusalama (security updates) unayapata kwa wakati. Tumia wifi nzuri ili usije ukapata gharama za ziada unapotumia bando lako la simu (ambalo kwa watu wengi hupigiwa bajeti kali).

Sasa tumekuwekea makala zingine kwa ajili ya kukupa maarifa na taarifa zaidi kuhusu namna nzuri ya kutumia teknolojia hizi kwa manufaa yako binafsi na manufaa ya uchumi wa biashara yako binafsi. Gusa link kisha makinika:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO KIMEDUKULIWA
  3. YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO (CYBER ATTACK) NA ATAHARI ZAKE KATIKA BIASHARA YAKO

Kiufupi hii ndo Windows10 na umuhimu wake. Kama hujawahi kutumia OS zingine, hii inakufaa. Ukiwa na maoni yoyote ama ushauri kuhusu kufanya installation ya Windows10 katika computer yako, tafadhali wasiliana nasi kupitia namba yetu ya simu ya 0765834754 au barua pepe info@rednet.co.tz. Karibu sana.

FAHAMU KUHUSU MFUMO WA MAWASILIANO YA SIMU (MOBILE ECOSYSTEM) NA FAIDA ZAKE KATIKA BIASHARA

Je Wajua?

Mfumo wa mawasiliano ya simu (mobile ecosystem) huchangia shemu muhimu sana katika uchumi wa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara? Uchumi wa nchi hizo kwa pamoja umefikia thamani ya dola za kimarekani bilioni 110 ($110 b) ambayo ni sawa na 7.1% ya pato la taifa (GDP) katika mwaka 2017. Hii inajumuisha faida za moja kwa moja za mfumo huo, faida zisizo za moja kwa moja (indirect impact) pamoja na ukuaji wa uzalishaji unaoletwa na matumizi ya huduma za simu na teknolojia.

Tukigusia faida za moja kwa moja za mfumo huu wa mawasiliano ambao unajumuisha makampuni ya simu, watengenezaji wa huduma za miundombinu ya kiteknolojia, wasambazaji wa huduma/ bidhaa za simu, wafanyabiashara wa reja reja, watengenezaji wa simu na vifaa vyake pamoja na watengenezaji wa maudhui/applications/huduma za mtandaoni; mchango wao katika uchumi hukadiriwa kwa kupimwa thamani wanayochangia katika uchumi wa nchi husika ambayo hujumuisha bima ya wafanyakazi, faida ya ziada ya biashara pamoja na kodi.

Mwaka 2017, thamani iliyozalishwa na mfumo huu wa mawasiliano katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara ulikuwa dola bilioni 40 ambayo ni sawa na 2.5% ya pato la Taifa (GDP) ambapo makampuni ya simu peke yake yalijumuisha takribani 75% ya mchango huu.

Ukiachana na faida za moja kwa moja, zipo pia faida ambazo si za moja kwa moja (indirect impact) ambapo sekta hii hununua vifaa/huduma mbali mbali kutoka sekta nyingine. Kwa mfano makampuni ya simu hulazimika kununua umeme kutoka sekta ya nishati hali kadhalika wasambazaji na wafanya biashara wa reja reja wa vifaa/huduma za simu huhitaji usafiri kuwafikia wateja wao.

Kwa pamoja uzalishaji huu wa faida isiyo ya moja kwa moja ulitengeneza takribani 60$ mwaka 2017 (ambayo ni takribani 4% ya pato la taifa). Kiujumla ukiongezea na faida za moja kwa moja, sekta hii ya mawasiliano ya simu ilitengeneza 110$ bilioni sawa na 7.1% ya pato la taifa katika ukanda huu.

Hii inaleta picha gani Kibiashara?

Matumizi ya teknolojia ya simu pamoja na maendeleo ya simu za rununu (smartphones) huendesha uchumi kwa kuboresha uzalishaji, kupunguza costs za uendeshaji pamoja na kurahishisha upatikanaji wa huduma/bidhaa za kibinadamu.

Chanzo: Ripoti ya shirika la mawasiliano ya simu duniani la GSMA toleo la mwaka 2019.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”

TEKNOLOJIA KATIKA BIASHARA ZA KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA (TECHNOLOGY IN SUB SAHARAN BUSINESS )

Kwa watumiaji wengi wa simu za mkononi waishio Kusini mwa jangwa la Sahara, simu ya mkononi si kwamba ni kifaa cha mawasiliano tu, lakini zaidi ni kifaa muhimu cha kuperuzi mtandaoni na kupata huduma mbalimbali za msingi za kibinadamu. Ujio wa simu za rununu (Smartphones) eneo hilo umekuwa maradufu katika miaka ya hivi karibuni. Watumiaji wa simu za rununu wameongezeka kutoka 25% mwanzoni mwa muongo huu (2010’s) mpaka kufikia 44% mwishoni mwa mwaka 2017. Hii ni chini ya wastani wa kidunia wa 66% katika ongezeko hilo la watumiaji wa simu za mkononi. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa shirika la kimataifa la mfumo wa mawasiliano ya simu GSMA.

Watumiaji hao wa simu ambao ni 44% ya jumla watu waishio katika eneo hilo sawa na watu milioni 444 ambao pia ni aslimia 9% tu ya watumiaji wote wa simu za mkononi duniani wanatajwa kupatikana katika eneo hilo la kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia inatajwa kwamba ongezeko hilo la watumiaji litakuwa katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) kwa 4.8 katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2022, ambacho ni zaidi ya mara mbili ya CAGR ya dunia nzima katika kipindi hicho hicho.

Moja ya vitu vinavyotoa nguvu katika ongezeko hili ni pamoja na uwezo wa simu za rununu (janja) kuunganisha watu wengi kupitia huduma za intaneti na mitandao ya kijamii ambapo katika mitandao hio ndipo panapotumiwa na watu wengi kama sehemu ya kukutana, kubadilishana mawazo, kuburudika na kufanya biashara. Hivyo kufanya mitandao hio ya kijamii kuzidi kuwa na umuhimu kadiri muda unavyokwenda.

Kibiashara hii ina maana gani?

Ripoti hio ya GSMA iliyochapishwa mwaka 2018 inataja kwamba ukuaji wa teknolojia umerahisisha mambo mengi muhimu yakiwemo utolewaji wa elimu, maswala ya afya na tiba na pia kuwezesha mazingira bora ya kufanyika biashara katika kutunza na kuonyesha kumbukumbu mbalimbali, miamala ya kifedha na jinsi bora ya kumhudumia mteja hata akiwa mbali na mzalishaji kupitia majukwaa ya huduma za kifedha za kimtandao na IoT (Internet of Things). Ripoti hio pia inaakisi kasi ya ukuaji wa matumizi ya simu za rununu (samrtphones) pamoja na vifaa vya kiteknolojia mpaka kufikia mwaka 2025 katika utendaji na utoaji wa huduma mbalimbali za kibinadamu pamoja na shughuli za kibiashara katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”
  5. https://rednet.co.tz/kuanzishwa-kwa-eneo-huru-la-biashara-barani-africa-afcta-kuna-manufaa-gani-kwako/ yenye kichwa “KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?”
Unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA KATIKA BIASHARA YAKO?

Bila kujali unafanya biashara ya aina gani, teknolojia ya intaneti na kompyuta imekuwa kwa kiwango kikubwa sana duniani hivyo kupelekea kuathiri mfumo mzima wa uendeshaji biashara duniani. Mwaka 2011 mwandishi Marc Andreessen alinukuliwa akisema, “Softwares are eating the world” akiwa na maana ugunduzi wa programu za kompyuta unarahisisha shughuli nyingi za kibinadamu kufanyika kwa haraka, kwa unafuu na kwa ufanisi zaidi kila siku zinavyozidi kwenda mbele. Sasa unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Leo tufahamu kwa undani.

Kufikia Octoba, mwaka 2018 tovuti ya Lifehacks (lifehacks.io) iliripoti kwamba jumla ya tovuti bilioni 1.9 zilithibitika uwepo wake kwenye intaneti pamoja na kuripotiwa kuwepo kwa machapisho (posts) zaidi ya milioni tano (5) ya blogu mbali mbali duniani kila siku. Tafiti hii ya kimtandao inakupa sababu mbali mbali za kukuwezesha kufanya biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta. Fuatana nasi.,

1. KUWA NA MPANGO WA BIASHARA ILI KUJUA KIUNDANI UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA:

Ukiwa na ndoto za kufanya biashara yako iwe na mafanikio maradufu, huna budi kuwa na mpango madhubuti wa kibiashara ambao utaainisha aina ya biashara unayoifanya, Jina la biashara linaloendana na aina ya bidhaa/huduma unayotoa, maudhui bora ya tovuti, soko unalolilenga na mbinu stahiki za kulikamata soko la kudumu.

Unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

MPANGO WA BIASHARA

2. TAFUTA NA CHAGUA JINA ZURI LA TOVUTI YA BIASHARA YAKO MTANDAONI:

Unapofikiria kuanzisha biashara, fikiria soko kwanza kabla ya aina ya biashara unayoitaka. Yaani tizama kwenye jamii, changamoto zilizopo ambazo hazijatatuliwa au hazionekani kama ni changamoto sana kwa muda huo, halafu tafuta suluhisho la changamoto hizo. Suluhisho hilo liendane na Jina zuri la kuwasilisha kile unachotaka kutatua kwenye jamii.

Uza suluhisho na si bidhaa kama bidhaa. Ukishapata Jina zuri, tengeneza tovuti yako au tafuta wataalamu waliobobea kwenye ujenzi na uendelezaji wa tovuti bora za kibiashara. KUMBUKA Tovuti sio Bidhaa bali ni Jukwaa la kufanyia biashara zako kama ilivyo ofisi yako, Fremu au Meza ya kuuzia bidhaa zako kila siku. Tofauti na ofisi, fremu au meza., tovuti ni jukwaa la kimtandao linalokuwezesha kuonyesha bidhaa/huduma zako dunia nzima kiurahisi zaidi mara moja. Kuhusu Umuhimu na faida za tovuti (website) katika biashara yako tayari nimekuwekea makala hizi hapa. Zitakufaa sana katika kuimarisha biashara yako ukizipitia zote.

3. TANGAZA NA WEKA UTARATIBU WA KUFUATILIA BIASHARA YAKO:

Dunia inakadiriwa kuwa na watu zaidi ya bilioni 7 mpaka sasa. Kati ya hao watumiaji wa mitandao ya kompyuta wanakadiriwa kufika bilioni 4 ikiwa ni takwimu zilizowasilishwa na yovuti ya lifehacks. Katika watu zaidi ya bilioni 4 ambao ni watumiaji mubashara wa mitandao ya kompyuta na simu, zaidi ya watu bilioni 2.234 wamegundulika kuwa ni watumiaji wa mtandao wa kijamii wa facebook peke yake.

Mfumo wa kimtandao wa kompyuta uitwao Internet Live Stats (ILS) unatumika kufuatilia watumiaji mubashara wa watumiaji wa Intaneti duniani kote kila siku. Hii ina maana kwamba zaidi ya nusu ya jumla ya watumiaji wote wa mitandao ya kompyuta na simu duniani wanapatikana facebook. Vilevile asilimia thelathini (30%) ya jumla ya idadi nzima ya watu wanaoishi duniani ni watumiaji wa facebook.

Kwa kusema hivyo, tayari tumekuwekea makala maalum itakueleza kwanini ni muhimu uitangaze biashara yako kila siku. Tafadhali ipitie makala hio mpaka mwisho kupitia link hii hapa yenye kichwa KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO.

unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Hivyo kwa kuutumia vyema mtandao wa facebook peke yake kibiashara unajiweka kwenye nafasi ya kuwafikia zaidi ya watu bilioni 2 ambao wanaweza kuwa wateja wazuri katika biashara unayoifanya. Vile vile watu zaidi ya bilioni 1 wamefahamika kuwa ni watumiaji wa mtandao unaoshika kasi wa Instagram.

Zaidi ya hayo pia kama mfanyabiashara mwenye kiu ya mafanikio una wajibu wa kufuatilia maendeleo ya biashara/kampuni/taasisi yako katika muktadha wa kuichumi na masoko. Biashara inabidi iwe inakua katika viwango vinavyohitajika kulingana na kasi ya soko la dunia.

Hivyo baada ya kujiuliza unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?, sasa unao uwezo wa kufuatilia biashara yako kwa kutumia takwimu sahihi kama ongezeko la wateja ndani ya muda fulani (wiki, mwezi au mwaka), ongezeko la faida, taarifa za mapato na matumizi na zaidi, usalama wa taarifa zako kibiashara.

Pia katika ufuatiliaji unaweza kuongeza njia kusambaza taarifa kuhusu biashara yako. Moja ya njia hizo ni Search Engine Optimization ambayo ni huduma inayotolewa na makampuni ya programu za kompyuta na mitandao. Huduma hii hukupatia nafasi ya kusambaza links za tovuti au mifumo yako ya kompyuta ambapo mtu yeyote anapotafuta bidhaa au huduma zako katika mtandao, basi inakuwa rahisi zaidi kukupata kwa kuandika maneno yanayohusu huduma hio unayotoa.

4. JIBU KWA WAKATI NA KWA UWELEDI ILI UNAPOJIULIZA UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA MTANDAONI UPATE ULE MVUTO WA KIBIASHARA

Unapokuwa mfanyabiashara au mhusika katika kampuni/taasisi fulani maana yake upo hapo kwa ajili ya wateja wako, hivyo unapaswa kutoa majibu na ufafanuzi wowote unaofika kwako kutokea kwa wateja wako. Aina ya majibu au ufafanuzi wako huchangia kwa kiasi kikubwa kupata wateja wapya kila siku au kupoteza wateja kila siku. Waswahili wanasema “Kauli Njema ni Silaha.” Hivyo kwenye kauli zako za kuhudumu ni lazima uweke uweledi wa hali ya juu ili kumvutia na kumridhisha mteja na bidhaa/huduma zako.

Kulingana na elimu ya wanasaikolojia mtu yeyote hupenda kujibiwa mara moja pale anapokuwa na shauku ya kujua jambo fulani. Hivyo unaposhindwa kujibu au kutoa ufafanuzi wa jambo fulani kuhusu bidhaa/huduma kwa wakati, unajiweka kwenye nafasi mbaya ya kupoteza wateja wengi kila siku.

5. BADILIKA KULINGANA NA SOKO LINAVYOKUHITAJI KUBADILIKA:

Dhana ya Biashara na masoko inafanana na dhana ya muziki na mtu anayeucheza muziki huo. Yaani unapaswa kuendana na mdundo wa muziki pale unapokuhitaji. Hali kadhalika unapokuwa katika ulimwengu wa biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta soko lako linakuwa ni kuwafikia watu bilioni 7 waliopo duniani.

unawezaje kupata wateja mtandaoni unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Na bahati ni kwamba duniani wapo watu/kampuni/taasisi nyingi ambazo zinafanya biashara unayoifanya wewe, hivyo unapaswa kuwa mbunifu kila siku, unapaswa kuongeza ubora wa bidhaa na huduma, kuongeza mtandao wa washirika wako duniani, bidhaa/huduma mpya na mambo mengi ambayo hujitokeza kila siku kulingana na uhitaji wa wateja. Hapa inakubidi uwe mwanafunzi mwenye uwezo wa kunyumbulika wakati wowote kwa ajili ya wateja wako.

Kwanini ufanye hivyo? Majibu zaidi yanapatikana kupitia makala hizi hapa:

Zaidi, tambua Tovuti ya kwanza kabisa kuundwa duniani bado ipo hewani (info.cern.ch). Tovuti hii ilitengezwa kwa lugha ya kuundia mifumo ya kimtandao ya HTML na inaonyesha mistari michache tuu. Lakini sasa mambo ni tofauti sana katika uwanda wa usanifu na uendelezaji wa programu za kompyuta na tovuti. Kama mwandishi Marc Andreessen alivyonukuliwa mwaka 2011 akisema programu za kopyuta zinaila dunia.

Je unajiandaa vipi kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Tafadhali toa maoni yako kupitia comments hapo chini..

KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?

Iwe ni shirika binafsi, taasisi za uma(serikali), mashirika ya dini au biashara binafsi, matangazo ni muhimu sana katika maisha ya taasisi au biashara binafsi. Kutuma barua pepe, kuanzisha kurasa katika mitandao ya kijamii au kufikisha taarifa za ana kwa ana kwa uma ni bure (haijumuishi gharama za moja kwa moja). Lakini kutangaza biashara ni gharama zaidi, hata hivyo inakulazimu kuitangaza biashara yako. Makampuni na mashirika duniani hutumia gharama kubwa sana katika kujitangaza japokuwa tayari wana majina makubwa na bidhaa/huduma zao zinajulikana duniani kote. Sasa swali la msingi, kwanini uitangaze biashara yako? Makinika hapa leo kupata majawabu.

Coca cola Company kwa mfano, mwaka 2015 walitumia dola bilioni 3.96, 2016-dola bilioni 4, 2017-dola bilioni 3.96. Kwa upande mwingine Pepsi ambao ni mpinzani wa kibiashara wa Coca cola duniani wao mwaka 2015 walitumia dola bilioni 2.4 kufanya matangazo yao, mwaka 2016- dola bilioni 2.5, mwaka 2017 dola bilioni 2.4. Hii ni kwa mujibu wa tovuti ya Investopedia (http://www.investopedia.com). Sasa, jiulize Kwanini ni muhimu uitangaze biashara yako.!?

1. MASOKO: Katika muktadha wa ulimwengu wa kibiashara, masoko ndiyo moyo wa biashara haswa. Yaani ili biashara yoyote iweze kuendelea kufanya vizuri, haina budi kuwa na soko la kutosha la kuhudumia. Jiulize, bidhaa unazosambaza/unazouza au huduma unayotoa, kuna kampuni au biashara ngapi ambazo zinafanya kitu hicho hicho unachokifanya.!? Kama hauko peke yako, basi hauna budi kutafuta masoko kwa hali na mali ili biashara yako ipate hadhira ya kuhudumia.

2. KUTAMBULISHA BIDHAA/HUDUMA MPYA: Ukuaji wa biashara/kampuni au taasisi yako hujumuisha kwa kiasi kikubwa ubunifu kila siku. Sehemu ya ubunifu huo pia huchagiza utambulisho wa huduma/bidhaa mpya kwa wateja wako. Ili uweze kuwafikishia taarifa wateja wako kuhusu huduma/bidhaa mpya unayoongeza katika biashara/kampuni au taasisi yako, unalazimika kuitangaza huduma/bidhaa hio mpya ili ifike kwa urahisi na usahihi kwa wateja wako.

3. ELIMU KUHUSU BIDHAA/HUDUMA ZITOLEWAZO NA TAASISI:Taasisi yako inapotoa huduma/bidhaa zake kwa mlaji wa mwisho au mteja wako hujumuisha zaidi sana elimu ya jinsi ya kutumia bidhaa/huduma hio. Sio watu wote watajua jinsi au njia za kuipata na kutumia kwa usahihi bidhaa/huduma zinazotolewa na taasisi yako. Vile vile ili elimu hio kuhusu bidhaa/huduma zako ipate kufika kwa mlaji wa mwisho au mteja wako huna budi kufanya tangazo. Hivyo matangazo ya namna hii yenye lengo la kutoa elimu ni muhimu sana katika kuhakikisha huduma/bidhaa zako zinafika kwa wateja lakini zaidi zinatumika kwa usahihi ule unaohitajika.

4.KUTENGENEZA MVUTO WA KIBIASHARA:

Matangazo ni njia bora zaidi kutengeneza mvuto wa kibiashara. Hapa kuna namna nyingi sana katika kutengeneza mvuto huu wa kibiashara kwa kutumia teknolojia ya matangazo. Aina ya mavazi au sare zinazohimizwa kuvaliwa katika taasisi yako, muundo wa rangi rasmi za taasisi, logo ya taasisi pamoja na jina la taasisi linavyohusiana na aina ya bidhaa/taasisi inayotolewa. Mvuto huu wa kibiashara hufanya matangazo ya kiautomatiki yanayokwenda moja kwa moja katika maisha ya kila siku ya mlaji wa mwisho au mteja. Huku mtandaoni tunatumia teknolojia ya SEO kutengeneza mvuto huu. Sasa kufahamu zaidi kuhusu SEO fuatana na makala hii hapa;

5. KUKUZA JINA LA KAMPUNI DUNIANI:

Matangazo ni sauti ya taasisi kuhusu bidhaa/huduma zake kwa wateja wao. Hivyo taasisi inavyofanya matangazo ndivyo inavyozidi kujiongezea wigo wa sauti yake kufika duniani kote. Duniani kuna kadiriwa kuwa na watu zaidi ya bilioni 7, hivyo unapofanya tangazo moja ni ngumu sana kuwafikia watu wote hao zaidi ya bilioni 7 duniani. Hivyo unapofanya matangazo kwa ajili ya wateja wako duniani mara kwa mara, unaimarisha jina la kampuni kitu ambacho huimarisha bidhaa/huduma zako zaidi pia.

6. KUJIKITA KWA WATEJA MAALUM TAASISI INAYODHAMIRIA KUWAPATA:

Kwa kawaida unapojihusisha na biashara ya kuuza nguo kama taasisi, wateja wako wakubwa watakuwa ni wauzaji wa nguo wadogo wadogo, wanamitindo na watu wengine wanaopenda kuvaa nguo za aina mbali mbali kila siku. Hivyo unapofanya matangazo ya taasisi yako, unajiweka kwenye nafasi ya kuwapata wateja haswa wale ambao taasisi imedhamiria kuwafikia.

7. UWEZO WA TAASISI KUHUDUMU:

Kwa kiasi kikubwa matangazo huimarisha uwezo wa taasisi kuhudumu. Hivyo taasisi yako inapofanya matangazo inajiweka kwenye nafasi ya kujiweka tayari kuhudumu kwa wateja wale wote wanaoletwa na matangazo hayo. Hivyo taasisi inayofanya matangazo hujiweka kwenye nafasi ya kuwa na ufanisi zaidi kwenye utendaji wake wa kila siku.

Hivyo kwa ufupi hayo ni baadhi ya mambo muhimu kuhusu Umuhimu wa Ufanyaji wa Matangazo katika taasisi/kampuni au biashara yako. Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi tukupatie usaidizi pale unapohisi kukwama katika biashara zako katika muktadha wa teknolojia ya habari na mawasiliano.

Namna bora ya kuitangaza biashara yako ni kupitia matumizi ya tovuti rasmi ya biashara yako pamoja na matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii ili kuhakikisha biashara yako inabaki katika akili za wateja wako kila siku. Hivyo pitia makala kupitia links hizo hapo chini ili uzidi kufahamu mambo muhimu kwa ajili ya afya ya biashara yako.

  1. https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “KWANINI NI MUHIMU KUWA NA TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/website-inasaidia-vipi-kuimarisha-biashara-yako/ yenye kichwa “WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?” 
  3. https://rednet.co.tz/ifahamu-nguvu-ya-mitandao-ya-kijamii-katika-biashara-yako/ yenye kichwa “IFAHAMU NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO”

Una maoni au lolote kuhusu makala hii ya leo? Tafadhali, acha comment yako hapo chini na changia hoja yako. Karibu sana.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uitangaze biashara yako?