Tag: business plan

OFA YA MSIMU WA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN

Tunawatakia Ndugu zetu Waislamu wote Ramadhan Kareem! Rehema za Mwenyezi MUNGU zikawe pamoja nanyi katika kipindi hiki. Kwa kutambua umuhimu wa Kipindi Hiki kitakatifu, OFA YA MSIMU WA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN IMEFUNGUKA ambapo sasa utajipatia huduma hizi kwa gharama nafuu ili kuzidi kuimarisha biashara yako:

i. Website Design (500k ✔️ 1.2m❌)

ii. Business Plan + 100 Business cards (350k ✔️ 600k❌)

iii. Ushauri na Usimamizi (mentorship) BURE kabisa.

Kuendana na OFA hio kuna makala hizi hapa ambazo kwa hakika zitakusaidia sana katika kuendesha biashara yako huku mtandaoni. Fuatana nazo mpaka mwisho:

https://rednet.co.tz/yafahamu-mashbulizi-ya-kimtandao-cyber-attacks-na-athari-zake-katika-biashara-kampuni-yako/ yenye kichwa YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO (CYBER ATTACKS) NA ATHARI ZAKE KATIKA BIASHARA/KAMPUNI YAKO.

https://rednet.co.tz/kwanini-uitangaze-biashara-yako/ yenye kichwa KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?

https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-teknolojia-ya-intaneti-na-kompyuta-katika-biashara-yako/ yenye kichwa UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA KATIKA BIASHARA YAKO.

https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE/TOVUTI RASMI YA BIASHARA YAKO.

Zaidi, Karibu DM tuwasiliane kwa undani. Muda wa kuimarisha biashara yako ndio huu. Usiache OFA hii ikupite.

Simu/Whatsapp: 0765834754
email: info@rednet.co.tz / fvitalice@gmail.com
Web: https://rednet.co.tz

Makusudio (purpose) ya biashara yana umuhimu gani?

MAKUSUDIO (PURPOSE) YA BIASHARA YANA UMUHIMU GANI?

Umeshawahi kujiuliza, Hivi siku biashara yako ikifa, Je, mteja wako au/na Dunia itapungukiwa nini? Unaufanikisha vipi mpango wako wa kuhakikisha biashara yako inakuwa na upekee wake ambao unawavutia zaidi wateja? Makusudio (purpose) ya biashara yana umuhimu gani? Makinika mpaka mwisho hapa ufahamu zaidi..

Bila shaka wakati unaanzisha biashara yako kuna dhamira ambayo ilikusukuma kuanzisha biashara hio. Lakini waswahili wanasema “Mipango sio matumizi”. Kwa hakika umeshashuhudia watu wanapoanza mwaka mpya huwa wanapanga mambo mengi, lakini mangapi huwa yanafanikiwa kufikia December?

Wataalam wanakwambia “ukipanga sana utakufa na mipango yako kichwani”. Unahitaji uthubutu na utekelezaji ili kuhakikisha kile unachokipanga kinafanikiwa. Kusudio (Purpose) la biashara ni utamaduni wa kuendesha biashara katika uelekeo ule ambao wewe mfanyabiashara umeunuia tangu mwanzo. Leo hapa tutashare mambo machache kuhusu umuhimu na jinsi ya kutengeneza hayo Makusudio. Kwa undani zaidi huwa tunashare kila siku kwa wale tu wenye namba yetu ya WhatsApp kupitia status zetu. Gusa namba hii hapa 0765834754 kisha hakikisha unaisave kwenye contacts zako, ukimaliza nitumie text yenye jina lako.

KWANINI UWE NA DHAMIRA/KUSUDI (PURPOSE) KATIKA BIASHARA YAKO?

Hebu anza kujiuliza, “Kwanini ninafanya hiki ninachokifanya”. Share jibu lako kwenye replies hapo chini. Sasa utafiti uliofanywa na shirika la kimataifa la EY mwaka 2017 ulionyesha, Wakurugenzi wa Biashara wakisema kuwa wanahitaji kufanya bidii zaidi ili kuhakikisha makusudio (purposes) yao waliyojiwekea katika biashara zao yanaleta mafanikio zaidi hasa katika maeneo ya Uongozi, Mafunzo na Huduma kwa wateja. Hii ina faida gani katika biashara?

i. UKUAJI: Kampuni/Biashara zinazoendeshwa kwa dhamira thabiti walizojiwekea hukua kwa haraka zaidi kuliko zile zenye dhamira dhaifu. Tafiti zinaonyesha kuwa 48% ya kampuni zilizojiwekea dhamira na makusudio ya dhati zimekua kwa 10% au zaidi ndani ya miaka 3 iliyopita ukilinganisha na 42% ya kampuni/biashara ambazo hazikujiwekea makusudio/dhamira kwa maendeleo yao ndani ya walau miaka 5.

Biashara zenye makusudio na dhamira inayoeleweka wa wafanyakazi ndani ya taasisi zimeonekana kuwa uwezekano wa zaidi ya 50% ya kupata masoko Mapya.

ii. KUHUSU MTEJA WA KUDUMU: Japokuwa mission na values zs biashara yako huchangia kwa kiasi kikubwa kupata wateja wa kudumu. Hata hivyo imeonekana 80% ya wakurugenzi wa biashara walikubali kuwa “Taasisi Imara ni ile inayoshirikisha makusudio yake na watu hupata wateja wengi zaidi wa kudumu”.

Jambo ambalo huongeza thamani ya biashara kwa watu kadiri ya siku za kuhudumu zinavyosonga kwa kuwa mteja amepewa nafasi ya kuona na kutambua jinsi kampuni/biashara inamjali katika kutoa bidhaa bora na huduma zinazokidhi mahitaji.

iii. KUHUSU UBUNIFU: Utafiti uliofanya na shirika la Deloitte unaonyesha kuwa Biashara yenye makusudio ya dhati huhamasisha shughuli za ubunifu zaidi kwa wafanyakazi wake kuliko zile zisizo na makusudio yaliyo wazi. Wafanyabiashara wanaozingatia dhamira na makusudio yao ya wazi katika biashara hujiweka katika nafasi ya kunasa ubunifu muhimu ambao utabadili uelekeo wa taasisi kuelekea katika mafanikio.

iv. UKUAJI WA KIUCHUMI: Hatimaye, lengo kuu la biashara/kampuni yoyote ni kuhakikisha Faida inatengenezeka na uchumi unaimarika. Hata hivyo unapokuwa na makusudio yanayoeleweka wazi ni rahisi zaidi kupata faida na kuimarisha uchumi wa biashara kwa kipindi kirefu zaidi.

Imeonekana kuwa na makusudio dhahiri huongeza hadhi ya biashsra katika jamii na kuchochea upatikanaji wa wateja wa kudumu kila kukicha. Hapo Makusudio (purpose) ya biashara yana umuhimu gani? Umeshaanza kupata picha sasa?

UNAWEZAJE KUTENGENEZA MAKUSUDIO YA BIASHARA YAKO?

Faida za kugundua makusudio ya biashara yako ni kubwa na zisiyopingika. Lakini Unapataje “Kusudi” la Biashara/Kampuni yako? Tuone hatua zifuatazo za kutengeneza Makusudio ya kuanzisha na kuendesha biashara yako.

Hatua 1: Pitia zile Core Values za biashara yako. Ni mambo yapi ambayo biashara yako inayajali zaidi (mf; Heshima, Uwajibikaji, Kuchapa Kazi, Upendo n.k) Biashara yako inazingatia mambo yepi katika utendaji wake wa kila siku? Tupe majibu katika replies hapo chini.

Hatua 2: Fuatilia kwa ukaribu biashara/kampuni ambazo zinakuvutia na ambazo ungependa kuiga utendaji wake (sio lazima biadhara/kampuni hizo uwe nazo field moja ya kuuza bidhaa au kutoa huduma) Lengo hapa ni kujifunza mambo mengi ya msingi katika utendaji wako wa kila siku.

Hatua 3: Hii ni ngumu kidogo, hebu jiulize, biashara/kampuni yako leo haipo duniani, je, wateja wako watapungukiwa na nini? Wateja wako watakukumbuka kwa lipi? Biashara/Kampuni yako itaacha legacy gani duniani? Ukipata ufumbuzi wa maswali haya utakuwa umefika mbali sana.

Hatua 4: Kama umeshafanya hatua 3 zilizopita basi hapo jua umeshafungua koki, kilichopo mbele ni kazi tu. Hebu jiulize, Biashara/Kampuni inajiwekea malengo gani ndani miaka fulani ijayo? Malengo hayo bila shaka huja kutokana na zile values zako ambazo ulishajiwekea.

Hatua 5: Sasa kusanya hayo malengo utayoyapata katika hatua iliyopita ili kutengeneza dhamira na makusudio ya kampuni/biashara yako. Ukimaliza jiulize tena, “je makusudio haya yataleta mapato?” Hakikisha makusudio unayoweka yanakusaidia kunasa mapato zaidi.

Hatua 6: Zama field sasa. Hakikisha kila mmoja anaelewa makusudio yaliyowekwa kwenye taasisi/kampuni hio mara moja. Ikitokea watu hawajaelewa makusudio hayo waelekezwe mpaka waelewe, ama sivyo badili dhamira na ibadilishwe.

Hata hivyo habari njema ni kwamba, kama unahisi hujaweza kung’amua makusudio (purpose) ya biashara hio unafanya, inawezekana kabisa hujatakari kwa kina na kuyaona. Kiuhalisia hakuna biashara ambayo haina Kusudio, lazima tu kusudio lipo na ndio linafanya biashara iendelee kuwepo.

Na zaidi inawezekana wafanyabiashara/wafanyakazi wenzako tayari wanajua wateja na dunia inataka nini kutoka kwenye taasisi yako. Hivyo mbinu ya kwanza ya kung’amua kitendawili hiki ni kubadili namna ya kuwazs na kuelewa mambo kutoka sub-conscious understanding (nimekosa kiswahili chake).

Mpaka kuwa conscious understanding. Halafu kifuatacho ni kuingiza utamaduni huo moya katika shughuli zako za kila siku katika biashara. Makusudio ni Utamaduni, sio mabadiliko ya fasheni tu. Una lolote la kuchangia na kuongezea kwenye makala yetu ya leo kuhusu Makusudio (purpose) ya biashara yana umuhimu gani? Tafadhali karibu.

Pitia makala hizi hapa ili kupata mfululizo mzuri wa maarifa kutoka kwenye somo ulilolipata leo. Gusa links zifuatazo kisha jifunze zaidi..

  1. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  2. USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA
  3. FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI

FAHAMU KUHUSU MFUMO WA MAWASILIANO YA SIMU (MOBILE ECOSYSTEM) NA FAIDA ZAKE KATIKA BIASHARA

Je Wajua?

Mfumo wa mawasiliano ya simu (mobile ecosystem) huchangia shemu muhimu sana katika uchumi wa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara? Uchumi wa nchi hizo kwa pamoja umefikia thamani ya dola za kimarekani bilioni 110 ($110 b) ambayo ni sawa na 7.1% ya pato la taifa (GDP) katika mwaka 2017. Hii inajumuisha faida za moja kwa moja za mfumo huo, faida zisizo za moja kwa moja (indirect impact) pamoja na ukuaji wa uzalishaji unaoletwa na matumizi ya huduma za simu na teknolojia.

Tukigusia faida za moja kwa moja za mfumo huu wa mawasiliano ambao unajumuisha makampuni ya simu, watengenezaji wa huduma za miundombinu ya kiteknolojia, wasambazaji wa huduma/ bidhaa za simu, wafanyabiashara wa reja reja, watengenezaji wa simu na vifaa vyake pamoja na watengenezaji wa maudhui/applications/huduma za mtandaoni; mchango wao katika uchumi hukadiriwa kwa kupimwa thamani wanayochangia katika uchumi wa nchi husika ambayo hujumuisha bima ya wafanyakazi, faida ya ziada ya biashara pamoja na kodi.

Mwaka 2017, thamani iliyozalishwa na mfumo huu wa mawasiliano katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara ulikuwa dola bilioni 40 ambayo ni sawa na 2.5% ya pato la Taifa (GDP) ambapo makampuni ya simu peke yake yalijumuisha takribani 75% ya mchango huu.

Ukiachana na faida za moja kwa moja, zipo pia faida ambazo si za moja kwa moja (indirect impact) ambapo sekta hii hununua vifaa/huduma mbali mbali kutoka sekta nyingine. Kwa mfano makampuni ya simu hulazimika kununua umeme kutoka sekta ya nishati hali kadhalika wasambazaji na wafanya biashara wa reja reja wa vifaa/huduma za simu huhitaji usafiri kuwafikia wateja wao.

Kwa pamoja uzalishaji huu wa faida isiyo ya moja kwa moja ulitengeneza takribani 60$ mwaka 2017 (ambayo ni takribani 4% ya pato la taifa). Kiujumla ukiongezea na faida za moja kwa moja, sekta hii ya mawasiliano ya simu ilitengeneza 110$ bilioni sawa na 7.1% ya pato la taifa katika ukanda huu.

Hii inaleta picha gani Kibiashara?

Matumizi ya teknolojia ya simu pamoja na maendeleo ya simu za rununu (smartphones) huendesha uchumi kwa kuboresha uzalishaji, kupunguza costs za uendeshaji pamoja na kurahishisha upatikanaji wa huduma/bidhaa za kibinadamu.

Chanzo: Ripoti ya shirika la mawasiliano ya simu duniani la GSMA toleo la mwaka 2019.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”

TEKNOLOJIA KATIKA BIASHARA ZA KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA (TECHNOLOGY IN SUB SAHARAN BUSINESS )

Kwa watumiaji wengi wa simu za mkononi waishio Kusini mwa jangwa la Sahara, simu ya mkononi si kwamba ni kifaa cha mawasiliano tu, lakini zaidi ni kifaa muhimu cha kuperuzi mtandaoni na kupata huduma mbalimbali za msingi za kibinadamu. Ujio wa simu za rununu (Smartphones) eneo hilo umekuwa maradufu katika miaka ya hivi karibuni. Watumiaji wa simu za rununu wameongezeka kutoka 25% mwanzoni mwa muongo huu (2010’s) mpaka kufikia 44% mwishoni mwa mwaka 2017. Hii ni chini ya wastani wa kidunia wa 66% katika ongezeko hilo la watumiaji wa simu za mkononi. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa shirika la kimataifa la mfumo wa mawasiliano ya simu GSMA.

Watumiaji hao wa simu ambao ni 44% ya jumla watu waishio katika eneo hilo sawa na watu milioni 444 ambao pia ni aslimia 9% tu ya watumiaji wote wa simu za mkononi duniani wanatajwa kupatikana katika eneo hilo la kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia inatajwa kwamba ongezeko hilo la watumiaji litakuwa katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) kwa 4.8 katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2022, ambacho ni zaidi ya mara mbili ya CAGR ya dunia nzima katika kipindi hicho hicho.

Moja ya vitu vinavyotoa nguvu katika ongezeko hili ni pamoja na uwezo wa simu za rununu (janja) kuunganisha watu wengi kupitia huduma za intaneti na mitandao ya kijamii ambapo katika mitandao hio ndipo panapotumiwa na watu wengi kama sehemu ya kukutana, kubadilishana mawazo, kuburudika na kufanya biashara. Hivyo kufanya mitandao hio ya kijamii kuzidi kuwa na umuhimu kadiri muda unavyokwenda.

Kibiashara hii ina maana gani?

Ripoti hio ya GSMA iliyochapishwa mwaka 2018 inataja kwamba ukuaji wa teknolojia umerahisisha mambo mengi muhimu yakiwemo utolewaji wa elimu, maswala ya afya na tiba na pia kuwezesha mazingira bora ya kufanyika biashara katika kutunza na kuonyesha kumbukumbu mbalimbali, miamala ya kifedha na jinsi bora ya kumhudumia mteja hata akiwa mbali na mzalishaji kupitia majukwaa ya huduma za kifedha za kimtandao na IoT (Internet of Things). Ripoti hio pia inaakisi kasi ya ukuaji wa matumizi ya simu za rununu (samrtphones) pamoja na vifaa vya kiteknolojia mpaka kufikia mwaka 2025 katika utendaji na utoaji wa huduma mbalimbali za kibinadamu pamoja na shughuli za kibiashara katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”
  5. https://rednet.co.tz/kuanzishwa-kwa-eneo-huru-la-biashara-barani-africa-afcta-kuna-manufaa-gani-kwako/ yenye kichwa “KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?”
Unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA KATIKA BIASHARA YAKO?

Bila kujali unafanya biashara ya aina gani, teknolojia ya intaneti na kompyuta imekuwa kwa kiwango kikubwa sana duniani hivyo kupelekea kuathiri mfumo mzima wa uendeshaji biashara duniani. Mwaka 2011 mwandishi Marc Andreessen alinukuliwa akisema, “Softwares are eating the world” akiwa na maana ugunduzi wa programu za kompyuta unarahisisha shughuli nyingi za kibinadamu kufanyika kwa haraka, kwa unafuu na kwa ufanisi zaidi kila siku zinavyozidi kwenda mbele. Sasa unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Leo tufahamu kwa undani.

Kufikia Octoba, mwaka 2018 tovuti ya Lifehacks (lifehacks.io) iliripoti kwamba jumla ya tovuti bilioni 1.9 zilithibitika uwepo wake kwenye intaneti pamoja na kuripotiwa kuwepo kwa machapisho (posts) zaidi ya milioni tano (5) ya blogu mbali mbali duniani kila siku. Tafiti hii ya kimtandao inakupa sababu mbali mbali za kukuwezesha kufanya biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta. Fuatana nasi.,

1. KUWA NA MPANGO WA BIASHARA ILI KUJUA KIUNDANI UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA:

Ukiwa na ndoto za kufanya biashara yako iwe na mafanikio maradufu, huna budi kuwa na mpango madhubuti wa kibiashara ambao utaainisha aina ya biashara unayoifanya, Jina la biashara linaloendana na aina ya bidhaa/huduma unayotoa, maudhui bora ya tovuti, soko unalolilenga na mbinu stahiki za kulikamata soko la kudumu.

Unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?MPANGO WA BIASHARA

2. TAFUTA NA CHAGUA JINA ZURI LA TOVUTI YA BIASHARA YAKO MTANDAONI:

Unapofikiria kuanzisha biashara, fikiria soko kwanza kabla ya aina ya biashara unayoitaka. Yaani tizama kwenye jamii, changamoto zilizopo ambazo hazijatatuliwa au hazionekani kama ni changamoto sana kwa muda huo, halafu tafuta suluhisho la changamoto hizo. Suluhisho hilo liendane na Jina zuri la kuwasilisha kile unachotaka kutatua kwenye jamii.

Uza suluhisho na si bidhaa kama bidhaa. Ukishapata Jina zuri, tengeneza tovuti yako au tafuta wataalamu waliobobea kwenye ujenzi na uendelezaji wa tovuti bora za kibiashara. KUMBUKA Tovuti sio Bidhaa bali ni Jukwaa la kufanyia biashara zako kama ilivyo ofisi yako, Fremu au Meza ya kuuzia bidhaa zako kila siku. Tofauti na ofisi, fremu au meza., tovuti ni jukwaa la kimtandao linalokuwezesha kuonyesha bidhaa/huduma zako dunia nzima kiurahisi zaidi mara moja. Kuhusu Umuhimu na faida za tovuti (website) katika biashara yako tayari nimekuwekea makala hizi hapa. Zitakufaa sana katika kuimarisha biashara yako ukizipitia zote.

3. TANGAZA NA WEKA UTARATIBU WA KUFUATILIA BIASHARA YAKO:

Dunia inakadiriwa kuwa na watu zaidi ya bilioni 7 mpaka sasa. Kati ya hao watumiaji wa mitandao ya kompyuta wanakadiriwa kufika bilioni 4 ikiwa ni takwimu zilizowasilishwa na yovuti ya lifehacks. Katika watu zaidi ya bilioni 4 ambao ni watumiaji mubashara wa mitandao ya kompyuta na simu, zaidi ya watu bilioni 2.234 wamegundulika kuwa ni watumiaji wa mtandao wa kijamii wa facebook peke yake.

Mfumo wa kimtandao wa kompyuta uitwao Internet Live Stats (ILS) unatumika kufuatilia watumiaji mubashara wa watumiaji wa Intaneti duniani kote kila siku. Hii ina maana kwamba zaidi ya nusu ya jumla ya watumiaji wote wa mitandao ya kompyuta na simu duniani wanapatikana facebook. Vilevile asilimia thelathini (30%) ya jumla ya idadi nzima ya watu wanaoishi duniani ni watumiaji wa facebook.

Kwa kusema hivyo, tayari tumekuwekea makala maalum itakueleza kwanini ni muhimu uitangaze biashara yako kila siku. Tafadhali ipitie makala hio mpaka mwisho kupitia link hii hapa yenye kichwa KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO.

unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Hivyo kwa kuutumia vyema mtandao wa facebook peke yake kibiashara unajiweka kwenye nafasi ya kuwafikia zaidi ya watu bilioni 2 ambao wanaweza kuwa wateja wazuri katika biashara unayoifanya. Vile vile watu zaidi ya bilioni 1 wamefahamika kuwa ni watumiaji wa mtandao unaoshika kasi wa Instagram.

Zaidi ya hayo pia kama mfanyabiashara mwenye kiu ya mafanikio una wajibu wa kufuatilia maendeleo ya biashara/kampuni/taasisi yako katika muktadha wa kuichumi na masoko. Biashara inabidi iwe inakua katika viwango vinavyohitajika kulingana na kasi ya soko la dunia.

Hivyo baada ya kujiuliza unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?, sasa unao uwezo wa kufuatilia biashara yako kwa kutumia takwimu sahihi kama ongezeko la wateja ndani ya muda fulani (wiki, mwezi au mwaka), ongezeko la faida, taarifa za mapato na matumizi na zaidi, usalama wa taarifa zako kibiashara.

Pia katika ufuatiliaji unaweza kuongeza njia kusambaza taarifa kuhusu biashara yako. Moja ya njia hizo ni Search Engine Optimization ambayo ni huduma inayotolewa na makampuni ya programu za kompyuta na mitandao. Huduma hii hukupatia nafasi ya kusambaza links za tovuti au mifumo yako ya kompyuta ambapo mtu yeyote anapotafuta bidhaa au huduma zako katika mtandao, basi inakuwa rahisi zaidi kukupata kwa kuandika maneno yanayohusu huduma hio unayotoa.

4. JIBU KWA WAKATI NA KWA UWELEDI ILI UNAPOJIULIZA UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA MTANDAONI UPATE ULE MVUTO WA KIBIASHARA

Unapokuwa mfanyabiashara au mhusika katika kampuni/taasisi fulani maana yake upo hapo kwa ajili ya wateja wako, hivyo unapaswa kutoa majibu na ufafanuzi wowote unaofika kwako kutokea kwa wateja wako. Aina ya majibu au ufafanuzi wako huchangia kwa kiasi kikubwa kupata wateja wapya kila siku au kupoteza wateja kila siku. Waswahili wanasema “Kauli Njema ni Silaha.” Hivyo kwenye kauli zako za kuhudumu ni lazima uweke uweledi wa hali ya juu ili kumvutia na kumridhisha mteja na bidhaa/huduma zako.

Kulingana na elimu ya wanasaikolojia mtu yeyote hupenda kujibiwa mara moja pale anapokuwa na shauku ya kujua jambo fulani. Hivyo unaposhindwa kujibu au kutoa ufafanuzi wa jambo fulani kuhusu bidhaa/huduma kwa wakati, unajiweka kwenye nafasi mbaya ya kupoteza wateja wengi kila siku.

5. BADILIKA KULINGANA NA SOKO LINAVYOKUHITAJI KUBADILIKA:

Dhana ya Biashara na masoko inafanana na dhana ya muziki na mtu anayeucheza muziki huo. Yaani unapaswa kuendana na mdundo wa muziki pale unapokuhitaji. Hali kadhalika unapokuwa katika ulimwengu wa biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta soko lako linakuwa ni kuwafikia watu bilioni 7 waliopo duniani.

unawezaje kupata wateja mtandaoni unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Na bahati ni kwamba duniani wapo watu/kampuni/taasisi nyingi ambazo zinafanya biashara unayoifanya wewe, hivyo unapaswa kuwa mbunifu kila siku, unapaswa kuongeza ubora wa bidhaa na huduma, kuongeza mtandao wa washirika wako duniani, bidhaa/huduma mpya na mambo mengi ambayo hujitokeza kila siku kulingana na uhitaji wa wateja. Hapa inakubidi uwe mwanafunzi mwenye uwezo wa kunyumbulika wakati wowote kwa ajili ya wateja wako.

Kwanini ufanye hivyo? Majibu zaidi yanapatikana kupitia makala hizi hapa:

Zaidi, tambua Tovuti ya kwanza kabisa kuundwa duniani bado ipo hewani (info.cern.ch). Tovuti hii ilitengezwa kwa lugha ya kuundia mifumo ya kimtandao ya HTML na inaonyesha mistari michache tuu. Lakini sasa mambo ni tofauti sana katika uwanda wa usanifu na uendelezaji wa programu za kompyuta na tovuti. Kama mwandishi Marc Andreessen alivyonukuliwa mwaka 2011 akisema programu za kopyuta zinaila dunia.

Je unajiandaa vipi kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Tafadhali toa maoni yako kupitia comments hapo chini..