Tag: business growth

Njia ya Kompyuta katika kuhifadhi data utajuaje pale biashara yako inapojiendesha kwa hasara changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika

CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.

Bila shaka umeshasikia misemo kama ‘survival for the fittest’ ama ‘Bahari tulivu haizalishi nahodha hodari’, wengine wanakwambia “Mwanzo mgumu”. Sasa kwenye biashara, mambo yapo hivyo hivyo, changamoto haziepukiki. Sasa leo tuazione changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika kabisa. Twende sambamba.

Leo hii, duniani kunaripotiwa kuwapo takriban kampuni/biashara 150 milioni zinazoanza (startups), huku kukiwa na ongezeko la kampuni hizo milioni 50 kila mwaka. Kwa wastani kuna kampuni zinazoanza 137,000 zinaanzishwa kila siku. Hebu niambie, umeshaanzisha biashara ngapi hadi leo? ngapi zimeshakufa? Ngapi upo nazo mpaka leo? tuambie kwenye comments pale chini.

Lakini swali la msingi ni je, hizi kampuni zinazoanza, zinaweza vipi kuhimili mawimbi makali ya changamoto zilizopo katika ulimwengu wa biashara duniani? haswa eneo la Kusini mwa jangwa la Sahara (ambalo linatajwa kuwa na changamoto nyingi zaidi za kibiashara).

unaweza vipi kukabiliana na hasara katika biashara yako?

changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika

Takwimu zinaonyesha kuwa 80% ya biashara/kampuni zinazoanza hufa ndani ya mwaka wa kwanza tu tangu kuanzishwa kwake. Na katika hizo 20% zilizobaki 10% hufa ndani ya miaka mitano tangu kuanzishwa. Tatizo ni nini? Wafanyabiashara hawa wanakosea wapi? Ni changamoto gani hizo ambazo pengine wafanyabiashara/waanzilisi wa kampuni hizo hawakuwa wanazijua mpaka zinapelekea biashara/kampuni zao kufa kabla hazijafikia ndoto na malengo yale makubwa ambayo waanzilishi walijiwekea mwanzoni. Hizi changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika kabisa.

Sasa leo tuzione hizo changamoto katika biashara mpya/inayoanza, ni funzo lisiloepukika kweli?;

1. USHINDANI MKALI

Hakuna wakati katika historia ya mwanadamu biashara zimekuwa zikifanyikwa kwa ushindani kama sasa. Yaani usitegemee kuanzisha biashara ambayo haina ushindani. Pia ni ngumu sana kuanzisha biashara ambayo haijawahi kufanyika kabisa hapo kabla. Hivyo jipange na ujiandae kisaikolojia.

Ujio wa matumizi ya intaneti umeongeza sana hali ya ushindani ambapo kwa sasa masoko hutafutwa kwa njia za kidijitali zaidi. Biashara zinahamia mtandaoni na hivyo huna budi kuhakikisha unatafuta wateja kwa nguvu sana kwa njia za Digital marketing, social media marketing, affiliate marketing na nyingine nyingi ili kuhakikisha biashara yako inaendelea kupata wateja wapya na kuwafikia wale ulio nao kirahisi zaidi.

Lakini njia rahisi (japo sio nyepesi) ya kuepuka ushindani sokoni ni kuwa MKIRITIMBA (Being a Monopoly). Hii ni ile hali ya kucontrol soko na kukamata wateja wengi kiasi kwamba washindani wako hawana nguvu ya kupambana na wewe sokoni. Zaidi kuhusu ukiritimba fuatilia makala hii hapa

2. WATU SAHIHI

Waswahili wanasema, Biashara ni watu. Hii haiishii kwa watu kwa maana ya wateja peke yake, watu hawa haswa wanangukia kwenye wabia, wafanyakazi na washauri wako katika biashara. Hawa wana mchango mkubwa na muhimu sana katika kuua au kuendeleza biashara yako.

Hii Rednet ni mfano sahihi katika sehemu hii kwa kuwa mwanzoni Rednet Technologies ilihisusha watu 6. Lakini kutokana na kutoshare vision na sababu zingine, Rednet haikuweza kushamiri katika mwaka wake wa kwanza mpaka tulipoamua kupunguza watu mpaka kupata watu sahihi wa kufanya nao kazi kwa maslahi mapana ya kampuni. Unapoamua kuanzisha biashara/kampuni mpya hakikisha unazungukwa na watu sahihi watakaoimarisha zaidi biashara/kampuni hio. Wahenga wanasema “Ndege wanye manyoya yanayofanana, ndio wanaoruka pamoja”. Take that note.

3. MASWALA YA FEDHA

Moja kati ya vitu vinaua biashara/kampuni nyingi ni Kutokujua kutofautisha maswala ya fedha ya kampuni na yale binafsi. Elewa, ukishaingiza pesa kwenye biashara/kampuni, pesa hio sio Binafsi tena. Inatakiwa izunguke mpaka itoe return/faida ambayo ndio inaweza kutumika kwa matumizi binafsi. Hii ni changamoto kubwa na inayohitaji umakini mkubwa ili kuihimili. Lile gepu la masikini na tajiri kwa kiasi kikubwa huwa linapigwa kutokana na uwezo wa kupambana na changamoto hii.

changamoto katika biashara mpya/inayoanza, hili ni funzo lisiloepukika

4. UFINYU WA RASILIMALI

Miongo michache iliyopita kuanzisha biashara/kampuni mpya ilimlazimu mtu kuwa na mtaji mkubwa ama kuwa na uwezo wa kufanya harambee ya kukuza mfuko wa uwekezaji. Kwa wakati huo mawazo mengi yalishindwa kuwa biashara/kampuni zenye tija.

Lakini leo hii kunakadiriwa kuanzishwa takribani biashara mpya 137,000 kila siku duniani kote. Hii ni kutokana na kukua kwa kasi ya teknolojia katika shughuli za kibiashara ambayo imerahisisha sana upatikanaji wa rasilimali. Lakini swala la maarifa ghafi (softskills) bado limekuwa ni changamoto katika uendeshaji wa biashara nyingi ambapo licha ya kuwa na wazo zuri ama mtaji wa kifedha, bado kuwa na maarifa ya kuendesha biashara/kampuni inabaki kuwa ni changamoto. Hivyo ukitoa Wazo, Vifaa vya kufanyia kazi na Pesa ya uwezeshaji, Maarifa ni rasilimali muhimu zaidi.

5. UWEZO WA KUTOA MAAMUZI SAHIHI

Katika kuanzisha biashara/kampuni mpya, moja kati ya Changamoto kubwa zinazowakabili waanzilishi ni Uwezo wa Kutoa maamuzi sahihi kulingana na wakati na hatua biashara/kampuni inayopitia. Moja kati ya changamoto zinazosumbua sana katika biashara.

Ukiwa mfanyabiashara/mbia wa kampuni unalazimika kufanya maamuzi mengi kila siku. Katika maamuzi hayo utajikuta wakati mwingine unafanya makosa kutokana na maamuzi yako, na pengine maamhzi hayo yanaweza kukukatisha tamaa na hata kuua biashara/kampuni yako ndani ya muda mchache.

Usiogope. Hakikisha unajifunza katika kila maamuzi unayochukua hata kama hayakuleta madhara katika biashara/kampuni yako. Wahenga wanasema “Busara hujengwa katika maamuzi“. Note hio, halafu ifanyie kazi kila siku. Kulifahamu hili kwa undani fuatana na makala hii hapa..

6. KUPATA UAMINIFU WA WATEJA

Hebu niambie, ilikuchukua muda gani kupata mteja wako wa kwanza tangu ulipoanzisha biashara/kampuni yako? Cocacola ilichukua mwaka mzima kuuza chupa moja ya soda katika mwaka wake wa kwanza tangu kuanzishwa.

Rednet ilichukua miezi 8 mpaka kumpata mteja wetu wa kwanza tangu tulipoanza shughuli zetu hapo mwaka 2016. Ni wakati mgumu sana katika biashara, lakini wahenga wanasema “Mteja ni mfalme.” Hivyo kupata mfalme wa kuhudumia kwa vyovyote si rahisi. Siku zote kizuri kinajiuza chenyewe ambapo huduma nzuri huvuta wateja zaidi kwa kutumia mbinu ya “Word of mouth“. Mbinu hii huzalisha wateja wa kudumu zaidi ambao huwa mabalozi wazuri wa biashara/kampuni yako. Jinsi ya utendaji katika biashara yako lazima ijengwe kumzunguka na kuridhisha wateja wako. Mteja asiporidhika, bado hujafanikiwa kibiashara. Zaidi tiririka na makala hii hapa kwa ajili yako..

7. USALAMA WA KIMTANDAO

Wakati huu tunaoishi ni wakati wa Kidijitali. Biashara/kampuni nyingi zinazoanzishwa zama hizi hufanyia shughuli zake mtandaoni, hivyo miundombinu ya utendaji katika biashara za kisasa kwa zaidi ya 75% hutegemea Nguvu ya mtandao.

Hata hivyo, Wadukuzi wa kimtandao wanafanya mazingira ya kiutendaji mtandaoni kuwa magumu na yenye kuhofisha. Matukio ya udukuzi na uhalifu wa kimtandao yanazidi kuongezeka kila uchwao. Tafiti zinaonyesha kufukia mwaka 2021 matukio ya uhalifu wa kimtandao yatakuwa yakitokea kila baada ya sekunde 11 duniani kote. Ili kujilinda dhidi ya uhalifu huu wa kimtandao, biashara zinazoanza hazina budi kuwa na miundombinu ya kimtandao ambayo ni imara zaidi kila wakati.

Zaidi kuhusu Usalama wa kimtandao unaweza kupata makala yetu mahsusi kupitia link hii KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?

Kifupi hizo ni changamoto chache ambazo zinazikabili biashara/kampuni inazoanza, ni funzo lisiloepukika kweli kweli. Je, wewe umepitia changamoto zipi wakati unaanzisha hio biashara yako uliyo nayo? Umeshajaribu kufanya biashara ngapi bila mafanikio mpaka kufikia sasa? Tafadhali tushirikishe ili watu wengine wapate kujifunza zaidi. Karibu.

Pia hakikisha unapitia makala hizi tumekuwekea hapa chini ili kuhakikisha unapata muendelezo mzuri kutokana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Gusa link kisha makinika..

  1. KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?
  2. BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA?
  3. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA
  4. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO

Ni matumaini yangu leo umefahamu kwa undani changamoto katika biashara mpya/inayoanza, funzo lisiloepukika. Utakwenda kukabiliana nazo vipi changamoto hizi za leo? Niambie kwenye comment hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu(website design, logo design, Digital consultacy n.k) BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

LIPA KODI KWA FAIDA YA BIASHARA YAKO

Wamiliki wengi wa biashara huanza katika Biashara binafsi (machinga/sole proprietor). Baadae hukua kufikia partnerships, wabia wa kampuni mpaka mashirika. Kadiri unavyotengeneza mifumo ya biashara yako ndivyo inakuwa rahisi kulipa kodi.

Kodi huja katika namna nyingi, unapofanya kazi, unalipwa ujira/mshahara, hapo utalipa “Income Tax”. Kutegemea na kiasi cha pesa unacholipwa, asilimia fulani hukatwa na muajiri wako na kulipwa kwenye Mamlaka za Kodi, % hio huitwa “Withholding Tax”, hii hutaiona kwenye paycheck yako kwani hulipwa na mwajiri moja kwa moja kwenda kwa Mamlaka za kodi.

Ukinunua bidhaa, fahamu kuna kodi pale unalipa ambayo inajumuishwa katika bei ya bidhaa hio. Kodi hio huitwa “VAT” ambayo ni kodi maarufu na yenye kuingiza mapato makubwa sana katika mamlaka za Kodi. Kama unamiliki mali/ardhi unalipa Kodi iitwayo “Property Tax” kulingana na thamani ya mali/ardhi yako hio.

Kulipa kodi ni wajibu wa kizalendo, lakini zaidi ni matakwa ya kisheria. Usipolipa kodi unajiweka kwenye mazingira ya kulipishwa faini au adhabu kwa mujibu wa sheria. Kodi unayolipa inakwenda sehemu mbalimbali za kiserikali kama mishahara ya watumishi wa serikali, polisi, jeshi la zimamoto na uokoaji, kuimarisha miundombinu, sekta ys afya n.k.

UNAEPUKA VIPI RUNDO LA KODI KWA MANUFAA?

Kuendesha biashara kunajumuisha gharama nyingi sana. Na katika kila gharama kuna kiasi cha kodi unatozwa. Fahamu, Ukinunua unalipa kodi, Ukiuza unamlipisha mtu kodi. Jambo hili linafanyika ukiwa unajua na hata bila ya wewe kujua.

1. MANUNUZI

Kodi ya VAT (Value of Added Tax/Kodi ya Ongezeko la Thamani) ambapo unaponunua bidhaa/huduma yoyote unakuwa unanunua kitu chako pamoja na kukilipia kodi yake ya VAT hapo hapo. Kodi hiyo huwa ni 18% ya thamani kamili ya bidhaa/huduma inayouzwa. Mfano unaponunua umeme wa 2,000/-, hapo unakuwa umelipia na kodi yake ambayo imejumlishiwa kwenye hio 2,000/- (indirect tax). Hali kadhalika katika bidhaa/huduma zingine kama mafuta, vocha, computer, chakula, gesi n.k. Kila unachonunua kina kodi yake, Hivyo kama mfanyabiashara hakikisha manunuzi yako yote yahusuyo gharama za uendeshaji (umeme, maji, chakula, mafuta, maintenance, usafi) yanakuwa na risiti zake halali. Risiti zako hueleza kodi zile ulizokatwa “withheld” katika manunuzi/matumizi ya biashara yako. Hivyo jambo hili litakupa unafuu katika kulipa kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).

2. MAUZO

Wafanyabiashara huwalipisha wateja wao VAT lakini wengi hawapendi kulipa kiasi hiko cha kodi katika Mamlaka ya Kodi. Jambo hili ni kinyume na sheria na linaweza kukuweka kwenye mikono ya kisheria yanayoweza kukufilisi mali, kukupeleka gerezani au vyote vikakupata.

Hivyo unapofanya mauzo katika biashara yako hakikisha unatoa risiti halali ili bidhaa unazouza ziwe kwenye uwiano mzuri wa thamani na Mamlaka za kodi

CHANGAMOTO:

i. Tafiti zinaonyesha kuwa zaidi ya 70% biashara hazilipi kodi. Hii inachochewa na upungufu wa elimu ya kodi pamoja na morali ya wananchi katika kulipa kodi.

ii. Pia kumekuwepo na sekta ambazo hazilipi kodi ipasavyo, mfano sekta ya madini, uvuvi, misitu na utalii. Hii imetokana na kutokuwepo na njia bora za ukusanyaji wa kodi katika maeneo hayo, hivyo kudidimisha mapato yao katika kodi.

iii. Kuwepo kwa misamaha mikubwa ya kodi (tax exemptions) kwa wawekezaji wa ndani na wale wa nje. Mbinu hii iliwekwa ili kuwavutia wawekezaji wazidi kumininika lakini matokeo yake yamekuja kudhoofisha sekta zingine za biashara kutokana na kutokuwepo kwa usawa katika makusanyo.

iv. UFISADI: Inarudisha maendeleo nyuma sana hali ya kutokuwepo kwa makusanyo ya kodi. Hali hii kwa kiasi kikubwa huchochewa na kukithiri kwa vitendo vya Ufisadi katika Mashirika ya Umma pamoja na Mamlaka za Kodi. Watu huishiwa morari ya kulipa kodi pale wakiona kodi zao zinaishia mifukoni mwa watu wachache tena kwa manufaa binafsi. Jambo hili ni baya sana katika maendeleo ya biashara. Likemewe kwa nguvu zote.

MATUMIZI YA ICT KATIKA MFUMO WA KODI:

Teknolojia ya ICT imekuja kuwa mkombozi katika mifumo ya mapato na kodi katika biashara na Mamlaka za Kodi katika kutunza kumbukumbu za walipa kodi. Teknolojia imeleta afadhali katika kukusanya kodi kupitia matumizi ya mashine za EFD ambayo hutumika kukusanya taarifa za kodi, mauzo na manunuzi katika biashara.

Mashine hizi za EFD zilianza rasmi kutumika mwaka 2013 zikiwa na lengo la kusajili wafanyabiashara wote pamoja na miamala yote ya mauzo na manunuzi nchini Tanzania. Mwaka 2014/15 Halmashauri ya manispaa ya jiji la Arusha ilianza kutumia mfumo wa LGRCIS (Local Government Revenue Collection Information System). Zaidi kuhusu mfumo wa mapato ya serikali za mitaa unaweza kupata kupitia makala kwenye link hii https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-na-mapato-ya-serikali-za-mitaa/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NA MAPATO YA SERIKALI ZA MITAA”

Kuanzia hapo Halmashauri 8 nchini Tanzania zilianza kutumia mfumo huo wa LGRCIS kama mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi katika Halmashauri zao. Hata hivyo mwaka 2016 mifumo yote ya makusanyo iliunganishwa katika mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi wa TRA.

Lakini bado mpaka sasa mfumo wa LGRCIS unaendelea kutumika ktika kukusanya mapato ya halmashauri ikijumuisha Ushuru, Tozo na kodi za leseni za biashara. Mfumo huo umerahisisha malipo ya kodi kupitia njia za malipo ya kielektroniki kama MPESA, Bank transfer, Tigopesa n.k.

Hivyo, katika mifumo ya kodi kupitia makala haya ni matumaini yangu umejifunza kitu muhimu katika namna unavyoendesha biashara yako kwa faida bila kukwaruzana na Mamlaka za Kodi. Una maoni yoyote? Tafadhali weka comment yako hapa chini. Pia unaweza kushare link ya makala hii ili kuhakikisha inawafikia watu wengi zaidi kwa faida ya biashara zetu.

Sasa tumekuandalia makala hizi hapa chini zenye lengo la kukuimarisha katika namna ya kulipa kodi na kuifahamu mifumo yake zaidi. Zitakusaidia sana ukizisoma zote. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-nchini-tanzania/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NCHINI TANZANIA”
  2. https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-urasinishaji-harmonization-katika-biashara/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA”
  3. https://rednet.co.tz/ukiritimba-katika-biashara-ni-asali-au-shubiri/ yenye kichwa “UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI”

FAHAMU KUHUSU MFUMO WA MAWASILIANO YA SIMU (MOBILE ECOSYSTEM) NA FAIDA ZAKE KATIKA BIASHARA

Je Wajua?

Mfumo wa mawasiliano ya simu (mobile ecosystem) huchangia shemu muhimu sana katika uchumi wa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara? Uchumi wa nchi hizo kwa pamoja umefikia thamani ya dola za kimarekani bilioni 110 ($110 b) ambayo ni sawa na 7.1% ya pato la taifa (GDP) katika mwaka 2017. Hii inajumuisha faida za moja kwa moja za mfumo huo, faida zisizo za moja kwa moja (indirect impact) pamoja na ukuaji wa uzalishaji unaoletwa na matumizi ya huduma za simu na teknolojia.

Tukigusia faida za moja kwa moja za mfumo huu wa mawasiliano ambao unajumuisha makampuni ya simu, watengenezaji wa huduma za miundombinu ya kiteknolojia, wasambazaji wa huduma/ bidhaa za simu, wafanyabiashara wa reja reja, watengenezaji wa simu na vifaa vyake pamoja na watengenezaji wa maudhui/applications/huduma za mtandaoni; mchango wao katika uchumi hukadiriwa kwa kupimwa thamani wanayochangia katika uchumi wa nchi husika ambayo hujumuisha bima ya wafanyakazi, faida ya ziada ya biashara pamoja na kodi.

Mwaka 2017, thamani iliyozalishwa na mfumo huu wa mawasiliano katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara ulikuwa dola bilioni 40 ambayo ni sawa na 2.5% ya pato la Taifa (GDP) ambapo makampuni ya simu peke yake yalijumuisha takribani 75% ya mchango huu.

Ukiachana na faida za moja kwa moja, zipo pia faida ambazo si za moja kwa moja (indirect impact) ambapo sekta hii hununua vifaa/huduma mbali mbali kutoka sekta nyingine. Kwa mfano makampuni ya simu hulazimika kununua umeme kutoka sekta ya nishati hali kadhalika wasambazaji na wafanya biashara wa reja reja wa vifaa/huduma za simu huhitaji usafiri kuwafikia wateja wao.

Kwa pamoja uzalishaji huu wa faida isiyo ya moja kwa moja ulitengeneza takribani 60$ mwaka 2017 (ambayo ni takribani 4% ya pato la taifa). Kiujumla ukiongezea na faida za moja kwa moja, sekta hii ya mawasiliano ya simu ilitengeneza 110$ bilioni sawa na 7.1% ya pato la taifa katika ukanda huu.

Hii inaleta picha gani Kibiashara?

Matumizi ya teknolojia ya simu pamoja na maendeleo ya simu za rununu (smartphones) huendesha uchumi kwa kuboresha uzalishaji, kupunguza costs za uendeshaji pamoja na kurahishisha upatikanaji wa huduma/bidhaa za kibinadamu.

Chanzo: Ripoti ya shirika la mawasiliano ya simu duniani la GSMA toleo la mwaka 2019.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”

TEKNOLOJIA KATIKA BIASHARA ZA KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA (TECHNOLOGY IN SUB SAHARAN BUSINESS )

Kwa watumiaji wengi wa simu za mkononi waishio Kusini mwa jangwa la Sahara, simu ya mkononi si kwamba ni kifaa cha mawasiliano tu, lakini zaidi ni kifaa muhimu cha kuperuzi mtandaoni na kupata huduma mbalimbali za msingi za kibinadamu. Ujio wa simu za rununu (Smartphones) eneo hilo umekuwa maradufu katika miaka ya hivi karibuni. Watumiaji wa simu za rununu wameongezeka kutoka 25% mwanzoni mwa muongo huu (2010’s) mpaka kufikia 44% mwishoni mwa mwaka 2017. Hii ni chini ya wastani wa kidunia wa 66% katika ongezeko hilo la watumiaji wa simu za mkononi. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa shirika la kimataifa la mfumo wa mawasiliano ya simu GSMA.

Watumiaji hao wa simu ambao ni 44% ya jumla watu waishio katika eneo hilo sawa na watu milioni 444 ambao pia ni aslimia 9% tu ya watumiaji wote wa simu za mkononi duniani wanatajwa kupatikana katika eneo hilo la kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia inatajwa kwamba ongezeko hilo la watumiaji litakuwa katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) kwa 4.8 katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2022, ambacho ni zaidi ya mara mbili ya CAGR ya dunia nzima katika kipindi hicho hicho.

Moja ya vitu vinavyotoa nguvu katika ongezeko hili ni pamoja na uwezo wa simu za rununu (janja) kuunganisha watu wengi kupitia huduma za intaneti na mitandao ya kijamii ambapo katika mitandao hio ndipo panapotumiwa na watu wengi kama sehemu ya kukutana, kubadilishana mawazo, kuburudika na kufanya biashara. Hivyo kufanya mitandao hio ya kijamii kuzidi kuwa na umuhimu kadiri muda unavyokwenda.

Kibiashara hii ina maana gani?

Ripoti hio ya GSMA iliyochapishwa mwaka 2018 inataja kwamba ukuaji wa teknolojia umerahisisha mambo mengi muhimu yakiwemo utolewaji wa elimu, maswala ya afya na tiba na pia kuwezesha mazingira bora ya kufanyika biashara katika kutunza na kuonyesha kumbukumbu mbalimbali, miamala ya kifedha na jinsi bora ya kumhudumia mteja hata akiwa mbali na mzalishaji kupitia majukwaa ya huduma za kifedha za kimtandao na IoT (Internet of Things). Ripoti hio pia inaakisi kasi ya ukuaji wa matumizi ya simu za rununu (samrtphones) pamoja na vifaa vya kiteknolojia mpaka kufikia mwaka 2025 katika utendaji na utoaji wa huduma mbalimbali za kibinadamu pamoja na shughuli za kibiashara katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”
  5. https://rednet.co.tz/kuanzishwa-kwa-eneo-huru-la-biashara-barani-africa-afcta-kuna-manufaa-gani-kwako/ yenye kichwa “KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?”
Unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA KATIKA BIASHARA YAKO?

Bila kujali unafanya biashara ya aina gani, teknolojia ya intaneti na kompyuta imekuwa kwa kiwango kikubwa sana duniani hivyo kupelekea kuathiri mfumo mzima wa uendeshaji biashara duniani. Mwaka 2011 mwandishi Marc Andreessen alinukuliwa akisema, “Softwares are eating the world” akiwa na maana ugunduzi wa programu za kompyuta unarahisisha shughuli nyingi za kibinadamu kufanyika kwa haraka, kwa unafuu na kwa ufanisi zaidi kila siku zinavyozidi kwenda mbele. Sasa unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Leo tufahamu kwa undani.

Kufikia Octoba, mwaka 2018 tovuti ya Lifehacks (lifehacks.io) iliripoti kwamba jumla ya tovuti bilioni 1.9 zilithibitika uwepo wake kwenye intaneti pamoja na kuripotiwa kuwepo kwa machapisho (posts) zaidi ya milioni tano (5) ya blogu mbali mbali duniani kila siku. Tafiti hii ya kimtandao inakupa sababu mbali mbali za kukuwezesha kufanya biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta. Fuatana nasi.,

1. KUWA NA MPANGO WA BIASHARA ILI KUJUA KIUNDANI UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA:

Ukiwa na ndoto za kufanya biashara yako iwe na mafanikio maradufu, huna budi kuwa na mpango madhubuti wa kibiashara ambao utaainisha aina ya biashara unayoifanya, Jina la biashara linaloendana na aina ya bidhaa/huduma unayotoa, maudhui bora ya tovuti, soko unalolilenga na mbinu stahiki za kulikamata soko la kudumu.

Unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

MPANGO WA BIASHARA

2. TAFUTA NA CHAGUA JINA ZURI LA TOVUTI YA BIASHARA YAKO MTANDAONI:

Unapofikiria kuanzisha biashara, fikiria soko kwanza kabla ya aina ya biashara unayoitaka. Yaani tizama kwenye jamii, changamoto zilizopo ambazo hazijatatuliwa au hazionekani kama ni changamoto sana kwa muda huo, halafu tafuta suluhisho la changamoto hizo. Suluhisho hilo liendane na Jina zuri la kuwasilisha kile unachotaka kutatua kwenye jamii.

Uza suluhisho na si bidhaa kama bidhaa. Ukishapata Jina zuri, tengeneza tovuti yako au tafuta wataalamu waliobobea kwenye ujenzi na uendelezaji wa tovuti bora za kibiashara. KUMBUKA Tovuti sio Bidhaa bali ni Jukwaa la kufanyia biashara zako kama ilivyo ofisi yako, Fremu au Meza ya kuuzia bidhaa zako kila siku. Tofauti na ofisi, fremu au meza., tovuti ni jukwaa la kimtandao linalokuwezesha kuonyesha bidhaa/huduma zako dunia nzima kiurahisi zaidi mara moja. Kuhusu Umuhimu na faida za tovuti (website) katika biashara yako tayari nimekuwekea makala hizi hapa. Zitakufaa sana katika kuimarisha biashara yako ukizipitia zote.

3. TANGAZA NA WEKA UTARATIBU WA KUFUATILIA BIASHARA YAKO:

Dunia inakadiriwa kuwa na watu zaidi ya bilioni 7 mpaka sasa. Kati ya hao watumiaji wa mitandao ya kompyuta wanakadiriwa kufika bilioni 4 ikiwa ni takwimu zilizowasilishwa na yovuti ya lifehacks. Katika watu zaidi ya bilioni 4 ambao ni watumiaji mubashara wa mitandao ya kompyuta na simu, zaidi ya watu bilioni 2.234 wamegundulika kuwa ni watumiaji wa mtandao wa kijamii wa facebook peke yake.

Mfumo wa kimtandao wa kompyuta uitwao Internet Live Stats (ILS) unatumika kufuatilia watumiaji mubashara wa watumiaji wa Intaneti duniani kote kila siku. Hii ina maana kwamba zaidi ya nusu ya jumla ya watumiaji wote wa mitandao ya kompyuta na simu duniani wanapatikana facebook. Vilevile asilimia thelathini (30%) ya jumla ya idadi nzima ya watu wanaoishi duniani ni watumiaji wa facebook.

Kwa kusema hivyo, tayari tumekuwekea makala maalum itakueleza kwanini ni muhimu uitangaze biashara yako kila siku. Tafadhali ipitie makala hio mpaka mwisho kupitia link hii hapa yenye kichwa KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO.

unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Hivyo kwa kuutumia vyema mtandao wa facebook peke yake kibiashara unajiweka kwenye nafasi ya kuwafikia zaidi ya watu bilioni 2 ambao wanaweza kuwa wateja wazuri katika biashara unayoifanya. Vile vile watu zaidi ya bilioni 1 wamefahamika kuwa ni watumiaji wa mtandao unaoshika kasi wa Instagram.

Zaidi ya hayo pia kama mfanyabiashara mwenye kiu ya mafanikio una wajibu wa kufuatilia maendeleo ya biashara/kampuni/taasisi yako katika muktadha wa kuichumi na masoko. Biashara inabidi iwe inakua katika viwango vinavyohitajika kulingana na kasi ya soko la dunia.

Hivyo baada ya kujiuliza unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?, sasa unao uwezo wa kufuatilia biashara yako kwa kutumia takwimu sahihi kama ongezeko la wateja ndani ya muda fulani (wiki, mwezi au mwaka), ongezeko la faida, taarifa za mapato na matumizi na zaidi, usalama wa taarifa zako kibiashara.

Pia katika ufuatiliaji unaweza kuongeza njia kusambaza taarifa kuhusu biashara yako. Moja ya njia hizo ni Search Engine Optimization ambayo ni huduma inayotolewa na makampuni ya programu za kompyuta na mitandao. Huduma hii hukupatia nafasi ya kusambaza links za tovuti au mifumo yako ya kompyuta ambapo mtu yeyote anapotafuta bidhaa au huduma zako katika mtandao, basi inakuwa rahisi zaidi kukupata kwa kuandika maneno yanayohusu huduma hio unayotoa.

4. JIBU KWA WAKATI NA KWA UWELEDI ILI UNAPOJIULIZA UNAWEZAJE KUTUMIA TEKNOLOJIA YA INTANETI NA KOMPYUTA MTANDAONI UPATE ULE MVUTO WA KIBIASHARA

Unapokuwa mfanyabiashara au mhusika katika kampuni/taasisi fulani maana yake upo hapo kwa ajili ya wateja wako, hivyo unapaswa kutoa majibu na ufafanuzi wowote unaofika kwako kutokea kwa wateja wako. Aina ya majibu au ufafanuzi wako huchangia kwa kiasi kikubwa kupata wateja wapya kila siku au kupoteza wateja kila siku. Waswahili wanasema “Kauli Njema ni Silaha.” Hivyo kwenye kauli zako za kuhudumu ni lazima uweke uweledi wa hali ya juu ili kumvutia na kumridhisha mteja na bidhaa/huduma zako.

Kulingana na elimu ya wanasaikolojia mtu yeyote hupenda kujibiwa mara moja pale anapokuwa na shauku ya kujua jambo fulani. Hivyo unaposhindwa kujibu au kutoa ufafanuzi wa jambo fulani kuhusu bidhaa/huduma kwa wakati, unajiweka kwenye nafasi mbaya ya kupoteza wateja wengi kila siku.

5. BADILIKA KULINGANA NA SOKO LINAVYOKUHITAJI KUBADILIKA:

Dhana ya Biashara na masoko inafanana na dhana ya muziki na mtu anayeucheza muziki huo. Yaani unapaswa kuendana na mdundo wa muziki pale unapokuhitaji. Hali kadhalika unapokuwa katika ulimwengu wa biashara kwa kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta soko lako linakuwa ni kuwafikia watu bilioni 7 waliopo duniani.

unawezaje kupata wateja mtandaoni unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?

Na bahati ni kwamba duniani wapo watu/kampuni/taasisi nyingi ambazo zinafanya biashara unayoifanya wewe, hivyo unapaswa kuwa mbunifu kila siku, unapaswa kuongeza ubora wa bidhaa na huduma, kuongeza mtandao wa washirika wako duniani, bidhaa/huduma mpya na mambo mengi ambayo hujitokeza kila siku kulingana na uhitaji wa wateja. Hapa inakubidi uwe mwanafunzi mwenye uwezo wa kunyumbulika wakati wowote kwa ajili ya wateja wako.

Kwanini ufanye hivyo? Majibu zaidi yanapatikana kupitia makala hizi hapa:

Zaidi, tambua Tovuti ya kwanza kabisa kuundwa duniani bado ipo hewani (info.cern.ch). Tovuti hii ilitengezwa kwa lugha ya kuundia mifumo ya kimtandao ya HTML na inaonyesha mistari michache tuu. Lakini sasa mambo ni tofauti sana katika uwanda wa usanifu na uendelezaji wa programu za kompyuta na tovuti. Kama mwandishi Marc Andreessen alivyonukuliwa mwaka 2011 akisema programu za kopyuta zinaila dunia.

Je unajiandaa vipi kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako? Tafadhali toa maoni yako kupitia comments hapo chini..