Tag: biashara

Makusudio (purpose) ya biashara yana umuhimu gani?

MAKUSUDIO (PURPOSE) YA BIASHARA YANA UMUHIMU GANI?

Umeshawahi kujiuliza, Hivi siku biashara yako ikifa, Je, mteja wako au/na Dunia itapungukiwa nini? Unaufanikisha vipi mpango wako wa kuhakikisha biashara yako inakuwa na upekee wake ambao unawavutia zaidi wateja? Makusudio (purpose) ya biashara yana umuhimu gani? Makinika mpaka mwisho hapa ufahamu zaidi..

Bila shaka wakati unaanzisha biashara yako kuna dhamira ambayo ilikusukuma kuanzisha biashara hio. Lakini waswahili wanasema “Mipango sio matumizi”. Kwa hakika umeshashuhudia watu wanapoanza mwaka mpya huwa wanapanga mambo mengi, lakini mangapi huwa yanafanikiwa kufikia December?

Wataalam wanakwambia “ukipanga sana utakufa na mipango yako kichwani”. Unahitaji uthubutu na utekelezaji ili kuhakikisha kile unachokipanga kinafanikiwa. Kusudio (Purpose) la biashara ni utamaduni wa kuendesha biashara katika uelekeo ule ambao wewe mfanyabiashara umeunuia tangu mwanzo. Leo hapa tutashare mambo machache kuhusu umuhimu na jinsi ya kutengeneza hayo Makusudio. Kwa undani zaidi huwa tunashare kila siku kwa wale tu wenye namba yetu ya WhatsApp kupitia status zetu. Gusa namba hii hapa 0765834754 kisha hakikisha unaisave kwenye contacts zako, ukimaliza nitumie text yenye jina lako.

KWANINI UWE NA DHAMIRA/KUSUDI (PURPOSE) KATIKA BIASHARA YAKO?

Hebu anza kujiuliza, “Kwanini ninafanya hiki ninachokifanya”. Share jibu lako kwenye replies hapo chini. Sasa utafiti uliofanywa na shirika la kimataifa la EY mwaka 2017 ulionyesha, Wakurugenzi wa Biashara wakisema kuwa wanahitaji kufanya bidii zaidi ili kuhakikisha makusudio (purposes) yao waliyojiwekea katika biashara zao yanaleta mafanikio zaidi hasa katika maeneo ya Uongozi, Mafunzo na Huduma kwa wateja. Hii ina faida gani katika biashara?

i. UKUAJI: Kampuni/Biashara zinazoendeshwa kwa dhamira thabiti walizojiwekea hukua kwa haraka zaidi kuliko zile zenye dhamira dhaifu. Tafiti zinaonyesha kuwa 48% ya kampuni zilizojiwekea dhamira na makusudio ya dhati zimekua kwa 10% au zaidi ndani ya miaka 3 iliyopita ukilinganisha na 42% ya kampuni/biashara ambazo hazikujiwekea makusudio/dhamira kwa maendeleo yao ndani ya walau miaka 5.

Biashara zenye makusudio na dhamira inayoeleweka wa wafanyakazi ndani ya taasisi zimeonekana kuwa uwezekano wa zaidi ya 50% ya kupata masoko Mapya.

ii. KUHUSU MTEJA WA KUDUMU: Japokuwa mission na values zs biashara yako huchangia kwa kiasi kikubwa kupata wateja wa kudumu. Hata hivyo imeonekana 80% ya wakurugenzi wa biashara walikubali kuwa “Taasisi Imara ni ile inayoshirikisha makusudio yake na watu hupata wateja wengi zaidi wa kudumu”.

Jambo ambalo huongeza thamani ya biashara kwa watu kadiri ya siku za kuhudumu zinavyosonga kwa kuwa mteja amepewa nafasi ya kuona na kutambua jinsi kampuni/biashara inamjali katika kutoa bidhaa bora na huduma zinazokidhi mahitaji.

iii. KUHUSU UBUNIFU: Utafiti uliofanya na shirika la Deloitte unaonyesha kuwa Biashara yenye makusudio ya dhati huhamasisha shughuli za ubunifu zaidi kwa wafanyakazi wake kuliko zile zisizo na makusudio yaliyo wazi. Wafanyabiashara wanaozingatia dhamira na makusudio yao ya wazi katika biashara hujiweka katika nafasi ya kunasa ubunifu muhimu ambao utabadili uelekeo wa taasisi kuelekea katika mafanikio.

iv. UKUAJI WA KIUCHUMI: Hatimaye, lengo kuu la biashara/kampuni yoyote ni kuhakikisha Faida inatengenezeka na uchumi unaimarika. Hata hivyo unapokuwa na makusudio yanayoeleweka wazi ni rahisi zaidi kupata faida na kuimarisha uchumi wa biashara kwa kipindi kirefu zaidi.

Imeonekana kuwa na makusudio dhahiri huongeza hadhi ya biashsra katika jamii na kuchochea upatikanaji wa wateja wa kudumu kila kukicha. Hapo Makusudio (purpose) ya biashara yana umuhimu gani? Umeshaanza kupata picha sasa?

UNAWEZAJE KUTENGENEZA MAKUSUDIO YA BIASHARA YAKO?

Faida za kugundua makusudio ya biashara yako ni kubwa na zisiyopingika. Lakini Unapataje “Kusudi” la Biashara/Kampuni yako? Tuone hatua zifuatazo za kutengeneza Makusudio ya kuanzisha na kuendesha biashara yako.

Hatua 1: Pitia zile Core Values za biashara yako. Ni mambo yapi ambayo biashara yako inayajali zaidi (mf; Heshima, Uwajibikaji, Kuchapa Kazi, Upendo n.k) Biashara yako inazingatia mambo yepi katika utendaji wake wa kila siku? Tupe majibu katika replies hapo chini.

Hatua 2: Fuatilia kwa ukaribu biashara/kampuni ambazo zinakuvutia na ambazo ungependa kuiga utendaji wake (sio lazima biadhara/kampuni hizo uwe nazo field moja ya kuuza bidhaa au kutoa huduma) Lengo hapa ni kujifunza mambo mengi ya msingi katika utendaji wako wa kila siku.

Hatua 3: Hii ni ngumu kidogo, hebu jiulize, biashara/kampuni yako leo haipo duniani, je, wateja wako watapungukiwa na nini? Wateja wako watakukumbuka kwa lipi? Biashara/Kampuni yako itaacha legacy gani duniani? Ukipata ufumbuzi wa maswali haya utakuwa umefika mbali sana.

Hatua 4: Kama umeshafanya hatua 3 zilizopita basi hapo jua umeshafungua koki, kilichopo mbele ni kazi tu. Hebu jiulize, Biashara/Kampuni inajiwekea malengo gani ndani miaka fulani ijayo? Malengo hayo bila shaka huja kutokana na zile values zako ambazo ulishajiwekea.

Hatua 5: Sasa kusanya hayo malengo utayoyapata katika hatua iliyopita ili kutengeneza dhamira na makusudio ya kampuni/biashara yako. Ukimaliza jiulize tena, “je makusudio haya yataleta mapato?” Hakikisha makusudio unayoweka yanakusaidia kunasa mapato zaidi.

Hatua 6: Zama field sasa. Hakikisha kila mmoja anaelewa makusudio yaliyowekwa kwenye taasisi/kampuni hio mara moja. Ikitokea watu hawajaelewa makusudio hayo waelekezwe mpaka waelewe, ama sivyo badili dhamira na ibadilishwe.

Hata hivyo habari njema ni kwamba, kama unahisi hujaweza kung’amua makusudio (purpose) ya biashara hio unafanya, inawezekana kabisa hujatakari kwa kina na kuyaona. Kiuhalisia hakuna biashara ambayo haina Kusudio, lazima tu kusudio lipo na ndio linafanya biashara iendelee kuwepo.

Na zaidi inawezekana wafanyabiashara/wafanyakazi wenzako tayari wanajua wateja na dunia inataka nini kutoka kwenye taasisi yako. Hivyo mbinu ya kwanza ya kung’amua kitendawili hiki ni kubadili namna ya kuwazs na kuelewa mambo kutoka sub-conscious understanding (nimekosa kiswahili chake).

Mpaka kuwa conscious understanding. Halafu kifuatacho ni kuingiza utamaduni huo moya katika shughuli zako za kila siku katika biashara. Makusudio ni Utamaduni, sio mabadiliko ya fasheni tu. Una lolote la kuchangia na kuongezea kwenye makala yetu ya leo kuhusu Makusudio (purpose) ya biashara yana umuhimu gani? Tafadhali karibu.

Pitia makala hizi hapa ili kupata mfululizo mzuri wa maarifa kutoka kwenye somo ulilolipata leo. Gusa links zifuatazo kisha jifunze zaidi..

  1. FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA
  2. USAFIRISHAJI NA MIUNDOMBINU KATIKA USTAWI WA BIASHARA AFRIKA
  3. FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

UONGOZI vs UTAWALA KATIKA MIRADI/BIASHARA, KIPI KINAFAA ZAIDI?

“Nafikiri Kiongozi mzuri ni yule anayewafanya watu wanaomzunguka kuwa bora zaidi.” Alinukuliwa Dana Brownlee (CEO Professionalism Matters). Vipi kuhusu hali ya kuwa Mtawala, inaathiri vipi biashara? Unadhani kati ya Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi? Fuatilia makala hii mpaka mwisho kufahamu zaidi.

Tunafahamu ilivyo, ukiwa mjasiriamali/mfanyabiashara huna budi kuvaa kofia nyingi, majukumu kila kona. Ukiwa mfanyabiashara jua unawajibika kujenga na kuimarisha masoko yako, kubuni/kusimamia miradi, kutunza hesabu nakadhalika.

Hata hivyo biashara inavyozidi kukua, vitu vya kusimamia pia vinaongezeka, hivyo mfanyabiashara/mjasiriamali makini lazima aanze kufikiria namna ya kuendesha biashara yake kwa urahisi bila kuathiri shughuli za kila siku. Unahitaji msaada kutoka kwa watu wengine. Wakati huu sasa ndipo anahitajika Kiongozi zaidi kuliko Mtawala, hasa katika biashara.

KIONGOZI ANA SIFA ZIPI?

i. ANAFANYA KAZI NA TIMU YAKE: Ukiwa Kiongozi hili ni jukumu muhimu sana. Usiishie tu kutoa amri na maagizo, hapo utakuwa Mtawala, tena asiyefaa. Kiongozi anafanya kazi bega kwa bega na timu yake, kila anapohitajika kuweka mchango wake anafanya hivyo. Katika biashara za kisasa hii ina maana Kusaidia hatua za uzalishaji zizidi kuwa bora, kuboresha maudhui ya mtandaoni ya kampuni, kuhamasisha viwango katika kazi, kuongea na wateja ili kuboresha huduma. Kiongozi anaelewa vyema watu wote anaofanya nao kazi na wateja anaowahudumia, muda wote yupo updated. Njia bora zaidi ya kuwasiliana na kujua tabia na mwenendo wa watendaji katika timu pamoja na mwenendo wa wateja ni kupitia mitandao ya kijamii. Sasa mitandao ina mchango gani, tafadhali pitia makala yako hii IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO.

ii. KIONGOZI BORA NI MNYENYEKEVU: Hakuna mtu anapenda kufanya kazi na mtu mwenye kiburi, majivuno au mjuaji sana. Hata hivyo inafaa sana kwa Kiongozi kutambua pale anapokosea na kujisahihisha mara moja, vile vile Kiongozi huruhusu timu yake kutambua makosa yao na kuwasaidia kutatua changamoto mbalimbali kwa kadiri zinavyotokea. Unyenyekevu (Being Humble) husaidia kuimarisha morali ya ufanyaji kazi katika miradi/biashara kuliko kiburi na majivuno.

 Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

iii. MAWASILIANO WAZI: Katika vitu muhimu vya kufanya katika kufanya biashara/mradi kwa mafanikio ni namna timu inawasiliana kwa uwazi. Kila mtu anayefanya kazi katika timu hujihisi ana umuhimu pale anapokuwa na taarifa kamili kuhusu mambo yote yanayoendelea ndani ya timu yake na pale anapoweza kuwasiliana na yeyote ndani ya timu na kujuzwa mambo kwa uwazi. Unapokuwa na jukumu la kuhudumu ndani ya timu ni muhimu kuwa straight-forward kwa kuwa biashara/kampuni yako ni taswira yako mwenyewe kama Kiongozi. Hivyo, unapokuwa muwazi katika mawasiliano pamoja na kuzingatia maadili ya kiweledi (ethical behaviors) katika utendaji wa shughuli za kila siku, timu nzima unayoiongoza itafuata taswira hio.

iv. KUWA MSIKIVU: Kama Kiongozi ni jukumu lako kusikikiza kwa umakini mara zote mwingine anapozungumza iwe katika timu ama mteja. Usikivu humpa mzungumzaji nafasi ya kusema kile anadhani kinafaa katika kuboresha shughuli za kibiashara/kimradi ambazo ni muhimu sana katika ukuaji wa kampuni/biashara. Usikivu humfanya mzungumzaji kuungana moja kwa moja na wewe kama kiongozi katika kuimarisha mradi/biashara.

Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi?

Usikivu pia huimarisha Mvuto (impression) wako katika macho na akili za watu ulionao katika mazungumzo. Tafiti zinaonyesha mzungumzaji husema kile kilichopo moyoni mwake kuhusu vile anataka kuhudumiwa au kutoa wazo la kuimarisha biashara pale anaposikilizwa kwa umakini.

v. KUWA NA MTAZAMO CHANYA: Katika kufanya shughuli za kila siku za mradi/biashara, changamoto hazikosekani. Iwe ni changamoto ndogo au kubwa, kama Kiongozi jinsi unavyoshughulika na mazingira hasi katika mradi/biashara yako hutafsiri mengi kuhusu maarifa ya kiuongozi uliyonayo. Robert Mann (mwandishi ya kitabu The Measure of a Leader) ananukuliwa “Look at three positive things about a problem before you identify what makes it dissatisfying. The more you look at the positives in a problem, the more positive people react with one another.”

Katika utafiti wake bwana Mann aligundua kuwa baada ya watu kuona mambo mazuri katika mazingira yenye changamoto, hufikiria namna ya kukabiliana na changamoto hio ili kufikia lile jambo lenye faida. Sawa sawa na vile jinsi Kiongozi anavyotaka kuimarisha mbinu za kiutendaji.

vi. FAHAMU BIASHARA/MRADI WAKO: Njia bora ya kufahamu kitu unachokifanya ni kwa kutumia uchambuzi wa SWOT ambao unakusaidia kufahamu Strength (nguvu/faida ya biashara), Weaknesses(Udhaifu wa mradi/biashara), Opportunities (fursa zinazokuja na biashara hio) pamoja na Threats(matishio yanayoikabili biashara). Kwenye kufanya uchambuzi huu zingatia haya;

STRENGTH (Nguvu/Faida ya biashara/mradi wako): Unaweza kuboresha jambo gani zaidi ya washindani wako? Uongeze malighafi/huduma gani ambazo washindani wako bado hawana? Mteja wako anafuraha?

•WEAKNESSES(Madhaifu ya mradi/biashara): Ni malighafi/huduma gani ambazo washindani wako wanazo ila wewe bado huna? Ni kipi unahitaji kuimarisha katika mradi/biashara yako? Una uzoefu wa kutosha kushindana na wafanyabiashara wengine? Unafanyaje baada ya hapo?

OPPORTUNITIES (Fursa): Unaona fursa gani katika mradi/biashara yako? Sheria za nchi, unaweza vipi kuzitumia vizuri katika kuimarisha mradi/biashara yako? Nje ya biashara/mradi wako kuna jambo/trend gani maarufu linaendelea? Unaweza vipi kulitumia jambo hilo kwa faida yako?

Je, kuna matamasha, matukio ya kijamii katika kalenda yako hivi karibuni? Unaweza vipi kuyatumia matukio hayo kwa faida ya biashara/mradi wako?

•THREATS (Matishio yanayoweza kuikumba biashara/mradi wako): Una changamoto za kifedha? Biashara/mradi wako utajiendesha vipi? Je vyanzo vyako vya kifedha ni vya kuaminika na kutegemeka (reliability)? Biashara/mradi wako unaweza kuhimili maendeleo ya kiteknolojia yanayozidi kushika kasi duniani? Kuna mambo gani binafsi yanayoweza kuathiri biashara/mradi wako? Katika timu yako, kuna mtu anapitia wakati mgumu katika kukabiliana na mambo binafsi kama msiba, ugonjwa au harusi?

Hayo ni baadhi ya maswali ambayo unaweza kujiuliza wewe kama kiongozi pamoja na timu yako ili uweze kuifahamu biashara yako na mazingira inayopitia ili kutengeneza njia nzuri zaidi ya kufanikiwa.

MTAWALA ANAATHIRI VIPI BIASHARA/MRADI?

Mazingira ya biashara/mradi ni sehemu inayohitaji mahusiano mazuri zaidi ili kuhakikisha biashara inakuwa na kudumu kwa miaka mingi zaidi. Lakini unapoingiza Utawala unaingiza ile hali ya kuhitaji zaidi na kuweka mbele matakwa binafsi.

•Mtawala anatoa amri na maagizo pasi na kuangalia hali ya utendaji ya timu yake.

•Si mara zote mtawala anakuwa muwazi kwa timu yake. Jambo linalohatarisha utendaji bora wa timu.

•Kiburi na majivuno humfanya kiongozi bora kuwa mtawala dhalimu ambaye hahitajiki katika biashara.

Hizo ni baadhi ya athari za Uongozi na Utawala katika maendeleo ya Biashara/Miradi. Je unadhani kati ya Uongozi vs Utawala katika miradi/biashara, kipi kinafaa zaidi? Makala zifuatazo katika link ni muendelezo mzuri wa somo ulilolipata katika makala hii ya leo. TUJADILI..

  1. FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI
  2. UKWELI KUHUSU PROPAGANDA
  3. KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?
unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako leo?

UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO LEO?

Umeshasikia mara ngapi kampuni inakuwa na vyanzo vingi vya taarifa kuhusu bidhaa/soko/wateja lakini bado haivitumii sawia vyanzo hivyo au haifahamu hata kuwa inavyo vyanzo hivyo? Sasa leo tuangalie unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako leo?

Taarifa ndio kila kitu katika ulimwengu wa leo. Taarifa(Data) zina thamani kubwa ingawa thamani yake hutegemea jinsi unavyozikusanya na kuzichambua. Kama haujafanyika uchambuzi na upembuzi yakinifu, data hukosa maana yake halisi.

Sasa ili uweze kukusanya, kuchambua, kudadavua na kufanya tathmini sahihi hapo ndipo UJASUSI WA KIBIASHARA unapokuja kuhusika. Ujasusi huu unahusika zaidi na data za ndani ya kampuni kuhusu taarifu za wateja, aina za bidhaa/huduma zinazozalishwa, ubora wa bidhaa, huduma kwa wateja, kiwango cha usambazaji, mrejesho kutoka kwa wateja/wabia, Utendaji wa wafanyakazi pamoja na matumizi ya teknolojia.

Kuyafanya yote haya katika kiwango kinachotakiwa na kuleta majibu chanya, Biashara/kampuni haina budi kutengeneza mifumo mizuri ya kukusanya data pamoja na kuwa na wachambuzi (analysts) wazuri wa data hizo. Ndani ya miaka michache iliyopita Ujasusi wa Kibiashara (BI) umebadilika sana na kujumuisha taratibu mbalimbali ili kuhakikisha Utendaji wa Kibiashara Unaimarika.

Taratibu hizo zinajumuisha;

1. DATA MINING (UVUNAJI WA TAARIFA)

Hii ni ile jinsi kampuni hukusanya data kupitia taarifa mbalimbali za wateja wao pale wanapotembelea majukwaa yao, haswa yale ya kimtandao. Taarifa zinazokusanywa hapa ni kama majina na anwani, location, aina ya bidhaa/huduma zinazotumiwa zaidi, tovuti zinazotembelewa zaidi nakadhalika. Makampuni makubwa duniani hutumia sana njia hii kuvuna data za watumiaji wao na kuziuza kwa makampuni mengine kulingana na matakwa ya kibiashara. Kujua zaidi jinsi ya kutumia mitandao ya kijamii katika kukusanya data tafadhali tembelea makala kupitia makala hii IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA.

2. REPORTING

Kiutaratibu kazi ikishafanyika huripotiwa katika mamlaka za juu katika kampuni/biashara ili kutoa maamuzi. Kushirikishana taarifa za uchambuzi katika biashara/kampuni hufanya zoezi la kutoa maamuzi kuwa jepesi na lisilotumia muda mrefu.

3. KULINGANISHA UTENDAJI

Utendaji wa biashara huimarika kirahisi pale kunapokuwa na kumbukumbu katika nyakati tofauti ambazo huonyesha viwango vya utendaji na hivyo kuchochea kufikia malengo ya kampuni kwa wepesi zaidi. Hii ni kama kumbusho kuwa Utendaji unapaswa kuimarika kuliko ulivyokuwa wakati uliopita.

4. UCHAMBUZI WA KITAKWIMU

Data zilizofanyiwa kazi huweza kuwekwa vizuri kupita michoro ya kitakwimu ambayo hutoa picha nzuri kuhusu data zilizokusanywa na hivyo kupatikana maamuzi sahihi kuhusu biashara.

5. UANDAAJI WA DATA

Ujumuishaji wa vyanzo mbalimbali vya taarifu, kutambua vipimo mbalimbali kwa pamoja hufanya zoezi la uchambuzi kuwa rahisi zaidi. Hapa wengine huita ‘Kuunganisha dots’.

UJASUSI UNA FAIDA GANI KWENYE BIASHARA?

Ukusanyaji wa data, uchambuzi, upembuzi mpaka inapofika wakati wa kutoa maamuzi, Ujasusi huleta matokeo chanya pale unapofanyika katika Biashara/Kampuni kwa kuzingatia taratibu zilizoelezwa hapo awali. Hapo ndipo utaelewa unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako (Business Intelligence). Baadhi ya faida zinazoweza kupatikana kutokana na ujasusi huu ni;

i. Kugudua njia za kuongeza faida katika biashara. Likiwa ni lengo kuu la biashara yoyote, kupata faida kunaweza kuongezeka ama kupungua ikiwa utazingatia jinsi Ujasusi wako unavyoufanya katika shughuli za kila siku.

ii. Kuchambua tabia za wateja kuhusu bidhaa/huduma wanazozipenda zaidi na zile wasizozipenda, mtiririko wa manunuzi na mauzo.

iii. Kuwa na uwezo wa kupima, kufuatilia na kutabiri kuhusu mauzo na utendaji imara wa maswala ya kifedha katika biashara/kampuni yako.

iv. Kuimarisha Huduma kwa wateja na utaratibu wa kufikisha bidhaa/huduma kwa wakati.

v. Kutengeneza mipango mizuri ya kifedha, bajeti na makadirio ya kitaalamu zaidi.

vi. Kuwa na uwezo wa kuona fursa katika ushindani mkali wa masoko. Data hukuhakikishia nini cha kufanya ili kupata Soko kubwa katikati ushindani mkali unaoendelea duniani hivi sasa.

UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO (BUSINESS INTELLIGENCE)?

Kampuni na biashara zote hunufaika sana pale zinapotumia ujasusi katika shughuli zao. Lakini kuna vidalili ambavyo ukiviona basi huna budi kuanza kutumia mbinu za kijasusi ili kunusuru biashara/kampuni yako. Wacha tuzione dalili hizo kwa uchache hapa:

i. Kukosekana kwa nidhamu katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji wa kampuni/biashara kama maswala ya fedha, mfumo wa habari na taarifa.

ii. Kampuni/biashara inapokua kwa ghafla kutokana na kupata faida kubwa katika wakati mfupi au kuongezeka kwa uwekezaji. Hapa usipotumia ujasusi vizuri utajikuta unarudi sifuri chap.

iii. Pale unapohitaji kupata taarifa fulani za kiutendaji zilizo sahihi na kwa haraka bila kufanya upembuzi yakinifu au kwa kudhania.

iv. Kuongezeka idadi ya wateja/watumiaji wanaohitaji taarifa/bidhaa/huduma fulani zilizothibitika kiuchambuzi. Hapa ndipo yanapokuja maswala ya ‘zimazoto’ sasa.

Je wajua kuwa bando lako ni Mtaji

unawezaje kutumia Ujasusi katika biashara yako leo?

Unapokumbana na dalili hizi katika utendaji wa biashara/kampuni yako, ni dhahiri huna budi kupitia upya mfumo mzima wa kukusanya taarifa mbalimbali katika biashara yako kama aina ya bidhaa/huduma zinazopendwa/zisizopendwa, bidhaa/huduma kulingana na hali ya hewa, aina ya wateja wako wakubwa, wanapopatikana kwa wingi nakadhalika. Baada ya kufahamu hilo hakikisha unaandika na kuandaa ripoti mara kwa mara kwa kadiri inayowezekana (kwa mwezi, miezi3/6, mwaka). Halafu hakikisha unafanya uchambuzi vizuri kila unapoandaa ripoti yako. Jambo hili litakuongezea uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kila wakati unapohitajika kufanya hivyo. Usiache kutumia ujasusi huu.

BIASHARA ZIPI ZINAWEZA KUTUMIA UJASUSI HUU?

Biashara zote zinao uwezo wa kutumia ujasusi katika shughuli zao za kila siku. Utaratibu huu ni msaada mkubwa kwa biashara za aina zote na viwanda kutoka vidogo mpaka vile vikubwa. Ni mbinu inayotumika dunia nzima.

Katika biashara za rejareja, Wal-Mart kwa mfano, hutumia data nyingi sana katika nyanja mbalimbali ili kuhakikisha wanaendelea kuliteka soko. Harrah’s amebadilisha sana ushindani katika michezo ya televisheni kutoka kujenga makasino makubwa mpaka kutengeneza Aplikesheni za kwenye simu zilizotengenezwa kukidhi haja za wateja na zenye huduma bora zaidi. Amazon na Yahoo sio tu tovuti za e-commerce, zimekithiri uchambuzi wa data na hufuata mbinu ya “test and learn” katika kubadili biashara zao kulingana na soko.

TEKNOLOJIA ZINAZOTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA

Microsoft Power BI: Hii ni software ambayo huzalisha data nyingi sana pamoja na uchambuzi katika namna ambayo ni rahisi kutumia ikijumuisha Dashboard yenye ripoti mbalimbali, uchambuzi na utabiri wa kibiashara. Software hii huwasiliana na MS Office na hivyo kukurahisishia zoezi la kuingiza data ambazo hazijachakatwa kutoka vyanzo mbalimbali. Zingine ni Sisense na Zoho Analytics. Zote hizo zinapatikana mtandaoni kirahisi kwa kufuara utaratibu uliowekwa.

Sasa niwaulize wafanya biashara wa humu ndani. Mnatumiaga taratibu zipi za kijasusi kuhakikisha biashara zenu zinashamiri? Tupe maoni yako tafadhali kisha fuatana na makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata leo. Gusa link kisha makinika.

  1. IFAHAMU TEKNOLOJIA YA QR CODE KATIKA BIASHARA YAKO
  2. BRANDING vs MARKETING. KIPI NI KIPI?
  3. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO?
teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)

Uchumi wa Africa mpaka sasa hukua kwa kutegemea sekta za asili kama kilimoufugaji na biashara. Hata hivyo ujio wa teknolojia ya huduma za kifedha kwa njia ya kielektroniki (Fintech) utasaidia kwa kiasi kikubwa kuendesha uchumi katika kufanikisha maendeleo kiujumla. Sasa tuangalia teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech), zina mchango gani kwako leo?

Uchunguzi umeonyesha kwamba matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu za mkononi yameongezeka sana ndani ya miaka 10 iliyopita ambapo imeonekana eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara ndio limekuwa kinara wa kubuni na kutumia huduma hizi za kifedha kwa kutumia simu za mkononi duniani kwa sasa.

Utafiti uliofanywa na Shirika la Fedha duniani (IMF) umebaini kwamba takriban 10% ya pato la taifa katika miamala ya kifedha hufanyika kwa huduma za kifedha kupitia simu za mkononi. Hii ni matokeo bora zaidi ukilinganisha na 7% ya GDP katoka bara Asia na chini ya 2% ya GDP kutoka sehemu zingine za dunia.

Sasa swali, hii Fintechs ni nini!? Na ina manufaa gani kwa wafanyabiashara walio Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Shirika la EY linaifafanua FinTech kama Shirika/Kampuni inayojumuisha ubunifu katika utendaji wa biashara pamoja na technolojia ya programu za kompyuta katika kubuni, kuwezesha na kusambaza huduma za kifedha. Hizi FinTechs zinaweza kuwekwa kwenye makundi mawili;

i. FinTechs zinatoa huduma za kifedha e.g TALA App.

ii. FinTech zinazowezesha huduma za kifedha Vodacom na MPESA n.k (tutayajadili zaidi kwenye makala zetu zijazo)

Sekta hii ya FinTech katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara (SSA) inajumuisha zaidi ya makampuni 260 ambapo 80% katika hizo ni kampuni za ndani na 20% ni kampuni za kimataifa. Vile vile imeonekana idadi ya makampuni haya mapya imeongezeka katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) cha 24% ndani ya miaka 10 iliyopita.

Hata hivyo ripoti zinaonyesha kwamba Afrika Mashariki itaendelea kuongoza katika ukuaji wa sekta hii kwa 6.3% ya ukuaji wa uchumi mwaka huu 2019. Hii ni kutokana na Ethiopia, Rwanda, Tanzania na Uganda zote zinatarajia kurekodi pato la Taifa la zaidi ya 6% mwaka huu ambayo ni zaidi ya nchi zilizo maeneo mengine ya Africa. Hii ni kutokana na uwekezaji katika miundombinu na utanuzi wa huduma za kifedha na mawasiliano.

Takriban theluthi moja (1/3) ya michango ya harambee zilizofanyika barani Africa mwaka 2017 iliwezeshwa na kampuni za FinTechs. Hii inatiliwa mkazo kwa kuwa 60% ya akaunti za huduma za kifedha kwa njia ya simu duniani zimegundulika kuwepo katika eneo la SSA. Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliofanya na benki ya Ecobank.

Pia imeonekana sekta hii ya FinTechinaendelea kuwa imara katika muda wa miaka 3 kutoka makadirio ya dola za kimarekani 200 milioni mwaka 2018 hadi 3$ bilioni mwaka 2020. Kiasi kikubwa cha uwekezaji katika muda huu kimeonekana kuelekezwa KenyaNigeria na Afrika Kusini. Vile vile inategemewa kwamba kufanikiwa kwa Fintechs katika nchi hizo kutatanua mafanikio katika nchi zingine za Kiafrika.

MAENDELEO: Ujio wa FinTechs umebadili sana jinsi ya kufanya biashara duniani. Kutoka Crowdsourcing ambayo ni njia inayotumika kufanya usaili wa miradi mbalimbali mtandaoni kupitia intaneti na kupokea ruzuku, mpaka njia ya huduma za kifedha kwa njia ya simu. Wafanyabiashara na wajasiriamali hawajawahi kupata njia rahisi zaidi kwenye utandaji wa biashara zao kwenye maswala ya fedha kuliko hii.

Kupitia Fintechs sasa wafanyabiashara wanaweza kusambaza bidhaa/huduma kwa watu mbali mbali na kupata malipo ndani ya muda mfupi zaidi. teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) inazidi kujisombea watumiaji kwa sababu inaonyesha namna inavyoweza kusaidia katika kujikwamua kwenye maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni.

TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH) HAINA MIPAKA:

Kutuma pesa nje ya mipaka ya nchi napo imekuwa rahisi zaidi. Mfumo huu ulioondoa mipaka ya kijiografia kwenye kurusha pesa umepunguza gharama kutoka ilivyokuwa mwanzo kwa njia ya benki ambayo ni ghali mno. Hivyo FinTech imewawezesha wajasiriamali na viwanda vidogo kutuma na kupokea pesa kwa gharama ndogo zaidi.

KUONGEZA THAMANI KATIKA UTOAJI WA HUDUMA ZA KIFEDHA: Eneo hili limetawaliwa na ubunifu ambao unawezesha kuongezeka kwa thamani katika matumizi ya huduma za kifedha. Kwa kuyumia malipo kwa njia ya simu, wateja walioko kusini mwa Jangwa la Sahara wanapata uwezo wa kupata huduma za kibenki kupitia simu za mkononi (mobile banking) pamoja na huduma zingine kama kugungua akaunti, kuchukua mkopo, kupata bima, kupata huduma za mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na masoko ya hisa. Haya yote kupitia FinTech yanawezeshwa kirahisi tuu katika simu yako ya rununu (smartphone) au laptop.

teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech)

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi. Umejifunza nini hapa katika teknolojia ya huduma za fedha kwa njia ya kielektroniki (fintech) leo?

Zaidi unaweza kupitia makala hizi hapa chini ili kupata ufahamu mpana kuhusu biashara za mtandaoni:

  1. MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA
  2. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  3. UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-COMMERCE BUSINESS)?
  4. FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia comments section hapo chini;

FAHAMU KUHUSU MFUMO WA MAWASILIANO YA SIMU (MOBILE ECOSYSTEM) NA FAIDA ZAKE KATIKA BIASHARA

Je Wajua?

Mfumo wa mawasiliano ya simu (mobile ecosystem) huchangia shemu muhimu sana katika uchumi wa nchi zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara? Uchumi wa nchi hizo kwa pamoja umefikia thamani ya dola za kimarekani bilioni 110 ($110 b) ambayo ni sawa na 7.1% ya pato la taifa (GDP) katika mwaka 2017. Hii inajumuisha faida za moja kwa moja za mfumo huo, faida zisizo za moja kwa moja (indirect impact) pamoja na ukuaji wa uzalishaji unaoletwa na matumizi ya huduma za simu na teknolojia.

Tukigusia faida za moja kwa moja za mfumo huu wa mawasiliano ambao unajumuisha makampuni ya simu, watengenezaji wa huduma za miundombinu ya kiteknolojia, wasambazaji wa huduma/ bidhaa za simu, wafanyabiashara wa reja reja, watengenezaji wa simu na vifaa vyake pamoja na watengenezaji wa maudhui/applications/huduma za mtandaoni; mchango wao katika uchumi hukadiriwa kwa kupimwa thamani wanayochangia katika uchumi wa nchi husika ambayo hujumuisha bima ya wafanyakazi, faida ya ziada ya biashara pamoja na kodi.

Mwaka 2017, thamani iliyozalishwa na mfumo huu wa mawasiliano katika ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara ulikuwa dola bilioni 40 ambayo ni sawa na 2.5% ya pato la Taifa (GDP) ambapo makampuni ya simu peke yake yalijumuisha takribani 75% ya mchango huu.

Ukiachana na faida za moja kwa moja, zipo pia faida ambazo si za moja kwa moja (indirect impact) ambapo sekta hii hununua vifaa/huduma mbali mbali kutoka sekta nyingine. Kwa mfano makampuni ya simu hulazimika kununua umeme kutoka sekta ya nishati hali kadhalika wasambazaji na wafanya biashara wa reja reja wa vifaa/huduma za simu huhitaji usafiri kuwafikia wateja wao.

Kwa pamoja uzalishaji huu wa faida isiyo ya moja kwa moja ulitengeneza takribani 60$ mwaka 2017 (ambayo ni takribani 4% ya pato la taifa). Kiujumla ukiongezea na faida za moja kwa moja, sekta hii ya mawasiliano ya simu ilitengeneza 110$ bilioni sawa na 7.1% ya pato la taifa katika ukanda huu.

Hii inaleta picha gani Kibiashara?

Matumizi ya teknolojia ya simu pamoja na maendeleo ya simu za rununu (smartphones) huendesha uchumi kwa kuboresha uzalishaji, kupunguza costs za uendeshaji pamoja na kurahishisha upatikanaji wa huduma/bidhaa za kibinadamu.

Chanzo: Ripoti ya shirika la mawasiliano ya simu duniani la GSMA toleo la mwaka 2019.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”