Tag: biashara huru

FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA

Watu wengi hufikiri kwamba Kuwekeza ni swala la kupata Utajiri ndani ya muda mfupi, Kustaafu mapema au kupata gawio (interest) kubwa kila baada ya muda fulani kwa haraka. Ukweli ni kwamba Kuwekeza sio chanzo cha kukufanya ushinde unakula upepo wa bahari, kutumia pesa hovyo(kula bata) au kusafiri vile unataka. Usikariri maisha, leo makinika mpaka mwisho wa makala hii ili uweze ku fahamu siri ya kufanikiwa katika kuwekeza.

Watu wanafanya kazi sana ili kupata pesa, na kazi zaidi kutunza pesa. Lakini wachache sana ndio hugundua njia bora zaidi ya kutengeneza na kuzungusha pesa katika biashara zao. Leo hii nitakujuza mambo 10 muhimu ya kuzingatia katika UWEKEZAJI (INVESTING) kwa mafanikio ya biashara yako hio hio unayoifanya/unayotaka kuifanya.

Kuwekeza zaidi katika biashara dhumuni lake ni kuhakikisha biashara yako ina uwezo wa kujiendesha yenyewe hata bila ya wewe kuwepo hapo ofisini kila siku. Sasa ili kuweza kufikia lengo hilo inatakiwa ile energy ambayo mjasiriamali anakuwa nayo wakati anaanza uwekezaji wake wa kwanza ndio hio hio anatakiwa kuwa nayo hata pale anapofanikiwa. Kama misuli inayohitaji mazoezi ili iwe mikubwa na yenye nguvu, the same kwenye biashara yako. Biashara inahitaji muendelezo wa uwekezaji ili kuleta matokeo yenye tija. Vitu kama Mtaji, Masoko, rasilimali watu, connection, wafanyakazi n.k, vinahitaji kukua sana. Hii ni muhimu sana katika ku fahamu siri za kufanikiwa katika kuwekeza popote pale duniani.

Sasa kifupi ni kwamba kuna aina nyingi sana za Uwekezaji duniani (Stocks, Bonds, Real Estate, Commodities n.k). Lakini leo tujadili kuhusu Uwekezaji kwenye Biashara Unayoifanya/Unayowaza kuifanya (kuuza viatu, nguo, chakula, furnitures n.k) Hapa nitakuwa nimekupa kitu unachohitaji sana, si ndio?

Kama umeshawahi kujaribu basi utakubaliana namimi kwamba Kutunza Fedha kwenye kibubu, chini ya godoro, benki, mpesa, tigopesa ni ngumu kweli kweli. Halafu kibaya zaidi, pesa sio kiumbe hai, usitegemee ukiichimbia itazaliana.

Hizi hapa ni njia Bora za kuwekeza na kuzungusha pesa yako vizuri ili uweze fahamu siri ya kufanikiwa katika kuwekeza:

1. FIKIRIA MBALI:

Unapotaka kuwekeza kwenye biashara yako, waza hivi; mwaka 2030 au 2040 nitakuwa katika hatua gani kibiashara? nataka niwafikie watu/wateja/maeneo mangapi mpaka mwaka 2030/2040? Ukiwa na mipango ya mbali katika biashara yako unapata energy ya kusimamia vizuri na kufanikiwa. Kila mafanikio huanzia kwenye fikra na mipango thabiti.

2. ANZA KUWEKEZA KILE ULICHONACHO:

Watu wengi hasa vijana wanapenda kufanya biashara lakini wanalalamika changamoto ni Mtaji. Fahamu, biashara ni kama ile siku mpenzi wako anapokupa taarifa za mimba. Niambie hapa kama ulianza kulea mimba kwa milioni 1 kwa mwezi ule wa kwanza. Utagundua ni ngumu. Hali kadhalika biashara yako inahitaji kulishwa kidogo kidogo kwanzia ingali ndogo.

Unailisha biashara kwa vitu kama Maarifa, aina bora za bidhaa/huduma zinazotakiwa, wapi pa kuzipata, aina za wateja, taarifa sahihi nk. Pesa ni kitendea kazi muhimu lakini tambua pesa ni sehemu ya mtaji tu.

3. WEKEZA PALE UNAPOPAWEZA

“Baba yako hawezi kukufanya uwe tajiri, wala mama yako, wala rafiki yako, wala mwalimu, wala serikali, badala yake ni wewe mwenyewe wa kubadili maisha yako ukianza na namna unavyofikiria (mindset)” Maneno sumu ya jamaa yangu SirJeff Dennis. Hapa nataka kuongelea Uwezo wako specifically. Wewe unaweza kufanya nini katika kiwango kikubwa? Na unaweza vipi kutumia huo uwezo kwa manufaa? Jitambue wewe kwanza.

4. JIFUNZE NA FANYA UCHUNGUZI

Hili swala sio la kufanya mwanzoni wakati unaanza biashara halafu unakuja kuacha mbeleni, Hapana. Kama ilivyo kuwekeza hakuna mwisho kwenye biashara yako, hakikisha pia Unaendelea kujifunza mbinu mpya na kufanya Uchunguzi kuhusu biashara mbalimbali mara zote kabla hujawekeza. Ishi nayo hii kwa sababu Elimu haina mwisho.

5. TENGENEZA NA FANYA KAZI KWENYE TIMU

Kuna mtu mmoja aliwahi kusema “Kama huwezi kutengeneza pesa ukiwa umelala, huwezi kuwa tajiri”, Ni kweli kabisa. Mimi nakuongezea, kama kwenye Uwekezaji wako, wewe ndo kila kitu, hio biashara haiwezi/ni ngumu sana kukua. Gawa majukumu, sio kila kitu unataka kufanya wewe, uzalishaji wewe, marketing wewe, customer care wewe, presentations wewe. Utafeli, hakikisha mfumo wa biashara yako unaweza jiendesha wenyewe hata usipokuwepo.

 fahamu siri za kufanikiwa katika kuwekeza.

fanya kazi kwenye timu

6. KUWA NA MSIMAMO (CONSISTENCE AND RESSILIENCE)

Biashara yako ili iweze kukua na kufanikiwa dhidi ya ushindani wa masoko, dhoruba za kiuchumi, teknolojia nk, Unapaswa kuwa na msimamo/consistency. Wazungu wanasema “Practice makes perfect”. Hutakiwi kukata tamaa, licha ya changamoto ambazo unaweza kukutana nazo kila siku, hakikisha unaendelea kuzalisha/kuhudumu, tafuta wateja wengi zaidi, jisahihishe, jitangaze, pambana. Uwekezaji unakuhitaji uwe na ngozi ngumu kwelikweli kwa sababu katika kuwekeza kuna nyakati za kuanguka na kukata tamaa, sasa hakikisha unao uweza wa kusimama na kuendelea kupambana.

7. KUWA MWOGA PALE WENGI WANAPOKUWA WALAFI

Ulimwengo wa Uwekezaji katika biashara unaendeshwa kiakili na kijasusi sana. Usiwe bendera kufuata upepo, Usiwe mtu wa kufuata mkumbo. Ni afadhali kuwa mwoga na kuishi miaka mingi, kuliko kuingia vitani bila maandalizi, hutachukua raundi. Tulia, changa karata zako vizuri na kwa mipango sahihi.

8. KUWA AGGRESSIVE PALE WENGI WANAPOKUWA WAOGA

Sehemu pazuri zaidi kuwekeza ni pale mahali kuna changamoto nyingi. Uwekezaji wako unapotatua changamoto hapo ndo pakutoboa kabisa. Kuna mahali hamna maji wapelekee hapo, hamna chakula, fungua mgahawa. Pambana na changamoto za wateja wako. Wasikilize wateja wako wanahitaji nini kila wakati kwa sababu kwenye maumivu ya wateja wako ndipo mafanikio ya uwekezaji wako yalipo. Shikilia hapo.

9. PUNGUZA MATUMIZI YASIYO NA ULAZIMA

Fahamu kuwa katika biashara yako kila shilingi ina mchango muhimu katika Uwekezaji endelevu. So hakikisha unazingatia matumizi yale muhimu zaidi katika uwekezaji. Hili zoezi ni gumu lakini linawezekana ukiweka Nia ya Kukuza Biashara yako.

10. TAWANYA UWEKEZAJI/DIVERSIFY

Ili kuhakikisha biashara yako inakuwa na misuli ya kiushindani, lazima Utawanye uwekezaji wako. Unauza nguo kwa sasa, ongeza na viatu, soksi, vipodozi na jitahidi ufungue matawi mikoani. Kama unauza mbao, ongeza karakana za fenicha maeneo mbalimbali, TANUKA.

fahamu siri za kufanikiwa katika kuwekeza.

11. TUMIA VIZURI TEKNOLOJIA

Katika eneo muhimu la kuzingatia katika kufanya uwekezaji wa kibiashara, basi hakikisha unatumia vyema teknolojia katika maana ya kutumia kwa usahihi Mitandao ya kijamii, tovuti bora ya biashara yako, software za kutunza hesabu nakadhalika. Eneo la teknolojia ni pana, hivyo nimekuwekea mambo muhimu ya kuzingatia katika makala hizi hapa chini:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO?
  3. IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA YAKO
  4. MAGEUZI YA INTANETI (IoT) KATIKA BIASHARA NA MAISHA
  5. MBINU ZA KUWEZA KULIFIKIA SOKO LA MTANDAONI

NOTE: Uwekezaji katika biashara ni jambo endelevu, kama mtoto mdogo, “kadiri ya umleavyo ndivyo akuavyo.” wamesema wahenga. Ukizingatia mambo haya bila shaka bishara yako itakuwa na afya tele. Tafadhali sambaza makala haya kwa yeyote aliye karibu yako na usisite kucoment hapa chini.

Je umeweza fahamu siri ya kufanikiwa katika kuwekeza katika biashara yako kupitia makala hii ya leo? Niambie katika comments hapo chini.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

siri ya kufanikiwa katika kuwekeza.
yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

YAFAHAMU MASHAMBULIZI YA KIMTANDAO NA ATHARI ZAKE

Yaani ni 8% tu ya makampuni ndio wana uwezo wa kugundua wizi wa taarifa zao ndani ya dakika chache. 62% wanaweza kugundua wizi ndani ya siku kadhaa. Wewe unatumia muda gani kugundua upotevu/wizi wa data katika kampuni yako? Makala hii tutaangazia mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) kiundani. Leo, yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake. Makinika mpaka mwisho.

Kama Unavyoona biashara zinavyozidi kushamiri kiteknolojia ndivyo wadukuzi nao wanazidi kutafuta mbinu za kufanya mashambilizi zaidi. Mwaka 2019 peke yake, zaidi ya 2$ billion zilipotelea mikononi mwa wadukuzi duniani. Utafiti wa Juniper unaonesha namba hio inaongezeka kila mwaka.

Unalikumbuka shambulizi lilioitwa NotPetya? Basi jarida la WIRED linalitaja shambulizi hilo kama “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA”. Ndani ya masaa machache tu virusi vya shambulio hilo (malwares) viliathiri kutoka biashara ndogo za Software nchini Ukraine mpaka kusambaa katika vifaa vya kielektroniki dunia nzima. Shambulizi lilidhoofisha mashirika makubwa duniani kama FedEx, TNT, Express na Maersk kwa wiki kadhaa na kusababisha hasara ya zaidi ya $10 bilioni kwa ujumla. Upotevu wa data kwa kiwango hiki unaonyesha namna katili ya dunia tuishiyo ambapo inaonekana hakuna mwenye kinga madhubuti mtandaoni. Kutoka Mashirika makubwa, serikali, mitandao ya kijamii, mifumo ya migahawa na sehemu yoyote unayojua inatumia teknolojia ya IT, Kila mmoja yupo hatarini.

TUMEFIKAJE HAPA?

Ripoti ya mwaka 2019 ya shirika la Accenture Security kuhusu Matishio ya kimtandao (Cyber Threatscape), imeonyesha sababu za wadukuzi kuendelea kuwa tishio dhidi ya taarifa binafsi/za mashirika kwa manufaa yao. Hizi ni baadhi sababu hizo:

1. Wadukuzi wa kimtandao hufaidika zaidi na teknolojia mpya na kukosekana mawasiliano madhubuti katika sheria na tawala za maeneo/nchi mbalimbali duniani.

2. Mitandao ya kihalifu muda wote inakwenda ikibadilika, hasa kuelekea katika makundi ya kihalifu ya siri (syndicates) pasi na kujulikana chanzo chake kwa kutumia nyaraka halali kwa nia halifu.

3. Malengo mseto katika kuimarisha tabia za virusi (kama kujiendesha vyenyewe: self replication)

4. Kuimarika kwa mifumo ya Ulinzi wa Kimtandao (cybersecurity hygiene) inapelekea wadukuzi nao wazidi kujiimarisha kimbinu na maarifa katika uwanda wa kiteknolojia na matumizi ya internet.

Baada ya kujua sababu zinazowasukuma Wadukuzi na wahalifu wa Kimtadao kuendelea kufanya mashambulizi, Leo, uta yafahamu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako, Fuatana nami..

Duniani kunazo aina nyingi za mashambulizi ya kimtandao kulingana na sababu nilizozieleza hapo juu kama ifuatavyo:

1. RANSOMWARE ATTACK: Katika shambulio hili, virusi maalum (specific malware) ambavyo hukusanya na kufunga taarifa/kifaa katika mtandao ili kumnyima mtumiaji haki na uwezo wa kufanyia kazi taarifa zake kama kawaida. Haki na uwezo (access) huo humrudia mtumiaji pale tu matakwa ya mdukuzi yatakapotimizwa ambayo mara nyingi huwa ni pesa au rushwa kwa mapana yake.

Saa ingine wadukuzi wanaweza kugoma kurudisha haki za matumizi kwa mhusika hata wanapotimiziwa matakwa yao, hivyo kuongezea hasara kwa kampuni/biashara. Mbaya zaidi, ripoti ya mwaka 2019 ya Uhalifu wa kimtandao inaonyesha kutokea kwa shambulizi hili kila sekunde11 ya mwaka 2021.

2. ADVANCED PERSISTENT THREATS (APT): Shambulizi hili sio la mojakwamoja (passive attack) ambapo mdukuzi anapata access ya computer/mtandao fulani kwa muda mrefu pasi na kujulikana, hivyo kujichotea taarifa na kuzitumia kwa manufaa yake. Aina hii pia huitwa Trojan Horse attack.

3. PHISHING: Je wajua? Mpaka 32% ya wizi wa data husababishwa na shambulizi hili. Hii ni aina ya shambulizi maarufu sana la kijamii (social engineering) ambapo mdukuzi humtegea mtu adownload file lililo na virusi kupitia SMS, email au link na kuingiza virusi katika kifaa chake.

unawezaje kujilinda dhidi ya shambulizi la kimtandao la phishing katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

4. SQL INJECTION: Umeshawahi kuona ile unaingia kwenye website ukakuta haipo ghafla tu, au kwenye system flani unanashangaa kuna mafiles huyaoni bila sababu ya msingi. Sasa kwa kutumia virusi halifu (malicious codes) shambulizi hufanyika katika servers zinazohifadhi taarifa muhimu za watumiaji na kuzifuta, kuziiba au kuzibadili ili kutimiza azma fulani ya wadukuzi na/au genge lao. Mara nyingi shambulio hili hufanyika kwenye servers zinazohifadhi taarifa ghafi za watu au vitu (personal identifiable information: PII) kama namba ya kadi, username and passwords.

5. DDOS ATTACK: Kirefu huitwa Distributed Denial of Services attack ambapo hutokea pale wadukuzi wanapofurika tovuti au kifaa chako kwa either kupunguza au kondoa kabisa utendaji wa kawaida na hivyo kuiacha kampuni/biashara kuhangaika kurejesha performance ya mifumo yake wakati wao (wadukuzi na virusi vyao) wakitumia mwanya huo kuiba na kufanya uhalifu katika mifumo hio iliyoathirika.

6. MAN IN THE MIDDLE (MITM): Hii hutokea pale mdukuzi anapoingilia mawasiliano halali ya kampuni bila ya wao kujua. Pia shambulio hili hufahamika kama eavesdropping pale linapofanyika baina ya mawasiliano binafsi ya simu kati ya mtu na mtu.

Mawasiliano katika MITM hiungiliwa pia kupitia APN za Wi-Fi za uongo (deceptive wifi). Zaidi ya kuingilia mawasiliano, hapa mdukuzi anaweza pia kuwasiliana akitumia utambulisho (ID) ya wahusika pasi na kufahamika mara moja.

7. PASSWORD ATTACK: Licha ya kuwa shambulizi maarufu zaidi duniani, bado kuna watu huangukia mtego wa kuibiwa nywila zao. Kwa urahisi wake, wadukuzi hutumia mbinu zenye viwango na ujanja kupata nywila dhaifu na kufungua accounts za watumiaji kirahisi. Hapa tunaangukia kwenye usalama wa vifaa vyetu vya mtandaoni. Je viko salama kiasi gani? Fuatana na makala hii hapa kufahamu zaidi..

UNAWEZAJE KUZUIA MASHAMBULIZI HAYO?

Katika yetu iliyopita tumeeleza kwa kirefu kuhusu namna ya kujiepusha na mashambulizi ya kimtandao (Cyber attacks), pitia hapa KWANINI USALAMA WA KIMTANDAO (CYBER SECURITY) NI MUHIMU KWAKO?“. Leo pia, tutaona njia zingine za kuendelea kujiimarisha na kuzuia mashambulizi hayo yasiathiri Biashara/Kampuni yako. Mashambulizi mengi niliyoyaelezea leo yanazuilika kwa njia ambazo tayari tulishaziona katka makala zilizopita isipokuwa:

MITM Attack: •Tumia SSL Certificates za (https) katika website yako. Hii ni boresho la http SSL certificate ambayo ni ya zamani na usalama wake mi mdogo.

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

•Tengeneza VPN yako kama ngao ya ziada dhidi ya wi-fi halifu (deceptive wi-fi). Mashambulizi haya katika biashara yako yana madhara makubwa ikiwemo Kupotea kwa Fedha, faida ya biashara, mauzo, matengenezo, Hadhi ya biashara kushuka au kupotea kabisa na madhara ya kisheria.

Hivyo unapaswa kuwa makini na kufuata ushauri wa kitaalamu kuhusu maboresho ya kimtandao (updates & maintenance) ili kuhakikisha unatumia teknolojia ya kisasa zaidi ambayo ni salama huku ikiwa imeambatana na Passwords zako zilizo bora. Utajuaje kama simu/computer yako ikiwa imedukuliwa? Majibu tayari yanapatikana kwenye makala iliyo hapa UTAJUAJE KAMA KIFAA CHAKO (SIMU/COMPUTER) KIMEDUKULIWA?.

Usalama wa Kimtandao ni jukumu langu. Ni jukumu lako. Ni jukumu letu sote. Tuchukue tahadhari muda wote tuwapo mtandaoni. Basi ni matumaini yangu leo mengi umeyafahamu kuhusu mashambulizi ya kimtandao (cyber attacks) na athari zake katika biashara/kampuni yako. Ukiwa na swali au nyongeza tafadhali tuandikie katika comments hapo chini..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo? Umejifunza nini katika ku yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake katika biashara/kampuni yako.

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

Unawezaje kujikinga dhidi ya mashambulizi ya kimtandao katika biashara yako?

yafahamu mashambulizi ya kimtandao na athari zake

THIS IS THE ONLINE BUSINESS MONITORY SYSTEM (BIMOS)

Je, Ungependa kuwa na uwezo wa kuhifadhi na kufuatilia rekodi za biashara yako ukiwa popote duniani? Kwa kutumia Online Business Monitory System (BIMOS) unaweza kuweka rekodi mbalimbali kuhusu biashara yako kama mapato, matumizi, orodha ya wateja, suppliers, nyaraka za kiashara (documents) kama PO’s, orodha mbalimbali na wafanyakazi (cashiers) wako kirahisi sana.

Vilevile mfumo huu wa BIMOS unakuwezesha kupata ripoti sahihi kuhusu mwenendo wa Biashara yako, hivyo kukuwezesha katika kuimarisha biashara yako zaidi na zaidi.

Ungependa kutumia mfumo huu? fungua link ifuatayo kisha weka credentials as;

Username: admin

Passwords: admin123

www.bimos.sil.co.tz

Wasiliana nasi muda huu ili kuimarisha Biashara yako leo:

0765834754 / 0713497275

http://www.rednet.co.tz