Tag: aina za uwekezaji

10 ZA JE WAJUA?

Kama unajua ni kheri, sasa unapata nafasi ya kujua zaidi. Na kama ulikuwa hufahamu basi leo unapata nafasi ya kujua mambo mapya zaidi. Katika jukwaa letu la @ElimikaWikiendi . Sasa leo tuzione zile 10 za je wajua katika Teknolojia na Biashara.

1. Je, wajua kuwa tovuti ya kwanza kabisa kuundwa duniani bado ipo hewani? Hii hapa kwenye link http://info.cern.ch Tovuti hio imetengenezwa kwa kutumia lugha ya HTML na inaonyesha mistari michache tu.

chanzo: https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-teknolojia-ya-intaneti-na-kompyuta-katika-biashara-yako/

2. Ile Teknolojia ya kuongeza uwezekano wa Taarifa kupatikana kwa urahisi na kiwango cha juu katika injini za mitafuto za mtandaoni (Search Engine Optimization, SEO) ilianzishwa mwaka 1991. Teknolojia hii ina umri mkubwa kuliko GOOGLE ilioanzishwa mwaka 1998.

3. Mtandao maarufu wa kutizama mubashara filamu na tamthilia wa NETFLIX ulianzishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1997 huko Carlifonia nchini Marekani. Mtandao huo una umri mkubwa kuliko YouTube ambayo ilianzishwa mwaka 2005. Tuambie, Netflix umeijua lini wewe?

4. Takriban 10% ya pato la Taifa kwa nchi za Kusini mwa Afrika huchangiwa kupitia huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi. Hii ni zaidi ya 7% ya GDP kutoka Asia na chini ya 2% ya GDP kutoka sehemu zingine dubiani.

chanzo: https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/

5. Kusafirisha gari kutoka Japan mpaka Abidjan nchini Ivory Coast (km 14,075) hugharimu $1500. Lakini kusafirisha gari hilihilo kutoka Abidjan hadi Addis Ababa(km 6626) inagharimu takriban $5000. Gharama hii ni ghali mara 3 zaidi ya ile ya kutoka Japan.

Pia kusafirisha gari ndogo kutoka Japan mpaka Dar es salaam (km 11,256) inagharimu $900 bila makato na kodi. Hata hivyo, kusafirisha gari hilo hilo kutoka bandari ya Dar es salaam mpaka jijini Lusaka (km 1937.3), Zambia inafikia $650 bila makato na kodi.

Kutokana na hali duni ya miundombinu, gharama za usafirishaji barani Afrika ni kati ya zile ghali zaidi duniani. Hii pia huletwa na viwango vikubwa vya forodha, tozo za ucheleweshaji, ajali pamoja na ukosekanaji wa fursa zingine.

chanzo: https://rednet.co.tz/usafirishaji-na-miundombinu-katika-ustawi-wa-biashara-afrika/

6. Kufikia Octoba 2018, duniani tovuti bilioni 1.9 zilikuwa zipo hewani (online). Pia kuliripotiwa kuwapo na machapisho mapya (posts) zaidi ya milioni 5 kila siku kutoka kwenye tovuti na blogu mbalimbali duniani. Fikiria leo hali iko vipi..

chanzo: https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-teknolojia-ya-intaneti-na-kompyuta-katika-biashara-yako/

7. Kila siku kunaongezeka watumiaji wapya wa huduma za Intaneti takriban milioni moja duniani kote. Kwa wastani mtumiaji wa kawaida hutumia masaa 6:42 akiwa mtandaoni kwa siku. Kama wewe ni mjasiriamali bila shaka umeshaona fursa hapa.

8. Unalikumbuka shambulizi lililoitwa NOTPETYA? June 27, 2017 malwares hizo ziliathiri kutoka biashara ndogo za software nchini Ukraine mpaka kusambaa duniani kote. Hilo liliitwa “SHAMBULIZI LA KIMTANDAO HARIBIFU ZAIDI KUWAHI KUTOKEA DUNIANI”

chanzo: https://rednet.co.tz/yafahamu-mashbulizi-ya-kimtandao-cyber-attacks-na-athari-zake-katika-biashara-kampuni-yako/

9. June 23, 2020 Jumuiya ya SADC ilipitisha muongozo wa kurasinisha(to harmonize) shughuli za kibiashara baina ya nchi wanachama. Sasa mtu akisema watu waende Burundi kutafuta unafuu wa maisha, watu watatumia fursa hio wakaenda Zambia na kwinginepo ndani ya nchi wanachama wa SADC kufanya biashara na maisha yataendelea kama kawaida.

chanzo: https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-urasinishaji-harmonization-katika-biashara/

10. Kufikia mwaka 2022, mwakani tu hapo, 10% ya watu duniani watakuwa wakivaa nguo zilizounganishwa na Intaneti. Imagine nguo yako ina lebo ambayo inaweza kutumika kama tiketi ya kuingia kweny muvi, mpirani au club. Baunsa anascan nguo tu mzigo unajipa.

BONUS: Serikali za duniani zitaanza kutoza kodi katika jukwaa la Blockchain kwa mara ya kwanza mwaka 2023. Sasa wale Traders na Investors wa Bitcoins na Cryptos kupitia Blockchain mjiandae kisaikolojia mkimalizia Tax-holiday yenu huko kwenye Blockchain.

Hayo ndio tuliyotaka kukujuza leo katika 10 za je wajua. Jambo lipi limekushangaza zaidi? Tujuze katika comments hapo chini kisha share makala hii kwa ndugu, rafiki na jamaa zako ili nao wapate kufahamu haya tulokujuza leo.

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) – 5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

mpesa lipa namba ya Rednet Technologies.

LIPA KODI KWA FAIDA YA BIASHARA YAKO

Wamiliki wengi wa biashara huanza katika Biashara binafsi (machinga/sole proprietor). Baadae hukua kufikia partnerships, wabia wa kampuni mpaka mashirika. Kadiri unavyotengeneza mifumo ya biashara yako ndivyo inakuwa rahisi kulipa kodi.

Kodi huja katika namna nyingi, unapofanya kazi, unalipwa ujira/mshahara, hapo utalipa “Income Tax”. Kutegemea na kiasi cha pesa unacholipwa, asilimia fulani hukatwa na muajiri wako na kulipwa kwenye Mamlaka za Kodi, % hio huitwa “Withholding Tax”, hii hutaiona kwenye paycheck yako kwani hulipwa na mwajiri moja kwa moja kwenda kwa Mamlaka za kodi.

Ukinunua bidhaa, fahamu kuna kodi pale unalipa ambayo inajumuishwa katika bei ya bidhaa hio. Kodi hio huitwa “VAT” ambayo ni kodi maarufu na yenye kuingiza mapato makubwa sana katika mamlaka za Kodi. Kama unamiliki mali/ardhi unalipa Kodi iitwayo “Property Tax” kulingana na thamani ya mali/ardhi yako hio.

Kulipa kodi ni wajibu wa kizalendo, lakini zaidi ni matakwa ya kisheria. Usipolipa kodi unajiweka kwenye mazingira ya kulipishwa faini au adhabu kwa mujibu wa sheria. Kodi unayolipa inakwenda sehemu mbalimbali za kiserikali kama mishahara ya watumishi wa serikali, polisi, jeshi la zimamoto na uokoaji, kuimarisha miundombinu, sekta ys afya n.k.

UNAEPUKA VIPI RUNDO LA KODI KWA MANUFAA?

Kuendesha biashara kunajumuisha gharama nyingi sana. Na katika kila gharama kuna kiasi cha kodi unatozwa. Fahamu, Ukinunua unalipa kodi, Ukiuza unamlipisha mtu kodi. Jambo hili linafanyika ukiwa unajua na hata bila ya wewe kujua.

1. MANUNUZI

Kodi ya VAT (Value of Added Tax/Kodi ya Ongezeko la Thamani) ambapo unaponunua bidhaa/huduma yoyote unakuwa unanunua kitu chako pamoja na kukilipia kodi yake ya VAT hapo hapo. Kodi hiyo huwa ni 18% ya thamani kamili ya bidhaa/huduma inayouzwa. Mfano unaponunua umeme wa 2,000/-, hapo unakuwa umelipia na kodi yake ambayo imejumlishiwa kwenye hio 2,000/- (indirect tax). Hali kadhalika katika bidhaa/huduma zingine kama mafuta, vocha, computer, chakula, gesi n.k. Kila unachonunua kina kodi yake, Hivyo kama mfanyabiashara hakikisha manunuzi yako yote yahusuyo gharama za uendeshaji (umeme, maji, chakula, mafuta, maintenance, usafi) yanakuwa na risiti zake halali. Risiti zako hueleza kodi zile ulizokatwa “withheld” katika manunuzi/matumizi ya biashara yako. Hivyo jambo hili litakupa unafuu katika kulipa kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).

2. MAUZO

Wafanyabiashara huwalipisha wateja wao VAT lakini wengi hawapendi kulipa kiasi hiko cha kodi katika Mamlaka ya Kodi. Jambo hili ni kinyume na sheria na linaweza kukuweka kwenye mikono ya kisheria yanayoweza kukufilisi mali, kukupeleka gerezani au vyote vikakupata.

Hivyo unapofanya mauzo katika biashara yako hakikisha unatoa risiti halali ili bidhaa unazouza ziwe kwenye uwiano mzuri wa thamani na Mamlaka za kodi

CHANGAMOTO:

i. Tafiti zinaonyesha kuwa zaidi ya 70% biashara hazilipi kodi. Hii inachochewa na upungufu wa elimu ya kodi pamoja na morali ya wananchi katika kulipa kodi.

ii. Pia kumekuwepo na sekta ambazo hazilipi kodi ipasavyo, mfano sekta ya madini, uvuvi, misitu na utalii. Hii imetokana na kutokuwepo na njia bora za ukusanyaji wa kodi katika maeneo hayo, hivyo kudidimisha mapato yao katika kodi.

iii. Kuwepo kwa misamaha mikubwa ya kodi (tax exemptions) kwa wawekezaji wa ndani na wale wa nje. Mbinu hii iliwekwa ili kuwavutia wawekezaji wazidi kumininika lakini matokeo yake yamekuja kudhoofisha sekta zingine za biashara kutokana na kutokuwepo kwa usawa katika makusanyo.

iv. UFISADI: Inarudisha maendeleo nyuma sana hali ya kutokuwepo kwa makusanyo ya kodi. Hali hii kwa kiasi kikubwa huchochewa na kukithiri kwa vitendo vya Ufisadi katika Mashirika ya Umma pamoja na Mamlaka za Kodi. Watu huishiwa morari ya kulipa kodi pale wakiona kodi zao zinaishia mifukoni mwa watu wachache tena kwa manufaa binafsi. Jambo hili ni baya sana katika maendeleo ya biashara. Likemewe kwa nguvu zote.

MATUMIZI YA ICT KATIKA MFUMO WA KODI:

Teknolojia ya ICT imekuja kuwa mkombozi katika mifumo ya mapato na kodi katika biashara na Mamlaka za Kodi katika kutunza kumbukumbu za walipa kodi. Teknolojia imeleta afadhali katika kukusanya kodi kupitia matumizi ya mashine za EFD ambayo hutumika kukusanya taarifa za kodi, mauzo na manunuzi katika biashara.

Mashine hizi za EFD zilianza rasmi kutumika mwaka 2013 zikiwa na lengo la kusajili wafanyabiashara wote pamoja na miamala yote ya mauzo na manunuzi nchini Tanzania. Mwaka 2014/15 Halmashauri ya manispaa ya jiji la Arusha ilianza kutumia mfumo wa LGRCIS (Local Government Revenue Collection Information System). Zaidi kuhusu mfumo wa mapato ya serikali za mitaa unaweza kupata kupitia makala kwenye link hii https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-na-mapato-ya-serikali-za-mitaa/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NA MAPATO YA SERIKALI ZA MITAA”

Kuanzia hapo Halmashauri 8 nchini Tanzania zilianza kutumia mfumo huo wa LGRCIS kama mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi katika Halmashauri zao. Hata hivyo mwaka 2016 mifumo yote ya makusanyo iliunganishwa katika mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi wa TRA.

Lakini bado mpaka sasa mfumo wa LGRCIS unaendelea kutumika ktika kukusanya mapato ya halmashauri ikijumuisha Ushuru, Tozo na kodi za leseni za biashara. Mfumo huo umerahisisha malipo ya kodi kupitia njia za malipo ya kielektroniki kama MPESA, Bank transfer, Tigopesa n.k.

Hivyo, katika mifumo ya kodi kupitia makala haya ni matumaini yangu umejifunza kitu muhimu katika namna unavyoendesha biashara yako kwa faida bila kukwaruzana na Mamlaka za Kodi. Una maoni yoyote? Tafadhali weka comment yako hapa chini. Pia unaweza kushare link ya makala hii ili kuhakikisha inawafikia watu wengi zaidi kwa faida ya biashara zetu.

Sasa tumekuandalia makala hizi hapa chini zenye lengo la kukuimarisha katika namna ya kulipa kodi na kuifahamu mifumo yake zaidi. Zitakusaidia sana ukizisoma zote. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-nchini-tanzania/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NCHINI TANZANIA”
  2. https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-urasinishaji-harmonization-katika-biashara/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA”
  3. https://rednet.co.tz/ukiritimba-katika-biashara-ni-asali-au-shubiri/ yenye kichwa “UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI”

UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-commerce BUSINESSES)?

Japokuwa imechelewa, lakini kwa sasa Africa ndio inaongoza mbio katika kufanya mapinduzi ya kidijitali kuliko sehemu yoyote duniani. Namna ya kufanya biashara inazidi kubadilika ikionyesha nia ya dhati kufanya maendeleo ya kiuchumi, miundombinu na maswala ya kijamii. Mwaka 2018 nchi wanachama wa Umoja wa Africa walipiga hatua kubwa katika mfumo wa kufanya biashara na muingiliano wa kiuchumi baada ya kuanzisha Eneo Huru la Kufanyia Biashara barani (Continental Free Trade Area AfCFTA). Eneo hili lililoanzishwa linashirikisha nchi 22 zilizoweka sahihi tayari na utekelezwaji wake ulipangwa kuanza mwaka 2019 (tayari umeshaanza).

Hata hivyo mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuzishirikisha nchi ambazo bado si wanachama wa eneo hili jipya, inatarajiwa eneo hili kufikia soko la watu takribani bilioni 1.2 barani wakiwa na jumla ya pato la ndani la taifa (GDP) la dola za kimarekani trilioni 2.5 kwa pamoja, kwa mwaka. Hii inatarajiwa kuwa ni mapinduzi makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nyanja ya uchumi wa Afrika.

Sasa, swali linakuja; Afrika(wafanyabiashara, makampuni/mashirika na Serikali) imejiandaa vipi na mapinduzi haya ya uchumi wa kidijitali? Na zaidi, watunga sera/sheria wataangalia vipi biashara za kielektroniki (e-commerce) kama mada muhimu katika eneo hilo jipya la kufanya biashara huru barani?

Tume ya kudhibiti uchumi wa Africa ya Umoja wa Mataifa (ECA) ikishirikiana na Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) pamoja na Baraza la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo ya kibiashara (UNCTAD) mwaka huu 2019 imechapisha ripoti yake ikiangazia maendeleo ya Afrika kiujumla katika nyanja za kiuchumi, siasa na kijamii.

URAHISI: Imeonekana kwamba e-commerce inaweza kufanya biashara ya bidhaa na huduma kwa urahisi zaidi ambapo itarahisisha mwenendo mzuri wa biashara kati ya wazalishaji, wafanyabiashra na walaji pamoja na kumbukumbu zao na miamala ya kifedha.

MITANDAO YA KIJAMII: Pia imeonekana kwamba e-commerce inapatikana na kufanyika kirahisi katika mitandao ya kijamii kama facebook na Instagram ambapo ndipo mahali kuna watumiaji wengi zaidi wa Intaneti duniani (zaidi ya watu bilioni 2 kati ya watumiaji bilioni 4 wa intaneti).

KUTOKUWA NA MIPAKA: Mfumo wa uchumi wa Kidijitali kiasili umetengenezwa kuepuka mipaka ya kijiografia katika kufanya biashara na kubadilishana fedha ambapo mabadiliko haya ya kiteknolojia yataongeza umakini zaidi katika mwenendo wa masoko na gharama. Lakini bado wimbi kubwa la watu watakaoshiriki kwenye soko barani wanaonekana wataachwa nyuma kutokana na kutokuingiliana kwa lugha na vita/ghasia za mara kwa mara katika baadhi ya jamii/nchi.

BIASHARA: Kwa mujibu wa UNCTAD mwaka 2016 kwa dunia nzima e-commerce iliweza kupitisha mauzoya takribani dola trilioni 26 ambapo 90% ilikuwa ni Biashara kwa Biashara (B2B e-commerce) na 10% ilikuwa ni Biashara kwa Mlaji (B2C e-commerce). Hata hivyo kupima mwenendo wa e-commerce katika baadhi ya nchi zinazoendelea imekuwa ni changamoto kupata data na takwimu, haswa katika nchi za Afrika.

IMPORTATION: Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kwamba Biashara kati ya nchi na nchi imekua kwa kiasi kikubwa Afrika ambapo zimechagizwa na vituo vichache vya kiteknolojia (Hubs) ambavyo vimerahisisha mno mwenendo wa biashara. Biashara kati y nchi na nchi (Intraregional import) imekuwa zaidi ya mara 3 katika miongo miwili iliyopita kufikia 12%- 14% sawa na dola bilioni 100 ikichagizwa na uwepo wa jumuiya za kiuchumi barani (Subregional Economic Communities REC‘s).

UZOEFU: Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na umri wa Jumuiya hizi za Kimaendeleo barani Afrika ambapo uzoefu huo hutumika kuongeza jitihada katika kuboresha namna ya ufanyaji biashara kuelekea uchumi wa kidijitali kiteknolojia. Uzoefu huo pia hutumika kuunganisha jumuiya moja na nyingine (mf, SADC na COMESAna EAC) ambapo zitazalishwa nafasi nyingi zaidi za kufanya biashara kati ya nchi wanachama na ripoti zinaonyesha 75% ya biashara hizi ndani ya jumuiya barani Afrika zimefanyika mwaka 2017 peke yake na nusu ya biashara hizo zilifanyika katika jumuiya ya SADC.

Chini ya mwavuli wa AfCFTA nchi wanachama zinatarajia kufuta tozo/ushuru kwa 90% ya bidhaa zote zitakazopitishwa na kufanyiwa biashara katika eneo hilo. Hii itaruhusu uwezekano wa kupunguza mlolongo wa kodi au kuongeza idadi na thamani ya bidhaa na huduma zitakazohusishwa. Matokeo yoyote katika punguzo hilo linalotarajiwa katika muktadha wa biashara kidijitali yataleta picha tofauti. Kupunguza mlolongo wa tozo za mipakani baina ya nchi na nchi kutapungua kwa 15% pekee ikitegemea thamani ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi husika. Hii ni kwa mujibu wa Tume inayoshughulikia Uchumi wa Afrika kutoka Umoja wa Mataifa (UNECA) mwaka 2018.

Sasa mwaka 2018 Jumuiya ya COMESA ilibuni mfumo wa kudhibiti eneo huru la kibiashara kidijitali (Digital Free Trade Area DFTA). Mfumo huu umeundwa na mambo yafuatayo;

•E-trade: Hili ni jukwaa mahsusi kwa ajili ya kufanya biashara za kimtandao na kuwezesha malipo ya kielektroniki, mobile apps kwa ajili ya wafanyabiashara walioko katika Jumuiya hio.

•E-logistics: hili ni jukwaa maalum kwa ajili ya kuwezesha biashara ya usafirishaji wa mizigo baina ya nchi wanachama wa jumuiya.

•E-legislation: huu ni mfumo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara rasmi ambao unawawezesha kufanya miamala na malipo kielektoniki.

Mfumo huu uliobuniwa na Jumuiya ya COMESA umelenga kutangaza biashara za wanajumuiya katika nchi wanachama ikijumuisha kupitia majukwaa ya e-commerce. Mfumo huu ulikuwa ni mfanano wa mfumo uliotengenezwa na kuzinduliw na nchi ya Malaysia mwaka 2017 katika muktadha wa kufanya biashara huru ndani ya eneo maalum.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.

Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana, shuka nazo:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-biashara-ya-fedha-za-kidijitali-cryptocurrency-business/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)”
  2. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia;

e-mail: info@rednet.co.tz

tovuti: https://rednet.co.tz

Simu:+255765834754

FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)

Waswahili wanasema “Nyakati ngumu hazidumu bali watu wagumu ndio hudumu.” Na pia “Baada ya dhoruba huja shwari.” Sasa mnamo mwaka 2008 uchumi wa dunia ulikumbwa na mtikisiko mkubwa zaidi kuwahi kutokea baada ya ule Mtikisiko wa kiuchumi wa mwaka 1933. Katika mdororo huo taasisi na mashirika ya kifedha duniani yalijikuta yakishindwa kuzuia hali duni ya uchumi katika bei za bidhaa ghafi kama mafuta na mikopo ya aina mbali mbali ambapo ilipelekea huduma hizo muhimu kupatikana eidha kwa tabu sana au kwa bei isiyokidhi usawa wa soko.

Hivyo ni katika hali hio ya mdororo wa kiuchumi ndipo lilipoibuka jina la Satoshi Nakamoto ambalo linasadikiwa kuwa ni jina la kifumbo la mtu mmoja au kikundi cha watu wasiofahamika hadharani mpaka sasa ambao ndio waliotengeneza sarafu ya kwanza kabisa ya mtandaoni na wakaiita BITCOIN. Pia mtu/watu hao ambao wanasadikiwa kuwa na asili ya Kijapani walitengeneza mfumo wa kwanza wa database ya Teknolojia ya Blockchain kwa kupitia kiunzi (ledger) cha kimtandao ambacho hakitegemei hifadhi moja. Yaani taarifa za miamala ya kifedha katika BITCOIN hufanyika kupitia Miundombinu ya Blockchain ambayo huwa ni ya siri mno na iliyotawanyika duniani kote na hivyo kuzifanya sarafu za mtandaoni zisiweze kudhibitiwa na taasisi na mashirika ya kifedha au hata vyombo vya kiserikali.

Kwanini ikawa hivi? Fuatana nasi kujua zaidi..

Kwa mujibu wa tovuti za study.com na Investopedia, Sarafu za mtandaoni au Cryptocurrency ni sarafu za kidijitali zinazoakisi thamani ya fedha ambapo kukua au kudorora kwa thamani hio hutegemea na uhitaji wa sarafu hio duniani kwa muda huo. Mfano wa sarafu hizi ni kama bitcoin, ethereum, Litecoin, Libra na kadhalika. Mpaka kufikia tarehe 20 June, 2019 BITCOIN thamani yake ilikuwa ni dola za kimarekani 9,259.37 na ETHEREUM ikapatikana kwa dola 269.11, Litecoin ikapatikana kwa dola 136.29 na kadhalika. Inakadiriwa mpaka kufikia February, 2019 tayari mtandaoni kulikuwa na sarafu 2500 tofauti tofauti za kimtandao ambapo pia iliripotiwa kuwa na miamala au mizunguko ya Bitcoin peke yake zaidi ya milioni 17.53 ambayo thamani yake inakadiriwa kuwa ni takribani dola bilioni 63.

Hata hivyo mpaka sasa soko la sarafu za mtandaoni limekua mpaka kufikia zaidi ya dola bilioni 120 huku sarafu ya Bitcoin peke yake ikichukua zaidi ya nusu ya thamani ya soko zima.

DHUMUNI LA KUANZISHWA CRYPTOCURRENCIES:

Neno Cryptocurrency ni mjumuisho wa maneno mawili, ‘Crypto’ na ‘currency’. Yaani sarafu iliyobadilishwa katika ulinzi wa kimtandao uitwao cryptography ambao huipa sarafu thamani yake ya kipekee na pia kuweza kuifanya sarafu hio isiweze kudukuliwa kirahisi.

Kutengeneza urahisi zaidi wa kulipia huduma na bidhaa mtandaoni, huduma za hoteli, migahawa, kurusha fedha kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa uhuru na wepesi zaidi na pia kubadilisha fedha katika masoko ya kimtandao ya kubadili fedha. Hizi ni baadhi ya sababu za kuanzishwa kwa sarafu hizi za mtandaoni, lakini sababu kubwa ni kuhakikisha ulinzi madhubuti na uhuru wa mtu kuhifadhi na kutumia fedha zake katika muda wowote atakaohitaji bila kufuatiliwa na taasisi au mashirika ya kifedha au vyombo vya serikali. Yaani kuwa na uhuru halisi juu ya fedha zako.

ZINAFANYAJE KAZI SARAFU HIZI?

Cryptocurrency zinafanya kazi kwa mfanano kama kadi ya benki ambayo huruhusu kufanyika miamala mbalimbali ya kutuma na kupokea fedha katika mfumo tata wa kielektroniki wa kifedha. Utofauti na utendaji wa kadi ya benki ni inaweza kufuatiliwa na taasisi za kifedha na mashirika ya kiserikali na pia huhifadhi kumbukumbu za wateja mahali pamoja.

Miamala hutumwa baina ya kompyuta washirika kwa kutumia programu ziitwazo “cryptocurrency wallets” ambapo mtu anayefanya muamala hutumia programu hio ya wallet kutuma fedha kutoka akaunti moja kwenda akaunti nyingine. Hata hivyo, ili kuweza kutuma au kupokea fedha katika mfumo huu, huna budi kuwa na nywila(password) au ufunguo binafsi ambayo inahusiana na akaunti yako. Miamala hio inayohusisha kompyuta washirika hufichwa katika msimbo wa kimtandao (encryption) halafu hutumwa katika mtandao wa sarafu hizo duniani ambapo huorodheshwa katika forodha ya jumla iliyohifadhiwa mtandaoni. Kiasi cha miamala inayopitishwa huwa ni wazi, lakini anayetuma muamala huo hufichwa, hii huitwa pseudo-anonymous ambapo ambapo kila muamala huwa na seti ya kipekee ya nywila (keys/passwords) na yeyote anayemiliki nywila hizo ndiye anayemiliki sarafu zote zilizo ndani ya akaunti hio. Kama ilivyo tuu kwamba anayemiliki akaunti ya benki ndiye anamiliki fedha zote zilizo ndani ya akaunti hio.

UNAWEZAJE KUWEKEZA KWENYE CRYPTOCURRENCY?

Sababu kuu ambayo huvutia watu wengi kuwekeza katika cryptocurrency ni kuweza kupata fedha nyingi zaidi muda mchache tuu baada ya kuwekeza mtaji. Hata hivyo kwa mujibu wa mtandao wa Forbes haya hapa chini ni baadhi ya mambo ya msingi zaidi ya kuzingatia kabla hujaamua kuweka fedha zako kama mtaji katika biashara hii:

1. AMUA AINA IPI YA CRYPTOCURRENCY UNGEPENDA KUSHUGHULIKA NAYO ZAIDI: Kama ilivyo muhimu kujua kujua kiasi cha mtaji unachokwenda kuwekeza, vile vile ni busara kuwa na mipango mizuri katika kuelewa misingi ya cryptocurrency hiyo kwa kuwa itachangia kwa kiasi kikubwa jinsi ya kujikinga na matishio yajayo ya kiuchumi.

2. AMUA UTATAKA KUWA NA UWEKEZAJI WA NAMNA GANI: Kwa kawaida utalazimika kuwa na mpango kama unataka kuingia katika masoko ya cryptocurrency. Swali ni mipango yako inaweza kuwa ya muda mrefu, wastani au ya muda mfupi. Hii itategemeana na fedha ulichonacho.

3. KUMBUKA, TAKWIMU ZA SOKO NI MUHIMU ZAIDI: Soko la sarafu za crypto ni tete muda wote. Huweza kubadilika hata kwa asilimia 20 kwa siku, hivyo ni muhimu kufuatilia taarifa za soko kwa ukaribu zaidi.

Umejifunza jambo gani kwenye makala haya? Tafadhali pitia makala tumekuwekea hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala hii ya leo kisha, acha maoni yako chini hapo kwenye sehemu ya comments..

  1. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  2. https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-biashara-za-kielektroniki-e-commerce-businesses/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI?”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-mapinduzi-ya-teknolojia-ya-5g-katika-biashara-na-uchumi-wa-afrika/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU MAPINDUZI YA TEKNOLOJIA YA 5G KATIKA BIASHARA NA UCHUMI WA AFRIKA”
  4. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO (BUSINESS INTELLIGENCE)?

TEKNOLOJIA KATIKA BIASHARA ZA KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA (TECHNOLOGY IN SUB SAHARAN BUSINESS )

Kwa watumiaji wengi wa simu za mkononi waishio Kusini mwa jangwa la Sahara, simu ya mkononi si kwamba ni kifaa cha mawasiliano tu, lakini zaidi ni kifaa muhimu cha kuperuzi mtandaoni na kupata huduma mbalimbali za msingi za kibinadamu. Ujio wa simu za rununu (Smartphones) eneo hilo umekuwa maradufu katika miaka ya hivi karibuni. Watumiaji wa simu za rununu wameongezeka kutoka 25% mwanzoni mwa muongo huu (2010’s) mpaka kufikia 44% mwishoni mwa mwaka 2017. Hii ni chini ya wastani wa kidunia wa 66% katika ongezeko hilo la watumiaji wa simu za mkononi. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa shirika la kimataifa la mfumo wa mawasiliano ya simu GSMA.

Watumiaji hao wa simu ambao ni 44% ya jumla watu waishio katika eneo hilo sawa na watu milioni 444 ambao pia ni aslimia 9% tu ya watumiaji wote wa simu za mkononi duniani wanatajwa kupatikana katika eneo hilo la kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia inatajwa kwamba ongezeko hilo la watumiaji litakuwa katika kiwango cha CAGR (Compound Annual Growth Rate) kwa 4.8 katika kipindi cha mwaka 2017 hadi 2022, ambacho ni zaidi ya mara mbili ya CAGR ya dunia nzima katika kipindi hicho hicho.

Moja ya vitu vinavyotoa nguvu katika ongezeko hili ni pamoja na uwezo wa simu za rununu (janja) kuunganisha watu wengi kupitia huduma za intaneti na mitandao ya kijamii ambapo katika mitandao hio ndipo panapotumiwa na watu wengi kama sehemu ya kukutana, kubadilishana mawazo, kuburudika na kufanya biashara. Hivyo kufanya mitandao hio ya kijamii kuzidi kuwa na umuhimu kadiri muda unavyokwenda.

Kibiashara hii ina maana gani?

Ripoti hio ya GSMA iliyochapishwa mwaka 2018 inataja kwamba ukuaji wa teknolojia umerahisisha mambo mengi muhimu yakiwemo utolewaji wa elimu, maswala ya afya na tiba na pia kuwezesha mazingira bora ya kufanyika biashara katika kutunza na kuonyesha kumbukumbu mbalimbali, miamala ya kifedha na jinsi bora ya kumhudumia mteja hata akiwa mbali na mzalishaji kupitia majukwaa ya huduma za kifedha za kimtandao na IoT (Internet of Things). Ripoti hio pia inaakisi kasi ya ukuaji wa matumizi ya simu za rununu (samrtphones) pamoja na vifaa vya kiteknolojia mpaka kufikia mwaka 2025 katika utendaji na utoaji wa huduma mbalimbali za kibinadamu pamoja na shughuli za kibiashara katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia unaweza kupitia makala hizi hapa chini ambazo zinarandana na somo ulilolipata kwenye makala ya leo. Zitakusaidia sana ukimaliza kuzisoma zote.

  1. https://rednet.co.tz/unawezaje-kutumia-ujasusi-katika-biashara-yako-business-intelligence/ yenye kichwa “UNAWEZAJE KUTUMIA UJASUSI KATIKA BIASHARA YAKO?”
  2. https://rednet.co.tz/uwiano-wa-mali-assets-na-madeni-liabilities-katika-biashara-ukweli-ni-upi/ yenye kichwa “UWIANO WA MALI(assets) NA MADENI(liabilities) KATIKA BIASHARA, UKWELI NI UPI?”
  3. https://rednet.co.tz/changamoto-katika-biashara-mpya-inayoanza-funzo-lisiloepukika/ yenye kichwa “CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA MPYA/INAYOANZA, FUNZO LISILOEPUKIKA.”
  4. https://rednet.co.tz/fahamu-mchango-wa-ict-katika-maendeleo-ya-sekta-binafsi-barani-africa/ yenye kichwa “FAHAMU MCHANGO WA ICT KATIKA MAENDELEO YA SEKTA BINAFSI BARANI AFRIKA”
  5. https://rednet.co.tz/kuanzishwa-kwa-eneo-huru-la-biashara-barani-africa-afcta-kuna-manufaa-gani-kwako/ yenye kichwa “KUANZISHWA KWA ENEO HURU LA BIASHARA BARANI AFRIKA, KUNA MANUFAA GANI KWAKO?”