Tag: afrika mashariki

D.R.C NDANI YA E.A.C, MFANYABIASHARA ANAFAIDIKA VIPI?

Hatimaye tar29 March Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ilipata kibali cha kuwa mwanajumuiya wa Afrika Mashariki (EAC) na mwezi July mwaka huo 2022 DRC iliingia rasmi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuwasilisha matakwa yote makao makuu ya jumuiya hio jijini Arusha. Hii ni baada ya kuendesha mchakato uliodumu kwa takriban miaka minne. Sasa DRC inapoingia ndani ya EAC mfanyabiashara anafaidika vipi?

DRC inakuwa mwanachama namba 7 wa EAC huku ikiwa ndio nchi kubwa zaidi kijiografia katika ukanda huo. Inasemekana DRC ndio nchi yenye rasilimali (madini, mafuta, misitu n.k) nyingi zaidi duniani. Pia nchi hio ina idadi ya watu takribani milioni 90 ambao ni mtaji muhimu kiuchumi.

MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU D.R.C:

Kukubalika kwa DRC kunamaanisha kwamba soko la Afrika Mashariki linatanuka na kuwafikia watu zaidi ya milioni 300 waishio ndani ya jumuiya hio tu, huku uchumi wa jumla ukiwa na thamani ya 250$ bilioni. Sasa DRC ina nini cha ziada usichokijua?

1. MIPAKA YA KIJIOGRAFIA:

Ikiwa ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa jiografia barani, DRC inapakana na nchi zingine 9. Nchi hizo ni Angola, Burundi, Jumhuri ya Afrika ya Kati, Rwanda, Jamhuri ya Congo (Brazaville), Sudani Kusini, Uganda, Zambia na Tanzania. Muingiliano wa kibiashara ni mkubwa sana hapa.

Zaidi upande wa magharibi mwa jiji la Kinshasha inapakana na bahari ya Atlantiki. Sasa Kongo kupakana na nchi 9 na kuwa na ufukwe wa bahari ya Atlantiki kunaifanya iweze kutanua fursa kwa wafanyabiashara kupitisha mali kwenda nchi nyingi zaidi barani na hata nje ya bara.

DRC na mipaka yake. Milango ya biashara za kimataifa kwa EAC.

2. KUHUSU VIVUTIO VYA UTALII:

Mbuga ya wanyama kongwe zaidi barani ipo DRC, inaitwa Virunga. Hapo utawakuta wale Sokwe wakubwa (Gorillas), simba na tembo. Lakini mbuga hii ipo kwnye tishio la kutoweka kwa sababu kuna mafuta na kampuni ya Uingereza ya Soco tayari imetia timu kuanza kuchimba mafuta hapo mbugani.

Hawa gorilla ni kivutio kizuri sana cha utalii lakini miaka ya hivi karibuni wamekuwa adimu na kutokana na shughuli za mwanadamu, wanyama hawa wapo kwnye tishio la kutoweka kabisa. Je, DRC kuingia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kutadhibiti hatari ya sokwe hawa kutoweka?

Kuhusu namna utalii unaweza kuleta manufaa katika biashara tafadhali fuatana na makala hii hapa chini:

3. KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NA MIUNDOMBINU:

Ni 1.8% tu ya barabara nchini DRC ndio ina kiwango cha lami, huku chini ya 10% ya nyumba za makazi ndio zina umeme. Hii ni hali mbaya sana katika kukuza uchumi wa Taifa. Hata hivyo Benki ya Dunia imetangaza kifurushi za 1$ bilioni kwa ajili ya miundombinu ya DRC.

Moja kati ya vitu vinavyorudisha nyuma juhudi za wajasiriamali na mashirika kuwekeza nchini DRC ni maendeleo duni ya miundombinu. Ukizingatia ukubwa wa nchi hio, imekuwa ni nafuu kusafiri kwa njia ya anga kuliko barabara. Sasa @jumuiya itachangia vipi maendeleo ya miundombinu?

4. BIASHARA ZA NJE YA NCHI (EXPORTS):

Muziki wa DRC ndio mali inayouzwa zaidi nje ya nchi (export). Kuanzia miaka ya 90 muziki wa Bolingo ndio ulikua unasikilizwa na kupendwa zaidi bara zima la Afrika. Ndio maana wasanii kama Fally Ipupa na Koffi Olomide ni matajiri sana. Madini na malighafi zingine zote chali.

5. LUGHA INAYOTUMIKA ZAIDI:

Jiji la Kinshasa ni la pili kwa matumizi ya lugha ya Kifaransa likitanguliwa na jiji la Paris. Yaani Wakongo hawa wanaongea kifaransa zaidi kuliko hata miji ya nchini Ufaransa. Hata hivyo hii inachangiwa na idadi ya watu wanaoishi kwenye jiji hilo, watu milioni 10 mchezo!

Ukiacha Kifaransa raia wa Kongo pia wanazungumza lugha zingine kama Kilingala, Kiingereza, Kiswahili na lugha za makabila asilia. Hivyo ukiwa kama mfanyabiashara na moja kati ya lugha tajwa unazifahamu vyema basi nafasi ni yako kuingia DRC na kutanua biashara zako.

6. KUHUSU UGONJWA WA EBOLA:

Kwamba kupata Ebola nchini DRC ni rahisi kama kupata mafua ukiwa sehemu nyingine? HAPANA. Baada ya ugonjwa huo kufumuka mwaka 1995 na kuua watu zaidi ya 200, milipuko mingine ya ugonjwa huo imekuwa ikidhibitiwa kwa kiwango kikubwa. Hivyo Congo ni salama.

7. KUHUSU MADINI:

Lile bomu la atomiki lililodondoshwa kwenye miji ya Hiroshima na Nagasaki katika WWII lilitengenezwa kwa madini ya Uranium kutoka mgodi wa Shinkolobwe, mkoani Katanga nchini DRC. Hata hivyo mgodi huo ulifungwa mwaka 2004 kutokana na kuishiwa madini ukiiacha DRC patupu.

Kongo imenyonywa sana katika madini yake. Hali kadhalika nchi zingine katika Jumuiya zimepitia hali hio. Hivyo itakapowekwa sera ya pamoja ya kulinda na kusimamia rasilimali zilizopo ndani ya Jumuiya, bila shaka madini na rasilimali ambazo zipo DRC zitakuwa na manufaa sana.

8. HISTORIA YA UNYONYAJI:

Mfalme Leopold II wa Ubelgiji alijitangazia Kongo kuwa mali yake binafsi kuanzia mwaka 1870. Koloni hilo ndio lilikua mali binafsi kubwa zaidi kuwahi kumilikiwa na mtu mmoja kwenye historia. Umiliki huo ulisababisha vifo vya watu milioni10. Huu ndio mwanzo wa nchi kuharibika.

Mfalme Leopold II aliagiza watu kukusanya zao la mpira ambalo kwa kipindi hiko ndio lilikua zao bora zaidi la kibiashara. Wale walioshindwa kukusanya zao hilo kama kodi waliadhibiwa kwa kunyimwa chakula na kukatwa mikono yao. Ukatili huo ulikua mbaya sana dhidi ya ubinaadam.

9. HALI YA USALAMA NA VITA:

DRC imekuwa ikikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na migogoro isiyokwisha ambayo imepelekea vifo vya watu takriban milioni 6. Hali hio ya vita visivyokwisha imepewa jina la “Vita vya Dunia vya Afrika”.

Vita hivyo kwa sehemu kubwa vimekuwa vikisababishwa na vikundi fulani (kampuni, mashirika na raia wa kawaida) kugombania rasilimali katika eneo fulani. Huyu anataka kuchimba, raia wanataka kunufaika. Je, DRC kuingia kwenye @jumuiya itasaidia kumaliza janga la vita visivyokwisha?

10. KUHUSU MTO CONGO:

Ukiwa na urefu wa kilomita 4,700, mto Congo ndio mto mrefu wa pili barani Afrika ukitanguliwa na mto Nile. Pia huo ndio mto wenye kina kirefu zaidi duniani. Cha kufurahisha zaidi, Mto Congo na Mto Nile yote inapatikana katika EAC. Inakupa picha gani hii kiuchumi?

Je, EAC itaweza kuzalisha umeme wa pamoja kupitia sehemu za mto huo? Je shughuli za kiuchumi kama uvuvi, usafiri, utalii biashara ya mazao ya misitu zitaweza vipi kusimamiwa na Jumuiya kuhakikisha faida zinarudi kwa wanachi wa Kongo na wa jumuiya nzima kiujumla?

ZIADA: MSITU WA CONGO

Msitu wa pili kwa ukubwa duniani, msitu wa Congo unapatikana nchini DRC. Hata hivyo msitu huo ni mkubwa kiasi kwamba umeingia kwenye nchi zingine kama Cameroon, Jamhuri ya Afrika Ya Kati, Jamhuri ya Congo(Brazaville), Guinea ya Ikweta na Gabon. Msitu huu ni utajiri mtupu.

msitu wa mvua wa Congo
Msitu wa Congo

Katika msitu huo kuna fursa nyingi zikiwamo biashara ya magogo, madawa ya kutibu watu, mazao na wanyama, mbao, karatasi na bidhaa zote zitokanazo na misitu. Ukiwa kama mfanyabiashara ambaye sasa una uhuru wa kwenda kuwekeza DRC kirahisi, utaitumiaje fursa hii?

Sasa hayo ni baadhi ya mambo ambayo pengine ulikua huyafahamu kuhusu DRC. Mambo hayo kama yakifanyiwa kazi ipasavyo ndani ya @jumuiya basi ni wazi kutapunguza hali ya umasikini na kuimarisha amani kwa watu wa Kongo na kuimarisha uchumi wa Jumuiya nzima. Mapema mwaka 2021 jumuiya ya nchi za Afrika kwa kauli moja ilianzisha eneo huru la biashara barani (AfCFTA) ambapo nchi wanachama wanaweza kufanya biashara kwa uhuru bila ya vizuizi vya mipakani. Zaidi soma hapa chini

Jumuiya hii inatoa uhuru kwa wanachi wake kuishi na kufanya biashara popote ndani ya nchi wanachama. Jambo hili linatoa fursa kwa Wajasiriamali wa aina zote kuzurura na kutafuta masoko yao kirahisi. Ukiweza vema kutumia majukwaaa ya kimtandao kama websites, mitandao ya kijamii ujue unayo nafasi ya kuwafikia watu milioni 300 waishio ndani ya Afrika Mashariki. Sasa tuambie wewe mtu wa Teknolojia, website designer, mtaalam wa kutengeneza android app, mkulima, engineer nk, unataka ufaidike vipi hapa? Tuambie..

Je umependezwa na makala yetu hii ya leo?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER)5432715 ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA yetu muda wowote yaani 24/7.

M-PESA LIPA NAMBA
Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara

BIASHARA YAKO INAWEZA VIPI KUWA TAASISI IMARA

Biashara nyingi zimekuwa zikiendeshwa katika mtindo wa “Kujiajiri” ambapo wajasiriamali wengi huteseka wakifanya kazi kwa bidii usiku na mchana lakini hujikuta siku moja tu wasipofanya kazi basi biashara inashindwa kuzalisha. Yaani mfanyabiashara unajikuta unakuwa mtumwa kwenye biashara yako mwenyewe? Hio dhana ya kujiajiri inakuwa na maana gani sasa? Leo sasa tuangalie Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara inayojitegemea? Makinika mpaka mwisho wa makala hii.

Septemba 21 kila mwaka ni Siku ya Kimataifa ya Amani. Sasa katika Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (UN), Lengo Na. 16 limekazia katika kudumisha Amani, Haki na Taasisi Imara. Amani ni mbolea muhimu katika ukuaji wa uchumi mahali popote. Mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa uliokaa mwaka 2001 ulithibitisha kuweka Siku maalum ya kutafakari na kudumisha Amani, Haki na Taasisi Imara duniani, ambapo siku hio ni September 21 kila mwaka.

Hii ni kutokana na vitendo vya uvunjifu wa amani, taasisi dhaifu na kukosekana haki si za kidemokrasia katika utendaji, serikali hizi ambazo mara nyingi huwa ni za kidikteta au za kifalme, mara nyingi huendeshwa kwa sheria zinazokandamiza upande mmoja na kuimarisha kikundi kidogo cha watu kwa maslahi yao binafsi.

Jambo hili hutokea pale viongozi (watu wanaopewa dhamana) kushindwa kuwajibika kwa wanachi na hivyo kujiundia sheria ambazo zinawapa mamlaka ya kutumia rasimali za nchi huku zikiwaacha wanachi katika hali ya upofu wasiwe na nguvu ya kuuliza na kusimamia matumizi sahihi ya rasilimali zao. Hili ni jambo baya na linalopaswa kuagamizwa mahali popote kwanzia ngazi ya familia, biashara, kampuni, shirika mpaka serikalini.

Mwandishi mahiri Robert Kiyosaki katika kitabu chake cha CASH FLOW QUADRANT amefafanua kwanini Matajiri huendelea kuwa matajiri huku Watu wa Uchumi wa kati wakiendelea kukimbia mbio za panya na masikini wakizidi kuwa masikini. Kwa haraka haraka, katika Njia 4 za kuingiza mapato ambazo zimeonyeshwa kwa herufi za E, S, B na I, zimetajwa kuwa ndio chanzo kikuu cha mapato ya watu duniani.

SEHEMU ZA KUIFANYA BIASHARA YAKO KUWA TAASISI IMARA?

Waswahili wanakwambia “Kila mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake” lakini katika uwanda wa kiuchumi na biashara duniani, kila mtu anao uwezo wa kubadilika na kufanya uchaguzi ulio bora zaidi kwa maisha yake ya kiuchumi na kijamii. Na hii ni kwa kujifunza na kufanya kazi tu.

E = EMPLOYEE (MWAJIRIWA): Kitu cha kwanza ambacho kipo kichwani kwa mwajiriwa yeyote ni uhakika wa kibarua chake (job security). Mwajiriwa hufanya kazi kwa bidii ili apate mkate wa kila siku na zaidi awe na hakika kuwa ataendelea kupokea mshahara kila mwisho wa mwezi kwa miaka mpaka atakapostaafu au kumaliza mkataba wake. Dhana ya kuwa majiriwa huathiri ubunifu wa mtu katika kutaka kujaribu shughuli nyingine itakayoimarisha uchumi wake zaidi ya ajira.

Mwajiriwa anapohitaji kukua kiuchumi hutafuta ajira itayomlipa zaidi na si fursa za biashara mpya.

udalali wa mtandaoni ongea na watu uvae viatuBiashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara

S= SELF-EMPLOYED (KUJIAJIRI): Hii ni njia ya mateso makubwa, japokuwa vijana wengi eti ndio hupenda kufanya shughuli za kujiajiri wakihisi kuwa huko kuna uhuru mkubwa na pesa nyingi. #VijanaWenzangu acheni kujidanganya. Unapojiajiri fahamu kuwa utajinyima uhuru wako binafsi ili biashara yako iweze kuwa hai. Wewe ndio unakua CEO, sales manager, mhasibu wewe, mtu wa masoko wewe, yaani wewe ndio unakuwa kila kitu. Hata hivyo kwa biashara inayoanza si vibaya kupitia katika hatua hii japo hutakiwi kukaa muda mrefu hapa, lazima biashara ivuke hiki kiunzi.

B=BUSINESS OWNER (MMILIKI WA BIASHARA): Tofauti na walio katika Chumba “S” Mtu anayemiliki biashara sio lazima awe anafanya kazi katika biashara hio. Yeye anamiliki mfumo wa utendaji au bidhaa ambayo ndio huzalisha pesa muda wote hata asipokuwepo. Mfano, mtu anayemiliki kiwanda cha kutengeneza nguo. Sio lazima awe ndio mtendaji mkuu wa kutengeneza nguo, hata hivyo yeye anaweza kuajiri watu wa kiwandani na kuwalipa ili waendelee kuzalisha bidhaa zitazoendelea kuingiza pesa.

I=INVESTOR (MUWEKEZAJI): Huyu ndiye mtu mwenye uelewa mkubwa zaidi kati ya wote ambao tumewajadili hapo juu. Mtu huyu hutafuta Mali (Assets) zaidi kuliko madeni (Liabilities). Mara nyingine hutumia pesa za watu wengine (mkopo) ili kuhakikisha anapata Mali itakayozalisha (asset). Ukitaka kufahamu kwa undani kuhusu Uwiano unaofaa wa Mali na Madeni katika biashara gusa link hii Uwiano wa Mali (assets) na Madeni (Liabilities) kwenye biashara.

Mtu huyu hutumia faida anayopata kutoka kwenye assets zake kununua assets nyingine nyingi zaidi, na hujikuta akifurahia maisha ya kuingiza kipato kutoka kwenye assets kuliko vyanzo vya matumizi (liabilities). Kama ulikua hufahamu basi Matajiri unaowajua duniani wote ni Wawekezaji huku wakitumia kanuni ya 70% kwa 30% katika shughuli zote za kifedha. Kiufupi kanuni hio hutumika katika kupanga matumizi ya mapato ambayo hugawanywa katika mafungu matatu ya:

i. 70% Matumizi ya kawaida (Normal Expenses including taxes, rents, food, accomodations etc)

ii. 30% (20% Servings + 10% Charity) Mwekezaji anapohitaji pesa hutafuta assets zaidi kuliko kufanya matumizi yanayofyonza pesa za biashara.

Sasa basi, hayo yote niliyoyaeleza, hayatakuwa na maana kama hayatafanyika katika muundo wa Taasisi Imara.

BIASHARA KAMA TAASISI IMARA INA SIFA ZIPI?

Taasisi Imara ni ile jumuiya ya kiuchumi/Kijamii ambayo inaendeshwa kwa mujibu wa katiba katika utendaji wake wa kila siku. Jumuiya hio inaweza kuwa ni Serikali, Shirika, Kampuni, Chama, Biashara au Familia. Familia (Ndoa) ndio Taasisi ya kwanza kabisa kuwahi kuanzishwa na binadamu duniani. Ndio maana wahenga wanakwambia “Maendeleo yanaanzia nyumbani.

Maendeleo ya taasisi hutegemea uwepo wa sheria zitakazokuwa muongozo wa kila kinachofanyika kila siku ndani ya taasisi hio. Hata hivyo ili iwe taasisi imara inapaswa kuwa na sifa hizi:

1. SHERIA MBELE, MTU NYUMA: Taasisi imara hutambua na kutekeleza matakwa ya kisheria na kamwe si matakwa ya mtu binafsi. Sheria hizi huandikwa katika mfumo wa Katiba (constitution/memorandum/articles of assosciation, Taratibu (regulations) na sheria ndogondogo (by-laws). Taasisi zinazoongozwa vema kwa mujibu wa sheria bila kumuogopa mtu huwa imara sana kiutendaji na hufikia malengo yake kiurahisi zaidi.

2. UTAMADUNI: Katika utendaji bora, Utamaduni huzingatiwa kama silaha bora zaidi katika uzalishaji/utoaji huduma wenye viwango vya juu vinavyitakiwa. Wahenga walishasema “Culture eats strategy for breakfast” yani, hakuna mbinu ambayo itaweza kufanya kazi kwa mafanikio isipofanywa kama sehemu ya utamaduni. Hivyo Taasisi imara hufanya shughuli zake katika Utamaduni uliotengenezwa kwa muda mrefu katika kufikia malengo yaliyowekwa. Mfano, utamaduni wa kupongeza mtendaji bora, utamaduni wa kumhudumia mteja kwa njia ya mtandao na utamaduni wa kuzingatia viwango.

3. UWAJIBIKAJI: Ili iwe Taasisi imara lazima watendaji wawajibike katika majukumu ya kila siku. Watendaji wanapaswa kuwajibika kwa Kupongezwa, Kujiuzulu au Kuongeza kiwango cha uzalishaji/utoaji huduma kwa wateja wao. Taasisi imara haipaswi kufumbia macho swala la uwajibikaji.

Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara

4. KWELI NA HAKIKA: Hakuna Taaasisi Imara ambayo haijiendeshi katika namna ya Ukweli na Uhakika kwa wateja wake. Hata hivyo, hakuna mifumo ya Taasisi inayofanya kazi kwa ubora wa 100%, ni vema kuhakikisha jambo hili linazingatiwa.

Tulizoziona leo ni baadhi ya sifa zinazotengeneza Taasisi Imara. Kwa mujibu wa malengo Endelevu ya kimataifa ya UN, imepangwa kutimiza lengo la kuwa na Taasisi Imara ifikapo mwaka 2030 (#Agenda2030). Tujadili kupitia Replies, Retweets na Share ili watu wengi zaidi wanufaike.

Tuungane kwa pamoja kuhakikisha Biashara yako inaweza vipi kuwa taasisi imara. Endelea kupata makala muhimu kuhusu Biashara, Uchumi na Teknolojia kupitia links hizi hapa:

  1. WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?
  2. KWANINI UITANGAZE BIASHARA YAKO?
  3. UMUHIMU WA TAKWIMU KATIKA UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA WATEJA
  4. TEKNOLOJIA KATIKA KUKUZA BIASHARA KUPITIA SEKTA YA UTALII
Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

BRANDING Vs MARKETING, KIPI NI KIPI?

Unapofanya biashara, moja kati ya malengo makubwa ni Kupata/kuendelea kupata wateja kila siku. Wateja ndio Roho ya biashara. Hakuna biashara kama hakuna wateja. Lakini unawapataje wateja hao? Unatumia vipi mbinu za Marketing na Branding? Branding vs Marketing, Kipi ni kipi?

Unapokuwa unaitengeneza biashara yako unatumia mbinu nyingi sana kujitangaza na kuvuta wateja wengi kwa kadiri inavyowezekana. Kuna wanaotumia ndugu, jamaa wa karibu, classmates, colleagues n.k. Ili mradi tu connections zinahusika kwa ukubwa wake. Kuna wengine wanatumia mitandao ya kijamii, kuna wanaofanya company visits na wengine wanatumia mbinu ya Umachinga (Kutembeza Barabarani). Lakini wote hao wanatumia Mbinu mbili tu kimsingi. Ni Either Marketing au Branding.

MARKETING na BRANDING ni nini?

Marketing ni mjumuisho wa vitendea kazi, utaratibu na mbinu za kuhakikisha bidhaa/huduma zako zinapigiwa debe ipasavyo ili ziuzike. Marketing ni mbinu ya kumfanya mteja anunue bidhaa/huduma zako. Ndo kupiga debe kwenye huko. Upande wa pili, Branding ni ile namna unajiweka/unaiweka biashara yako ili iweze kupokea wateja zaidi.

unawezaje kupata wateja mtandaoni unawezaje kutumia teknolojia ya intaneti na kompyuta katika biashara yako?Branding Vs Marketing. Kipi ni kipi?

Ule unauweka utambulisho wa biashara yako, unavyofanyia kazi Dira, Malengo na Mipango yako na vile vitu vinavyokufanya wewe kuwa tofauti na washindani wako kibiashara. Hio ndio BRAND yako. Kama Marketing ni sumaku ya kuvuta wateja, basi Branding ni sukari ya kuwafanya waendelee kuwepo.

KIPI KINAANZA – BRANDING au MARKETING?

Fahamu, Branding ipo kwenye ule msingi kabisa wa Mbinu zako za kimasoko (marketing strategy), hivyo Branding lazima itangulie. Ukiitengeneza vizuri Brand yako hata kama ni changa, swala la Marketing linakuwa rahisi maradufu. Brand yako unayoitengeneza ndio itawafanya wateja waendelee kukujia na kuongezeka kwa mabalozi wa kujitolea wa bidhaa/huduma zako, ambao ndio wateja wenyewe haohao. Hii inaitwa “Customer’s Loyalty” (nimekosa kiswahili chake). Mfano, tizama Pepsi, pengine ndio soda inayouzika na kunyweka zaidi duniani kwa sasa, nikikuuliza umekunywa pepsi ngapi tangu mwaka huu umeanza pasi na shaka huna jibu, yaani umekunywa nyingi zisizo na idadi. Sasa hio ni kwa kuwa watengenezaji wa soda hio walitengeneza tabia zinazokufanya uendelee kuitumia miaka na miaka. Tabia hizo ni pamoja na Usafi wa chupa, Ubora, ladha n.k.

Pata huduma za Website, SEO, Social Media Marketing na nyinginezo nyingi kutoka Rednet TechnologiesBranding vs Marketing. Kipi ni kipi?

Katika biashara za namna bora zaidi ya kuji-Brand ni kutumia mitandao ya kijamii. Sasa unatumiaje mitandao ya kijamii kwa manufaa ya biashara yako? Branding vs Marketing, Kipi ni kipi? Tafadhali songa na makala hii kwenye link IJUE NGUVU YA MITANDAO YA KIJAMII KATIKA BIASHARA

Hivyo linapokuja swala la marketing, ni rahisi zaidi kuipromote Pepsi ikauzika kuliko Fanta passion. Branding ni ile kutengeneza utamaduni, mhenga mmoja alishasema, “Culture eats strategy for breakfast”. Yaani hata uwe na mbinu gani, kama hujazifanya mbinu zako kuwa utamaduni unaoishi, hapo andika maumivu. Ndio maana wanamichezo makini hufanya mazoezi kama utamaduni wao wa kila siku, na ndio hao ambao wanafanikiwa zaidi. Branding vs Marketing, Kipi ni kipi?

Branding vs Marketing, Kipi ni kipi? Tofauti ni ipi?

1. Marketing ni ile mbinu ya kutengeneza mhemko(attention) kwa wateja, Branding ni namna ya kuwafanya wateja waendelee kuwa wateja wako.

2. Marketing ni mbinu ya kufanya mauzo, Branding ni namna ya kutengeneza Jina, Heshima na Ushawishi kwa wateja.

3. Branding ndio inayoanza kuonekana katika biashara yako, Marketing inafuata.

4. Mbinu za kufanya Marketing hubadilika kulingana na wakati na mahitaji, lakini Branding ni Mbinu ya kutengeneza Utamaduni wa kudumu kizazi na kizazi.

5. Branding inahusika sana katika kufanya shughuli za kila siku za ndani ya biashara/kampuni yako, na vile wateja wanaziishi huduma/bidhaa kutoka kwako. Ndio utamaduni wenyewe.

Kwa chochote unachokifanya, fahamu biashara yako ni moja kati ya biashara nyingi duniani ndani ya bahari ya Ushindani wa kimasoko. Unahitaji mbinu bora katika kutengeneza Brand (Recognition) yako pamoja na Marketing (sales) za kila siku.

Kwa maneno mengine mbinu hizi hujieleza kupitia Dira (Vision) na Malengo (Missions) ya biashara yako. Leo nataka useme hapa Vision na Missions ambazo umejiwekea katika biashara yako ni zipi? Ukiweza kuzieleza na kuzisimamia vizuri basi, basi Utakuwa unaiweka pazuri bishara yako. Mfano, Rednet Technologies ilianzishwa ikiwa na Dira(vision) ya “Kuhakikisha Wafanyabishara wadogo na wakati (SME’s) wote nchini Tanzania na Afrika Mashariki wanatumia Teknolojia za kisasa katika utendaji wa biashara zao za kila siku.”

Mipango(Missions) ipo mingi lakini baadhi ni:

i. Kutengeneza websites bora kwa matumizi ya biashara mbalimbali kama ecommerce, corporate, funding na normal profile.

ii. Kutengeneza mifumo ya kuhifandhi na kuendesha mauzo na rekodi mbalimbali za kibiashara.

iii. Kuhakikisha wafanyabiashara wanapata taarifa muhimu kuhusu mbinu, takwimu na habari za Uchumi na mabadiliko ya kibiashara haswa kupitia Mapinduzi ya Viwanda yanayochochewa na mabadiliko ya kiteknolojia yanayotokea duniani kila uchwao. Taarifa hizo unaweza kuzipata kupitia tovuti yetu maridhawa ya https://rednet.co.tz Kupitia Vision na Missions hizo ulizoziona, Niambie ni rahisi kiasi kubuni mbinu ya kufanya Marketing? Je unaweza kuanzisha Marketing strategy gani kwa wakati huu unaosoma makala hii? Majibu yote unayo wewe mwenyewe.

Jinsi ya kuongeza mbinu za kulifikia soko la Mtandaoni.Branding vs Marketing. Kipi ni kipi?

Sasa makala hizi hapa chini zitakupa muendelezo mzuri kuhusu somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana kama ukizisoma zote. Gusa link kisha makinika:

  1. KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE RASMI YA BIASHARA YAKO
  2. UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI?
  3. IFAHAMU TEKNOLOJIA YA QR CODE KATIKA BIASHARA YAKO

Tueleze leo vision ya biashara yako ili tujue utamaduni wako ni upi, watu tuanze kuufuatisha. Hakikisha unasambaza makala hii kwa watu wengi kuhakikisha Biashara zinashamiri na unazidi kupata wateja wapya kupitia hapa. Tuanze.

LIPA KODI KWA FAIDA YA BIASHARA YAKO

Wamiliki wengi wa biashara huanza katika Biashara binafsi (machinga/sole proprietor). Baadae hukua kufikia partnerships, wabia wa kampuni mpaka mashirika. Kadiri unavyotengeneza mifumo ya biashara yako ndivyo inakuwa rahisi kulipa kodi.

Kodi huja katika namna nyingi, unapofanya kazi, unalipwa ujira/mshahara, hapo utalipa “Income Tax”. Kutegemea na kiasi cha pesa unacholipwa, asilimia fulani hukatwa na muajiri wako na kulipwa kwenye Mamlaka za Kodi, % hio huitwa “Withholding Tax”, hii hutaiona kwenye paycheck yako kwani hulipwa na mwajiri moja kwa moja kwenda kwa Mamlaka za kodi.

Ukinunua bidhaa, fahamu kuna kodi pale unalipa ambayo inajumuishwa katika bei ya bidhaa hio. Kodi hio huitwa “VAT” ambayo ni kodi maarufu na yenye kuingiza mapato makubwa sana katika mamlaka za Kodi. Kama unamiliki mali/ardhi unalipa Kodi iitwayo “Property Tax” kulingana na thamani ya mali/ardhi yako hio.

Kulipa kodi ni wajibu wa kizalendo, lakini zaidi ni matakwa ya kisheria. Usipolipa kodi unajiweka kwenye mazingira ya kulipishwa faini au adhabu kwa mujibu wa sheria. Kodi unayolipa inakwenda sehemu mbalimbali za kiserikali kama mishahara ya watumishi wa serikali, polisi, jeshi la zimamoto na uokoaji, kuimarisha miundombinu, sekta ys afya n.k.

UNAEPUKA VIPI RUNDO LA KODI KWA MANUFAA?

Kuendesha biashara kunajumuisha gharama nyingi sana. Na katika kila gharama kuna kiasi cha kodi unatozwa. Fahamu, Ukinunua unalipa kodi, Ukiuza unamlipisha mtu kodi. Jambo hili linafanyika ukiwa unajua na hata bila ya wewe kujua.

1. MANUNUZI

Kodi ya VAT (Value of Added Tax/Kodi ya Ongezeko la Thamani) ambapo unaponunua bidhaa/huduma yoyote unakuwa unanunua kitu chako pamoja na kukilipia kodi yake ya VAT hapo hapo. Kodi hiyo huwa ni 18% ya thamani kamili ya bidhaa/huduma inayouzwa. Mfano unaponunua umeme wa 2,000/-, hapo unakuwa umelipia na kodi yake ambayo imejumlishiwa kwenye hio 2,000/- (indirect tax). Hali kadhalika katika bidhaa/huduma zingine kama mafuta, vocha, computer, chakula, gesi n.k. Kila unachonunua kina kodi yake, Hivyo kama mfanyabiashara hakikisha manunuzi yako yote yahusuyo gharama za uendeshaji (umeme, maji, chakula, mafuta, maintenance, usafi) yanakuwa na risiti zake halali. Risiti zako hueleza kodi zile ulizokatwa “withheld” katika manunuzi/matumizi ya biashara yako. Hivyo jambo hili litakupa unafuu katika kulipa kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).

2. MAUZO

Wafanyabiashara huwalipisha wateja wao VAT lakini wengi hawapendi kulipa kiasi hiko cha kodi katika Mamlaka ya Kodi. Jambo hili ni kinyume na sheria na linaweza kukuweka kwenye mikono ya kisheria yanayoweza kukufilisi mali, kukupeleka gerezani au vyote vikakupata.

Hivyo unapofanya mauzo katika biashara yako hakikisha unatoa risiti halali ili bidhaa unazouza ziwe kwenye uwiano mzuri wa thamani na Mamlaka za kodi

CHANGAMOTO:

i. Tafiti zinaonyesha kuwa zaidi ya 70% biashara hazilipi kodi. Hii inachochewa na upungufu wa elimu ya kodi pamoja na morali ya wananchi katika kulipa kodi.

ii. Pia kumekuwepo na sekta ambazo hazilipi kodi ipasavyo, mfano sekta ya madini, uvuvi, misitu na utalii. Hii imetokana na kutokuwepo na njia bora za ukusanyaji wa kodi katika maeneo hayo, hivyo kudidimisha mapato yao katika kodi.

iii. Kuwepo kwa misamaha mikubwa ya kodi (tax exemptions) kwa wawekezaji wa ndani na wale wa nje. Mbinu hii iliwekwa ili kuwavutia wawekezaji wazidi kumininika lakini matokeo yake yamekuja kudhoofisha sekta zingine za biashara kutokana na kutokuwepo kwa usawa katika makusanyo.

iv. UFISADI: Inarudisha maendeleo nyuma sana hali ya kutokuwepo kwa makusanyo ya kodi. Hali hii kwa kiasi kikubwa huchochewa na kukithiri kwa vitendo vya Ufisadi katika Mashirika ya Umma pamoja na Mamlaka za Kodi. Watu huishiwa morari ya kulipa kodi pale wakiona kodi zao zinaishia mifukoni mwa watu wachache tena kwa manufaa binafsi. Jambo hili ni baya sana katika maendeleo ya biashara. Likemewe kwa nguvu zote.

MATUMIZI YA ICT KATIKA MFUMO WA KODI:

Teknolojia ya ICT imekuja kuwa mkombozi katika mifumo ya mapato na kodi katika biashara na Mamlaka za Kodi katika kutunza kumbukumbu za walipa kodi. Teknolojia imeleta afadhali katika kukusanya kodi kupitia matumizi ya mashine za EFD ambayo hutumika kukusanya taarifa za kodi, mauzo na manunuzi katika biashara.

Mashine hizi za EFD zilianza rasmi kutumika mwaka 2013 zikiwa na lengo la kusajili wafanyabiashara wote pamoja na miamala yote ya mauzo na manunuzi nchini Tanzania. Mwaka 2014/15 Halmashauri ya manispaa ya jiji la Arusha ilianza kutumia mfumo wa LGRCIS (Local Government Revenue Collection Information System). Zaidi kuhusu mfumo wa mapato ya serikali za mitaa unaweza kupata kupitia makala kwenye link hii https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-na-mapato-ya-serikali-za-mitaa/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NA MAPATO YA SERIKALI ZA MITAA”

Kuanzia hapo Halmashauri 8 nchini Tanzania zilianza kutumia mfumo huo wa LGRCIS kama mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi katika Halmashauri zao. Hata hivyo mwaka 2016 mifumo yote ya makusanyo iliunganishwa katika mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi wa TRA.

Lakini bado mpaka sasa mfumo wa LGRCIS unaendelea kutumika ktika kukusanya mapato ya halmashauri ikijumuisha Ushuru, Tozo na kodi za leseni za biashara. Mfumo huo umerahisisha malipo ya kodi kupitia njia za malipo ya kielektroniki kama MPESA, Bank transfer, Tigopesa n.k.

Hivyo, katika mifumo ya kodi kupitia makala haya ni matumaini yangu umejifunza kitu muhimu katika namna unavyoendesha biashara yako kwa faida bila kukwaruzana na Mamlaka za Kodi. Una maoni yoyote? Tafadhali weka comment yako hapa chini. Pia unaweza kushare link ya makala hii ili kuhakikisha inawafikia watu wengi zaidi kwa faida ya biashara zetu.

Sasa tumekuandalia makala hizi hapa chini zenye lengo la kukuimarisha katika namna ya kulipa kodi na kuifahamu mifumo yake zaidi. Zitakusaidia sana ukizisoma zote. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-nchini-tanzania/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NCHINI TANZANIA”
  2. https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-urasinishaji-harmonization-katika-biashara/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA”
  3. https://rednet.co.tz/ukiritimba-katika-biashara-ni-asali-au-shubiri/ yenye kichwa “UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI”

FANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA MUDA SAHIHI

Hebu piga hii hesabu hapo chap. Kwa mwezi unaingiza kiasi gani kama faida kutoka kwenye biashara yako? Tuseme 500,000/-. Na matamanio yako ni kuingiza kiasi gani kila mwezi? Jiambie hapo “Nataka niwe naingiza kiasi flani kila mwezi.” Tuseme 2,000,000/- kwa kukadiria.

Sasa kwa kuzingatia mfano huo hapo juu, ukweli ni kwamba kila mwezi unavyoshindwa kufikia matamanio yako unagharamika kiasi cha shilingi milioni 1.5 kwa kutofanya maamuzi sahihi kwa wakati na kuimarisha biashara yako.

MAAMUZI SAHIHI NI YAPI?

Wahenga walishasema “Kupanga ni kuchagua.” Lakini zaidi unapochelewa kuchukua uamuzi sahihi, fahamu kuwa unajiandaa kushindwa.

“Liwezekanalo leo lisingoje kesho” wanaongezea wahenga, Hii kwenye biashara ina maana kubwa sana, hasa kama wewe ni mtu makini unayetamani kuiona biashara yako ikikua na kuzidi kufanikiwa kila siku. Sasa leo ukimaliza kusoma makala hii utakuwa umepata mbinu sahihi za kukuza faida maradufu katika biashara yako. Hakikisha unazifanyia kazi mbinu hizi:

1. TAFUTA WATEJA WAPYA

Hii ni dhahiri kabisa. Lakini inatajwa kuwa ndio mbinu ngumu zaidi kuifanyia kazi. Kupata mteja mpya sio kazi ndogo. Wateja ndio moyo wa biashara yoyote ile. Tafiti zinaonyesha hugharimu mpaka mara 8 ya pesa kumpata mteja mpya zaidi ya kiasi kinachotumika kwa mteja aliyezeoleka/wa kudumu. Njia bora ya kupata wateja wapya ni kuhakikisha unajenga ukaribu na wateja wako wote hasa waliopo kwa kuwa Kizuri chajiuza chenyewe. Wengine wanaita Network Marketing, lakini watu wa mjini wanaita Connections. Hivyo, ukitaka kuongeza wateja hakikisha unakuza Connections zako.

2. BADILI MASHABIKI KUWA WATEJA

Hivi umeshawahi kuona huku kwenye mitandao (facebook, twitter, instagram nk) kuna mtu ana followers wengi 50k, 100k, 500k lakini bado anahangaika kupata wateja pindi akitangaza biashara yake fulani. Changamoto hii imekua ikichangiwa kwa kiasi kikubwa na mambo kama kununua account za mitandao ya kijamii. Mfano wewe unauza viatu halafu kwa kuwa huna followers ukatafuta account yenye followers wengi uinunue ukidhani ndo itaboost biashara yako ya viatu. Lakini bahati mbaya account uliyokuja kununua ni ya mtu aliyekuwa anapost picha za nusu uchi au maudhui ya kilimo. Unafikiri utatoboa hapo? Ni ngumu kwa kuwa awali watu walifollow accounts hizo kutokana na muendelezo wa maudhui yake. So ukinunua account kwa kigezo cha kuongeza wigo wa biashara yako, hakikisha maudhui yaliyokuwepo kabla yanaendana na unachokifanya. Hapo kutoboa ni rahisi zaidi.

3. BADILI UTARATIBU WA UENDESHAJI

Unahitaji kuongeza mapato ya biashara yako huku ukipunguza gharama za uendeshaji kwa kadiri inavyowezekana. Ili kuongeza mauzo yako hakikisha unaongeza bidhaa/huduma za ziada zinazoendana na bidhaa/huduma kuu. Yani kwa mfano unauza chakula, tengeneza na juisi/ongeza na matunda hapo. Kama unatoa huduma za kisheria basi ongeza na machapisho kuhusu sheria mbalimbali na madiliko yake mara kwa mara. Ongeza ujazo wa malighafi za biashara yako. Yani hakikisha mteja wako anakuganda kwa kuwa anafaidi zaidi ya pesa anayolipa kupata huduma/bidhaa zako. Fanyia kazi hii.

4. TANUA WIGO WA SOKO LAKO

Hapa utake usitake, Teknolojia ya ICT lazima ichukue nafasi yake. Njia bora zaidi za kisasa kuhakikisha unafikia soko kubwa zaidi duniani na kwa haraka ni kutumia Huduma za Kimtandao kama matumizi ya mitandao ya kijamii kama facebook, twitter, instagram na LinkedIn na matumizi ya blogu na tovuti(website). Majukwaa haya ya kimtandao yamekuwa madhubuti katika kutengeneza soko kwa bidhaa/huduma mbalimbali dunia nzima. Kujua zaidi kuhusu umuhimu wa tovuti katika biashara unaweza kutembelea link hii https://rednet.co.tz/kwanini-ni-muhimu-kuwa-na-websitetovuti-rasmi-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “KWANINI NI MUHIMU KUWA NA WEBSITE(TOVUTI) RASMI YA BIASHARA YAKO?” . Katika kutanua wigo wako huu wa kimasoko unaweza kutengeneza magroup ya facebook au LinkedIn ili kuonyesha bidhaa/huduma zako mpya na umuhimu wake kwa wateja wako, podcasts, tutorials na demos. Pima njia ipi inakufaa na yenye gharam ndogo zaidi.

5. TIZAMA BEI ZAKO TENA

Ukichunguza utagundua kuwa mteja siku zote anataka kupata huduma/bidhaa bora kwa bei nafuu. Upande wako kama mfanyabiashara unataka kupata faida zaidi kwa kila bidhaa/huduma unayomfikishia mteja. Hivyo hapo lazima busara na ushawishi wa hali ya juu utumike ili kuhakikisha kila upande unanufaika. Huu mchezo hauhitaji hasira. Angalia sokoni kwa watu wanaofanya biashara kama unayofanya wewe, angalia bei zao, angalia huduma wanazotoa, rudi kwako sasa ili kujua utaongeza/kupunguza kitu gani ili uweze kuhimili ushindani wa soko. Ikiwezekana katika vipindi fulani katika mwaka (sabasaba, eid, nanenane, Pasaka, Christmass, Mwaka Mpya, Nyerere Day) weka punguzo la bei (discount) kwa wateja wako. Hakikisha unawaweka karibu muda wote yani. Hii itakupa nafasi kubwa ya kutengenezea biashara yako uaminifu na uthubutu wa kununua kwa mtu yeyote.

6. KUWA NA MUENDELEZO MZURI (CONSISTENCY)

Unaweza kufanya yote tuliyojadili tangu mwanzo, lakini unapokosa muendelezo hapo unajisumbua tu. Hii dunia imejaa ushindani na tambua hauko peke yako unayefanya biashara hio unayoifanya. Hivyo cha msingi ni kuhakikisha unasurvive sokoni. Ukikaa kimya, hakuna mtu atakujua, hutapata wateja wapya, hata wale waliopo wataanza kukutilia shaka. Tambua pia, gharama za uendeshaji(umeme, maji, mafuta nk) huwa hazipungui kirahisi, lakini mapato ya biashara yanategemea juhudi yako ya kuuza. Usipouza huli. Zingatia hili.

7. FANYA KAZI

Hata kwenye Biblia imeandikwa, “asiyefanya kazi na asile.” Yani hakikisha mambo haya yote tuliyojadili hapa unayaweka kwenye uhalisia. Yasiishie kwenye makaratsi tu, toka nje, kutana na watu, onyesha umuhimu wako na jiuze kibiashara kwa kadiri inavyowezekana.

Ukiona matukio kama NyamaChomaFestival au TOTBonanza, hakikisha unashiriki ili kujijenga kibiashara na kuimarisha Connections zako. Mimi binafsi hizi mambo hazinipitagi ndio maana leo najivunia kukutana na watu mbalimbali kama kaka Togolani Mavura, Debora Da Silva kutoka Amici Designs, Angelika Farhan, wataalam kutoka TOTTech na wengineo wengi na kujenga ukaribu nao katika nyanja mbalimbali za kijamii, kiuchumi, Teknolojia na Uchumi. Kuna nguvu kubwa katika kujumuika. Hakikisha kila unapojumuika na watu mbalimbali unaitumia fursa hio kwa manufaa zaidi. Usiache nafasi hizo zikakupita hivi hivi.

Tayari tumekuwekea makala hizi hapa chini katika links ili kusudu zikusaidie kuelewa somo la leo kwa undani zaidi. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”
  2. https://rednet.co.tz/ifahamu-teknolojia-ya-qr-code-katika-biashara-yako/ yenye kichwa “IFAHAMU TEKNOLOJIA YA QR CODE KATIKA BIASHARA YAKO”
  3. https://rednet.co.tz/website-inasaidia-vipi-kuimarisha-biashara-yako/ yenye kichwa “WEBSITE INASAIDIA VIPI KUIMARISHA BIASHARA YAKO?”

Unalo lolote la kutushirikisha? Tafadhali usisite kuwasiliana nasi muda wowote utakapohisi umekwama. Tupo hapa kukuhudumia. Karibu.