Tag: African GDP

UFAHAMU MFUMO WA KODI NA MAPATO YA SERIKALI ZA MITAA

Serikali za mitaa zikiwa ndani ya Halmashauri za miji/Majiji na Wilaya zina mamlaka ya kukusanya mapato na ushuru kutoka vyanzo mbalimbali vya kodi. Pia zina mamlaka ya kutumia mapato hayo kwa mujibu wa sheria.

Kulingana na mipaka ya kisheria inayowekwa na Serikali Kuu, hizi Serikali za mitaa zina uwezo wa kutengeneza sera zake za mapato ili kuleta maendeleo katika shughuli zinazogusa kwa ukaribu maendeleo jamii nzima kama mashule, hospitali, mazingira ya mitaa na ulinzi shirikishi.

Mapato haya yanayokusanywa yanapata Mamlaka kutoka katika Sheria ya Mapato ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1983 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Sasa leo ukimaliza kusoma makala haya, utakuwa umezijua kodi/tozo zote zinazokusanywa pamoja na matumizi yake kwa ujumla.

Idadi ya kodi na ushuru unaokusanywa chini ya Mamlaka ya serikali za mitaa hutofautiana kutoka Halmashauri moja na Halmashauri nyingine. Mambo yanayoleta utofauti huu ni maendeleo katika sekta za Biashara, makazi, Uwepo wa maliasili na shughuli za kiuchumi.

Kuna baadhi ya tozo hukusanywa kwa siku, zingine mlipakodi hutozwa kwa mwaka, na zingine humpa nafasi mlipakodi kuchagua wakati wa kulipa (kwa mwezi, wiki, miezi mitatu/sita au kwa mwaka). Mfano; ushuru wa masoko, huu kawaida hukusanywa kwa siku. Hata hivyo Halmashauri zingine hutoa nafasi kwa mlipakodi kulipia ushuru huu kwa mwezi, miezi 3/6 au kwa mwaka mzima. Mwisho wa mwaka wa fedha kila Halmashauri inatakiwa kuandaa akaunti za kifedha ikiwa na wadau wafuatao:

i. Halmashauri Nzima

ii. Muwakilishi wa wizara (TAMISEMI)

iii. Ofisi ya Waziri Mkuu

iv. Ofisi ya Mdibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG)

v. Umma

Serikali za Mitaa hupata mapato yake kutoka katika vyanzo vikuu vitatu :

1. Mapato yake yenyewe

2. Ruzuku kutoka Serikali Kuu

3. Misaada kutoka mifuko ya Maendeleo ya ndani na nje ya nchi.

MAPATO/KODI ZINAZOTOZWA NI ZIPI?

1. USHURU WA BIDHAA (PRODUCE CESS)

Ushuru huu hutozwa na halmashauri kutoka katika mauzo ya mazao kama mahindi, mchele, kahawa, chai, pamba korosho pamoja na mifugo. Ushuru huu hutozwa kutokana na uzito/ujazo wa bidhaa yenyewe. Hii hufanya thamani ya bidhaa kutokua thabiti ikitegemea uzito/ujazo wa bidhaa (the source to be inelastic unless adjustments become frequent enough to catch up with inflation), hapa watu wa uchumi mtakuwa mmenipata vizuri sana. Viwango vya ushuru huu hubadilika kutegemeana na Halmashauri kutokana na Jiografia ya eneo, misimu ya hali ya hewa pamoja na hadhi ya kiuchumi ya Halmashauri husika.

2. LESENI ZA BIASHARA

Kodi hizi hutozwa kutokana na ukubwa na aina ya biashara, yaani maduka mawili ya rejareja yatatozwa kodi ya leseni sawasawa bila kujali ukubwa wa mitaji yao au hesabu zao wanazowasilisha kwenye mamlaka za mapato (turnovers).

3. ADA YA MASOKO

Aina hii ya Ushuru kwa kawaida hutozwa kwa siku kwa wafanyabiashara wanaouza bidhaa zao katika maeneo ya sokoni. Viwango vya tozo hii hubadilika kulingana na bidhaa zainazouzwa.

4. KODI YA ARDHI/MAJENGO

Kisheria, Serikali kuu inatakiwa kukusanya kodi kutoka kwenye mali zote zinazohamishika, wakati Serkali za Mitaa zitakusanya kodi katika mali zote zisizohamishika. Hata Hivyo, kodi ya ardhi na majengo haijaweza kutumika ipasavyo katika mambo ya kisiasa na uongozi katika nchi zinazoendelea. Katika kitabu chake kuhusu kodi ya ardhi, Richard Bird (1974:223) anasema, “The administrative constraint on effective land on effective land tax administration is so severe in most developing countries today that virtually all the more refined fiscal devises beloved by theorists can and should be discarded for this reason alone. Not only will they not be well administered, they will in all likelihood be so poorly administered as to produce neither equity, efficiency, nor revenue.” Nadhani hoja yake imeeleweka.

5. USHURU WA HOTELI/NYUMBA ZA WAGENI

Kodi hii kisheria hutegemea na tathmini binafsi kuhusu hesabu za hoteli/nyumba za wageni. Viwango vikubwa vya kodi huhamasisha ukwepaji wa kodi hasa kwa kurekodi hesabu mara mbilimbili. Katika utekelezaji, hasa kwa biashara ndogo ambazo hazitoi risiti, turnover zao hukadiriwa tu na hivyo kupunguza mapato kwenye serikali za mitaa. Hata hivyo, biashara kubwa ambazo pia hazitoi risiti huwekewa utaratibu wa kufanya maridhiano kati ya wakusanya kodi na walipa kodi. Utaratibu huu unaongeza gharama za uendeshaji na kuongeza mianya ya rushwa. Hata hivyo, kutokana na makusanyo haya kuzingatia asilimia za mapato ya biashara, makusanyo yanategemewa kubadilika kadhalika.

6. KODI YA MABANGO/MATANGAZO

Hii kodi wafanyabiashara wengi huilalamikia, wengine wasijui kwanini wanatozwa wakiweka tu mabango katika biashara zao. Viwango vya kodi hii hutegemea ukubwa wa bango, kama linawaka taa usiku na muda bango hilo litakavyokuwa wazi. Mapato ya mabango yanaendelea kukua kutokana na kuongezeka kwa biashara ambazo pia zinahitaji matangazo kujiimarisha.

7. USHURU WA MCHANGA

Unashangaa? Hadi mchanga wa kujengea unalipiwa kodi ndio katika baadhi ya halmashauri. Gharama ndogo za mchanga pamoja na kuongezeka kwa kasi ya watu kujenga kumechochea mmomonyoko wa udongo kwenye machimbo jambo lilifanya serikali kupiga marufuku Uchimbaji holela wa mchanga na kuanzisha utaratibu mpya wa kuchimba mchanga katika maeneo maalum na hivyo kudhibiti mapato yatokanayo na mchanga.

8. USHURU WA MACHINJIO/MAEGESHO

Halmashauri nyingi ambazo zina machinjio ya wanyama na maengesho ya magari hutoza kodi hio vizuri. Mapato yatokanayo na kodi hii yamekuwa yakiongezeka hasa maeneo ya mijini ambapo kumekuwa na uhitaji mkubwa wa maegesho ya magari na pikipiki pamoja na kuongezeka kwa wanyama wanaonmchinjwa katika maeneo maalum. Hii ni kwa kuwa serikali imefanikiwa kudhibiti machinjio zote za mitaani na kulazimisha wanyama wote kuchinjwa maeneo maalum ya machinjio ambayo yana udhibiti wa kiserikali na kuzingatia viwango vya nyama kwa manufaa ya walaji. Wale wanaopajua vingunguti watakuwa wamenipata sawasawa hapa.

9. KODI ZINGINE

Serikali za Mitaa hukusanya kodi nyingine nyingi sana. Unaweza kuzipata kwa ufupi katika tovuti rasmi ya Wizara ya Fedha kupitia link hii https://mof.go.tz/mofdocs/revenue/revlocal.htm…

Serikali za mitaa hazitozi kodi ambazo zipo nje ya zilizopo kwenye listi iliyo kwenye link hio.

Vile vile unaweza kupata maelezo kuhusu Kodi na wajibu wake katika matumizi ya mwaka 2018/2019 kupitia link hii hapa chini

https://rednet.co.tz/download/taxes-and-duties-at-a-glance-2018-2019…

HIZO KODI ZINATUMIKA VIPI?

Kodi zinazokusanywa na Halmashauri za Wilaya/Miji/Majiji hutumi kodi hizo kuimarisha mambo yafuatayo:

i. Ulinzi shirikishi

ii. Barabara za mitaani pamoja na miundombinu yake

iii. Zimamoto na uokoaji

iv. kuimarisha shughuli za kiuchumi (masoko, biashara) nk

Mfumo wa kodi wa serikali za mitaa kwa muda mrefu umekuwa tata sana na usio na uwazi katika makusanyo ya mapato yake mpaka matumizi. Lakini tangu kuzinduliwa kwa mfumo maalum wa makusanyo ya kodi kwa njia ya kielektroniki wa Local Government Revenue Collection Information System (LGRCIS) mnamo mwaka 2014, mfumo huo umekuwa mkombozi katika kurekodi makusanyo sahihi na kudhibiti matumizi katika Halmashauri. Mfumo huo wa kisasa umekuwa bora zaidi katika kukusanya Mapato ambapo unatoa urahisi wa kutumia njia mbalimbali za kulipia kodi kama MPESA, TIGOPESA, AIRTEL MONEY, Njia ya Benki na kadhalika.

Kuna makala hizi hapa chini tumekuwekea kwenye links. Zitakusaidia kufahamu zaidi kuhusu mifumo ya kodi na mapato hasa nchini Tanzania. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-nchini-tanzania/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NCHINI TANZANIA”
  2. https://rednet.co.tz/lipa-kodi-kwa-faida-ya-biashara-yako/ yenye kichwa “LIPA KODI KWA FAIDA YA BIASHARA YAKO”
  3. https://rednet.co.tz/unaweza-vipi-kukabiliana-na-hasara-katika-biashara-yako-mwaka-huu-2021/ yenye kichwa “UNAWEZA VIPI KUKABILIANA NA HASARA KATIKA BIASHARA YAKO MWAKA HUU 2021”

LIPA KODI KWA FAIDA YA BIASHARA YAKO

Wamiliki wengi wa biashara huanza katika Biashara binafsi (machinga/sole proprietor). Baadae hukua kufikia partnerships, wabia wa kampuni mpaka mashirika. Kadiri unavyotengeneza mifumo ya biashara yako ndivyo inakuwa rahisi kulipa kodi.

Kodi huja katika namna nyingi, unapofanya kazi, unalipwa ujira/mshahara, hapo utalipa “Income Tax”. Kutegemea na kiasi cha pesa unacholipwa, asilimia fulani hukatwa na muajiri wako na kulipwa kwenye Mamlaka za Kodi, % hio huitwa “Withholding Tax”, hii hutaiona kwenye paycheck yako kwani hulipwa na mwajiri moja kwa moja kwenda kwa Mamlaka za kodi.

Ukinunua bidhaa, fahamu kuna kodi pale unalipa ambayo inajumuishwa katika bei ya bidhaa hio. Kodi hio huitwa “VAT” ambayo ni kodi maarufu na yenye kuingiza mapato makubwa sana katika mamlaka za Kodi. Kama unamiliki mali/ardhi unalipa Kodi iitwayo “Property Tax” kulingana na thamani ya mali/ardhi yako hio.

Kulipa kodi ni wajibu wa kizalendo, lakini zaidi ni matakwa ya kisheria. Usipolipa kodi unajiweka kwenye mazingira ya kulipishwa faini au adhabu kwa mujibu wa sheria. Kodi unayolipa inakwenda sehemu mbalimbali za kiserikali kama mishahara ya watumishi wa serikali, polisi, jeshi la zimamoto na uokoaji, kuimarisha miundombinu, sekta ys afya n.k.

UNAEPUKA VIPI RUNDO LA KODI KWA MANUFAA?

Kuendesha biashara kunajumuisha gharama nyingi sana. Na katika kila gharama kuna kiasi cha kodi unatozwa. Fahamu, Ukinunua unalipa kodi, Ukiuza unamlipisha mtu kodi. Jambo hili linafanyika ukiwa unajua na hata bila ya wewe kujua.

1. MANUNUZI

Kodi ya VAT (Value of Added Tax/Kodi ya Ongezeko la Thamani) ambapo unaponunua bidhaa/huduma yoyote unakuwa unanunua kitu chako pamoja na kukilipia kodi yake ya VAT hapo hapo. Kodi hiyo huwa ni 18% ya thamani kamili ya bidhaa/huduma inayouzwa. Mfano unaponunua umeme wa 2,000/-, hapo unakuwa umelipia na kodi yake ambayo imejumlishiwa kwenye hio 2,000/- (indirect tax). Hali kadhalika katika bidhaa/huduma zingine kama mafuta, vocha, computer, chakula, gesi n.k. Kila unachonunua kina kodi yake, Hivyo kama mfanyabiashara hakikisha manunuzi yako yote yahusuyo gharama za uendeshaji (umeme, maji, chakula, mafuta, maintenance, usafi) yanakuwa na risiti zake halali. Risiti zako hueleza kodi zile ulizokatwa “withheld” katika manunuzi/matumizi ya biashara yako. Hivyo jambo hili litakupa unafuu katika kulipa kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).

2. MAUZO

Wafanyabiashara huwalipisha wateja wao VAT lakini wengi hawapendi kulipa kiasi hiko cha kodi katika Mamlaka ya Kodi. Jambo hili ni kinyume na sheria na linaweza kukuweka kwenye mikono ya kisheria yanayoweza kukufilisi mali, kukupeleka gerezani au vyote vikakupata.

Hivyo unapofanya mauzo katika biashara yako hakikisha unatoa risiti halali ili bidhaa unazouza ziwe kwenye uwiano mzuri wa thamani na Mamlaka za kodi

CHANGAMOTO:

i. Tafiti zinaonyesha kuwa zaidi ya 70% biashara hazilipi kodi. Hii inachochewa na upungufu wa elimu ya kodi pamoja na morali ya wananchi katika kulipa kodi.

ii. Pia kumekuwepo na sekta ambazo hazilipi kodi ipasavyo, mfano sekta ya madini, uvuvi, misitu na utalii. Hii imetokana na kutokuwepo na njia bora za ukusanyaji wa kodi katika maeneo hayo, hivyo kudidimisha mapato yao katika kodi.

iii. Kuwepo kwa misamaha mikubwa ya kodi (tax exemptions) kwa wawekezaji wa ndani na wale wa nje. Mbinu hii iliwekwa ili kuwavutia wawekezaji wazidi kumininika lakini matokeo yake yamekuja kudhoofisha sekta zingine za biashara kutokana na kutokuwepo kwa usawa katika makusanyo.

iv. UFISADI: Inarudisha maendeleo nyuma sana hali ya kutokuwepo kwa makusanyo ya kodi. Hali hii kwa kiasi kikubwa huchochewa na kukithiri kwa vitendo vya Ufisadi katika Mashirika ya Umma pamoja na Mamlaka za Kodi. Watu huishiwa morari ya kulipa kodi pale wakiona kodi zao zinaishia mifukoni mwa watu wachache tena kwa manufaa binafsi. Jambo hili ni baya sana katika maendeleo ya biashara. Likemewe kwa nguvu zote.

MATUMIZI YA ICT KATIKA MFUMO WA KODI:

Teknolojia ya ICT imekuja kuwa mkombozi katika mifumo ya mapato na kodi katika biashara na Mamlaka za Kodi katika kutunza kumbukumbu za walipa kodi. Teknolojia imeleta afadhali katika kukusanya kodi kupitia matumizi ya mashine za EFD ambayo hutumika kukusanya taarifa za kodi, mauzo na manunuzi katika biashara.

Mashine hizi za EFD zilianza rasmi kutumika mwaka 2013 zikiwa na lengo la kusajili wafanyabiashara wote pamoja na miamala yote ya mauzo na manunuzi nchini Tanzania. Mwaka 2014/15 Halmashauri ya manispaa ya jiji la Arusha ilianza kutumia mfumo wa LGRCIS (Local Government Revenue Collection Information System). Zaidi kuhusu mfumo wa mapato ya serikali za mitaa unaweza kupata kupitia makala kwenye link hii https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-na-mapato-ya-serikali-za-mitaa/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NA MAPATO YA SERIKALI ZA MITAA”

Kuanzia hapo Halmashauri 8 nchini Tanzania zilianza kutumia mfumo huo wa LGRCIS kama mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi katika Halmashauri zao. Hata hivyo mwaka 2016 mifumo yote ya makusanyo iliunganishwa katika mfumo mkuu wa makusanyo ya kodi wa TRA.

Lakini bado mpaka sasa mfumo wa LGRCIS unaendelea kutumika ktika kukusanya mapato ya halmashauri ikijumuisha Ushuru, Tozo na kodi za leseni za biashara. Mfumo huo umerahisisha malipo ya kodi kupitia njia za malipo ya kielektroniki kama MPESA, Bank transfer, Tigopesa n.k.

Hivyo, katika mifumo ya kodi kupitia makala haya ni matumaini yangu umejifunza kitu muhimu katika namna unavyoendesha biashara yako kwa faida bila kukwaruzana na Mamlaka za Kodi. Una maoni yoyote? Tafadhali weka comment yako hapa chini. Pia unaweza kushare link ya makala hii ili kuhakikisha inawafikia watu wengi zaidi kwa faida ya biashara zetu.

Sasa tumekuandalia makala hizi hapa chini zenye lengo la kukuimarisha katika namna ya kulipa kodi na kuifahamu mifumo yake zaidi. Zitakusaidia sana ukizisoma zote. Gusa link kisha makinika:

  1. https://rednet.co.tz/ufahamu-mfumo-wa-kodi-nchini-tanzania/ yenye kichwa “UFAHAMU MFUMO WA KODI NCHINI TANZANIA”
  2. https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-urasinishaji-harmonization-katika-biashara/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU URASINISHAJI (HARMONIZATION) KATIKA BIASHARA”
  3. https://rednet.co.tz/ukiritimba-katika-biashara-ni-asali-au-shubiri/ yenye kichwa “UKIRITIMBA KATIKA BIASHARA, NI ASALI AU SHUBIRI”

TEKNOLOJIA KATIKA KUKUZA BIASHARA KUPITIA SEKTA YA UTALII

Inasemekana binadamu anajua zaidi mazingira ya mwezini kuliko ajuavyo mazingira ya ndani/chini ya bahari. Sasa kampuni ya usafirishaji ya Uber tarehe 23 May 2019 ilizindua manuwari ndogo iitwayo ScUber kwa ajili ya kutalii ambapo mradi huo umeanzia jijini Queensland, Australia. Moja kati ya sababu ikiwa ni kutoa fursa kwa wageni/watalii kuweza kuzuru eneo maarufu la bahari liitwalo The Great Barrier Reef nchini humo. Sasa tunaweza vipi kutumia teknolojia katika kukuza biashara kupitia sekta ya utalii? Kumbuka Tanzania ina vivutio vingi sana vya utalii na vijana wengi wamejikita katika kuhudumia watalii hao, watumieje teknolojia kujiletea manufaa? Twende sambamba mpaka mwisho wa makala hii kufahamu zaidi.

utalii na teknolojia

Turudi Australia, manuwari hio ndogo yenye uwezo wa kubeba watu watatu kwa wakati mmoja ni ya kwanza kabisa duniani kufanya shughuli za kutalii kwa mtu yeyote anayehitaji kufanya hivyo na ambayo huduma yake inapatikana kirahisi kupitia Application ya Uber inayopatikana Playstore ya Google na Appstore ya iOS (Je, wewe ni mmoja kati ya wale waliozoea kuziona manuwari kwenye muvi na kusikia manuwari za kivita tu? 😂). Haya ni mapinduzi makubwa katika kufanya biashara kupitia nyanja nyingine ya kichumi (kutoka usafirishaji mpaka utalii).

Sekta ya utalii inatajwa kuwa ni sekta muhimu sana katika ukuaji wa uchumi na kutengeneza ajira duniani kote. Sekta hio inatajwa kujumuisha 8.8% ya ajira zote duniani, sawa na watu milioni 258. Vile vile 9.1% ya wastani wa pato la taifa GDP inatokea katika sekta hii ambayo ni sawa na $6 trilioni. Zaidi, 5.8% ya bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi (exports) huhusishwa na sekta hii ambayo ni takribani $1.1 trilioni. Hata hivyo, sekta hii ya utalii huchochea sana uwekezaji ambapo 4.5% ya uwekezaji wote unaofanywa duniani hupitia katika sekta hii ambayo ni sawa na $652 bilioni za kimarekani.

Tukiangazia eneo la kusini mwa jangwa la Sahara inakadiriwa kwamba ajira 3.8 milioni zikijumuisha ajira 2.4 ambazo si za moja kwa moja (indirect jobs) zinakadiriwa kutengenezwa katika miaka 10 ijayo. Hii ni kwa mujibu wa Baraza la usafiri na utalii duniani (WTTC).

Sasa changamoto; Sekta hii ya utalii inachangia vipi katik kukuza biashara barani Afrika? Teknolojia inachangia vipi katika maendeleo haya ya utalii na biashara?

Kutoka ziara za watalii 6.7 milioni mwaka 1990, nchi za ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara zilitembelewa na watalii 33.8 milioni kufikia mwaka 2012 kwa pamoja ambapo stakabadhi za wageni mwaka huo 2012 peke yake zilionyesha zaidi ya dola za kimarekani 36 bilioni zilipatikana huku mchango wa moja kwa moja ukiwa ni 2.8% katika pato la ndani la taifa GDP (Jumla ya mchango ikiwa ni mchango wa moja kwa moja na ule usio wa moja kwa moja, ilifikia 7.3% ya GDP). Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya baraza la WTTC mwaka 2013.

Lakini, ili kufanikiwa zaidi katika kufanya Utalii na kuendeleza biashara, ukanda huo wa SSA (Subsaharan Area) inabidi ujidhatiti katika mambo yafuatayo; upatikanaji wa ardhi, ruhusa ya wawekezaji katika maswala ya fedha, matangazo ya utalii, kodi za uwekezaji katika utalii, utaalamu na ujuzi katika utalii, ulinzi na usalama, maswala ya afya, mahitaji ya viza na ukiritimba. Sasa teknolojia inaleta mchango gani katika kukuza biashara kwa kupitia utalii? Kuhusu namna unavyoweza kuitangaza biashara yako katika nyanja hii ya utalii fuatana na makala hii hapa

Tuzione baadhi ya njia za kiteknolojia zinazotumika katika nyanja hio;

E-TOURISM:

Huduma za intaneti zimeleta mapinduzi makubwa sana kwenye sekta hii ya utalii ambapo watalii na wageni sasa wanaweza kupata taarifa muhimu kuhusu mahali wanapotaka kwenda kutalii kama mbuga za wanyama, bidhaa za kiasili na utamaduni, hoteli, majumba ya makumbusho na historia mbalimbali kwa kutumia vifa vyao vya kielekroniki vilivyoungwa na huduma za intaneti kama simu za rununu na kompyuta mpakato (laptop). Matokeo yake wageni na watalii wamekuwa na mahitaji makubwa kwa bidhaa za kiasili na utamaduni pamoja na kujali thamani ya pesa zao pamoja na thamani ya muda wao. Hii imerahisisha sana ufanyaji wa biashara haswa kupitia majukwaa ya ecommerce (ambayo unaweza kuyapata kwetu Rednet Technologies kirahisi sana., gusa link hii kupata huduma zetu zenye ubora Our Services🙋).

E-HOSPITALITY;

Teknolojia ya ICT imepenya mpaka katika mifumo ya huduma kwa wageni kwa haraka mno, huku ikizama katika utendaji wa hoteli, kuunda upya shughuli za masoko, kukuza huduma kwa wateja, kuimarisha huduma za kifedha, huduma za usafiri wa anga pamoja na huduma za kuwezesha ufanyaji wa biashara mtandaoni. Hii imeleta mafanikio zaidi baada ya kugunduliwa mifumo ya Computerized Reservetion Systems (CRS‘s) kuchukua nafasi ya mfumo wa zamani wa kuandikisha wageni katika mahoteli na katika vituo vya afya.

E-TRAVEL AGENCIES:

Teknolojia ya ICT imeleta maendeleo makubwa katika uendeshaji wa shughuli za taasisi mbalimbali na wakala wa kusafirisha na kutembeza wageni na watalii ambapo imeimarisha sana shughuli za ndani kama uhasibuukaguzi na rasilimali watu pamoja na shughuli za nje kama huduma kwa wateja, mifumo ya tiketi na mawasiliano ya wabia. Licha ya kuwa na 15% ya idadi yota ya watu duniani, Afrika ilikuwa ikihudumia 4% tu ya abiria wa safari za ndege duniani. Hata hivyo huduma hio ilipanda kufikia 6.5% katika kipindi cha mwaka 1998-2009 huku Carpe Verde, Msumbiji, Ethiopia na Tanzania(kabla ya kuimarishwa kwa AirTanzania) zikikuwa kwa makumi ya asilimia (WorldBank report). Maendeleo haya yanaakisi ukuaji wa matumizi ya teknolojia katika eneo hilo ambapo kumekuwepo pia na matumizi ya mifumo ya kudhibiti tiketi (OTS) na mifumo ya kuwasiliana na wateja (CRM‘s). Zaidi mifumo ya kudhibiti tiketi imekuwa muhimu katika kuratibu idadi ya wageni pamoja na kudhibiti maswala ya fedha kiteknolojia.

E-DESTINATION:

Hii ni maalum kwa waendeshaji wa Hoteli, Nyumba za wageni (Guest Houses & Lodges) pamoja na migahawa ya chakula. Sasa teknolojia imeleta mifumo mahsusi kwa ajili ya kurahisisha huduma katika kutafuta soko na kusajili wageni/watalii kirahisi wakiwa popote duniani kwa kutumia simu za rununu au kompyuta. Mfumo wa Destination Management System (DMS) umekuwa muhimu sana licha ya 10% tu ya vyumba vya hoteli 390,000 zinazopatikana katika ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara kuwa na hadhi ya kimataifa, huku Afrika Kusini ikishikilia nusu ya vyumba hivyo. Hata hivyo Kenya, Mauritius, Shelisheli na Tanzania zinaonyesha kuwekeza zaidi katika huduma za hoteli na teknolojia.

E-COMMERCE:

Jukwaa maarufu zaidi duniani katika kufanya biashara kwa njia ya mtandao kielektroniki. Hii ni muhimu kwa wafanyabiashara wa bidhaa za kiasili na kitamaduni kama shangavinyago na batiki ambapo sasa wanaweza kuweka bidhaa zao katika majukwaa hayo na kufikisha bidhaa zao duniani kote kirahisi zaidi, hivyo kukuza mauzo yao (Majukwaa haya ya ecommerce yanapatikana hapa Rednet Technologies, pitia tovuti yetu kwa kugusa link hii Rednet Technologies).

Kufahamu zaidi kuhusu e-commerce tafadhali fuatilia makala hii hapa kwenye link https://rednet.co.tz/unafahamu-nini-kuhusu-biashara-za-kielektroniki-e-commerce-businesses/ yenye kichwa “UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI?”

Una la zaidi? Tafadhali, weka comment yako hapo chini ili tuweze share mawazo na hoja kuhusu makala haya juu ya unaweza vipi kutumia teknolojia katika kukuza biashara kupitia sekta ya utalii? Kazi kwako mfanyabiashara.

Je umependezwa na makala zetu zilizomo katika website yetu hapa?

Unataka kufanya malipo kwa huduma zetu bila kuhofia makato ya miamala?

Sasa tumekuletea huduma ya LIPA NAMBA ya M-PESA (TILL NUMBER) na QR CODE ambapo unaweza kututumia TIP ya kutupongeza kwa kazi nzuri au Kulipia huduma unazozipata kutoka kwetu BILA MAKATO ya miamala.

Tumia LIPA NAMBA kwenye picha hapa muda wote 24/7.

Kwanini uwe na website ya biashara yako?

UNAFAHAMU NINI KUHUSU BIASHARA ZA KIELEKTRONIKI (e-commerce BUSINESSES)?

Japokuwa imechelewa, lakini kwa sasa Africa ndio inaongoza mbio katika kufanya mapinduzi ya kidijitali kuliko sehemu yoyote duniani. Namna ya kufanya biashara inazidi kubadilika ikionyesha nia ya dhati kufanya maendeleo ya kiuchumi, miundombinu na maswala ya kijamii. Mwaka 2018 nchi wanachama wa Umoja wa Africa walipiga hatua kubwa katika mfumo wa kufanya biashara na muingiliano wa kiuchumi baada ya kuanzisha Eneo Huru la Kufanyia Biashara barani (Continental Free Trade Area AfCFTA). Eneo hili lililoanzishwa linashirikisha nchi 22 zilizoweka sahihi tayari na utekelezwaji wake ulipangwa kuanza mwaka 2019 (tayari umeshaanza).

Hata hivyo mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuzishirikisha nchi ambazo bado si wanachama wa eneo hili jipya, inatarajiwa eneo hili kufikia soko la watu takribani bilioni 1.2 barani wakiwa na jumla ya pato la ndani la taifa (GDP) la dola za kimarekani trilioni 2.5 kwa pamoja, kwa mwaka. Hii inatarajiwa kuwa ni mapinduzi makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nyanja ya uchumi wa Afrika.

Sasa, swali linakuja; Afrika(wafanyabiashara, makampuni/mashirika na Serikali) imejiandaa vipi na mapinduzi haya ya uchumi wa kidijitali? Na zaidi, watunga sera/sheria wataangalia vipi biashara za kielektroniki (e-commerce) kama mada muhimu katika eneo hilo jipya la kufanya biashara huru barani?

Tume ya kudhibiti uchumi wa Africa ya Umoja wa Mataifa (ECA) ikishirikiana na Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) pamoja na Baraza la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia maendeleo ya kibiashara (UNCTAD) mwaka huu 2019 imechapisha ripoti yake ikiangazia maendeleo ya Afrika kiujumla katika nyanja za kiuchumi, siasa na kijamii.

URAHISI: Imeonekana kwamba e-commerce inaweza kufanya biashara ya bidhaa na huduma kwa urahisi zaidi ambapo itarahisisha mwenendo mzuri wa biashara kati ya wazalishaji, wafanyabiashra na walaji pamoja na kumbukumbu zao na miamala ya kifedha.

MITANDAO YA KIJAMII: Pia imeonekana kwamba e-commerce inapatikana na kufanyika kirahisi katika mitandao ya kijamii kama facebook na Instagram ambapo ndipo mahali kuna watumiaji wengi zaidi wa Intaneti duniani (zaidi ya watu bilioni 2 kati ya watumiaji bilioni 4 wa intaneti).

KUTOKUWA NA MIPAKA: Mfumo wa uchumi wa Kidijitali kiasili umetengenezwa kuepuka mipaka ya kijiografia katika kufanya biashara na kubadilishana fedha ambapo mabadiliko haya ya kiteknolojia yataongeza umakini zaidi katika mwenendo wa masoko na gharama. Lakini bado wimbi kubwa la watu watakaoshiriki kwenye soko barani wanaonekana wataachwa nyuma kutokana na kutokuingiliana kwa lugha na vita/ghasia za mara kwa mara katika baadhi ya jamii/nchi.

BIASHARA: Kwa mujibu wa UNCTAD mwaka 2016 kwa dunia nzima e-commerce iliweza kupitisha mauzoya takribani dola trilioni 26 ambapo 90% ilikuwa ni Biashara kwa Biashara (B2B e-commerce) na 10% ilikuwa ni Biashara kwa Mlaji (B2C e-commerce). Hata hivyo kupima mwenendo wa e-commerce katika baadhi ya nchi zinazoendelea imekuwa ni changamoto kupata data na takwimu, haswa katika nchi za Afrika.

IMPORTATION: Takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF) zinaonyesha kwamba Biashara kati ya nchi na nchi imekua kwa kiasi kikubwa Afrika ambapo zimechagizwa na vituo vichache vya kiteknolojia (Hubs) ambavyo vimerahisisha mno mwenendo wa biashara. Biashara kati y nchi na nchi (Intraregional import) imekuwa zaidi ya mara 3 katika miongo miwili iliyopita kufikia 12%- 14% sawa na dola bilioni 100 ikichagizwa na uwepo wa jumuiya za kiuchumi barani (Subregional Economic Communities REC‘s).

UZOEFU: Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na umri wa Jumuiya hizi za Kimaendeleo barani Afrika ambapo uzoefu huo hutumika kuongeza jitihada katika kuboresha namna ya ufanyaji biashara kuelekea uchumi wa kidijitali kiteknolojia. Uzoefu huo pia hutumika kuunganisha jumuiya moja na nyingine (mf, SADC na COMESAna EAC) ambapo zitazalishwa nafasi nyingi zaidi za kufanya biashara kati ya nchi wanachama na ripoti zinaonyesha 75% ya biashara hizi ndani ya jumuiya barani Afrika zimefanyika mwaka 2017 peke yake na nusu ya biashara hizo zilifanyika katika jumuiya ya SADC.

Chini ya mwavuli wa AfCFTA nchi wanachama zinatarajia kufuta tozo/ushuru kwa 90% ya bidhaa zote zitakazopitishwa na kufanyiwa biashara katika eneo hilo. Hii itaruhusu uwezekano wa kupunguza mlolongo wa kodi au kuongeza idadi na thamani ya bidhaa na huduma zitakazohusishwa. Matokeo yoyote katika punguzo hilo linalotarajiwa katika muktadha wa biashara kidijitali yataleta picha tofauti. Kupunguza mlolongo wa tozo za mipakani baina ya nchi na nchi kutapungua kwa 15% pekee ikitegemea thamani ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi husika. Hii ni kwa mujibu wa Tume inayoshughulikia Uchumi wa Afrika kutoka Umoja wa Mataifa (UNECA) mwaka 2018.

Sasa mwaka 2018 Jumuiya ya COMESA ilibuni mfumo wa kudhibiti eneo huru la kibiashara kidijitali (Digital Free Trade Area DFTA). Mfumo huu umeundwa na mambo yafuatayo;

•E-trade: Hili ni jukwaa mahsusi kwa ajili ya kufanya biashara za kimtandao na kuwezesha malipo ya kielektroniki, mobile apps kwa ajili ya wafanyabiashara walioko katika Jumuiya hio.

•E-logistics: hili ni jukwaa maalum kwa ajili ya kuwezesha biashara ya usafirishaji wa mizigo baina ya nchi wanachama wa jumuiya.

•E-legislation: huu ni mfumo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara rasmi ambao unawawezesha kufanya miamala na malipo kielektoniki.

Mfumo huu uliobuniwa na Jumuiya ya COMESA umelenga kutangaza biashara za wanajumuiya katika nchi wanachama ikijumuisha kupitia majukwaa ya e-commerce. Mfumo huu ulikuwa ni mfanano wa mfumo uliotengenezwa na kuzinduliw na nchi ya Malaysia mwaka 2017 katika muktadha wa kufanya biashara huru ndani ya eneo maalum.

Makala haya ya leo yamelenga wafanyabiasha kujidhatiti kidijitali kwa kutumia teknolojia za kisasa katika biashara zao za kila siku ili kuweza kunufaika vyema na masoko pamoja na fursa kede ndani na nje ya nchi.

Makala hizi hapa zinarandana na somo ulilolipata leo. Zitakusaidia sana, shuka nazo:

  1. https://rednet.co.tz/fahamu-kuhusu-biashara-ya-fedha-za-kidijitali-cryptocurrency-business/ yenye kichwa “FAHAMU KUHUSU BIASHARA YA FEDHA ZA KIDIJITALI (CRYPTOCURRENCY BUSINESS)”
  2. https://rednet.co.tz/teknolojia-ya-huduma-za-fedha-kwa-njia-ya-kielektroniki-fintech/ yenye kichwa “TEKNOLOJIA YA HUDUMA ZA FEDHA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (FINTECH)”
  3. https://rednet.co.tz/fahamu-siri-ya-kufanikiwa-katika-kuwekeza/ yenye kichwa “FAHAMU SIRI YA KUFANIKIWA KATIKA KUWEKEZA”

Ukiwa na lolole, tafadhali unaweza kuwasiliana nasi kupitia;

e-mail: info@rednet.co.tz

tovuti: https://rednet.co.tz

Simu:+255765834754